Category Archive Uncategorized

Fahamu Mithali 20:11 Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake;

SWALI: Nini maana ya Mithali 20:11 inaposema;

Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake; Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.


JIBU:  Mwandishi anatuonyesha kuwa tabia ya mwanadamu yoyote, huwa haijifichi kufuatana na umri wake, kwamba yaweza kukaa ndani  tu kipindi cha utotoni isionekane ikaja kudhihirika ghafla ukubwani. Hapana, anasema “Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake; Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili”.

Ikiwa na maana katika utoto ule ule unaweza kuuchunguza mwenendo wa mtoto, ukautambua. Na hiyo itakupa fursa ya kuurekebisha ukiwa ni mbaya, au kuuimarisha ukiwa ni mzuri, akiwa katika vipindi kile kile. Usione mwanao anayotabia ya udokozi, ukasema huyu ni mtoto tu, haelewi anachokifanya. Hapana unapaswa umrekebishe mapema, kwasababu hicho kitu kipo ndani yake, Ukiona mtoto anapenda kutazama biblia, anapenda kukaa kanisani, anapenda kusikiliza nyimbo za injili. Usiseme, huyu ni mtoto, ukampuuzia tu, kwa kuishia  kusema ‘ubarikiwe mwanangu’ kinyume chake, mwendelezee mazingira hayo, kwasababu mwelekeo wa maisha yake, ni huko.

Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo, tabia zake zilianza kuonekana tangu utotoni, wazazi wake walimstaajabia, kumwona  katika umri ule mdogo, yupo hekaluni, amekaa na waalimu na wakuu wa dini akiwauliza maswali, Kinyume chake wazazi wake hawakumkemea, bali waliyaweka yote mioyoni mwao, na kukubali kuutambua mwelekeo wa mtoto wao.

Hii ni kufundisha nini? 

Lipo funzo la rohoni, lakini pia la mwilini.

La mwilini ni kuwa yatupaswa tuwatazame watoto, bila kupuuzia kitendo chochote wanachokidhihirisha katika umri ule wa chini. Ikiwa ni chema tukipalilie, ikiwa ni kibaya, tukikemee, na kushughulika nacho kwelikweli kabla hakijaweka mizizi. Hivyo hakuna mzazi au mlezi anaweza kusema, huyu mwanangu kabadilika tu ghafla. Ukweli ni kwamba mabadiliko yalianza kuwepo tangu zamani, isipokuwa kwa namna moja au nyingine tulipuuzia, tulipoyaona ndani yao tukadhani ni tabia za utoto tu. Wazazi wanaowajenga wanao katika maadili na vipawa tangu utotoni, ukiwatazama watoto wao wanapokuwa watu wazima, huwa wanakuwa na ufanisi na ujuzi wa hali ya juu sana, zaidi ya wale ambao watajijengea wenyewe wanapokuwa watu wazima. Hivyo mzazi jali maisha ya kiroho ya mwanao.

Vilevile rohoni, wapo ambao ni wachanga kiroho. Ikiwa na maana katika kanisa ni wale ambao wameokoka hivi karibuni. Halikadhalika hawa nao utaweza kutambua karama zao, sio mpaka wawe wakomavu kiroho. Aliye Mwinjilisti, utaona anapenda kushuhudia, lakini pia anauwezo wa kuwavuta wengine kwa Bwana.  Aliye mwalimu, utaona anapenda sana kujifunza, aliye nabii, utaona karama za maono, ndoto, huwa zinamjia mara kwa mara, hata kwa namna ambazo hazielewi elewi, mwimbaji atapenda wakati mwingi kujifunza kuimba hata kama hawezi. Hivyo, kila mmoja wetu, kitu ambacho Mungu amekiweka ndani yake, hujidhihirisha mapema sana pindi ameokoka. Sio mpaka awe amekomaa sana kiroho kama wengi wanavyodhani.

Pindi unapookoka, kipindi hicho hicho karama yako inaanza kufanya kazi, unapachopaswa tu, ni kujishughulisha na utumishi wa Bwana, ndivyo utakavyoruhusu mambo hayo kutokea kwa wepesi na urahisi zaidi?

