BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

by Admin | 23 December 2020 08:46 pm12

Zamani  enzi za biblia  Njia kuu ya mfalme, ilikuwa ni njia iliyotengenezwa mahususi kuunganisha mataifa mengi na miji mingi, na lengo lilikuwa ni kurahisisha shughuli za kibiashara na usafirishaji katikati ya mataifa hayo wana chama., njia hiyo ilitoka Misri, na  kupita Yordani, na moja kwa moja mpaka Nchi ya Syria, ..Ilikuwa ni maarufu kwa mataifa mengi sana zamani zile,

Hivyo Safari katika barabara hii ilikuwa ni uhakika kwasababu vizuizi vyote vya  barabarani vilidhibitiwa, palipokuwa na mito paliwekwa madaraja, palipokuwa na mabonde palisawazishwa, hivyo mtu yeyote aliyesafiri kwa njia hii safari yake ilikuwa ni ya uhakika na ya kuchukua muda mfupi sana kulinganisha na mtu aliyesafiri kupitia njia nyingine.

Kama tu vile leo hii tunavyoiona ile  “barabara kuu ya kaskazini”  almaarufu kama (The great north Road) ambayo inatoka Cape town kule Afrika ya kusini na kwenda moja kwa moja mpaka  Cairo Misri Afrika ya kaskazini.  Barabara hii imekatiza pia katika nchi ya Tanzania Dodoma-babati  na nchi ya  Kenya.  Na lengo la kuwekwa barabara hii ni sababu zilezile za kibiashara na kimaendeleo. Hivyo mtu akitaka kusafiri kutoka Kaskazini mwa Afrika kwenda Kusini, kwa miguu au kwa gari akipitia barabarani hii, basi safari  ni ya uhakika, na salama bila kukutana na kipingamizi chochote njiani.

Sasa Tukirudi katika biblia wakati wana wa Israeli walipokuwa jangwani wakiendelea katika safari yao kuelekea nchi ya ahadi, tunaona walipita katika na mji wa Edomu,(kwa sasa ni kusini mwa Yordani) walipofika katika taifa lile wakawaomba wapite katikati yao kuifauata sasa hii njia kuu ya mfalme.. Lakini kama tunavyosoma Waedomi, waliwakatalia, wakawatishia kupigana nao, hivyo ikawabidi wana wa Israeli wapitie njia nyingine ndefu zaidi ili kuwazunguka waendelee na safari yao.

Hesabu 20:17 “tafadhali utupe ruhusa tupite katika nchi yako; hatutapita katika mashamba, wala katika mashamba ya mizabibu, wala hatutakunywa maji ya visimani; TUTAIFUATA NJIA KUU YA MFALME, tusigeuke kwenda upande wa kuume, wala upande wa kushoto, hata tutakapopita mpaka wako.

18 Edomu akamwambia, Hutapita katika nchi yangu, nisije nikakutokea kupigana nawe kwa upanga.

19 Wana wa Israeli wakamwambia, Tutakwea kwa njia kuu; tena kama tukinywa maji yako, mimi na wanyama wangu wa mifugo, ndipo nitakulipa thamani yake; nipe ruhusa nipite kwa miguu yangu wala sitaki neno lingine lo lote.

20 Akamwambia, Hutapita katika nchi yangu. Kisha Edomu akamtokea ili kupigana naye, na watu wengi, na kwa mkono wa nguvu.

21 Basi hivyo Edomu akakataa kumpa Israeli ruhusa kupita katika mipaka yake; kwa hivyo Israeli akageuka na kumwacha.

22 Kisha wakasafiri kutoka Kadeshi; wana wa Israeli, mkutano mzima, wakafikilia mlima wa Hori”.

Tunaona tena walipofika mbele tena kidogo, walikutana na watu wa taifa lingine walioitwa Waamori, na wao pia wakawaomba wapite  kuifuata hiyo  njia kuu ya mfalme, wakiahidi kuwa hawatachukua chochote au kuleta dhara lolote katika nchi yao,. Lakini mfalme wa Waamori akawakatalia na zaidi ya yote akapanga vita kupigana nao, lakini walipigwa na kutekwa nyara mji wao wote.

