Category Archive Uncategorized

Je! Paulo, alikuwa na injili yake tofauti na wengine?(Warumi 2:16)

SWALI: Je! Paulo, alikuwa na injili yake, tofauti na wengine?  sawasawa na (Warumi 2:16)

Warumi 2:16 katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu.


JIBU: Katika habari hiyo mtume Paulo hakumaanisha kwamba anayo injili nyingine ya kipekee tofauti na mitume wengine wa Kristo, na kwamba ya kwake tu  ndiyo Mungu atakayoitumia kuzihukumu siri za wanadamu.

Hapana mitume wote walikabidhiwa “injili moja”. Nayo ni kushuhudia wokovu ulioletwa duniani na mtu mmoja tu, ambaye ni YESU KRISTO, kwa lile tendo la kufa na kukufuka kwake kama fidia ya dhambi za ulimwengu, ambapo mtu akiamini basi amepokea ondoleo la dhambi na uzima wa milele. Na mtu yeyote ambaye hatamwamini huyu basi hukumu ya Mungu inakuwa juu yake.

Kwahiyo Paulo kama mmoja wa hao waliokabidhiwa injili hiyo, alikuwa na ujasiri kuwaeleza watu wale wa Rumi, kwamba kupitia injili yake hiyo sahihi, Mungu atawahukumu wanadamu, kwasababu anayehubiriwa ni Yesu Kristo. Ni sawa tu na Petro, au Yohana, au Yakobo, wangesema maneno kama hayo, wasingewezeka kupingana na Paulo kwasababu wanachokishuhudia wote ni kitu kimoja. Ndio maana tunaona maneno ya mitume wote, yameunganishwa katika kitabu kimoja kinachoitwa BIBLIA.

Lakini kwa nini Paulo aliongeze Neno hilo “sawasawa na injili yangu” Na asingeishia kwenye injili tu?.

Ni kwasababu wakati ule kulikuwa na watu waliomhubiri Yesu mwingine na injili nyingine, tofauti na ile waliyoihubiri mitume wa kweli.  Na hawa watu, wengi wao walikuwa ni  wayahudi wa tohara, Hivyo ilimbidi aliweke wazi hilo ili watu wabakie kwenye injili sahihi ya kweli.

Injili hizo Paulo aliziona kwenye makanisa kadha wa kadha kama tunavyosoma katika vifungu hivi;

2Wakorintho 11:4 Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!

Na..

Wagalatia 1:6 Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na

kugeukia injili ya namna nyingine. 7 Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo.

Umeona, hiyo ndio sababu ya Paulo na kule Rumi kuitamka kauli hiyo, “sawasawa na injili yangu”. Ili kuwapa ufahamu kuwa hizo nyingine wanazozisikia huko nje, hazina uhai wowote wa kumwokoa mtu, au kumtetea siku ile ya hukumu.

Hata sasa, mambo ni yale yale, kumekuwa na madhehebu mengi, imani nyingi, ambazo zote zinadai ni za kikristo, lakini ukiangalia uhalisia wake humwoni Kristo ndani yake, wala injili ya Kristo. Fundisho lililo mule ndani sio fundisho la mitume. Watu hawahubiriwi  tena toba ya kweli na kumwangalia Kristo kama kiini cha wokovu wao. Wanafundishwa mambo mengine kabisa wengine mafanikio, wengine  uchawi, wengine  miujiza n.k kama ndio utimilifu wa ukristo. Sasa mambo kama hayo, hayaweza kumtetea mtu siku ya hukumu.

Bali injili ya Yesu Kristo, kupitia mitume wake. Ambayo ni hii biblia tuliyonayo, ndio tunayopaswa tuiegemee, kwasababu katika hiyo ndio tutakayohukumiwa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

je! Paulo aliwalaani Wagalatia na Wakorintho?

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Rudi Nyumbani

Print this post

Silwano  ni nani,kama tunavyomsoma kwenye biblia?(1Petro 5:12)

Silwano ni matamshi mengine ya jina la Sila. Kwa kiyunani ni Sila, lakini kwa kilatino ni silwano. Hivyo Silwano ndio Sila yule tunayemsoma kwenye maandiko.

Habari ya Silwano/Sila hasaa tunaipata katika kitabu cha matendo ya mitume, huyu ni mmoja wa manabii wawili walioteuliwa na wazee wa kanisa la Yerusalemu kuambatana na Paulo na Barnaba katika kupeleka waraka wa makubaliano kwa makanisa ya mataifa.(Matendo 15:22).

Tunaona Sila na Yuda walipofika Antiokia, na kumaliza huduma yao, Yuda alirejea Yerusalemu, lakini Sila aliamua kuungana na Paulo katika ziara zake za kupeleka injili kwa mataifa.

Tunafahamu nini kuhusu Silwano/sila?

> Sila alipigwa na kufungwa pamoja na Paulo kule Filipi (Matendo 16:19-25).

> Sila anatajwa kama mwandishi mwenza wa kitabu cha Wathesalonike pamoja na Paulo(1&2 Wathesalonike 1:1).

 “Paulo, na Silwano, na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba, na

katika Bwana Yesu Kristo. Neema na iwe kwenu na amani.”

> Sila alihudumu Beroya.

Matendo ya Mitume 17:10

[10]Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi.

> Alihudumu pia   Makedonia,  na Korintho pamoja na Paulo na wakati mwingine Timotheo (Matendo 15-18)

> Silwano anatajwa kama mjumbe wa mtume Petro, kama mwandishi wa ile barua yake ya kwanza,

> Lakini pia anatajwa kama mtu mwaminifu.

