14 ambaye katika yeye TUNA UKOMBOZI yaani, MSAMAHA WA DHAMBI”.
Tusome tena Waefeso 1:7..
Waefeso 1:7 “Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao UKOMBOZI WETU, MASAMAHA YA DHAMBI, sawasawa na wingi wa neema yake”.
Kumbe! Maana ya “Ukombozi” ni “MSAMAHA WA DHAMBI”.
Kwamba Tunapopata Msamaha wa dhambi zetu, tunakuwa tumekombolewa na tena tumeokolewa na Nguvu za giza, na kuingizwa katika ufalme wa Mwana wa Pendo lake?.
Hivyo maombi makuu ya Ukombozi ni maombi ya Toba!, kwasababu tunapoomba Toba na kusamehewa katika roho tumepata ukombozi, jambo ambalo ni kuu sana.
Je umemwamini Bwana YESU na kutubu dhambi zako ili upate msamaha wa dhambi??..
Fahamu kuwa hakuna maombi yoyote ya ukombozi zaidi ya yale ya KUTUBU DHAMBI kwa kumaanisha kuziacha kwasababu adui wa kwanza wa mtu ni dhambi ikaayo ndani yake.
Hiyo ndio inayomfunga mtu, na kumharibia njia yake duniani, na njia pekee ya mtu kukombolewa na laana, vifungo, mikosi na kila aina ya vifungo ni kwa njia ya kutubu dhambi.
Ukitaka ndoa yako ikombolewe, tubu na acha uzinzi unaoufanya nje ya ndoa, kama unafanya hayo, hapo ukombozi wa ndoa utazalika wenyewe.
Ukitaka ukombozi wa kazi yako, watoto wako, na mambo yako yote suluhisho ni kutubu na kupata msamaha wa dhambi!.
Lakini tukiikwepa toba na kujitumainisha katika maombi ya kuombewa na kuvunjiwa laana, hakuna ukombozi wowote tutakaopata na hiyo ni Biblia sio theolojia wala mapokeo..
Tubu dhambi leo upate ukombozi, na ufurahie wema wa MUNGU.
Bwana akubariki.