NINYI AKINA BABA MSIWACHOKOZE WATOTO WENU

by Admin | 6 April 2023 08:46 am04

Majukumu ya Mzazi ni kumlea mtoto katika njia inayompasa, kwasababu hekima ya Mungu inasema, hataiacha njia hiyo hata atakapokuwa mzee.

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”

Lakini pamoja na kumlea mtoto katika njia impasayo ya kiMungu, mzazi pia hapaswi kumchokoza mwanae sawasawa na maandiko yafuatayo…

Waefeso 6:4  “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana”.

Wakolosai 3:21 “Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa”

Sasa utauliza nini maana ya kuchokoza?

Kuchokoza kama ilivyotumika hapo, ni “kitendo cha kumfanya mtoto awake hasira, pasipo kuwa na sababu ya msingi”

Na baadhi ya sababu hizo ambazo zinaweza kumfanya mtoto awake hasira, hata kufikia hatua ya kukata tamaa au kufanya dhambi  kama za kutoa maneno mabaya mdomoni au moyoni..ni kama zifuatazo.

1.Ukali wa mzazi uliopitiliza.

Mzazi anapokuwa mtu wa kufoka mara kwa mara, na kushutumu kwa ukali mambo yasiyo na mashiko ni rahisi kumfanya mtoto akate tamaa au awake hasira, na kitendo hicho kibiblia kinatafsirika kama “Mzazi kamchokoza mwanae”.

2. Kumwadhibu mtoto mara kwa mara bila kuwa na sababu ya msingi.

Wapo wazazi ambao mtoto akifanya kosa dogo tu, tayari wamekamata kiboko na kutoa adhabu kali. Ni lazima mzazi apime kosa, kama linastahili adhabu au linastahili kuonya tu!.. Lakini sio kila kosa hukumu yake iwe viboko!. Hilo linaweza kumfanya mtoto achukizwe sana badala ya kujengeka, na kibiblia ikahesabika kama umemchokoza mwanao na si kumjenga.

3. Kumdhalilisha mtoto

Wapo wazazi wasiowatia moyo watoto wao, badala yake wanawadhalilisha mbele ya watoto wenzao, au mbele ya jamii.. Jambo kama hili pia kibiblia linatafsirika kama mzazi kamchokoza mwanae.

Tunapaswa siku zote kuwathaminisha watoto wetu mbele ya watoto wengine, vile vile kuwatia moyo katika mambo mazuri wanayoyafanya.

Na wazazi wengi hawajui kama wanawachokoza watoto wao, na kuwaharibu utu wao wa ndani kwa ukali wao.

Hivyo kama mzazi, zingatia mambo hayo (Usiwachokoze watoto wako) na Bwana atakubariki na vile vile kuwabariki watoto wako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2023/04/06/ninyi-akina-baba-msiwachokoze-watoto-wenu/