Category Archive Uncategorized

Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?

Kitabu hiki katika lugha ya kiebrania kinasomeka kama “Devarim” ambayo tafsiri yake ni “Maneno”

Na ndio maana mstari wa kwanza kabisa un itaanza Kwa kusema. “Haya ndiyo maneno”

Kumbukumbu la Torati 1:1

[1]Haya ndiyo maneno Musa aliyowaambia Israeli wote ng’ambo ya Yordani barani, katika Araba lililoelekea Sufu, kati ya Parani, na Tofeli, na Labani, na Hazerothi, na Dizahabu.

Lakini katika tafsiri ya kigiriki Cha kale (septuagint),  kilisomeka kama “deuteronomioni” chenye maana ya “Mrudio wa sheria” ambapo Kwa sisi kinasomeka kama “kumbukumbu la sheria/torati”. 

Ni kitabu Cha Tano ambacho kiliandikwa na Musa karibia na mwisho wa Ile miaka 40, wakati walipokuwa ng’ambo ya Yordani katika nchi ya Moabu.

Lengo la kuandikwa kitabu hicho ni kukumbushwa sheria na maagizo ya Mungu, kwasababu kundi kubwa la Wana wa Israeli lililopokea sheria Kule mlima Sinai mwanzoni, lilifia jangwani, hivyo kile kizazi kipya Hakikuwa na msingi imara juu ya sheria za Mungu. Na ndio hapa Musa anaagizwa na Mungu awakumbushe Wana wa Israeli sheria yake.

Kitabu hiki kimeanza kuwakumbushia safari Yao Toka Misri, pia kikagusia jukumu lao la kumpenda Mungu na kuzishika sheria zake. Ikafuatana na baraka na laana ambazo zitampata mtu katika kutii au kutokutii, na mwisho kifo cha Musa.

Je ni Nini tunajifunza kuwepo kwa kitabu hiki ? 

Bwana anataka na sisi tuweke kumbukumbu la agano lake mioyoni mwetu, Kwa vizazi vijavyo tupende kuwafundisha vizazi vinavyochipukia Neno la Mungu, tusiwaache tukadhani wataelewa tu wenyewe kisa biblia ipo, bila kukumbushwa Kwa kufundishwa.

Musa alifanya vile ndio maana kizazi kile kikawa imara baada ya pale.

Na sisi tuwe watu wenye tabia hii, Sio kwa watoto tu hata Kwa kondoo wa Bwana kanisani. Mara Kwa mara tuwakumbushe maagizo ya Mungu.

Kwa maelezo ya ziada kuhusu kitabu hichi pitia hapa >>> https://wingulamashahidi.org/2019/05/13/vitabu-vya-biblia-sehemu-ya-2/

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya ki-Mungu?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Nini maana ya “Atamwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake”. (2Wathesalonike 2:8).

Rudi nyumbani

Print this post

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Safari ya wokovu ya mkristo inafananishwa na safari ya Wana wa Israeli kutoka Misri kwenda Kaanani. 

Na kama vile maandiko yanavyotuonyesha walikombolewa wote Kwa damu ya Mwana kondoo, Kisha Wakabatizwa katika bahari ya Shamu, wakawa chini ya wingu la Roho Mtakatifu kule jangwani,.. Lakini katika hayo yote bado tunaambiwa wengi wao hawakuweza kuiona Ile nchi ya ahadi. Isipokuwa wawili tu, (yaani Yoshua na Kalebu), waliotoka nchi ya Misri.

Biblia inatuonyesha walipishana na majaribu 5, ambayo yaliwafanya waangamie jangwani. Na majaribu yenyewe tunayasoma katika 1Wakorintho 10:1

1 Wakorintho 10:1-12

[1]Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; [2]wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;

[3]wote wakala chakula kile kile cha roho; [4]wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. [5]Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.

[6]Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani. [7]Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.

[8]Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu. [9]Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

[10]Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu. [11]Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. [12]Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.

Kama tunavyosoma hapo. Makosa hayo yalikuwa ni haya;

  1. Kutamani mabaya
  2. Kuabudu sanamu
  3. Kufanya uasherati
  4. Kumjaribu Mungu
  5. Kunung’unika

1) Kutamani mabaya

Mungu aliwapa MANA kama chakula pekee ambacho wangekula jangwani, wao na mifugo Yao, lakini, baadaye waliikinai wakataka NYAMA, na vyakula vingine (Hesabu 11:4-35), matokeo yake ikiwa Mungu kuwaua, wengi wao.

Kama wakristo tuliookoka MANA yetu ni NENO LA MUNGU, Hatupaswi kulikinai, tukakimbilia chakula kingine kisicho Cha kiMungu. Tukataka tuongozwe na mifumo ya kidunia. Ndugu ni hatari mbaya sana. Kumbuka Ile mana ijapokuwa kilikuwa ni chakula Cha aina Moja, lakini hawakuwahi kuumwa, Wala kudhoofika, Wala miguu yao kupasuka, tofauti na walivyokuwa Misri penye vyakula vingi, lakini vimegubikwa na magonjwa. 

Ndugu Lipokee Neno la Mungu, ishi Kwa hilo, hata kama halitavutia (kidunia), lakini limebeba virutubisho vyote vya kimwili na kiroho. Wanaotembea Kwa Neno la Mungu, hawatikisiki hustawi milele.

2) kuabudu sanamu:

Walipomwona Musa amekawia mlimani, na Mungu hazungumzi chochote Kwa wakati ule  wakajiundia sanamu zao za ndama waziabudu. Wakacheza, wakala na kinywa (Kutoka 32). Hii ni kuonesha kuwa kitu chochote kinachokufanya ushangilie  tofauti na Mungu wako, ni ibada ya sanamu.

