Kuna Malaika wangapi?

by Admin | 10 October 2019 08:46 pm10

Biblia haijataja kuna idadi gani ya Malaika walioko mbinguni…Lakini tukisoma Biblia tunaweza kujua au kupata picha kuwa kuna idadi kubwa kiasi gani ya Malaika walioko mbinguni..

Kama maandiko yanasema katika…

Mathayo 18:10 “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni”.

Mstari huo unatuonesha kwamba kila mtu aliyezaliwa mara ya Pili, anaye malaika wake akimlinda, akipeleka habari zake njema mbele za Mungu, na akimsaidia katika Kuishikilia Imani.

Sasa hebu fikiri endapo watu wote wangempa Kristo maisha yao, ina maana kila mtu angekuwa na angalau malaika mmoja.

Hivyo mbingu haiwezi kuwa na watenda kazi wachache wa kutuhudumia sisi kiasi kwamba kuna wanadamu wanaweza kukosa Malaika wa kuwahudumia. (Malaika wa Mungu watakaa mbali nasi endapo tu tutakuwa tunajitia unajisi na dhambi), lakini sio kwamba kuna idadi ndogo….Kwahiyo kama wanadamu duniani leo tupo Bilioni 7, basi Malaika ni wengi zaidi ya hiyo idadi…Hivyo unaweza kuona ni jeshi kubwa kiasi gani lililopo mbinguni.

Na Biblia pia inaonesha wazi kwamba inawezekana mtu kutembea na Malaika zaidi ya mmoja.. Soma (2Wafalme 6:16-17).


Mada Nyinginezo:

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.

JE! MBINGUNI KUNA MALAIKA WA KIKE?. NA JE! TUKIFIKA MBINGUNI TUTAFANANA WOTE?


Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/10/10/kuna-malaika-wangapi/