Category Archive Uncategorized

WAPENDENI ADUI ZENU, WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

Nakusalimu katika jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuyatafakari maneno ya uzima.

Tukimtafakari Yesu, jinsi alivyopendwa na Mungu kiasi cha kukabidhiwa vyote na Baba, jinsi alivyojaliwa kutenda miujiza mikubwa ambayo hata vitabu vyote  duniani vingeandika habari zake visingetosha kueleza biblia inasema hivyo, tunatamani sana kuwa kama yeye. Yesu ni mtu pekee ambaye alikuwa akimwomba Mungu kitu chochote anapewa saa hiyo hiyo, Lakini mwisho wa siku anakuja kutoa siri ya kukubaliwa kwake..Siri ambazo anasema manabii wengi na wafalme walitamani kuyafahamu hayo wasiyafahamu(Luka 24:10). Lakini mimi na wewe tunazifahamu.

Na siri mojawapo ni hii inayohusiana na namna ya kudili na maadui zetu na wale wanaotuudhi. Alisema hivi,

Mathayo 5:44  “lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi”,

Mwanzoni nilipokuwa nasoma huu mstari nilidhani  nimeulewa vizuri, lakini baadaye nilikuja kujua kimatendo kuwa nipo mbali sana nao, nilipotafakari matukio ambayo niliudhiwa na watu, Na muda niliotenga kuwaombea hao watu walioniudhi na kunichukia.. Nikagundua kuwa sijawahi kufanya hivyo.

Ni kweli nilisamehe, lakini kusamehe kwangu kuliishia tu katika ‘kusamehe’  na baada ya hapo ikawa ni kujiepusha naye ili asiniudhi tena. Lakini kwa Mungu huo bado sio ukamilifu, Ukamilifu ni kumwombea huyo anayekuudhi.. Na Zaidi sana kumpenda yule ambaye unahisi ni adui kwako.

Bwana wetu Yesu Kristo ni mtu aliweza kuishi kile alichokisema, Vinginevyo angekuwa ni mnafki.. Yeye ni mtu ambaye aliweza kuishi na mmoja wa maadui zake hatari sana. Adui aliyemuuza mbele ya macho yake. Na huyo si mwingine Zaidi ya Yuda. Yesu alimjua tangu mwanzo kuwa  ndiye atakayemsaliti, Lakini hakuwahi kumfukuza, hakuwahi kumnenea mabaya, Zaidi sana alimwita RAFIKI, na pale alipokula chakula kizuri alimchagua Yuda kula naye(Yohana 13:18).. Na tunajua Yesu si mnafki, alipomwita Yuda rafiki(Mathayo 26:50), alimaanisha kweli, kwamba yule alikuwa ni rafiki yake tena hata Zaidi ya mitume wengine.

Tengeneza picha Japo Yesu alijua unafiki wake, lakini ndani yake hakukuwa na sababu ya kutomwona kama yeye ni rafiki tu. Aliweza kuishi naye miaka yake yote ya kiutumishi, akamwongezea na neema juu ya kutoa Pepo na kufanya miujiza. Alipopanda kuwaombea wanafunzi wake, alimwombea na Yuda pia, japokuwa alijua kuwa huyo ndiye msaliti wake. Yuda hakuwahi kumrudishia fadhili Yesu wakati wowote, hata kipindi kile yule mwanamke anamwagia marahamu, yeye bado alipinga. Lakini Yesu alimpenda.

Tujiulize na sisi tuliookoka tunaweza kuwa kama mwana wa Mungu Yesu Kristo. Kuishi na maadui zetu tunaojua wanakwenda kutuchinja na Zaidi sana tunawaombea na kuwabariki? Huo ndio ukamilifu ambao Mungu anataka kuuona kwetu.

Hii ndio sababu kwanini Yesu anasema tuwe watu wa namna hiyo na si vinginevyo anasema..

 Mathayo 5:45  “ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki”.

Umeona? Kwasababu tabia ya Mungu ndio hiyo, anawarehemu watu wote, wanaomshukuru na wasiomshukuru, hata maadui zake, anawapa chakula. Kwasababu anajua huwenda siku moja watatubu. Hata sisi pia kabla ya kuokolewa, tulikuwa katika dhambi, tulimkosea sana yeye, lakini hakututendea jambo lolote baya, akatusamehe,. Vivyo hivyo anataka na sisi tufanye kwa maadui zetu, na kwa wale wanaotuchukia.

Ikiwa ni mfanyakazi wako anakuudhi, chukuliana naye tu..Hamna namna, mwombee, mbariki, usiwe mwepesi kumfukuza kazi. Ikiwa ni mpendwa mwenzako anakukwaza mara kwa mara, hupaswi kumsamehe tu na kujiepusha naye mbali, bali umwombee, na Zaidi umwite rafiki yako.

Tabia kama hii, haitokani na sisi wanadamu bali na Mungu, kwa nguvu zetu hatutaweza, lakini tukiwa na Neno la Mungu sana mioyoni mwetu, atatusaidia kuidhihirisha tabii yake hii ya kiMungu. Na kama tukifaulu kushinda, Basi tujue ndivyo Baba atakavyotukaribia, na kujifunua kwetu. Kwasababu tunafanya yanayompendeza.

Hivyo, tumwombe Bwana atusaidie, na sisi tuonyeshi bidii katika kudhihirisha jambo hilo, ili tuwe wakamilifu kama yeye alivyomkamilifu.

Tahadhari:

Epuka mahubiri, unayoambiwa walete maadui zako hapa tuwapige kwa moto wa Roho Mtakatifu wafe. Epuka sana, hayo hayakusaidii kitu Zaidi sana yanakuongezea chuki na visasi moyoni mwako. Ambayo ni zao la shetani na sio Roho Mtakatifu. Bali penda ushauri wa Bwana Yesu, kisha uutende hata kama ni mgumu, lakini ndio njia yenyewe ya kumfikia Mungu, hakuna nyingine.. Wapende maadui zako, kisha waombee

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

RACA

UMUHIMU WA KUBATIZWA.

USIMPELEKEE BWANA MASHITAKA, YA MAADUI ZAKO.

YAFAHAMU MAPENZI KAMILI YA MUNGU KWA MAADUI ZAKO.

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?

SWALI: Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani? Ni mpangalio wake upoje kulingana na mwandishi?


JIBU: Kitabu Cha Zaburi hakikuandikwa na mtu mmoja, Bali ni mjumuisho wa waandishi mbalimbali. Kitabu hiki ndio kilichoandikwa na waandishi wengi kuliko vyote kwenye biblia.

Kiliandikwa katika nyakati mbalimbali Kwa kipindi Cha miaka elfu moja na zaidi..kitabu hiki kimebeba mashahiri, maombolezo, nyimbo na maombi.

WAANDISHI:

  1. DAUDI

Mfalme Daudi ndiye aliyeandika Kwa sehemu kubwa  kitabu hichi; 

Jumla Zaburi zilizojuliakana kuwa zimeandikwa na Daudi ni 73. Lakini pia zipo nyingine 2 ambazo hazikutajwa moja Kwa moja lakini waandishi wengine katika nyaraka zao walinukuu baadhi ya maneno kwenye Zaburi, na kusema ni ya Daudi.

Ambazo ni Zaburi 2 ambayo sehemu ya maandishi hayo yanatajwa katika Matendo 4:25, 

Na Zaburi 95 Waebrania 4:7

Hivyo kudhaniwa kuwa Daudi aliandika Zaburi 75;

Hizi ndio orodha ya hizo Zaburi 73 alizoziandika yeye;

3-9

11-32

34-41

51-65

68-70

86

101

103,

 108-110

122

124

131

133

138-145

2. SULEMANI

Mwandishi mwingine ni Sulemani yeye aliandika Zaburi mbili tu..ambazo ni  Zaburi 72 na Zaburi 127″

3. ETHANI na HEMANI

Nyingine zimeandikwa na Ethani na Hemani, Hawa ni watu ambao waliokuwa na hekima nyingi mfano wa Mfalme Sulemani, wanatajwa katika vifungu hivi;

1 Wafalme 4:30-31

30 Hekima ya Sulemani ikapita hekima ya wana wote wa mashariki, na hekima zote za Misri.31 Kwa kuwa alikuwa na hekima kuliko watu wote; kuliko Ethani Mwezrahi, na Hemani, na Kalkoli, na Darda, wana wa Maholi; zikaenea sifa zake kati ya mataifa yote yaliyozunguka.

Ethani aliandika Zaburi moja tu nayo ni Zaburi 89

Hemani pia aliandika Zaburi moja ambayo ni Zaburi 88

4. MUSA

Mwandishi mwingine alikuwa ni  Musa yeye pia aliandika Zaburi 1 ambayo ni ya 90.

5. ASAFU

Zaburi nyingine 12 ziliandikwa na Asafu na familia yake.

Ambazo ni 

50, 73-83

6. WANA WA KORA

Wana wa Kora, waliandika Zaburi 11

  42, 44-49,84-85, 87-88 

7. WASIOTAMBULIKA

Na Zaburi nyingine 48, zilizobakia hazijulikani waandishi wake.

Hivyo Kwa ufupisho ni kwamba Daudi aliandika Zaburi 73, Sulemani 2, Musa 1, Ethani 1, Hemani 1, Asafu 12, Wana wa Kora 11, wasiotambulika ni 48.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata uchauzi zaidi ya kitabu Cha Zaburi pitia link hii >> https://wingulamashahidi.org/2020/11/27/vitabu-vya-biblia-sehemu-ya-9-kitabu-cha-zaburi/

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.

Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Neno hili limetajwa mara moja katika biblia, kwenye kitabu cha;

Matendo 1:12 “Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato”.

Ni mwendo ambao ulitengwa maalumu wa mtu kusafiri siku ya sabato, ambao urefu wake ulikuwa ni dhiraa elfu mbili (2000), ambao ni sawa na Kilometa moja kwa makadirio.

Kutoka mlima wa mizetuni mpaka mjini Yerusalemu, ni umbali uliokuwa  ndani ya hiyo kilometa moja, ndio huo walisafiri mitume wa Bwana siku hiyo.

Lakini Je! Agizo hilo tunalipata wapi katika agano la kale?

Hakuna andiko la moja kwa moja katika torati ya Musa linaloeleza kuwa mwendo wa sabato, ulipaswa uwe ndani ya hizo dhiraa elfu mbili. Bali Marabi wa kiyahudi baadaye walidhani hivyo kulingana na uhalisia wa maandiko haya.

Kutoka 16:29 “Angalieni, kwa kuwa Bwana amewapa ninyi hiyo Sabato, kwa sababu hii huwapa siku ya sita chakula cha siku mbili; kaeni kila mtu mahali pake, mtu awaye yote asiondoke mahali pake kwa siku ya saba

Kwamba anaposema Usiondoke mahali pako, anamaanisha ndani ya mipaka ya mji wako, hii ikiwa na maana ukiwa ndani ya mipaka uliruhusiwa kutembea, utakavyo. Na kama ikitokea unatoka, basi hupaswi kusafiri Zaidi ya hizo dhiraa elfu 2000.

Na hiyo waliirithi kufuatana na sheria ya malisho ya nje ya mji ambayo walipewa walawi katika..

Hesabu 35:4 “Na yale malisho ya miji mtakayowapa Walawi, ukubwa wake utakuwa tangu ukuta wa mji kupima kiasi cha dhiraa elfu pande zote.  5 Nanyi mtapima hapo nje ya mji upande wa mashariki dhiraa elfu mbili, na upande wa kusini dhiraa elfu mbili, na upande wa magharibi dhiraa elfu mbili, na upande wa kaskazini dhiraa elfu mbili, huo mji ulio katikati. Hayo ndiyo yatakayokuwa kwao malisho ya miji”.

Hivyo kwa kurejea sheria hizo, wakahitimishi kuwa mwendo wa mtu kusafiri nje ya mji siku ya sabato ni hizo dhiraa elfu mbili(2000) au kilometa moja . Ndio Wakauita mwendo wa Sabato. Lakini hakukuwa na sheria ya moja kwa moja inayoeleza mwendo huo ulipaswa uwe katika vipimo hivyo.

Lengo la kufanya vile ni kuwafanya watu wasitawanyike mbali na eneo la kuabudia, ndani ya mji, siku hiyo ya Bwana.

Hata sasa. Ni lazima Kila mmoja wetu awe na mwendo wake wa sabato katika siku ya Bwana..kumbuka jumapili ni siku ya Bwana, hupaswi kwenda mbali na uwepo wa Mungu, siku hiyo sio siku ya kufanya biashara, sio siku ya kwenda kwenye mihangaiko isiyokuwa na lazima, Bali ni siku maalumu Kwa ajili ya ibada..penda kuwepo kanisani, mikutanoni, kwenye semina, kwenye mafundisho redioni,mitandaoni, kwenye vitabu vya kiroho.n.k.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

Je ni kweli ilikuwa desturi ya Bwana kuishika sabato?(Luka 4:16)

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

Rudi nyumbani

Print this post

Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?

SWALI: Kwanini vitabu vya biblia vipo katika mtiririko ule, na sio kinyume chake?

Ni vema kufahamu kuwa mtiririko wa kibiblia wa agano la kale na agano jipya, haukuwekwa na Mungu, kwamba kianze kitabu hiki kifuate hiki, kianze cha Mwanzo kisha kifuate cha Kutoka. Hapana bali ni utaratibu uliowekwa na wanadamu, ambao kimsingi unamaudhui mazuri, na uligawanya hivyo ili kumsaidia msomaji kufahamu vizuri, kuliko vingeorodheshwa  tu kila kimoja eneo lake, ingewia nguvu kwa msomaji anayependa kujifunza Biblia kuelewa kiwepesi.

Mtiririko ambao sisi tunaoutumia ni tofauti na mtiririko ambao Wayahudi wanautumia kwa vitabu vya agano la kale.

Kwa mfano mtiririko wetu (Ambao unajulikana kama mtiririko wa kiprotestanti), una vitabu 39 vya Agano la kale. Lakini mtitiriko wa Kiyahudi, una vitabu 24 kwa agano hilo hilo la kale,.

Vitabu vyetu ni kama vifuatavyo

Vitabu vya Sheria

  1. Mwanzo
  2. Kutoka
  3. Mambo ya Walawi
  4. Hesabu
  5. Kumbukumbu la Torati

Vitabu vya Historia

  • Yoshua
  • Waamuzi
  • Ruthu
  • 1Samweli
  • 2Samweli
  • 1Wafalme
  • 2Wafalme
  • 1Mambo ya Nyakati
  • 2Mambo ya Nyakati
  • Ezra
  • Nehemia
  • Esta

Vitabu vya Mashairi

  1. Ayubu
  2. Zaburi
  3. Mithali
  4. Mhubiri
  5. Wimbo ulio bora

Vitabu vya Manabii (Wakubwa)

  • Isaya
  • Yeremia
  • Maombolezi
  • Ezekieli
  • Danieli

Vitabu vya manabii (Wadogo)

  • Hosea
  • Yoeli
  • Amosi
  • Obadia
  • Yona
  • Mika
  • Nahumu
  • Habakuki
  • Sefania
  • Hagai
  • Zekaria
  • Malaki                                                     

Lakini utajiuliza kwanini biblia ya kiyahudi iwe na vitabu 24 na sio 39? Je vingine vimeondolewa? Jibu ni hapana, bali baadhi yao vilijumuishwa kama ni kitabu kimoja kwamfano.

> Vitabu viwili vya wafalme kwao ni kitabu kimoja.

> Vitabu viwili vya Mambo ya Nyakati kwao ni kitabu kimoja.

> Vitabu viwili vya Samweli kwao ni kitabu kimoja.

> Ezra na Nehemia vimeweka kama kitabu kimoja.

> Vitabu 12 vya Manabii wadogo kwao ni  kitabu kimoja.

Jumla yake ni vitabu 24 Badala ya 39.

Hivyo tukirudi katika biblia yetu, yenye vitabu 39 kwa agano la kale, Orodha ile haijawekwa kulingana na vipindi vilipoandikwa, bali kulingana na ‘asili ya vitabu’. Ndio hapo utaona hiyo migawanyo mikuu mitano (Yaani vitabu vya Sheria, vya historia, vya mashairi, vya Manabii wakubwa na wale wadogo).

Kutaja manabii wakubwa haimaanishi kuwa walikuwa na vyeo vya juu au walikuwa na nguvu zaidi ya wale wengine hapana, bali ni kutokana na wingi wa uandishi wao, yaani waliokuwa na uandishi mwingi waliwekwa katika kundi hilo la manabii wakubwa.

Tukirudi katika agano jipya.

Vipo vitabu 27, na vyenyewe pia havijaandikwa kulingana na wakati wa uandishi, japo havipishani sana na wakati wa uandishi.

Huu ndio mgawanyo wake.

