Category Archive Uncategorized

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Bwana Yesu alitupa dalili za kurudi kwake, akatuambia mkiona dalili Fulani Fulani kama vile matetemeko, mlipuko wa magonjwa, manabii wa uongo, vita n.k. Basi tujue yupo mlangoni kurudi. Lakini kamwe hakutupa dalili ya SIKU yenyewe atakayorudi itakuwaje.. Na hiyo ndio hatari Zaidi kwasababu watu wengi leo hii japokuwa wanajua Yesu atarudi siku yoyote kutokana na kuwa dalili hizo zimeshatimia zote, Lakini bado wanachunguza chunguza siku yenyewe, wakidhani  labda watashtukia lolote.

Bwana Yesu alisema siku ya kuja kwake, inafanana na siku zile za Nuhu, Siku zile mpaka Nuhu anaingia kwenye Safina hakuna mtu yeyote alitambua kuwa tayari Mungu ameshaihukumu dunia.. mpaka zikapita siku saba, nyingine ndipo mvua ya gharika ikashuka kwenye dunia.

Mathayo 24:38 “Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina,

39 WASITAMBUE, HATA GHARIKA IKAJA, IKAWACHUKUA WOTE, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.

40 Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;

41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.

42 Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu”.

Unaona? Leo hii, kama wewe sio “bibi-arusi” wa kweli wa Kristo, nikimaanisha, kama sio mkisto aliyesimama katika wokovu kweli kweli, usitazamie utatambua lolote siku  Kristo anarudi kuwanyakua watakatifu wake. Kwasababu hata Bibi-arusi wake mwenyewe hatojua siku hiyo itakavyokuwa sembuse wewe?..

Na ndio maana aliwaambia mpaka na wateule wake, kwamba wajiweke tayari, waifanye kazi yake, watimize wajibu wao walioitwa hapa duniani wa kuitangaza injili yake, kwasababu saa wasiodhani ndio atakayokuja..

Mathayo 24:43 “Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.

44 Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika SAA MSIYODHANI MWANA WA ADAMU YUAJA.

45 Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?

46 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47 Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.”

Hakuna mtu atakayeitambua siku hiyo, itakuja ghafla tu bila hodi, hakuna dalili yoyote itakayotutambulisha, itakuwa kama tu ilivyo leo, au jana,  wakati ambapo watu wanapanga mipango yao ya kimaisha, wanalijenga taifa lao, wanauza pombe, na kufanya biashara hapo hapo, Unyakuo unapita , mmoja anatwaliwa mmoja anaachwa..

Watu wengi sana wataingiwa na butwaa, wakisema mbona Bwana hakutupa taarifa au kiashirio fulani, mbona, angani hakukuonekana chochote, mbona tulitazamia jambo Fulani kwanza tulione, ndio unyakuo upite, imekuwaje, amesharudi, wakati watu wengine hawajahubiriwa bado injili. Lakini ndio hivyo tayari watakatifu wameshaondolewa.

Wakati huo upo karibu sana ndugu yangu, ridhika na dalili tunazoziona, kwasababu hakutakuwa na nyingine Zaidi ya hizo zilizoandikwa kwenye biblia.  Usidhani malaika atatokea hapo mawinguni kutuhubiria injili kwamba kesho Yesu ndio anarudi.

Kama utakosa unyakuo, basi ujue, utakuwa katika majuto na vilio na kusaga meno kusikokuwa kwa kawaida. Majuto hayo, unaweza ukayaona sio kitu leo kwasababu bado hayajakukuta, lakini  subiri siku hiyo ikufikie, hutatamani uishi. Hicho kiburi cha uzima ulichonacho leo, siku hiyo kitayeyuka chote, utamtafuta Mungu hutamwona. Utalia hakuna atakayekusikia, makanisa yatakuwa hayana faida yoyote kwako. Hakuna chochote kitakuwa na maana kwao, kwasababu hata pesa hazitafanya kazi wakati huo.

Ndugu, ndani ya hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho bado unayo nafasi ndogo sana ya kutubu, Tubu leo kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako, na Kristo atakupokea.

Shalom.

Kumbuka katika saa usiyodhani Kristo anakuja!

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

Je! ile habari ya watu wawili wenye pepo inajichanganya?

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

MATESO YA KUZIMU.

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA VILE UMEME UTOKAVYO MASHARIKI UKAONEKANA HATA MAGHARIBI.

Ni kipi kinakupa ujasiri wa kuishi ukristo ya juu juu tu ndugu ?

Bwana atusaidie tujue majira tunayoishi..

Ulishawahi kutafakari kwa makini kwanini Bwana alifananisha kuja kwake na umeme? Kama tunavyosoma katika kitabu cha  Mathayo 24:27-28

“Kwa maana kama vile umeme utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.

28 Kwa kuwa po pote ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai”.

Umeme unaozungumziwa hapo sio huu wa transforma unaowaka majumbani, hapana, ni ule wa radi tunaouona sana sana wakati wa mvua, ule mwanga, unaomulika kwa ghafla sana bila hodi, ambapo kwa kawaida ukimulika mara moja usiku, mahali hapo panabadilika unaweza ukadhani ni mchana, kwa jinsi unavyoangaza sana ..

Ndivyo Bwana Yesu alivyoifananisha na siku ya kurudi kwake kuja kulichukua kanisa, Nuru yake itamulika ulimwenguni kote kwa muda mfupi sana, ambao hakuna mwanadamu yoyote anaweza kuutazamia, na Nuru hiyo itamulika, kwa wakati mmoja ulimwenguni kote, kama vile mwanga wa radi unavyoonekana mashariki mpaka magharibi kwa wakati mmoja.

Kipindi hicho, ambacho kipo karibuni kutokea, Yesu atafunua siri ambazo, zitatuandaa moja kwa moja kwa ajili ya kwenda katika unyakuo. Na siri zenyewe hazijaandikwa hata kwenye biblia, kwasababu hakukuwa na umuhimu wa kuandikwa kwasababu, si za wakati wote, bali za wakati maalumu. Ambao ndio huo wa kurudi kwake kulinyakua kanisa lake.

Utauliza maneno hayo tumeyajulia wapi.?

Kumbuka, sikuzote, mwanga wa radi unapowaka angani, kinachofuata huwa ni Ngurumo. Hivi vitu viwili huwa vinakwenda pamoja. Sasa wakati huo ambao Kristo atakapoangaza Nuru yake ulimwenguni kote kwa kipindi kifupi sana.. Kutaambata na NGURUMO za rohoni,. Ndio zile ngurumo SABA zinazozungumziwa katika kitabu cha Ufunuo sura ya 10.

Ngurumo hizo Yohana alizisikia zikitoa sauti zao, lakini alipotaka kuziandika kwa ajili yetu sisi, alisikia sauti ikimwambia asiziandike bali azitie muhuri..Tusome.

Ufunuo 10:3 “Naye akalia kwa sauti kuu, kama simba angurumavyo. Na alipolia, zile ngurumo saba zikatoa sauti zao.

4 Hata ngurumo saba zilipotoa sauti zao, nalikuwa tayari kuandika. Nami nalisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Yatie muhuri maneno hayo yaliyonenwa na hizo ngurumo saba, usiyaandike”.

Umeona? Hizo ni jumbe, maalumu ambazo Kristo atazifunua kwa kanisa lake safi, kwa watu maalumu siku hizi za mwisho, wakati huo ambao MWANGA huo utamulika duniani kote. Hatujui ni nini Yesu kakiandaa kwa watu wake, lakini mpaka hakijafunuliwa sasa, ni kuonyesha kuwa ni mambo ya ndani sana ya siri, ambayo hayo ndio yatampa bibi-arusi wa Kristo Imani ya kwenda katika unyakuo.

Sasa mwanga  huo wa rohoni ukishamulika ulimwenguni kote, kama upo nje ya Kristo, basi ujue unyakuo utakupita tu, kwasababu hutaweza kuelewa hata Sauti ya hizo ngurumo saba zitakazonenwa ulimwenguni baada ya hapo.

Utauliza tena hilo tumelijuaje?

Ni kama tu kipindi kile cha Bwana Yesu sauti ilitoka juu mbinguni kuzungumza na makutano yaliyokuwa yanamfuata, lakini kwasababu NURU ilikuwa imeshawapita walichobakia kusikia tu ni ngurumo badala ya Sauti , ndivyo itakavyokuwa siku hiyo..

Yohana 12:28 “Baba, ulitukuze jina lako. Basi ikaja sauti kutoka mbinguni, Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.

29 Basi mkutano uliosimama karibu wakasikia, walisema ya kwamba kumekuwa ngurumo; wengine walisema, Malaika amesema naye.

30 Yesu akajibu, akasema, Sauti hiyo haikuwako kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu”.

Na ndio maana leo hii unaposisitizwa umtafute Kristo, maadamu muda mchache umebakia, wewe unachukulia mambo rahisi rahisi tu unadhani siku hiyo utaweza kuelewa kitu. Yesu alilijua hilo na ndio maana akatuambia, tujitahidi sasa kwa sababu upo wakati watu wengi watatamani waingie lakini wasiweze..wakati wenyewe ndio huo wakati wa NURU ya mwisho. Kwasababu itamulika kwa haraka sana kama vile radi, hatujui matukio hayo yatachukua muda gani pengine siku kadhaa tu, au wiki kadhaa tu, na kila kimekwisha.

Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako”;

Mimi sijui unasubiria nini, usiokoke, Wewe unadhani mambo yataendelea kuwa hivi milele? Hujui kuwa hii injili hadi sasa ingepaswa iwe imesharudi Israeli, maandalizi yao yapo tayari, usiku na mchana wanamlilia YEHOVA pale Yerusalemu kwenye ukuta ule wa maombolezo,  kuomba warudishiwe ufalme, lakini sisi tumekaa tu tukidhani, neema hii tutakuwa nayo milele.

Ni vizuri tukajua agenda ya Mungu kwetu ni ipi sisi watu wa mataifa, inashangaza kuona mkristo anachojua ni kutabiriwa tu, na injili za kupokea, na mafanikio ya mwilini basi hana habari na mambo ya ufalme wa mbinguni. Inahuzunisha sana.

Biblia inatuambia “utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.

Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu”, (Wafilipi 2:12-13)

Kumbuka: UMEME na NGURUMO vipo mbioni.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SIKU ILE NA SAA ILE.

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

UFUNUO: Mlango wa 14

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Mego ni nini kama tunavyosoma katika biblia? (Mithali 17:1)

Mithali 17: 1 Afadhali mego kavu pamoja na utulivu, Kuliko nyumba yenye karamu nyingi pamoja na magomvi.


JIBU: Mego ni neno linalotokana na  kitenzi “mega”,(kumega) kitu kilichomegwa, ni kama kimenyofolewa sehemu Fulani kwa udogo sana. Kwa lugha rahisi tunaweza kusema ni kitu kidogo sana.

Sasa hapo anaposema Afadhali mego kavu, anamaanisha afadhali chakula kidogo sana (Mfano wa mkate mkavu), pamoja na utulivu, au amani, au furaha, kuliko nyumba yenye karamu nyingi pamoja na magomvi, hasira, wivu, fitna, yaani, nyumba ambayo, utapata kila kitu, utakula chakula chenye mboga saba mezani, utakunywa kila aina ya kinywaji, lakini nyuma yake kuna vikwazo, na mafarakano.

Hiyo inatufundisha pia katika mambo ya Maisha, ni heri ufanye kazi mahali utalipwa mshahara mdogo lakini, utapata nafasi ya kutulia na Mungu wako, au utafanya kazi halali itakayokupa amani, kuliko kukimbilia kazi zenye mishara mikubwa, lakini nyuma yake inakukosesha, au haikupi muda wa kutosha kumtafakari Mungu wako.

Na ndio maana sehemu nyingine biblia  inatumia neno “konzi” ikiwa na maana kipimo cha mkono tu, uridhike nacho kuliko vipimo vingi lakini unataabika rohoni na mwilini.

Mhubiri 4:6 “Heri konzi moja pamoja na utulivu, Kuliko konzi mbili pamoja na taabu; na kujilisha upepo”.

Kabla hatujaamua jambo lolote tunapaswa tujihakikishie kwanza usalama wa roho zetu, si kila aina ya fursa inayokuja mbele yetu ni ya kuikimbilia kisa tu inatupa donge nono, au inatupa Maisha mazuri. Wengi wamerudi nyuma kiimani, kama sio kuupoteza wokovu wao kabisa kisa tu tamaa ya “VINGI” au Tamaa ya mali.

Yupo mtu mmoja aliacha kazi ya uchungaji alioitiwa na Mungu, kisa tu haimlipi vizuri, akaingia katika biashara, akaanza kufanikiwa na kuzidi, mpaka akawa anaenda China kuleta mzigo, sikumoja akiwa njiani anaelekea katika miradi yake Daresalaam, akapata ajali mbaya sana, akafa.

Jiulize huko anatapokwenda atakuwa mgeni wa nani?

Hivyo na wewe ridhika na kile unachokipata hata kama ni mego kavu, maadamu  kinakupa amani, na Muda kwa Mungu wako. Ridhika tu na hicho, hapa duniani tunapita.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

Rudi nyumbani

Print this post

MUNGU HAONI SHIDA KUMUHAKIKISHIA MWOVU ULINZI.

Baada ya Kaini kumuua ndugu yake, na Mungu, kumlaani kwa laana ile ya kwamba atakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani, utaona alimwomba Bwana ampunguzie adhabu yake, na baada ya kupunguziwa kwa kutiwa alama, haikuishia hapo,  bado Mungu alimuhakikishia usalama mwingine wa juu Zaidi.  Tusome;

Mwanzo 4:14 “Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.

15 Bwana akamwambia, KWA SABABU HIYO YE YOTE ATAKAYEMWUA KAINI ATALIPIZWA KISASI MARA SABA. Bwana akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga”.

Unaona hapo kwenye mstari  wa 15, Bwana akimuhakikishia ulinzi wa kipekee sana. Jambo ambalo si rahisi mtu mwovu kufanyiwa na mtu yeyote, kwasababu hakuna tendo lolote la kishujaa alilotenda Kaini mpaka alipiziwe kisasi mara saba, kwa yeyote atakayemuua,ni heri ingekuwa ni mara moja, lakini mara saba, hiyo angepaswa afanyiwe mtu mwenye haki.

Tengeneza picha diktekta, ambaye ameshutumiwa kwa mauaji wa maelfu ya watu, kama vile HITLER wa ujerumani, leo hii, unasikia Mungu anasema mtu yeyote atakayemuua Hitler atalipizwa kisasi mara saba, unaweza kudhani Mungu anafurahishwa na maovu. Ndivyo ilivyokuwa kwa Kaini, Mungu haoni shida kumuhakikishia mwovu ulinzi na mafanikio. Hilo tunapaswa tulijue.

Lakini afadhali ingeishia kwa Kaini tu, Tabia yake ya uuaji iliendelea mpaka kwa uzao wake. Utaona yupo mmoja aliitwa, Lameki, yeye alikuwa muuaji kuliko hata baba yake, anasema alimuua mtu kwa kumtia jeraha tu, alimuua mtu kwa kumchubua tu, akiwa na maana mtu aliyemkosea  kwa jambo dogo sana alikuwa  radhi kumuua, bila kujali chochote.

Huku akitumia kivuli kile kile cha baba yake, cha usalama aliohakikishiwa na Mungu, tena na Zaidi, anasema kama ikitokea mtu atataka kumlipizia kisasi kwa uuaji wake, basi akumbuke kuwa Mungu atamlipizia sio tu mara saba, bali mara saba sabini.

Mwanzo 4:23 “Lameki akawaambia wake zake, Sikieni sauti yangu, Ada na Sila; Enyi wake za Lameki, sikilizeni usemi wangu; Maana nimemwua mtu kwa kunitia jeraha; Kijana kwa kunichubua;

24 Kama Kaini akilipiwa kisasi mara saba, Hakika Lameki atalipiwa mara sabini na saba”.

Unaona? Walikuwa wanajiamulia kufanya mauaji tu kama vile kuchinja kuku, kwasababu walijua hakuna laana yoyote itakayowapata,. Hiyo ndio sababu ulimwengu wa kipindi kile ulizidi kuwa mwovu kupitiliza, mpaka ikafikia hatua ya Mungu kusema, mwisho wa kila mwanadamu umefika.

Mwanzo 6:5 “Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.

6 Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.

7 Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya…….

11 Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia ikajaa dhuluma.

12 Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani.

13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia.

Lakini siku moja ilipofika Gharika kubwa ilishuka ikauangamiza ulimwengu wote, wakapona tu watu 8, yaani Nuhu pamoja na familia yake. Na adhabu yao haikuishia tu, pale, bado huko kuzimu walipo sasa hivi, wanaendelea na mateso makali yasiyokuwa ya kawaida.

Ndugu yangu, fahamu kuwa Mungu anaweza kukuahidia ulinzi, na usalama, na afya na amani, na furaha, angali bado upo katika dhambi zako, hilo sio jambo gumu  kwake kukupa, liweke tu akilini, angali ukiwa unafanya uchawi wako bado Mungu anaweza kukuhakikishia Maisha ya heri hapa duniani, angali unaua watu, unauza madawa ya kulevya unauza pombe, unazini nje ya ndoa.. Bado Mungu atakuhakikishia ustawi wa mambo yako.

Hivyo usishangae kwanini waovu hawakumbwi na madhara yoyote, tena Zaidi ndio wanafanikiwa na kustarehe kama ulivyokuwa uzao wa Kaini, jinsi ulivyokuwa na mafanikio makubwa duniani, kuliko hata ule uzao wa Sethi lakini mwisho wao ulikuwa ni gharika.

Huu si wakati wa kustarehe katika dhambi, kisa tu hatuoni dhara lolote mbele yetu, tujue kuwa sisi watu wa kizazi hichi ndio tupo katika hatari kubwa ya kukumbana na ghadhabu kali ya Mungu, inayokaribia kuja duniani hivi karibuni, kuliko hata vizazi vingine vya nyuma vilivyotangulia.

Kwasababu maovu tunayoyafanya sasa hivi, yamezidi hata yale ya wakati wa Nuhu, licha ya kwamba sisi tumeshaufahamu ukweli wote na kuiona njia..

Bwana Yesu alisema.

Mathayo 11:23 “Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.

24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.

Ndugu, Tubu dhambi zako, usipumbazwe na ulinzi wa Mungu, angali upo bado katika dhambi, hizi ni  siku za mwisho, mwisho wa dunia upo karibu sana, dalili zote zimeshatimia, Jiulize UNYAKUO ukipita leo, utakuwa wapi ndugu yangu? Utamweleza nini Kristo siku ile ya hukumu, utamwambia mimi sikusikia injili? Na wale wa Sodoma na Gomora ambao sasahivi wapo kuzimu waseme  nini?

