Category Archive Uncategorized

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?

SWALI: Naomba kufahamu Wagalatia 1:8 ina maana gani? Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi?


JIBU: Tusome,

Wagalatia 1:8 “Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe”.

Ni vizuri tukafahamu kwanza ni kwanini mtume Paulo alisema kauli kama hiyo. Alisema hivyo kutokana na kuzuka kwa makundi ya watu ambao walianza  kuhubiri injili nyingine tofauti na ile waliyokuwa wanaihubiri yenye kiini cha Yesu Kristo, na matokeo yake ikapelekea mpaka imani za watu wengi kupinduliwa, ambao tayari walikuwa wameshaijua njia ya kweli.

Na ndio maana mistari ya juu yake Paulo anasema..

Wagalatia 1:6 “Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine.

7 Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo”.

Unaona? na jambo la hatari zaidi ni kuwa watu hao waliowafundisha , walikuwa wanasema mambo hayo wamefunuliwa na Mungu mwenyewe, kwa kupitia maono ambayo waliletewa na malaika wa mbinguni.

Utalithibitisha pia  hilo katika.

Wakolosai 2:18 “Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, KWA KUNYENYEKEA KWA MAPENZI YAKE MWENYEWE TU, NA KUABUDU MALAIKA, AKIJITIA KATIKA MAONO YAKE NA KUJIVUNA BURE, KWA AKILI ZAKE ZA KIMWILI;

19 wala hakishiki Kichwa, ambacho kwa yeye mwili wote ukiruzukiwa na kuungamanishwa kwa viungo na mishipa, hukua kwa maongeo yatokayo kwa Mungu”.

Sasa kwa namna ya kawaida ni rahisi mtu kuamini pale anapoambiwa maono hayo au maagizo hayo, yameletwa na malaika. Ni rahisi kudhani agizo hilo ni la Mungu.

Mpaka baadaye taarifa hizo zikawafikia mitume, ndipo hapo sasa tunaona mtume Paulo, akitoa maneno makali kama hayo, na kusema, “ ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe”.

Yaani akiwa na maana kuwa maono yoyote yanayosadikika yametoka mbinguni aidha kwa mkono wa malaika, au wa nabii au mitume wowote, lakini ni nje na mafundisho ya msingi ya mitume, basi na ALAANIWE.

Lakini kumbuka kauli hiyo haimaanishi kuwa malaika watakatifu wanaweza kuleta maono ambayo hayatokani na Mungu hapana, ni mapepo ndio yanayoweza kufanya hivyo. Isipokuwa tu  mtume Paulo hapo alikuwa anaweka msisitizo wa uhakika wa injili yao. Kwamba ni ya kweli na haiwezi kupinduliwa na kiumbe chochote kilicho juu mbinguni au kilicho chini duniani, kwasababu ni injili ya kweli ya Mungu mwenyezi.

Hata sasa, ndugu yangu wapo watu wanaoishi kwa maono na ndoto, wamelitupa kapuni Neno la Mungu, wapo tayari kutii kila wanachoambiwa au kusikia hata kama kinakwenda kinyume na Neno la Mungu. Kipindi hichi roho za udanganyifu zipo nyingi, na ndio maana tumeambiwa tusiziamini kila roho bali tuzipime kama zimetokana na Mungu au la!,(1Yohana 4:1 ). Utasikia mtu anasema Mungu amenifunulia,nikamwoe mke wa fulani au nikaongeze mke wa pili, na yeye bila kutathimini hayo maagizo kama yanaendana na Neno la Mungu, yeye anakwenda kufanya vile. Kumbe hajui kuwa tayari ameshapotea, anaishi katika uzinzi na siku ya mwisho atahukumiwa.

Hivyo tuwe makini sana, suluhisho pekee ni tudumu katika mafundisho ya mitume (Neno la Mungu), ndio tutakuwa salama daima. Usitishwe na maneno ya mtu yeyote anayekuambia malaika kanitokea au nimeonyeshwa maono. Lithibitishe kwanza katika Neno la Mungu. Kama linakinzana litupe kapuni, ishi kwa Neno.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika? Ina maana gani?

Nini maana ya kuabudu malaika? (Wakolosai 2:18)

Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

Rudi nyumbani

Print this post

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 3)

Sasa kumbuka kama tulivyoona katika malaka zilizotangulia, huko nyuma kote baada ya Mungu kuiumba dunia, alichokuwa anafanya ni UKARABATI TU, lakini sio uumbaji mwingine. Lakini hatua hii ambayo ndio ya mwisho Mungu atafanya uumbaji mwingine. Na uumbaji huu sio kwamba ataiondoa dunia yote, na kuitupa motoni, kama wengi wanavyodhani hapana, bali atafanya kama vile atakavyofanya kwenye miili yetu mipya ya kimbinguni.