Vitabu vya Injili

  1. Mathayo
  2. Marko
  3. Luka
  4. Yohana

Kitabu cha Historia

  • Matendo

Nyaraka za Paulo

  • Warumi
  • 1Wakorintho
  • 2Wakorintho
  • Wagalatia
  • Waefeso
  • Wafilipi
  • Wakolosai
  • 1Wathesalonike
  • 2Wathesalonike
  • 1Timotheo
  • 2Timotheo
  • Tito
  • Filemoni

Nyaraka kwa wote

  1. Waebrania
  2. Yakobo
  3. 1Petro
  4. 2Petro
  5. 1Yohana
  6. 2Yohana
  7. 3Yohana
  8. Yuda

Unabii

  • Ufunuo

Halikadhalika Nyaraka za Mtume Paulo ziliorodheshwa katika mpangilio ule kutoka na  urefu wa uandishi na sio umuhimu wa nyaraka Fulani zaidi ya nyingine, kwamfano utaona kitabu cha kwanza kwa urefu cha Mtume Paulo ni Warumi na ndio kilichowekwa cha kwanza. Vilevile kirefu zaidi ya vyote alivyoviandika kwa Watu, ni cha Timotheo ndicho kilichopangiliwa cha kwanza.

Lakini pamoja na kwamba havikuweka katika mpangalio wa nyakati za uandishi bado zinamtiririko mzuri unaelekeana na historia, kuanzia kitabu cha Mwanzo mpaka ufunuo.  Japo pia katika usomaji haimaanishi ufuate mtiririko huo, bali unaweza kuanza vyovyote upendavyo kwa jinsi Roho Mtakatifu atakavyokuongoza.Kwasababu hakuna sehemu yoyote katika maandiko tumewekewa mtiririko huo.

Pia zipo biblia nyingine mfano ile ya Kikatoliki yenye vitabu 73, ambayo kimsingi haijavuviwa na Roho wa Mungu kwani kuna baadhi ya vitabu vimeongezwa ambayo hukinzana na mafundisho ya msingi ya imani, na hivyo hatupaswi kuifuata. Biblia yetu ina vitabu 66 tu. Kama vilivyoorodheshwa hapo juu. Zaidi ya hivyo hutoka kwa Yule mwovu.

Bwana akubariki sana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

HISTORIA YA BIBLIA YA KING JAMES, INA FUNZO GANI KWETU?

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya kiMungu?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?

SWALI: Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?


Mimbari ni eneo lililoinuka ambalo limetengwa rasmi katika kanisa kwa ajili ya Neno la Mungu kuhubiriwa, au taarifa za kikanisa kuwasilishwa, au huduma nyingine za kiibada kutendeka kama vile uimbaji wa kwaya.

Lakini Madhabahu ni eneo la kanisa ambalo watu huenda kuomba, kutoa sadaka, kupeleka shukrani na sifa, na kushiriki meza ya Bwana (yaani mahali pa kukutana na Mungu). Madhabahuni pa Mungu sio tu pale mbele ya kanisa, bali ni lile eneo lote la kanisa. Isipokuwa tu lile la mbele ndio linasimama kama kitovu cha madhabahu yote.

Mara nyingi mimbari pia huwa palepale madhabahuni. Hivyo unaweza kusikia mtu anasema nakwenda kusimama madhabahuni kuhubiri, mwingine utamsikia anasema nakwenda kusimama mimbari. Wote wawili hawajabadili maana.

Hivyo ikiwa unakwenda kwa kuhubiri, au kuhutubu, au kuimba kwaya kiuhalisia hapo ni sawa na unasimama mimbarani, lakini ikiwa unakwenda kwa ajili ya kuomba, kutoa sadaka, kufanya ibada kama kusifu na kuabudu, hapo huisogelei mimbara bali madhahabu ya Mungu.

Mimbarani ni mahali pa kusikilizwa, lakini madhabahuni, ni mahali pa kushiriki

Mambo ambayo hupaswi kufanya mimbarani kama mhubiri.

  • Kutoka toka sana nje ya mimbari pindi uhubiripo
  • Kufundisha maudhui ambayo ipo nje ya Neno la Mungu. Mfano, siasa, michezo
  • Kujigamba/ Kujisifu zaidi ya kumtukuza Kristo
  • Kupuuzia kujiandaa, kimaombi na kiroho, kabla ya kusimama mimbarani

Mambo ambayo hupaswi kufanya uwapo madhahabuni kama mshirika.

  • Usitoe sadaka yako kama una neno na ndugu yako.(Mathayo 5:23-24)
  • Usivae mavazi yasiyo na utukufu machoni pa Bwana
  • Usizunguke zunguke, au kuzungumza ovyo uwapo kanisani (kuwa mtulivu). Kumbuka eneo lote la kanisa ni madhabahu ya Mungu, na sio pale mbele tu.
  • Hakikisha huchelewi kufika madhabahuni pa Mungu, wala huikatishi ibada na kuondoka

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?

Biblia inasema tujihadhari na “Mbwa” hawa mbwa ni akina nani? (Wafilipi 3:2)

UPAKO NI NINI?

Rudi nyumbani

Print this post

USIKWEPE USHIRIKA NA MADHABAHU YA KRISTO.

Upo umuhimu wa kufanya ushirika.

Ushirika unatokana na neno kushiriki.  Na matokeo ya kushiriki ni kuambukizwa sifa au tabia ya kile kitu unachoshirikiana nacho.

Watu wengi hatujui hata Neno USHIRIKINA limetokana na neno kushiriki. Washirikina wanashiriki mambo ya kipepo, ili wapate sifa za kipepo, au waambukizwe tabia zao ndani yao na ndio maana wanaitwa washirikina. Ndio hapo utaona mtu anakwenda kwa mganga, kisha anapewa dawa Fulani anaambiwa anywe au aweke chini ya biashara yake, halafu itamfanya wateja wavutiwe na biashara yake. Mtu huyo analivuta pepo la mauti ndani yake, kwa ushirika anaoufanya kisa lile pepo linasimama pale na kushawishi watu waovu , kisha Yule mtu anapata anachokitafuta kwa muda, halafu mwisho wa siku pepo lile linageuka na kumuua,.kwasababu hatma ya shetani sikuzote ni kuchinja na kuiba. Lakini ikiwa mtu huyo hatofanya ushirikina wowote, hawezi kuwa na uwezo huo wa kipepo.

Sasa na katika Mungu ni vivyo hivyo. Unapokuwa nyumbani mwa Mungu Usiwe ni mtu wa kwenda na kutoka tu, kama mtembeleaji. Huna ushirika wowote na watakatifu wengine, huna ushirika wowote na Mungu,. Ukifanya hivyo hutakuwa na nguvu zozote au sifa au tabia zozote za ki-Mungu ndani yako.

Ushirika wa Kikristo Ni upi?

  1. Kuhudumu
  2. Meza ya Bwana
  3. Kutawadhana miguu

Kwamfano Unapohudumu, yaani unapojishughulisha na jambo Fulani ndani ya Kanisa labda kufundisha, kujitoa kwa ajili ya maendeleo ya kanisa kama kuchagia, kufagia, kujenga, kupiga deki, na vyovyote vile. Hapo ni sawa unafanya ushirika na watakatifu wengine katika kuujenga mwili wa Kristo. Na hivyo rohoni, unapokea uwezo au sifa nyingine ya ziada ambayo hapo kwanza ulikuwa huna. Na moja ya uwezo huo ni ni nguvu ya kuendelea mbele katika imani.

Na pia Meza ya Bwana. Huna budi kushiriki. Kwasababu hiyo inakuunganisha na Mungu moja kwa moja. Embu soma maandiko haya upate kuelewa vema;.

1Wakorintho 10:14  “Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu. 15  Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo.

16  Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, JE! SI USHIRIKA wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, SI USHIRIKA wa mwili wa Kristo? 17  Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja.

18  Waangalieni hao Waisraeli walivyokuwa kwa jinsi ya mwili; wale wazilao dhabihu, je! Hawana shirika na madhabahu? 19  Basi niseme nini? Ya kwamba kile kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu? Au ya kwamba sanamu ni kitu?

20  Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani”.

Umeona? Kumbe kikombe na mkate ule ni USHIRIKA.. ambao sisi tunafanya na Mungu. Na hivyo una matokeo yake makubwa rohoni. Yesu alisema mtu asipoula mwili wangu, na kuinywa damu yangu hana uzima ndani yake. (Yohana 6:53)

Vivyo hivyo na kutawadhana miguu watakatifu. Unapomwosha mwenzako miguu, maana yake ni kuwa unajishusha na kujinyenyekeza kwake, hivyo unapokea neema ya Upendano wa ndugu ndani yako.

