Category Archive Uncategorized

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Mtu ni kiumbe cha kwanza kilichoumbwa na Mungu duniani, chenye mfano wake na sura yake, kilichoumbiwa utashi na ujuzi ndani yake, kilichotofautishwa  na wanyama wote na viumbe vyote vilivyoumbwa na  Mungu duniani Ndicho kinachoitwa mtu.

Tunasoma hilo katika,

Mwanzo 1:26

[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

Lakini jina Binadamu/mwanadamu, ni neno lililozuka kufuatana na jina la mtu wa kwanza aliyeitwa Adamu.

Jina hilo alipewa na Mungu..Hivyo watu wote waliozaliwa na yeye waliita “wana wa Adamu”kwa kifupi “wanadamu” ambapo jina hilo kwa kiharabu linatamkwa “bin-Adam” ambapo sisi tunatamka “Binadamu”

Lakini ni mtu yule yule..isipokuwa asingeweza kuitwa binadamu siku ile ya kwanza alipoumbwa kwasababu alikuwa bado hajapewa jina, na pia halikuwa hana baba wa mwilini.

Ni sawa na Neno mwebrania na mwisraeli… kabla ya Yakobo kubadilishwa jina lake wana wote wa Ibrahimu hata Ibrahimu mwenyewe aliitwa Mwebrania..(Mwanzo 14:13)

Lakini Yakobo alipobadilishwa jina na kuitwa Israeli, utaona uzao wake wote baada ya pale ulizoeleka na kuitwa waisraeli mpaka leo. Lakini bado mahali pengine waliendelea pia kuitwa waebrania kwa asili yao.

Ndivyo ilivyo kwa mtu na mwanadamu. Ni yule yule kulingana na majira.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

Uru wa Ukaldayo ni nini?

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Utasi ni ugonjwa gani? (Marko 7:32).

Mjoli ni nini/ ni nani katika biblia?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Neno ‘Kima’ linamaanisha nini Katika biblia? (Mathayo 27:9 )

Tofauti na “Kima” mnyama ambaye anajulikana (jamii ya nyani), ukirudi katika biblia Neno hili lina maana nyingine pia.

Kima maana yake ni “thamani ya kitu katika pesa”.

Kwa mfano tukisema kima cha nazi ni Tsh. 1000. Maana yake ni kuwa thamani ya nazi ni sh. 1000.

Kwamfano Neno hilo utalipata katika vifungu hivi;

Mithali 31:10 “Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani”.

Yaani thamani mke mwema, inazidi thamani ya madini ghali ya Marijani (Ruby).

Mathayo 27:9 “Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima;”

Walawi 27: 11 “Na kama ni mnyama ye yote asiye safi, wa namna ambayo hawamsongezi kwa Bwana, basi atamweka huyo mnyama mbele ya kuhani;

12 na kuhani atamtia kima, akiwa mwema akiwa mbaya; kama wewe kuhani utakavyomtia kima, ndivyo itakavyokuwa.

13 Lakini kwamba ataka kumkomboa kweli, ndipo atakapoongeza sehemu ya tano juu ya hesabu yako.

14 Na mtu atakapoiweka nyumba yake iwe wakfu kwa Bwana ndipo kuhani ataihesabu kima chake hiyo nyumba, ikiwa njema ikiwa mbaya; kama kuhani atakavyoihesabu kima chake ndivyo itakavyokuwa”.

Soma pia Walawi 27:23, Ayub 18:28, Matendo 7:16

Je, kipo kima kinachozidi thamani ya Bwana Yesu?

Yuda alijaribu, kumsaliti Bwana kwa kima cha fedha, lakini Pamoja na kupokea mapesa yote, bado mwisho wa siku aliona, thamani yake hailinganishwi na utajiri wowote wa ulimwengu, ijapokuwa alikuwa ni mwizi lakini utaona alirudisha fedha zao zote, na kwenda kujinyonga.

Sasa Ikiwa watu waovu wanauona uthamani wa Bwana, hadi kwenda kujiua, iweje wewe uone kazi ni bora kuliko Bwana Yesu, anasa ni bora kuliko ibada?.

Je! thamani ya Bwana wako inazidi thamani ya huu ulimwengu? Bwana Yesu alisema Itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima halafu upate hasara ya nafsi yako? Itakufaidia nini?

Tubu mgeukie Bwana..

Ikiwa hujampa Bwana Yesu Maisha yako, na upo tayari kufanya hivyo leo, kwa kumaanisha kabisa, basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa Sala ya Toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Konde la Soani ni nini? (Zaburi 78:12,43)

Deraya ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 59:17

Bushuti ni nini?

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Tunguja ni nini katika biblia? (Mwanzo 30:14).

Hisopu/ Hisopo ni nini katika biblia?(Zaburi 51:7)

Kuhusuru ni nini kibiblia? (Luka 19:43)

Kujuzu ni nini kama tunavyosoma katika 2Wakorintho 12:4?

Rudi nyumbani

Print this post

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

Ni eneo la pango ambalo lilikuwa karibu na mji wa Israeli unaoitwa Hebroni, ambalo Ibrahimu alilinunua kwa mtu mmoja aliyeitwa Efroni, kwa ajili ya maziko ya mke wake Sara.

Mwanzo 23:13 “Akamwambia Efroni, na watu wa nchi wanasikiliza, akisema, Tafadhali unisikilize; nitatoa kima cha shamba, nawe ukipokee kwangu, nami nitamzika humo maiti wangu.

14 Efroni akamjibu Ibrahimu, akamwambia,

15 Bwana wangu, unisikilize. Sehemu ya nchi, ambayo thamani yake ni shekeli za fedha mia nne, n’nini hii baina yako na yangu? Basi uzike maiti wako.