Rafiki kuwa makini Kwa wakati wa Leo mkristo kushabikia mipira, kwenda Disko, kutumikia Mali, kufuatilia vipindi vya sinema kulikopitiliza, chattings, kupenda anasa. Ni ibada za sanamu waziwazi.

 Kwasababu gani?. Kwasababu ndio bubujiko lako la roho lilipo kama ilivyokuwa Kwa Wana wa Israeli, Kwa sanamu zile. Ikapelekea watu wengi kufa siku Ile. Ibada Yako iwe Kwa Bwana. Mungu ni mwenye wivu. Mpira ukichukua nafasi zaidi ya Mungu wako ni kosa.

3) Kufanya uasherati

Walipokuwa jangwani Mungu aliwakataza wasitangamane na wageni, kwasababu watawageuza mioyo na kuiabudu miungu Yao. Lakini wao walipowaona wanawake wa taifa la Moabu, wakaenda kuzini nao, Kisha wakageuzwa mioyo wakaabudu miungu Yao. Hiyo ikawa sababu ya Mungu kuwaua waisraeli wengi sana idadi yake 23,000.

Na sisi kama wakristo tulishapewa tahadhari kwenye maandiko. Tusifungwe nira na wasioamini isivyo sawasawa (2Korintho 6:14-18). Kwasababu hakuna ushirika kati ya Nuru na Giza. Hivyo hatuna budi kuwa makini na ulimwengu, tushirikiane nao kwenye mambo ya kijamii na ya msingi, pale inapokuwa na ulazima, lakini ya kiroho, hatupaswi hata kidogo kuwa na urafiki nao kwasababu ni rahisi kugeuzwa moyo na kuambatana nao kitabia, na matokeo yake tukamwasi Mungu.

Sulemani aligeuzwa moyo, Wana wa Mungu tunaosoma kwenye Mwanzo 6 nao pia waligeuzwa mioyo Kwa jinsi hiyo hiyo, na wewe pia usipojiwekea mipaka na watu ambao ni wa kidunia, Unaweza kupoteza taji lako. Pendelea zaidi kuwa na kampani ya waliookoka. Ni Kwa usalama wako. Usijikute unafanya uasherati wa kiroho.

4) Kumjaribu Bwana

Wana wa Israeli walimjaribu Bwana, wakati Fulani wakamnun’gunikia Mungu na Musa, wakisema chakula hiki dhaifu, wakitaka Kwa makusudi Bwana awafanyie Tena muujiza mwingine, Mungu akakasirishwa nao, akawaangamiza Kwa nyoka (Hesabu 21:4-9).

Kama mkristo tambua kuwa Mungu haendeshwi kama “robot”. Kwamba ni lazima afanye jambo Fulani Kila tutakapo ndio tuthibitishe yeye yupo na sisi. Ndugu ukristo wa hivi ni hatari, wengi wameishia kuanguka kwasababu hii. Jaribu kama hili aliletewa Bwana Yesu na shetani jangwani. Ajitupe kutoka kinarani, kwasababu maandiko yanasema Mungu atamuagizia malaika wake wamchukue salama. lakini Bwana Yesu alimwambia shetani usimjaribu Bwana Mungu wako.

Kamwe usimwendeshe Mungu, mwache yeye ayaendeshe maisha Yako. Tuwe na hofu na Mungu wetu.

5) Kunung’unika.

Wana wa Israeli tangu mwanzo wa safari Yao Hadi karibia na mwisho, waligubikwa na manung’uniko tu,(Kutoka 23:20-21) wengi wao hawakuwa watu wa shukrani. Ijapokuwa walilishwa mana, waliouna utukufu wa Mungu Kwa wingi. Lakini bado manung’uniko yalizidi shukrani.

Biblia inatuasa sisi tuliookoka tuwe watu wa Shukrani (Wakolosai 3:15), Kwa kazi aliyoimaliza Yesu pale msalabani ya kuondolewa dhambi ni fadhili tosha zaidi hata ya wale Wana wa Israeli kule jangwani. Hata tukikosa Kila kitu, maadamu tumeahidiwa uzima wa milele. Hatuhitaji kuwa na hofu na jambo lolote. Wokovu wetu ndio uwe faraja.

Epuka Maisha ya manung’uniko.

Bwana akubariki.

Ikiwa tutashinda majaribu haya MATANO katika safari yetu ya wokovu. Basi tutalipokea taji timilifu Kwa Bwana  siku Ile mfano wa Yoshua na Kalebu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Habari iliyo katika 1Nyakati 21:25, na 2Samweli 24:24, ya Daudi kununua kiwanja  inajichanganya?

SWALI:  Ni ipi gharama sahihi ambayo Daudi aliilipia, kununulia shamba la Arauna, kwa ajili ya kumjengea Mungu hekalu. Je! Ni shekeli 600, au shekeli 50?. Je! Biblia inajichanganya.

JIBU:  Tusome,

2Samweli 24: 24 Lakini mfalme akamwambia Arauna, La, sivyo; lakini kweli nitavinunua kwako kwa thamani yake; wala sitamtolea Bwana, Mungu wangu, sadaka za kuteketezwa nisizozigharimia. Hivyo Daudi akakinunua hicho kiwanja cha kupuria na wale ng’ombe kwa shekeli hamsini za fedha.  25 Naye Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Basi Bwana aliiridhia nchi, na tauni ikazuiliwa katika Israeli.