Hivyo kwa ufupi ili utake kupokea tabia zote za Ki-Mungu ndani yako,  kama Upendo, utu wema, furaha, amani, Uvumilivu, huna budi kuwa katika ushirika wake. Nje ya hapo, huwezi.

Matendo 2:41  “Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42  Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali”

Usiukwepe ushirika wa Bwana.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

HUNA SHIRIKA NAMI.

MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.

KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.

HISTORIA YA BIBLIA YA KING JAMES, INA FUNZO GANI KWETU?

WANNE WALIO WAONGO.

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?

Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Rudi nyumbani

Print this post

TUUTAFUTE USEMI MMOJA. TUUJENGE MNARA WA MUNGU

Nakusalimu katika jina tukufu sana la mwokozi wetu Yesu Kristo, Nakualika katika kuyatafakari maneno ya uzima.

Leo tutajifunza siri mojawapo iliyokuwa nyuma ya watu wa zamani, ambayo tukiitumia na sisi italeta mageuzi makubwa sana katika ulimwengu huu tunaoishi. Wengi wetu tunadhani watu wa leo wanayoakili zaidi ya kuwashinda wale, lakini ukweli ni kwamba yapo mambo mengi yalifanywa na watu wa kale, ambayo mpaka leo hatuwezi kuyafanya. Mfano mmojawapo ni yale mapiramidi yaliyopo Misri (ambayo yapo katika maajabu saba ya dunia), teknolojia iliyotumika pale, hadi sasa hakuna ujenzi unaoweza kuwa kama ule, ijapokuwa tunazo teknolojia kubwa na za kisasa.

Tukisoma katika maandiko tunaona, Jinsi Babeli ilivyoanza kujengwa na kusitawi. Lakini hilo halikuwa jambo zito, kwasababu miji mingi pia ilikuwa inajengwa. Jambo lililoipelekea Babeli kuwa tofauti na miji mingine ni pale watu walipotaka kuunda Mnara, ndani ya mji ule, lengo lao likuwa ni kufika MBINGUNI, ili wajipatie jina. Sasa wengi wetu tunaona kama walikuwa ni wajinga kuunda hiyo Projekti yao. Tunadhani walikuwa wanafanya jambo la masiara au walikuwa hawaelewi kitu wanachokifanya. Ni sawa na leo mtu akumbie ninaunda ndege, ambayo itanifikisha mbinguni, ni rahisi kusema amerukwa na akili. Lakini maandiko yanatuonyesha watu hawa, walikuwa wanajua wanachokifanya mpango huo wangeweza kufanikiwa kama Mungu asingeingilia kati. Embu tusome habari hiyo tuombe jambo hilo;

Mwanzo 11:1 “Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja.  2 Ikawa watu waliposafiri pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya Shinari; wakakaa huko. 

3 Wakaambiana, Haya, na tufanye matofali tukayachome moto. Walikuwa na matofali badala ya mawe, na lami badala ya chokaa.  4 Wakasema, Haya, na tujijengee mji, na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina; ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote. 

5 Bwana akashuka ili auone mji na mnara waliokuwa wakiujenga wanadamu.  6 Bwana akasema, Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja; na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya, WALA SASA HAWATAZUILIWA NENO WANALOKUSUDIA KULIFANYA. 

7 Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao.  8 Basi Bwana akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi yote; wakaacha kuujenga ule mji.  9 Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko Bwana akawatawanya waende usoni pa nchi yote”.

Umeona hapo? Mungu hakusema hawa watu wamerukwa na akili, wanafanya kazi isiyokuwa na faida, bali alisema hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya. Maana yake ni kuwa watafanikiwa, Hivyo Mungu akaangalia NGUVU yao ya kufikia adhma yao ipo wapi? Akaona kuwa sio katika ile teknolojia, bali katika ule USEMI MMOJA waliokuwa nao.

Usemi maana yake ni NIA. Hawa watu waliingia maagano,wakapatana kwa moyo mmoja, kwamba kila mmoja atajitoa kwa akili, hali na mali, kuhakikisha Mnara huo unajengeka na kilele chake kinafika mbinguni, hata kama itawagharimu miaka 1000, lakini mwisho wa siku ni lazima wafike mbinguni. Lakini Mungu akaenda kuuchafua usemi wao wakawa hawaelewani baada ya pale, kwasababu walichokuwa wanakijenga ni kwa ajili ya JINA LAO na sio jina la MUNGU. Hivyo Usemi wao ukachafuliwa wakawa hawaelewani, mpaka na lugha zao zikageuzwa pia.

Ni nini Bwana anataka tuone hapo,

Ni nguvu ya USEMI MMOJA.

Na sisi kama kanisa la Kristo lililo hai. Nafasi yetu ya kuufikia utukufu WOTE wa Mungu ulio mbinguni tunao.

Kwasababu Tayari siku ile ya Pentekoste, Roho Mtakatifu alirudisha USEMI HUU mmoja katikati yetu. Na ndio maana siku ile utaona watu walianza kunena kwa lugha za mataifa mengine magheni, kuonyesha kuwa Sasa Mungu anataka mataifa yote wakaribie waliunde taifa la Mungu haijalishi lugha zao, jinsia zao, rangi zao. Alikuwambusha tukio lile la Babeli, kwamba sasa lianze kufanyika tena kwa jina la Bwana.Watu wale wakatii na siku ile ile kanisa likaanza. Mnara wa Mungu ukaanza kujengwa duniani.

Matendo 2:1  “Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.

2  Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. 3  Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

4  Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka. 5  Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. 6  Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.

7  Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? 8  Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo? 9  Warparthi na Wamedi na Waelami, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia.

10  Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu,.11  Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu.

12  Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya?

Na ndio maana hatushangai kwanini Kanisa la kwanza lilikuwa na mapinduzi makubwa sana. Kwa kipindi kifupi sana injili ilinea duniani kote, na walikuwa hawana vyuo vya biblia. Ni kwasababu walikuwa na USEMI mmoja.

Lakini leo kanisa limevunjika vunjika, shetani kalisambaratisha, kachafua lugha yetu. Hata ndani ya kanisa moja kila mmoja anao usemi wake. Ijapokuwa wote mnaliamini Neno hilo hilo moja. Kwasababu gani, ni kwasababu tunatafuta utukufu wetu wenyewe na sio ule wa Mungu.

Ni kweli tutaunganishwa na Neno lakini tusipotaka kujishusha na kutii, ili tumwinue Kristo na sio sisi wenyewe, kamwe hatutaona utukufu wa Mungu kama vile inavyopaswa. Hatutaufikia moyo wa Mungu mbinguni, hatutaona udhihirisho wa wazi wa Miujiza mikubwa ya Mungu katika kanisa. Ni sharti tujikane nafsi zetu kila mmoja tumfuate Yesu , ili tuujenge mnara huu wa Bwana.

Luka 14:27  “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. 28  Maana ni nani katika ninyi, KAMA AKITAKA KUJENGA MNARA, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia? 29  Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki”.

Tufahamu kuwa kanisa sio shirika la kijamii, sio huduma, wala sio chuo Fulani, bali ni udhihirisho wa Mungu duniani kupitia watu wake aliowakomboa. Hivyo ni lazima sisi kama viungo vya Kristo tujishikamanishe tuwe mwili mmoja Ili Kristo atende kazi zake duniani kama alivyokuwa anatenda zamani. Na hii inaanza na mtu mmoja mmoja, pale tunapodhamiria kuyatii maneno ya Kristo.

Bwana atujalie kuliona hilo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?

Pentekoste ni nini?

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?

USIIKARIBIE DHAMBI, KAA NAYO MBALI.

Kibiriti ni kitu gani? kama kinavyozungumziwa kwenye maandiko?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Rudi nyumbani

Print this post

Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma? 

SWALI: Nini maana ya haya maneno Mungu aliyomwambia Ayubu kuhusiana na  tabia za Mbuni?

Ayubu 39:13 Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma?  14 Kwani yeye huyaacha mayai yake juu ya nchi, Na kuyatia moto mchangani,  15 Na kusahau kwamba yumkini mguu kuyavunja, Au mnyama wa mwitu kuyakanyaga.  16 yeye huyafanyia ukali makinda yake, kana kwamba si yake; Ijapokuwa taabu yake ni ya bure, hana hofu;  17 Kwa sababu Mungu amemnyima akili, Wala hakumpa fahamu.  18 Wakati anapojiinua juu aende, Humdharau farasi na mwenye kumpanda. 