Sasa kama bado hujasoma sehemu ya kwanza na ya pili, basi bofya hapa chini upitie kwanza, ndipo uendelee na sehemu hii ya tatu na ya mwisho>>

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

Siku ile tutakapoenda mbinguni, Mungu atatushushia miili mipya isiyokuwa ya udongo, bali imetengenezwa kwa matirio ya kimbinguni. Na itakaposhushwa , hii miili ya sasa tuliyonayo haitauliwa na kutupwa motoni, hapana bali itavaliwa au itamezwa na ile mipya ya kimbinguni, biblia inasema hivyo katika.

1Wakorintho 15.51 “Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,

52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.

53 Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa.

54 Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda.

55 Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?”.

Umeona hapo, ndivyo itakavyokuwa pia juu ya mbingu mpya na nchi mpya. Sio kwamba dunia yetu, itaangamizwa kabisa iondolewe hapana, bali ITAGEUZWA, na kuwa DUNIA ya ajabu sana, ambayo mfano wake hauwezi kuelezeka, hauwezi kulinganishwa hata kwa chembe na ulimwengu huu wa sasa. Utukufu wake, utakuwa ni wa mbali sana sana sana, tena sana.

Vivyo hivyo na hizi mbingu zilizo juu yetu yaani (sayari, nyota, magimba n.k.) Vitakuwa na mwonekano mwingine tofauti kabisa, vitaanza kuwa na uhai navyo.

Ukisoma Ufunuo 21&22 yote Biblia inatoa tabia za hiyo mbingu mpya na nchi mpya jinsi zitakavyokuwa, nazo ni hizi;

  • Hakutakuwa na Bahari
  • Hakutakuwa na kilio
  • Hakutakuwa na maombolezo
  • Hakutakuwa na laana
  • Hakutakuwa na maumivu
  • Hakutakuwa na kifo
  • Hakutakuwa na Usiku.

Pia ile Yerusalemu mpya, (mji wa kimbinguni), ndio utashuka juu ya hii nchi mpya na mbingu mpya. Mji ambao utakuwa ni kitovu cha ulimwengu, ambao ni bibi-arusi tu na Kristo ndio watakaouingia.

Zaidi ya yote, ni kuwa Mungu atahamisha maskani yake, na kuileta duniani. Kwa mara ya kwanza mwanadamu ataishi na Mungu, na kuuona uso wake.

Ufunuo 21:3 “Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao”.

Vilevile Muda utaondolewa, hakutakuwa tena na kitu kinachoitwa muda, kwani tutaishi Milele na milele na milele isiyokuwa na mwisho. Katika furaha na amani na vicheko daima.

Hakika ni mambo ambayo hayaelezeki, yaani tutamfurahia Mungu kila inapoitwa leo. Hizi sayari zote zisizohesabika mabilioni kwa mabilioni huko angani zitakuwa na kazi nyingi sana, hazikuumbwa ziwe ukiwa, hatuwezi kufahamu kila kitu lakini tukifika huko ndipo tutajua.

Bwana Yesu alimalizia na kusema maneno haya;

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.

Ndugu yangu, kumbuka ili kufika huko, maandalizi yake yanaanza sasa. Inasikitisha kuona kuwa wapo watu ambao hawatafika huko, Ikiwa leo hii tunaishi maisha ya ukristo vuguvugu, tunasema tumeokoka lakini ulimwengu umejaa ndani yetu. Tunatazamia vipi, tuende mbinguni kwenye unyakuo?. Au tunatazamia vipi tuingie Yerusalemu mpya.

Hizi ni nyakati ambazo, si za kubembelezewa tena wokovu, ni wewe mwenyewe tu kuona, jinsi hali halisi ilivyo. Hakuna dalili ambayo haijatimia. Siku yoyote, unyakuo utapita, na dhiki kuu itaanza.

Ikiwa hujaokoka, embu leo fanya uamuzi sahihi, Tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kugeuka, kisha, nenda kabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, sawasawa na Matendo 2:38, Kisha Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, 

Ukikamilisha hizo hatua zote, basi ujue tayari wewe ni mwana wa ufalme, jukumu lako litakuwa ni kuutuzwa wokovu wako kwa maisha ya utakatifu na ya kumcha Mungu na ya ibada ya kweli utakayokuwa unayaishi. Ukisubiria unyakuo, na zaidi hiyo mbingu mpya na nchi mpya itakayokuja huko mbeleni.