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

(TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

MAANA WEWE, BWANA HUKUWAACHA WAKUTAFUTAO”.(Opens in a new browser tab)

Rudi nyumbani

Print this post

WAFALME WALIOTAWALA ISRAELI.

Wafalme waliotawala ISRAELI, ukiwatoa wale watatu wa Mwanzo (Yaani Sauli, Daudi na Sulemani) walikuwa ni Wafalme 19 tu, na hakukuwa na Malkia aliyetawala Israeli kama ilivyokuwa kwa YUDA.

Kati ya Wafalme hao 19 waliotawala Israeli, hakuna hata mmoja aliyekuwa Mkamilifu mbele za MUNGU katika ukamilifu wote kama ilivyokuwa kwa baadhi ya Wafalme waliotawala YUDA. Isipokuwa Mfalme mmoja tu aliyeitwa YEHU ndiye angalau alionekana kufanya Mema lakini pia alifanya na Mabaya.

UFUATAO NI UFUPISHO KWA NJIA YA TAKWIMU.

JINAMIAKA ALIYOTAWALAMATENDOMAREJEO
1.YEROBOAMU22MABAYA1Wafalme 12:25-33
2.NADABU2MABAYA1Wafalme 15:25-31
3.BAASHA24MABAYA1Wafalme 15:33-16:7
4.ELA 2MABAYA1Wafalme 16:8-14
5.ZIMRI7MABAYA1Wafalme 16:15-20
6.OMRI12MABAYA1Wafalme 16:21-27
7.AHABU22MABAYA1Wafalme 16:29-33
8.AHAZIA2MABAYA1Wafalme 22:51-53
9.YORAMU12MABAYA2 Wafalme 1:17, 3:1-3
10.YEHU28Nusu Mema-
Nusu Mabaya
2 Wafalme 9:30, 10:36
11.YEHOAHAZI17MABAYA2 Wafalme 13:1-9
12.YEHOASHI16MABAYA2 Wafalme 13: 10-25
13.YEROBOAMU II41MABAYA2 Wafalme 14:23-29
14.ZEKARIA6MABAYA2 Wafalme 15:8-12
15.SHALUMUMwezi 1MABAYA2 Wafalme 15:13-16
16.MENAHEMU10MABAYA2 Wafalme 15:17-22
17.PEKAHIA2MABAYA2 Wafalme 15:23-26
18.PEKA20MABAYA2 Wafalme 15:27-31
19.HOSHEA9MABAYA2 Wafalme 17:1-7

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Rudi nyumbani

Print this post

WAFALME NA MALKIA WALIOTAWALA YUDA

Wafalme waliotawala YUDA ni 19, na Malkia aliyetawala YUDA ni Mmoja (1), hivyo kufanya jumla ya Watawala 20 kupita katika Taifa la Yuda.

Kati ya hao Wafalme 19; waliofanya MEMA ni Wafalme saba (7) tu, wengine 12 waliosalia walifanya Mabaya. Na Malkia Mmoja aliyetawala naye pia alifanya Mabaya, hivyo kufanya jumla ya watawala 13 waliofanya mabaya.

UFUATAO NI UFUPISHO KWA NJIA YA TAKWIMU.

Tafuta jina la Mfalme hapa >>

N/AJINAJINSIAMIAKA ALIYOTAWALAMATENDOMAREJEO
1.REHOBOAMUM17MABAYA1Wafalme 11:42
2.ABIYAM3MABAYA1Wafalme 14:31-15:8
3.ASAM41MEMA 1Wafalme 15:8-24
4.YEHOSHAFATIM25MEMA1Wafalme 22:41-51
5.YEHORAMUM8MABAYA2Wafalme 8:16-24
6.AHAZIAM1 MABAYA2Wafalme 8:24-29
7.ATHALIAK6MABAYA2Wafalme 8:26, 11:1-20
8.YOASHIM40MEMA2Wafalme 11:21,12:1-21
9.AMAZIAM29MEMA2Wafalme 14:1-22
10.UZIAM52Mwanzo Mema-Mwisho-Mabaya2Wafalme 15:1-7
11.YOTHAMUM16MEMA2Wafalme 15:32-38
12.AHAZIM16MABAYA2Wafalme 15:38-16:20
13.HEZEKIAM29MEMA2Wafalme 18:1-20
14.MANASEM55MABAYA2Wafalme 21:1-18
15.AMONI M2MABAYA2Wafalme 21:18-26
16.YOSIAM31MEMA2Wafalme 21:26-23:30
17.YEHOAHAZIMMiezi 3MABAYA2Wafalme 23:30-34
18.YEHOYAKIMUM11MABAYA2Wafalme 23:34- 24:6
19.YEKONIA/
YEHOYAKINI
MMiezi 3MABAYA2Wafalme 24:6-17
20.SEDEKIAM11MABAYA2Wafalme 15:24:17-25:30

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengineyo:

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kwa namna gani, haki yetu inapaswa izidi ya mafarisayo?

Bwana alimaanisha nini katika Mathayo 5:20 aliposema..

[20]Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. 

Ni haki ipi hiyo.

JIBU: Katika andiko hilo tunaona Bwana akiainisha kigezo cha mtu kuingia kwenye ufalme wa Mungu..kwamba kigezo chenyewe ni “HAKI” …

Haki ni kitu kinachomstahilisha mtu kupokea kitu fulani. Kwamfano tunasema mtoto ana haki ya kulindwa…ikiwa na maana kilichomsababishia apate haki ya kulindwa ni ile hali ya utoto wake.

Mfano mwingine, tunasema ni mtu mzima ana haki ya kuoa au kuolewa na mtu amtakaye, katika wakati auchaguaye yeye. Tafsiri yake ni kwamba kinachompa haki ya kuwa hivyo ni kwasababu yeye ni “mtu-mzima”. Angekuwa mtoto asingekuwa na haki hiyo.

Sasa tukirudi katika habari hiyo tunaona kilichowafanya waandishi na mafarisayo wajihesabie haki kwamba wao ni warithi wa ufalme wa mbinguni. Ilikuwa ni kuitimiza sheria kwa matendo yao. Ambayo kimsingi wao wenyewe hawakuweza kuishika..kwa nje walionekana sawa lakini ndani walikuwa mbali na sheria yao. Kwasababu hakuwahi kutokea mtu hata mmoja aliyeweza kumpendeza Mungu kwa matendo yake, yeye mwenyewe.

Hivyo njia yao ya kupata haki, ambayo ni kwa matendo ya sheria haikuwa sawa. Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake na wale waliomsikia kwamba haki “ yao” isipozidi ya mafarisayo na waandishi kamwe hawataweza kuuingia ufalme wa mbinguni.

Swali je ya kwao inapaswa iweje. Je ya matendo ya sheria zaidi ya yale au vinginevyo?

Haki Yesu aliyoileta ambayo itampelekea mtu kurithi uzima wa milele ni kwa njia yake yeye mwenyewe .Ambayo sisi tunahesabiwa haki kwa kumwamini, kama mwokozi wa maisha yetu. Bila kutegemea matendo yetu ya haki. Yaani ni haki tuipatayo kwa neema.

Hivyo, wote wanaoipokea haki hiyo basi uzima wa milele ni wao. Na kwasababu ndio njia ambayo sisi tutamfikia Mungu. Basi neema yenyewe inatufundisha pia kuyazaa matunda ya Roho. Na hivyo tunaitimiza sheria ya Mungu mioyoni mwetu bila unafiki. Mbali na mafarisayo ambao walitegemea akili zako na nguvu zao.

Hata sasa ikiwa unategemea jitihada zako, zikupe haki mbele za Mungu, ndugu umepotea. Hutaweza Itegemee neema ya Mungu. Na hiyo itakusaidia kuyatimiza hayo mengine kwa Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

Nini maana ya kumsulibisha mwana wa Mungu mara ya pili?

Rudi nyumbani

Print this post

Isaya 40:12 ‘maji kwa konzi ya mkono, na mbingu kwa shubiri’

SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya Isaya 40:12 inaposema maji kwa konzi ya mkono, na mbingu kwa shubiri?

Isaya 40:12 “Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake, na kuzikadiri mbingu kwa shubiri, na kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi, na kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani”?


 JIBU: Ukianzia kusoma vifungu vya juu na kuendelea vile vya chini, utaona Mungu anawaambia watu wake Israeli kuwa atawajilia kama mchungaji awachungaye kondoo wake , na kuwalisha, na kuwakuongoza, na kuwakusanya kifuani mwake, hata wale walio wachanga, ndivyo atakavyowatendea watu wake na hilo litawezekana.

Lakini Israeli waliona kama jambo hilo linaweza lisiwe rahisi, Ndio hapo akawaambia sasa katika vifungu vifuatavyo maneno hayo. Kwamba “Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake”? Maji anayoyazungumzia hapo ni maji mengi, mfano wa bahari, na maziwa Je! Kuna mtu yeyote anayeweza kuyakusanya maji mengi namna hiyo kwenye viganja vyake? Jibu ni hapana! Lakini kwa Mungu ni jambo dogo sana.

Vilevile anawauliza ni nani awezaye ‘kuzikadiri mbingu kwa shubiri’?. Shubiri ni kipimo cha urefu, wa kiganja, toka kidole gumba mpaka kile cha katikati vinaponyooshwa. Na ni wazi hakuna mtu anayeweza kupima ukubwa wa mbingu, toka sayari moja hadi sayari nyingine, kwa kipimo chochote kile cha kibinadamu. Lakini kwa Mungu hilo ni jambo dogo sana, ni kama kuzipima kwa shubiri.

Halikadhalika anauliza  ni nani awezaye kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi?. Pishi ni kopo dogo, je kuna mwanadamu anaweza kuyakusanya mavumbi yote duniani, kama vile akusanyavyo yale machache kwenye kopo lake. Ni wazi hakuna awezaye kuwa na pipa la uwezo huo.

Vilevile anauliza ni nani anayeweza kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani?. Je! Kuna mizani yoyote ya kibinadamu inaweza kuiweka milima juu yake, na kutoa vipimo?. Jibu ni hakuna. Lakini kwa Mungu ni jambo dogo sana. Milima ni kama vipunje vidogo sana vya mchanga.

Ikiwa haya yanaonekana magumu kwa mwanadamu, lakini kwa Mungu ni mepesi. Vivyo hivyo jambo la kuwakusanya watu wake, au kuwasaidia, lisitizamwe kibinadamu, kwasababu uweza wa Mungu ni mkuu sana usioweza kufikirika kibinadamu. Maswali ya namna hii ndio kama yale Mungu aliyokuwa anamuuliza Ayubu, (Ayubu 38-41), na katika Mithali 30:4

Yesu kama mchungaji wetu mkuu, anauwezo wa kutukusanya kama kondoo wake. Haijalishi tutaonekana tumetawanyika mbali kiasi gani, lakini akisema jambo ni lazima liwe. Halikadhalika na katika mambo yetu yote ya kiroho na kimwili.

Hivyo kitabu cha Isaya sura ya 40 yote, kinaeleza uweza wa Mungu, usiopomika kibinadamu. Lakini Swali ni Je! Kristo amekusamehe dhambi zako? Kama ni la! Basi nafasi bado unayo leo. Mwamini yeye akuokoe. Na kukupa ondoleo la dhambi zako.

Kwa mwongozo wa namna ya kupokea wokovu basi fungua hapa>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

Kuna Mbingu ngapi?

Mbinguni ni sehemu gani?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya 1Wakorintho 4:7?

SWALI: Naomba kufahamu maana ya 1Wakorintho 4: 7 

Maana ni nani anayekupambanua na mwingine? Nawe una nini usichokipokea? Lakini iwapo ulipokea, wajisifia nini kana kwamba hukupokea?


JIBU: Ukianza kusoma tokea sura ya kwanza utaona Paulo, anakemea sana baadhi ya tabia ya matengano ambayo ilionekana katika kanisa hili la wakorintho. Iliyozuka kutokana na aina ya mafundisho au utendaji kazi wa waasisi wa huduma, au waliowabatiza, na sana sana kati ya Paulo na Apolo.

Hivyo matabaka haya yakawafanya wajivunue wanadamu, na mafundisho yao. Bila kufahamu kuwa kanisa ni la Kristo na si la wanadamu.

Ndipo Paulo, akaweka wazi kuwa kila mmoja aliitwa kwenye utumishi wa Kristo Yesu, ambao una mchango wake katika kanisa, lakini si kwamba huduma ya mmoja ni bora kuliko nyingine. Akasema mmoja anapanda mwingine anatia maji, lakini mkuzaji ni Mungu.

Sasa katika vifungu hivi anaendelea kuwaambia tabia ya kupambanua watumishi, au huduma, si sawa.  Ndio hapo anasema “Nawe una nini usichokipokea?. Akiwa na maana je! Kuna kipawa gani, au kitu gani chema katika kanisa ambacho hawakukipokea kutoka kwa Mungu,?

Lakini anasema..

Iwapo ulipokea, wajisifia nini kana kwamba hukupokea?. Yaani kama vyote vilitoka kwa Mungu na sio kwa wanadamu, mbona basi mnajisifia kana kwamba vimekuja kwa uweza wa kibinadamu?.

Kama tumepewa kwa neema iweje sasa tujisifie, kana kwamba tumevipokea kwa nguvu zetu na utashi wa watumishi wetu, na ukuu wao, na uwezo wao wa kuhubiri vizuri? Karama hizi za rohoni hakuna hata mmoja imetoka kwa mwanadamu, wenyewe wamefanyika vyote tu. Hivyo wa kujivunia hapo na kusifiwa hapo ni Mungu wala si Paulo au Apolo.

Jambo ambalo hata leo huonekana kwa baadhi ya watu wa kanisa la leo. Ikiwa tuna msingi katika Kristo, iweje kujivunia makanisa au huduma, na kujiona sisi ndio bora zaidi ya wale wengine?

Ni kweli zipo huduma ambazo si za kweli, hazina msingi sahihi wa Kristo Yesu. Lakini ikiwa wote Injili yetu ni ya Kristo aliyesulubiwa kutukomboa sisi, basi tofauti za kiutendaji kazi, au kiujuzi, zisitufanye tujione bora, kwasababu sio hao wanadamu walitoa hivyo vipawa bali ni Roho Mtakatifu. Na anatenda kazi kama apendavyo yeye, anampa huyu hiki, anampa Yule kile.

Mmoja atapanda, mwingine atatia maji, mwingine mbolea, mwingine mvunaji, lakini atakuzaye ni Mungu mmoja, katika shina la Yesu Kristo Bwana wetu.

Kama mkristo ukijiona una vita vya kiuhuduma, ujue bado ni mchanga kiroho, bado unatabia za mwilini.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Rudi nyumbani

Print this post

Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.(Yakobo 5:9)

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema “Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango”.

Yakobo 5:9  Ndugu, msinung’unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.


JIBU: Neno la Mungu halitoi nafasi ya sisi, kunung’unikiana kwasababu yoyote. Aidha ya kuonewa, au kudhulumiwa, kuaibishwa au kufanyiwa jambo ambalo halikupasa utendewe, Manung’uniko ni zao la kutokuwa na uvumilivu. Na kwamba tukifanya hivyo basi, tafsiri yake ni kuwa tunamfanya Mungu naye aghahiri uvumilivu wake kwetu.

Lakini anatoa, suluhisho, kwamba hayo tuyaache mikononi mwake. Kwasababu yeye ndio mwamuzi wetu. Na kwamba, sio tu mwamuzi lakini  ni mwamuzi ambaye yupo mlangoni. Akiwa na maana kuwa Kristo yupo karibu sana na maonevu, au dhuluma hizo, na kwamba yeye mwenyewe atalipa, wala hatakawia, kwasababu yupo mlango.