1Nyakati 21:25 “Basi Daudi akampimia Arauna thamani ya mahali pale shekeli mia sita za dhahabu kwa uzani  26 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akamlingana Bwana; naye akamwitikia kutoka mbinguni kwa moto juu ya madhabahu hiyo ya sadaka ya kuteketezwa”

Vifungu hivyo havijichanganyi,  vyote vipo sahihi. Mwandishi wa kitabu cha Samweli anaeleza lile eneo ambalo lilikuwa ni la kupuria tu, pamoja na wale ng’ombe gharama zake jumla ndio shekeli hamsini, lakini sio eneo lote la kiwanja. Tukirudi kwenye 1Nyakati mwandishi anaeleza sasa eneo lote, anatumia neno “mahali pale”. Kwamba jumla yake yote ni shekeli mia sita. Gharama zote za mahali pale zilikuwa ni shekeli 600

Kwamfano wewe unaweza ukawa umelenga kupanunua mahali Fulani kwa ajili ya shughuli zako za kimaendeleo. Lakini ikakugharimu ununue sehemu yote ili uweze kupamiliki vizuri na pale. Hivyo kama eneo lile tu moja gharama yake ilikuwa milioni 1, Lakini kwasababu ya kulipia fidia kwa watu kando kando kuwahamisha, na kodi, na ukarabati n.k. unajikuta unaenda mpaka milioni 20.

Ndicho kilichomkuta Daudi.

Kwahitimisho ni kuwa vifungu hivyo vipo sahihi havijichanganyi.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

NI KWANINI WATU WENGI WANASHINDWA KUMWELEWA MUNGU?

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?

Novena ni nini? Na je ipo kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

Waefso 6:18  kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote

Yuda 1:20  Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu

Watu wengi wanaamini kuomba katika Roho ni kuomba kwa “kunena kwa lugha tu”. Nje ya hapo sio kuomba kwa Roho. Lakini tukiwa na mtazamo huo basi tutakuwa na uelewa finyu kuhusu Roho Mtakatifu.

Ukweli ni kwamba hiyo ni namna mojawapo kati ya nyingi ambazo Roho wa Mungu anamjalia mtu kuomba.

Maana ya ‘kuomba katika Roho’ Ni kuomba ‘ndani ya Roho ya Mtakatifu/ ndani ya utaratibu/ uwepo wa Roho Mtakatifu’. Na hiyo ni zaidi ya kunena kwa lugha, Hii ikiwa na maana Mtu anaweza kuomba lakini asiwe katika uwepo huo. Na matokeo ya hivyo ni maombi kuwa makavu sana, yasiyo na nguvu.

Sasa mstari mama unaotufundisha juu ya uombaji wa Roho Mtakatifu ni huu;

Warumi 8:26  “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA”

Hapo anasema “kuugua kusikoweza kutamkwa” . Maana ya kuugua hapo ni kuweka uzito, au presha, au shauku  ya kuomba ndani ya mtu isiyokuwa ya kawaida. Tofauti na angejitahidi kwa nguvu zake yeye mwenyewe. Sasa mtu akifikia hatua hiyo, basi tayari kuanzia huo wakati anaomba katika Roho hata kama maneno yake ni ya kawaida anayoyatumia. Maombi hayo yana nguvu na yanasikika sana mbele za Mungu.

Kwamfano, ndio hapo utakuta mtu anaomba, lakini mara anasikia kububujika machozi ndani yake, mwingine anazidi kuona kiu ya kuendelea kuombea jambo lile lile kwa muda mrefu tofauti na sikuzote. Mfano wakati ule Bwana Yesu alipokuwa Gethsamane anaomba.

mwingine anajisikia wepesi usio wa kawaida, uchovu wote umeondoka ijapokuwa alikuwa amechoka sana, anaanzafurahia maombi, anafurahia kuendelea kubaki palepale muda mwingi kuendelea kuomba,

Sasa hali kama hizi ukizifikia, ujue tayari umeshazama katika Roho, umeshawezeshwa na Roho, maombi yako yanakuwa na nguvu sana,

Mwingine anasikia raha Fulani moyoni, akiwa anaomba, mwingine ndio anazama katika kunena kwa lugha (kwa kusukumwa na Roho), na sio kwa akili. Mwingine anasindikizwa na kuusikia uwepo wa Mungu umemfunika, nguvu za Mungu zinashuka mwilini mwake, anasikiswa, n.k. na unajikuta unafurahia sana maombi..

Kusudi la sisi kuomba sio kwenda kujitesa au kujiumiza, hapana bali ni mahusiano, tena ya kama mtu anazungumza na Baba yake. Kiasi kwamba ukitoka kwenye maombi unaona umetoka kweli kuwasiliana na mtu, sio umetoka kuusemesha ukuta, usiokuwa na mrejesho wowote, umeomba hewani hewani tu

Sasa ni mapenzi ya Mungu kwamba sisi watoto wake kila tuombapo tuombe katika Roho Mtakatifu. Tuzame, tuyafurahie maombi yetu. Sasa tunawezaje kufikia hatua hiyo?

Kabla ya kuona namna ya kufikia hicho kilele. Tuone kwanza vikwazo vinavyomzuia mtu asiombe kwa Roho.

VIKWAVYO VINAVYOPINGANA NA MTU KUOMBA KATIKA ROHO.

