Category Archive Uncategorized

MAGONJWA YAKUPATAYO MARA KWA MARA.

1Timotheo 5:23  “Tokea sasa usinywe maji tu lakini tumia mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara”

Haya ni maneno ya mtume Paulo kwa mtoto wake wa kiroho Timotheo, Ni rahisi kuyachukulia juu juu, lakini ukitazama kwa undani utaona jinsi watu wa kale walivyojitoa kwa Bwana,bila kuruhusu hali zao za mwilini kuwakwamisha.

Kama tunavyosoma, Timotheo alikuwa ni kijana mwenye bidii sana, aliyetumika na Mtume Paulo katika kuineza injili sehemu kubwa ya dunia, lakini kijana huyu hakuwa vizuri sana kiafya kama tunavyodhani, alikuwa anasumbuliwa na tumbo, lakini kama hilo halitoshi, alikuwa pia anapatwa na magonjwa ya MARA KWA MARA, tena katika ujana na sio uzee. Ni heri magonjwa hayo yangekuwa ni ya siku moja, bali ya mara kwa mara. Paulo aliishi naye kwa muda mrefu hivyo alikuwa anamwelewa sana, anashangaa leo yupo sawa, kesho, ni mgonjwa, wiki hii yupo sawa, wiki ijayo tumbo linamsumbua sana.

Lakini katika yote hayo, hakuwa kama Dema ambaye alimwacha Paulo, akaurudia ulimwengu, yeye aliendelea kuitenda kazi ya Bwana katika madhaifu yake ya mwili,  Ni mtu tu pekee ambaye Paulo alijiona amani kumwachia hata huduma yake aiendeleza duniani. Alikuwa kama Elisha kwa Eliya.

Hivyo mwishoni kabisa mwa huduma, tunaona hapa Paulo anamwandikia waraka huu na kumsisitiza, asinywe maji tu peke yake, bali na mvinyo kidogo kwa ajili ya magonjwa hayo ya mara kwa mara, Paulo hapa anampa ushauri wa kitabibu, zaidi ya ule wa kiroho, kwani zamani mvinyo , ulitumika kwa ajili ya baadhi ya magonjwa, lakini sasa kwa wakati wetu tunazo dawa za hospitalini. Unaweza kujiuliza Paulo ambaye Mungu alimtumia kwa ishara na miujiza ya kupita kawaida, angepaswa amweke, mikono, na kukemea magonjwa hayo ya mara kwa mara yamwachie, lakini alitambua kuwa si kila wakati hali itakuwa hivyo, mambo mengine Mungu anayaruhusu yatokee kwa sababu zake.

Ni kama Elisha, ambaye, alisumbuliwa na ugonjwa ambao ulikuja kumuua, lakini hakumwacha Bwana, na kusema Mungu gani huyu hanioni, aliendelea kuwa nabii wa Mungu,

2Wafalme 13:14 “Basi Elisha alikuwa ameshikwa na ugonjwa wake uliomwua; naye Yehoashi mfalme wa Israeli akatelemka amtazame, akamlilia mbele yake, akasema, Baba yangu! Baba yangu! Gari la Israeli na wapanda farasi wake!”

Ni nini Bwana anataka tujifunze?

Katika madhaifu yetu, kamwe tusipunguze spidi ya kumtumikia Mungu, kwasababu mambo tunayoyapitia sisi walishayapitia watakatifu wengine waliotutangulia. Kijana Timotheo, alikuwa ni mdhaifu sana kimwili, lakini aliichapa injili ya Kristo, bila kujali yamsibuyo. Alisafiri huko na huko.

Yawezekana na wewe, ni mhubiri au mtumishi wa Bwana, lakini vidonda vya tumbo, haviishi ndani yako ijapokuwa umemwomba sana Bwana aviondoe lakini bado huoni matokeo yoyote, endelea hivyo hivyo kutumika usisubiri upone, una magonjwa Fulani ya kichwa ambayo yanakuja na kuondoka, yanakuja na kuondoka, yasikukwamishe, mkumbuke Timotheo, kunywa dawa za hospitalini, songa mbele, unasumbuliwa na saratani, unasumbuliwa na sukari, inapanda, inashuka, kila siku ni kuchoma sindani, Usingoje kwanza Bwana akuponye, endelea, kwani huzijui njia za Bwana, hujui ni kwanini leo upo hivyo, huwenda amekusudia, uishi maisha marefu kuliko zaidi ya wengine katika hali hiyo hiyo ili jina lake litukuzwe, na uwaponye wengi wanaosumbuliwa na maradhi kama hayo, Elisha baada ya kufa katika ule ugonjwa wake, tunaona bado mifupa yake ilifufua wafu, Hivyo kuugua si kikwazo cha Mungu kutokututumia sisi.

Tujipe moyo tusonge mbele, Bwana anatupenda, kwani yeye mwenyewe alisema, pale tuwapo dhaifu ndipo tulipo na nguvu.

2Wakorintho12:9  “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. 12.10  Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu”.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Nini maana ya..“wakiwazuia watu wasioe” (1Timotheo 4:1)

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

KANSA/SARATANI INATIBIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE

Kuna wakati Bwana Yesu alianza safari ya kuchosha ya kutembea kutoka Yerusalemu kuelekea Galilaya..lakini maandiko yanatuonyesha katika safari yake yote hiyo hakuona mahali popote pa kupumzika, japo alikatiza katika vijiji na miji midogo midogo.

Lakini alipofika Samaria mahali ambapo hapakai wayahudi, aliingia katika eneo ambalo, huwenda alihisi amani  nyingi ya Mungu ikibubujika ndani yake, na hapo hapo akaona kisima cha maji akatulia apumzike kidogo.

Lakini maandiko yanatupa uelewa eneo hilo lilikuwa ni la namna gani mpaka likamfanya Yesu avutiwe nalo…yanasema..mahali pale palikuwa ni karibu na Shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe..

Yohana 4:3-8

[3]aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya.

[4]Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria.

[5]Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.

[6]Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.

[7]Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.

[8]Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.

Yesu aliiiona ardhi ile katika roho, aliona mbaraka ule wa Yakobo kwa mwanawe Yusufu unavyomkaribisha pale, hivyo hakuweza kupita hivi hivi bila kutenda jambo…aliiona haki ya Yusufu inamlilia shambani kwake.. Kumbuka Israeli yote ilikuwa ni Milki ya wana wote wa 12 wa Yakobo, lakini si kila shamba la mwana wa Yakobo Yesu alipumzika.

Hivyo kitendo cha Yesu tu kutulia pale, kama tunavyojua habari watu wengi wa Samaria wakapokea wokovu akawaokoa watu ambao hawakustahili wokovu kabisa (yaani wasamaria).

Unaweza kujiuliza ni wakati gani Yakobo alimpa Yusufu shamba hilo? Waweza kusoma habari hiyo katika..Mwanzo 48:21-22

Utaona akipewa sehemu mara dufu ya wenzake.. Na hiyo yote ni kwasababu Yakobo alimpenda Yusufu kwa tabia zake njema.

Ile Tabia ya Yusufu ya kumcha Bwana alipokea thawabu sio tu za wakati ule alipofanyika kuwa waziri mkuu wa Misri.. Lakini tunaona pia hadi kipindi cha Bwana Yesu baraka zake bado zilitembea.

Leo hii ukimcha Mungu wewe kama kijana, utawasababishia wengine kupokea neema ya wokovu  hata wakati ambapo haupo hapa duniani.. Kumcha Mungu ni uwekezaji mkubwa sana zaidi ya mali.

Bwana akikubariki uzao, basi huwenda vitukuu vyako vikawa majeshi hodari ya Kristo, kwasababu Yesu anapita kuangalia ni wapi mbaraka wa Yusufu upo  ili apumzike?akakuona wewe.

Akikubariki mashamba au mali, siku za mbeleni aidha uwapo hai au ufapo, Kristo atapita hapo na patakuwa kitovu cha madhabahu nyingi za Mungu.

Chochote kile ukiachacho duniani, kama sio mali, kama sio shamba, kama sio vitu..basi Mungu atatumia hata mifupa yako kuwaponya wengine.. Ndivyo Mungu alivyovyafanya kwa Elisha baada ya kufa na miaka mingi kupita ameshasahaulika, amebakia tu mifupa,kaburini, lakini maiti ilipoangukia mifupa yake, ile maiti ikafufuka.

Je ni tabia gani unaionyesha kwa Mungu sasa, hadi akupe shamba lake spesheli ambalo Kristo atakuja kupumzikia hapo siku za mbeleni? Watoto wako, vijukuu vyako, vitabrikiwaje kama wewe hutamcha Mungu sasa?

Tafakari maisha ya Yusufu, kisha fananisha na yako utapata majibu. Yatupasa tuichukie dhambi, tuchukie uasherati, tuchukie wizi, tuwe waaminifu, tuishi maisha yanayompendeza Mungu sikuzote. 

Na hatimaye na sisi tutakuwa wokovu kwa vizazi vyijavyo. 

Bwana atuponye..Bwana atusaidie.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

UVUMILIVU NA MIKAKATI YA ABSALOMU, INA FUNZA NYUMA YAKE.

Kuiaua Nchi ni kufanya nini? (Waamuzi 18:2).

Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.

Rudi nyumbani

Print this post

Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)          

Huu ni mwendelezo wa Mafundisho maalumu yawahusuyo wanawake.

Mithali 11:16          

[16]Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; ..”

Ujumbe huu ni kwako wewe binti/Mama/ ambaye unapenda kuheshimiwa na Mungu pamoja na wanadamu.

Kumbuka  heshima inatafutwa na si wote wanayo, kwasababu inagharama yake kuipata…heshima sio uzuri, heshima sio elimu, sio u-kisasa, wala sio pesa..Ni thamani yako ya ndani, inayoonwa na wengine.

Dada Ukitaka kufahamu ni nini kitakupa heshima usiwafuate mabinti wenzako,la! Hata na  akili zako pia usizifuate, Bali mtafute aliyekuumba ili akupe siri ni nini kitakuthaminisha hapa duniani kwa wanadamu.

Inatia huruma kuona, mabinti wengi wanadhani wanaheshimiwa kwa urembo wao..hivyo hubuni kila namna ya kujipamba, na kujichubua ngozi zao, wanavaa mawigi na makucha ya bandia, kisha kwa ujasiri wanatembe mbele ya watu..wakidhani kuwa ndio wanaonekana watu wa maana sana kwenye jamii..Ukifanya hivyo Binti umepotea!

Wanadhani kuonyesha miili yao barabarani, na kujifanya wakisasa ni heshima, dada hapo huheshimiwi unasanifiwa tu. Unachofanya ni kujiongezea nafasi tu ya kuwa kiburudisho cha macho ya wahuni..na ndio maana watakupigia miluzi na kukutazama tazama.mara mbili ili kesho urudie kufanya hivyo tena, wajiburudishe macho yao, lakini zaidi ya hapo wewe la FELIA…

Hivyo fahamu heshima yako inatoka wapi..

Biblia inaeleza heshima ya mwanamke inakuja katika mambo haya  saba

  1. Kumcha Bwanari
  2. Adabu
  3. Upole
  4. Kiasi
  5. Utulivu
  6. Kujisitiri
  7. Utiifu

Yote haya utayasoma katika vifungu hivi:

Mithali 31:30

[30]Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili;  Bali mwanamke AMCHAYE BWANA, ndiye atakayesifiwa.

1 Timotheo 2:9-11

[9]Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa MAVAZI YA KUJISITIRI, pamoja na ADABU nzuri, na MOYO WA KIASI; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

[10]bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.

[11]Mwanamke na ajifunze katika UTULIVU, AKITII kwa kila namna.

1 Petro 3:3-4

[3]Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

[4]bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya UPOLE NA UTULIVU, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

Ukiyazingatia haya binti/mwanamke, heshima itakufuata yenyewe…na lolote ulitamanilo kwa Mungu utalipata tu..Kama ni mume bora Mungu atakuletea, tena zaidi ya matarajio yako kama Ruthu alivyoletewa Boazi, 

Kama ni kibali, utakipata tena cheo kikubwa zaidi ya wengi, ikiwa ni utumishi, Bwana ataizidisha karama yako pakubwa sana..Na zaidi ya yote una uzima wa milele. Hata ukienda mbinguni unawekwa kuwekwa kundi moja na akina Sara na Ana na Debora, Mariamu, na wanawake wote mashujaa walioishindania imani ipasavyo.

Lakini kinyume chake ni kweli, usipoyashika hayo, utafanana tu na Yezebeli na ukienda kuzimu utawekwa kundi moja na yeye.

Usiiuze heshima yako.

Jithamini.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

USHAURI KWA MWANAMKE WA KIKRISTO.

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?

Rudi nyumbani

Print this post

Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala Mwangalie sana

SWALI: Mstari huu unamaana gani?

Mithali 23:1-3

[1]Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala, Mwangalie sana yeye aliye mbele yako.

[2]Tena ujitie kisu kooni, Kama ukiwa mlafi.

[3]Usivitamani vyakula vyake vya anasa; Kwa maana ni vyakula vya hila.


JIBU: Sulemani akiwa kama mfalme alielewa sana tabia za wafalme zilivyo na hivyo kwa uzoefu wake hapa anatoa mapendekezo yake kwa mtu yeyote ambaye ataitwa na mfalme au mtu yeyote mkuu kula chakula pamoja nao.

Anasema chukua tahadhari “Mwangalie sana”..uwe na kiasi na hizo zawadi zake akupazo, hapo ametumia lugha ya vyakula, lakini yaweza kuwa uongozi, fursa, pesa, n.k..anasema uwe na kiasi, kwasababu nyingi za hizo huwa ni za hila.

Kwasababu mfalme hawezi kumwalika mtu, kama haioni kuna faida fulani anaweza kuipata kwake, ingekuwa ni hivyo angekuwa anamwalika kila mtu tu, ikulu na kushiriki naye.

Mfano wa wazi tunauona, kwa malkia Esta alipomwalika Hamani, kama Hamani angelielewa andiko hili, angetafakari mara mbili mbili ni kwanini apewe tu yeye kipaumbele cha juu zaidi ya wengine..Lakini alikuwa anacheka na kufurahia tu mialiko, na matokeo yake yakawa ni kujipeleka mwenyewe kitanzini.

Ni kawaida ya shetani akishaona una hatari ya kuupindua ufalme wake, haji kwa hasira au kiboko, atakuja kwa anasa, alifanya hivyo kwa Bwana Yesu, na kumwambia “hivi vyote nitakupa, endapo utaanguka na kunisujudia”..Bwana akamkemea, na kumfukuza, wakati mwingine mfalme Belshaza alimwita Danieli, amtabirie vizuri juu ya ufalme wake akamuahidi atakuwa mtu wa tatu kwenye ufalme wake, Danieli hakupumbazika na kukaa pamoja naye katika utalawala wake wa dhambi, kinyume chake akakataa akatabiri na kuondoka zake..Lakini usiku huo huo kumbe ndio ulikuwa mwisho wa mfalme Belshaza, akavamiwa na wamedi, na kuuawa, sasa kama Danieli angekutwa pale anafanya anasa nao naye pia habari yake ingeishia pale.

Watumishi wengi wa Mungu wakubwa, wamepoozwa moto wao wa injili au utumishi wao kwa ujumla na watu wakuu au wa mamlaka, kwa kukosa kwao kiasi. 

Hivyo mstari huu unatupa tahadhari, katika ngazi yoyote ile,  iwe ni ngazi ya chini, katika kampuni,au shirika,  au katika serikali, tualikwapo, tuwe makini, kuchunguza ni mashauri gani yapo nyuma yake.

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU

NUHU WA SASA.

Rudi nyumbani

Print this post

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo aliye Bwana na mwokozi wetu. Utukufu na uweza ni vyake milele na milele. AMEN.

Leo tuone ni nini Bwana anasema nasi tena nyuma ya  tukio la Hajiri kijazi wa Sarai alipomtoroka bibi yake..