Lakini ikiwa utahitaji msaada wa kuokoka, au kubatizwa, au swali basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada zaidi. +255693036618/ +255789001312

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

MKESHA WA KUINGIA MWAKA MPYA KILA MWAKA NI WA KUUTHAMINI SANA.

UNYAKUO.

UFUNUO: Mlango wa 1

Rudi nyumbani

Print this post

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

Sasa kama tulivyotangulia kuona katika sehemu ya kwanza kuwa hii dunia yetu ilipoumbwa, ilipitia uharibifu wa mara kwa mara, na baadaye kukarabatiwa  tena na sasa imesaliwa na uharibifu mmoja wa mwisho ambao  utakuja ulimwenguni hivi karibuni, na uharibifu wenyewe hautakuwa wa maji tena, bali wa moto. (2Petro 3:6-7)

Kwahiyo Mungu atakapomaliza kuuharibifu huu ulimwengu na kuwaondoa waovu wote, ataikarabati hii dunia na kuirejeshea utukufu wake kwa ilivyokuwa pale Edeni.  Na sababu ya Mungu kufanya hivyo, ili kuruhusu YESU KRISTO kuja kutawala hapa duniani pamoja na watakatifu wake, kama Mfalme wa Wafalme, na Bwana wa Mabwana kwa kipindi cha  miaka elfu moja (1000).

Wakati huo dunia itakuwa yenye amani tele, watu wataanza kuishi umri mrefu kama mwanzo, biblia inasema, mtu atakayekuwa na umri wa miaka 100 ataitwa bado mtoto mchanga,

Isaya 65:20 “Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa”.

Watu watakuwa wakipanda na kujengwa wala hakuna atakayekuja kuharibu, au kuong’oa mazao yao. Wanyama wote watakuwa wapole, simba atakula majani, na mtoto atacheza kwenye tundu la nyoka na asidhuriwe kwa lolote (Isaya 65:21:25).

Lakini pamoja na hayo, biblia inarekodi pia watu waovu watakuwepo, ila dhambi haitatawala kwasababu shetani wakati huo atakuwa amefungwa, mtu akiasi kwa namna yoyote ile atauliwa,

Hivyo kwa ujumla ni kuwa utakuwa ni utawala wa amani nyingi sana, ni kipindi ambacho Mungu amewahifadhia watakatifu wake kuwafurahisha na kuwapa raha. Mimi na wewe tusikose hiyo sabato kuu ya Mungu ya utawala huo wa miaka 1000.

kwa urefu wa somo hilo la utawala wa miaka elfu, fungua hii link >>https://wingulamashahidi.org/2019/05/30/utawala-wa-miaka-1000/ 

Sasa mara baada ya utawala huo kupita, biblia inasema tena, shetani atafunguliwa kwa kipindi kifupi sana, kuwajaribifu wale waovu waliokuwa ndani ya dunia hiyo. Watakapo jaribu kuizunguka kambi ya watakatifu, wakati huo huo moto utashuka na kuwaangamiza wote. Kisha watahukumiwa na kutupwa katika lile ziwa la moto

Ufunuo 20:7 “Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake;

8 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari.

9 Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala.

10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele”.

Baada ya hapo, mpango wote wa ukarabatiji wa ulimwengu utakuwa umeisha, kinachofuata sasa hiyo ni mbingu mpya na nchi mpya, ambayo Mungu aliikusudia tangu zamani wanadamu waishi ndani yake.

Jambo ambalo ndio shabaha yetu kuu sisi watakatifu. Hiyo mbingu mpya na nchi mpya. Kama vile mtume Petro alivyosema katika.

2Petro 3:13 “Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.

14 Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake”.

Mpaka hapo utakuwa umeona jinsi Mungu alivyoiumba dunia yake, na kila ilipoharibiwa, baadaye aliiponya kwa sehemu au aliikarabati na kuirudisha kama mwanzo. Lakini hakuwahi kufanya uumbaji mwingine mpya, wa ulimwengu.

Hivyo fuatana nami katika sehemu ya Tatu na ya mwisho, ambayo inaelezea sasa, jinsi hiyo mbingu mpya na nchi mpya itakavyokuja kuwa.

Bofya chini kwa sehemu ya kwanza na ya tatu >>>

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 3)

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

NITAFANYA YERUSALEMU KUWA JIWE LA KUWALEMEA .

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

 Mithali 12:10 “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili”.


JIBU: Hapa ni Mungu alikuwa anaonyesha tabia za mtu mwenye haki jinsi zilivyo kwamba huruma zake haziishi tu kwa wanadamu wenzake, bali pia zitadhihirika mpaka na kwa wanyama.

Kama vile Mungu sasa anavyowajali wanyama wake, kiasi kwamba hakuna hata mmoja anayekufa bila ya yeye kujua, na vivyo hivyo na sisi tunapaswa tuwe na tabia hizo, alisema ..

Mathayo 10:29 “Je! Mashomoro wawili hawauzwi kwa senti moja? Wala hata mmoja haanguki chini asipojua Baba yenu;”

Sehemu nyingine Bwana Yesu alisema maneno haya;

Luka 14:5 Akawaambia, Ni nani miongoni mwenu, ikiwa ng’ombe wake au punda wake ametumbukia kisimani, asiyemwopoa mara hiyo siku ya sabato?

 Akimaanisha kuwa, kumbe watu wengi walikuwa wanainajisi sabato pasipo wao kujua na Mungu asiwahesabie makosa, kwa tendo tu hilo la kuwaokoa wanyama wao.

Utaona pia sehemu nyingine, Balaamu Yule nabii wa uongo alipompigia Yule punda wake, mara tatu, Mungu alichukizwa sana na kitendo kile.. Na ndio maana swali la kwanza aliloulizwa na Yule malaika ni kwanini amempiga Yule punda kiasi kile? (Hesabu 22:32)

 Kuonyesha kuwa Mungu hapendezwi na kitendo cha utesaji wanyama.

Hivyo na sisi pia kama tulikuwa na tabia za kuwatesa wanyama, au kutoijali mifugo yetu, kiasi kwamba ukimkuta mbwa unamsindikiza na mawe,tuache hizo tabia, kama wanaishi na sisi pasipo madhara yoyote, hakuna sababu ya kuwapiga piga ovyo, au kuwafuga na kutowahudumia.

Kwasababu kitendo cha kuwatendea mema, biblia inasema kinaongeza pia siku za kuishi duniani soma,

Kumbukumbu 22:6 “Kiota cha ndege kikitukia kuwa mbele yako njiani, katika mti wo wote, au chini, chenye makinda au mayai, naye koo ameatamia juu ya makinda, au juu ya mayai, usimtwae yule koo pamoja na makinda;

7 sharti umwache yule koo aende zake, lakini makinda waweza kuyatwaa uwe nayo; ili upate kufanikiwa, ufanye siku zako kuwa nyingi”.

Hiyo ndio maana ya huo mstari ..Mithali 12:10 “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Paulo, alihukumu wakati hukumu hairuhusiwi?

SWALI: Tukisoma katika Kitabu cha 1 Wakorintho Sura ile ya Tano, Tunaona Mtume Paulo Akizungumzia Habari Ya kutengwa Kwa Watu wenye kulichafua kanisa la Mungu,… sasa tukija katika Mstari wa 3, alisema hivi..

“ Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha KUMHUKUMU yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo”.

Swali langu ni hili, Katika Huo mstari wa Tatu, naona Mtume Paulo anasema kwamba, mtu wa namna ile, Yaani aliye mzinzi, mlevi N.K.. yeye Amekwisha Kumuhukumu,… Sasa na Tukisoma katika kitabu cha Mathayo, 7:1, Bwana Yesu alituonya Kwamba tusihukumu, kwa maana tukihukumu mtu nasi tutahukimiwa….Sasa hapa imekaaje kaaje?


JIBU: Hukumu Mtume Paulo aliyomaanisha hapo si kuhukumu ile inayozungumziwa katika Mathayo 7..Kwamba msihukumu msije mkahukumiwa,.. Ile inayozungumziwa inakuja pale mtu anapotoa maneno yanatoa hatma ya maisha ya mtu mwingine, kana kwamba ni Mungu , kwamfano,kumwambia mwenzako wewe ni wa motoni tu, hata iweje huwezi kuokoka.  Hapo umeshahukumu. Au unapowaona wenye dhambi, kama vile mashoga, na unaanza kusema wale makafiri Mungu hawezi kuwakubali milele, dhambi zao hazifutiki,..Hapo tayari umeshahukumu.

Lakini mtume alichokimaanisha hapo sio hicho, bali alimaanisha hukumu ya ADHABU. Yaani kuadhibiwa kwa huyo mtu.

Na jambo kama hilo Mungu ameliruhusu wakati mwingine katika kanisa kufanyika.. Kwamfano katika habari hiyo ukiendelea kusoma mistari inayofuata utaona, mtume Paulo alisikia wakorintho wamejihusisha na zinaa mbaya, iliyokithiri ambayo haipo hata kwa watu wenye dhambi, yaani mtu anazini na mama yake halafu bado yupo katika kanisa. Sasa kwa kosa kama hilo Paulo akawaambia wakorintho, hata kabla hajafika tayari ameshamuhukumia adhabu mtu kama huyo. Na adhabu yenyewe ni kumkabidhisha shetani amuue, mwili aungamie ili roho ipone siku ile ya hukumu.