Tafakari Maisha yako, duniani hapa tunapita, na vitu vyote vinapita,. Mgeukia Kristo ayabadilishe Maisha yako leo ili akufanye kuwa kiumbe kipya, kisha uishi  Maisha ya kama mtu anayemsubiria Kristo kweli kweli, na sio kama mtu wa kidunia, acha kudhani kuwa Mungu haioni maovu unayotenda.

Bwana atusaidie sote.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI.

USIOMBE MAOMBI YASIYOKUWA NA MAJIBU NA WALA USIMTUKANE MUNGU.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

UZAO WA NYOKA.

UFUNUO: Mlango wa 1

Rudi nyumbani

Print this post

USIJITUMAINISHE JUU YA SIRA YAKO ANGALI UPO KATIKA DHAMBI.

Yeremia 48:11 “MOABU AMESTAREHE TANGU UJANA WAKE, NAYE AMETULIA JUU YA SIRA ZAKE, WALA HAKUMIMINWA KUTOKA CHOMBO KIMOJA KUTIWA CHOMBO KINGINE, wala hakwenda kufungwa; kwa hiyo ladha yake anakaa nayo, wala harufu yake haikubadilika.

12 Basi, tazama, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo nitampelekea wamiminao, nao watammimina, nao watamwaga vyote vilivyomo vyomboni mwake, na kuzivunja chupa zake vipande vipande.

Unajua sira ni nini?

Sira ni yale makapi yanayosalia baada ya pombe kuchachushwa, ni  mchanganyiko wa maganda ya mbegu na wadudu waliokuwa wanaichachusha pombe hiyo. Kwa kawaida pombe kama divai inapomalizika kuchachushwa, wanachofanya ni kuimimina kwenye vyombo vingine kwa ajili ya matumizi na kuiacha Sira chini.. kwasababu yenyewe inakuwa kama  topetope au urojo urojo fulani hivi.

Lakini makapi haya huwa yanathamani kubwa sana kwa wachachushaji, kwasababu pombe inayokaa muda mrefu juu ya Sira, huwa inaubora tofauti na ile ambayo, imekaa kwa muda mfupi. Kwa jinsi itakavyokaa sana juu ya sira basi ladha ya divai ndivyo inavyokuwa nzuri sana, vilevile mwonekano wake na harufu yake inakuja Zaidi, Lakini ile ambayo imechachushwa tu na saa hiyo hiyo au baada ya kipindi kifupi ikaondolewa na kupelekwa katika vyombo vingine huwa haina uzuri saa kama ile iliyodumu muda mrefu juu ya sira.

Wanaotengeneza divai, za ghali kama vile zinazoitwa champagne, huwa zinaachwa muda mrefu juu ya sira, hata miezi 4 na Zaidi, hivyo ubora wake unakuwa wa juu Zaidi kulinganisha na divai nyingine za kawaida. (Soma pia Isaya 25:6)

Sasa tukirudi katika mstari huo tuliousoma hapo juu, biblia inasema..

“Moabu amestarehe tangu ujana wake, naye ametulia juu ya sira zake, wala hakumiminwa kutoka chombo kimoja kutiwa chombo kingine…”

Moabu katika historia ni taifa ambalo, tangu lilipozaliwa halikupitia migogoro kabisa, au kama lilipitia basi ni midogo midogo sana ambayo haikulisababishia taifa hilo madhara makubwa, ukilinganisha na mataifa mengine, Moabu haikuwa na majanga, wala vita, wala njaa wala shida shida, lakini pamoja na kwamba ilijaliwa hivyo haikujua ni kwanini Mungu aliwaacha wawe vile, kinyume chake yenyewe iliendelea tu kufanya maovu na matendo yasiyompendeza Mungu kwa muda mrefu.

Na ndio maana hapo inafananishwa na divai ambayo imekaa juu ya sira yake kwa muda mrefu, divai ambayo haikuharakishwa kumiminwa miminwa kwenye vyombo vingine, ikiwa na maana kuwa haikuchukuliwa utumwani, haikupitishwa katika matatizo, iliendelea kubakia katika ustawi wake kwa muda mrefu..

Ikawa inadhani kuwa kamwe haitakaa ukumbane na mabaya, yenyewe imebarikiwa tu, ikafikiria  hao wengine wanaoadhibiwa kama Israeli wana laaana na mikosi kutoka kwa Mungu.

Lakini tukisoma mistari inayofuata inasema hivi..

Moabu amestarehe tangu ujana wake, naye ametulia juu ya sira zake, wala hakumiminwa kutoka chombo kimoja kutiwa chombo kingine, wala hakwenda kufungwa; kwa hiyo ladha yake anakaa nayo, wala harufu yake haikubadilika.

12 Basi, tazama, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo nitampelekea wamiminao, nao watammimina, nao watamwaga vyote vilivyomo vyomboni mwake, na kuzivunja chupa zake vipande vipande.

Umeona, kuna wakati ulifika, wakaldayo walikuja na kuwaangamiza na kuwachukua utumwani na kuwaharibu kabisa, na uzuri wao ukapotea ghafla, jambo ambalo hawakutazamia kama lingekaa liwapate, kama wengine.

Ndugu yangu, leo hii unatenda dhambi lakini huoni chochote, unazini Bwana hakuadhibu kwa lolote, unafanya mambo yako machafu kwa muda mrefu sasa, unakwenda kwa waganga, hauumwi, kinyume chake unazidi kustawi, unaendelea kufanya anasa na ulevu, unasema mbona hakuna dhara lolote linalonipata, hujiulizi ni kwa nini? Unachodhani ni kuwa wewe ni spesheli sana kwake sio?  embu soma mstari huu tena ujifunze jambo..

Sefania 1:12 “Kisha itakuwa wakati ule, nitauchunguza Yerusalemu kwa taa; nami NITAWAADHIBU WATU WALIOGANDA JUU YA SIRA ZAO; wasemao katika mioyo yao, Bwana hatatenda mema, wala hatatenda mabaya”.

Umeona, Mungu utafika wakati atakuchunguza kwa taa, wewe ambaye umetulia juu ya Sira yako, huangaishwi angaishwi, unafanikiwa angali upo katika dhambi, unayesema, Mungu hawezi fanya jambo lolote hata nikiwa mwovu kiasi gani.

Jiangalie, hukumu ipo, utakufa ghafla, na moja kwa moja utajikuta upo jehanamu kama yule Tajiri wa Lazaro, ambaye hapa duniani alikuwa akijitumaisha katika Maisha yake ya anasa tu, hajali kama kuna kuzimu, au hukumu, hajali kama kuna kiama chake mbeleni.. Na wewe ndipo utakapojikuta huko kama hutatubu, ukilia na kuomboleza, ukisema laiti ningelijua, laiti ningelijua..

Wakati huo utakuwa umeshachelewa ndugu. Leo hii ukiona Mungu hafanyi chochote juu ya dhambi zako, sio kwamba anayafurahia hayo Maisha unayoishi, anakutazama tu, yamkini siku moja utatubu, lakini ikifikia wakati haoni badiliko lolote la wewe kumgeukia yeye, atakujia na kukuondoa duniani kama alivyofanya kwa Wamoabu.

Biblia inasema saa ya wokovu ni sasa, na wakati uliokubali ni leo, usingojee siku Fulani ukasema hiyo ndio itakuwa siku yako ya wokovu, haitakaa ije kamwe. Mpe Yesu Kristo Maisha yako leo ayaokoe, Tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kisha tafuta mahali ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO ili upate ondoleo la dhambi zako, na Kisha mwenyewe Mungu atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu ili akae na wewe siku zote za Maisha yako.

Hata kama ikitokea Maisha yako yamefikia ukingo leo, basi unaouhakika wa kuurithi uzima wa milele.

Ikiwa utapenda kuokoka, na unahitaji msaada huo basi unaweza, kutafuta kanisa la kiroho lililokaribu na wewe, wakusaidie au ukawasiliana na sisi kwa namba zetu hizi +255693036618 /+255789001312 kwa ajili ya Sala ya Toba na maagizo mengine.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE! ULEVI NI DHAMBI?.

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?

UFUNUO: Mlango wa 15

Rudi nyumbani

Print this post

ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.

Shalom, karibu tujifunze Neno la Mungu. Biblia inatuambia..

 “Ondoa takataka katika fedha, Na chombo kitatokea kwa mtakasaji; (Mithali 25:4)

Tunapoiona dhahabu au madini mengine yote, yanang’aa sana, mpaka kufikia kiwango cha kuuzwa kwa thamani kubwa sana, hatupaswi kudhani, huko chini yanapochimbwa yanatoka kama yalivyo. Hapana, mengi ya hayo yanakuwa yamechanganyikana na mawe mengine au uchafu mwingi tofauti tofauti, kiasi kwamba unaweza kukutana na mwamba mkubwa sana, na ndani yake kukawa na kiwango kidogo sana cha dhahabu au fedha.

Hivyo, ili kuitapata dhahabu yenyewe safi, inawagharimu wafuaji wafanye kazi ya ziada, na kazi yenyewe ndio hiyo ya kutenganisha madini hayo kutoka katika hizo takataka nyingine, Zipo takataka ambazo unaweza kuziondoka kwa kuzichuja tu au kupepeta, lakini zipo ambazo itakuhijitaji utumie moto ili kuzitenganisha, kwasababu inakuwa zzimechanganyikana na dini lenyewe hadi ndani.