16 Ibrahimu akakubali maneno ya Efroni. Ibrahimu akampimia Efroni ile fedha aliyotaja masikioni mwa wazawa wa Hethi, shekeli za fedha mia nne za namna inayotumika na wenye biashara”.

Eneo hilo baadaye lilikuja kugeuka kuwa kaburi la kifamilia, kwani hapo hapo ndipo Ibrahimu alipokuja kuzikwa na watoto wake, halikadhalika, ndipo Yakobo na Esau walipomzikia baba yako Isaka,

Na wakati wakiwa kule Misri, Yakobo aliwaagiza Watoto wake,pia  wakamzike katika kaburi hilo la familia, la Makpela.

Mwanzo 49:29 “Akawaamuru, akasema, Mimi ninakwenda kukusanywa pamoja na watu wangu; mnizike pamoja na baba zangu, katika pango iliyomo shambani mwa Efroni, Mhiti;

30 katika ile pango iliyomo shambani mwa Makpela, iliyo mbele ya Mamre katika nchi ya Kanaani, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake ya kuzikia.

31 Humo walimzika Ibrahimu, na Sara mkewe; humo wakamzika Isaka, na Rebeka mkewe; nami humo nikamzika Lea;

32 shamba na pango iliyomo lililonunuliwa kwa wazawa wa Hethi”.

Eneo hilo kwasasa, pale Israeli limejengwa msikiti, ujulikanao kama “msikiti wa Ibrahimi”, japo wote wayahudi na waislamu, hakuna hata mmoja anaweza kusema anao umiliki wa moja kwa moja wa hapo.

Lakini Je pango la makpela lina umuhimu kwetu hadi sasa au kwa Wayahudi?

Pango hili, au lolote lile ambalo lilizikiwa watakatifu, halina umuhimu wowote katika Imani yetu, Zaidi ya mambo ya kihistoria tu. Myahudi au mkristo yoyote ukizikwa karibu na eneo hilo, hakutakufanya uende mbinguni, Wapo wengine wanafikiri, wakienda Yerusalemu na kuomba kwenye ule ukuta wa Nehemia wa maombolezo, ndio maombi yao yatasikiwa. Au wakienda kubatizwa katika mto Yordani kama Bwana Yesu ndio ubatizo wao utapokelewa, jambo ambalo sio kweli.

Halikadhalika na Pango hilo la makpela halina umuhimu wowote, kwa mtu yeyote, kuzikiwa pale.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?

Je! ni halali kwa mtu wa Mungu kutumia njia za uzazi wa mpango,ikiwamo mipira?

Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

Uru wa Ukaldayo ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Kuna njia kuu sita(6)

Ni vema ukazifahamu hizi njia Mungu anazozungumza na watu, ili usitegemee tu njia moja uifahamuyo wewe, matokeo yake ukakosa shabaha ya kuzisikia sauti za Mungu kila siku maishani mwako zinapozungumza na wewe.

1. Ya kwanza ni Njia ya moja kwa moja:

Hii ni Aidha kwa Sauti, ndoto, au maono,

Ni mojawapo ya njia ambayo Mungu anazungumza na watu. Na ndio inayojulikana na kutegemewa na wengi.

Ayubu 33:14-15

[14]Kwa kuwa Mungu hunena mara moja,  Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. [15]Katika ndoto, katika maono ya usiku,  Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

Katika maisha yetu kwa namna moja au nyingine Mungu alishazungumza nasi kwa njia hii. Unaweza usione, maono au usisikie sauti lakini kila mtu huwa anaota. Na kwa njia hiyo Mungu huzungumza.

  1. Kwa njia ya Neno lake:

Hii ndio sauti ya Mungu namba moja ambayo inazungumza na mtu moja kwa moja na kwa wakati wote..ni sauti ambayo hailinganishwi na sauti nyingine zozote.

Ukiwa ni msomaji mzuri wa Neno, utamsikia Mungu katika nyanja zote za Maisha akikufariji, akikuonya, akikushauri, akikuongoza n.k. Ni pakeji iliyojitosheleza., ambayo hailinganishwi na njia nyingine yoyote.

2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;”

    3. Njia nyingine ni Amani.

Ikiwa wewe umeokoka, na umejazwa Roho Mtakatifu, basi ujue mara nyingi sana Mungu atatumia amani yake moyoni mwako kuamua mambo mengi..

Na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 10:11-13

[11]Na mji wo wote au kijiji cho chote mtakachoingia, tafuteni ni nani humo aliye mtu mwaminifu; mkae kwake hata mtakapotoka. [12]Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni.

[13]Na nyumba ile ikistahili, amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, amani yenu na iwarudie ninyi.

Wakolosai 3:15a “Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu;..”

Kuonyesha kuwa amani itokayo kwa Roho ni sauti ya Mungu kutuongoza, ikiwa umepoteza amani ghafla katika mazingira fulani kuwa makini sana hapo. Wakati mwingine ni Mungu anazungumza.

   4. Kwa kupitia watu.

Hapa anaweza akachagua aidha apitie mtu mwovu au mtu mwema. Mara nyingi sana Mungu anazungumza na watu kupitia watumishi wake, yaani wahubiri, waalimu, wainjilisti n.k.

Yeremia 25:4

[4]Naye BWANA ametuma kwenu watumishi wake wote, hao manabii, akiamka mapema na kuwatuma, lakini ninyi hamkusikiliza, wala hamkutega masikio yenu, msikilize.

Na mara nyingine tena anaweza kutumia watu wa kidunia kukuonya..kama vile maaskari, wakuu wa hii dunia n.k.

Hivyo ni kuzingatia sana unachokisikia au kufundishwa au kuonywa na watu, hususani watumishi wa Mungu..Mara nyingine sauti ya Mungu ipo nyuma yao.

     5. Kwa kupitia mazingira.

Mazingira yanaweza yakawa ya kimaisha, au ya kihali…kwa mfano Mungu akitaka uelewe jambo fulani, wakati mwingine hatumii sauti ya moja kwa moja, kwasababu pengine unaweza kulichukulia juu juu tu au usimwelewe, hivyo atakupitisha katika maisha fulani au mazingira fulani, na kwa kupitia hayo utajua kabisa hapo ni Mungu alikuwa akisema na wewe.

Mfano wa watu kama hawa alikuwa ni Nebukadreza, yeye alionywa na Mungu, awe mnyenyekevu na amche Mungu, lakini hakusikia, kinyume chake akapuuzia ule unabii aliopewa na Danieli. Matokeo yake baada ya miezi 12, akageuzwa kuwa kama mnyama, akawa anaishi huko misituni akila majani kama ng’ombe..mpaka siku alipoelewa somo kuwa aliye juu ndiye anayetawala falme zote za duniani. Ndipo akajinyenyekeza ,hivyo Mungu akamrudishia ufalme wote wa dunia. (Danieli 4)

   6. Kwa kupitia vitu vya asili na viumbe.

Sauti ya Mungu imejificha sana katika vitu vinavyotuzunguka na asili, kiasi kwamba tungefahamu vema basi tusingekuwa na ugumu wa kumwelewa Mungu.

Embu fikiri Bwana Yesu alivyotuambia..tafakarini Kunguru?..hawapandi hawavuni wala hawana maghala ya chakula lakini wanakula..Je sisi si mara nyingi zaidi ya hao? (Luka 12:24)

Hili ni neno ambalo lilikwepo tangu enzi na enzi kiasi kwamba watu wangekuwa wanalitafakari kabla hata ya Yesu, wasingekuwa na hofu ya maisha pale wanapotaka msaada kutoka kwa Mungu.

Vivyo hivyo utazamapo, bahari, milima, miti,  zipo sauti nyingi sana za Mungu nyuma yake .. Chukua muda mwingi kutafakari, utaisikia sauti ya Mungu waziwazi.

Mungu alimwambia Ibrahimu angalia juu tazama nyota za mbinguni na mchanga wa baharini upate imani kwangu.

Hivyo ni vizuri ukapata maarifa haya usije ukaangamia kwa kutomwelewa Mungu. Leo hii watu wanategemea njia moja tu..ile ya moja kwa moja..yaani kusikia sauti, au kuona maono au kuota ndoto. Na kusahau hizi nyingine.. Ndio hapo utasikia wakisema nimeomba sana, nimelia sana Mungu aseme na nini, lakini sijawahi kumsikia.

Ni kwanini? Nikwasababu wanalazimishia njia hiyo hiyo moja Mungu aseme nao..

Hawajui kuwa Mungu hapangiwi fomula ya kuzungumza.Hivyo wewe uombapo..kuwa mtulivu, soma sana Neno mtafakari Mungu..subiri azungumze kwa jinsi apendavyo yeye. Atakujibu tu aidha kwa Neno lake, au mtumishi wake, au amani moyoni mwako, au kwa kutazama mambo ya asili, ukiona hivyo basi ujue ni Mungu huyo.

Hivyo kaa katika utulivu wa Roho, zingatia kusoma Neno..kwasababu maarifa kama haya utayapata katika biblia na sio kwa kuota au kuona maono.

Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

Unyenyekevu ni nini?

ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.

Rudi nyumbani

Print this post

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

SWALI: Naomba kufahamu maombolezo ya Hadadrimoni tunayoyasoma katika Zekaria 12:11 ni maombolezo gani hayo?

Zekaria 12:11 “Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido”.


JIBU: Hadadrimoni ni eneo lililokuwa sehemu ya bonde lijulikanalo kama Megido huko Israeli. Bonde hili lilisifika kwa vita, na Zaidi sana kuuawa kwa baadhi ya viongozi wakubwa. Hivyo kupelekea maombolezo makubwa sana kwa watu waliouliwa viongozi wao.

Mfano katika Habari hii, inamlenga mfalme Yosia, ambaye ndiye aliyekuwa tumaini la mwisho la Taifa la Israeli. Kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka, Yosia alikuwa mfalme aliyemcha Mungu sana kuliko wafalme wote wa Israeli,tukimwondoa Daudi, na  yeye ndiye aliyefanikiwa kuondoa sanamu zote Israeli kipindi kile, Na ndiye mfalme ambaye kuzaliwa kwake kulitabiriwa miaka mingi sana kabla hajazaliwa.

Hivyo waisraeli walimwona kama ndiye tumaini pekee waliobakiwa nalo.

Lakini siku moja alitoka kwenda kupigana vita na mfalme wa Misri aliyeitwa Neko. Na kinyume na matazamio yake, aliuliwa, na mahali alipouliwa palikuwa ni hapo Hadadrimoni katika bonde la Megido.

Israeli nzima iliposikia, ilimwombolezea maombolezo makubwa sana,  taa ya Israeli kuzima ghafla, mpaka wakamwekea kumbukumbuku lake la kila mwaka akumbukwe.

2Wafalme 23:29 “Katika siku zake, Farao-neko, mfalme wa Misri, akakwea ili kupigana na mfalme wa Ashuru, akafika mto Frati; naye mfalme Yosia akaenda kupigana naye; naye mfalme wa Misri akamwua huko Megido, hapo alipoonana naye”.

2Nyakati 35:25 “Naye Yeremia akamlilia Yosia; na waimbaji wote waume kwa wake wakamtaja Yosia katika maombolezo yao, hata leo; hata wakayafanya kuwa ada kwa Israeli; nayo, tazama, yameandikwa katika maombolezo”.

Hivyo Mungu akatumia kivuli hicho kueleza jinsi taifa la Israeli litakavyokuja kuomboleza huko mbeleni, siku watakapopewa neema ya kumtambua Kristo. Biblia inasema wayahudi watamwombolezea Yesu waliyemchoma, watalia kama vile mtu aliyefiwa na mwana wake wa pekee, mfano wa pigo la wamisri la kuuliwa wazaliwa wao wa kwanza, jinsi walivyokuwa na maombolezo makuu.

Kama vile, maombolezo ya Yosia katika bonde la Hadadrimoni, Waisraeli walivyombolezea mfalme wao, kwa uchungu mwingi, ndivyo itakavyokuwa siku hiyo watakapomwagiwa neema ya kumtambua Kristo..

Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.

11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, KAMA MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI KATIKA BONDE LA MEGIDO.

12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;

13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.

14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.

Ndugu, Kipindi si kirefu hii neema inayochezewa leo hii, itageuka na kuwarudia wayahudi. Kipindi hicho unyakuo utakuwa umeshapita, na Roho Mtakatifu hayupo tena kwetu sisi watu wa mataifa, bali kwa watu wake Israeli. Dunia itastaajabia, kuona watu hawa wametolea wapi moyo huo wa kujuta kwa ajili ya Yesu ambaye leo hii wanamkataa.

Kwani wayahudi hawa wakati huo, biblia inasema watajitenga, familia kwa familia, ukoo kwa ukoo, kila moja atakuwa na maombolezo yake makuu sana haradharani na sirini, kudhihirisha kazi ya Roho Mtakatifu juu yao. Sasa wakati huo ndio Mungu atakuwa anawaandaa ili kuwarudishia  ufalme ambao waliutazamia kutoka kwa masihi wao, sawasawa na lile ulizo la mitume (Matendo 1:6)

Ndugu, ukishaona mabadiliko haya kwa wayahudi, ujue umeshaachwa katika unyakuo, vilevile hii dunia itakuwa na kipindi kifupi sana kisichozidi miaka 7 hadi iishe. Leo hii tumeshaona Israeli imekuwa taifa, wote wamesharudi kwao. Unadhani wanachosubiria ni nini kama sio kurudiwa wakati wowote.

Bwana Yesu alisema,

Mathayo 24:32 “Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu”;

Mtini unawakilisha taifa la Israeli (Yer 24), Hivyo tuonapo Israeli leo hii inachipuka, tujue kuwa wakati wa mavuno umeshafika.

Je!, unalitambua hilo? Bado unaipuuzia hii neema ambayo hatuna nayo muda mrefu?. Una Habari kuwa unyakuo ni wakati wowote, na hatua zake tayari zimeshaanza?. Wakati tulionao sasa si wakati wa kubembelezewa wokovu, Injili imeshazagaa kila mahali, watu wote wameshasikia, ni wakati wa kujitakasa, wewe ambaye tayari umeshaokoka. Lakini kama bado upo nje ya neema kipindi hichi? Utakuwa ni wa ajabu kweli.

Unasubiria siku Fulani, neema ikufikie? wakati neema ya wokovu ipo tayari kila mahali, unasubiria ikufikieje tena? Tambua kuwa  njia imeshasonga, na wengi wanatamani waingie wanashindwa, kwasababu upotofu mwingi upo duniani, na wewe bado tu unaisubiri.. Ni kuwa makini sana. Neema inakimbilia Israeli sasa, jicho la Bwana linaelekea kule sasa, kwani muda wetu umeshakwisha.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita.

Uru wa Ukaldayo ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Mtu ambaye hajaoa anaruhusiwa kulichunga kundi?

SWALI: Shalom… Pastor naomba kuuliza je ni sahihi mtumishi kuongoza kanisa hajafunga ndoa? na anaweza kubatiza washirika? Amina.


JIBU: Kigezo cha mtu kuwa Kiongozi wa kanisa, na kufanya kazi zote za madhabahuni, ikiwemo kubatiza, kuwawekea watu mikono ya utumishi, n.k. vimetolewa katika kitabu cha 1Timotheo 3:1-7

1 Timotheo 3 : 1-16

1 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.

2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;

3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;

4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;

5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)

6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.

7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.

Askofu maana yake ni mwangalizi wa kanisa, Hivyo yeyote anayelichunga kanisa, awe ni mchungaji, mwalimu, Mtume, maana yeye ndio mwangalizi basi vigezo hivyo vinamuhusu.

Lakini katika vigezo hivyo vyote, hakuna hata kimoja, kinachosema, ni lazima aoe.. Isipokuwa anasema Askofu ni lazima awe ni mume wa mke mmoja..Akiwa na maana kwamba ikiwa ni mwana-ndoa basi, anapaswa awe ni mume wa mke mmoja, na si Zaidi, kama anao wake wawili au watatu, tayari ameshakidhi vigezo vya kutostahili kuitwa mchungaji.

Lakini ikiwa ni mtu ambaye, hajaoa lakini ameshika vigezo vyote, hivyo, yaani, ni mtu asiyelaumika, si mlevi, mpole, si mpenda fedha, aliyeshuhudiwa na watu ni mwema, amekomaa kiroho. Basi huyo anavigezo vyote vya kuwa mchungaji, au kiongozi yoyote wa kanisa.

Mtume Paulo hakuwa ameoa, lakini alikuwa ni mwangalizi wa makanisa yote yaliyokuwa Asia, na mataifa mengine, Na Zaidi sana yeye ndiye aliyetoa mwongozi wa mafundisho ya ndoa.

Hivyo kuoa/ kutokuoa, si takwa, la kuwa askofu.

Kinyume chake mtume Paulo,alishauri  watu wote wawe kama yeye (yaani wasioe), kwasababu watu wasiooa inawapa wigo mpana wa kumtumikia Mungu bila kuvutwa na mambo mengine, ikiwa wamemaanisha kweli kujikita kwa Bwana.

1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”.

Lakini ikiwa huwezi kuishi Maisha hivyo, kwa jinsi ulivyoitwa, basi hakikisha unatumika kiuaminifu, hapo utakuwa umekidhi vigezo vya kulichunga kundi , kubatiza, n.k.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ndoa na Talaka

Ndoa ya serikali ni halali?

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Uvuvi bora hauchagui wa kuvua.

Askofu na mchungaji mkuu ni nani?

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

Rudi nyumbani

Print this post

JIHUDHURISHE, ILI AANZISHE MAZUNGUMZO NA WEWE

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetus Yesu Kristo, sifa na utukufu vina yeye milele na milele. Amina.

Unafahamu kuwa shetani ambaye ni adui yetu, si kila wakati anafanya mambo yake kwa kutegemea jitihada zake tu, anajua  kabisa mambo mengine huwa hayatoki isipokuwa kwa kufuata kanuni ambazo tayari Mungu alishaziweka.

Na huwa anazitumia hizo kanuni, kutuharibu sana, lakini sisi kama wana wa ufalme, hatuzitumii kumuharibu yeye.

Kwamfano madhara aliyopanga kumletea  Ayubu, alitambua kuwa haiwezekani kwa njia ya kawaida kuyatekeleza ,. Ndipo akatumia njia ya juu Zaidi ya kujishusha, kwa kwenda KUJIHUDHURISHA mbele za Mungu,.

Akashusha kiburi chake hadi chini kabisa, akaungana na Malaika watakatifu wa Mungu, kupanda mbinguni, akaenda mbele ya uwepo wa Mungu, kwa unyenyekevu wote, akitumaini kuwa kwa kutenda kule, ni lazima tu Mungu atamwangalia, kwasababu Mungu ni Mungu wa uumbaji wote.

Na kweli baadaye Mungu alipomwona anatembea tembea mbele ya uwepo wake kwa muda mrefu, akaanzisha mazungumzo naye, Akamuuliza unatoka wapi shetani, akasema duniani, katika mizunguko yangu, ndipo shetani akatumia fursa hiyo ya mazungumzo, kupeleka na mashataka yake yote. Na mwisho wa siku akapatiwa haja yake.

Akashuka chini, akamfanya Ayubu kama alivyoweza kumfanya..

Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.

7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.

8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu”.

Tunachopaswa tujue ni nini, Ikiwa mungu wa dunia hii, anajua siri ya mafanikio ya uharibifu wake, haitegemei tu nguvu zake mwenyewe, bali pia kwa kujihudhurisha mbele za Mungu ..Unategemea vipi wewe na mimi tusiwe watu wa namna hiyo?

Shetani anatushangaa sana, tunapomkimbia Mungu, anatushangaa sana tunapokwenda mbali na uwepo wa Mungu, kwa visingizio visivyokuwa na maana, hatutaki kwenda kumfanyia Mungu ibada hata mara moja kwa wiki tunasema tumechoka, kwasababu jumatatu tunakwenda kazini hivyo hatuna budi tulale!! Ndugu ukitegemea nguvu zako kuyaongoza haya Maisha jihesabie tu wewe ni MKIA Maisha yako yote. Ndivyo ilivyo..

Hilo shetani alijaribu akaona halifai, na wewe unalijaribu, alijua si kila wakati nitajiamulia tu mimi mwenyewe, kwa nguvu zangu..Lazima niwe na muda wangu wa kwenda kujinyenyekeza, tena kwa muda mrefu mbele za Mungu.

Ikiwa tunaona mikesha ni shida, hata mara moja kwa mwezi, tusahau Mungu kuanzisha mazungumzo yoyote na sisi. Ikiwa hatujizoezi kusali mara kwa mara, na kuutafuta uso wa Mungu hata kwa mifungo wakati mwingine, tujue tu mambo mengi sana tutafeli kuyatimiza maishani mwetu.

Faida za kujihudhurisha mbele za Bwana ni zipi?.

Tunapokuwa uweponi mwa Bwana muda mrefu, Mungu mwenyewe ataanzisha mazungumzo na sisi, atatuuliza, unasumbukia nini, una haja gani, unatafuta nini? Kama tu alivyofanya kwa shetani…Lakini akitutazama hatupo uweponi mwake, Tunazunguka zunguka tu duniani, na masumbufu ya Maisha haya kila wakati, siku saba kwa juma, siku 365 za mwaka, na yeye ataendelea na mambo yake, atatuacha tutaabike wenyewe..

Biblia inasema..

Yakobo 4:8 “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi..”

Ndugu tujizoezi, kumkaribia Mungu kila siku, ibada inayotoka rohoni iwe ni sehemu ya Maisha yetu, Na bila shaka tutaanza kumuona Mungu akisema na roho zetu.

Kumbuka uanzapo kufanya mambo kama hayo kwa bidii, hutasikia sauti kama sauti ikisema na wewe, bali rohoni Mungu atakuwa anazungumza na Maisha yako. Na mara utaona yote uliyokuwa unamwomba, au unayatamani yatendeke tangu zamani, Mungu anakufanikisha kwa njia ambazo hujazitazamia. Hivyo ndivyo Mungu anavyozungumza na watu.

Tukiijua kanuni hii, shetani atatuchukia sana, kwasababu tutakuwa tumeshajua siri ya mafanikio yetu, kama yalivyokuwa yake katika huu ulimwengu.