Atalipa aidha kwa wakati huu huu duniani,  au siku ile ya mwisho wa Hukumu. Kwake yeye ni lazima haki itendeke. Pia kwa upande mwingine anataka uogope kwasababu ukinung’unika yeye hayupo mbali kukusikia.

Wafilipi 4:5  Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, popote tusimamapo kutoa malalamiko, laumu, kuhesabu makosa, n.k. basi tutambua kuwa Kristo yupo hapo hapo katikati yetu kutusikia. Hivyo tusiwe wepesi ya kunena, bali tujifunze kuwa wavumilivu katika mambo yote. Ili Mungu atuachilie neema yake.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je, umebatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo? Kama ni hapana, basi wakati ndio huu, tubu dhambi zako, kwa kumwamini Yesu upokee ondoleo la dhambi zako, Na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu.

Ikiwa upo tayari kumkabidhi leo maisha yako. Basi  fungua hapa kwa mwongozo huo. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MWAMUZI WA KWELI:

“Kinga kilichotolewa motoni “Kinafunua nini kibiblia?

Bwana Yesu alikuwa anamaanisha nini kusema Marko 2:19″walioalikwa harusini wawezaje kufunga maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao?”

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Rudi nyumbani

Print this post

NI YESU YUPI UNATEMBEA NAYE?

NI ALIYEFIFIA MAVAZI AU MWENYE MAVAZI MEUPE?

Yesu anajifunua kwa watu kulingana na jinsi mtu huyo anavyotembea naye. Wapo watu wanatembea na Bwana Yesu katika mng’ao wake wa ajabu. Lakini wapo wanaotembea naye katika hali ya kawaida sana. Utajiuliza kwa namna gani.

Wakati mwingi sana, Yesu alipokuwa na wanafunzi pamoja na makutano. Zaidi ya asilimia 98 ya maisha yake, alikuwa hana tofauti na watu wengine wowote. Kiasi kwamba akijichanganya kati ya watu 10, huwezi mtofautisha na yoyote, kimwonekano. Ndio maana wengi, walishindwa kumngundua, alipokuwa na watu soma (Yohana 18:7).

Lakini kuna wakati, alibadilika sura, mpaka mwonekano wake. Tutaona ni nini kilichomfanya awe vile jambo lililowafanya mitume wake kumchukulia kitofauti sana tangu ule wakati.

Marko 9:2  “Hata baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani, peke yao; akageuka sura yake mbele yao; 3  mavazi yake yakimeta-meta, meupe mno, jinsi asivyoweza dobi duniani kuyafanya meupe.

4  Wakatokewa na Eliya pamoja na Musa, nao walikuwa wakizungumza na Yesu. 5  Petro akajibu, akamwambia Yesu, Rabi, ni vizuri sisi kuwapo hapa; na tufanye vibanda vitatu, kimoja chako wewe, kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya. 6  Maana, hakujua la kunena, kwa kuwa waliingiwa na hofu nyingi.

7  Kisha likatokea wingu, likawatia uvuli; sauti ikatoka katika lile wingu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, msikieni yeye. 8  Mara hiyo walipotazama huku na huku, hawakuona mtu pamoja nao ila Yesu peke yake.

9  Na walipokuwa wakishuka mlimani aliwakataza wasimweleze mtu waliyoyaona, hata Mwana wa Adamu atakapokuwa amefufuka katika wafu”.

Sababu iliyowafanya Petro, Yohana, na Yakobo, kumwona Bwana katika mwonekano ule. Ni mahali walipokwenda naye. Walikwenda naye mlimani “KUOMBA”. Maombi ndio yaliyopelekea, Yesu abadilike ghafla mbele yao na kuwa na ule utukufu wake wa asili.

Vivyo hivyo na sisi ili tumwone Kristo katika utukufu wake mkamilifu katika maisha yetu, Tupende maombi. Ukiwa mvivu katika kuomba, Yesu atakuwa ni wa kufifia maishani mwako. Hutafurahia uweza wake mtimilifu katika maisha yako, hutafurahia wokovu wako. Mfanye awe kama JUA kwako, ang’ae kweli kweli, mpe nafasi kwasababu yeye ndio Nuru ya ulimwengu. Penda maombi, kila siku omba, kutana naye hapo, hudhuria mikesha sana, omba kwa bidii, ondoa uvivu.