Hivyo wanachokifanya ni kwenda kuyachoma mawe hayo, kwa joto kali sana mpaka yayeyuke, na yakishayeyuka na kuwa kama uji uji,  ndipo sasa uchafu unajitenga na dhahabu yenyewe.  Kwa kupanda juu, hapo ndipo yule mfuaji anapoondoa uchafu ule,  na atarudia tena hizo hizo hatua kwa jinsi atakavyoweza, na kwa jinsi anatakavyozidi kuondoa takatakata hizo zote hata zile ndogo, ndivyo, mnga’o wa fedha hiyo unavyozidi kuja.. hatimaye, inatokea ikiwa nzuri sana yenye kunapendeza, tayari kwa matumizi yenye thamani.

Mithali 25:4 “Ondoa takataka katika fedha, Na chombo kitatokea kwa mtakasaji;”.

Hivyo na sisi pia kama wakristo, tunapookoka tunakuwa hatuna tofauti na fedha/dhahabu iliyochimbwa katikati ya miamba, tumetolewa huko tukiwa na mambo mengi ya kidunia  ambayo yameshikamana sana na sisi,

Sasa tunapookoka, kanuni ni ile ile inatugharimu tuingizwe katika moto, ili tuwe safi kabisa, Na moto huo anayetuingiza Mungu, na pia tunajiingiza sisi wenyewe.

Hapo ndipo utaona pale tunapokuwa wakristo tu, Mungu anaruhusu tupitishwe katika majaribu mbali mbali ya moto ili tuwekwe safi. Ndio maana biblia inasema;

1Petro 1:6 “Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;

7 ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo”.

Yakobo 1:2 “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;

3 mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi”.

Unaona, ni jambo la kawaida Mungu, kuwapitisha watoto wake katika majaribu ya namna mbalimbali, lengo sio kuwaangamiza, bali kuwaimarisha Zaidi.

Pia Neno la Mungu linatuambia na sisi wenyewe, tunapaswa tuondoe takataka katikati ya kila kitu tunachokifanya katika maisha yetu ya ukristo ili Mungu aweze kutufanya kama vile anavyotaka, iwe ni katika  huduma zetu, au  shughuli zetu n.k..

Tukitaka tumwone Mungu katikati ya Maisha yetu, tuondoe mambo ambayo hayampendezi, tuondoke uzinzi, tuondoe usengenyaji, tuondoke kuchat chati kusikokuwa na maana mitandaoni, na kutazama muvi muvi zisizotujenga, tuondoe mizaha, tuondoe unafki, tuondoe rushwa, tuondoe uvaaji mbovu,  n.k. Mambo kama haya tukiyazingatia basi Mungu, atatuletea ule mng’ao tunaostahili kuwa nao sisi kama wakristo, na tutakuwa wa thamani nyingi mbele zake na mbele za ulimwengu.

2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.

Kumbuka mambo kama haya kuyaondoa, haihitaji kuwa mlegevu legevu, inahitaji kujiingiza wewe mwenyewe katika moto wako, (kujinyima, kukataa na kuepuka) kila kitu ambacho unaona hakimpendezi Mungu. Hata kama nafsi yako inakitamani vipi, unakipinga. Unakubali kuonekana wa ajabu, lakini moyo wako uwe salama, na faida yake utaiona baadaye.

Vilevile hata katika Maisha yetu ya huduma, ili Kristo atende kazi vema, na ukuu wake uthibitike tunapaswa tuondoe mambo yote  maovu katikati ya kanisa, tusiwe radhi na wazinzi na wapotoshaji katikati yetu, na Mungu atajifunua miongoni mwetu.

Mithali 25:4 “Ondoa takataka katika fedha, Na chombo kitatokea kwa mtakasaji;

5 Mwondoe asiye haki mbele ya mfalme, Na kiti chake cha enzi kitathibitika katika haki”.

Bwana atusaidie sote, Na atubariki.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

Fuawe ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 41:7

NYAYO TUNAZOPASWA KUZIFUATA.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Mwandishi wa kitabu cha Warumi alikuwa ni Paulo au Tertio?

SWALI: Je! Mwandishi wa kitabu cha Warumi alikuwa ni Paulo au Tertio? kulingana na mstari huu;

Warumi 16:22 “Mimi Tertio, niliyeandika waraka huu, nawasalimu katika Bwana”.


JIBU: Paulo katika maneno yake ya utangulizi alishatupa  mwangaza kuwa yeye ndiye aliyekiandikia kitabu hicho, kiwaelekee watakatifu wote waliokuwa Rumi. Tusome;

Warumi 1:1 “PAULO, MTUMWA WA KRISTO YESU, ALIYEITWA KUWA MTUME, NA KUTENGWA AIHUBIRI INJILI YA MUNGU;

2 ambayo Mungu amekwisha kuiahidi kwa kinywa cha manabii wake katika maandiko matakatifu;

3 yaani, habari za Mwanawe, aliyezaliwa katika ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili,

4 na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu;

5 ambaye katika yeye tulipokea neema na utume ili mataifa yote wapate kujitiisha kwa imani, kwa ajili ya jina lake;

6 ambao katika hao ninyi mmekuwa wateule wa Yesu Kristo;

7 KWA WOTE WALIOKO RUMI, WAPENDWAO NA MUNGU, WALIOITWA KUWA WATAKATIFU. Neema na iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo”.