1 Petro 5:12

[12]Kwa mkono wa Silwano, ndugu mwaminifu kama nionavyo, nimewaandikia kwa maneno machache, kuonya na kushuhudia ya kuwa hii ndiyo neema ya kweli ya Mungu. Simameni imara katika hiyo.

Tunajifunza nini kwa Sila?

Uaminifu  aliokuwa nao ambao ulionekana na kutajwa mpaka kwa mitume, ni uaminifu wa kuwa tayari kujitoa maisha yake kwa ajili ya kuitetea injili bila kujali gharama yoyote.

Sila tunamfananisha na Ruthu, ambaye alipoambiwa arejee nyumbani kwake akakataa , akajilazimisha kwenda na Naomi katika hali ya ajane, katika nchi ya ugenini.

Ndivyo ilivyokuwa kwa Sila alikuwa na uwezo wa kurudi Yerusalemu pamoja na Yuda, kuhudumu kule lakini akakubali kwenda kwenda katika dhiki na Paulo mataifani. Lakini taabu yake haikuwa bure, bali kazi yake inatambulika mpaka leo.

Sila amekuwa kama kiungo wa kanisa la kwanza pamoja na mitume , tangu wazee wa kanisa Yerusalemu, mpaka Petro hadi Paulo anaonekana akihudumu nao tofauti na washirika wengine wa mitume, walikuwa wakiambatana na mtume Fulani maalumu, mfano tukimwona Timotheo hatuoni popote akihudumu pamoja na Petro, lakini Sila alikuwa kiungo kotekote.

Bwana atupe moyo kama wa Sila. Tupelekwapo, tunajitoa kikamilifu kabisa kwa kufanya zaidi ya tunavyoagizwa..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?

ORODHA YA MITUME.

Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.

Rudi Nyumbani

Print this post

BWANA, SISI TUNATAKA KUMWONA YESU.

SWALI: Kwanini wale wayunani, walimfuata Filipo na kumwambia tunataka kumwona Yesu, maudhui  ya tukio lile ni nini, mpaka lirekodiwe?


JIBU: Kipindi cha Bwana Yesu hadi kipindi chote cha mitume, yalikuwepo makundi mawili ya watu ambayo yalijikita kwa umakini sana katika kutafuta uhalisia na ukweli wote kuhusu masuala ya Mungu.

kundi la kwanza lilikuwa ni wayahudi, na kundi la pili ni wayunani. Tofauti ya wayahudi na wayunani ni kwamba. Wayahudi walijikita kuthibitisha kwa njia ya ishara. Lakini wayunani kwa hekima.

1 Wakorintho 1:22-23

[22]Kwa sababu Wayahudi wanataka ishara, na Wayunani wanatafuta hekima;  [23]bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi;

Hivyo Yesu ambaye ni jibu lao wote alipokuja, baadhi ya hawa wayahudi walipomwona Kristo wakaanza kumthibitisha kwa ishara kwa walivyotarajia, kwamba ndiye masihi na mkombozi waliyemtarajia la!.(wakitaka wafanyiwe matendo fulani ya ajabu mbele ya macho yao, waamini)

Ijapokuwa Mungu hathibitishwi kwa ishara, bado Kristo aliwapa ishara.. Na ishara hiyo ilikuwa ni ile ya Yona. kukaa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana na hatimaye kutoka mzima.

Mathayo 12:38 Hapo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu, wakasema, Mwalimu, twataka kuona ishara kwako.

39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi.

Hilo lilipokuja kutimia…tunaona wayahudi wengi waliamini, ikiwemo mitume (akina Tomaso). Na ndio ukawa mwanzo wa kumuhubiri Yesu aliyefufuka.

Lakini wale waliotazamia ishara walizoziwaza kwa akili zao, mfano  za kushusha moto, kama Eliya, na kusahau ile ya kufufuka ambayo imezidi zote, bado Kristo akabakia kikwazo kwao.

Halikadhalika na kwa wayunani. Walimtafuta Mungu kwa njia ya hekima, ya elimu, ya maarifa, walimtafuta Mungu mwenye siri zote za uumbaji, na ujuzi, na utashi zaidi ya wanadamu wote na viumbe vyote.Ambaye atawazidi wanafalsa wao kama Plato, Socrates, Aristotle.

Kwa muda mrefu hawakufanikiwa mpaka baadhi yao, wakaishia kumwabudu tu, huku wakikiri hawamjui.

Matendo  17:22-23

[22]Paulo akasimama katikati ya Areopago, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini.

[23]Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua.

Yaani wakiwa na maana tunasikia miungu mingi,.lakini katika hiyo yote bado hatujaona mwenye hekima ya kuitwa Mungu wa ulimwengu. Wote akili zao ni kama za kibinadamu tu.

Sasa tukirudi kipindi cha Yesu, tunaona tukio jipya linajitokeza,

sio tu wayahudi walimwamini, bali hadi hawa wayunani watafuta-hekima wengi wao waliposikiliza maneno ya Yesu, na kupima kwa jicho la hekima, wakaona hakika hajawahi tokea anayeweza kuelezea ukweli wote wa uumbaji kama Yesu.

Hilo liliwashawishi na kuwafanya kukiri kuwa huyu ndiye suluhisho la utata wetu kuhusu Mungu na elimu.

