Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

SWALI: Naomba nifahamishwe mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?


JIBU: Si kweli, Nguvu za giza huwa hazichagua, hali ya mtu ya kimaisha, zinawavaa matajiri vilevile vinawavaa maskini, zinawavaa wanaume, zinawavaa wanawake, zinawatesa watoto (Marko 9:21), vilevile zinawaathiri mpaka wanyama (Soma Mathayo 8:31 )..Kwasababu kazi ya shetani sikuzote ni kuuharibu mpango mzima wa Mungu kwa viumbe vyake vyote.

Hivyo usidanganyike kuwa matajiri hawawezi kuwa na mapepo, huwenda ni kwasababu wewe hujakutana na visa hivyo, lakini vipo vingi. Pia katika maandiko walikuwepo matajiri ambao walisumbuliwa na mapepo.

Soma..

Luka 8:1  “Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye,

2  na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3  na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao”

Umeona hapo, Hao wanawake wanaotajwa wote walikuwa ni matajiri, hakuna maskini, tukianzia na huyo Mariamu Magdalena, ambaye alitoa marhamu yake yenye thamani ya mamilioni ya pesa akammwagia Kristo miguuni pake, mpaka kwa Yoana mkewe Kuza, wakili wa Herode.

Mawakili kwa zamani ni sawa tu na mawaziri wakuu na wakuu wa majeshi  sasahivi, hivyo huyu mke wa waziri mkuu alikuwa akimfuata Yesu, huwezi kusema ni maskini, alikuwa tajiri na wanawake wengine hapo wakitajwa walikuwa wakimuhudumia kwa mali zao.

Hivyo, hakuna mtu aliye na ofa kwa Mungu au kwa shetani, kwasababu ya hali yake ya kimaisha. Sote tunahitaji wokovu, tunahitaji msaada kwa Kristo sawasawa, tunahitaji kufunguliwa na yeye.

Tahadhari:

Epuka  mahubiri yanayopigia kampeni utajiri, ambayo ndio yanayoendelea sikuhizi za mwisho kana kwamba ndio uhai wa mtu ulipo, yatakupoteza. Mkimbilie Kristo akupe uzima wa milele.

Efatha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini kuna watu wanafanyiwa deliverance (Maombi ya kufunguliwa), lakini baada ya muda wanarudiwa tena na hali ile ile sababu ni nini?

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 4)

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments