by Janet Mushi | 18 September 2025 08:46 pm09
Sauli (Mtume Paulo) alipokuwa anaelekea Dameski kwa lengo la kuwafunga na kuwatesa watakatifu, kama tunavyoifahamu habari alitokewa na Yesu njiani, mwanga Mkali ulimpiga machoni, akashindwa kuona, Wakamchukua mpaka ndani ya mji akiwa kipofu.
Lakini tunaona alipokuwa kule, hakuwa katika hali ya kawaida, bali katika maombolezo makubwa rohoni, hakula chakula chochote, wala maji..(maana Yake alikuwa katika mfungo), lakini si hilo tu zaidi sana alikuwa akiomba dua.
Baada ya hapo tunaona jambo lingine likitokea mtu mmoja aliyeitwa Anania anatokewa na Yesu, kisha anaagizwa amfuate Paulo. Lakini eneo analoagizwa ni katika njia iliyoitwa NYOFU…
Maana Yake “njia iliyonyoka”.
Matendo 9:8-12
[8]Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski.
[9]Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi.
[10]Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana.
[11]Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba;
[12]naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.
Unaweza kujiuliza kwanini apelekwe njia ile ..tena iitwe kwa jina la NYOFU na si lingine labda “njia kuu”, au “nzuri” au “panda” bali nyofu?
Ni kwasababu rohoni, Kristo huwaweka watu wake Katika hiyo njia. Njia iliyonyoka.
Hapo mwanzo Paulo alikuwa katika njia iliyoharibika, mbovu, ya kuupinga ukristo, ya uuaji, ya utukanaji, ya dhambi, ya mauti.
Lakini alipokutana na YESU, akatolewa huko akawekwa katika njia iliyonyooka ya utumishi wake.
Ni ajabu kuona watu wengi leo wanampinga Kristo, hawataki kuokoka, wakidhani udini ndio utawanyooshea mapito yao, fedha ndio zitawasawazishia mabonde Yao, elimu ndio zitaangusha milima yao.
Kumbe hawajui kuwa njia iliyonyooka ni maisha ndani ya Kristo tu!. Kwingine kote ni mabonde, milima Na mwishowe shimoni na mauti. Hakuna pumziko Nje ya Kristo.
Yohana mbatizaji aliliona hilo akapaza sauti yake kwa nguvu Akisema..
Yohana 1:23
[23]Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena nabii Isaya.
Kumwamini Yesu ndio kuinyoshe njia ya Bwana..
Je upo katika njia ya nyofu.
Okoka leo, uponywe kila kitu ndugu, kumbuka Umepotea nje ya Kristo,hakuna mjadala na huo ndio ukweli, hakuna tegemeo kama Yesu hajakuokoa. Fanya haraka utubu, leo uiamini kazi ya Kristo ya ukombozi iliyokamilishwa kwa ajili yako pale msalabani. Muda ni mchache mlango wa neema hautadumu Milele.
Ikiwa upo tayari leo kumkabidhi Yesu maisha yako. Basi bofya bofya hapa kwa mwongozo wa sala ya toba. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/09/18/katika-njia-iitwayo-nyofu/
Copyright ©2025 Wingu la Mashahidi unless otherwise noted.