 Usipomruhusu Yesu akupangie maisha yako, kimaombi, shetani atakusaidia kuyapanga.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

FAIDA ZA MAOMBI.

USIYAACHE MAVAZI YAKO NA KWENDA UCHI!

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 6:30 Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha

SWALI: Je!  Mithali 6:30 inamaana gani?

Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha, iwapo aona njaa;  31 Lakini akipatikana, atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake.

JIBU: Chukulia mfano mtu hajala siku tatu, halafu akaona kuna duka lipo wazi pale jirani, na mwenyewe ametoka, akashawishika kuingia haraka  na kubeba mkate, ili akale. Lakini mwenye duka aliporudi na kuona mkate umeibiwa, alianza kumfuatilia, mwishowe akamkuta amejificha mahali Fulani anakula akiwa katika hali mbaya.

Kibinadamu, atakapoona hali halisi ya mwizi, huwenda ataishia kukasirika tu, au kumgombeza, au kwenda kumwajibisha, kwa mambo madogo madogo. Kwasababu anaona alichokifanya ni kwa ajili ya kusalimu maisha yake tu, ale asife, lakini sio kwa lengo la kuchukua vya watu, akauze, au kuleta hasara kwa wengine.

Lakini sehemu ya pili ya mstari huo anaendelea kusema kama “akipatikana atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake”.

Maana yake ni kuwa kama “atapatikana na kosa”, basi atalipa mara saba. Atagharimikia vyote alivyoviiba mara saba. Sasa kauli hiyo haimaanishi kwamba mwizi huyo huyo aliyeiba kwa ajili ya kujishibisha tumbo lake ndio atalipa mara saba, hapana, vinginevyo mstari huo ungekuwa unajipinga unaposema “watu hawamdharau mwizi akiiba kwa kujishibisha”, bali  anamaanisha kama akipatikana na hatia tofauti na hiyo..mfano aliiba vitu ili akauze, aliiba fedha ili akajiendeleze kwenye mambo yake, alete hasara kwa wengine. Huyo atalipa gharama zote mara saba.

Ndio maana utaona adhabu nyingi za wezi huwa ni kubwa sana zaidi ya vile walivyoviiba, wanapigwa faini kubwa, wengine mpaka wanauliwa, kwa wizi tu mdogo. Hapo ni sawa na wamelipa mara saba.

Je! Hili linafunua nini rohoni?

Kama njaa ya mwilini, inaweza kumfanya mwizi asihesabiwe kosa. Kwasababu watu wanaelewa umuhimu wa kunusuru uhai kwa chakula, vipi kuhusu rohoni. Hata kuna wakati Daudi alikula mikate ya makuhani ambayo  hawakupaswa watu wengine kula, lakini kwasababu alikuwa na njaa yeye na wenzake haikuhesabiwa kwake kuwa ni kosa (1Samweli 21).

Vivyo hivyo rohoni, Mungu anatufundisha sio kwamba tuwe wezi, hapana, lakini anataka tuthamini sana roho zetu, pale zinapokuwa hazina kitu, zina njaa. Iweje mtu unakaa hadi unakufa kiroho halafu unaona ni sawa kuwa hivyo hivyo kila siku. Hufanyi jambo Fulani la kujinasua katika hiyo hali yako mbaya rohoni, unaendelea tu hivyo hivyo. Tafuta kwa bidii chakula cha kiroho usife ndugu. Jibidiishe.

Iba muda wako wa kufanya mambo mengine ili ukipate chakula cha kiroho. Ni kweli ulipaswa kuwepo mahali Fulani pa muhimu, embu ghahiri muda huo, nenda kasome biblia, nenda kaombe, nenda kasikilize mahubiri yatakayokujenga. Ulipaswa uwepo kazini, lakini kwasababu ibada ile ni muhimu embu usione shida kughahiri.

