Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

by Admin | 10 October 2020 08:46 pm10

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi?


Mlima Gerizimu ni mlima unaopatikana katika mji wa Samaria Israeli, unatazamana uso kwa uso na mlima Ebali, tazama picha juu, milima hii miwili ilikuwa maarufu kwa wana wa Israeli kukutanika kwa ajili ya kufanya sherehe ya kujikumbusha juu ya Baraka na laana katika Torati waliopewa na Mungu.

Kwani walipokuwa Jangwani Musa aliwaagiza watakapovuka Yordani na kufika katika nchi ya ahadi, watue katika milima hii miwili, kisha watafute mawe mawili makubwa, kisha waiandike Torati yote waliyopewa juu ya mawe hayo, kisha Nusu ya wana wa Israeli watasimama juu ya mlima Gezirimu na Nusu yake watakuwa upande wa pili juu ya mlima Ebali, na hapo katikati kwenye bonde watasimama makuhani na sanduku la Agano, na madhabahu ya mawe ambayo watakuwa wameitengeneza, kisha Walawi watazisoma  Baraka na Laana zote zilizoandikwa kwenye torati, sasa pindi wana walawi wanazisoma Baraka, ile nusu ya kwanza iliyo katika mlima Gerizimu watajibu wa kusema Amen( yaani Na iwe hivyo), mpaka watakapomaliza, na wakati wanazisoma Laana, vilevile ile nusu ya pili iliyo katika mlima Ebali, watajibu kwa kusema nao Amen(Na iwe hivyo). Kwa urefu wa habari hiyo soma Kumbukumbu 27 yote.

gerizimu na ebali

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyoijata milima hiyo miwili.

Kumbukumbu 11: 29 “Tena itakuwa, atakapokuleta Bwana, Mungu wako, na kukutia katika nchi uendeayo kuimiliki, ndipo uiweke baraka juu ya mlima wa Gerizimu, na laana uiweke juu ya mlima wa Ebali”.

Kumbukumbu 27:12 “Hawa na wasimame juu ya mlima wa Gerizimu kwa kuwabarikia watu, mkiisha vuka Yordani; Simeoni, na Lawi, na Yuda, na Isakari, na Yusufu, na Benyamini”;

Tunaona kweli siku walipovuka Yordani, Yoshua alilitekeleza agizo hilo la Musa, na kufanya kama alivyoagizwa. Tunasoma hilo katika;

Yoshua 8:33 “Na Israeli wote, na wazee wao, na maakida yao, na makadhi yao, wakasimama upande huu wa sanduku na upande huu, mbele ya makuhani Walawi, waliolichukua sanduku la agano la Bwana, huyo aliyekuwa mgeni pamoja na huyo mzalia; nusu yao mbele ya mlima Gerizimu, na nusu yao mbele ya mlima Ebali, kama Musa, mtumishi wa Bwana, alivyoamuru, ili wawabarikie watu wa Israeli kwanza”.

Mlima huu Gerizimu ulikuja kujulikana kama mlima wa Baraka.

Je! Milima hii katika agano jipya iliitwaje?

Japokuwa katika agano haijatajwa moja kwa moja, lakini mlima Gerizimu unadhiniwa kuwa ndio mlima ule, uliotajwa na Yule mwanamke msamaria, pale alipomwambia Bwana maneno haya;

Yohana 4:20 “Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia”.

Unaona Wasamaria bado waliendelea kuadhimisha mlima huu wa Gerizimu, kama mlima mtakatifu wa kuabudia, na kupokea Baraka kwa Mungu, lakini Yesu alimwambia milima au ma-hakalu hayana umuhimu tena katika kumtolea Mungu ibada ya kweli kwani ilikuwa ni kivuli tu cha mambo ya agano jipya.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa mlima Gerizimu, na Ebali ni milima iliyotumika kwa ajili ya sherehe ya kubariki, na vilevile kutoa laana kwa wavunjaji Torati.

Milima hii hata sasa rohoni inasimama, kwa wale wanamcha Mungu, Baraka za Neno la Mungu zitawafuata, kwani Mungu anawaweka katika gerizimu ya rohoni, lakini wale wasio mcha Mungu vilevile laana za Neno la Mungu ambao ni upanga, zitawafuata, kwani rohoni wanakuwa wamewekwa juu ya mlima Ebali,

Na kumcha Mungu kunaanza na kuokoka, kama hujaokoka, basi laana ipo tayari juu yako, Hivyo kama na wewe upo tayari leo kumpa Yesu maisha yako ayaokoe. Basi uamuzi huo ni wa busara sana kwako, hivyo fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

Israeli ipo bara gani?

Mkomamanga ni nini? Na katika biblia unawakilisha nini?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/10/10/mlima-gerizimu-na-ebali-ni-ipi-na-umuhimu-wao-rohoni-ni-upi/