Kama tuonavyo katika maandiko mateso yalipozidi, alikimbilia jangwani..lakini akiwa kule jangwani, alilia sana  Bwana, amsaidie kwasababu kama tujuavyo jangwani ni mahali ambapo hakuna mahitaji yoyote ya kijamii..ukizingatia na yeye alikuwa mjamzito, hawezi kujihudumia kwa lolote.

Lakini upo uamuzi ambao hajiri aliuchukua ambao kama asingeuchukua kwa wakati ule, haijalishi angemlilia Mungu namna gani asingepata msaada wowote, wala asingeisikia sauti ya Mungu, ilipokuwa inamtafuta kusema naye kule jamgwani..

Na uamuzi wenyewe ulikuwa ni ule wa kukimbilia kwenye CHEMCHEMI YA MAJI. 

Mwanzo 16:6-12

[6]Naye Abramu akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake.

[7]MALAIKA WA BWANA AKAMWONA KWENYE CHEMCHEMI YA MAJI katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri.

[8]Akamwambia, Hajiri, wewe mjakazi wa Sarai, unatoka wapi, nawe unakwenda wapi? Akanena, Nakimbia mimi kutoka mbele ya bibi yangu Sarai.

[9]Malaika wa BWANA akamwambia, Rudi kwa bibi yako, ukanyenyekee chini ya mikono yake.

[10]Malaika wa BWANA akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi.

[11]Malaika wa BWANA akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana BWANA amesikia kilio cha mateso yako.

[12]Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.

Ni vizuri tukaona kitu hapo…kumbe malaika alikuwa anamtafuta hamwoni…lakini alipofika katika ile chemchemi ya maji ndipo akamwona Hajiri kisha akazungumza naye na kumpa maagizo.

Hata sasa, watu wengi wanamlilia Mungu kweli awasaidie, wapo katika majangwa ya namna mbalimbali, na Mungu kweli anawasikia, lakini pale ambapo malaika wa Bwana wanatumwa kuwapa majibu yao hawawaoni, kwasababu hawapo katika chemchemi ya maji…wapo kwenginepo.

Na maandiko yanasema Yesu ndiye chemchemi ya maji ya uzima..

Yohana 4:13-14

[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;

[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

Ni mara ngapi tunakuwa wepesi wa kumlilia Mungu atusaidie, lakini kumuishi Kristo katika maisha yetu inakuwa ngumu.

Hatuna Muda wa kusoma Neno, hatuna muda wa kuomba, hatuna muda wa kufanya ibada, na kushuhudia habari njema, hatuna muda wa kudumu katika chemchemi ya maji ya uzima..lakini wakati huo huo tunalia Bwana tusaidie! Bwana tutetee! Bwana tubariki!, Bwana tuponye..tukiwa katika biashara zetu, katika kijiwe vyetu, katika mitandao ya kijamii tunachat, katika tv, tunaangalia movie, na tamthilia, katika party na starehe, tunakesha kila mwisho wa wiki, lakini kukesha kanisa mara moja kwa wiki hatuwezi. 

Tusahau kumwona malaika wa Bwana, akileta majibu ya maombi yetu..kwasababu macho yao hayaoni mahali pengine zaidi ya penye chemchemi ya maji ya uzima. Ndivyo walivyoumbwa, Kamwe malaika hawezi kukufuata kwenye kijiwe chako, au kwenye mihangaiko yako, kukupa majibu ya maombi yako. Atakuona tu, pindi uwapo uweponi mwa Kristo, hilo tu!…hawana shughuli na mambo ya ulimwengu huu.

Tumaanishe sasa kumrudia Bwana, kwa mioyo yetu yote..tujifunze kudumu uwepo mwa Kristo, Kuna faida nyingi. Ondoa uvivu wako katika masuala ya wokovu wa Roho yako. Ikiwa utaamka kila siku alafajiri kwenda kazini, kwanini uone uvivu kuhudhuria mikesha na ibada?

Bwana atusaidie…

Je umeokoka? Je! Unatambua ya kuwa tunaishi katika kizazi ambacho kinaweza kushuhudia tukio la kurudi kwa pili kwa Kristo duniani? Kwasababu dalili zote zimeshatimia. Na kanisa tunaloishi ndio la mwisho lijulikanalo kama Laodikia?

Umejiwekaje tayari, ikiwa upo tayari kumkabidhi Kristo maisha yako. Na unahitaji mwongozo huo, au utapenda kupata ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi 

+255693036618/ +254789001312

Bwana akubariki shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WEWE U MUNGU UONAYE.

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

NUNUA MAJI YA UZIMA.

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Rudi nyumbani

Print this post

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

(1Samweli 23:1-14)

Keila ni moja ya miji midogo  iliyokuwa Israeli, lakini kuna wakati ulipitia taabu kubwa sana ya kuvamiwa na wafilisti, wakateswa wakaibiwa nafaka zao, hivyo wakiwa katika mahangaiko hayo, na mateso hakuna wa kuwasaidia, Maandiko yanatuonesha akatokea Daudi katika maficho yake, alipokuwa anamkimbia Sauli..Akapita katikati ya mji huo,akasikia, kuwa wafilisti wapo huko wanawatesa watu wa Keila.

Lakini Daudi aliguswa sana moyo, hakujali Maisha yake na kuendelea na safari yake ya mafichoni bali alichokifanya ni kukiita kikosi chake kidogo, na kukiambia adhima yake ya kuwasaidia, japokuwa watu wake walikuwa wachache, walijitia nguvu, ndipo Daudi akaenda kumuuliza Mungu, kama akiwapigania watu wa Keila atashinda au hatashinda, Mungu akamwambia, hakika atashinda, akauliza tena na mara nyingine Mungu akamjibu hivyo hivyo kuwa watashinda.

Tengeneza picha, wenyeji wa mtu huyo wanasikia, Shujaa Daudi amekuja kuwasaidia, walifurahi kiasi gani, Na ndivyo ilivyokuwa Daudi akaenda kuwapigania watu hao, akashinda na kurejesha mateka yote, tena  na Zaidi akawarejeshea. 

Wanawake, wazee, vijana wa Keila wakahuika mioyo yao, wakafurahia kuona ng’ombe zao, ngano zao, watumwa wao, mali zao zimerudi.. Waliruka ruka na kucheza, na kumpenda sana Daudi.

Lakini habari mbaya ziliwafikia kwa ghafla watu wa Keila, biblia inasema, Sauli aliyekuwa anamwinda Daudi alipata taarifa kuwa adui yake amefika Keila, kuwasaidia watu wale. Hivyo, akatuma vikosi vyake, kwenda kumkamata. Lakini safari hii sio tena kumtafuta, bali kwenda kuwafuata wakuu wa mji huo, na kuwaambia wamkamate Daudi wamfikishe kwa Sauli ili amuue.

Lakini kabla Sauli hajatuma vikosi vyake, Daudi naye akapata taarifa kuwa Sauli amejua yupo kule, hivyo alichokifanya ni kwenda kumuuliza Mungu kama ilivyokawaida yake, kuhusiana na jambo hilo kama kweli watu wa Keila watamtoa na kumpa Sauli au La..

Matarajio ya Daudi yalikuwa ni hapana, akiamini kuwa wale watu aliowaokoa kwa mkono mkuu, watampa hifadhi watamficha, hawawezi kumsaliti, Lakini Bwana akamwambia Daudi kuwa, hao watu watakutoa kwa Sauli. Hapo Daudi akawa hana jinsi Zaidi ya kuingia tena maporini kwenda kutafuta mahali pa kujificha.

1Samweli 23:7 “Kisha Sauli aliambiwa ya kwamba Daudi amefika Keila. Sauli akasema, Mungu amemtia mkononi mwangu; kwa maana amefungwa ndani, kwa vile alivyoingia katika mji wenye malango na makomeo. 

8 Basi Sauli akawaita watu wote waende vitani, ili waishukie Keila, na kumhusuru Daudi na watu wake.  9 Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera. 

10 Ndipo Daudi akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mimi mtumwa wako nimesikia hakika ya kuwa Sauli anataka kuja huku Keila, ili kuuharibu mji kwa ajili yangu. 

11 Je! Watu wa Keila watanitoa, nitiwe mkononi mwake? Je! Sauli atashuka, kama mtumwa wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, nakusihi, umwambie mtumwa wako. Naye Bwana akamjibu, Atashuka. 

12 Ndipo Daudi akasema, Je! Watu wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwake Sauli? Bwana akasema, Watakutia. 

13 Basi Daudi na watu wake, ambao wapata kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda po pote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akaacha kutoka nje. 

14 Basi Daudi alikuwa akikaa nyikani ngomeni, akakaa katika nchi ya milima milima kwenye nyika ya Zifu. Naye Sauli alikuwa akimtafuta kila siku, lakini Mungu hakumtia mikononi mwake.”

Maana yake ni nini habari hii?

Wenyeji waliona ni heri mmoja wao aangamie lakini mji wote upone mikononi mwa jeshi la Sauli. Hawakujali msaada mkubwa aliowapatia, wakamwogopa mtu ambaye hakuwajali hata kidogo walipokuwa katika mateso yao. Mfano Dhahiri wa watu wa kipindi kile cha Bwana Yesu.. 

Hawakujali miujiza waliyotendewa, hawakujali wafu waliofufuliwa, pepo waliotolewa, vipofu walioona, habari njema za faraja zilizohubiriwa na Yesu, Watoto wao walioponywa. Lakini Waliposikia tu kuna hatari ya Herode kuja kuwaangamiza.. Wakasema ni heri Mmoja afe ili taifa zima lisiangamie.

Yohana 11:47  “Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi.

48  Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu.

49  Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;

50  wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima”

Wakamsulibisha mwokozi wao.. Hata Sasa hatushangai kuona, watu wakimfurahia Kristo anapowasaidia tu nyakati za mateso yao, anapowabariki, anapowalinda, anapowaponya.. Lakini ikija tu tufani ndogo ya ibilisi kwa ajili ya Kristo, tayari wanamsaliti, wanautupilia mbali wokovu, akiambiwa anafukuzwa kazi kisa Yesu wake, anasahau, mema yote aliyofanyiwa na Bwana siku zote za Maisha yake. Anamwacha. Akiona umri umeenda haolewi, anasema huku kuvaa magauni ya nini tena, ngoja nivae vimini nitembee nusu uchi, ili nipate mchumba.

Tusiwe kama watu Keila, ambao walimsaliti shujaa wao kisa mtu asiyewajali, tusimwache Yesu kisa vitisho vya shetani vidogo vinavyopita mbeleni yetu. Kisa wazazi hawapendezwi na Imani yetu. Tukumbuke yeye ndio jemedari wetu, kama alitupigania vipindi vya nyuma atatupigania hata sasa.

Tumpende Bwana Mungu wetu kwa mioyo yetu yote, kwa nguvu zetu zote, kwa roho zetu zote, na kwa akili zetu zote.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

Naivera ni nini? Kwanini Daudi aliihitaji alipomtafuta Mungu?

Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.

WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

Haya ni Mafundisho maalumu kwa ajili ya wanawake..

JIBU: Ni vema kujua mfungo ni nini na madhumuni yake ni yapi.

Mfungo ni kitendo cha kujizuia kufanya jambo fulani la lazima kwa kipindi fulani kwa lengo la kumkaribia Mungu zaidi..

Kwamfano mfungo hasaa hulenga kujizuia kula au kunywa , wengine huzuia usingizi, wengine kazi, wengine mawasiliano n.k. inategemea unalenga nini.

Hivyo pale unapojizuia kula au kunywa lengo lako ni upate utulivu wa kuwa karibu zaidi na Mungu katika maombi na kumtafakari.

Kwahiyo kwa jinsi unavyojiweka mbali zaidi na masuala ya mwili ndivyo unavyoupa zaidi mfungo wako nguvu.

Hivyo tukirudi katika swali je tunaruhisiwa kushiriki tendo la ndoa tuwapo katika mfungo? 

Jibu ni kuwa hakuna katazo lolote..kwasababu shabaha ya mfungo wako lilikuwa katika kujizuia kula au kunywa..

Lakini ikiwa utapenda kuzuia pia tendo la ndoa, ni vizuri lakini hapo ni jambo la makubaliano na mwenzi wako, ikiwa ataliridhia kwa wakati huo msafanye tendo la ndoa, ili mwelekeze fikra zenu zote kwa Bwana…hapana shida. Ni vema.

Lakini ikiwa mmoja wenu hajaridhia, hapo hupaswi kuzuia, kwasababu uolewapo au uoapo, huna amri juu ya mwili wako, isipokuwa mwenzako, kwahiyo akikataa hupaswi kupinga.Ni lazima ufanye.

Biblia inasema..

1 Wakorintho 7:3-5

[3]Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

[4]Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

[5]Msinyimane isipokuwa MMEPATANA kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.

Vilevile ikiwa nyote hamjaridhia…pia bado hakuharibu mfungo wenu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa kushiriki tendo la ndoa, ndani ya mfungo, hakubatilishi mfungo wa mtu. Isipokuwa tu maandiko yanatuelekeza  iwe ni kwa kiasi ili mpate na muda wa kusali 

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

Mwanazuoni ni mtu aliyejikita katika utafiti au usomi wa ndani katika tasnia Fulani, lengo lake likiwa ni kupata uvumbuzi wa yale magumu yenye utata au yaliyojificha.. Hivyo mwanazuoni wa biblia ni mtu anayeingia ndani kujifunza Biblia, ili kuieleza katika urahisi zaidi au katika ufasaha zaidi  kwa jamii au kutoa majibu ya mambo magumu yaliyo ndani ya biblia.

Mwanazuoni anajitofautisha na mwana-theolojia, kwa namna ya kwamba mwanatheolojia yeye yupo kisomi zaidi, kusoma kanuni na taratibu za kidini, hivyo anapohitimu, anakuwa amepata maarifa yale yale yaliyokwisha kuandaliwa. Lakini mwanazuoni, ni mtu ambaye hafungwi na taratibu, anaweza jitenga, kuchunguza, kusoma kwa ndani na kujua maana ya mambo.

Si kila mwanazuoni lazima apitie vyuo vya biblia.. Mtu akijikita katika kusoma biblia kwa undani na kujua siri nyingi zilizo ndani yake, huyo huitwa pia mwanazuoni.

Vilevile si kila mchungaji ni mwanazuoni. Mchungaji kazi yake ni kulichunga kundi la kulilisha, lakini ni vizuri pia mchungaji yeyote awe mwana-zuoni wa biblia. Kwasababu katika siku hizi za hatari zenye mafundisho mengi potofu, na udanganyifu mwingi wa dini za uongo, kila mmoja wetu hana budi kuwa mwanazuoni(mwanafunzi) wa biblia, ili awasaidie na wale ambao, hawajui kweli ya Neno la Mungu.

Lakini..

Kuna aina mbili za wanazuoni;

  1. Wanazuoni ambao hawana msukumo wa Roho Mtakatifu.
  2. Wanazuoni ambao huvuviwa na Roho Mtakatifu.

Mfano wa hilo kundi la kwanza, ndio wale waandishi na mafarisayo, waliokuwa kipindi cha Bwana Yesu, hawa waliipokea torati kama vitabu vya kidini tu, na kuvikariri, na kutunga hata na taratibu zao nyingine ambazo Mungu hakuwaagiza kabisa.

Walikuwa wanayachunguza maandiko, lakini wanamweka Mungu nyuma, Matokeo yake wakashindwa hata  kumwona Kristo katika kila kipengele cha torati walichosoma, badala ya kumpokea wakampinga..Ndipo hapo Yesu akawaambia..

Yohana 5:39  “Mwayachunguza maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. 40  Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima”

Lakini kundi la pili la wanazuoni ni lile ambalo lina nia ya kuujua ukweli, na kiu yao ni wokovu na sio mashindano au usomi, mfano wa hawa ni wale watakatifu wa Beroya, ambao tunawasoma katika..

Matendo 17:10  “Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi. 11  Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo. 12  Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa Kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache”.