Hivyo wakaamini, ndio sababu ya wao kumfata Filipo kumwomba wamwone Yesu. Hiyo ilikiwa ni heshima kubwa sana kwa Yesu  (kidini) mbele ya macho makuhani na mafarisayo wote, kwamba Mungu kathibitishwa kifalsafa. Kumbuka wayunani hawa waliokwenda hawakuwa watu tu wa kawaida. Bali ni watu wenye heshima ya juu sana na hadhi.

Hiyo ndio sababu Bwana Yesu  kusema saa imefika mwana wa  Adamu atukuzwe.

Yohana 12:20-26

[20]Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.

[21]Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu.

[22]Filipo akaenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu.

[23]Naye Yesu akawajibu, akasema, Saa imefika atukuzwe Mwana wa Adamu.

[24]Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.

[25]Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.

[26]Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.

Ni nini cha tunafundishwa katika habari hii ya wayunani?

Hata leo, Yesu anathibitika katika mambo yote endapo tu tutamaanisha kumwona katika namna hizo. Ndio maana katika makundi yote ya watu ni lazima utakuta waamini.

Katika ya wanasayansi utawaona, katikati ya wanajeshi utawaona, katikati ya watawala utawaona,katikati ya mamajusi utawaona, katikati ya  matajiri utawaona, katikati ya maskini utawaona, kati ya wanazuoni utawaona, kati ya madaktari utawaona,

Ukiuliza imekuwaje katika hali zao/ nafasi zao ambazo ni mbaya, na nyingine zenye majaribu, au zenye kumkana Mungu waziwazi, lakini wao wamemwamini Mungu?.

Ni kwasababu YESU anathibitika kila mahali.

Mtu kutokuamini ni yeye mwenyewe kataka. Hakuna atakayekuwa na udhuru siku ya mwisho, kwasababu Yesu amefunuliwa kila mahali.

Swali ni je! umemwamini Kristo?  kama ni la! unasubiri nini. Mwamini leo kwa kuikubali kazi aliyoikamilisha juu yako ya kuondoa dhambi kwa kifo na kufufuka kwake. Ambayo hiyo huambatana na toba ya kweli na ubatizo.

Baada ya hapo utakuwa umepokea ondoleo la dhambi zako bure, mpokee Yesu sasa

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani.

Utawanyiko wa Wayunani ulikuwaje?

ALIYOKUTANA NAYO YESU, YERIKO.

SAUTI NYUMA YA ISHARA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Biblia inamaana gani kusema ‘maana Mungu wetu ni moto ulao’ (Waebrania 12:29)

SWALI: Biblia inamaana gani kusema..maana Mungu wetu ni moto ulao?

Waebrania 12:29

[29]maana Mungu wetu ni moto ulao.

JIBU: Andiko hilo linaeleza sifa nyingine ya Mungu, kwamba si tu anajifananisha na maji, au nuru, au mafuta bali pia na “moto” tena ule “moto ulao”.

Kwanini aseme hivyo?

Ukianzia kusoma mistari ya juu utaona anaeleza  madhara ya kuikataa sauti ya Kristo, kwamba ghadhabu yake inapokuja huwa ni mbaya mfano tu wa ile ghadhabu aliyoidhihirisha kwa wana wa Israeli kule jangwani walipoasi.

Waebrania 12:25

[25]Angalieni msimkatae yeye anenaye. Maana ikiwa hawakuokoka wale waliomkataa yeye aliyewaonya juu ya nchi, zaidi sana hatutaokoka sisi tukijiepusha na yeye atuonyaye kutoka mbinguni;

Neno hili la moto ulao, mwandishi alilinukuu kwenye vifungu hivi vya agano la kale.

Kumbukumbu la Torati 4:23-24

[23]Jihadharini nafsi zenu, msije mkalisahau agano la BWANA, Mungu wenu, alilolifanya nanyi, mkajifanyia sanamu ya kuchonga, mfano wa umbo la kitu cho chote ulichokatazwa na BWANA, Mungu wenu,

[24]kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, ni moto ulao, Mungu mwenye wivu.

Mungu alijitambulisha kwa wana wa Israeli kwa sifa hii, ndio sababu hata mwanzoni kabisa alipomtokea Musa kule jangwani alijifunua kama kijiti kinachoungua lakini hakiteketei. Kufunua kuwa wakitembea katika njia zake moto wake hauwezi kuwala, hivyo wasiwe na hofu, bali utawalinda na kuwaimarisha,lakini wakiasi utawala hakika.

Moto huo ndio ule uliokuwa nguzo mbele yao kuwalinda. Na walipokosea waliadhibiwa kwa huo, wakaanguka watu wengi jangwani kwa yale mapigo tunayoyasoma.

Sasa tukirudi kwenye kitabu cha Waebrania. mwandishi anatoa angalizo pia kwamba tusiipuuzie sauti ya Mungu katika Kristo Yesu, kwasababu sasa hivi Mungu anazungumza na sisi moja kwa moja kutoka mbinguni, sio tena kwenye mahema au milimani,kama kule jangwani, hivyo tuongeze umakini

Tukikumbuka kuwa sifa zake ni zile zile…Yeye ni moto ulao hata sasa. Tunapofanya dhambi kwa makusudi tunapokengeuka na kudharau wokovu (Waebrania 6:4-8)…tuogope kwasababu moto wa wivu wake unaweza pita juu yetu, na kutuharibu kabisa, na kujikuta tupo katika ziwa la moto.

Lakini tunapotii, moto wake hautuharibu bali unatulinda na kutuimarisha..tunafananishwa na dhahabu, inayopitishwa kwenye moto kutakaswa.

Hivyo, maaana ya vifungu hivyo ni tunafahishwa kuwa Mungu ana sifa ya moto, tukilifahamu hilo tutautumiza wokovu wetu kwa kuogopa na kutetemeka. (Wafilipi 2:12). Wala hatutakwenda kutenda dhambi kwa makusudi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Biblia inamaana gani inaposema ‘tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao’?

Je ni Mungu au Malaika?

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Print this post

Wanawake wenye cheo ni akina nani? (Matendo 17:12)

SWALI: Wanawake wenye cheo wanaotajwa kwenye biblia ni akina nani? (Matendo 17:12)


JIBU: Mitume walipoanza kulitekeleza agizo kuu la Bwana Yesu la kuenenda ulimwenguni kote kuhubiri injili, biblia inatuonyesha walikutana na makundi mbalimbali ya walioamini.

Sasa mojawapo ya kundi hilo ambalo liliipokea injili, walikuwa ni hawa wanawake wenye cheo.

Kwamfano tunaweza kuona jambo hilo katika ziara ya mtume Paulo kule Beroya.. alipofika kule alikutana wa wanawake wa namna hii, na akawahubiria wakaipokea injili.

Matendo ya Mitume 17:10-12

[10]Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi.

[11]Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.

[12]Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa Kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache.

Wanawake wenye cheo ni wanawake waliokuwa na sifa ya aidha nafasi za juu za kiutalawa, au  ushawishi mkubwa kwenye jamii zao au wenye mali nyingi.

Wengi wao walipokutana na injili ya kweli ya Bwana Yesu Kristo waliipokea na kugeuka.

Lakini tunaona mahali pengine, mtume Paulo alipokwenda, wayahudi walimfanyia fitina kwa kuwatumia watu wa namna hii ili kuwataabisha..Kwamfano alipofika kule Antiokia mji wa Pisidia, na kuhubiri injili kwa ushujaa na wengi kuokoka. Wayahudi kwa sababu ya wivu wakawashawishi baadhi ya wanawake na wanaume wa namna hii..Ili wawapinge akina Paulo. Kwasababu walijua nguvu yao kijamii ni kubwa kiasi gani, hivyo itakuwa rahisi kutekeleza adhma yao.

Matendo ya Mitume 13:50

[50]Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao.

Hivyo hiyo ni kututhibitishia hata sasa, Watu wenye vyeo wana nafasi  ya kuwa washirika wa injili. Hivyo tusibague wa kumuhubiria,  kwasababu wote Kristo amewafia msalabani. awe ni mbunge, au waziri, awe ni tajiri, au maskini, msomi, au asiye na elimu,. wote ni wa Mungu na wanastahili wokovu, wasipotumiwa na Mungu wao, shetani atawatumia. Hivyo nguvu zetu za injili ziwe sawasawa kwa watu wote.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWANAMKE ABIGAILI ANAFUNZO GANI KWA WANAWAKE?

Apitaye cheo ni mtu wa namna gani?

Wale waliowekewa tayari ufalme ni akina nani?. (Mathayo 20:23).

Rudi Nyumbani

Print this post

Nguzo kuu za ukristo ni zipi?

Somo la nyuma tuliona msingi wa Ukristo ni nini.. kwamba Yesu Kristo Bwana wetu ndiye msingi  wenyewe..Yeye huitwa jiwe kuu la pembeni, na mwamba ambao juu yake sisi sote tumewekwa, pasipo Yesu hakuna ukristo. Yeye ndio msingi wa imani yetu.

Lakini pia kikawaida msingi ukishakaa chini, huwa nguzo zinafuata juu yake, kazi ya nguzo ni kulifanya jengo liweze kushikamana na kusimama vema toka juu kwenye paa mpaka chini kwenye msingi wenyewe.

Hivyo wewe kama mkristo ukishaweka msingi chini wa nyumba yako ya kiroho, fahamu pia moja kwa moja utanyanyua na nguzo zake, ili kuliunda jengo. Je nguzo zenye ni zipi?

Hizi ndizo nguzo kuu saba (7), za ukristo .

  1. UPENDO
  2. MAOMBI
  3. NENO
  4. USHIRIKA
  5. UTAKATIFU
  6. UINJILISTI
  7. UTOAJI

1.     UPENDO

Ni wajibu wa kila mwamini aliyekombolewa na Kristo, pindi tu alipookoka aanze kukua ki-upendo.  Hii ndio nguzo mama, kwasababu Mungu mwenyewe ni upendo (1Yohana 4:8). Zaidi sana anapaswa afahamu kuwa, upendo wa ki-Mungu sio kama ule wa kibinadamu

wa kupenda wanaokupenda, hapana ..huu ni upendo unaozidi usio na sharti wa kujitoa, ambao unapenda mpaka maadui, zaidi na kuwaombea wanaokuudhi.

Mtu asiyejijenga katika huu, haijalishi atajitaabisha vipi kwa Kristo, kazi yake itakuwa ni ya hasara siku ile ya mwisho.

1 Wakorintho 13 : 1-13

1 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.

2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi

cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.

3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama

sina upendo, hainifaidii kitu.

4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha,

zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.

2) MAOMBI

Ili   maisha ya mkristo yasimame vema, maombi ni nguzo nyingine inayomkamilisha. Biblia inasema maombi yanapaswa yawe ni jambo la daima.

Wakolosai 4:2 Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani;

Maombi ni sawa na maji mwilini, au mafuta kwenye gari, vikikosekana hivi vitu hakuna utendaji kazi wowote utakaoendelea, vivyo hivyo ukristo wako usipokuwa wa maombi, hautaendelea sana. Utakufa tu siku moja

Ili tujengeke vizuri kiwango cha chini Bwana alichotaka tuombe kwa siku ni saa moja (Mathayo 26:40). Bwana Yesu alikuwa mwombaji, mitume walikuwa waombaji, sisi yatupasaje?

3.     NENO (mafundisho)

Ukishaokoka, jambo linalofuata ni kuwa karibu na biblia yako. Katika hiyo utapata kuelewa mpango kamili wa Mungu katika maisha yako. Huku ukisaidiwa na waalimu na wakufunzi wako kwenye usomaji wako wa biblia, kama Bwana wetu Yesu alivyokuwa mdogo akifanya bidii kuwasikiliza waalimu wake.

Kujifunza na kusoma kunapaswa kuwe ni tendo la kila siku. Neno ni kama chakula na maombi ni maji. Hivi viwili ndivyo vinakukuza kiroho na kukujenga nafsi. Hupaswi kuacha kusoma.. Mkristo asiyeifungua biblia yake ni rahisi sana  kuchukuliwa na upepo wa ibilisi kwa mafundisho potofu. Kwasababu  hamjui Mungu.

Hekima, maarifa, imani, ufahamu,na  mamkala vinatoka katika kulijua Neno na mafundisho. Hivyo soma hiyo kila siku, pia sikiliza mafundisho kutoka kwa waalimu wako sahihi wa kweli, kwasababu ni muhimu sana kuvipata.

Matendo 2:41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.

42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.

1Timotheo 4:13 Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha

4.     USHIRIKA

Ushirika ni kukutana pamoja na wenzako kujengana. Ushirika ni umoja wa Roho katikati yetu.

Waebrania 10:25 wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.

Kama mtakatifu, hupaswi kujiaminisha utakuwa na utimilifu wote wa ki-Mungu ndani yako kivyako. Utahitaji kukamilishwa na wengine kwa sehemu baadhi, Ndio hapo suala la ushirika linakuja.

Ndio sababu Mungu ameweka karama tofauti tofauti ili tujengane. Katika ushirika mtaombeana, kushiriki meza ya Bwana pamoja, mtafarijiana, mtasaidiana n.k.

Na pia biblia inasema wawili walalapo watapata joto.

Mhubiri 4:9 Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.

10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!

11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona

moto?

12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatuhaikatiki upesi.

Muwapo pamoja kuna ulinzi wa kipekee unaongezeka juu yenu. Hivyo kamwe usijaribu ule ukristo wa kivyako-vyako. Ni lazima tuwe washirika wa kanisa. Kama kanisa la kwanza lilivyoweza kusimama kwa kanuni hiyo.

5.     UTAKATIFU

Utakatifu ni utambulisho wa ukristo. Huwezi kuwa mkristo, halafu ukawa mwovu, huwezi kupokea Roho Mtakatifu halafu sifa za utakatifu usizionyeshe ndani yako. Kwasababu maandiko yanasema Mungu tunayemtumikia ni Mtakatifu hivyo na sisi pia hatuna budi kuenenda katika utakatifu. Bwana Yesu pamoja na watakatifu wa kwanza walizingatia viwango vyote vya usafi na ukamilifu. Vivyo hivyo na sisi

1Petro 1:16 kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

 6) UINJILISTI

Ushuhudiaji unaanza pindi tu unapookoka.  Kila mkristo ameitwa kuitenda kazi ya Bwana. Na ni lazima afanye hivyo kama sehemu ya maisha yake, ili safari yake ya wokovu hapa duniani iwe imara ni lazima azae matunda.  Uwakili ni kazi yetu ya daima. Ukristo bila uinjilisti hauwezi kuwa imara. Kanisa la kwanza lilikuwa la kiinjilisti. Kila mmoja alitambua wajibu wake wa kuisambaza injili kila mahali walipokuwa wakilizingatia lile agizo la Bwana.

Matendo 8:4 Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.

.

7.     UTOAJI

Sifa ya Mungu ni utoaji, ndio maana mpaka leo tunanufanika na mengi katika ulimwengu wake. Hata tulipopotea katika dhambi alijitoa kwa ajili yetu kwa  kumtoa mwanawe awe fidia.

Na sisi kujitoa kihali na kifedha kwa ajili ya injili na kanisa la Kristo, ni nguzo muhimu sana. Unawajibu wa kuisapoti huduma inayokukuza kiroho, kwa zaka na changizo zako, pamoja na  kuwasaidia ndugu (maskini).  Kwasababu, Bwana Yesu na kanisa la kwanza lilikuwa na desturi hiyo.

1 Wakorintho

16:1 Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo

Hivyo sisi sote tukizitendea kazi nguzo hizo muhimu, basi tuwe na uhakika jengo letu la Imani litakuwa imara sana, linaloweza kustahili tufani na majaribu yote, lililoundwa vyema, kwa utukufu wa Mungu, hata siku ile ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU UKAE NANYI NYOTE.

USIKWEPE USHIRIKA NA MADHABAHU YA KRISTO.

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

Rudi Nyumbani

Print this post

AKAUKAZA USO WAKE KWENDA YERUSALEMU.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, karibu tuyatafakari maneno ya uzima. Leo napenda tujifunze tabia nyingine ya Bwana Yesu. Kwasababu yeye mwenyewe alituambia ‘tujifunze kwake’. Hivyo naamini tuna mengi ya kuyajua kuhusu yeye.

Habari hiyo tunaisoma katika vifungu hivi;

Luka 9:51  Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;

52  akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.

53  Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.

54  Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?

55  Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]

56  Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine.

Kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utakumbuka kuwa kuna wakati ulifika, ilikuwa wazi kwa watu wote, kuwa Yesu anatafutwa ili auawe, (hususani kule Yerusalemu). Na hilo lilimfanya mara kadha wa kadha asitembee kwa uwazi wote mbele ya makutano (Yohana 7:10), kwasababu, saa yake ya kuuawa ilikuwa bado haijafika.

Yohana 11:54  Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.

Lakini mambo yalikuja kubadilika baadaye,  hilo halikuendelea kwa wakati wote. Alipoona sasa kazi aliyopewa na Mungu ameimaliza, alionyesha tabia nyingine ambayo haikuwa ya kawaida. Biblia inatuambia, “aliukaza uso wake kuelekea Yerusalemu”, kule kule alipokuwa anatafutwa auawe.

Jambo ambalo lilileta mshtuko hata kwa mitume wake;

Yohana 11:7  Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena.

8  Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?

9  Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

Walishangaa, ujasiri huo ni wa namna gani? Ni sawa na wanajeshi waliokwenda vitani, halafu maadui wakawaua wanajeshi wote, akabakia mmoja tu, halafu huyo mmoja anasema nitakwenda kupambana na jeshi lote hilo peke yangu sitajificha. Ukweli ni kwamba inahitaji nguvu nyingine ya ziada ndani ya huyo mtu.

Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu, aliukaza uso wake, kwenda kututetea sisi. Embu Fikiria kama angeulegeza, na kuendelea kuzunguka mahali pengine na sio kule uyahudi(Yerusalemu), wokovu wetu tungeupatia wapi?

Ilibidi, alazamishe mambo, japo mwili wake ulikuwa hautaki, ndio maana akiwa pale bustanini, anaomwomba Baba, akisema ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke, ni kuonyesha kuwa hata mwili wake ulikuwa unagoma kuwepo kule Yerusalemu,  na si mwili tu, bado mazingira pia hayakutaka,  alipokuwa anakatiza kwa Wasamaria wenyeje wa pale hawakutaka kumruhusu akae kwao, kwasababu waliona kama anawaletea matatizo, ikumbukwe kuwa watu hao  hao ndio waliokuwa wanataka kumfanya mfalme hapo mwanzo. Kuonyesha kuwa mazingira yalimgomea. Si mazingira peke yake, hata mitume wake nao, walifanya kama kumsindikiza tu, lakini mioyo yao walishajiandaa kuchukua hatua yoyote lolote litakapotokea, ndio maana pale bustanini, wale watu walipokuja kila mmoja akakimbia na njia yake.

Kwa ufupi kila kitu kilikataa, isipokuwa roho yake tu. Ndio sababu ya kwanini maandiko yanatuambia ‘aliukaza uso wake’ kwasababu haikuwa rahisi, si jambo tena la kuomba, au kubembeleza, au kushawishi, au kusubiri msimu mzuri. Bali ni kujitoa tu wote wote, katika hayo. Watu wengi tunadhani Yesu aliuchukua msalaba wake siku ile alipobebeshwa ule mti, hapana, aliuchukua msalaba wake Kwa kitendo hichi cha kuamua kuukaza uso wake, kuelekea kifoni. Hata aliposema tujitwike misalaba yetu, alilenga, eneo hilo.

Ni nini na sisi tunapaswa tukipokee kwa Bwana Yesu?

Kwa kuwa Roho wake naye yupo ndani yetu, hatuna budi kufahamu kuwa yapo majira katika safari yetu ya wokovu, hatutahitaji mazingira yawe mazuri, ndio tulitimize kusudi la Mungu, au  ndugu kutukubalia, au marafiki kuafikiana na sisi, au miili kutuambia sasa ndio wakati, hapana..bali ni kujitwika misalaba yetu, “kwa kukaza nyuso zetu” na kumfuata Yesu.

Tukingoja vikwazo viondoke, au viondoshwe, tutajidanganya, na tutangoja sana, kwani vita vitaendelea kuwepo mpaka mwisho, mapambano hayaishi, tutashinda tu kwa kukaza tu nyuso zetu. Na Bwana atakuwa pamoja na sisi, ijapokuwa itaonekana ni kujipoteza lakini mwisho wake utakuwa ni uzima kama ulivyokuwa kwa Bwana Yesu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

RABI, UNAKAA WAPI?

MFALME ANAKUJA.

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya jivikeni silaha ya nia ile ile? (1Petro 4:1)

SWALI: Biblia inamaana gani kusema jivikeni silaha ya nia ile ile? (1Petro 4:1)

1 Petro 4:1-3

[1]Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi. 

[2]Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani. 

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;


JIBU: Tukiangalia undani wa hilo neno hapo anaposema silaha ya nia. Ni kutuonyesha kuwa kumbe  “Nia ”, inaweza kuwa silaha.

Mara nyingi tunapofikiria silaha kibiblia mawazo yetu moja kwa moja yanakimbilia zile za  Waefeso 6:10-18, silaha za haki, kama vile upanga wa Roho ambalo ni Neno la Mungu, chapeo ya wokovu, ngao ya imani, dirii ya haki n.k. 

Lakini hapa tunaonyeshwa kuwa ipo pia silaha ndani ya Nia, ambayo nayo tunashauriwa tuwe nayo, kwasababu ilikuwa kwanza ndani ya Kristo.

Na silaha  yenyewe ilikuwa ni kukubali kuteswa katika mwili ili kuiua dhambi. 

Bwana wetu Yesu Kristo alijua dhambi ina nguvu sana pale mwili unapopewa raha zake. Hivyo aliikubali Nia ya kuteswa, ili dhambi ife.

Kumbuka sababu ya yeye kuchukiwa na watu, kuudhiwa, kuwindwa auawe, kuteswa mpaka kusulubiwa ni kwasababu alitangaza uadui na dhambi, Vinginevyo asingepitia maudhi yale katika mwili. Na tunaona mwisho wake ulikuwa ni ushindi. Kwani kwa kifo chake dhambi ilihukumiwa kabisa kabisa.

Alisema..

Yohana 7:7

[7]Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu. 

Hivyo maandiko yanatuambia na sisi pia, tujivike nia ile ile ya kukubali pia mateso kwa ajili ya Kristo. Kwasababu tukifanya hivyo tunaonyesha kuwa tumeachana na dhambi(tumeihukumu dhambi).

Kwa ufupi ni kuwa ukichukia maisha ya dhambi, tafsiri yake ni kukubali dhiki katika mwili kwa ajili ya Kristo. Hivyo zipende sasa dhiki hizo kama Kristo alivyozipenda, ili dhambi isikutawale. Hiyo ni Silaha kubwa sana.

2 Timotheo 3:12

[12]Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa. 

kubali shida, kwasababu umeamua kuacha ile biashara haramu, furahia kutengwa na kuonekana mshamba, kwasababu umeamua kuacha mienendo ya marafiki wabaya, penda kupigwa na kufungwa kwasababu unahubiri kweli. Hiyo ndio SILAHA YA NIA. iwezayo kuishinda dhambi.

Ndio maana vifungu vinavyofuata anasema..

“Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani. 

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali; 

Daima tujivike silaha hii, tukikumbuka kuwa vita vyetu si vikali tena kama vile alivyovipiga Kristo.

Waebrania 12:4

[4]Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi; 

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

NDUGU,TUOMBEENI.

DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)

KIKWAZO CHA EUODIA NA SINTIKE.

Rudi Nyumbani

Print this post

Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia

Kitabu cha Wagalatia ni moja ya nyaraka ambazo mtume Paulo aliziandika kwa makanisa aliyoyapanda. Tunaona mwanzoni kabisa mwa waraka huu Paulo mwenyewe anajitambulisha akionyesha kuwa yeye ndiye mwandishi.

Waraka huu unamwonyesha Paulo akiwastaajabia watakatifu wa kanisa la Galatia kwa kuacha Imani ambayo aliwaachia hapo mwanzo, alipokuwa analisimamisha kanisa hilo, jambo ambalo lilimfanya mpaka imani yake impelekee kufikiri kuwa wamelogwa(Wagalatia 3:1), kwa jinsi tu walivyoiacha imani kwa haraka.

Kwa mujibu wa waraka huu, tunaona Paulo alilijenga kanisa hilo katika msingi wa imani katika neema ya Yesu Kristo.Na si katika msingi wa matendo ya sheria kama kigezo cha kukubaliwa na Mungu.

Kutokana na kuwa kanisa hili lilikuwa na mchanganyiko wa wayahudi pamoja na watu wa mataifa waliomwamini Kristo.Hapo ndipo tatizo lilipoanzia baada ya baadhi ya wakristo wa kiyahudi kuanza kuwashurutisha watu wa mataifa kwa kuwaambia kwamba hawawezi kuokolewa kama hawataishika torati ya Musa, kama hawatatimiza maagizo kama tohara, kushika siku, miezi, na miaka.(Wagalatia 4:8-10)

Hivyo hiyo ikawafanya watu kuacha kuishi tena kwa Imani iliyo katika neema ya Kristo Yesu, na kuangalia matendo ya sheria kama ndio kigezo cha kukubaliwa na Mungu?

Hivyo Paulo alipojua mageuzi hayo, ndio akawaandikia waraka huo kwa ukali, akiwaambia wokovu wetu huja kwa imani iliyo katika Yesu Kristo itendayo kazi katika upendo. Na si katika matendo ya sheria. Kwasababu kama ingekuwa hivyo Kristo alikufa bure. Torati ingeendelea tu kutawala.

Wagalatia 5:6

[6]Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.

Akasema torati, haikuwahi kumkamilisha mtu, na mtu anayeishi kwa hiyo ametengwa na Kristo, bado yupo chini ya laana.

kuishi kwa sheria ni kurudia mafundisho manyonge.

Lakini Swali ambalo alitarajia lingeulizwa na wagalatia, ni hili;

Je sasa hatuna haja ya kuyatazama matendo mema, tuishi tu, kama tunavyotaka kwasababu tunahesabiwa haki kwa neema ya Kristo tu?

Mbeleni kabisa katika sura ya tano, Mtume Paulo alitolea ufafanuzi, na kuwaambia tukishaokolewa, Maana yake ni kuwa tumeusulubisha mwili pamoja na tamaa zake mbaya..Hivyo hakuna nafasi ya dhambi kupata nguvu ndani yetu.

Wagalatia 5:24

[24]Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.

Je hilo inawezekanaje? kama hatuna sheria?

Linawezekana kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Ambaye tumepewa na Mungu.

