by Nuru ya Upendo | 10 August 2025 08:46 pm08
Kitabu hicho hakijafunua jina la mwandishi wake moja kwa moja kama baadhi ya vitabu vingine vinavyofunua..Hivyo kwa kuwa hakina uthibitisho wowote wa jina la mwandishi, miongoni mwa wayahudi na wakristo wengi, kumekuwa Na mitazamo tofauti tofauti juu ya muhusika wa uandishi ule.
Baadhi husema ni mordakai, wengine husema ni Ezra, wengine Nehemia na wengine myahudi fulani ambaye alikuwa na uelewa mzuri wa kihistoria katika dola uajemi wakati ule.
Lakini uzito mkubwa umewekwa kwa Mordekai, kutokana na habari zake kuchukua sehemu kubwa katika kitabu hichi.
Lakini pia maneno Yake mwenyewe kunukuliwa katika kitabu hichi; kuonyesha kuwa yamkini ni yeye ndiye mwandishi wa kitabu hichi.
Esta 9:20-21
[20]Basi Mordekai aliyaandika mambo hayo; naye akapeleka barua kwa Wayahudi wote waliokaa katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero, waliokuwa karibu na waliokuwa mbali,
[21]kuwaonya wazishike siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, na siku ya kumi na tano yake, mwaka kwa mwaka,
Lakini pia upatikanaji wa taarifa za ndani ya kwenye jumba la kifalme, mfano karamu za kifalme, hukumu zao, sasa taarifa kama hizi ni wazi kuwa hujulikana na watu walio karibu na ikulu za kifalme, mfano wa Mordakai ambaye alikuwa mfungua malango (Esta 2:19,21)
Lakini pia Kuhifadhiwa Kwa kumbukumbu ya sikukuu ya Purimu (Esta 9: 29-32).
Kwani kitabu kinaonyesha kuwa yeye ndiye aliyesambaza habari…hivyo ni sawa kufikiri pia habari hizo angetaka zihifadhiwe Hata katika vizazi vijavyo vya mbeleni, ambazo ndio hizi mpaka sasa tunazisoma.
Esta 9:29-31
[29]Ndipo malkia Esta, binti Abihaili, pamoja na Mordekai Myahudi, alipoandika kwa mamlaka yote kuithibitisha barua hii ya pili ya Purimu.
[30]Akapeleka barua kwa Wayahudi wote katika majimbo yote mia na ishirini na saba ya ufalme wake Ahasuero, maneno ya amani na kweli,
[31]ili kuzithibitisha siku hizo za Purimu kwa majira yake, kama Mordekai Myahudi na malkia Esta walivyoamuru, na kama walivyojiagizia juu yao wenyewe, na juu ya wazao wao, kwa habari ya kufunga na kilio.
Kwa hitimishi ni kubwa…awe ni Mordekai au mwingine yoyote, Lililo la msingi ni kufahamu agizo la Kristo lililo nyuma ya kitabu hichi.
Hivyo kwa msaada wa uchambuzi wa mafundisho kadha wa kadha yaliyo katika kitabu hichi..basi fungua hapa uweze kujifunza.. >>>
Mabibi wastahiki walikuwa ni watu gani? (Esta 1:18).
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?.
Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote” (1Petro 5:10)
Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/08/10/kitabu-cha-esta-kiliandikwa-na-nani/
Copyright ©2025 Wingu la Mashahidi unless otherwise noted.