  1. Mwili
  2. Shetani

Hawa ndio maadui wawili wakubwa wa mtu kuzama. Ndio maana wewe kama mwombaji ni lazima uwafahamu, na ujue kabisa huna budi kushindana nao na ni lazima ukutane nao. Vinginevyo usipowatilia  maanani kila siku maombi yako yatakuwa ni ya “kawaida sana” na kila utakapofikiria  kitu kinachoitwa maombia utaona kama vile unapelekwa gerezani.

Ndugu Mungu hajakusudia tujihisi hivyo sisi watoto wake tunapomkaribia yeye, tuwe kama tunaliomba sanamu lisilonena, amekusudia kutupa mrejesho, na ndio hiyo zawadi ya Roho kuugua ndani yetu. Lazima atupe mrejesho wake kwamba yupo nasi.

Sasa uanzapo, hakikisha unaunyima mwili wako, raha zote, zinazokinzana na wewe kuomba. Kuwamfano, ukijiona mwili unasinzia au unapoa wakati wa kuomba usipende kukakaa kwenye kiti, ni heri upige magoti, ukishindwa tembea-tembea. Tena ni vizuri ukanyoosha na mikono yako juu, huku umefunika macho. Kisha anza kuomba.

Usiogope adhabu hizo za mwanzoni hazitadumu muda mrefu sana utaingia katika Roho, ni mwili tu unakuambia wacha, kunitesa, wewe ulazimishe tu, ukikuambia leo siku nzima umefanya kazi legea-legea, pinga hayo mawazo. Hivyo ukiwa Sasa katika hali hiyo. Anza kuomba lakini pia tumia ahadi za Mungu zilizopo kwenye biblia ni muhimu sana, kulingana na jambo unaloliombea, mkumbushe Bwana, ulisema hivi, na hivi kwenye Neno lako,, Ulisema ni nani aliye Baba, mtoto wake akimwomba mkate atampa jiwe, mkumbushe mwambie ulisema, kama ungetazama dhambi zetu ni nani angesimama,..mwambie ulisema niite nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa na magumu usiyoyajua n.k..Tumia njia hiyo, kujimimina kwa Bwana

Omba huku umetilia ukamini (concentrate), mawazo yako ukiyalazimisha yasiende nje ya Mungu. Tengeneza picha halisi Mungu amesimama mbele yako kukusikia, fumba macho. Usiruhusu kufikia mambo ya nje, kwasababu akili yako itakuwa shapu kukutoa, ukitoka rudi, endelea kuomba. Ndio ni kipindi kifupi utataabika , lakini hatimaye utazama tu.. Sasa ukiendelea kudumu kwa kung’ang’ania huko  kwenye maombi hayo kwa kipindi fulani. Hayo mazingira rafiki ya Roho Mtakatifu kuyaingilia maombi yako. Utashangaa tu, wepesi usio wa kawaida umezuka ndani yako. Tangu huo wakati endelea kuomba kwa jinsi usikiavyo rohoni, kwani hayo maneno unayoyaomba mengine hutaelewa unayatolea wapi, huyo ni Roho Mtakatifu anaomba na wewe.

Ndio maana akasema msifikiri-fikiri, kwasababu Roho mwenyewe atawajalia.  Wengine kabla ya kuomba wanasema sijui nitaomba nini? Ndio hujui kwasababu bado hujazama, ukishazama utaweza tu kuomba kwasababu ni yeye ndio anayekujalia. Wengine wanasukumwa kunena kwa lugha n.k.

Adui wa pili ni shetani. Huyu anapaswa apingwe kwa kukemewa. Kabla ya kuanza maombi, hakikisha unayateka mazingira yako ya kimaombi. Ukimwomba Mungu, afukuze uwepo wote wa mapepo, hapo ulipo.  Dalili ya shetani, ni pale unashangaa ukiwa unataka kuomba kichwa kinauma au tumbo, au hali Fulani isiyo ya kawaida inakuvaa katika mwili wako. Huyo ni shetani, mpinge kwa kukemea kisha endelea na maombi. Au mwingine anaona mazingira ya kusumbuliwa, mara kelele Fulani za nje, au simu zinaingia, ambazo si kawaida sikuzote kuwepo. Ndio maana ni vizuri katika kuomba kwako uzime simu. Ukae mbali na mazingira yenye mwingiliano, hiyo itakufanya umpe adui wakati mgumu kukusumbua.

Zingatia tu: Shetani haogopi sana maombi ilimradi maombi, anaogopa sana maombi yaliyo katika Roho, Hata kama ni ya muda mfupi, hayapendi, na ndio atakayoyapiga vita sana. Hivyo usiwe mwepesi mwepesi kupenda kuomba juu juu.

Kwahiyo ukizingatia mambo hayo mawili kutakufanya uzame rohoni katika maombi yako yote. Na utayafurahia na utaona matokeo pia.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika sanduku la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

JE! TUNAPASWA TUOMBE MARA NGAPI KWA SIKU?

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

Rudi nyumbani

Print this post

Wakili ni nani kibiblia? Uwakili ni nini?

Wakili kibiblia ni mtu aliyepewa usimamizi wa nyumba (Au kaya) ya mtu mwingine. Na usimamizi huo unajumuisha kuanzia kwenye ngazi ya kifamilia, mpaka mali alizonazo bwana wake.

Uwakili tunaona tangu enzi za agano la kale, kwamfano, Eliezeri alikuwa ni wakili wa Ibrahimu. Na tunaona yeye ndio alikuwa mwangalizi wa mali zake, lakini pia ndiye aliyehusika kwenda kumtafutia Isaka, mke katika ukoo wa baba zake Ibrahimu(Mwanzo 15:2, Mwanzo 24).

