Mistari ya biblia kuhusu maombi.

by Nuru ya Upendo | 30 January 2024 08:46 am01

Ifuatayo ni mistari michache ya biblia inayohusu maombi.


Zekaria 10:1 “Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni.”

Mathayo 7:7 “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;

8  kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.”

Marko 13:33 “Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo”

Luka 22:40 “ Alipofika mahali pale aliwaambia, Ombeni kwamba msiingie majaribuni.”

Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.”

Yohana 16:24 “Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu”

Wafilipi 4:6 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu”.

Marko 11:24  “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu”.

Wakolosai 4:2 “Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani”

Waefeso 6:18  “kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote”

1Wathesalonike 5:17 “ombeni bila kukoma;”

1Yohana 5:14  “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia”.

1Timotheo 2:1 “Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote”

Yakobo 5:16  “Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii”

Kwa mwongozo wa maombi ya kujikuza kiroho  fungua hapa >> MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.[1]

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10[2]

Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,[3]

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.[4]

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU BARAKA[5]

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.[6]

IFAHAMU FAIDA YA KUMKIRI KRISTO UKIWA HAPA DUNIANI.[7]

Rudi nyumbani[8]

WhatsApp
DOWNLOAD PDF
Endnotes:
  1. MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.: https://wingulamashahidi.org/2023/12/08/mwongozo-wa-maombi-ya-kujikuza-kiroho/
  2. https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10: https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
  3. Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,: https://wingulamashahidi.org/2022/12/01/nijapokuwa-sipo-kwa-mwili-lakini-nipo-pamoja-nanyi-kwa-roho/
  4. MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.: https://wingulamashahidi.org/2020/08/06/mistari-ya-biblia-kuhusu-ndoa/
  5. MISTARI YA BIBLIA KUHUSU BARAKA: https://wingulamashahidi.org/2023/03/10/mistari-ya-biblia-kuhusu-baraka/
  6. MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.: https://wingulamashahidi.org/2020/09/04/mistari-ya-biblia-ya-faraja/
  7. IFAHAMU FAIDA YA KUMKIRI KRISTO UKIWA HAPA DUNIANI.: https://wingulamashahidi.org/2023/10/30/ifahamu-faida-ya-kumkiri-kristo-ukiwa-hapa-duniani/
  8. Rudi nyumbani: https://wingulamashahidi.org

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/01/30/mistari-ya-biblia-kuhusu-maombi/