JIBU: Ukianzia kusoma mistari michache ya juu katika hiyo hiyo  sura  ya 39, Utaona Mungu anamweleza Ayubu baadhi ya wanyama ambao wanauwezo fulani mkubwa lakini hauwasidii kufanya mambo ya msingi, kwamfano mstari wa 5-8, anamtaja punda-milia, ni mnyama anayefanana na punda, ana nguvu na uwezo wa kukimbia zaidi hata ya punda, lakini je! Anamuuliza Ayubu unaweza kumkamata na kumfanya mtumwa wako akubebe mizigo? Au akulimie. Jibu ni la!

Mstari wa 9-12, anamtaja tena, Nyati, anamsifia nguvu zake, kwamba ni nyingi sana, lakini je utaweza kumfunga nira na kumwambia akulimie shamba lako kama ufanyavyo kwa ng’ombe? Jibu ni la kwasababu jambo hilo halipo ndani yake.

Na hapa kwenye mstari wa 13-18 Anamtaja tena Ndege mbuni na sifa zake. Anasema mabawa yake ni bora na mazuri, kiasi cha kuweza kuyatamia vema mayai ardhini zaidi ya ndege wengine wote duniani. Lakini kinyume chake ni kuwa mbuni ni ndege asiyejali mayai wala vifaranga vyake kuliko ndege wote unaowafahamu. Japokuwa anaouwezo mkubwa wa kuwashinda maadui zaidi ya ndege wote, lakini uwezo wake hautumii katika mambo yaliyo na faida. Mbuni anataga popote tu, hata kando ya njia,

hawezi kutafuta sehemu iliyo salama kama ndege wengine ambao huenda sehemu za maficho na kutaga huko ili watoto wao wawe salama pindi wazaliwapo lakini yeye hilo halijali, anataga popote apaonapo, matokeo yake ni aidha mayai yake kukanyagwa na wanyama wakubwa au kuibiwa na kenge au wanyama wengine wezi. Mbuni anaouwezo wa kutaga mpaka mayai 60 na kutamia yote yakatotolewa, lakini kwa tabia yake ya kutokujali anaweza kuambulia vifaranga viwili au vitatu tu. Anaweza kuyasahau mayai yake mchangani, jua au joto la mchangani likamsaidia kotolesha.

Na akishazaa, watoto wake awahudumii, kama wafanyavyo ndege wengine wadogo, ambao huakikisha wanazunguka huko na huko kutafuta vyakula vya watoto wao. Lakini bado maandiko haya yanaonyesha jinsi gani alivyomshapu kuliko hata farasi. Mwendo wa mbuni unauzidi mwendo wa farasi yoyote duniani. Kuonyesha jinsi alivyo mwepesi kujipigania lakini sio watoto wake.

Ni nini Mungu alikuwa anamwonyesha Ayubu ni kwamba, uwezo wa kufanya jambo Fulani sio tija ya mtu huyo kulitenda, kama Mungu hakumpa moyo huo. Wapo wenye mali nyingi, lakini hawana moyo wa kusaidia wanyonge, wapo wenye vipawa vizuri lakini hawezi kumwimbia Mungu. Nguvu zao ni bure hazina faida, wapo wenye uwezo wa kufundisha lakini hawewezi kujinyenyekeza chini ya makusudi ya Mungu watumiwe ili kuujenga ufalme wa Mungu, wanakuwa tu kama punda-milia wa nyikani.

Wapo wenye uwezo wa kulichunga kundi la Mungu lakini wanakuwa kama mbuni, nguvu zao, ukubwa wao hauwasaidii katika kujali kazi ya Mungu. Lakini Bwana akikupa moyo huo, basi utafanya hata kama utakuwa ni dhaifu, utafanya tu. Na hili ndio jambo ambalo tunapaswa tumwombe Bwana . ATUPE MOYO WA KUMTUMIKIA YEYE. Tusitazame kwamba mpaka tupate kitu Fulani ndio tuweze, mpaka tukasomee uchungaji ndio tuweze kuchunga, mpaka tupate pesa ndio tuweze kuisapoti kazi ya Mungu, Bwana atupe moyo huo tangu sasa wakati hatuna uwezo wowote. Kwani huo ndio utakaotusukuma kufanya makubwa.

Lakini pia yapo mambo matatu tunaweza kujifunza:

Jambo la kwanza ni sisi wenyewe, tusiwe kama mbuni ambao hatujali kuhudumia vinavyozalika ndani ya roho zetu. Kwa kutengeneza viota vyetu mahali salama,kinyume chake tunamwachia shetani azichukue mbegu zetu rohoni zinazopandwa, tunaziacha juu juu na matokeo yake ibilisi anakuja kuzila sawasawa tu na mfano wa mpanzi ambao Yesu aliutoa juu ya zile mbegu zilizoangukia njiani ndege wakazila. Ndivyo ilivyo maisha ya wengi, wanapolisikia Neno la Mungu badala walitunze na kulipalilia ndani yao  ili liwazalie matunda wao wanazembea tu, wanaishi kama wanavyotaka. Hivyo tunakuwa wapumbavu kama mbuni, kwa kutokuzalisha chochote.

Jambo la pili: Linahusu familia: Wazazi wasiowajali watoto wao, Ni wajibu kwa mzazi kuwatunza wanawe, kwa kuwahudumia kimwili na kiroho. Imekuwa rahisi leo hii wazazi kujali sana Elimu za watoto wao jambo ambalo ni zuri, lakini kuhusiana na maisha yao ya kiroho wamewaweka nyuma . Hiyo ni hatari kubwa sana, usipompa Mungu watoto wako awalee, shetani atakusaidia kuwaelea. Na matokeo yake utayaona baadaye watakapokuwa watu wazima. Kama mzazi jali sana maisha ya kiroho ya watoto wako, wapeleke Sunday school, wapeleke katika semina za watoto kanisani, wahubirie, wafundishe kuomba, kufunga, kuimba nyimbo za wokovu n.k.

Jambo la tatu: Ni kuhusu watumishi wa Mungu. Bwana hataki tuwe kama Mbuni katika eneo la kulichunga kundi lake. Tunachowaza ni kujijali sisi tu, lakini kuwafuatilia na kuwachunga kondoo wa Bwana tunaona uvivu. Tunasahau kuwa shetani huko nje! Anafanya kazi usiku na mchana kuwarudisha tena ulimwenguni. Hivyo ni angalizo kwetu sisi watumishi wa Mungu. Popote ulipo hakikisha unalilisha na kulichunga kundi la Mungu dhidi ya Yule mwovu. Tuwe na hekima za ‘chungu’

Bwana akubariki sana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

“Humfukuza punda wake asiye baba”, nini maana ya mstari huu? (Ayubu 24:3)

HUDUMA YA (ELIFAZI, SOFARI, NA BILDADI).

Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).

KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?

Marijani ni nini katika biblia(Ayubu 28:18,Mithali 8:11)?

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Jina la mwokozi wetu Yesu Kristo litukuzwe milele na milele. Nakualika Tena wakati huu tujifunze maneno ya uzima wa Roho zetu.

Wengi wetu tunavutiwa na maisha ya Yesu alipoanza huduma, tunafurahishwa na jinsi alivyokuwa anafanya miujiza mikubwa, alivyokuwa anahubiri kwenye miji na vijiji, alivyokuwa anaponya wagonjwa,kutoa Pepo na kufufua wafu n.k.

Lakini ni Wachache sana wanaweza kuyatafakari maisha ya Yesu kabla ya huduma. Na hayo ndio Yana umuhimu sana kwetu kuliko Yale aliyoyadhihirisha baadaye.

Maandiko yanasema Yesu alimpendeza Mungu kabla hata hajaanza huduma yoyote ya kuhubiri, kutoa Pepo, na kuokoa watu…alishampendeza Mungu kabla ya hayo yote, tunalithibitisha hilo katika kitabu Cha Mathayo 3 siku Ile anabatizwa na Yohana, 

Mathayo 3:16-17

[16]Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake;

[17]na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.

Umeona alishampendeza Mungu kabla hata ya utumishi wowote, kuanza..tofauti na Leo tunavyodhani kwamba ili tumpendeze Mungu, ni sharti tuwe wahubiri wakubwa, au tuwe na upako, au tuwe wachungaji..hiyo sio kanuni ya Mungu.

Hivyo ni lazima tujue Mungu alipendezwa na Yesu kwa kipi? Ni kitu gani alikuwa anafanya mpaka kimfanye akubaliwe na Mungu namna Ile?