Mfano tena wa hawa, ni Nabii Danieli.. ambaye pia biblia inatuonyesha alikuwa ni mtafiti (mwanazuoni) aliyekuwa anasoma sana vitabu, na matokeo yake akagundua hesabu ya miaka ambayo wangekaa Babeli, hivyo akajinyenyekeza mbele za Mungu akaomba dua na rehema, na Mungu akamsikia, na kumfunulia zaidi..

Danieli 9:1 “Katika mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo;  2 katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini”.

Mwingine ni mtume Paulo ambaye mpaka uzee wake alikuwa anasoma vitabu, soma (2Timotheo 4:13), na ndio maana hatushangai  ni kwanini Mungu alimjalia mafunuo mengi namna ile.. mpaka akamuasa na Timotheo naye awe vilevile..

1Timotheo 4:13  “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha”.

Zipo faida nyingi za kila mmoja wetu kuwa mwanazuoni, Kama Apolo asingekuwa mwanafunzi mzuri wa maandiko, asingeweza kuwashinda wayahudi ambao walilisumbua sana kanisa la kwanza kwa imani zao potofu..(Soma Matendo 28:24-28).

Hivyo kuwa mwanazuoni huchangiwa na;  kwanza kwa kuwa na bidii ya kusoma biblia binafsi,  pili kuhudhuria mafundisho ya biblia kanisani, tatu kusoma vitabu mbalimbali vya Kikristo, Nne kusikiliza mafundisho yenye maudhui ya biblia kwenye radio, televisheni na bila shaka, kwenye tovuti kama yetu hii www.wingulamashahidi.org.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyotuhimiza kuwa wasomi/wanafunzi wa biblia..wenye lengo la kujifunza  kumjua Mungu, (lakini sio mfano wa waandishi na mafarisayo, ambao lengo lao lilikuwa ni vyeo na ukubwa, na heshima waonekane wanayajua maandiko mengi, wasomi, wakubwa waogopwe). Lakini tukiwa na kiu ya kujua mapenzi ya Mungu katika maandiko, ni bora kwetu na kwa wengine..

Wakolosai 4:6  “Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.

Mathayo 4: 4  “Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu”.

Yoshua 1:8 “Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

TUNAMHITAJI SANA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUYAELEWA MAANDIKO.

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Biblia ni nini?USIACHE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU

Gombo ni nini?

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Wakati ambapo Israeli inapitia manyanyaso makali kutoka kwa wakaanani kwa miaka 20, mpaka yakawafanya wamlilie Mungu kwa nguvu ili awaokoe..Tunasoma kwenye biblia Mungu alisikia kilio chao akawanyanyulia mwamuzi Debora pamoja na baraka..

Hivyo Mungu akawaagiza wana wa Israeli wapange majeshi, ili wakapigane na adui zao, na hakika Bwana atawashindia..makabila mengi yalikubali kupeleka majeshi yao, lakini yapo makabila mengine hayakutaka kujishughulisha na jambo hilo..na hayo si mengine zaidi ya  Dani, Asheri, na nusu ya kabila la Manase na Gadi. Haya yote yalikuwa mbali kidogo na eneo la vita, Yaliona kama vile vita haviwahusu wao, hivyo yakawa bize kuendelea na mambo yao..

Waamuzi 5:17

[17]Gileadi alikaa ng’ambo ya Yordani, 

Na Dani, mbona alikaa katika merikebu? 

Asheri alikaa kimya penye bandari ya bahari, 

Alikaa katika hori zake.

Kwamfano kama hapo maandiko yanasema Dani alikaa katika merikebu, maana yake ni kuwa alikuwa ni mfanya biashara, aliona kuacha biashara zake za melini, za uchukuzi, na kwenda kujishughulisha na vita, ni upotezaji wa muda, kupigania taifa la Mungu ni kazi kichaa, wacha niendelee na biashara zangu..Na ndivyo hata hayo mataifa mengine yalivyokuwa, yalichowaza ni biashara, na mahangaiko ya hii dunia mpaka Agizo la Mungu likawa halina maana tena kwao, hata utumwa wa taifa lao hawakuuona, mateso na dhihaka taifa lao lilipokuwa linapitia hawakuona kama ni kitu zaidi ya biashara.

Ndipo Debora akaongozwa na Roho kutunga wimbo huo wa kuwashutumu ambao mpaka sasa tunausoma..

Hata sasa, tabia za makabila haya kama Dani zipo miongoni mwa wakristo wengi, ni mara ngapi utamwambia mkristo twende tukashuhudie, kwasababu tumeamuriwa kufanya hivyo na Kristo..lakini atakuambia sina muda, nipo buzy, sina mtu wa kumuacha kwenye biashara yangu…

Anaona biashara yake ni bora kuliko kuokoa roho za watu wanaopotea, huyu ni Dani anayekaa merikebuni..kipaumbele chake ni shughuli za huu ulimwengu, kazi, pesa, ndizo anazozitaabikia kutoka Januari mpaka Disemba, mwaka kwa mwaka, hana rekodi ya kufanya chochote kizuri  kwa ajili ya ufalme wa Mungu, lakini yupo tayari kujenga majumba, na mahoteli, na ma-meli ili kutanua wigo wake wa kibiashara..

Ni kweli Mungu anaweza kuokoa watu wake pasipo wewe, lakini vilevile kumbuka Mungu anaweza kubaki na mbingu yake pasipo wewe..usipokwenda mbinguni hakumpunguzii yeye kitu.