Wagalatia 4:6

[6]Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.

Hivyo Paulo anaendelea kueleza ni wajibu wa kila mwamini kutembea katika Roho. Ili awasaidie Roho kuzishinda tamaa zote za mwili, na mambo maovu.

Wagalatia 5:16-21

[16]Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

[17]Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

[18]Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.

[19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

[20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

,[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Je waraka huu ulilenga hasa nini?

Kwamba kwa nguvu zetu, au dini zetu au torati kamwe hatuwezi kumpendeza Mungu bali tuitegemee neema ya Kristo ambayo kwa hiyo tumepokea Roho awezaye kutufanya wakamilifu.

Hivyo ni wajibu wako kama mkristo. Kila wakati wote kujawa Roho (Waefeso 5:18). Ambayo hiyo huja kwa kuwa waombaji, wasomaji Neno, na kufanya ibada mioyoni mwetu wakati wote..

Tukiwa watu wa namna hiyo sheria wala dhambi inakuwa haina nguvu ndani yetu. Kwasababu tunakuwa chini ya neema ya Yesu Kristo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni uchafu gani unaozungumziwa katika Wagalatia 5:19?

je! Paulo aliwalaani Wagalatia na Wakorintho?

Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).

Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Mungu auweke Mti wa Mema na Mabaya katikati ya bustani?

Swali: Kulikuwa na sababu gani ya Bwana MUNGU kuuweka mti wa mema na mabaya katikati ya bustani ili hali anajua kuwa mti huo ndio utakaowakosesha Adamu na Hawa, kwanini Mungu asingeondoa, na kuubakisha tu ule mmoja wa uzima katikati ya bustani?


Jibu: Ni kweli inaweza kuonekana ni busara mti mmoja tu kuwepo pale bustanini lakini ukweli ni kwamba endapo Mti mmoja tu ungekuwepo pale bado MTI WA UZIMA, usingeeleweka na wala maana yake isingekuwepo..

Kwani ili kuuthibitisha wema lazima uwepo ubaya mahali fulani… kwasababu wema hauwezi kujilikana kama ubaya haujadhihirishwa, vinginevyo ule wema utaonekana ni kitu cha kawaida, lakini ukifunuliwa ubaya ndipo wema unapopata kujulikana na kueleweka.

Nuru haiwezi kujulikana kama ni njema na kitu kizuri, kama giza halipo.. lakini ili Nuru ipate sifa, na kuheshimika ni lazima giza liwepo mahali ili nuru ilishinde giza.

Vile vile Mungu aliuweka ule mti wa ujuzi wa mema na mabaya ambao matunda yake ni MAUTI, ili kuuthibitsha MTI WA UZIMA ambao matunda yake ni UZIMA.

Adamu na Hawa wasingeweza kuelewa nini maana ya UZIMA kama kisingekuwepo kingine kinachoelezea/kuhubiri MAUTI, vile vile hata sisi leo tusingejua Uzima ni nini kama MAUTI isingekuwepo, vile vile hatuwezi kujua Amani ni nini, kama hatujawahi kusikia kuhusu vita, au kupitia vita..

Hatuwezi kujua umaskini ni nini kama hatujawahi kuona utajiri, vile vile hatuwezi kujua utajiri ni nini kama hatuwahi kuona au kupitia umasikini,.. hatuwezi kujua kuwa tuna afya kama hatujawahi kuona wagonjwa, wala hatuwezi kujijua kuwa tuna ugonjwa kama hatujawahi kuona wenye afya, au sisi wenyewe kuwa na afya, huwezi kujua hiki ni kirefu kama kifupi hakipo, wala huwezi kujua hiki ni kirefu kama kifupi hakijawekwa mahali kama mfano.

Hivyo utaona kuwa uwepo wa vibaya au vyenye kasoro ni ili kuvithibithisha vile vilivyo vizuri na visivyo na kasoro.. Na lengo la Mungu kuuweka mti ule wa ujuzi wa mema na mabaya lilikuwa ni kuwapa kuelewa Adamu na Hawa Uzima ni nini, na thamani yake, na ili wauthamini na kuushika… na wala lengo lake si kuwatega!.

Hebu pia tengeneza picha miili yetu isingekuwa na maumivu, je unadhani ni nini kingetokea?…bila shaka hakuna mtu ambaye angehangaika kuutunza… hakuna mtu angeogopa kujikata na kisu, au kutembea peku kwenye miiba, au kunywa maji ya moto yale yanayotokota… lakini maumivu yamewekwa ili tujue na kutamani kuwa katika hali ya kutokuwa na maumivu na vile vile kuitunza miili yetu na kuushikilia uzima vizuri .

Hali kadhalika uwepo wa mti ule wa ujuzi wa mema na mabaya ni ili kuuthaminisha mti wa UZIMA. Ili mtu ajue umuhimu wa UZIMA, na RAHA ya Uzima, faida za uzima.

Je wewe umempokea YESU, na kuoshwa dhambi zako? Kumbuka YESU ndiye njia ya Mti wa UZIMA, na yeyote anayempokea humpa matunda hayo na kuishi milele, ndani yake.

Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”.

Ufunuo 2:7 “Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu”

Bwana akubariki.

Kujua kwanini BWANA MUNGU awazuie wasile matunda ya Mti wa Uzima baada ya kula ya ujuzi wa mema na mabaya fungua hapa >>>

Kwanini Bwana MUNGU aliwazuia Adamu na Hawa wasile matunda ya Mti wa uzima waishi milele?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post