Lakini pia tunamwona Yusufu, naye alikuwa ni wakili katika nyumba ya Potifa, aliachiwa vyote avisimamie, (Mwanzo 39:5-7).

Vilevile tukirudi kwenye agano jipya tunaona,  Bwana Yesu alitumia mifano ya mawakili, kuwawakilisha watumishi wake wanaofanya kazi ya kuhudumu/kulichunga kundi lake, kwamba kwa mifano ya wao na sisi tujifunze utumishi uliosahihi kwake.

Kwamfano Luka 12:40-48 Inasema;

“Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu. 41  Petro akamwambia, Bwana, mithali hiyo umetuambia sisi tu, au watu wote pia? 42  Bwana akasema, Ni nani, basi, aliye WAKILI mwaminifu, mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya utumishi wake wote, awape watu posho kwa wakati wake? 43  Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta anafanya hivyo. 44  Kweli nawaambia, atamweka juu ya vitu vyake vyote. 45  Lakini, mtumwa yule akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia kuja, akaanza kuwapiga wajoli wake, wanaume kwa wanawake, akila na kunywa na kulewa; 46  bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wasioamini. 47  Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. 48  Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi”

Ikiwa wewe umepewa dhamana ya kulichunga/kulisimamia kundi, basi tambua kuwa Bwana anataka aone uaminifu wako wa kuwahudumia na kuwalinda watu wake aliokupa. Yesu alipomuuliza Petro Je! Wanipenda akasema ndio nakupenda!, Hapo hapo akamwambia chunga kondoo zangu, lisha kondoo wangu. Kuonyesha kuwa ikiwa wewe ni mtumishi na unasema unampenda Bwana, basi ujue upendo wako ni kuwachunga na kuwalisha kondoo wa Bwana.

Lakini pia uwakili sio tu kwa waliowatumishi wa Mungu, bali pia kwa kila mwaminio, aliyeokoka, amepewa uwakili wa kuifanyia kazi  kwa ile talanta aliyopewa.

Bwana Yesu alitumia mfano wa Yule mtu aliyesafiri, akawaita watumwa wake, akawawekea mali yake yote kawafanyie biashara, Hivyo mmoja akapewa talanta 5, mwingine 2, mwingine 1. Kama tunavyoijua habari wale wawili wa kwanza wakafanikiwa kuzalisha, lakini Yule mmoja wa mwisho hakuifanyia chochote talanta yake, akaiacha mpaka aliporudi bwana wake. Matokeo yake ikawa ni kunyang’anywa na kutupwa katika giza la nje (Mathayo 25:14-30).

Hiyo ni kutufundisha kuwa hakuna hata mmoja wetu, ambaye hajapewa karama na Mungu, hivyo unapaswa ujiulize, je! Talanta yangu ninaitumiaje, Uwakili wangu ninautumiaje Je! Ni katika kuujenga ufalme wa Mungu, au katika mambo yangu mwenyewe.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa waliokoka wote ni mawakili wa Kristo. Na hivyo Bwana anataka aone wakihudumu katika nyumba yake kwa uaminifu wote. Na ndivyo mitume wa Bwana walivyojiona mbele za Mungu.

1Wakorintho 4:1  Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.2  Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.

Vifungu vingine ambavyo utakutana na neno hili ni hivi; Luka 16:1-13, 1Wakorintho 9:17, Waefeso 3:2, Wakolosai 1:25.

Bwana akubariki.

Swali ni je! Umeokoka? Kama sio unasubiri nini? Mpokee sasa Bwana Yesu ili akupe uzima wa milele bure. Kumbuka hizi ni siku za mwisho, Yesu yu mlangoni kurudi , akikukuta hujaitendea kazi talanta yako utamjibu nini, Na umeshaisikia injili?

Ikiwa upo tayari leo kumpokea Bwana, akusamehe dhambi zako, basi fungua hapa kwa mwongozo huo wa sala ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

ANGALIA JINSI USIKIAVYO:

Mtakatifu ni Nani?

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Tirshatha ni nini? (Ezra 2:63)

Beelzebuli ni nani? (Mathayo 12:24).

Mierebi ni Nini kwenye biblia? (Isaya 15:7)

Rudi nyumbani

Print this post

Hadaa ni nini kibiblia? (2Petro 2:14)

Kuhadaa ni kudanganya, au kulaghai, kutumia njia isiyosahihi/ ya mkato kufanikisha au kupata jambo.

Neno hilo utalipata katika vifungu hivi baadhi;

Mwanzo 31:20 “Yakobo akamhadaa Labani, Mshami, kwa kuwa hakumwambia ya kwamba anakimbia”

Mithali 12:5 “Mawazo ya mwenye haki ni adili; Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa”

Warumi 1:28  Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. 1.29  Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na HADAA; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya

2Petro 2:14  wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, wenye kuhadaa roho zisizo imara, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana;

2Petro 2:18  Maana wakinena maneno makuu mno ya kiburi, kwa tamaa za mwili na kwa ufisadi huwahadaa watu walioanza kuwakimbia wale wanaoenenda katika udanganyifu;

Mifano halisi ya kuhadaa ni hii;

> Kama mume, unapotoka na kwenda kwenye kumbi za starehe kucheza miziki na kuzini na kulala huko na makahaba, kisha unamwambia mke wako umesafiri, huko ni kuhadaa.

>Kama mfanyabiashara, unapopunguza uzito jiwe la mizani, ili umpimie mteja kipimo kidogo kwa bei ileile, au unapozidisha bei ya bidhaa juu zaidi ya ile iliyo elekezi, huko ni kuhadaa.