Hatushangai hata ni kwanini hili kabila la Dani halionekani miongoni mwa makabila ya Israeli yatakayookolewa siku za mwisho (Ufunuo 7:1-8). Sababu mojawapo ni hii..Na sisi tujichunguze tutambue kipaumbele chetu kwa kwanza ni kipi. Je siku ile tutakuwa na ujasiri wa kusimama mbele ya Kristo?

Bwana atupe kuliona hili.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.

Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?.

NYOTA ZIPOTEAZO.

Kuna tofauti gani kati ya ‘Mungu’ na ‘Mola’?

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?

Rudi nyumbani

Print this post

AKAKIVUNJA KIBWETA AKAIMIMINA KICHWANI PAKE.

Yesu alipokuwa nyumbani kwa Yule Simoni mkoma, alitokea mwanamke mmoja na kufanya jambo ambalo lilizua malalamika mengi sana kwa wale waliokuwa pale, kama tunavyoifahamu habari, mwanamke Yule alikuwa na kibweta (kijagi), kilichojaa marhamu(pafyumu), na thamani yake ilikuwa ni kubwa sana, ni sawa na pesa za kitanzania, milioni 6, Mshahara wa mwaka wa mtu anayelipwa vizuri.

Lakini maandiko yanatuambia, mwanamke Yule hakufungua tu kile kifuniko cha kibweta ili aimimine pafyumu  kichwani pa Yesu hapana, bali “ alikivunja kabisa”, kwa namna nyingine aliharibifu kijagi hicho, kuonyesha kuwa hii pafyumu haitatumiwa tena sehemu nyingine yoyote, itaishia yote hapa, na hilo ndio lililowafanya wale watu waliokuwa pale walalamike, na kusema upotevu wote huu wa nini?..

Anaimwaga pafyumu yote kama maji, lakini Yule mwanamke hakujali, aliimaliza yote, mpaka nyumba yote ikiwa inanuka pafyumu.

Tusome kidogo..

Marko 14:3  “Naye alipokuwapo Bethania, nyumbani mwa Simoni mkoma, ameketi chakulani, alikuja mwanamke mwenye kibweta cha marhamu ya nardo safi ya thamani nyingi; akakivunja kibweta akaimimina kichwani pake.

4  Palikuwa na watu waliochukizwa katika nafsi zao wakisema, Kwani kupoteza marhamu namna hii? 5  Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa dinari mia tatu na kuzidi, wakapewa maskini. Wakamnung’unikia sana yule mwanamke.

6  Yesu akasema, Mwacheni; mbona mnamtaabisha? Amenitendea kazi njema;7  maana sikuzote mnao maskini pamoja nanyi, na kila mpendapo mwaweza kuwatendea mema; lakini mimi hamnami sikuzote.

8  Ametenda alivyoweza; ametangulia kuupaka mwili wangu marhamu kwa ajili ya maziko. 9  Amin, nawaambia, Kila ihubiriwapo Injili katika ulimwengu wote, na hili alilotenda huyu litatajwa kwa kumbukumbu lake”

Nachotaka tuone juu ya habari hii, ni kwamba tunaweza kudhani kuwa ni huyu mwanamke tu, ndiye aliyekuwa na kibweta kile cha thamani,..Ukweli ni kwamba wale wote walikuwa na vibweta vyao, isipokuwa tu katika maumbile tofuati.. kuna mahali walivivunja au watavivunja, na kutumia kwa ajili ya vitu watakavyoviona vya thamani..

Hata sasa, kila mmoja wetu anachokibweta chake, ni suala tu la muda.. Utajiuliza, unamtazama msanii Fulani kwenye tv, anamwaga pesa, na kuwapa makahaba, au ananunua gari la kifahari, halafu wewe unaanza kulalamika na kusema upotevu wote huo wa nini, si ni heri angewasaidia maskini, kuliko kutumia kwa anasa.. Usimlaumu kibweta chake ndio amekivunjia hapo.

Leo hii, utaona, mtu kumtolea Mungu, au kusapoti huduma ambazo zinamsaidia kiroho ni ngumu, hata halifikirii.. Lakini mwanawe akitaka kwenda shule, atahangaika kila mahali kumtafutia ada, au akiumwa, anahitaji kwenda kutibiwa India, atauza, gari mpaka shamba, kusudi kwamba aokoe maisha ya mwanawe..Hicho ni kibweta chake amekivunja.

Kuonyesha kuwa kumbe anaweza kupoteza chochote cha thamani kwa ajili ya kitu cha muhimu. Tujiulize, Utasema mimi sina kibweta cha thamani..Ukweli ni kwamba unacho, bado hujaona mahali pa muhimu pa kukimwaga. Wakati utafika tu,.

Tujiulize, vipi kuhusu Mungu wetu..Yesu wetu aliyetuokoa, twaweza kudhubutu kuwa kama huyu mwanamke? Ambaye alikivunjia kwa Bwana?..Hakujua kwa kufanya vile, injili yake itahubiriwa kizazi baada ya kizazi.. Na Yesu ni yeye Yule jana na leo na hata milele.. Kama alimfanyia huyu, anaweza pia akakufanyia na wewe, kwa namna yako..Lakini ni lazima ukivunje kibweta chako kwake..Kumbuka Bwana anasema maskini manao siku zote,..Unafurahi vipi, Bwana akuhudumie, halafu wewe umuhudumii?

Tafakari.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Rudi nyumbani

Print this post