JIBU lipo katika Maisha aliyokuwa anaishi Kwa ile miaka 30 kabla ya huduma. Na hapa ndipo tunapaswa tupaangalie sana. Na tujifunze ili na sisi tufanane naye.

Watu wengi wanaona kama maisha yake ya awali yalifichwa sana, zaidi ya Yale aliyoyatenda katika huduma. Ni kweli ukitazama Kwa jicho la nje sehemu kubwa ya injili imeandika juu ya huduma ya Yesu, yaani ile miaka mitatu na nusu ya mwisho ya maisha yake. Lakini ukweli ni kwamba maisha ya Yesu kabla ya huduma ndio yameandikwa kwa wingi zaidi kuliko Yale aliyoyafanya katika huduma.

Hivyo Kwa neema za Bwana tutaona  juu ya maisha yake yalikuwaje, tangu utotoni mpaka anakaribia kuanza huduma.

Sehemu ya kwanza tutaona Mahali ambapo maandiko yameeleza moja Kwa moja maisha yake yalivyokuwa. Na sehemu ya pili tutaona maandiko ambayo sio ya moja Kwa moja, lakini yalimwelezea Yesu maisha yake.

Tukianza na maandiko yanayoeleza moja Kwa moja juu ya maisha yake. Kama yafuatavyo;

1) YESU ALIISHI MAISHA YA KUMPENDEZA MUNGU PAMOJA NA WANADAMU.

Luka 2:52

[52]Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

Maisha yake yote alikuwa ni mtu mwenye bidii sana kuhakikisha hafanyi jambo lolote ambalo ni kinyume na mapenzi ya Mungu. Alikuwa yupo makini sana na hilo, lakini zaidi sana alihakikisha katika jamii hawi na harufu mbaya. Alizingatia kuwa na adabu na heshima Kwa Kila mtu aliyekutana naye.

Si ajabu watu walipomuona walimsifia sana, na kusema yule kijana anaheshima, yule kijana ni mtaratibu, natamani watoto wangu wangekuwa kama yule, hatumuoni kwenye kampani za wahuni, hatumuoni akiruka ruka na mabinti barabarani, hatumuoni akitembea Kwa majigambo barabarani, muda wote anatabasamu, hakasiriki haraka, anahekima kama za mtu mzima wakati bado ni kijana..

Yesu alipata sifa isiyo ya kawaida katika jamii, alipoishi duniani, hakuna mtu alimchukia Kwa Tabia zake, alijitoa kwelikweli kuishi kikamilifu katika jamii yake.

Na sisi pia hichi ndio kitu Mungu anataka kukiona katika maisha yetu tunapookoka kabla hata ya kufikiria kuwa wahubiri ,je  mtaani kwako unaonekanaje, shuleni kwako Tabia zako zikoje? Mwonekano wako unawavutiaje watu, ofisini kwako kauli zako na wanyakazi wenzako Zina mvuto gani mpaka watu wakuone wewe ni mtu Bora kuliko wengine wote?

2) YESU ALIKUWA MTIIFU

Luka 2:51

[51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.

Aliwatii wazazi wake, hakukuwa na kiburi ndani yake, Neno utiifu kwa Yesu lilikuwa ni kama pumzi kwenye mapafu. Alipoagizwa alifanya, alipotumwa alikwenda, maisha yake yalikuwa ni ya namna hiyo, ili kutunza hadhi yake aliyokuwa nayo ya kuwapendeza watu wote..

Na sisi je tunaweza tukawa watiifu Kwa wazazi wetu wa kimwili na wa kiroho? Tuwatii viongozi wetu wa kiroho hata kama tutakuwa tunafahamu jambo Fulani zaidi ya wao, maadamu Bwana katuweka chini Yao.Hatuna budi kufanana na Yesu. Bwana atusaidie juu ya hilo.

3) ALIPENDA KUKAA NYUMBANI MWA BABA YAKE

Hii ni sifa nyingine inayomwelezea Yesu Tabia yake.

Luka 2:41-49

[41]Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka, wakati wa sikukuu ya Pasaka.

[42]Na alipopata umri wake miaka kumi na miwili, walipanda kama ilivyokuwa desturi ya sikukuu;

[43]na walipokwisha kuzitimiza siku, wakati wa kurudi kwao, yule mtoto Yesu alibaki nyuma huko Yerusalemu, na wazee wake walikuwa hawana habari.

[44]Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao;

[45]na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta.

[46]Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.

[47]Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.

[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.

[49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?

Akiwa kijana mdogo wa miaka 12, hakujali atakula nini, atalala wapi, ataoga wapi..alinogewa na ibada na mafundisho hekaluni akaona hata ule muda wa sikukuu hautoshi yeye kukata kiu yake Kwa Mungu, akaendelea kubaki palepale siku tatu, akiwa amefunga, yeye ni kujifunza tu, na kuyatafakari maneno ya Baba yake..

Wazazi wake hawakujua kuwa angekuwa na kiu Kali namna ile, lakini baada ya pale walimzoea, ikawa ndiyo desturi ya maisha yake yote.

Yesu alikuwa ni mtu asiye mtoro wa ibada, alikuwa anatumia majira yake mengi, kwenda kwenye masinagogi na kutafakari Neno la Mungu pamoja na viongozi wake wa kidini. Hakuwa mtu wa kujitenga Tenga, kama watu wanavyodhani.

Lakini pia alikuwa ni jemedari wa maombi kweli kweli na Dua.

Alikuwa anaomba sana Kwa bidii, Kwa kulia na machozi sana, na kwa kujimimina sana. Maandiko yanasema hivyo;

Waebrania 5:7

[7]Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;

Na sisi je tunaweza tukaiga Tabia hii ya Bwana. Je! Furaha yetu ni kuwepo uweponi MWA Bwana muda mwingi au kuwepo katika anasa za Dunia? Au katika biashara zetu? Ni lazima Bwana apewe kipaumbele Cha kwanza.

4) YESU ALIISHI MAZINGIRA YA KUFANYA KAZI

Pamoja na kuwa alikuwa ni mtiwa mafuta wa Bwana ameandaliwa Kwa kusudi moja tu la kuwaokoa watu. Lakini kipindi anasubiri wakati wa Bwana, hakukaa hivi hivi tu, Mungu aliruhusu afanye kazi.

Marko 6:3

[3]Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake.

Yesu hakuwa kama Yohana mbatizaji, Kukaa majangwani mbali na watu muda wote, lakini alikuwa ni mtu ambaye yupo katikati ya jamii, anayejulikana, anafahamika, alifanya kazi pamoja na baba yake ya useremala. 

Kwasasa tunaweza kusema alikuwa kariakoo akiuza vifaa vya majumbani na baba yake.

Lakini katika hayo yote aliishi maisha makamilifu ya kujichunga na kuwa na kiasi. 

Hii ni kutuonyesha kuwa unapookoka, uwapo popote pale iwe ni kazini, au kwenye biashara Yako, bado unaweza kumpendeza tu Mungu. Hivyo tusiruhusu kazi ziwe kisingizio cha sisi kutoishi maisha makamilifu. Yesu alikuwa ni mtu wa kujichanganya, lakini hakuruhusu dhambi iwe juu yake. Alipouza kabati hakukwepa kulipa Kodi, hakumuuzia mtu meza Kwa bei isiyoendana na thamani yake.  Hivyo ikampelekea Mungu ampende sana

Hayo ni maandiko ya moja Kwa moja yanayoeleza maisha ya Yesu yalivyokuwa.

Lakini maandiko mengine tunayapata wapi?

JIBU ni kuwa tunayapata katika kinywa Cha Yesu mwenyewe. Kwa kawaida mtu hawezi kusema maneno ambayo yeye hayaishi. Vinginevyo atakuwa ni mnafki, na Yesu yupo mbali sana na unafki, aliukemea sana, hata alipouona ndani ya mafarisayo na waandishi,walipowafundisha watu mambo ambayo wao hawayaishi.(Mathayo 23:1-5)

Hivyo ukitaka kufahamu Kwa kina maisha ya Yesu yalikuwaje sikikiza maagizo yote aliyokuwa anayatoa katika vitabu vyote vya injili.

Kwamfano. Mathayo soma sura yote ya 5-7 utaona maneno kadha wa kadha aliyokuwa anawafundisha makutano.

Anasema wapendeni adui zenu na kuwaombea(Mathayo 5:43-44): Yesu alikuwa anawaombea watu wote waliokuwa wanamchukia Kwa kumwonea wivu. Badala ya kuwatakia mapigo anawatakia maisha marefi, kuwaombea toba wageuzwe.

Anasema mtu akupigaye shavu la kuume mgeuzie la kushoto(Mathayo 5:38-40). Kuonyesha kuwa hakuwa mtu wa Shari, sikuzote alipotukanwa, au alipoaibishwa hakurudisha majibu, Bali alikubali kuaibishwa zaidi, ili aipushe malumbano zaidi.

Anasema amtazamaye mwanamke Kwa kumtamani amekwisha kuzini naye(Mathayo 5:28). Hakuwa na uvumilivu na macho yake, hakuwahi kuruhusu tamaa itawale maisha yake. Alijitenga na vichocheo vyote vya uzinzi, na mazungumzo yote yasiyofaa.

Alikuwa ni mtu wa kusamehe mara Saba sabini, hakuwa anawahukumu watu, au kuwalaumu(Mathayo 7:1-4)

Alikuwa si mtu wa kuruhusu hasira, aliona ukiwa hivyo adhabu Yako inakupasa ziwa la moto (Mathayo 5:21).

Bado alijishuhudia kuwa yeye ni mpole na mnyenyekevu (Mathayo 11:29), aliishi Kwa kujishusha, bila kumdharau yoyote, watu wote walikuwa na nafasi sawa kwake..

Na maandiko mengine mengi, aliyotuelekeza. Hivyo itoshe kusema maisha ya Yesu yaliyomfanya Mungu ampende kabla hata ya huduma ndiyo haya tunayoyasoma katika vitabu vya injili…

Hivyo ndugu Mimi na wewe yatupasa,. Tufikie hapo, acha kumuomba Mungu upako. Utakuja wenyewe tu endapo utampendeza Mungu kwanza kama Bwana Yesu, ukiwa unauhitaji. Penda mema chukia maasi..ndivyo Yesu alivyokuwa hapa duniani, hakuivumilia dhambi kwa namna yoyote, na matokeo yake Bwana akamtia nguvu kuliko mwanadamu yoyote aliyewahi kutokea hapa duniani.

Waebrania 1:9

[9]Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.

Bwana atusaidie sasa tuishi kama Kristo, ili baadaye tutende kama Kristo.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Kibiriti ni kitu gani? kama kinavyozungumziwa kwenye maandiko?

Nini maana ya Ukuta uliopakwa chokaa (Matendo23:3)?

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

WITO WA MUNGU

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

Zaburi 144:1 “Na ahimidiwe Bwana, mwamba wangu, Anifundishaye mikono yangu vita, Vidole vyangu kupigana

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno yake ya uzima. Leo tutaona namna ya kuomba maombi ya vita. Tukisema maombi ya vita tunamaanisha maombi ya kushindana na nguvu zote za Yule mwovu katika ulimwengu wa Roho, maombi ya kulegeza vifungo na nira, na minyororo, na kuangusha ngome pamoja na kuta za Yule mwovu zinazokinzana na sisi katika ulimwengu wa Roho, kupitia majeshi yake ya mapepo wabaya.

Ndugu ni lazima ufahamu, Kuna aina nyingi za maombi, kuna maombi ya shukrani, maombi ya mahitaji, maombi ya upatanisho n.k.. Yote haya yana wakati wake wa kuyatumia. Lakini pia yapo maombi ya Vita, ambayo ni lazima sana na ni muhimu kwa Mkristo kuyatumia.

Hivyo siku ya leo tutaona ni jinsi gani tunaweza kutumia maombi haya ili tuziangushe ngome za adui yetu ibilisi kiwepesi.

Baadhi ya watakatifu hawajui namna ya kuomba, wanafikiri pale unaposema shindwa shetani! Shindwa shetani! Kwa Saa tatu, au usiku kucha ndivyo wanavyomwangusha ibilisi. Uhalisia ni kwamba, hatumshindi ibilisi kwa maneno yetu kuwa mengi, Bali tunamshinda ibilisi kwa Neno la Mungu kukaa ndani yetu kwa wingi. Ambalo hilo litakusaidia kujua SILAHA unazopaswa uzitumie kumpiga nazo shetani. Bila kufahamu Silaha zako za kiroho, ni ngumu sana kumshinda shetani kimaombi. Kwasababu maombi yako yatakuwa ni ya juu juu, yasiyokuwa na nguvu za kiroho.

Bwana asipokufundisha kupigana vita, haijalishi maombi yako yatakuwa na maneno mengi kiasi gani, huwezi angusha ngome za adui. Hivyo penda sana kulisoma Neno la Mungu kwa kulitafakari kwasababu huko ndiko utakapojifunza kupigana vita vyako.

Kibiblia zipo silaha nyingi ambazo Mungu alizitumia kuwapigania watu wake, na Leo tutaziorodhesha chache, na tutaona jinsi tunavyoweza pia kuzitumia rohoni. Kwasababu kumbuka Neno la Mungu halijaandikwa kutupa stori  Fulani tu, tuifurahie halafu basi hapana, bali kila tendo, kila Neno linatafsiri kubwa sana rohoni.

Hivyo hizi ni baadhi ya silaha ambazo Mungu alizitumia kuwasaidia watu wake kupigana vita;

MVUA YA MAWE:

Mvua ya mawe

Mungu aliangusha mvua ya mawe kubwa sana, kwa wale watu wa Yerusalemu na wenzake walioungana kupigana na Yoshua kipindi kile wanaenda kuimiliki nchi yao, Utaona baadhi yao waliuliwa na Israeli, lakini wengi wa hao Mungu alimalizia kutoa hazina yake ya mvua kubwa ya mawe ikawaangamiza wengi sana kuliko hata wale waliouliwa na Yoshua.

Yoshua 10:11 “Kisha ikawa, hapo walipokuwa wakimbia mbele ya Israeli, hapo walipokuwa katika kutelemkia Bethhoroni, ndipo Bwana alipowatupia mawe makubwa kutoka mbinguni juu yao hata kufikilia Azeka, nao wakafa; hao waliokufa kwa kuuawa na hayo mawe ya barafu walikuwa ni wengi kuliko hao waliouawa na wana wa Israeli kwa upanga”

Jinsi ya kuomba: Bwana peleka, mawe yako ya barafu, katika madhabahu Zote za ibilisi, peleka mvua yako ya barafu katika vilinge vya kichawi, vinavyosimama kinyume na imani yangu. Haribu, bomoa, kila mbinu iliyoundwa dhidi yangu mimi (Taja maeneo yote ya maisha yako). Kama ulivyomshindia Yoshua nishindanie na mimi. [Hivyo Endelea kuita mvua hiyo na katika ulimwengu wa Roho, kwa jinsi unavyoiita kwa imani ndivyo inavyokuwa].

KIKOTO:

Yesu alipoingia hekaluni, alikutana na watu walioigeuza nyumba ya Mungu kuwa pango la wanyang’anyi. Ndipo akaunda kikoto kile, akapindua meza zote na kuwachapa wote waliofanya biashara pale, akawafukuza hekaluni kwa mamlaka yote, hekalu likawa safi kwa muda mfupi.

Yohana 2:15 “ Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng’ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao; 16  akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara”

Namna ya kuomba: Bwana naunda kikoto chako, napindua madhahabu zote za kipepo zilizoundwa moyoni mwangu na Yule adui, ninatawanyisha, ninasambaratisha, kila uovu, kila sanamu iliyopachikwa na Ibilisi (taja maeneo yote yanayohitaji maombi), kinyume na mapenzi ya Mungu. Ninavuruga kazi zote za ibilisi, kikoto cha Bwana kisafishe mwili wangu, kisafishe ibada yangu, kisafishe maisha yangu ya rohoni, kisafishe nyumba yangu, Naondosha uovu wa kila namna hata katika kazi yangu. [Sasa kwa jinsi unavyoomba kwa bidii na kurejea tukio hilo, ndivyo katika Roho Bwana anamnyuka shetani kwa namna ile ile. Ng’ang’ania hapo omba kwa imani kwa muda mrefu, kwasababu ndivyo ibilisi anavyodondoshwa].

KELELE ZA VITA:

kelele za vita

Bwana hutumia vitisho pia, kuwaondoa maadui, utakumbuka wakati Fulani wana wa Israeli, walizungukwa na maadui kwa muda mrefu. Hadi nchi ikaingiwa na njaa, watu wakaanza kulana ili waishi. Lakini jinsi Mungu alivyowaondoa maadui zao inashangaza. Kwasababu alifanya tu, kuwasikilizisha sauti za vita. Hivyo wale maadui waliposikia waliogopa sana wakawa wanakimbia kwa hofu kubwa sana huku wanaacha nyara zao nyuma. Baadaye Wayahudi kwenda wanashangaa hawawaoni maadui zao, wakijuliza ni nini kimetokea, mpaka waache na nyara, wakagundua kuwa ni Bwana ndiye aliyewatetea. Ndipo wakazichukua nyara kiwepesi na vita vikawa vimeisha kwa namna ile.

2Wafalme 7:6 “Kwa maana Bwana alikuwa amewasikizisha Washami kishindo cha miendo ya magari, na kishindo cha farasi, kama kishindo cha jeshi kubwa; wakaambiana, Tazama, mfalme wa Israeli amewaajiri wafalme wa Wahiti, na wafalme wa Wamisri, waje wapigane nasi.  7 Kwa hiyo wakaondoka, wakakimbia kungali giza bado, wakaziacha hema zao, na farasi zao, na punda zao, na kimo chao vile vile kama kilivyokuwa, wakakimbia wapate kujiponya nafsi zao”

Namna ya kuomba: Bwana peleka sauti zako za vita, katika ngome ya ibilisi, wafukuze waende mbali nami, hazina zote na vipawa vyote walivyoniibia katika roho na mwili ninavirejeza kwa Sauti yako ya vita. Watawanyike kwa njia saba. Vyote walivyoviiba navirejesha, fungua mipaka yangu, safisha hema yangu, adui atoweke kwa sauti za vita vya Bwana. [ Omba kwa kutaja maeneo yote ambayo unataka Bwana akutetee katika hayo].

UPOFU:

Wale malaika wa Bwana walioshuka Sodoma ili kuipeleleza, walikutana na wenyewe wa mji ule, ambao walitaka kulala nao. Hivyo malaika wale wakiwa nyumbani kwa Lutu. Maandiko yanaema waliwapiga upofu watu wale wasiweze kuiona nyumba mpaka asubuhi. Utakumbuka pia Paulo alipofika katika kile kisiwa kilichoitwa. Alishindana sana na Yule mchawi mpaka akamwomba Mungu ampige kwa upofu akawa kipofu kwa muda.

Mwanzo 19:10”Lakini wale watu wakanyosha mikono yao, wakamwingiza Lutu kwao nyumbani, wakaufunga mlango.  11 Kisha wakawapiga hao watu walioko mlangoni kwa upofu, wadogo kwa wakubwa, hata wakachoka kwa kuutafuta mlango”.

Namna ya kuomba: Bwana piga upofu majeshi ya mapepo yote mabaya yaliyokuja kufanya vita kinyume changu mimi, wasione roho yangu, uufiche uhai wangu ndani yako, shusha kiwi na giza mbele yao. Wapapase, wasione huduma yangu, (taja mambo yako yote ambayo unatamani ibilisi asiyaone), waangamie na kuishia shimoni, watafute lakini wasione. [Hivyo Kwa jinsi unavyosimamia vifungu hivyo ndivyo unavyoshinda vita rohoni kiwepesi kwasababu mambo hayo yanatendeka kwelikweli].

JIWE LA MUNGU:

maombi ya vita jiwe la Yesu

Jiwe la Mungu ni Yesu. Yeye mwenyewe alijifananisha na jiwe hilo lililo zito sana na gumu. Akasema. Likimwangukia mtu linamsaga tikitiki, na yoyote atakayeliangukia atavunjika vunjika Kuonyesha ni jinsi gani lilivyo bora, ndio lile lililopiga sanamu ya Nebukadreza, na kuisaga kama unga, na kupotea kabisa(Danieli 2:34).

Mathayo 21:44  “Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika; naye ye yote ambaye litamwangukia, litamsaga tikitiki”.

Namna ya Kuomba: Yesu simama mwenyewe unitetee, kama jiwe lililo hai lenye nguvu na imara. Piga kila aina ya kuta nzito za ibilisi zinazozuia upenyo wangu. Nazibomoa kwa jiwe hili, ninalirusha katika kila Nyanja, impige ibilisi katika kipaji cha uso wake, aanguke kama Goliathi mbele ya Daudi. Wewe uliye jiwe piga kila ngome, ya mwovu lisage na kuharibu na kusagasaga, kazi zote za mwovu mbele yangu ziwe kama makapi mbele ya Upepo.[Lielekeze jiwe hili, liangushe kwelikweli kwa imani ndivyo itakavyokuwa katika ulimwengu wa roho]

Natumai mpaka hapo umeshapata mwangaza wa namna ya kulitumia Neno kuomba maombi haya ya vita, Kwasababu ya muda, hatuwezi toa maelezo ya silaha zote zilizo katika biblia, Hivyo hizi ni silaha nyingine ambazo zitumie, zikusaidie.

6) UPEPO WA KUSULISULI NA RADI:  Andiko la kusimamia (Zaburi 77:18). Omba Bwana avuruge, na kuichosha mikakati yote ya adui dhidi yako mfano wa kisulisuli kizungushacho makapi.

7) GHARIKA YA BWANA: Andiko la kusimamia (Mwanzo 6:17). Kama Bwana alivyoangamiza waovu wakati ule wa Nuhu kwa gharika Omba Bwana akafungue madirisha yake ya mbinguni, agharikishe majeshi ya kipepo yanayokufuatilia yakuangamize, yaangamie kama majeshi ya Farao katika bahari ya Shamu.

8) UPANGA WA BWANA: Andiko la kusimamia (Ufunuo 19:15). Omba ule upanga wa Bwana ukatao kuwili, ukate, na kuua mambo yote maovu ya adui yanayosimama mbele yako

9) KUTAWANYWA USEMI: Andiko la kusimamia (Mwanzo 11:7-9). Kama alivyouvuruga usemi wa wajenzi wa Babeli wasielewane, vivyo hivyo akaruge hila za ibilisi na mapepo yake zisipatane juu yako.

10) MOTO WA BWANA: Andiko la kusimamia (2Wafalme 1:10). Moto ukaunguze mapando yote, ya ibilisi, aliyoyapanda moyoni mwako,

11) NZIGE, PARARE, MADUMADU, TUNUTU: Andiko la kusimamia (Yoeli 2:25). Bwana akatume jeshi lake la waharibuo, wakatafune kazi zote za mwovu, wakalete hasara, warudishe nyuma, na kudhoofisha ufalme wote wa giza.

12) MAJIPU YA BWANA: Andiko la kusimamia (Kutoka 9:9). Bwana alete hali mbaya ya mateso, kwa wakuu wote wa giza wafanyao vita kinyume na wewe.

13) TETEMEKO: Andiko la kusimamia (1Samweli 14:15) . Bwana alete utisho na mashaka, na tetemeko kwa wakuu wa giza na mapepo yasimamo kinyume cha kazi ya Mungu.

14) UKAME (kiu na njaa): Andiko la kusimamia (Amosi 8:11). Bwana alete ukame wa kiroho, kwa majoka yote yanayosimama kutaka kumeza watu wa Mungu, yafe na kuteketea kwa kukosa mawindo ya watu.

15) RUNGU LA BWANA: Andiko la kusimamia (Yeremia 51:20).  Lipige na kuleta majeraha katika ufalme wa giza, liziraishe mapepo yote na vikaragosi vyake vyote vifanyavyo vita na wewe.

Zipo na silaha nyingine nyingi katika maandiko Hatuwezi kuziorodhesha zote, Hivyo kwa jinsi Neno la Mungu linavyokaa ndani yako, ndivyo utakavyoweza kuzivumbua na kuzitumia. Na zote hizo ni sharti tuziombe katika jina la Yesu na uweza wa damu yake.Maombi ya namna hii yana nguvu sana, na yatakufanya udumu kwa muda mrefu katika kuomba. Na kufungua vifungo vingi sana katika ulimwengu wa Roho.

Kumbuka pia, vita hivi hatuvielekezi kwa wanadamu, bali kwa Shetani na majeshi yake ya mapepo na kazi zake zote. Kwasababu maandiko yanasema vita vyetu sio juu ya damu na nyama, maana yake ni kwamba sio juu ya wanadamu wenzetu. Bali ni juu ya falme za giza, zikawaachilie mateka, waje kwa Bwana, na sio tuwaue wao pamoja na mateka wao.

Waefeso 6:12  “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 6.13  Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

VITA DHIDI YA MAADUI

NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

Kwanini kuna watu wanafanyiwa deliverance (Maombi ya kufunguliwa), lakini baada ya muda wanarudiwa tena na hali ile ile sababu ni nini?

Nini maana ya “Andiko huua, bali Roho huhuisha (2Wakorintho 3:6)

Rudi nyumbani

Print this post