FASHION! NI DHAMBI KWA BINTI ZA MUNGU.

FASHION! NI DHAMBI KWA BINTI ZA MUNGU.

Bwana YESU ni yeye yule jana, na leo na hata milele hajabadilika wala hana kigeugeu, na NENO lake ni lile lile. Kama maandiko yanavyosema mwanamke wa kikristo anapaswa avae mavazi ya kujisitiri.(1Timotheo 2:9) hilo Neno hata leo bado linaendelea kufanya kazi kwa binti za Mungu.

Leo hii vichaa wapo wengi mitaani tunawaona, lakini ni mara chache sana kumuona kichaa mwanamke akitembea uchi barabarani, ingawa vichaa wanaume ni rahisi kuwaona wakiwa uchi, lakini sio kwa wanawake vichaa utawakuta wamevaa matambara na kujisitiri mwili mzima japo ni vichaa. Je! ni kwanini iwe hivi?? Jibu ni Kwasababu uchi wa mwanamke ni wathamani zaidi kuliko wa mwanamume hivyo unastahili muda wote usitiriwe.

Lakini leo hii mwanamke mwenye akili timamu ambaye uchi wake unathamani ambaye angepaswa afunikwe, ndiye anayeongoza kwa kutembea uchi barabarani, SASA HAPO KICHAA NI NANI?  lakini mwanamume ambaye uchi wake usiokuwa na thamani nyingi utakuta kajisitiri, kafunika shingo yake kwa shati na tai, huwezi kuona mgongo wake uko wazi wala mapaja yake wazi akitembea barabarani, miguu yake imesitiriwa yote kwa viatu na soksi, ni mtu huyo ambaye uchi wake hauna thamani sana, Leo hii huwezi kuona mwanaume anaenda na vesti kazini, lakini hili jambo ni la kawaida kwa wanawake kutembea migongo wazi na vifua wazi hata sasa imekuwa kawaida mpaka kwenye sehemu za ibada.


Swali ni Je! roho gani ipo hapo katikati? jibu ni rahisi ni ile ile roho iliyokuwa kwa mwanamke Yezebeli wa kwa maana yeye ndiye mwanamke pekee aliyekuwa anapaka uso rangi katika biblia.Lakini tuna wadada hao hao ambao Bwana Yesu amewaambia yeye mwenyewe wasifanye  mambo kama hayo na wametii yaani, kujipodoa uso, kupaka wanja, kuvaa vimini, suruali, kaptura, vesti, tight, pedo, kupaka lipstick, kupachika kucha, wigi n.k. lakini cha ajabu utamkuta mdada mwingine anajiita mkristo na anadai  amepokea Roho Wa Mungu lakini bado anajiona salama kufanya vitu hivyo.

Jiulize ni roho gani iliyoko ndani yako? kwanini YESU yule yule amkataze dada yule kufanya hivyo vitu na wewe asikukataze? jiulize sana, kama Roho wa Mungu kweli anakaa ndani yako atakushuhudia kwamba haya mambo hayafai na yanakupeleka kuzimu.

 Lakini kaa ukifahamu tu, wanawake wote wanaofanya hivyo sehemu yao ni katika lile ziwa la moto HIVI ASEMA BWANA.. (warumi 1).

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa mawasiliano/Ushauri/kuokoka/Whatsapp. Namba zetu ni hizi

+255693036618/+255789001312


Mada Nyinginezo:

MAVAZI YAPASAYO.

CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE

BWANA YESU ALIKUWA ANAMAANISHA NINI KUSEMA MARKO 2:19″WALIOALIKWA HARUSINI WAWEZAJE KUFUNGA MAADAMU BWANA-ARUSI YUPO PAMOJA NAO?”

PAULO ALIMWAMBIA TIMOTHEO ATUMIE MVINYO KIDOGO KWA AJILI YA TUMBO LAKE, JE! TUNARUHUSIWA NA SISI PIA KUTUMIA POMBE?


Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments