Category Archive Uncategorized

Anaposema zijapokuwa nyekundu kama bendera, ana maana gani?

SWALI: Mungu anaposema dhambi zetu zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. Ana maana gani, kwenye hilo neno bendera?

Isaya 1:18 Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.  19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi;


JIBU: Hapa ni Mungu anaeleza mambo mawili hayuhuso dhambi walizotenda watu wake.

  • Jambo la kwanza ni ukubwa/wingi wa dhambi walizonazo. Ndio hapo anafananisha rangi nyekundu sana, ukilinganisha na kitu kilicho cheupe sana mfano wa theluji.

Tunajua theluji inang’aa sana mfano wa jua, Kuonyesha ni jinsi gani hawa watu walivyokuwa mbali sana na ukamilifu, yaani jinsi gani walivyokuwa hawakaribii hata kidogo kuwa wema mbele za Mungu, walau wangeonekana wa rangu ya kijani, basi wangekuwa na afadhali, lakini ni mbali sana, wana rangi ya damu. Ndivyo ilivyokuwa Israeli yake.

  • Jambo la pili ni usugu wa dhambi uliokuwa ndani yao.Ndio hapo anafananisha na Bendera, ukilinganisha ni sufu nyeupe.

Zamani bendera nyingi zilichovywa katika rangi nzito nyekundu, inayodumu sana, kwasababu ni kitu cha kudumu muda mrefu, hivyo haikuhitajika rangi inayofubaa haraka. Sio tu bendera, lakini mpaka mavazi ya kifalme, au nguo za thamani za sufu.

Hivyo unaposoma habari za bendera hapo, si bendera ya kila rangi, mfano wa bendera tulizonazo sikuhizi zina rangi mbalimbali, zamani nyingi zilichovya kwa rangi  nyekundu. Hivyo Mungu anawaambia ijapokuwa ni nyekundu kama bendera, basi zitageuzwa na kuwa nyeupe kama Sufu, (akiwa na maana ambayo haijachovywa), Yaani Mungu anaweza kuiondoa hiyo rangi sugu, kwenye hicho kitambaa kana kwamba hakijachovywa kabisa.

Kufunua nini,

Yesu Kristo mwokozi wetu ndiye aliyetimiza huo unabii. Kuonyesha kuwa dhambi zote tulizotenda haijalisha ni nyingi kiasi gani, haijalishi ni mbaya namna gani yeye kwa damu yake anaweza kuzifuta kabisa kabisa. Dhambi tulizotenda haijalishi hazisameheki namna gani, hazineneki, ni sugu namna gani, yeye anao uwezo wa kuziondoa, kwa neema yake.

Swali ni je! Umesamehewa dhambi zako? Kama ni la! Unangoja nini kuipokea neema hii, ya WOKOVU mkuu namna hii? Pokea sasa msamaha wa dhambi kwa kutubu dhambi zako, na kumaanisha kuishi maisha mapya ya wokovu. Kisha moja kwa moja atakupokea na kukupa ondoleo la dhambi zako. Na baada ya hapo unahesabiwa kuwa huna dhambi yoyote, umestahili uzima wa milele, bure.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo basi, fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa maombi mafupi, na kwa kupitia sala hiyo kwa imani utakuwa umeshampokea Yesu Kristo, na amekusamehe dhambi zako zote.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

ALAMA ZA BENDERA YA ISRAELI ZINAWAKILISHA NINI?

MAANA YA RANGI KIBIBLIA.

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

Merikebu ya Iskanderia kwanini itajwe jina lake ‘Ndugu Pacha’?

SWALI: Je kulikuwa na umuhimu wowote wa ile merikebu ya Iskanderia  walioipanda Paulo na wafungwa wengine kutajwa jina lake ‘ndugu Pacha’,?

Matendo 28:11  Baada ya miezi mitatu tukasafiri katika merikebu ya Iskanderia iliyokuwa imekaa pale kisiwani wakati wa baridi; na alama yake ni Ndugu Pacha. 12  Tukafika Sirakusa, tukakaa siku tatu. 13  Kutoka huko tukazunguka tukafikia Regio; baada ya siku moja upepo wa kusi ukavuma, na siku ya pili tukawasili Puteoli. 14  Huko tukakuta ndugu, wakatusihi tukae nao siku saba; na hivi tukafika Rumi.


JIBU: Safari ya mtume Paulo kama mfungwa, kutoka Kaisaria kwenda Rumi kuhukumiwa, haikuwa rahisi, iligubikwa na misuko suko mikubwa ambayo ilihatarisha maisha yao ukisoma Matendo 27, utaona mtume Paulo alionywa na Roho Mtakatifu kuhusu hatari hiyo lakini alipomwambia akida na manahodha, walipuuzia agizo lake, kwasababu watu wale hawakuamini habari za “miungu kabisa”. Maandiko yanasema walipoona upepo wa kusi umevuma kidogo tu, unaoruhusu kusafiri, wakadhani itakuwa hivyo mbeleni.

Lakini tunaona walipofika katikati, ghafla ile bahari iliwachafukia sana, upepo wa nguvu ukavuma merikebu yao ikawa karibu na kuzama, baadaye ilivunjika kabisa, na wakaokoka kwa shida kwasababu Mungu alimuhakikishia Mtume Paulo kuwa hakuna hata mmoja wao atakayeangamia.

Walipookoka na kufika kisiwa kile kilichoitwa Melita, walikaa miezi mitatu pale, kuruhusu hali ya hewa kutulia, kabla ya kuondoka. Lakini tunaona walipotaka kuondoka, safari hii wale mabaharia pamoja na maakida, hawakuichukulia safari yao kirahisi rahisi, yaani hivi hivi tu bila uongozo wowote. Ndipo walipojifunza kuchagua merikebu yenye “ulinzi wa kiroho”. Wakaipata hiyo ya Iskanderia iliyokuwa na nembo ya “Ndugu Pacha” kwa mbele.

Ndugu Pacha ni miungu ya kipagani ya kiyunani, ukisoma tafsiri nyingine za biblia imewataja moja kwa moja miungu hiyo kama Castor na Pollux. Ni miungu ambayo waliamini inahusika na ulinzi wa  safari za majini. Hivyo kwa imani yao ya kipagani, wakachukua nembo yao kuonyesha tunaiabudu na kuiheshimu hii miungu, na kutaka iwaongoze  salama katika safari yao, hawategemei tena elimu zao na nadharia zao.

Sasa tukirudi kwenye swali, linalouliza, kulikuwa ni umuhimu gani, hiyo merikebu ya Iskanderia kutajwa hadi nembo yake ya ndugu Pacha. Sababu ndio hiyo, Sio kwamba biblia inatufundisha, na sisi tukaweke miungu ya kipagani, kwenye vyombo vyetu vya usafiri kutuhakikishia ulinzi, hapana!

Bali inatufundisha Safari ya maisha hapa duniani. Kila mwanadamu anasafiri, lakini Je! Katika safari yako ni kitu gani kinakuongoza na kukulinda ili kukufikia ng’ambo yako salama?

Hakuna mwanadamu ambaye anaweza kujiongoza mwenyewe. Na ndio maana utaona hawa kwasababu hawakumjua Mungu wa kweli iliwabidi wakatafuta vinyago visivyoweza kuwasaidia kitu viwaongoze, na kama sio mtume Paulo kuwepo ndani ya Merikebu ile, safari yao ndio ingekuwa mbaya mara mbili zaidi. Hawakujua tu waliongozwa na Kristo Yesu pasipo wao kujua kwa neema tu!. Kwasababu watumishi wa Mungu walikuwa ndani.

Na sisi, hapa tulipo, fahamu kuwa maisha yako, bila KRISTO ni mauti mbele. Shetani hakuwazii mema, wala akili zako mwenyewe hazikusaidii ndugu, hiyo elimu ni kazi bure, huo uzoefu na ujuzi ulionao ni bure rafiki. Unamuhitaji Kristo, yeye ndio awe nembo  ya maisha yako. Mwamini leo akupe msamaha wa dhambi, mwamini leo akuokoe, safari yako iwe salama hapa duniani. Ukifa leo katika hali hiyo, fahamu ni jehanamu moja kwa moja. Umesikia injili ikihubiriwa mara ngapi, kwamba Yesu ni mwokozi lakini unapuuzia? Walio kuzimu wanatamani hata dakika moja, watubu hawawezi kwasababu kule hakuna maisha ya kuishi. Lakini wewe unaishi.

Usikiapo maneno haya, ugeuze moyo wako, umruhusu Kristo leo akuokoe, ikiwa upo tayari kumgeukia Bwana Yesu , na unatamani upate mwongozo wa kimaombi kwa ajili ya wokovu wako. Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii, bure.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Rudi nyumbani

Print this post

 UNAUELEWA, HISOPO UMEAO UKUTANI?

1Wafalme 4:32 Naye akanena mifano elfu tatu, na nyimbo zake zilikuwa elfu moja na tano.  33 Akanena habari za miti tangu mwerezi ulioko Lebanoni hata HISOPO UMEAO UKUTANI; pia akanena habari za wanyama, na za ndege, na vitambaavyo, na samaki.

Salaam! karibu tujifunze na kutafakari bahari za mwokozi wetu Yesu Kristo na uzuri wake maishani mwetu.

Habari yetu itaanzia kwa mfalme Sulemani ambaye Mungu alimjalia hekima nyingi zaidi ya wanadamu wote waliokuwa duniani kwa wakati ule. Na moja ya mambo ambayo, aliyatafakari sana, hayawakuwa tu yanayowahusu wanyama na viumbe hai, lakini ni pamoja na mimea mbalimbali.

Hivyo kama tunavyosoma katika vifungu hivyo, aliweza kutambua hekima iliyokuwa imejificha nyuma ya miti mikubwa na yenye umaarifu kama mierezi, lakini, kilichomtafakarisha pia sio katika mimea mikubwa, lakini pia midogo  mfano wa Hisopo, na jinsi inavyomea. Na hapo tunaona anaeleza sifa yake, kwamba ni mmea unaomea ukutani.

Ikiwa na maana, mahali palipo na ardhi ngumu, au mwamba au jiwe, wenyewe unamea, na kukua na kuzaa bila shida yoyote. Tofauti na mimea mingine mingi yenye nguvu, itahitaji  udogo mlaini mwingi, tena tifutifu, lakini huu wa hisopo ni wa kipekee unahitaji mahali pagumu.

Kufunua nini?

Mmea huu unamfunua Bwana wetu Yesu Kristo,yeye  Hakuhitaji mahali palipoandaliwa pa kitajiri, ili kulitimiza kusudi la kifalme duniani,  hakuhitaji familia ya kidini maarufu, au kabila la kikuhani,  ili aishi maisha makamilifu, hakuhitaji kuishi mji mtakatifu Yerusalemu ili ampendeze Mungu. Bali alitokea mahali ambapo ni vijijini (Nazareti), familia maskini, tena nyakati za kipagani, ambazo imani ilikuwa imekongoroka sana, pia, kabila lisilojiuhusisha na mambo yoyote ya kikuhani kabisa. Hivyo Yesu aliishi katika jamii ya wapagani.

Wakati sisi katikati ya dhiki nyingi (yaani penye mwamba mgumu) tunanyauka. Yeye ndio alikuwa anasitawi. Aliweza kustahimili mapingamizi ya kila namna zaidi ya mwanadamu yoyote aliyewahi kutokea hapa duniani. Alichukiwa na ulimwengu, alisalitiwa, alikanwa, aliachwa peke yake, aliaibishwa, alipigwa mpaka kuuawa. Lakini hakuwahi kuanguka au kutenda dhambi yoyote. Haleluya! Anastahili hakika mwokozi wetu Yesu Kristo.

Ni hisopo umeao ukutani. Mahali ambapo mimea mingine imeshindwa, yeye ameweza.

Na ndio maana Neno linasema;

Waebrania 12:2  tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.

3  MAANA MTAFAKARINI SANA YEYE ALIYEYASTAHIMILI MAPINGAMIZI MAKUU NAMNA HII YA WATENDAO DHAMBI JUU YA NAFSI ZAO, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.

4  Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;

Umeona ni kwa namna gani Yesu alivyokuwa mwamba imara wa kutegemea sana?

Na ndio maana maandiko sasa yanasema, kwa kuwa alijaribiwa kama sisi, basi anaweza kuchukuliana na sisi pia katika mambo yetu ya udhaifu.

Waebrania 4:14  Basi, iwapo tunaye kuhani mkuu aliyeingia katika mbingu, Yesu, Mwana wa Mungu, na tuyashike sana maungamo yetu.

15  Kwa kuwa hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.

16  Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.

Hivyo ndugu, ni nini unachongoja, usiokoke leo?. Wewe peke yako hutaweza, kuushinda huu ulimwengu, unaihitaji neema ya Yesu Kristo ikusaidie. Mpokee leo, upate ondoleo la dhambi zako,  Akupe na Roho wake mtakatifu ili kukusaidia sasa kuishi maisha ya ushindi kama yeye alivyoishi.

Ukipita katika miamba lakini unaendelea kumea.  Hivyo chukua uamuzi huo leo. Ikiwa upo tayari kuokoka basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!

VITA BADO VINAENDELEA.

TUKAZE MWENDO KWA TULIYOANDALIWA.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Rudi nyumbani

Print this post

NI LAZIMA NIWE MBWEHA WA KRISTO!

Kama mwamini hizi si nyakati za kuishi kilegevu, unapoona, watu wanakufa katika dhambi na kwenda jehanamu bila kumjua Kristo, unajisikiaje, unapoona kazi za shetani zinasitawi, na kuwaharibu watu unawezaje kutujulia moyoni mwako?

Ni Funzo gani unalipata nyuma ya hasira ya Samsoni? Alipoona mke wake ameuzwa kwa wageni na baba-mkwe wake, je alitulia, na  kusema basi tu hii siyo bahati yangu? Kinyume chake Alinyanyuka kwa hasira akasema ninakwenda kulipiza kisasi, kwa hawa wafilisti.

Unajua alifanya nini?

Alikwenda kuwachukua mbweha mia tatu (300), Akawafunga wawili wawili mikia yao, kisha, akawafungia mienge ya moto, na kuwaachia waingie kwenye mashamba ya ngano ya wafilisti. Baada ya hapo ni jambo gani akawa analifanya? Ni kuwaangalia tu wale mbweha walivyokuwa wanayateketeza mashamba ya ngano hekari kwa mahekari. Jambo lililowafanya wafilisti waamke wote kwenye majumba yao wamtafute huyu Samsoni ni nani?

Waamuzi 15:3 “Samsoni akasema, Safari hii nitakuwa sina hatia katika habari za hawa Wafilisti, hapo nitakapowadhuru.  4 Samsoni akaenda akakamata mbweha mia tatu; kisha akatwaa vienge vya moto akawafunga mbweha mkia kwa mkia, akatia kienge kati ya kila mikia miwili.  5 Alipokwisha kuviwasha moto vile vienge, akawaachia mbweha kati ya ngano ya Wafilisti, akayateketeza matita, na ngano, hata na mashamba ya mizeituni”

Akimfunua nani?

Ni Yesu Kristo,

Bwana alipoona kazi za adui zinapaswa ziharibiwe pale Israeli. Alichofanya ni kuwachukua wanafunzi wake pia, akawatuma wawili-wawili akawaambia waende mahali alipotaka yeye kwenda, akawapa amri ya kutoa pepo, kupooza magonjwa na kuhubiri habari njema. Na unajua ni nini kilitokea baada ya pale, ndani ya kipindi kifupi, waliporudi?

Yesu alikuwa akiwaangalia “MBWEHA WAKE” katika roho wakiziharibu kazi za shetani, akasema, nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme.. Ha! ha! ha! ha! Mbweha wamfanya kazi.

Luka 10:17  “Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. 18  Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. 19  Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.

Na sisi (yaani mimi na wewe), tuliookoka, Ikiwa umeshajazwa “Roho Mtakatifu” wewe tayari ni mbweha, Sijui unasubiri nini kwenda kuziharibu kazi za shetani, kwa kumuhubiri Kristo, na wokovu wake? Unasubiri nini mpendwa?

Angalia Yesu alichokisema..

Luka 12:49  “Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi?

Moto umekwisha kuwekwa kwenye mkia wako, angalia usije ukazima kabla haujafanya kazi yake. Ndio huo moto wa Roho Mtakatifu unaochoma ndani yako, kukuagiza uhihubiri neema ya Kristo kwa ndugu zako na watu wengine ili waokoke.

Kwa pamoja tunaweza upindua ulimwengu. Tumuhubiri Kristo, hilo ndilo agizo kuu kwa wanadamu wote. Kila mmoja wetu ni mbweha wa Kristo. Simama sasa, pokea ujasiri, kamuhubiri Kristo, watu waokoke.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

KITENDAWILI CHA SAMSONI

HUDUMA YA MALAIKA WAWILI.

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

Hizi ni sababu kuu nne (4), ambazo zinampa sababu mwaminio yoyote kuihubiri injili kwa nia yote kutoka moyoni.

1) Kwasababu ni agizo kuu la Bwana.

Marko 16:15  “Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. 16  Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”

Bwana wetu alituagiza, na kutupa jukumu la kufanya sisi kama wakristo. Sio tu kusema sisi tumeokoka halafu basi, hapana bali ni pamoja na kuwafanya wengine kuwa kama sisi, kuwafanya kuwa wanafunzi wa Kristo.

2) Kwasababu ya ushuhuda wako mwenyewe.

Mitume walikuwa na ujasiri wa kumuhubiri Kristo, kwasababu ya ushuhuda wao wenyewe kwa mambo waliyoyaona kwa  Bwana Yesu akiwatendea.

Matendo 4:18  Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu.

19  Petro na Yohana wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe;

20  maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.

Ukisoma pia 1Yohana 1:1-3  Mtume Yohana anasema..

1Yohana 1:1  Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima;

2  (na uzima huo ulidhihirika, nasi tumeona, tena twashuhudia, na kuwahubiri ninyi ule uzima wa milele, uliokuwa kwa Baba, ukadhihirika kwetu);

3  HILO TULILOLIONA NA KULISIKIA, TWAWAHUBIRI NA NINYI; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.

Hii ikiwa na maana, kuwa kila mkristo aliyekombolewa, anaoushuhuda wa mambo makuu aliyotendewa na Yesu tangu siku alipookoka, Tofauti kubwa aliyoipata katika maisha yake mpya ukilinganisha na yale ya zamani, jinsi mizigo yake ilivyotuliwa, hofu kuondolewa, magonjwa yake kuponywa, kufunguliwa, kupokea furaha ya wokovu isiyo na kiasi, amani, utulivu. N.k.

Yote haya kwa mkristo anayethamini wema wa Mungu hataona aibu kutamani na wengine wauonje uzuri huo ulio katika Kristo Yesu. Na hivyo atatoka nje! na kwenda kuwahubiria wengine Injili ya Yesu Kristo,kama mitume walivyofanya.

3) Kwasababu watu wanaouhitaji wa kusikia habari za Injili.

Hili lilimkuta mtume Paulo, Hapo mwanzoni alidhani yeye ndio anayekwenda kuwashawishi watu kuhusu Yesu, lakini siku moja aliona maono, watu wa mbali Makedonia wakiwa na uhitaji mkubwa sana wa kumjua Mungu. Hivyo akalitii ono lile akaenda.

Matendo 16:9  Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie.

10  Basi alipokwisha kuyaona yale maono, mara tukataka kutoka kwenda Makedonia, kwa kuwa tuliona hakika ya kwamba Mungu ametuita tuwahubiri Habari Njema.

Hata sasa, wapo watu wengi wana kiu ya kuijua njia ya kweli, mioyoni mwao wakiwa na shauku ya kuifahamu hiyo NJIA. Lakini sisi tukikaa na kusema hakuna mwenye haja, twajidanganya. Hatupaswi kuona watu kwa nje wanatuchekea, wanafurahi, wana raha, tukadhani hali zao rohoni ndio hivyo zilivyo, tukapuuzia kuwahubiria injili. Wengi wapo kwenye vifungo na wanatamani wapate msaada wa kutoka huko, hawasemi tu. Na anayeweza kuwatoa hapo ni Kristo tu peke yake. Siku ukizungumza nao ndio utajua kweli walikuwa na haja na Kristo. Hivyo usichague wa kumshuhudia. Fahamu tu watu wana haja na kuujua ukweli. Hubiri injili ya Kristo.

4) Kwasababu roho za watu zinakwenda kuzimu.

Tunajua mtu akifa nje ya Kristo, hakuta tumaini, ni moja kwa moja jehanamu. Tengeneza picha ndugu zako uwapendao, rafiki zako, wazazi wako, na wanadamu wenzako wanakwenda kwenye moto wa milele. Wewe una raha gani leo hii usiwashuhudie habari za Yesu Kristo?.Embu tengeneza picha habari ya Yule tajiri na Lazaro, (Luka 16:19-30) alitamani, mtu atoke kuzimu akawahubirie watu injili ili wasifike mahali pale pa mateso, lakini akaambiwa wapo Musa na manabii huko duniani (ambao ndio sisi), tuwahubirie.

Hivyo kwa sababu hizo kuu nne (4), wewe kama mwaminio uliyeokoka, huna budi kuwashuhudia wengine habari za Kristo. Utasema mimi sina uzoefu, Kumbuka Yesu haitaji uzoefu wako, kuwaokoa watu, kwasababu hata wewe hukuupokea kwa uzoefu wowote, anahitaji kuwaambia Yesu anasemehe dhambi, anaokoa wanadamu, anatoa uzima wa milele bure, anatuepusha na hukumu ya milele, anatua mizigo ya watu, anafariji, anaponya roho, anatupa nguvu ya kuushinda ulimwengu na dhambi. Njoo kwake, akufanye kiumbe kipya upokee uzima wa milele. Hivyo tu. Na hayo mengine mwachie yeye, usifikiri fikiri atakuongoza kwa jinsi utakavyokuwa unasema.

Mathayo 10:20 “ Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu”.

Anza sasa.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI INJILI GANI UNAHUBIRI?

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

Rudi nyumbani

Print this post

FAHAMU VIASHIRIA VYA MTU ALIYESAMEHEWA DHAMBI ZAKE.

Si kila mtu anayesema “amemwamini” Yesu ni kweli, ameokoka, au amepokea msamaha wa dhambi zake. Ukweli ni kwamba kuupokea msamaha wa dhambi kwa kuiamini kazi aliyoimaliza Yesu Kristo pale msalabani ya ukombozi wa wanadamu si kugumu, Lakini haiji kwa kusema “naamini tu” halafu basi ndio uwe tayari umetiwa muhuri na Mungu kwamba ni wake milele.

Imani ya namna hiyo inatiwa imani ya” bure” (1Wakorintho 15:2).

Na sehemu nyingine inajulikana kama  “imani ya wote” ambayo hata mashetani wanayo. Wanamwamini Yesu kuwa ni mwokozi, lakini pia wanaiamini vizuri sana kazi ya msalaba (Yakobo 2:19). Lakini je! Wamesamehewa dhambi zao?

Zipo injili zinazowafundisha watu, “kuamini tu” au “kukubali tu msamaha” inatosha. Hakuna la ziada baada ya hapo. Ndugu hizo sio sifa za mwaminio yoyote.

Neno “kuamini” kwa kigiriki ni PISTIS, lenye maana ya sio tu kuwa na ujasiri na Mungu wako kwa kile anachokupa au kukuelekeza,lakini pia kuwa ‘mwaminifu”.

Maana yake ni kuwa ili tuseme tumeamini ni lazima pia tuwe waaminifu kwa Yule tuliyemwamini.

Sasa mtu yeyote aliyemwamini Kristo. viashiria hivi vitatu(3) utaviona ndani yake

  1. Atakuwa ni kondoo

Yohana 10:2  Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo. 3  Bawabu humfungulia huyo, na kondoo humsikia sauti yake; naye huwaita kondoo wake kwa majina yao, na kuwapeleka nje. 4  Naye awatoapo nje kondoo wake wote, huwatangulia; na wale kondoo humfuata, kwa maana waijua sauti yake. 5  Mgeni hawatamfuata kabisa, bali watamkimbia; kwa maana hawazijui sauti za wageni…

27  Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata. 28  Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu. 29  Baba yangu aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote; wala hakuna mtu awezaye kuwapokonya katika mkono wa Baba yangu.

Umeona, ni kondoo tu, ndio hawawezi kupokonywa katika mikono ya mchungaji wake. Lakini mbuzi wanaweza, kwasababu hawategemei sana sauti ya mchungaji, wanaweza kujichunga wenyewe. Ukiona mtu anasema ameokoka, halafu, maisha yake ni kama ya mbuzi, ujue huyo si wa Kristo. Haisikii sauti ya Kristo ikimwelekeza aache maisha ya kiulimwengu, ajitofautishe na watu wa kidunia, . Ujue huyo bado hajapokea kweli msamaha wa dhambi, kwasababu hajaamini. Anapaswa ashuhudiwe mpaka aamini. Na aseme kuanzia leo, Kristo ndio kiongozi wa maisha yangu na sio dunia tena. Akubali TOBA ya kweli.

2. Atakuwa Ni kiumbe kipya.

Yesu alisema..

Yohana 1:12  Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.

13  waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu

Wenye sifa ya kwamba wamemwamini Yesu ni lazima pia wawe wamegeuzwa kuwa watoto wa Mungu, yaani wamezaliwa mara ya pili kwa mbegu isiyo ya kibinadamu, bali ya Mungu mwenyewe.

Na kama tunavyofahamu mtoto hubeba tabia za Baba. Vivyo hivyo mwaminio ni lazima moyoni mwake kuwake, tamaa za Baba yake. Maandiko yanasema Baba ni Mtakatifu, vivyo hivyo tamaa ya mwaminio huyo mpya itakuwa ni kupenda utakatifu, na kuutafuta huo kwa bidii.

Haiwezekani mtu aliyemwamini Yesu, awe na raha tena katika maisha ya kidunia ya dhambi. Au asipige hatua yoyote ya kuutafuta ukamilifu. Halafu tuseme ni mwaminio si kweli.

1Yohana 3:9  Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu

3) Atakuwa ni mwanafunzi

Mwaminio mpya amefananishwa na mwanafunzi, na mwanafunzi sikuzote huwa yupo tayari kujifunza, na kukua kiufahamu.

Matendo 2:41  Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42  Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.

Hivyo mtu yoyote anayesema amemwamini Yesu, na hapendi fundisho, hapendi kuchungwa, hapendi kufuatiliwa maendeleo yake ya kiroho, anapinga ubatizo, na wakati mwingine kufanya ushirika, huyo mtu bado hajaamini.

Lakini akiwa na sifa zote hizo tatu, ni uthibitisho kuwa amemwamini Yesu, na hivyo kaupokea pia msamaha wa dhambi. Mtu wa namna hiyo wokovu kwake ni uhakika. Kwasababu Yesu ameumbika ndani yake. Kazi ya Mungu kamilifu imetimilika ndani ya mwanadamu.

Je! Na wewe Umepokea ondoleo la dhambi zako? Je! Ni mwanafunzi, ni kondoo, ni mwana wa Mungu?. Kama bado basi fahamu unamwihitaji Kristo, fungua moyo wako mkaribishe ndani yako akuokoe. Sasa, Maanisha tu tangu sasa kuwa na badiliko na yeye mwenyewe atakuokoa.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

JE! UNAMPENDA BWANA?

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

KUUMBWA TU, HAITOSHI YAPO MAMBO MENGINE MAWILI

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya Mungu ya uzima.

Kama kichwa cha somo kinavyosema. “Kuumbwa tu haitoshi”. Ikiwa na maana yapo mengine yanapaswa yafanyike ili uumbaji huo ukamilike.

Ukisoma kitabu cha Mwanzo mstari wa kwanza kabisa wa kitabu kile unasema.

Mwanzo 1:1Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. 

Lakini cha ajabu ni kuwa uumbaji ule haukuukamlisha ulimwengu wetu, ndio maana ukisoma vifungu vinavyofuata anasema..

Mwanzo 1:2a “ Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji;…”

Dunia Ilikuwa ni Utupu, na ukiwa.  Na yenye giza, kitu cha kutisha. Ndio hapo Mungu anachukua hatua nyingine kuu MBILI (2), ili kuikamilisha. Ya kwanza ni “ROHO WA MUNGU” kutua juu yake, na ya pili kutamka “NENO” lake.

Baada ya hapo ulimwengu ukaanza kuumbika vizuri, na kuwa makao ya mwanadamu, pamoja na kila kiumbe kilichohai kilichoumbwa na mwenyezi Mungu, kama alivyokusudia yeye.

Mwanzo 1:2b…Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.  3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.  4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza

Kwamba kiumbe chochote kilichoumbwa, Kikikosa Roho wa Mungu, na Neno la Mungu. Kiumbe hicho ni Ukiwa na utupu haijalishi kitakuwa hodari, kikubwa, kina utashi  kiasi gani.

Ni kufunua nini?

Mimi na wewe tumeumbwa na Mungu tukaitwa wanadamu, ni vizuri. Lakini hiyo haitoshi. Bado hatujakamilika kama Neno La Mungu halijafunuliwa ndani yetu. Na Neno hilo si mwingine zaidi ya YESU. Yeye ndio ile sauti ya Mungu tangu pale mwanzo, iliyosema na iwe NURU. Ambayo baadaye ikaja  kufanyika mwili, likakaa na sisi;

Yohana 1:1  “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

2  Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

3  Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

4  Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, NAO ULE UZIMA ULIKUWA NURU YA WATU. 5  NAYO NURU YANG’AA GIZANI, WALA GIZA HALIKUIWEZA”

Maana yake ni kuwa kama huna KRISTO YESU maishani mwako. Wewe ni bure.

Vilevile na Roho wake MTAKATIFU kuwa juu yako.

Warumi 8:9  Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote ASIPOKUWA NA ROHO WA KRISTO, HUYO SI WAKE.

Ndio maana kwanini upo umuhimu wa mtu kuzaliwa mara ya pili. Kwa kumpokea Kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yake, ili apate msamaha wa dhambi. Lakini pia kupokea Roho wake Mtakatifu.

Ukikamilisha hayo mawili wewe hapo unakuwa mtu KAMILI na HALISI, aliyeumbwa na Mungu. Unayeweza kumzalia Mungu matunda yote anayotaka.

Okoka ndugu, Fahamu kuwa hakuna maisha nje ya Kristo,  hizi ni siku za mwisho. Kristo anakaribia kurudi, ulimwengu upo ukingoni. Umejiandaaje na karamu ya mwanakondoo mbinguni? Ukamilifu wako upo wapi?

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Nitajuaje kuwa nimesamehewa dhambi zangu?

AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.

Rudi nyumbani

Print this post

Mtande ni nini? Ni funzo gani lipo nyuma yake?

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi.

Waamuzi 16:13 Delila akamwambia Samsoni, Hata sasa umenidhihaki, umeniambia maneno ya uongo; niambie sasa, waweza kufungwa kwa kitu gani? Akamwambia, Ukivifuma hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo. 

14 Basi akazifunga kwa msumari, akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Naye akaamka usingizini, akaung’oa ule msumari, na ule mtande. 

15 Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi.

Mtande ni kifaa maalumu kinachotumika kufumia nyuzi za nguo, kwa kuzisokota pamoja ili kuunda nguo. Tazama mfano wa picha.

Hivyo nyuzi za nguo zilipitishwa katikati ya kamba hizo ngumu za mtande, kisha kuvutwa na kukazwa na mfumaji.

Katika habari hiyo tunaona Delila kazi yake huwenda ilikuwa ni ya ufumaji. Kwasababu ya uwepo wa kifaa hicho katika nyumba yake. Lakini katika harakati zake za kutaka kujua asili ya nguvu za Samsoni, biblia inatuambia, Samsoni alimdanganya kwa kumwambia ikiwa atavifuma vishungi vyake saba vya nywele katika mtande ule, basi, hatakuwa na nguvu za kujinasua, mahali pale.

Delila kusikia vile akaamini ni kweli, kwasababu kwa kawaida mtu ukishikwa tu nywele zako, si rahisi kuleta vurugu kwasababu utakuwa unajiumiza mwenyewe. Delila akizingatia kuwa alijua pia namna ya kufuma nyuzi vizuri. Hivyo alijihakikishia kuwa hilo linawezekana. Na cha kuongezea akapigilia na msumari kabisa, ili atakapojaribu kuzivuta nyewe zake, kutoka pale ashindwe. Kisha wafilisti waje kumchukua.

Lakini bado tunaona hilo halikuwezekana. Samsoni aling’oa misumari ile na kuuvunja mtande ule, Delila alipomwamsha.

Ni nini Tunajifunza katika habari hiyo kama waaminio?

KATIKA USINGIZI MUNGU ANAUMBA, NA SHETANI NAYE ANANASA.

Jiulize kwanini majaribio hayo yote Delila aliyafanya wakati ambao Samsoni amelala?. Alijua kabisa wakati akiwa macho Samsoni hawezi kukubali. Lakini pia swali lingine watu wanalojiuliza, iweje Samsoni, asisikie lolote wakati anatendewa vitendo vile. Kwamfano mpaka Delila anachukua nywele zake na kuziingiza kwenye mtande na kuzibana na kuzipigia misumari, asisikie chochote, ni usingizi wa namna gani?

Ndugu Mitego ya shetani, si rahisi kuigundua, kwasababu anaoutashi wa kuiweka kiasi cha kukufanya wewe usiwe mwepesi kuitambua, au kuisikia. Utashutukia tu umeshanaswa. Hivyo kama mwaminio ni kukimbia usingizi wowote wa kiroho kwa hali zote. Kwa kumtazama na kumfuata Yesu wakati wote. Unapomtazama Yesu, na kumtii kwa kuyakimbia machafu ya dunia. Hapo hujalala kiroho.

Lakini Pia katika usingizi Mungu pia hufanya jambo, na hilo si lingine zaidi ya kuumba. Utalithibitisha hilo kipindi kile alipomuumba Adamu, Mungu anasema.

Mwanzo 2:21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 

22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 

23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.

Umeona? Ukitulia kwa Bwana, akapumzika kwa Bwana, ukalala kwake. Jiandae kuumbiwa jambo lako bora kuliko yote katika maisha yako. Kama vile Mungu alivyomuumbia Adamu, msaidizi bora kuliko wote.

Kulala kwa Bwana ni kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yako, akupe ondoleo la dhambi. Kisha kuamua kuacha mambo yote ya kidunia na kumfuata yeye kwa uaminifu kwa kulitii Neno lake baada ya hapo. Na hapo ndipo unakuwa umelala kwake.

Hivyo chagua leo “Kuumbwa” badala ya “Kunaswa”. Mpokee Yesu sasa, ikiwa upo tayari kufanya hivyo. Basi fungua hapa kwa mwongozo huo wa sala ya Toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KITENDAWILI CHA SAMSONI

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

Je Bwana Yesu alikuwa na nywele ndefu?

Rubani ni nani katika biblia? (Ezekieli 27:8)

Rudi nyumbani

Print this post

YESU KATIKA KUCHOKA KWAKE.

Mahali pekee ambapo maandiko yanaeleza kuchoka kwa Yesu, ni siku ile alipokuwa anatoka Uyahudi anakwenda Galilaya. Kwasababu safari yake ilikuwa ndefu, ya saa nyingi, ilibidi waweke kituo kwanza kwenye mji wa mmoja wa wasamaria, wapumzike. Yeye na wanafunzi wake kwenye kile kisima cha Yakobo.

Yohana 4: 5  Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe. 6  Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu AMECHOKA KWA SAFARI YAKE, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.

Jua la mchana likiwa kali, anasikia mwili ni mchovu hautaki, kufanya kazi yoyote, njaa zinauma, mpaka mitume wakaondoka kwenda kutafuta chakula mjini. Lakini katika mazingira hayo hayo Analetewa na Mungu mtu mwenye dhambi amshuhudie habari za neema ya wokovu. Ndio Yule mwanamke msamaria.

Lakini Yesu hakuwa na udhuru kwa kusema, huu ni muda wangu wa kupumzika, ni muda wangu wa kulala, ni muda wangu wa lunch nile na wanafunzi wangu. Alitii vilevile katika uchovu wake, akaanza kuongea na Yule mwanamke habari za ukombozi, kwa kipindi kirefu kidogo.

Lakini mwisho wa mazungumzo yao haukuwa bure, Yule mwanamke aliondoka, lakini baada ya muda mfupi alirudi na jopo la watu, ili kuja kumsikiliza Bwana Yesu, maneno aliyoshuhudiwa na yeye (Yohana 4:1-42). Na baada ya hapo tena, Samaria yote ikamwamini, sehemu nyingine mpaka wakawa wanataka hata kumfanya mfalme.

Lakini ni nini tunapaswa tujifunze katika habari hiyo?  Wengi wetu hatujui kufanikiwa kwa huduma ile ya Yesu pale ndani ya mwanamke Yule zaidi ya wengine wengi, kulitokana na gharama ambazo Yesu aliingia. Yaani katika kipindi cha KUCHOKA kwake, alikuwa tayari kulitimiza kusudi la Mungu. Kitendo hicho rohoni huwa kinageuka na kuwa IMANI, kubwa sana mbele za Mungu.

Je! Na sisi, tunaweza kujifunza jambo hili kwa Bwana. Je! visingizio cha kuchoka, tumeshindwa kutimiza makusudi mangapi ya Mungu, yenye matokeo makubwa kama haya? Nimetoka kazini, nimefanya kazi wiki nzima, hivyo nimechoka siwezi kwenda kuomba. Weekend ni siku yangu ya kupumzika, siwezi kwenda  kwenye ushuhudiaji?

Hatujui kuwa hapo ndipo Mungu anapathamini, tunataka siku ambayo tupo “free” tu.

Ukweli ni kwamba tukiwa watu wa kungojea siku ambazo tuna nafasi ya kutosha, au tuna afya, au tuna  fursa, au tume-relax si rahisi kuzalisha vema kama wakati ambao tutajiona sisi ni dhaifu. Katika dunia hii ya masumbufu na mahangaiko ya maisha, utajikuta mpaka unamaliza maisha yako hujapata hata huo muda wa kupumzika vema. Hivyo tumia fursa hiyo sasa.

Isaya 40:29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.  30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;  31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.

Hubiri injili nyakati zote, omba nyakati zote, soma Neno nyakati zote. Kumbuka wakati wa kuchoka, ipo nguvu ya Mungu kukusaidia. Jenga ufalme wa Mungu. Na Bwana atakutia nguvu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

WALIKUWA WAMECHOKA NA KUTAWANYIKA KAMA KONDOO WASIO NA MCHUNGAJI.

NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Farao alikufa kwenye maji pamoja na jeshi lake au alipona?

Maandiko hayaelezi moja kwa moja kifo cha Farao. Lakini baadhi ya hivi vifungu vinatuonyesha Farao alizama na jeshi lake katika bahari ya shamu.

Zaburi 136:15

[15]Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;  Kwa maana fadhili zake ni za milele. 

Kuonyesha kwamba sio tu jeshi lake, lakini pia pamoja na yeye..walizamishwa baharini.

Pia vifungu hivi…

Kutoka 14:28

[28]Yale maji yakarudi yakafunikiza magari na wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja. 

Maandiko hayo, hapo mwishoni yanasema hakusalia hata “mtu mmoja”. Ikiwa na maana hata Farao mwenyewe alikwenda na maji.

Lakini pia andiko linaendelea kusema zaidi…

Kutoka 15:19

[19]Kwa maana farasi za Farao na magari yake na wapanda farasi wake waliingia ndani ya bahari, BWANA akayarudisha maji ya bahari juu yao; bali wana wa Israeli walikwenda katika nchi kavu katikati ya bahari. 

Maana yake ikiwa kama magari yake mwenyewe yalizama baharini, ni uthibitisho kuwa hata na yeye mwenyewe alikuwa juu ya gari lake. Haiwezekani yeye kama mfalme aruhusu gari lake liende halafu abakie kwa miguu.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Farao alikufa katika bahari ile, pamoja na jeshi lake. Na Mungu ilimpasa awahakikishie wokovu kamili watu wake. Kwa kumwangamiza aliye kichwa cha adui zao. Kwasababu tangu mwanzo, masumbufu yote yalishinikizwa na Farao, hivyo alikuwa hana budi kuondolewa na yeye. Ili Israeli waufurahie wokovu mkuu wa Mungu.

Bwana akubariki.

Kutufundisha nini?

Mungu huwa anawahakikishia wokovu kamili watu wake, hata sasa tunao ukombozi mkamilifu ndani ya Yesu Kristo kwa kumwimini yeye, adui yetu shetani na mapepo yake yanafukuzwa,mbali na sisi. Lakini yatupasa tusiwe watu wa kutokuamini kama wana wa Israeli jangwani kwa kuishi kama wapagani, kwasababu ijapokuwa Mungu aliwaahidia nchi nzuri iliyobubujika maziwa na asali, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kuiingia isipokuwa wawili. Vivyo hivyo na sisi hatuna budi kuishindania Imani yetu. Ili tusionekane tumekosa kuingia kwenye ufalme wa Mungu wetu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

YONA: Mlango 1

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

USIMWABUDU SHETANI!

Rudi nyumbani

Print this post