Hata sasa, matendo kama haya, yanaendelea katika kanisa la Kristo, leo hii limekuwa ni jambo la kawaida kusikia wachungaji wanazini na washirika wao, wengine wanavuka mipaka hadi na watoto wadogo, utasikia askofu anazini na muumini pamoja na mama yake, jambo ambalo huwezi kuliona hata kwa watu wenye dhambi. Na wenyewe wanaona ni sawa kwasababu hakuna mtu wa kuwakabidhisha kwa shetani.

Paulo anasema, ni heri ukabidhiwe kwa shetani uuawe, walau hasira ya Mungu utapoa juu yako, na siku  ile ya hukumu unusurike, kuliko kuendelea kuishi, katika hali hiyo hiyo mpaka kufa kwako, kwani adhabu yako itakuwa kubwa sana siku ile.

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana”.

Hivyo hiyo inatukumbusha  tuwe makini sana, katika ukristo wetu, vilevile  na katika wito wetu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

KAMA SI YESU, HABARI YETU INGEKUWA IMEISHA ZAMANI SANA.

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

JIBU: Kumbuka Mungu ameiandika injili yake katika sehemu kuu mbili. Sehemu ya kwanza ni katika kitabu, na sehemu ya pili ni katika moyo wa mwanadamu.

Watu wengi tunadhani, ni mpaka tusikie ndio tutahukumiwa hapana, hiyo ni sehemu ya kwanza, lakini kuna sheria ambayo Mungu tayari kashiweka katika moyo wa kila mwanadamu ajapo hapa duniani, ambayo hiyo inathibitishwa na kutetewa na “dhamiri na mawazo” ya mtu mwenyewe.

Biblia inasema..

Warumi 2:14 “Kwa maana watu wa Mataifa wasio na sheria wafanyapo kwa tabia zao yaliyo ndani ya torati, hao wasio na sheria wamekuwa sheria kwa nafsi zao wenyewe.

15 Hao waionyesha KAZI YA TORATI ILIYOANDIKWA MIOYONI MWAO, dhamiri yao ikiwashuhudia, na mawazo yao, yenyewe kwa yenyewe, yakiwashitaki au kuwatetea;”

Umeona? Ikiwa na maana kuwa, hata ukienda katika jamii za watu ambao wamejitenga kabisa huko maporini, hawajui chochote kinachoendelea ulimwenguni, kazi yao ni kuwinda na kukusanya tu..bado utawakuta na tabia ambazo zinaendana kabisa na sheria za Mungu, kana kwamba wanaijui torati. Kwamfano utakuta wanapinga vitendo vya uuaji, wizi, au uzinzi n.k.

Mambo kama hayo, hawakuyasoma kwanza kwenye biblia, bali tayari yalishaandikwa mioyoni mwao kana kwamba walikuwa wanaijua biblia. Na ndio katika hayo Mungu atawahukumu. Kwasababu kama tulivyosoma hapo, kwamba kama mtu atafanya yaliyo ndani ya sheria, hata kama hajaisikia, basi tayari anaitenda sheria hiyo ndani ya moyo wake.

Lakini wakati wasasa tunaoishi, injili ya Kristo imeshasambaa ulimwenguni kote, Tumesikia, na bado mioyo yetu inatushuhudia. Haijalishi utaiamini, au huiamini,  Hivyo tujue kuwa tusipoitii hatutakuwa na udhuru siku ile ya hukumu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?

Rudi nyumbani

Print this post

WAPENZI, MSIIAMINI KILA ROHO.

Wakati tunaoishi ni wakati ambao kuna machafuko mkubwa sana ya rohoni kuliko hata nyakati nyingine zilizowahi kupita huko nyuma,. Na muasisi wa hayo  ni shetani kwasababu anajua katika agano letu jipya kiini cha Kanisa ni ROHO MTAKATIFU. Hivyo anajua akiruhusu Roho wa Mungu peke yake alitawale kanisa, atawakosa watu wengi sana.

Hivyo tangu ule wakati wa mitume, alibadilisha mbinu zake za kivita, akitaka kulishambulia kanisa, haji tena mwilini, bali, ni anakuja na roho za udanganyifu zinazofanana sana na Roho Mtakatifu wa kweli kumbe sio.

Hivyo kuanzia ule wakati alianza kutoa matoleo mengi sana ya roho hizo. Mpaka sasa matoleo aliyonayo ni ya hali ya juu sana, kiasi kwamba usipokuwa makini utaweza ukavamiwa na roho za udanganyifu ukadhani ni Roho Mtakatifu kumbe ni uongo. Tupo katika wakati ambao si wa kiziamini kila roho zinazohubiriwa na watu.

Na ndio maana mitume walituonya na kusema..

1 Yohana 4:1 “Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani”.

Sasa ili tuwe salama ni vizuri tukajua tabia za kweli za  Roho Mtakatifu zipoje, ili tuwe na amani na tulichokipokea.

  1. Tabia ya kwanza ni kuwa Atakufanya uwe Mtakatifu: 

Kama jina lake lilivyo, “Roho Mtakatifu”, ndicho anachokifanya ndani ya mtu pale anapokuja juu yake rasmi, Atamfanya awe mtakatifu. Kama alivyosema katika 1Wakorintho 3:16, kuwa miili yetu ni lazima iwe mitakatifu kwasababu huyo Roho anayekaa ndani yetu ni Mtakatifu. Hivyo Ni lazima ahakikishe kuwa yale matunda yote ya roho yapo ndani yako sawasawa (Wagalatia 5:22-23)

Hivyo ukiona umepokea Roho, ambayo ndani yako haikupi kiu ya kuwa mtakatifu, yaani kuacha anasa, kuacha uvaaji mbovu, kuacha, miziki ya kidunia, kuacha vimini, na milegezo, kuwa na upendo, na kiasi, basi ujue hiyo sio Roho ya Mungu, haijalishi utanena kwa lugha muda mrefu kiasi gani.. Kimbia hapo, haraka sana.

2) Atakuongoza katika kuijua kweli yote(Yohana 16:13): 

Kazi nyingine ya Roho wa kweli wa Mungu, ni kuwa hatakuacha katika hali hiyo hiyo,ya ujinga wa kiroho uliokuwa nao sikuzote, ni lazima akupigishe hatua za kiufahamu mpaka kufikia kusimama imara katika maandiko. Lakini ukiona umeokoka na miaka nenda rudi, hujui chochote kuhusiana na Neno la Mungu, wewe unachojua ni habari za wachawi na mapepo, ujue kuwa Huyo sio Roho Mtakatifu uliyempokea bali ni roho nyingine ya adui ipo ndani yako.

3) Atamshuhudia Kristo ndani yako : 

Roho Mtakatifu kazi yake ni kutoa ushuhuda wa Kristo katikati ya kanisa lake, na sio wa mwanadamu yoyote. Ikiwa na maana kiini cha kanisa ulilopo, au huduma, unayoitumikia msingi wa hapo ni lazima awe Bwana Yesu Kristo. Na sio mwanadamu Fulani, au mtakatifu Fulani. Ukiona Kristo hapewi kipaumbele chochote, au anachukuliwa kama mtu wa ziada tu, ujue roho ya mpingakristo ipo hapo.

1Yohana 4:2 “Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu.

3 Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani”.

4) Ataweka karama au huduma ndani yako (1Wakorintho 12):

Karama hiyo/ huduma hiyo Roho Mtakatifu anaiweka kwa lengo la kulijenga kanisa la Mungu. Haiwezekani, ukawa umeokoka muda mrefu na miaka mingi, na umesema umepokea Roho Mtakatifu lakini kazi yako katika ufalme wa mbinguni haionekani. Wakati mojawapo ya kazi ya Roho Mtakatifu ni kuweka vipawa ndani yetu.

Hivyo kama hutakuwa mchungaji, au nabii, au mwinjilisti, au shemasi, au mwenye karama ya lugha, n.k basi utakuwa ni nyingine yenye faida katika kanisa kama kukirimu, kuimba, kufadhili n.k. Lakini haiwezekani kiungo kikawa hakina kazi kabisa katika mwili wa Kristo, kama mshirika anayekuja na kuondoka, miaka yote, ukiona hivyo ujue kuwa Roho uliyempokea si wa Mungu, bali ni wa adui.

5) Atachochea kuomba ndani yako. (Warumi 8:6)

Maandiko yanasema Roho Mtakatifu anaugua ndani yetu, kwa namna isiyoweza kutamkwa. Ikiwa na maana Mkristo wa kweli aliyepokea Roho, hataona amani kukaa wiki, miezi, miaka bila kuomba. Ile furaha ya wokovu itaondoka tu ndani yake, Hivyo atalazimika, kuwa mwombaji mzuri, kuhudhuria mikesha, na kufunga wakati mwingine.

Lakini ukiona unayo amani, kukaa mwezi mzima bila kuomba, na ndani yako husikii chochote, au mzigo wowote, hapo umepokea Roho nyingine ya adui. Jitathimini tena.