> Kutumia ujuzi wako, au utumishi wako, kusema uongo, ili kupata maslahi Fulani kutoka kwa huyo mtu. Kwamfano wewe ni mchungaji, halafu unasema Bwana ameniagiza mtoe kiwango Fulani cha fedha kila mmoja ili kupokea uponyaji kutoka kwangu, . Hapo umewahadaa watu wa Mungu, kwasababu unajua kabisa tumeambiwa tutoe bure, kwasababu tulipokea bure.

Tabia ya kuhadaa ni tabia ya shetani, kwani ndio silaha ya kwanza aliyoitumia kumwangusha mwanadamu pale Edeni, alipokwenda kumuhadaa Hawa, kwa kumwaminisha kuwa akila matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya hatokufa. Lakini ilikuwa kinyume chake.

Bwana Yesu anasema, shetani ni baba wa uongo. Hivyo na sisi tunapodhihirisha tabia hii ya kutumia udanganyifu na hila, ni wazi kuwa tudhihirisha tabia za wazi na za asili za shetani.  Kumbuka Hadaa ni zao la wivu na kutokupenda maendeleo kwa wengine.

Tukiwa na upendo. Tabia hii itakufa ndani yetu. Tuutafute upendo wa Mungu

Je! Unasumbuliwa na dhambi hii au dhambi nyingine yoyote? Yesu pekee ndio tiba, atakusaidia kuishinda. Ikiwa upo tayari leo kumfanya kuwa Bwana na kuupokea msamaha wake bure. Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

WENYE KUHADAA ROHO ZISIZO IMARA.

Sukothi ni nini? (Mwanzo 33:17).

Kuba ni nini (Ayubu 22:14)?

Ipi tofauti kati ya matoleo na sadaka?

Maana ya Mithali 19:15 ‘Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;

Fahamu Maana ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu maana 1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;

SWALI: Bwana Yesu asifiwe naomba kufahamu maana ya hili andiko;

1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima”

JIBU: Kwa kawaida mtoto mchanga anakuwa kama mjinga, haelewi mambo mengi, anachofahamu ni kile tu kilichopo nyumbani, mambo mengine ya nje, hayajui, na ndicho kinachomfanya asijisumbue na hayo mengine, ambayo watu wazima wanayasumbukia,. Vivyo hivyo na Mungu anataka katika suala la uovu, tuwe hivyo. Kama wajinga, hatujui kinachoendelea, hatuna maarifa nayo, hatuwezi kuyaelewa. Na hiyo itatufanya tuwe salama.

Kwamfano ukiulizwa habari za nyimbo Fulani mpya za kidunia zilizotoka, huna taarifa nazo, Ukiulizwa habari za ligi za mipira, ni kama taarifa usizozielewa, ukisemeshwa na mambo ya kubeti, ni kama mtu anazungumza na wewe  kwa lugha za mafumbo.

 Ndio maana andiko hili linasema hivyo;

1Wakorintho 16:19b  “…lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya”

Kutokujua kila kitu katika huu ulimwengu sio dhambi, na wala hilo halitakuzuia uishi vema. Hivyo tunapaswa tuchuje, ni nini kinatufaa na kipi kisichotufaa, Vile visivyotufaa tuviweke kando, tuwe watoto katika hivyo, lakini vile vitujengavyo, ambalo ni NENO LA MUNGU, basi tuwe watu wazima. Tulijue sana hilo kwasababu ndio uzima wetu ulipo.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?

Nini maana ya vifungeni viuno vya Nia zenu? (1Petro 1:13)

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)

Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)

Nitajuaje kuwa nimesamehewa dhambi zangu?

Rudi nyumbani

Print this post

Rhema ni nini, katika biblia?

SWALI: Nimesikia hili neni Rhema, likitajwa sana Kwa watumishi na sehemu mbalimbali, naomba nifahamishwe maana yake Nini, mbona silioni kwenye biblia?


JIBU: Ni vema kutambua kuwa Biblia, katika eneo la agano jipya sehemu kubwa imeandikwa kwa lugha ya kiyunani. Hivyo Kuna baadhi ya maandishi ambayo tukiyasoma katika lugha nyingine mfano kwenye yetu hii ya kiswahili, tunaweza kuona yalimaanisha jambo lile lile moja lakini tukirudi kwenye lugha ya asili ya kiyunani yalimaanisha maana zaidi ya Moja.

Kwamfano, tunapokutana na hili Neno “NENO”. kwenye tafsiri yetu ya kiswahili, Mahali pote limeandikwa hivyo hivyo tu “Neno” likimaanisha Neno la Mungu.

Lakini tukirudi  kwenye lugha ya asili ya kiyunani zipo sehemu limelitajwa kama “Logos”na sehemu nyingine kama “Rhema”

Logos ikiwa na maana Neno la Mungu la Daima/ wazo la Mungu/mpango wa Mungu ulioandikwa  na pia kama Yesu Kristo mwenyewe, ambaye ndio Neno lililofanyika mwili.

Lakini ‘Rhema’: maana yake ni “Neno lililosemwa na Mungu” . Ni neno la wakati husika, sio la daima.

Mfano wa maandiko yanayolitaja Neno kama Logos ni haya: Yohana 1:1-18, Yakobo 1:22, Waebrania 4:12. N.k

Na mfano wa maandiko yanayolitaja Neno la Mungu kama Rhema ni haya;

Mathayo 4:3-4

[3]Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. [4]Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

Hapo Bwana aliposema, “ila Kwa Kila Neno litokalo katika kinywa Cha Bwana”..alimaanisha Neno lisemwalo na Bwana.. mfano wa Eliya alipomwambia yule mwanamke mjane, Bwana asema hivi; “lile pipa la unga halitapinguka, Wala Ile chupa ya mafuta haitaisha”. (1Wafalme 17:14). Halikuwa Neno ambalo lilitumika Kwa wakati wote, ambalo hata sasa tunaweza litumia sisi, Bali la wakati ule ule tu, amefunuliwa, akalisema na ikiwa hivyo.

Lakini ‘Rhema’ ni yaliyonenwa Kwa wakati huo tu..tofauti ya Yale yaliyokuwa Daima.

Neno lingine ambalo linasomeka kama Rhema katika biblia,. Ni wakati ule mitume wamehangaika usiku kucha kutafuta samaki, lakini kulipokucha Yesu akawaambia watweke.mpaka vilindini wakavue. Petro akasema maneno haya;

Luka 5:5

[5]Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.

Aliliamini Neno lililosemwa na Bwana (na ikiwa vile).

Ili kuelewa vizuri tunaweza kusema  “logos” ni BIBLIA TAKATIFU, na Rhema’ ni Neno mtu analofunuliwa Kwa kipindi Fulani.

JE! MUNGU ANASEMA NA SISI HATA SASA KAMA RHEMA?

Ni kweli Mungu ameshatupa njia yake kuu ya kusema na sisi, ambayo ni Kwa kupitia Biblia. Lakini pia bado Mungu anasema nasi, na kutushushia Neno lake Kwa wakati husikia litufae.

Tuwapo katika kanisa. Mungu hutumia karama mbalimbali, kusema nasi, au kutupa ujumbe wake. Anasema kutumia unabii au fundisho, au Neno la hekima, au maono, au ndoto, kutuwasilishia Neno lake.

Lakini pia ni lazima tujue kuwa Neno hilo lililofunuliwa ni sharti lisikinzane na Neno lake lililoandikwa. Vyote viwili vikichanganyikana huleta matokeo makamilifu na kutufanya tumwone Mungu katika uhalisia wake zaidi katika maisha yetu, kwasababu yeye Yu hai.

Lakini ipo hatari kubwa sana. Kwani katika siku hizi za mwisho wapo baadhi ya watu wanalichukua Neno liliokuwa kama Rhema, na kulifanya logos yao. Ndio hapo wanaposoma Bwana Yesu alitema mate chini akachanganya na udongo, akampaka mtu machoni akaona, hivyo na wenyewe wanafanya hivyo Kwa kisingizio kuwa andiko limeruhusu. Au wanapomsoma mtume Paulo anatoa leso yake, Kisha watu wanapona kupitia Ile, na wenyewe wanafanya hivyo hivyo, wakisema andiko limeruhusu. Hawajui kuwa ulikuwa ni ufunuo wa wakati ule ambao si agizo kuu, ni Rhema’. 

Na madhara ya jambo hili ndio linageuka kuwa ibada ya sanamu. Tunayo mifano kadhaa katika biblia ya watu ambao waligeuza Rhema kuwa Logos, ikawapelekea kuingia katika laana. Kipindi Wana wa Israeli wakiwa jangwani, walipomkosea  Mungu alimwagiza Musa aunde nyoka wa shaba, ili Kila amtazamaye apone. Na kweli ilikuwa vile. Lakini baada ya pale haikuwa sheria mama kama vile torati, kana kwamba waendelee kufanya vile.  lakini tunaona baadhi ya watu walikuja kuifanya kama ndio sehemu Yao ya ibada ya uponyaji Kwa Mungu,.mpaka Mungu akachukizwa ikawapelekea kupelekwa tena utumwani Babeli, ikiwa kama mojawapo ya sababu.(2Wafalme 18:4)

Agizo letu la wakati wote ni JINA LA YESU TU! ndio logos yetu Bwana aliyotuagiza tutumie, wakati wote. Ikiwa hujafunuliwa kutumia kisaidizi/kiambatanishi kingine basi usifanye kwani huyo sio Mungu nyuma yake. Tegemea Biblia zaidi.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

Kujikinai/kukinai ni nini?

Neno hilo kama linavyotumika kwenye biblia..linamaanisha aidha mojawapo ya mambo haya matatu:

  1. Kushiba Hadi kufikia hatua ya kutokipenda Tena kile ulichokipokea Mwanzo.
  2. Kuwadharau wengine Kwa kufanya mambo ambayo huruhusiwi kuyafanya
  3. Kujigamba/kujiona wewe unajitosheleza Kwa HAKI yako.

1. Kwamfano katika vifungu hivi limetumika kwa tafsiri ya kushiba,..

Mithali 27:7

[7]Nafsi iliyoshiba hukinai sega la asali;  Bali nafsi yenye njaa huona kila kitu kichungu kuwa kitamu.

Mithali 25:17

[17]Mguu wako usiingie katika nyumba ya jirani yako ila kwa kiasi;  Asije akakukinai na kukuchukia.

Mhubiri 1:8

[8]Mambo yote yamejaa uchovu usioneneka, jicho halishibi kuona, wala sikio halikinai kusikia.

2). Lakini pia vifungu hivi, vinaeleza kukinai kama kuonyesha kudharau wengine, kwa kukaidi maagizo kwa makusudi.

Kumbukumbu la Torati 17:12

[12]Na mtu afanyaye kwa kujikinai, kwa kutomsikiza kuhani asimamaye hapo kwa kumtumikia BWANA, Mungu wako, au mwamuzi, na afe mtu huyo; nawe utauondoa uovu katika Israeli.

Soma pia.. Kutoka 21:14

3) Halikadhalika mahali ambapo kunaonesha kujikinai kama kujihesabia haki mwenyewe ni hapa

Luka 18:9-14

[9]Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.

[10]Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.

[11]Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.

[12]Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.

[13]Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.

[14]Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

Soma pia 2Petro 2:11, 

Hivyo na sisi hatupaswi kuwa na sifa hizo mioyoni mwetu. Uendapo mbele za Bwana, Acha kujihesabia haki, Bali jinyenyekeze penda kuomba rehema Kwa Bwana, zaidi ya kueleza sifa zako..na hatimaye Mungu atakuridhia, kwasababu Mungu anawapinga wenye kiburi na kuwapa neema.wanyenyekevu.

Amen

Je! Umeokoka? Ikiwa bado na unapenda Kristo akusamehe dhambi zako zote, na akupe uzima wa milele. Basi fungua hapa ili uweze kupata mwongozo sala ya toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?

Mawaa ni nini? Kama tunavyosoma katika biblia?

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

Tofauti ya deni na dhambi ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

“Romans road to salvation”

Njia ya wokovu ndani ya kitabu Cha Warumi ni Nini? 

Ni mpango wa wokovu wa mwanadamu, ambao umeainishwa vyema kutoka katika kitabu Cha Warumi.

Kitabu hichi kinaeleza jinsi mtu anavyoweza kuupokea wokovu kutoka Kwa Mungu.

Hivyo ikiwa wewe bado hujaufahamu mpango wa Mungu kwako, wa namna ya kuupokea wokovu basi kitabu hichi kimeanisha vifungu ambavyo vinakuonesha ni jinsi gani utaweza kuupokea.

Lakini pia ikiwa wewe hujui ni wapi pa kuanzia unapokwenda kuwashuhudia watu habari za wokovu, basi kitabu hichi kinakupa mwongozo wa namna ya kuwahubiria wengine habari njema. Na vifungu muhimu vya kusimamia..

Hivi ni vifungu “mama”

Cha kwanza: Warumi 3:23

Warumi 3:23

[23]kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;

Tuendapo Kwa Mungu, lazima tujue hakuna mwenye haki hata mmoja sote Tumepungukiwa na utukufu wa Mungu. Tumetenda dhambi, Vilevile ikiwa wewe ni mhubiri/mshuhudiaji, huna budi kumuhubiria mtu jambo hilo, kwamba hakujawahi kutokea mwema hapa duniani. Hivyo wote tunauhitaji mpango wa Mungu wa wokovu katika maisha yetu.

Kifungu Cha pili: Warumi 6:23

[23]Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.

Hapa, Mungu anatuonesha, matokeo ya kudumu katika dhambi zetu, ambazo wote tulikuwa nazo, kuwa ikiwa tutaendelea kubaki katika Hali hiyo hiyo basi tutakutana na mauti ya milele, lakini tukipokea zawadi ya Mungu basi tutapata uzima wa milele.

Kifungu Cha Tatu:  Warumi 5:8

[8]Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.

Kwamba sasa hiyo zawadi ya Mungu ambayo itapelekea uzima wa milele ni Yesu Kristo, yeye ndiye aliyetolewa na Mungu kuzichukua dhambi zetu zote, kwa kifo cha pale msalabani. Pale tuliposhindwa sisi wenyewe basi Yesu alikuja kutusaidia kuchukua makosa yetu.

Kifungu Cha nne: Warumi 10:9-10.

Hiki sasa kinaeleza Namna ya kuupokea wokovu;

Warumi 10:9-10

[9]Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

[10]Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.

Kwa kuamini kwetu kuwa Yesu Yu hai, na kwamba anakomboa wanadamu, na vilevile kumkiri Kwa kinywa kuwa ndiye Bwana na mwokozi wetu. Basi tunaupokea msamaha huo wa dhambi Bure, bila gharama yoyote. Na deni letu la dhambi linakuwa limefutwa tangu huo wakati

Hivyo ni sharti ujue kuwa msamaha wa dhambi hauji Kwa matendo Yako mema, Bali unakuja Kwa kuikubali kazi ya Yesu msalabani iliyofanyika Kwa ajili ya ukombozi wako.

Halikadhalika Wewe kama mshuhudiaji vifungu hivi viwepo kichwani mwako.

Kifungu Cha tano cha mwisho: Warumi 5:1

[1]Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,

Maana yake ni kuwa baada ya mtu kumkiri Kristo, na kumkubali kama Bwana na mwokozi wake. Basi anapaswa awe na AMANI na Mungu kwasababu hakuna mashtaka yoyote ya adhabu juu yako. Hakuna hukumu yoyote ya mauti ipo juu yake.

Huo ndipo mpango wa awali wa wokovu wa Mungu Kwa mwanadamu. Ambapo tunapaswa kufahamu kama ulivyoanishwa katika  kitabu hichi Cha Warumi.

Kisha baada ya hapo tunawafundisha watu kuitimiza haki yote au kusudi lote la Mungu juu yetu, Ikiwemo ubatizo wa maji, na ule wa Roho Mtakatifu.

Ikiwa bado hujaokoka, na utapenda kuupokea msamaha wa Yesu Bure maishani mwako, basi Unaweza kuwasiliana na sisi Kwa namba uzionazo chini ya chapisho hili kwa ajili ya mwongozo huo Bure. Vilevile na Ule wa ubatizo.

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?

Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?

USIISHIE TU KUPATA HAKI, BALI PATA NA WOKOVU.

Rudi nyumbani

Print this post