Huna biblia Iba hata pesa yako ya matumizi ya muhimu kanunue, acha uonekane mjinga nenda kanunue biblia au vitabu vya rohoni vikujenge. Tafuta ile MANA iliyofichwa.

Siku hizi ni za mwisho. Na Bwana alishatabiri duniani kutakuwa na njaa, sio ya kukosa chakula au maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Mungu ya kweli. Usipojiongeza katika eneo la ukuaji wako kiroho.  Ni ngumu kuvuka hizi nyakati mbaya  za manabii wengi wa uongo, na mafundisho ya mashetani. Usipoyajenga maisha yako ya kiroho, shetani akusaidie kuyajenga kwake.

Amosi 8:11 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana”

Penda biblia, penda kujifunza, penda maombi zaidi ya vingine.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.

NJAA ILIYOPO SASA.

(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

(Opens in a new browser tab)KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.(Opens in a new browser tab)

Rudi nyumbani

Print this post

KIMBIA MACHAFU YA DUNIA. (2Petro 2:20)

2 Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia MACHAFU YA DUNIA kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza”. 

Mstari huo unatupa uelewa kwamba kumbe tukimjua mwokozi wetu Yesu Kristo, ni lazima kuambatane na kuyakimbia machafu ya dunia. Haiwezekani mtu akamjua Yesu Kristo halafu asiyakimbie Machafu ya dunia Kwa mujibu wa huo Mstari.

Machafu ya dunia ni yapi?

Machafu ya dunia ni Yale mambo maovu uliyokuwa unayafanya ulipokuwa mwenye dhambi, mfano ulevi, uzinzi, wizi, ushirikina, anasa, utoaji mimba, ulawiti,  n.k.

Sasa ikiwa ukinaswa, na kushindwa kutoka huko, maandiko yanasema hali yako ya mwisho inakuwa mbaya kuliko Ile ya kwanza, maana yake kama ulikuwa ni mgonjwa kidogo, kutokana na madhara uliyoyapata katika Ile dhambi, basi ugonjwa unakuwa mara dufu zaidi, kama ulikuwa unaweza kujizuia usilewe mara Kwa mara, basi nguvu ya ulevi inakulemea mara mbili unakuwa mlevi yule wa kupindukia kabisa kabisa.. hiyo ni kutuonyesha ni jinsi gani tunapaswa tuwe makini kama vile maandiko yanavyosema  pindi tuokokapo tuutimize wokovu wetu Kwa kuogopa na kutetemeka.

Wafilipi 2:12  “Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Bwana Yesu alitumia mfano wa Yule mtu ambaye alikuwa na pepo, lakini alipomtoka hakujiweka sawa, matokeo yake ikawa ni Yule pepo kuchukua pepo wengine saba waovu kuliko yeye, na hali yake ya mwisho ikawa mbaya kuliko ile ya kwanza. (Mathayo 12:43)

Lakini ikitokea tayari umeshaanguka kwenye machafu ya dunia, ambayo uliyaacha huko nyuma. Je ufanyaje?

Ni kutubu haraka sana. Angali nafasi unayo. Kumbuka hapo anasema “akinaswa na kushindwa”

Maana yake ni kuwa kama umenaswa, ni kufanya hima ujinasue kabla mwindaji wako (ibilisi), hajakuweka mikononi mwako kabisa kabisa. Lakini ukishindwa.basi Ndio mwisho wako umefika.

Ikiwa ulirudia uzinzi, ulirudia ulevi, ulirudia anasa, ulirudia kujichua, kutazama picha chafu mitandaoni.. Acha haraka sana, toka huko kwa kasi zote, jitakase kwa Bwana, kisha maanisha kumfuata Yesu, huku ukiutimiza wokovu wako kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu huo tumekabidhiwa mara moja tu.

Na Bwana atakurehemu.

Bwana akubariki.

Ikiwa bado hujaokoka na utapenda leo kumpokea Kristo maishani mwako. Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?

MFALME ANAKUJA.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

Rudi nyumbani

Print this post