DHAMBI YA ULIMWENGU.

DHAMBI YA ULIMWENGU.

Dhambi ipo moja tu! nayo ni kutomwamini BWANA YESU KRISTO, hayo mengine ni matokeo ya dhambi, uwizi, usengenyaji, rushwa, uasherati, utukanaji, uuaji n.k si dhambi bali ni matokeo ya dhambi iliyo moja tu! nayo ni KUTOKUMWAMINI BWANA YESU KRISTO.

Na kumbuka kumwamini Yesu Kristo, sio kumsoma na kuamua kumwamini, hapana! Bali ni kupata ufunuo wa yeye ni nani, alitoka wapi, alikuja kufanya nini, na umuhimu wake kwa ulimwengu ni upi?.…ukishamwelewa kwa namna hiyo, basi ndani yako kutawaka shauku ya kutaka kujishughulisha na mambo yake (hapo utakuwa tayari umeshamwamini).

Kwahiyo kama dhambi ni moja tu! ambayo ni kutokumwamini Kristo Yesu Kristo, hayo mengine ni matokeo ya hiyo dhambi, Hivyo siku ya hukumu Bwana hatamuhukumu mtu kwasababu alikuwa mvuta bangi, au kwasababu alikuwa mwasherati, au kwa sababu alikuwa mwongo…hapana atamuhukumu mtu kwanza kwa sababu hakumwamini YESU KRISTO, MWANA WA MUNGU. Hiyo ndiyo dhambi ya msingi kabisa..

Yohana 3: 17 “Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.

18 Amwaminiye yeye hahukumiwi; ASIYEAMINI AMEKWISHA KUHUKUMIWA; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu”.

Tuchukue mfano mwepesi, kuna kichaa mahali Fulani, kaonekana akivunja vioo vya magari ya watu, na kupiga watu barabarani, na kaharibu mali, na kisha wakamkamata na kumfunga kamba! Je! wale waliomfunga kamba watamhukumu kwanza kwa kuanza kumuuliza kwanini amevunja vioo vya magari?, au kwanini anapiga watu, au kwanini ni mwaribifu…utagundua kwamba! Hawataweza kufanya hivyo…watajua tatizo halipo katika matendo anayoyafanya, bali tatizo lipo katika akili zake nalo ni ile hali ya ukichaa iliyondani yake!!…Hivyo wakitaka wapate ufumbuzi wa tatizo lao, watashughulika kwanza na tiba ya akili yake, zaidi ya tiba ya mambo anayoyafanya, hawawezi kumshauri aache uaribifu, au aache kupiga watu katika hali yake ya ukichaa aliyokuwepo, ni sawa na kupaka rangi upepo.. sharti wamtibu kwanza tatizo lake hilo moja!..Na mengine yatatibika yenyewe.

Ndivyo ilivyo kwa mtenda dhambi yoyote yule aliye mwasherati, mwizi, muuaji, mla rushwa, msengenyaji n.k….tatizo lake ni moja tu HAJAMWAMINI YESU KRISTO. Hajapata ufunuo utakaoweza kumfanya aache vitendo viovu. Na njia pekee ya kuviacha hivyo haitaokani na bidii au nguvu za mtu binafsi, anaweza akajitahidi kufanya hivyo leo na kesho lakini kesho kutwa akarudia uchafu wake ule ule wa kale, bali hiyo inakuja kwa kumwamini yule awezaye kuondoa mambo hayo ndani ya mtu. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

Biblia inasema “ Yohana 1:29 “Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, AICHUKUAYE DHAMBI YA ULIMWENGU!”

Ukisoma hapo kwa makini utaona hakusema “AZICHUKUAYE DHAMBI ZA ULIMWENGU” bali imesema “AICHUKUAYE DHAMBI YA ULIMWENGU”..ikimaanisha kuwa hiyo dhambi NI MOJA TU! sio nyingi nayo ni KUTOKUAMINI. Ndugu Yesu pekee ndiye anayeweza kuwa tiba ya hofu unayopitia sasa hivi, yeye pekee ndiye anayeweza kuwa kimbilio lako yeye pekee ndiye nguvu zako na faraja yako, yeye pekee ndiye kila kitu kwako, wewe peke yako hutaweza kuondoa dhambi yoyote ndani yako, kadhalika mwingine yoyote hakuna. Hivyo Ndivyo ilivyo, na ndivyo itakavyokuwa daima. Na huo ndio ukweli. Hakuna mwingine, na mtu akimpinga huyo basi amethibitisha kwamba yeye mwenyewe anaweza kujiokoa na kusimama kwa nguvu zake kumshinda shetani na dhambi…Lakini fahamu kuwa hakuna ambaye alishawahi kuwa mkamilifu kwa nguvu zake mwenyewe tangu dunia kuumbwa isipokuwa YESU pekee.

Kwa yeyote atakayemwamini na kumpokea HATI hiyo ya dhambi itaondolewa juu yake. Na kutakaswa kila siku wa Roho wake. Lakini kwa atakapuuzia hukumu hatoikwepa kwa namna yoyote.

Bwana alisema sharti injili ikahubiriwe kwa kila kiumbe, ndipo ule mwisho uje!! Na ni kwasababu Neno lake huwa halipiti! Ni lazima kila mtu atasikia habari za Yesu Kristo, wengine mara moja tu! wengine mara mbili mbili, wengine mara tatu tatu..Lakini mwisho injili itasikika kwa kila mtu, Roho Mtakatifu atanyanyua watu wake popote pale, iwe mijini, iwe vijijini, iwe shuleni, iwe mtaani, iwe gerezani iwe ikulu..Injili itafika..Na wewe unayesoma ujumbe huu, leo imekufikia kwa njia hii, sijui kwako hii ni mara ya ngapi?..labda ni mara ya kwanza, au mara ya 20..jibu unalo wewe… Lakini umesikia habari za Huyu Yesu Mkombozi wa ulimwengu na Madhara ya kutomwamini. Ni heri ukamtafuta leo kabla nyakati za hatari hazijafika…Ukimpokea na kumwamini atausafisha uovu wako wote, na kukufanya wewe kiumbe kipya.

1 Yohana 5.3 “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.

4 Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.

5 Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, ISIPOKUWA NI YEYE AAMINIYE YA KWAMBA YESU NI MWANA WA MUNGU?

6 Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu, Yesu Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu.

7 Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli”.

Tafadhali “share” na pia wahubirie wengine habari njema za msalaba kwa kadri uwezavyo popote ulipo.Na pia tembelea website yetu /www wingulamashahidi org/ kwa mafundisho ya ziada.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! SISI NI WAFALME NA MAKUHANI KWA NAMNA GANI?

BIBLIA INASEMA “HAMJUI YA KUWA MTAWAHUKUMU MALAIKA? (1WAKORINTHO 6:2-3) ” TUTAWAHUKUMUJE?.

NADHIRI.

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.


Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments