MPE MUNGU MAJUTO YAKO.

by Nuru ya Upendo | 20 January 2026 08:46 pm01

Kila mwanadamu maadamu amezaliwa na kuishi duniani, ndani yake lazima kuna kiwango tu cha majuto..

Wengine wana majuto makubwa sana, wengine kiasi.

Majuto ni hali ya kuhuzunishwa na matokeo ya machaguzi au maamuzi yaliyofanyika katika maisha.

Kwamfano kijana anaweza kuchagua kukatisha masomo kisha aende mtaani, kuuza peremende, sasa hayo ni maamuzi yake, lakini baadaye anapoona haoni matokeo makubwa, kinyume chake anawaona wenzake waliosoma wamepiga hatua kubwa anaanza kuingiwa na huzuni ya kujishitaki mwenyewe, sasa hayo ndio majuto.

Mwingine amechagua kuishi na mtu bila kufunga naye ndoa, hatimaye akazalishwa, watoto wengi na kuachwa..baadaye umri umeenda anataka kuoelewa, inakuwa shida…anaingiwa na majuto.

Mwingine amepoteza miaka mingi duniani kumtumikia shetani, sasa ameshakuwa mzee anajisikitikiza miaka yake ya ujana aliyoipoteza yenye nguvu alikuwa wapi asimtumikie Mungu…

Majuto yapo ya namna nyingi, na kila mtu kwa sehemu yake anayo majuto fulani, haijalishi unaishi wapi, au umefanikiwa vipi…kuna mahali ulikosea na yakaingia..

Kimsingi majuto sio dhambi, ni hali ya ki-Mungu kabisa ambayo mwanadamu ameumbiwa ndani yake..

Lakini ni vema kujua namna ya kuyaweka mahali pake..kwasababu yasipoweza kutenganishwa ipasavyo hupelekea hasara kubwa mno ndani ya maisha ya mtu.

Katika biblia kulikuwa na watu wawili ambao walihuzunishwa na maamuzi walillyoyafanya …mmoja ni Petro, mwingine ni Yuda.

 Yuda alihuzunishwa lakini huzuni yake ilimpelekea kujinyonga…Petro alihuzunishwa lakini huzuni yake ilipelekea kulilia msaada wa Mungu..(badiliko)

Petro aliruhusu majuto yake yabebwe na Mungu, Yuda aliruhusu yabebwe na shetani.

Lakini majuto yalikuwa yale yale…Yuda hakukosea kujuta hadi kurudisha pesa

2 Wakorintho 7:8-11

[8]Kwa sababu, ijapokuwa naliwahuzunisha kwa waraka ule, sijuti; hata ikiwa nalijuta, naona ya kwamba waraka ule uliwahuzunisha, ingawa ni kwa kitambo tu. 

[9]Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote. 

[10]Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti. 

[11]Maana, angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo. 

Umeona Majuto ya ki-Mungu huleta toba.. lakini majuto ya shetani hupelekea mauti..

Ukishaanza kujiona kama wewe huwezi tena, Mungu kakuacha, hufai, huna maana, hustahili, ujue shetani yupo nyuma ya juto hilo, ambalo anataka kukusababishia usiinuke tena, ujitenge, ujiue, uache kwenda kanisani, aache maombi, uache kumtafuta Mungu, uache uchungaji …

Kinyume chake unapokosea jione kama ulikuwa unapitishwa katika funzo ambalo sasa unapewa nafasi nyingine usiitmie vibaya…

Watu wengi, unaowaona wamekata tamaa, wamepoa, hawana mabadiliko tena, wamejitenga, lakini hapo zamani walikuwa vizuri, wana mashaka na hofu ya ndani kwa ndani, asilimia kubwa ni majuto mabaya yanawasonga ndani yao.

Daudi alipoanguka katika dhambi ya uzinzi, alimrudia Bwana kwelikweli, ijapokuwa ilimgharimu pakubwa…hakwenda kujificha na uso wa Mungu kama Adamu.

Lakini ya ki-Mungu huturudisha kumtazama Mungu…Rudi umwangalie Mungu wako kisha chukua hatua nyingine, kwani hiyo huwa na nguvu na matokeo ya haraka zaidi ya mwanzo.

Petro baada ya pale alikuwa na ujasiri mkubwa wa kumshuhudia Kristo, zaidi ya mitume wengine wote, ikiwa umefeli mahali fulani embu amka tena kwa nguvu, usikubali kunyong’onyea kama Yuda na mfalme Sauli ambaye alijiua..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUWA MWOMBOLEZAJI.

NI KIPI KINAKULEWESHA?

TUNASHINDA NA ZAIDI YA KUSHINDA

WhatsApp
DOWNLOAD PDF

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2026/01/20/mpe-mungu-majuto-yako/