Tabia hizi tano (5), ukiziona ndani yako. Basi ujue Roho uliyempokea ni kweli Roho Mtakatifu, uwe na amani. Lakini kama hivyo vyote havipo ndani yako, Roho uliyepokea ni ya adui ibilisi. Unachopaswa ufanye ni umaanishe kuokoka katika maisha yako.

Maana yake, utubu dhambi zako kweli kweli, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO (Matendo 2:38). Kisha baada ya hapo, Roho wa kweli ataingia ndani yako, kuanza kukupigisha hizo hatua.

Kumbuka hizi ni siku za mwisho, na tumeaswa sana tuzijaribu hizo roho, usiridhike, na tabia mojawapo tu, jiulize je! Zote hizo zinaonekana ndani yako?

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Torati na manabii”?

SWALI: Tukisoma katika maandiko tunaona sehemu kadha wa kadha likitajwa neno “Torati na manabii”. Sasa hii torati na manabii maana yake ni nini? Kwamfano  Mathayo 7:12  inasema

“Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii”.

JIBU: Bwana Yesu aliposema Torati na manabii, alimaanisha Agano la kale, ambalo ndio limeundwa na vitabu vya Musa (Torati), ambavyo ni vitano (5), Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati.  Pamoja na vitabu vyote vya manabii, kama vile, Yeremia, Isaya, Danieli, Ezekieli, Hababuki, Amosi, n.k. hapa ikijumuisha pia, vile vingine kama  Waamuzi, Zaburi, Ayubu, Wafalme,  Mithali, Ruthu n.k. Ambavyo sio moja kwa moja vya manabii, lakini vimebeba nabii za Mungu ndani yake.

Kwahiyo torati na manabii kwa ufupi ni lile agano lote la kale. Hivyo Pale Bwana Yesu alipokuwa anawafundisha juu ya kanuni za kufuata, alirejea biblia yao, akiwaambia kuwa kiini cha biblia hiyo ni UPENDO. Wala hakuna siri nyingine nyuma yake, Torati yote, pamoja manabii wote, walichokuwa wanahubiri ni Upendo, (Ambao umegawanyika, wa Mungu na wanadamu)

Hata sisi wa leo tulio katika agano jipya, tunaposoma biblia yote tujue Ujumbe mkuu tunaoupata katika agano letu ni ule ule UPENDO. Na ndio maana Mtume Paulo alisema.

1Wakorintho 13:1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.

2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.

3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu”.

Hivyo na sisi, tunapaswa tuutafute huu, kwa bidii zote, ili tuonekane kuwa wakamilifu mbele za Mungu.

Shalom

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Roho za manabii huwatii manabii?

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

JE UPENDO WAKO UMEPOA?

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Yesu aliwaambia wale wakoma wakajionyeshe kwa makuhani?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wale watu wenye ukoma waende kujionyesha kwa makuhani?, kwanini asiwaponye tu hivyo hivyo na kuwaacha mpaka awaambie waende kwa makuhani.

Luka 17:12 “Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!

14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika”.


JIBU: Kama vile Injili ya Kristo inavyowafikia watu katika namna mbili, wengine kuwaokoa na wengine kama ushuhuda kwao (Mathayo 24:14)

Vivyo hivyo na uponyaji wake alivyouachia, alikusudia uwafikie watu kwa namna mbili. Kuokoa na wakati huo huo kuwa Ushuhuda.Si kila uponyaji au muujiza Yesu aliokuwa anaufanya ulikuwa ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Hapana, bali ponyaji nyingine aliziruhusu mahususi kwa lengo la kuwa ushuhuda kwa wengine, ili siku ile ya hukumu wasije wakasema hatukuona, au hatukusikia.

Tunasoma jambo kama  hilo katika..

Mathayo 8:1 “Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.

2 Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.

3 Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika.

4 Yesu akamwambia, Angalia, usimwambie mtu; ila enenda zako, ukajionyeshe kwa kuhani, ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa, IWE USHUHUDA KWAO”.

Ndicho kilichowakuta Makuhani, pamoja na mafarisayo na waandishi. Ni watu ambao walikuwa hawataki kusikia wala kuamini, Hivyo Bwana Yesu, alipowaponya baadhi ya watu hakuwaacha tu hivi hivi waende,kama alivyofanya sehemu nyingine, bali aliwaagiza waende kuwaeleza makuhani miujiza iliyowakuta,. Hivyo walikuwa wanapokea shuhuda nyingi sana kutoka kwa watu  mbalimbali walioponywa.. Pengine kwa siku  hata watu 100. Na kila walipoulizwa ni nani kawaponya wanasema YESU.

Hivyo hata sasa na sisi, tusifurahie tu miujiza ya Mungu anatuletea miujiza mingi, watu wanaponywa, wanafunguliwa, na huku maisha yetu yapo nje ya Kristo. tusifurahie kwasababu tujue ni hukumu tu tunajiandikia. Na ndio maana Bwana alisema maneno haya sehemu fulani;

Mathayo 11:21 “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.

22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.

23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.

24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.

Hivyo hiyo ndio iliyokuwa sababu kwanini aliwaambia wakajionyeshe kwa makuhani, kwasababu wao ndio waliokuwa hawamwamini wala kuziamini kazi zake.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

MIUJIZA YA KRISTO, HAITEGEMEI KANUNI ZA KIBINADAMU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda na sio kwenye koo nyingine kama vile  Yusufu?


JIBU: Hatma ya yale makabila 12, na tabia zao tunaona kwa mara ya kwanza zikifunuliwa na Yakobo Baba yao siku ile alipokuwa anakaribia kufa, alipowaita na kuwabariki. ukisoma pale utaona kila mtoto alinenewa habari zake. Kwasasa hatuwezi kuziandika zote hapa lakini kwa muda wako soma Mwanzo 49:1-28. Utaona.

Sasa,  kulingana na tabiri zile ni kabila moja  la Yuda, ndio lilibeba, vimelea vikuu sana, vimstahili Kristo.

Kwamfano pale makabila hayo yalipofananishwa na Wanyama, utaona Ni Yuda peke yake ndiye aliyefananishwa na SIMBA. Wakati wengine kama vile Naflati lilifananishwa na Ayala, Isakari  kama na Punda, Dani kama na nyoka aumaye, Benyamini kama mbwa-mwitu mkali. Yusufu kama mti mchanga uzaao. Lakini Yuda ni kama SIMBA .

Na sikuzote simba anajulikana kama ni mfalme wa pori, tena jasiri.

Mwanzo 49:8 “Yuda, ndugu zako watakusifu, Mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako. Wana wa baba yako watakuinamia.

9 Yuda ni mwana-simba, Kutoka katika mawindo, mwanangu, umepanda; Aliinama akajilaza kama simba, Na kama simba mke; ni nani atakaye mwamsha?

10 Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake, Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki, Ambaye mataifa watamtii.

11 Atafunga punda wake katika mzabibu, Na mwana-punda wake katika mzabibu mzuri. Amefua nguo zake kwa mvinyo, Na mavazi yake kwa damu ya zabibu.

12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa mvinyo, Na meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa”.

Vilevile kama tunavyosoma utabiri wake, utaona anaambiwa, FIMBO YA ENZI, haitaondoka kwake, ikimaanisha  kuwa fimbo ya kifalme, itakuwa katika uzao wake daima. Yaani kabila hili la Yuda litakuwa ni kabila la kifalme.

Mambo ambayo yanabeba kabisa tabia zote za masihi atakayekuja. Kwamba ni lazima AWE simba, jasiri, mwenye nguvu, na hodari.. Na ndio maana hatushangai kwanini  Bwana Yesu alijiita Simba wa Yuda (Ufunuo 5:5).

Vilevile ni lazima awe Mfalme mkuu sana mwenye nguvu sawasawa na unabii wa (Isaya 9:6). Hivyo kabila lenye enzi za kifalme lilikuwa ni hili na tunathibitisha hilo tangu enzi wa Daudi.

Hivyo hiyo ndio sababu kwanini Bwana Yesu hakutokea kabila lingine lolote Zaidi ya kabila la Yuda, Kwasababu, ilimpasa awe juu ya yote..Lakini kama angetokea kabila ya Yusufu ambalo limetajwa kama kabila lenye mafanikio makubwa, ni wazi kuwa kusingekuwa na vimelea vyovyote vya kifalme kwake.. Jambo ambalo haliwezekani kwa Kristo. Yeye ni lazima awe juu, atawale kama Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana. Hivyo ni lazima tabia hizo zianze kuonekana tokea mbali sana, kwenye vizazi vya vya nyuma, hadi kumfikia yeye.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Makanwa ni nini katika biblia? (Danieli 6:22)

FUNGUO WALIZOKUWA NAZO MABINTI WATANO WA SELOFEHADI!

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Rudi nyumbani

Print this post

UTAPENDA KUCHANGIA HUDUMA HII?

Tutamshukuru Mungu kwa ajili yako, kwa mchango wako, ili kuifanya injili hii isonge mbele Tuma sadaka yako kwa namba hizi:
Airtel:+255789001312 -Devis Magembe
Mpesa: +255767992434-Denis Magembe