Category Archive Uncategorized

LAKINI WAKATI WA TAABU WATASEMA, SIMAMA UKATUOKOE.

Ulishawahi kukutana na kundi la watu ambao linakutafuta tu wakati wa shida, kama ndio, kuna hali Fulani unajisikia ambayo sio nzuri, ni kweli wapo ambao mazingira yanawabana washindwe kukutafuta nyakati nyingine, lakini wapo ambao wewe kwao ni mtu wa kuwatatulia tu matatizo, Habari nyingine na wewe hawana..

Kuna mtu mmoja alikuwa ananifuata nimtatulie tu matatizo yake, lakini baada ya hapo ukimpigia hata simu umsalimie, hapokei, na anabadilisha line ya simu moja kwa moja ili usimpate, baadaye anakuja kukutafuta tena, na jambo linalofuata hapo ni kuomba msaaada..

Unajua hata kama utamsaidia, lakini utasema kwanini iwe hivi, kwanini tusiwe na mahusiano hata na nyakati nyingine zote..

Sasa hiyo hali ndiyo ambayo Mungu anapitia sasahivi kwa wanadamu wengi duniani, biblia inasema..

Yeremia 2:27 “waliambiao gogo la mti, Wewe u baba yangu; na kuliambia jiwe, Ndiwe uliyenizaa; kwa maana wamenipa mimi visogo, wala hawakunielekezea nyuso zao; LAKINI WAKATI WA TAABU WATASEMA, SIMAMA UKATUOKOE”.

Umeona, wanadamu wengi sasa kinachowapeleka kwa Mungu, si kingine Zaidi ya kuomba, wafunguliwe, kuomba waponywe, kuomba wafanikishwe kiuchumi, kuomba kazi, n.k.

Lakini ukiangalia mahusiano waliyonayo na Mungu ni hafifu sana au hakuna kabisa.. Hana muda wa kusoma biblia kuyajua mapenzi ya Mungu ni nini katika Maisha yake, kumaliza hata dakika 20 kila siku katika kutafakari Neno la Mungu hawezi, kuomba kunamshinda, kwenda ibadani ni mara moja kwa mwezi, ikizidi sana mara mbili, na hata akienda ni ili Mungu amjibu lile ombi lake alilomuomba lakini sio kumwabudu katika Roho na Kweli.

Anachokiona  kirahisi kwake, ni kwenda kununua maji ya upako na mafuta, ili amwage kwenye biashara zake, ili mambo yake yaende sawa.. Au pale anapopitia hali mbaya sana ya magonjwa ndipo anapomfuata Mungu ili amsaidie,. Hapo ndipo atafunga na kuomba, na kusoma Neno kila siku kwa bidii..Lakini siku nyingine zote anaishi maisha ya dhambi.

Ndugu, tujue kabisa Mungu hapendezwe na huo mfumo wetu wa Maisha, Mungu ametuzira watu wengi sana na sisi hatujui, ndio maana inakuwa ngumu sana kusaidiwa na Mungu kwasababu, Maisha yetu ni ya kinafki mbele zake.

Lakini ukiendelea kusoma pale Bwana anasema..

Yeremia 2:27 “waliambiao gogo la mti, Wewe u baba yangu; na kuliambia jiwe, Ndiwe uliyenizaa; kwa maana wamenipa mimi visogo, wala hawakunielekezea nyuso zao; lakini wakati wa taabu watasema, Simama ukatuokoe.

28 LAKINI WAKO WAPI MIUNGU YAKO ULIOIFANYA? Na wasimame hao, kama wakiweza kukuokoa wakati wa taabu yako; kwa maana hesabu ya miungu yako ni sawasawa na hesabu ya miji yako, Ee Yuda.

29 MBONA MNATAKA KUTETA NAMI? Ninyi nyote mmeniasi, asema Bwana”.

Umeona tusimgeuze Mungu kama ni sehemu ya kutatulia matatizo yetu tu, ili hali Maisha yetu hayaendani na wokovu. Tusitete na Mungu, Mambo hayo kayafanye kwa waganga wa kienyeji lakini usifanye kwa Mungu, kwasababu utajikuta unaangukia tu laana badala ya baraka.

Hivyo tuanze sasa, kumtafuta Mungu nyakati zote, tuhakikishe tunayatenda mapenzi yake, tuonyeshe bidii zetu kwake, kwamba tunampenda sio kiunafiki, bali kwa mioyo yetu kweli. Tunamtafuta sio atufanye kuwa mabilionea, bali atufanye kuwa wana wake kama Yesu Kristo. Na ndio sasa hata hayo mengine atasaidia bila hata kutumia nguvu wala kumwomba..

Kumbuka katika nyakati hizi za mwisho, watakaokwenda kwenye UNYAKUO, sio kila mtu asemaye ninamwamini Mungu tu, halafu basi,..Bali ni watu wayatendao mapenzi ya Mungu kikamilifu sawasawa na Neno la Kristo.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Bwana atupe jicho la kuona, na kuyatendea kazi.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

USIJARIBU KUMGEUZA MUNGU MGANGA WA KIENYEJI,UTAKUFA.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

WAKATI ULIOKUBALIKA NALIKUSIKIA

JINSI UNAJISI UNAVYOMGHARIMU MTU.

Rudi nyumbani

Print this post

Maana vitu vyote ni watumishi wako(Zaburi 119:91)

SWALI: Biblia inamaana gani kusema “ maana vitu vyote ni watumishi wako”?. Je wanaotumia vifaa vya upako kama vile chumvi, maji, udongo, kuombea watu, wanatimiza kusudi lile lile la Mungu kwasababu na vyenyewe vinafanya kazi ya Mungu kwa nafasi hiyo? Je kwa mujibu wa andiko hilo ni sawa?

Zaburi 119:90 “Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, Umeiweka nchi, nayo inakaa.

91 Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, MAANA VITU VYOTE NI WATUMISHI WAKO”.


JIBU: Ni kweli kama andiko hilo linavyosema, vitu vyote tunavyoviona katika mbingu na  katika nchi ni watumishi wa Mungu, yaani, jua, mwezi, nyota, mawingu, milima, moto, maji, upepo, mafuta, udongo, mende, mbu, nzi, konokono, kipepeo vyote vinamtumikia Mungu.

Lakini swali ambalo tunapaswa tujiulize je vinamtumkia Mungu katika utumishi gani?

Ulishawahi kwenda kumuomba mjusi akusaidie kuomba rehema mbele za Mungu? Ulishawahi kuliomba jua likupe rizki, ulishawahi kuamka asubuhi na kuuambia mwezi ukuponye magonjwa yako, na ukuepushe na ajali?

Kwanini usifanye hivyo, ilihali vyote vinamtumikia Mungu?.. Lazima ufahamu utumishi wao ni upi mbele za Mungu, kwamfano, biblia inasema..

Zaburi 19:1 “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake”.

Ikiwa na maana kuwa tutazamapo mbingu na anga, basi tunahubiriwa utukufu wa Mungu kwa kupitia hivyo,  hapo tayari vimeshamtumikia Mungu, lakini hatuwezi kwenda kutumia mawingu ili Bwana atujibu maombi yetu.

Mungu kaweka njia kwa kila jambo, Na njia pekee ambayo alituchagulia sisi ili tumfikie Mungu, na kupokea wokovu wetu, na baraka zetu ni kwa kupitia YESU KRISTO tu na JINA LAKE Hapo ndipo tunapoweza kusaidiwa  mahitaji yetu, na dua zetu. Kwasababu hatuna jina lingine au kitu kingine chochote kiwezacho kutuokoa sisi isipokuwa Jina lake tu. . (Matendo 4:12)

Sasa wapo watu wanasema, mbona, Yesu alitumia udongo, mbona manabii walitumia chumvi,..Wanashindwa kuelewa yapo MAINGILIO YA MUNGU. Ambapo  Mungu mwenyewe upo wakati anashuka mahali Fulani kwa muda , kulitimiza kusudi lake Fulani, ndipo anapotumia chochote apendacho, kisha baada ya hapo hakuna kitu kingine cha ziada katika hicho kitu.

Ndio maana utaona wakati  ule alipomtumia punda kuzungumza na Balaamu, hatuona tena, punda wakitumika kuzungumza na watu, kana kwamba ndio kanuni, halikadhalika, Elisha alipoambiwa alale juu ya yule kijana kisha atakuwa mzima, hatuona tena, tendo hilo likifanyika hadi leo hii, tukilala juu ya wagonjwa ili  wapate afya.

Ipo hatari kubwa sana ya kutumia vitu vya Mungu na kuvigeuza kuwa  ndio kanuni za uponyaji, kosa mojawapo lililowafanya wana wa Israeli Mungu achukizwe nao, hadi kupelekwa tena utumwani Babeli, lilikuwa ni kuitumia ile sanamu ya shaba, Musa aliyoagizwa na Mungu aitengeneze kule nyikani, watu waiangaliapo wapone.

Hivyo watu wasiomjua Mungu, na MAINGILIO YAKE YA MUDA, wakaigeuza kuwa ndio sehemu ya ibada, walipofika nchi ya ahadi wakaiundia madhabahu kisha wakaanza kumwomba Mungu kupitia ile, mwisho wa siku wakawa wanaabudu mapepo pasipo wao kujijua na matokeo yake wakapelekwa Babeli utumwani.

Hivyo nawe pia ukiona mahali popote uendapo, vitu kama hivyo vimefanywa kama kanuni, kila wiki ni maji ya upako, mafuta, chumvi, au kingine chochote, ujue kuwa huna tofauti na wale waabudu sanamu, na jua na mwezi, na unayemwabudu hapo sio Mungu bali ni shetani mwenyewe. Na Unamkasirisha Bwana sana.

Jina ambalo tumepewa sisi, tulitegemee kwa kila kitu, na kila saa ni jina la YESU KRISTO TU.. Hilo ndio uligeuze kuwa sanamu yako, na si kitu kingine chochote. Kama ulikuwa unafanya hivyo basi acha mara moja.

Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Hivyo, kwa hitimisho ni kuwa, mstari huo  haumaanishi  maji, au chumvi, au udongo, au kitu kingine chochote kinaweza kufanya shughuli ya upatanisho wa mwanadamu. Hapana ni uongo.  Vinamtumikia Mungu, lakini sio katika mambo ya wokovu wetu.

Bwana atuepushe na sanamu.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NEHUSHTANI (NYOKA WA SHABA).

USIJARIBU KUMGEUZA MUNGU MGANGA WA KIENYEJI,UTAKUFA.

KWA KUWA WASEMA MIMI NI TAJIRI.

Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”

Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani,

Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?

Unyenyekevu ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

Jina la mwokozi wetu Yesu Kristo lihimidiwe milele. Karibu tuyatafakari maandiko. Na leo tutaona ofisi kuu tatu za shetani, ambazo, zinafanya kazi humu duniani.

Biblia inasema..

Ufunuo 16:13 “Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.

14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi”.

Hapa, tunaona watatu wanatajwa, ambao ni;

  1. Joka
  2. Mnyama
  3. Nabii wa uongo

Haya ni mapepo makuu matatu ya juu sana na yanayofanya kazi kwa kushirikiana, na kichwa chao akiwa ni ibilisi mwenyewe. Muunganiko huu ndio unaoukamilisha utawala mchafu wa mashetani unaofanya kazi duniani.

Sasa Ofisi ambayo, inafanya kazi sasa kwa nguvu ni hiyo ya JOKA, lakini hizo nyingine mbili zilizosalia yaani ya Mnyama na Nabii wa Uongo, kwasasa zinafanya kazi katika siri, lakini zitakuja kufanya kazi vema, katika kipindi cha dhiki, baada ya unyakuo kupita. Kipindi hicho ndio zitawepa mamlaka kamili ya kujidhihirisha duniani.

Sasa tuone kazi za hizi roho tatu ni zipi;

  1. Tukianzana na huyo wa kwanza yaani Joka.

Kama tunavyofahamu kazi kuu ya JOKA ni kumeza: Biblia inapomtaja joka (shetani), inalenga moja kwa moja katika kummeza Kristo mahali popote anapozaliwa,

soma Ufunuo 12:3-5

“3 Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.

4 Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.

5 Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi”.

Na ndio maana utaona pindi Kristo anazaliwa duniani, Joka hili lilisimama ndani ya Herode, kutaka kumuua, lakini lilishindwa..Hivyo mahali popote Kristo anapozaliwa, ni lazima joka ajitokeze kuleta vita, hata sasa mtu anapotaka kuokoka kwa kumaanisha kweli kumfuata Kristo, ajue kuwa ni lazima atakutana na vita vya hili joka, kwasababu sikuzote halitaki kumwona Kristo katika mioyo ya watu.

Na ndio mwishoni biblia inasema, likaenda kusimama katika mchanga wa bahari, yaani mahali ambapo, nchi kavu na Habari vinakutana, fukwe (beach), Yaani ikifunua kuwa lipo mpakani, kuwazuia watu wanataoka kutoka katika giza kuja katika nuru, hapo ndipo vita ilipo.. Kwa maelezo marefu juu ya hili fungua link hii usome >>>> NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.

Ufunuo 12:17 “Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”.

Hivyo, fahamu kuwa ukitaka kuwa mtakatifu, basi ujue pia joka litasimama kukupinga vikali. Lakini halitaweza kukushinda, ikiwa umedhamiria kweli kumfuata Kristo. Lakini ukiwa nusu nusu, yaani unataka hutaki, litameza Kristo wako, na hutazalisha chochote katika wokovu wako.

          2.  Mnyama.

Biblia inapotaja mnyama, inazungumzia utawala ya ibilisi kupitia falme kubwa za dunia. Alishatumia falme za dunia kadha wa kadha huko nyuma, kama vile Babeli, Umedi, Uyunani na Rumi, kuangusha watakatifu wa Mungu. Na utaunyanyua tena ufalme mwingine ambao utakuwa na nguvu sana, ufalme huu kichwa chake kitakuwa ni RUMI,  na utafanya kazi kwa kipindi kifupi sana yaani miaka pungufu ya saba (7), lakini utaleta, mabadiliko makubwa sana duniani, kiasi kwamba kila mtu atalazimishwa aufuate huo utawala.

Usipoufuata, hutaweza kuuza wala kununua, wala kuajiriwa. Biblia inasema utawala huo wa kishetani ambao utakuwa na chapa ya 666 nyuma yake, utafurahiwa na watu wote watatakaokuwa wamesalia, ambao majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha mwana-kondoo kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu. Lakini wale wote watakaoonyesha dalili ya kuukataa au kuupinga, mwisho wao utakuwa ni kifo cha mateso makali sana ya dhiki.

Ufunuo 13:8 “Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia”.

Jambo ambalo wengi wetu hatulijui ni kuwa, utawala huu tayari ulishafanya kazi huko nyuma,ambao ni ni Rumi, na ulishawaua watakatifu wengi sana Zaidi ya milioni 80, Lakini sasa Mungu ameuzuia kwa muda, lakini ndio utakaokuja kuzuka tena na kuyaongoza mataifa yote, katika utawala mpya, moyo wa utawala huo ni Vatican, Rumi, utakuwa na nguvu nyingi Zaidi ya ule wa kwanza, kwasababu utakuwa na sapoti ya mataifa yote makubwa unayoyajua leo hii duniani.

Ufunuo 17:8 “Yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu. Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ya kwamba alikuwako, naye hayuko, naye atakuwako”.

   3.   Nabii wa Uongo.

Kama jina lake lilivyo, ni nabii, kazi yake ni kuwapotosha watu, kwa kuwapa maagizo ya uongo, wadhani kuwa wanapokea maagizo kutoka kwa Mungu kumbe ni kwa ibilisi. Biblia inasema hata sasa wapo manabii wa uongo, ambao wanaiga kazi ya mkuu wao, atakayekuja. Nabii huyu ndiye mpinga-kristo mwenyewe.

1Yohana 2:18 “Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho”.

Mpinga-Kristo huyu ambaye atakuja rasmi mara baada ya unyakuo wa kanisa kupita, atapewa uwezo wa kufanya ishara za uongo na shetani mwenyewe,atapewa uwezo wa kutenda miujiza feki kama ile ya Yane na Yambre kipindi cha Musa.

2Wathesalonike 2:6 “Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.

7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.

8 Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;

9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo”;

Na kazi yake kubwa itakuwa ni kuwashurutisha watu, waipokee ile chapa ya mnyama, na wengi watamuamini sana na kuipokea kwasababu ya zile ishara atakazokuwa anazifanya duniani.

Ufunuo 13:12 “Naye atumia uwezo wote wa mnyama yule wa kwanza mbele yake. Naye aifanya dunia na wote wakaao ndani yake wamsujudie mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.

13 Naye afanya ishara kubwa, hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu.

14 Naye awakosesha wale wakaao juu ya nchi, kwa ishara zile alizopewa kuzifanya mbele ya huyo mnyama, akiwaambia wakaao juu ya nchi kumfanyia sanamu yule mnyama, aliyekuwa na jeraha la upanga naye akaishi.

15 Akapewa kutia pumzi katika ile sanamu ya mnyama, hata ile sanamu ya mnyama inene, na kuwafanya hao wote wasioisujudu sanamu ya mnyama wauawe.

16 Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao;

17 tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.

18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.

Na mwisho kabisa, roho hizi zote tatu, yaani ya joka, mnyama na nabii wa uongo, zitaungana, na kuwaendelea wafalme wote wa duniani, ikiwemo wa hilo taifa lako unaloishi,  ili wapatane kwa kitu kimoja, kupigana na Mungu mwenyezi, pale Israeli, katika vita ile ya Harmagedoni, kipindi hicho ndicho Kristo atahitimisha vyote kwa kuwaua wanadamu wengi sana, na kuanzisha utawala wake mpya wa amani wa miaka elfu moja hapa duniani, naye atatawala kama MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA. Haleluya.

Hivyo ndugu, fahamu kuwa hizi ni nyakati za mwisho, kipindi kifupi sana tumebakiwa nacho,  Unyakuo ni siku yoyote, dalili zote zimeshatimia, mfumo wa yule mnyama upo tayari, unatendakazi tu kwa siri kwa dini ya uongo ya rumi, ni wakati wowote kunyanyuka, Tubu dhambi zako mgeukie Bwana Yesu kwa kumaanisha. Kubali kujitwika msalaba wako umfuate, kwasababu parapanda italia siku yoyote.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

UFUNUO: Mlango wa 12

UFUNUO: Mlango wa 13

UFUNUO: Mlango wa 17

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

DANIELI: Mlango wa 1

NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”

Moja ya maagizo ambayo Bwana Yesu aliwapa wanafunzi wake alipowatuma kwenda kuhubiri injili mbali, lilikuwa ni kutokulipisha fedha katika huduma yoyote watakayoitoa, halikadhalika   kutokubeba chochote katika safari yao. Yaani wasiwe na maandalizi yoyote ya njiani, Lakini mwishoni kabisa mwa maagizo yake aliyasema maneno haya “maana mtenda kazi astahili posho lake”.. Sasa swali linakuja Je hili posho ni lipi alilostahili huyu mtandakazi ili hali ameitwa atoe bure?

Mathayo 10:8 “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.

9 Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;

10 wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, wala fimbo; maana mtenda kazi astahili posho lake”.

JIBU: Posho alilostahili ni lile ambalo Bwana Yesu mwenyewe atampa katika kazi ya injili anayoipeleka, kwa kupitia watu wakarimu ambao Bwana Yesu mwenyewe atawagusa moyo huko waendako aidha kwa kuwapa maji, au chakula, au nguo, na wakati mwingine hata fedha.

Hiyo yote ni kuonyesha kuwa Bwana Yesu anaweza kumtunza mtumwa wake, katika mazingira yoyote atakayomtuma. Na ndio maana mwishoni kabisa akawaambia maneno haya;

Luka 22:35 “Akawauliza, Je! Hapo nilipowatuma hamna mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu? Wakasema, La!

Ni ni kufunua kuwa hatupaswi kuwa na wasiwasi wa maandilizi yoyote ya huduma ya Kristo, pale ambapo hatuna chochote,  Bwana anataka tuwe wepesi (SIMPLE), tusijali sana tutakula nini, tutavaa nini huko tuendako, kesho tutatolea wapi nauli ya kurudi, hilo jambo Bwana hataki sisi kama watumwa wake tulifikirie, kwasababu ameahidi kabisa ikiwa tunatenda kazi yake kiuaminifu, basi tumestahili posho lake, hivyo anza kutumika.

Lakini haimaanishi kuwa, wakati wote, hata kama unacho, ndio ujifanye hauna, hapana, bali, upo wakati wewe kama mtumishi wa Mungu utabarikiwa na utakuwa na vya kuendea huko katika ziara, hivyo vitumie hivyo, Na ndio maana wakati mwingine Bwana aliwaambia wajibebe fimbo ya njiani, na kujifungia viatu, wakati sehemu nyingine kama tuliyosoma hapo juu aliwakataza.(Marko 6:8-9)

Kwahiyo, kwa vyovyote vile, Bwana atatunza, ilimradi tunamtumkia yeye kwa uaminifu. Tusiwe na wasiwasi na huduma yake, Haleluya..

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

ANGALIENI MWITO WENU.

WITO WA MUNGU HAUVUKI NENO LAKE.

MAAGIZO AMBAYO HAYAJAAGIZWA!

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Rudi nyumbani

Print this post

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Yapo maombi ya namna tofauti tofauti, lakini yote  ni lazima yaangukie katika mojawapo ya makundi haya Matano (5).

1)   Kusifu na Kuabudu.

Wengi hawafahamu kama sifa zetu ni maombi yanayojitegemea kwa Mungu, haya ni maombi yanayomwasilia Mungu katika mfumo wa nyimbo, halikadhalika pia kwa kumwadhimisha kwa matendo yake makuu aliyoyafanya kwa kuzungumza kwa vinywa vyetu.. ndio maombi ya kwanza yenye nguvu. Tunapomsifu Mungu katika Roho na kweli, ni Zaidi ya maombi mengine yote tunayoweza kuyapeleka kwake.,

Biblia inasema Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu;(1Nyakati 16:29), Na pia Mataifa yote yamsifu yeye. Mambo mengi, na vifungo vingi huwa vinafunguka, pale tu tunapomsifu Mungu kwa kumaanisha katika Roho na kweli, Kwasababu ni maombi yanayouvuta uwepo wa Mungu kwa haraka sana juu ya mtu, Na ndio maana ibada zote lazima zitanguliwe na maombi haya.

2) Maombi ya Upatanisho.

Ni maombi ya kuwaombea wengine, Zaidi ya kwako mwenyewe. Kuwaombea watakatifu,  kuwaombea, wanyonge, kuliombea taifa, viongozi, hata maadui zako n.k. Haya ni maombi ambayo yanampendeza Mungu sana. Danieli alifunga na kuomba kwa ajili ya taifa lake Israeli, na dhambi zao, Na Mungu akamsikia akamrehemu (Danieli 9:1-27).

 Bwana Yesu alipokuwa duniani, sehemu kubwa ya maombi yake ilikuwa ni kutuombea sisi (Yohana 17) hivyo akasema pia, tuombeane sisi kwa sisi ili tupate kuponywa (Yakobo 5:16). Ikiwa na maana wengi hawawezi kuokoka/kufunguliwa wenyewe, ikiwa sisi hatutawaombea, Na pale maombi haya yanapokuwa ya muda mrefu (ya dua), basi huwa yana nguvu Zaidi, kupelekea kutupa kibali cha kupendwa na Mungu, kama ilikuwa kwa Danieli.

3) Maombi ya Mahitaji.

Ni maombi ya kupeleka haja zetu kwa Mungu, ikiwemo, kumwomba Roho wake, rizki, amani, furaha,  uponyaji, kibali, fursa, gari n.k. Bwana Yesu alisema pia, tuombapo tuombe Bwana atupe rizki zetu,(Mathayo 6:11). Na pia alisema tuombe nasi tutapewa. Haya ndio maombi yanayojulikana na kuombwa na watu wengi sana.

Luka 11:11 “Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka?

12 Au akimwomba yai, atampa nge?

13 Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”

4) Maombi ya Shukrani.

Ni maombi muhimu kwa kila mwanadamu, ni maombi ya wakati wote, ya asubuhi, ya mchana, na jioni, tunamshukuru Mungu, kwa uhai, afya, chakula, makazi, Malazi, familia,

Wakolosai 3:15 inasema “….tena iweni watu wa shukrani.”. Ulishawahi kushukuriwa kwa wema Fulani uliomtendea mtu, ukaona hali unayojisikia ndani ya moyo wako kwa shukrani ile..Ndivyo ilivyo kwa Mungu anapoona Sio kila majira tunaenda kumpelekea tu mahitaji yetu..Bali wakati mwingine tunamkaribia kumshukuru kwa vile anavyotufanyia. Inampendeza sana moyo. Na wakati mwingine kupelekea hata kupewa vile vilivyosalia, kwasababu tunaonyesha kuthamini neema yake.

5) Maombi ya Vita.

Ni maombi ya kushindana, na nguvu za giza, kwa mamlaka ya rohoni tuliyopewa katika damu ya Yesu, Hapa tunatangaza ushindi, na pia kutamka kwa Imani katika Neno la Mungu. Yapo mambo mengine ibilisi hawezi kuyaachia kirahisi rahisi. Hivyo inahitaji kukemea, kuamuru, kuvunja, na kubomoa, kwa Imani.

Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.

11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.

Hivyo kama watakatifu tukijifunza kutumia aina hizi tano za maombi, bila kupuuzia hata moja, basi, tutakuwa ni askari wazuri sana katika roho.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA

LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA.

Matulizo ya mapenzi ni nini? (Wafilipi 2:1)

Rudi nyumbani

Print this post

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo, utukufu na heshima vina yeye milele na milele.AMEN. Nakukaribisha katika kuyatafakari maneno ya Mungu, na leo tutaona vile uaminifu unavyomshawishi Mungu, kukupa neema Zaidi ya unachokiomba.

Tumekuwa na maombi mengi sana mbele za Mungu, wakati mwingine tunatamani Mungu atutumie kama Fulani katika biblia, Lakini tusipojua kanuni za Ki-Mungu, kamwe hatutakaa tuvipate, haijalishi tutakuwa ni waombaji au wafungaji wazuri namna gani mbele za Mungu.

Mungu kumfanya Musa, kuwa Mchungaji wa taifa la Israeli, haikuwa ni kwasababu ni mwisraeli tu au anaomba sana. Hapana, ni kwasababu ya maamuzi aliyoyafanya zamani, ambayo yalimponza hata kuwa vile kama alivyokuwa kwa miaka 40. Musa aliona kustarehe katika jumba la kifalme, si kitu, moyo wake ukaanza kuugua juu ya ndugu zake waebrania aliokuwa anaona wanateswa, hivyo siku moja alipoona mmojawapo anaonewa na Mmisri, alikuwa radhi kumtetea ndugu yake, mpaka kumuua yule mmisri, kuonyesha kuwa aliwapenda waebrania kwelikweli, Hata siku ya pili yake, alipoona hao hao waebrania wanagombana, hakuwaacha hivi hivi tu, bali alikwenda kutafuta namna ya kuwapatanisha ili wawe na umoja.  Lakini yule aliyemtapeli mwenzake, akamwambia unataka kuniua kama ulivyomuua yule mmisri jana.

Musa angeweza kukana hayo mashtaka hata kwa rushwa kwasababu alikuwa na uwezo huo.. Lakini kinyume chake, akawa tayari, kukubali mashutumu, kwamba yeye ndiye aliyefanya vile, akakimbia akaenda zake jangwani, huku moyo wake ukiugua tu kwa ajili ya ndugu zake. Utaona japokuwa hakujua njia sahihi ya kuwaokoa ndugu zake, lakini alijitahidi kwa kadiri ya uwezo wake, kufanya awezacho.(Matendo 7:22-40)

Huyo ndio mtu ambaye baada ya miaka 40, Mungu anamtokea katika kijiti cha moto, akimwambia, nakutuma uenda Misri ukawaokoe watu wangu kwa mkono mkuu. Ndipo Mungu akamtumia kwa uwezo mkubwa namna ile, kwasababu aliona uaminifu wake, katika kile alichokitamani.

Matendo 7:35 “Musa huyo waliyemkataa, wakisema, Ni nani aliyekuweka kuwa mkuu na mwamuzi? Ndiye aliyetumwa na Mungu kuwa mkuu na mkombozi, kwa mkono wa yule malaika aliyemtokea katika kile kijiti.

36 Huyo ndiye aliyewatoa, akifanya ajabu na ishara katika nchi ya Misri, na katika bahari ya Shamu, na katika jangwa muda wa miaka arobaini”.

Ukitamani kuwa mchungaji, onyesha tabia hizo tangu sasa kabla hujawa mchungaji wa kanisa la Kristo, ili Bwana ashawishwe, kukupa huduma hiyo, je, unalipenda kundi la Mungu, je unalithamini? , je upo tayari kuwalisha watu chakula cha kiroho, na kusimama nao katika shida zao, bila kuruhusu ibilisi awameze?

Hilo ni jambo la muhimu sana, kulifanya sasa ndugu..

Daudi kabla hajafanywa na Mungu kuwa mchungaji wa Israeli, aliwahi kuwa mchungaji wa kondoo na mbuzi, lakini alipoona adui wanataka kuja kulishambulia kundi, hakuliacha na kukimbia, bali aliweza kupambana na simba, Pamoja na dubu na kuwashinda, akiwa na fimbo tu.  Mungu akamuona kuwa huyu anafaa hata kwa watu wangu Israeli kwasababu anathamini, kundi analoliongoza, hata kuwa tayari kuyahatarisha Maisha yake, kwa ajili ya hili..(1Samweli 17:34-36)

Umeona, Bwana Yesu alisema..

Luka 16:10 “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia”.

Je ni sisi tuitwao wachungaji/Waalimu, wainjilisti,  tunazo tabia hizi?

Wapo watu wengine wanasema, Bwana naomba unipe mali nyingi kama Sulemani, ili nizitumie kuisogeza injili yako mbele. Kumbuka, kabla Mungu hajakupa, atahitaji kwanza, aone ulichonacho unakitoaje? Umebarikiwa laki moja, Je!, ulishawahi kuwa radhi kutoa vyote, au sehemu kubwa ya mali zako kwa Mungu mara nyingi, hata kuwa tayari kulala njaa,  au kukosa mahitaji yako, kwa Mungu?

Ikiwa hivyo hufanyi, unaishia tu kuomba, jua kuwa utajiri huo unaouhitaji, kamwe hutaweza kuupata.

Mtume Paulo, alilijua hilo, ndio maana akawa mwaminifu sana katika kumtumikia Mungu, katika udogo, ndipo Mungu akamfanya kuwa mtume na Mwalimu wa mataifa.

1Timotheo 1:12 “Nami namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu kwa sababu aliniona kuwa mwaminifu, akaniweka katika utumishi wake;”

Hivyo ndugu, chochote, ukitamanicho kwa Mungu, waweza kukupata, lakini, anza sasa, kujitoa kwa hicho, kuwa tayari kuiponza roho yako, hata wakati mwingine kupoteza kila kitu, kwa ajili ya utumishi huo, na hakika yake utakipata kwa Mungu.

Uaminifu wako sasa ni mtaji wa ukitakacho kesho.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?

THAWABU YA UAMINIFU.

Gongo na Fimbo ni nini?

Unyenyekevu ni nini?

NIFANYE NINI ILI NIPENDWE NA MUNGU?

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya huu mstari,

Mithali 16:2 “Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe; Bali Bwana huzipima roho za watu”.


JIBU: Kama vile Biblia inavyosema moyo huwa mdanganyifu kuliko kitu kingine chochote, (Yeremia 17:9), ikiwa na maana ni kawaida ya mwanadamu, kuziona njia zake zote alizozichagua ni sawa mbele zake, ni mara chache sana, kusikia mtu anakiri kuwa uamuzi anaoufanya ni wa kishetani,

Nimekutana na waganga wa kienyeji wanasema kitu tunachokifanya ni sawa, hakina madhara yoyote, ukienda kwa waabudu sanamu, watakuambia vivyo hivyo hizi ni ishara tu, tunaabudu Mungu yuleyule, Ukienda kwa wauza pombe watakuambia nao maneno hayo hayo  n.k… Kwasababu biblia inasema njia “ZOTE” (sio moja) za mtu ni safi machoni pake mwenyewe.

Lakini Bwana huzipima roho za watu. Ikiwa na maana, Mungu anazichunguza nia zetu. Yeye hashawishwi na kile tunachokiona ni sawa, kwa macho yetu, au kwa mitazamo yetu, bali anatazama ndani Zaidi ya mwanadamu, anaweka kwenye mizani, anatazama nia, ya mtu ilikuwa  ni nini, na matokeo yake yatakuwa ni nini mwishoni..

Kwamfano Mafarisayo na Masadukayo, walijihesabia haki, kwa mapokeo yao, wakijiona kuwa ni watakatifu, na bora kuliko wengine, lakini Bwana Yesu aliwaita wanafki. Kwasababu, kazi yao ilikuwa ni kusafisha kikombe kwa nje tu, lakini ndani ni kuchafu, wanafunga ili waonekane na watu, wanaomba ili waonekane ni wazuri katika mambo hayo. Walikuwa wanajifanya kumwita Yesu Rabi, lakini ndani wamejaa wivu. (Mathayo 23:1-39)

Hivyo nasi twapasa tulijue hilo, ili tusidanganyike.

Kitabu cha 1Wakorintho 13, inasema nijaposema kwa lugha za wanadamu na Malaika, nijapoutoa mwili wangu uungue moto, nijapotoa mali zangu zote niwape maskini, nijapokuwa na unabii, na Imani timilifu ya kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo mimi si kitu, ni sawa na bure tu.

Waweza kuwa mhubiri mzuri, mkubwa, unaokoa roho za watu, nawe ukaona njia hiyo ndiyo inayompendeza Mungu zaidi, lakini ndani yako unahubiri kwasababu ya fitina, kama inavyosema Wafilipi 1:15, au upate umaarufu, au upate fedha,.ujue unachokifanya ni bure.

Hivyo, katika lolote tulifanyalo, ili liwe na faida njema nyuma yake, lazima tujue nia yetu ya dhati kufanya hivyo ni nini, Ndicho Bwana anachokitazama sana, kuliko, hichi cha nje tukionyeshacho.

Kulikuwapo na wale watu, waliokataa, kwenda harusini walipoalikwa, na ukitazama kibinadamu sababu za wao kutokwenda zina mashiko kabisa, mwingine anasema ninaoa, hivyo ni sharti niwe na mke wangu kwa kipindi hiki, lakini Bwana Yesu aliona kama ni UDHURU wanatoa wote, kwasababu yeye ndio anayechunguza mioyo, akaona kutoa kwao udhuru ni kwasababu hawakuthamini wito wake tangu mwanzo.

Luka 14:16 “Akamwambia, Mtu mmoja alifanya karamu kubwa akaalika watu wengi,

17 akamtuma mtumwa wake saa ya chakula awaambie wale walioalikwa, Njoni, kwa kuwa vitu vyote vimekwisha kuwekwa tayari.

18 Wakaanza wote kutoa udhuru kwa nia moja. Wa kwanza alimwambia, Nimenunua shamba, sharti niende nikalitazame; tafadhali unisamehe.

19 Mwingine akasema, Nimenunua ng’ombe jozi tano, ninakwenda kuwajaribu; tafadhali unisamehe.

20 Mwingine akasema, Nimeoa mke, na kwa sababu hiyo siwezi kuja.

21 Yule mtumwa akaenda, akampa bwana wake habari ya mambo hayo. Basi, yule mwenye nyumba akakasirika, akamwambia mtumwa wake, Toka upesi, uende katika njia kuu na vichochoro vya mji, ukawalete hapa maskini, na vilema, na vipofu, na viwete.

22 Mtumwa akasema, Bwana, hayo uliyoagiza yamekwisha tendeka, na hata sasa ingaliko nafasi.

23 Bwana akamwambia mtumwa, Toka nje uende barabarani na mipakani, ukawashurutishe kuingia ndani, nyumba yangu ipate kujaa.

24 Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”.

Hivyo na sisi tusitoe udhuru katika mambo ya ki-Mungu, unapoitwa uokoke, hata kama unazo sababu elfu za kutokuacha hicho unachokifanya ikiwa Mungu anataka ukiache, tii tu. Kwasababu hatuwezi kumshawishi Mungu kwa mitazamo yetu tu, kwa vile tuonavyo sisi kuwa ni bora, au vafaa Zaidi kwasasa, naye akashawishika, bali anaelewa kila kitu, na matokeo ya vyote mwishoni utakuwaje..

Hatuna budi, kumtii Mungu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

KUWA MWAMINIFU KWA MANENO YAKO MWENYEWE,

AKETIYE MAHALI PA SIRI PAKE ALIYE JUU.

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

VIACHENI VYOTE VIKUE HATA WAKATI WA MAVUNO.

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

Rudi nyumbani

Print this post

LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA.

Biblia inasema..

1 Wakorintho 2:10-12

[10]Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.

[11]Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.

[12]LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA, BALI ROHO ATOKAYE KWA MUNGU,makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.

Zipo Roho mbili tu huku duniani.

Roho wa Mungu, na roho ya dunia. Kama mtu usipoipokea Roho ya Mungu, basi utaipokea roho ya dunia.

Hakuna mwanadamu anayejiongoza yeye mwenyewe  hapa duniani kwa roho yake tu. Hilo halipo.

Sasa kama jinsi hayo maandiko yanavyotuambia Roho wa Mungu huchunguza yote hata mafumbo ya Mungu.. Maana yake ni kuwa  yeye ndiye anayetufunulia siri za ufalme wa mbinguni, pamoja mambo ambayo Mungu anataka sisi tuyafanye tukiwa hapa duniani..ukisoma Yohana 16:13 inasema

[13]Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Umeona hiyo ndio kazi ya Roho wa Mungu..ndio maana mtu aliyepokea kweli Roho Mtakatifu hawezi ishi kidunia kwasababu ni roho nyingine kutoka mbinguni kwa baba ipo yake ikimfundisha kuishi kulingana na misingi ya Mungu.

Lakini kinyume chake ni kweli. Watu wote ambao hawana Roho wa Mungu, wanayo roho ya dunia

Na yenyewe inachunguza mambo ya ulimwengu huu na kuwafundisha watu kuishi kiulimwengu. Ndio maana hushangai kuona tabia nyingi mbaya kila siku zikivumbiliwa lengo tu ni kuwafanya kuwa wakidunia.

Ukiona mwanamke unapenda fashion, vimini, kujichubua, unavaa suruali, unaweka mak-eups, kijana unavaa milegezo, unanyoa viduku, unakunywa pombe, unacheza kamari, unasikiliza nyimbo za kidunia,  unakwenda disco, unafanya ushirikina, unazini, unakula rushwa, unaiba, unapenda fedha, unadanganya ni uthibitisho kuwa roho ya dunia imekuvaa ndio maana inakuhimiza na kukufundisha kufanya hayo mambo kwa bidii.

Na mwenye roho hii ni shetani mwenyewe..Na kama ikitokea  Bwana Yesu amerudi leo..basi ujue utabaki hapa duniani. Kwasababu roho yako ni ya hapa hapa na ka  ikitokea umekufa basi utaenda moja kwa moja kuzimu kwasababu huko ndiko hatma ya roho hiyo itakapoishia..

Biblia ipo wazi kabisa inasema..

Warumi 8:9

[9]Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. LAKINI MTU AWAYE YOTE ASIPOKUWA NA ROHO WA KRISTO, HUYO SI WAKE.

Ukikosa Roho wa Mungu, mbinguni huendi. Huu si wakati wa kumvumilia zaidi shetani, au kuwa rafiki wa dunia. Tunapojichanganya na mambo yake ndipo tunapovaliwa na roho hii chafu. Jiponye nafsi yako, ndugu, hizi ni siku za mwisho.

1 Yohana 2:15

[15]Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

Hivyo ndugu, njia pekee ya kuipokea Roho ya Mungu ambayo itakusaidia na kukufundisha kuishi  maisha yanayompendeza Mungu. Ni kutubu kwa kumaanisha kabisa kugeuka na kuuacha ulimwengu..kisha ukishafanya hivyo unakuwa tayari kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ikiwa kama haukubatizwa hapo mwanzo.

Baada ya huo wakati ni kuanza kuonyesha bidii ya kujifunza biblia, kuomba, kuzingatia fellowship zitakazokusaidia kukua kiroho. Na Roho wa Mungu akishaona umemaanisha hivyo, atashuka juu yako na kukutia Muhuri, na kukusaidia kuishi maisha ya wokovu.

Huku ukingojea siku yako ifike uende mbinguni, Roho hiyo ilipo.

Ikiwa utahitaji msaada ya kupokea wokovu, àu ubatizo sahihi.Basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi

+255693036618/ +255789001312

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizo

Mada Nyinginezo:

MFALME ANAKUJA

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

Kusubu ni nini? Miungu ya kusubu ni ipi?

Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kusubu ni nini? Miungu ya kusubu ni ipi?

Kusubu kibiblia ni kitendo cha kuyeyusha dhahabu au  fedha au ‘kito’ chochote kwa lengo la kuunda kitu kingine kipya.

Neno hilo utalisoma sehemu nyingi katika biblia kwa mfano hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utakutana nalo;

Mambo ya Walawi 19:4

[4]Msigeuke kuandama sanamu, wala msijifanyizie miungu ya kusubu mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

Maana yake msaifanye sanamu za kuyeyusha,

Kumbukumbu la Torati 27:15

[15]Na alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga, au ya kusubu, machukizo kwa BWANA, kazi ya mikono ya fundi, akaisimamisha kwa siri. Na watu wote wajibu, waseme, Amina.

Soma pia..

2Nyakati 24:4, 28:2, Waamuzi 17:3, Hesabu 33:52, 1Wafalme 7:23.

Maana yake ni ipi kiroho?

Hata sasa watu wengi, wanajiundia sanamu zao za kusubu rohoni bila wao kujijua…kwa kugeuza maumbile ya vitu vyema na kuvitumia isivyopasa..mpaka kuviabudu.

Kwa mfano fedha si mbaya lakini leo hii watu wameigeuza fedha kuwa mungu wao..kiasi kwamba kwao Mungu si kitu zaidi ya fedha, maisha yao yote ni kuhangaikia mali, kana kwamba hiyo ndio itakayowafikisha mbinguni, kaacha kumtumikia Mungu, hata muda na ibada hana, dai lake ni “Natafuta pesa’’ Sasa hizo ndio sanamu za kusubu..

Wengine biashara kwao zimeshageuka na kuwa sanamu za kusubu, wengine wanadamu., wengine muvi, wengine magemu, wengine mipira.

Tunapaswa tujilinde sana kwasababu sanamu za namna hii zinamtia Mungu WIVU, na wivu ni mbaya kuliko ghadhabu..

Ni heri Mungu akukasirikie kwa makosa mengine kuliko kwa kukuonea wivu.

kwasababu adhabu ya wivu ni mbaya sana kuliko ya hasira..

Mithali 27:4

[4]Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika;

Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu.

Tujilinde mioyo yetu na ibada za sanamu. Mungu hakuwahurumia wana wa Israeli walipotengeneza ndama ya kusubu na kuiabudu kule jangwani. Japokuwa yeye ndiye aliyewaokoa kwa mkono hodari.

Vivyo hivyo na wewe ukisema umeokoka, epuka kugeuza kitu chochote kuwa Mungu wako. Usiruhusu kamwe chochote kuchukua sehemu ya Mungu yako.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Shetri ni nini kama tunavyosoma katika Marko 3:38?

Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).

Zeri ya Gileadi ni nini?

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

Kuna majira yakupasa uisikie sauti ya Mungu, kuliko hasara utakayoingia, ili kuiponya nafsi yako.

Kuna mfalme mmoja wa Yuda anaitwa Amazia, Huyu mfalme siku moja alijikuta anaingia katika vita na maadui zake (Waedomi), Hivyo alichokifanya ni kupanga vikosi vya wanajeshi yake, ili kwenda kushindana nao. Lakini bado aliona majeshi yake hayatoshi, hivyo akaenda kwa ndugu zake, waliokuwa upande wa Israeli, ili awaajiri wanajeshi wao kwa fedha nyingi sana..

Hivyo akawaajiri wanajeshi takribani Laki moja (100,000).

Lakini tunaona alipokuwa anakaribia kwenda vitani, nabii wa Mungu alimfuata, akamwambia, achana na hao askari uliowaajiri, kwasababu mimi sipo nao..Nenda mwenyewe na jeshi lako vitani.

Likawa ni jambo gumu kwake, kwasababu tayari anapunguza nguvu, na kama hiyo haitoshi, tayari alishalipa fedha nyingi sana kwa ajili ya majeshi hayo..Amewekeza fedha zake nyingi katika vita na haziwezi kurudishwa.

Lakini kwasababu Amazia alikuwa anamcha Mungu, alitii sauti ya Mungu, akawa tayari kuipokea hasara, hiyo. Akaenda vitani na jeshi lake dhaifu, na Bwana akamsaidia kushinda, tena kwa ushindi mnono.

2Nyakati 25:6 “Akaajiri pia watu mashujaa mia elfu wa Israeli kwa talanta mia za fedha.

7 Lakini mtu wa Mungu akamjia, akasema, Ee mfalme, usiwaache jeshi la Israeli waende nawe; kwa kuwa Bwana hayupo pamoja na Israeli, yaani, wana wote wa Efraimu.

8 Lakini ukitaka kwenda, haya, jitie nguvu upigane; Mungu atakuangusha mbele ya adui; maana MUNGU ANAZO NGUVU ZA KUSAIDIA, NA KUANGUSHA.

9 Amazia akamwambia mtu wa Mungu, Lakini tuzifanyieje zile talanta mia nilizowapa jeshi la Israeli? MTU WA MUNGU AKAJIBU, BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO”.

Ni mara ngapi, watu wengi wanashindwa kumfuata Yesu, kisa hasara watakazoingia kwa uamuzi huo?

Niliwahi kuzungumza na mtu mmoja, anasema anampenda Mungu kweli, lakini anamiliki bar tena sio moja bali kadha wa kadha, na anasema ndipo anapopatia rizki. Nikamwambia hana budi kuacha biashara hiyo, kwasababu Mungu anaouwezo wa kumpa kitu kingine bora kuliko hicho, ikiwa tu atamtii Kristo. Lakini jambo hilo likawa bado ni gumu kwake kulipokea, akaendelea na biashara yake.

Mwingine pia tulimshuhudia akawa yupo  tayari kuokoka, lakini madai yake ni kuwa hana kazi, anatumia njia ya kujiuza ili apate pesa za kulipa kodi, na bili za maji na umeme.. Anasema kabisa nikiokoa najua hii kazi nitaacha, na sitakuwa na chanzo chochote cha mapato, nitaishije mjini?

Ndugu ikiwa na wewe ni mmojawapo wa watu wanaoshindwa kuacha kazi za ibilisi, kisa tu, umewekeza pesa nyingi katika hizo, au unahofia utakuwa maskini, au ukifanya kazi nyingine utapata kipato kidogo.. Nataka ukumbuke hilo andiko hapo juu kuwa “Bwana anazo nguvu za kusaidia, na kuangusha”.. Na “tena, Anaweza kukupa Zaidi sana kuliko hizo”

Anaweza kukupa mara dufu ya hivyo. Na hata kama hatokupa basi anaweza kukufanya uishi kwa raha na amani kuliko hata hapo ulipokuwepo. Bwana Yesu anasema,..Itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima, kisha upate hasara ya nafsi yako?. Amazia, alikubali kuingia hasara akijua kabisa Mungu kweli atampa Zaidi ya vyote alivyovipoteza.

Ni heri ukampa Yesu Maisha yako ayaokoe, kipindi hichi cha kumalizia, watu wengi wamenaswa kwenye vitanzi hivi…Wakiangalia mitaji yao yote imelalia kwenye michezo ya kamari, imelalia kwenye madawa ya kulevya, imelalia kwenye biashara za pombe na sigara, imelalia kwenye mavazi ya kikahaba na kidunia.

Achana nayo, mwamini Mungu anayekuita. Utakuwa salama, na atakusaidi kumudu Maisha yako..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

Kwanini wakristo wengi ni maskini?

ORODHA YA WAFALME WA ISRAELI.

JAWABU LA MAISHA YA MTU.

APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).

ENZI NA MAMLAKA AMEZIFANYA KUWA MKOGO

Uru wa Ukaldayo ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post