Kama wewe ni mtakatifu, anza sasa kumpa Mungu muda wako wa kutosha, huko ndiko kujihudhurisha mbele zake, usiwe na udhuru wa kutokwenda ibadani, usiwe na udhuru wa kutohudhuria mikesha na wenzako, usiwe na udhuru wa kutokufunga na kuomba, na kujifunza Neno kila siku. JIHUDHURISHE kwa kadiri uwezavyo mbele za Mungu.

Ndivyo Mungu atakavyoanzisha mazungumzo na wewe.

Bwana akubariki.

Ikiwa bado upo nje ya Kristo, kumbuka kuwa, hatuna muda mrefu hapa duniani, Unyakuo ni wakati wowote, kulingana na kutimia kwa dalili zote zilizotabiriwa katika maandiko, na kama hilo halitoshi fahamu kuwa mlango wa neema, umeshaanza kufungwa, usipoiamini injili, leo, kesho itakuwa ni ngumu Zaidi, na siku moja hutaiamini kabisa. Kwasababu neema haidumu milele, maandiko yanasema hivyo!.

Hivyo tubu dhambi zako kwa kumaanisha leo, mgeukie Kristo, injili tuliyobakiwa nayo sasa sio ya kubembelezwa, ni wewe mwenyewe uone hali halisi, umgeukie muumba wako.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TUSIRUHUSU MAMBO YA KUSUBIRISHA, YAVURUGE MUDA WETU NA MUNGU.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

“Vya Kaisari mpeni kaisari”  ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?.

Rudi nyumbani

Print this post

 SWALI: Ni njia gani itumike kuwaongoza mabubu sala ya toba?

JIBU: Tukumbuke kuwa “sala ya Toba” sio wokovu, Sala ya toba ni njia mojawapo, inayotumiwa kuukaribisha wokovu ndani ya mtu, lakini sala kama sala yenyewe sio wokovu, Ikiwa na maana zipo njia nyingine, Na ndio maana huwezi kuona mahali popote mitume waliwaambia watu wafuatisha sala fulani, kwamba kwa hiyo ndio wataokoka..Huwezi kuona.

Wokovu unatoka moyoni. Pale mtu anapojitambua kuwa ni mwenye dhambi, na hivyo anahitaji kukombolewa kutoka katika mauti na Yesu Kristo, kitendo kinachompelekea kuyasalimisha maisha yake yote kwa Bwana Yesu ayaongoze, na kuachana na mambo ya ulimwengu, Huo ndio wokovu.

Sasa jambo kama hili likishatokea ndani ya mtu, udhihirisho wa nje ndio unafuata, ambao mojawapo ndio kukiri kwa kinywa chako, na cha pili ni Matendo yako.

Kutimiza lile andiko la Warumi 10:9

“Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka”.

Sasa mabubu, hawajajaliwa kuongea, hawawezi kumkiri Kristo kwa vinywa vyao..Lakini wanaweza kuonyesha kuwa wamemwanini Kristo kwa matendo yao. Wakifanya hivyo tayari huo ni wokovu tosha, kutoka kwa Bwana.. Hivyo mtu kama huyu ikiwa tayari ameshamwani Bwana muhimize tu, aanze kuenenda sawasawa na kuamini kwake.

Tutakumbuka kisa kile cha Yule mwanamke ambaye Bwana Yesu alisema alikuwa na dhambi nyingi, jinsi alivyomwendea na kulia sana miguuni pake, kudhihirisha majuto ya makosa yake, kisha kumpangusa kwa nywele zake, Utaona pale Bwana Yesu hakuzungumza naye maneno yoyote, kwamba njoo nikuongoze sala ya toba, au sema maneno haya au yale, hapana isipokuwa alipoona tu moyo wake wa toba ulivyomaanisha kwelikweli alimwambia.. “Mwanamke umesamehewa dhambi zako”

Luka 7:36-48

 “36 Mtu mmoja katika Mafarisayo alimwalika ale chakula kwake; akaingia katika nyumba yake yule Farisayo, akaketi chakulani.

37 Na tazama, mwanamke mmoja wa mji ule, aliyekuwa mwenye dhambi, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu.

38 Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu.

39 Basi, yule Farisayo aliyemwalika alipoona vile, alisema moyoni mwake, Mtu huyu kama angekuwa nabii, angemtambua mwanamke huyu amgusaye, ni nani, naye ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi…..

44 Akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, Wamwona mwanamke huyu? Niliingia nyumbani kwako, hukunipa maji kwa miguu yangu; bali huyu amenidondoshea machozi miguu yangu, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake

45 Wewe hukunibusu; lakini huyu tangu nilipoingia hakuacha kunibusu sana miguu yangu.

46 Hukunipaka kichwa changu mafuta; bali huyu amenipaka miguu yangu marhamu.

47 Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi, kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo.

48 Kisha alimwambia mwanamke, Umesamehewa dhambi zako.

Hii kuonyesha kwamba, pale unaoonyesha geuko la kweli moyoni mwako, kabla hata hujazungumza chochote tayari umeshasamehewa.

Ndivyo ilivyo kwa mabubu, haijalishi hawataweza kukiri sala yoyote kwa vinywa vyao, lakini ikiwa moyoni mwao wameonyesha mabadiliko, hicho ndicho Mungu anachokitaka. Imekuwa desturi leo hii kuona kundi kubwa la watu wanasema wameongozwa sala ya toba na kumkiri Yesu , lakini ukitazama matendo yao hayaendani na walichokikiri. Huo ni unafki ambao unamchukiza Bwana sana.

Mathayo 15:7 “Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema,

8 Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami”.

Bwana anataka tumfuata na tumwabudu katika Roho na kweli. Na sio katika maneno matupu. Ikiwa mtu asiweza kuongea, amesimama katika wokovu, huyo mtu ni wa thamani sana mbele za Mungu

Swali ni je wewe, uliyemkiri Bwana, unayemsifu, unayemuhubiri, unayemtangaza. Je! Ni kweli kitokacho mdomoni mwako, kimeambatana na badiliko la ndani?

Majibu tunayo.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Utasi ni ugonjwa gani? (Marko 7:32).

Kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate. Ina maana gani?

Kuongozwa sala ya toba.

Dusumali ni nini katika biblia?

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

SWALI 1: Je! Shetani anaweza kuumba, kama Mungu? Kama sio Mbona kipindi cha Farao, tunaona wale waganga waliweza kuleta vyura na nyoka, kama alivyofanya Musa. Je wale vyura aliwaumbaje, uhai alitolea wapi kama sio Mungu?


JIBU:  Bwana Yesu anasema; Shetani ni mwongo, na sio tu mwongo, bali ni Baba wa huo;

Yohana 8:44 “..wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”.

Maana yake ni kwamba ufalme wake ameujenga juu ya misingi ya uongo. Alitumia uongo kumnyang’anya Adamu nafasi yake ya umiliki. Vivyo hivyo hadi sasa anatumia uongo kuwadanganya watu wasiutambue ukweli  wote kuhusu yeye.

Anataka kuwadanganya watu, wadhani kuwa yeye ana nguvu za kuweza kukaribiana hata na Mungu au anao uwezo wa kuumba kama Mungu. Lakini ukweli ni kwamba, shetani au kiumbe chochote kile hakiwezi kuumba hata sisimizi. Uwezo huo anao Mungu tu, peke yake.

Kama ni hivyo, ni nini alikifanya kipindi cha Farao?

Alichokifanya kipindi cha Farao, si kingine zaidi ya uongo. Kutokana na maarifa aliyokuwa nayo kipindi kile ambayo anayo hadi sasa, shetani anaweza kubaliki kitu fulani kionekane ni kitu kingine mbele tu ya macho ya watu, au hata kujibadilisha yeye, aonekane ni malaika wa kweli, kumbe ndani ni yeye Yule yule shetani..Biblia inatuambia uwezo huo anao..

2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru”.

Hivyo tabia hiyo anayo.. kipindi kile hakuumba nyoka wenye pumzi ya uhai, kama nyoka wengine, au vyura wapya..bali alifanya kazi yake hiyo ya kubadilisha maumbile ya vitu mbele ya macho ya watu.. Kwa lugha ya sasa wanaita “kiini-macho” au “mazingaumbwe”, na ndio maana nyoka wa Musa, hakuwaona wale kama ni nyoka wenzake, wanaohitaji mapambano, bali aliona kama ni chakula tu, akala.

Ni sawa na mwanadamu ambaye amefikia maarifa ya kutoa ‘photocopy’ kitu orijino, Shetani naye hapo amepafikia.Lakini hana uwezo wa kutengeneza orijino.

Kama shetani angekuwa na uwezo wa kuumba chura, hata mbwa angeweza, hata ng’ombe pia angeweza, na  sokwe nao. Na matokeo yake dunia, ingejawa na vitu vilivyoumbwa na Mungu, na vilivyoumbwa na shetani, leo hii tungesikia wale nguruwe si wa Mungu bali ni wa shetani, usiwaguse. Lakini hadi sasa hakuna rekodi ya kitu chochote kilichoumbwa na shetani, zaidi sana rekodi aliyonayo ni kuumba uovu na uasi duniani.

Pia tazama..

1 Jehanamu ni wapi?
2 Nini kinatokea baada ya kifo?
3 Freemason ni nini?
4 Siku ya unyakuo itakuwaje?
5 Upendo ni nini, je kuna aina ngapi za upendo?
6 Je! umepokea Kweli Roho Mtakatifu?
7 Mauti ya pili ni nini?
8 Faida za maombi
9 Jinsi ya kusoma biblia.
10 Je! kuna aina ngapi za malaika?

SWALI 2 : Je! Jini au pepo ni roho tu au pia wana miili inayoonekana, kiasi kwamba tunaweza kuwashika? Kama ndivyo Mbona Bwana Yesu alisema.

Luka 24:39 “Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.

JIBU: Ni kweli sawasawa na maneno ya Bwana Yesu, hakuna jini au pepo, au kiumbe chochote cha rohoni, chenye mwili, na kikaweza kuishi hapa duniani kama sisi.. Hakuna.

Kumbuka, Bwana Yesu alisema..

Mathayo 12:43 “Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.

44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.

45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”.

SWALI 2 : Je! Jini au pepo ni roho tu au pia wana miili inayoonekana, kiasi kwamba tunaweza kuwashika? Kama ndivyo Mbona Bwana Yesu alisema.

Maandiko hayo ni kutuonyesha kuwa, mapepo, hayana miili yao wenyewe ya kuishia hapa duniani, yanategemea watu,au wanyama,ili kutembea duniani, kama wakati ule yalivyomwomba Bwana yawaingie wale nguruwe. Lakini yenyewe kama yenyewe, hayawezi kusimama na kuwa kama wanadamu kutembea duniani.

Lakini Je! Wale wanaoshuhudia kwamba mapepo yanawatokewa, na pengine kuzuni nao, ni nini vile?

Mapepo yanaouwezo wa kujidhihirisha mbele ya mtu kwa taswira ya kitu fulani, aidha ya mtu, au kitu, kukutisha au kukufanya uogope,  (Mathayo 14:26), au kukutokea katika ndoto,au maono.. lakini zaidi ya hapo yasiweza,  kuendelea na kuchukua maumbile na kuwa kama mwanadamu mwingine na kuishi hapa duniani, kama vile kula, kunywa, kufanyabiashara, kuoa, au kuolewa n.k. huo uwezo hawana kwasababu hawana miili. Pepo haliwezi kuzaa na wewe.

Vinginevyo, shetani angeshajidhihirisha siku nyingi na kuwa mfalme wa dunia. Lakini mpaka sasa ni roho tu, na atabakia kuwa roho, mpaka atakapotupwa kwenye ziwa la moto na mapepo yake.

Lakini kumbuka ukiwa ni mtu wa kujishughulisha na mambo ya ushirikina, aidha wewe ni mganga, au mchawi, au ulishawahi kwenda huko, ukafanyiwa matambiko, au kufanyiwa mazindiko ya kipepo, au ukala vitu vyao, Huo nao ni mlango unaoongeza wigo mkubwa sana, wa shetani au mapepo yake, kujidhihirisha kwako, kwasababu umeingizwa katika mtandao wao wa kiroho, hivyo inakuwa rahisi sana kwao kujidhihirisha kwako, na pengine kuchukua umbile ya kitu chochote kukuletea madhara mwilini. Tofauti na mtu ambaye  yupo mbali na mambo hayo.

Hivyo dawa pekee, ya kumfukuza shetani na majini yake, yasikutokee tokee au yasikufuate fuate ni kumkabidhi Yesu maisha yako. Kwa kumaanisha kabisa kuacha maisha ya dhambi, na baada ya hapo, ukazingatia kusoma NENO..

Kwasababu kuokoka ni sehemu ya kwanza, ya kuwekwa huru.. Ili kuukamilisha uhuru wako ni lazima Neno la Mungu likae ndani yako kwa wingi ili uweze kumshinda kabisa kabisa shetani.

 Biblia inasema.

Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Bwana Yesu, alikuwa ni mtakatifu wa Mungu, ambaye hakutenda dhambi, lakini hilo halikumzuia shetani asimjie, na kuzungumza naye. Lakini utaona alimshinda kwa Neno la Mungu lililokuwa ndani yake, na si kitu kingine.

Vivyo hivyo na wewe, ikiwa tayari umeshaokoka, Jifunze sana Neno, ujue mamlaka, na haki uliyonayo katika Msalaba wa YESU KRISTO. Hiyo itakufanya usiishi maisha ya woga,wala wasiwasi wa nguvu zozote za giza, kwasababu utakuwa tayari umeshajua uwezo uliopewa jinsi ulivyo mkubwa kuliko wa ibilisi

Lakini ukiwa ni mkristo, mvivu, Neno husomi ujue kabisa shetani ataendelea kukusumbua tu, haijalishi utakuwa ni mwombaji kiasi gani.

Hivyo zingatia hayo mambo mawili.

  1. Wokovu
  2. Neno

Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari leo, kumpa Yesu maisha yako, ili akusamehe na kukupa wokovu, na kuyafukuza maroho yote machafu yaliyokuvamia. Basi uamuzi huo ni wa busara sana kwako, ambao hautakaa uujutie milele.

Hivyo fungua hapa, kwa mwongozo wa sala hiyo>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Mjoli ni nani katika biblia?

Gombo ni nini?

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

Rudi nyumbani

Print this post

TATIZO LA VISIGINO KUUMA KIBIBLIA

Tatizo la visigino kuuma ni ishara ya nini kibiblia?..Au visigino kuwaka moto?.

1) Visigino kuuma.

Kama unafanya shughuli yenye kuhusisha miguu, kwamfano kulima au kutembea umbali mrefu, au michezo..basi ni jambo la kawaida visigino kuuma, au visigino kuwaka moto.

Suluhisho la tatizo hilo ni kupunguza shughuli hizo zinazohusisha miguu, na miguu itarudia hali yake.

Lakini kama huna shughuli zozote unazozifanya na umeenda hospitali na hujapata suluhisho, na hujui sababu, na pengine umeshafanyiwa hata na maombezi, na tatizo bado lipo palepale..

Basi suluhisho la tatizo hilo,linaweza kuwa la kimaandiko,na maandiko yafuatayo yatakufungua…

Yeremia 13:22 “Nawe ukisema moyoni mwako, Mbona mambo haya yamenipata mimi? Ni kwa sababu ya WINGI WA UOVU WAKO, marinda yako yamefunuliwa, na visigino vya miguu yako vimeumia”.

Jiangalie maisha yako ni wapi hapako sawa na Mungu..tubu makosa yako kwa Mungu kwa kumaanisha kuyaacha.

Angalia mahali unapofanyia kazi, au mahali unapoishi, jinsi unavyoenenda, tafakari mawazo ya mioyo yako, je yanampendeza Mungu?..

Je unao upendo?, Wewe ni mvumilivu, ni mtu wa kusamehe au wa vinyongo?, Je ni mtu unayemcha Mungu na kumwogopa?.

Kama sio basi hiyo ndio sababu kwanini visigino vyako vinauma, au vinawaka moto, na umekosa ufumbuzi kila mahali.

Litafakari sana hilo na Mungu akusaidie, yeye ni mwaminifu tukiungama dhambi zetu kwa lengo la kuziacha kabisa, anatusamehe na kuponya magonjwa yetu na majeraha yetu, kwasababu lengo lake sio sisi tuteseke, bali tuwe na furaha na tupate mema, ndio maana saa nyingine anaruhusu vitu fulani vitutokee ili tutubu, na mwishoni atubariki zaidi.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.

WITO WA MUNGU

Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)

Rudi nyumbani

Print this post