JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?

by Admin | 2 October 2019 08:46 pm10

Hakuna mahali popote Biblia imerekodi kifo cha Mariamu, wala  hakuna  mahali popote Biblia imerekodi kifo cha Mtume Petro, wala Yusufu mume wake Mariamu, wala Mtume Paulo, wala Mtume Adrea wala Tomaso, Nathanieli, n.k…manabii wengi sana na mitume vifo vyao havijarekodiwa kwenye Biblia takatifu..

Na ni kwanini biblia havijarekodi vifo vya hawa watu, ni kwasababu sio vitu vya muhimu sana kuvijua kwetu sisi…Inatusaidia nini sisi kujua Petro alikufa mwaka gani? au mwezi gani?.. unaona haitusaidii chochote! Lakini tunajua kuwa Petro alikufa, Paulo alikufa, Yusufu alikufa…kadhalika na Bikira Mariamu alikufa vile vile.

Mariamu hakuwa mtu wa tofauti sana na watu wengine…Eliya ambaye hakufa bali  alipaa, Biblia inamtaja kuwa mtu wa mwenye tabia sawa na sisi, (soma Yakobo 5:17) itakuwaje Mariamu ambaye hakupaa?..Ni mmoja tu ndiye aliyekuwa wa kipekee ambaye biblia inasema alikufa na kufufuka na akapaa mbinguni, na huyo ni Yesu Pekee yake, ndio maana wokovu upo kwake. Kulikuwa hakuna haja ya kuja Bwana Yesu kama Mariamu alikuwa na wokovu .

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Mariamu alikufa kama watu wengine.


Mada Nyinginezo:

JE MARIAMU NI NANI?

JE! NI SAHIHI KUMUITA MARIA MAMA WA MUNGU?

JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?

KWANINI MUNGU AWACHOME WATU KWENYE ZIWA LA MOTO NA HALI YEYE NDIYE ALIYEWAUMBA?


Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/10/02/je-bikira-mariamu-alikufa/