Hesabu 21:22 “Nipe ruhusa nipite katika nchi yako; hatutageuka kando kwenda mashambani, wala kuingia katika mashamba ya mizabibu hatutakunywa maji ya visimani; TUTAKWENDA KWA NJIA KUU YA MFALME, hata tutakapokuwa tumepita mpaka wako.

23 Lakini Sihoni hakukubali kumwacha Israeli kupita katika mpaka wake; bali Sihoni akawakutanisha watu wake wote, akatoka aende kupigana na Israeli jangwani, akafika mpaka Yahasa; akapigana na Israeli.

24 Israeli wakampiga kwa makali ya upanga, na kuimiliki nchi yake, tangu mto wa Arnoni hata mto wa Yaboki, mpaka nchi ya wana wa Amoni; kwa kuwa mpaka wa wana wa Amoni ulikuwa una nguvu”.

Unaona? Unaweza ukajiuliza swali moja, pamoja na kwamba walikuwa wanafukuzwa lakini hawakuchoka kuitafuta njia kuu ya mfalme? Hiyo yote Ni kwasababu walijua urahisi na wepesi uliopo kwa kuifuata njia ile, hajalishi kuwa maadui wengi kiasi gani walisimama katikati yao kuwazuia. Waliitafuta kwa bidii hii njia kuu ya mfalme.

Tunapata fundisho gani?

Kumbuka Agano la kale ni kivuli cha mambo yanayoendelea katika agano jipya.

Hata sasa ipo njia kuu ya mfalme mmoja ambayo inaunganisha dunia na mbingu. Kaisi kwamba mtu akiifuata njia hiyo, uhakika kwa kufika mbinguni upo bila vizuizi vyovyote hapa katikati kwani, tayari imeshatengenezwa, na hukakikishwa. Na njia yenyewe ni YESU KRISTO.

Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, MIMI NDIMI NJIA, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”.

Hakuna njia nyingine yoyote ya kando kando itakayokufikisha mbinguni ikiwa utaikataa hii ya Yesu Kristo, mtu yeyote anayejiita mtume hawezi kukufikisha mbinguni, dini yoyote haiwezi kukufikisha mbinguni, wala raisi, au kiongozi yoyote ya kiimani, anayeweza kukufikisha mbinguni. Ni Yesu tu peke yake, Ukimwamini yeye, ukamtii na ukamfuata, uhakika wa kumuona Mungu ni asilimia zote. Hivyo mkaribishe leo maishani mwako uanze kupita juu ya njia hii kuu moja ya uhakika. Nyingine zote zitakupoteza ndugu yangu.

Utatumia gharama kubwa, utatoa jasho jingi, lakini mwisho wa siku utapotea. Kwasababu safari hii ya hapa duniani ni ndefu, yenye mabonde mengi, na milima mingi, yenye utelezi mwingi, na miiba mingi njiani, hivyo utahitaji NJJIA moja tu ya uhakika ya iliyounganika bila kukatika katika ili kukufikisha kule ng’ambo na hiyo ni Yesu tu peke yake.

HUO NDIO UKWELI PEKEE ULIODUMU DUNIANI KWA WAKATI WOTE.

Hivyo Ikiwa utapenda kumpa Yesu leo maisha yako, basi fungua hapa kwa maelekezo ya sala ya Toba >>> SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312 Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

MAMA UNALILIA NINI?

JIFUNZE KUTOA KATIKA HAZINA YAKO VITU VIPYA NA VYA KALE.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/12/23/biblia-inaitaja-njia-kuu-ya-mfalme-njia-hii-ni-ipi/