Lakini baadaye karibia na mwishoni mwa waraka huu tunakuja kumwona mtu mwingine aliyeitwa Tertio akijitokeza na kusema ameuandika waraka ule. Sio kwamba mtume Paulo hakuhusika hapana, Jibu ni kwamba Tertio alikuwa ni mwandishi wa mtume Paulo, aliyekuwa anamwandikia nyaraka zake. Aidha kwa kuandika kile alichokuwa anaambiwa au kwa kunakili kile alichoandikiwa na Paulo, japo hakuna sehemu nyingine katika biblia Tertio anaonekana akitajwa.

Na kulikuwa na sababu ya mtume Paulo kutokutumia mkono wake mwenyewe kuandikia waraka huu, pengine Tertio alikuwa ni mwandishi  mwaminifu anayejulikana sana  na watakatifu waliokuwa Rumi kwa umahiri na ufanisi wa kazi zake zilizothibitishwa. Hivyo mtu akiona waraka ulionakiliwa na yeye, basi ilikuwa ni rahisi kuamini uhalisia wa yule mwandishi husika. Kwasababu wakati huo walikuwepo pia watu waliojifanya ni mitume, na kutoa kopi zao wakidai kuwa ni za mitume, ili tu kuwachanganganya watu.

Na ndio maana mtume Paulo ili kuthibitisha nyaraka zake, sehemu nyingine alikuwa anatia sahihi yake mwishoni, soma(2Wathesalonike 3:17), na pia na hapa aliona  ni vema amtumie huyu Tertio kuuandika kwa warumi, iwe kama sahihi yake.

Hivyo waraka huu uliandikwa na Paulo, lakini aliyeunakili ni Tertio.

Hii ni kutufundisha kuwa, si kila kazi ya Mungu, hata kama tutaiona  ni nyepesi kiasi gani, tuifanye sisi mwenyewe, wakati mwingine tutahitaji tushirikiane na viungo vingine vya Kristo, ili kuleta ufanisi Zaidi wa kazi hiyo kwa watu wake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA FILEMONI.

Kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?

SWALI: Kitabu cha Henoko ndio kitabu kipi hicho, Je! Sisi kama wakristo tunapaswa kukiamini?


JIBU: Kitabu cha Henoko ni moja ya vitabu vya Apokrifa ambavyo viliandika kati ya miaka 200 kabla ya Kristo(KK), na  miaka 400 baada ya Kristo(WK). Vitabu hivi  vinaaminiwa na baadhi ya wakristo kuwa  vilihifadhiwa kwa siri, kutokana na kuwa vilikuwa na siri za ndani sana kuhusu Mungu na historia ya ulimwengu kwa ujumla, kiasi kwamba havikuweza kujumuishwa moja kwa moja kwenye biblia yenye vitabu 66 ambayo tunayo hivi sasa.

Lakini si kweli, vitabu hivi havikujumuishwa katika biblia takatifu kwasababu vilikuwa na siri za Mungu hapana badala yake vilionekana kujaa habari nyingi za kutungwa, ambazo zinakinzana na misingi ya imani ya Kikristo.

Sasa tukirudi katika hichi kitabu cha Henoko, kiligunduliwa kwenye miaka ya 1700 huko Ethiopia, baadaye kikasafirishwa mpaka Uingereza kwa ajili ya kutafsiriwa katika lugha nyingine, Kitabu hichi kilijulikana kama Henoko wa  Kwanza (1Henoko), kwasababu kulikuja kuwa pia na matoleo mengine yaliyofuata baadaye.

Vipande vya nyaraka vya kitabu hichi pia viligunduliwa huko Israeli mnao mwaka 1947, kwenye mapango yalikuwa katika fukwe za bahari ya chumvi (dead sea), Na kwenye mapango hayo kulionekana pia machapishi ya vitabu vyote vya agano la kale isipokuwa tu kitabu cha Esta, inasadikika ni vitabu ambavyo vilikuwa vimehifadhiwa huko na watu wa kale ambao waliishi kabla hata ya Kristo kuja duniani.

Sasa kitabu hiki kinamueleza Henoko ambaye alikuwa ni mtu wa saba kutoka Adamu kama tunavyosoma katika biblia Mwanzo 5:18-24…Henoko hakuonja mauti kama ilivyokuwa kwa wanadamu wengine, bali alinyakuliwa kama Eliya. Hiyo imekuwa ikawafanya watu wengi waamini kuwa mtu huyu alipewa siri nyingi za rohoni na kuziandika kwa ajili ya watu wa baadaye.

Hivyo kitabu hichi kilipogunduliwa, kilidhaniwa  kuwa mwandishi wake  ni Henoko, japo hilo jambo halikuthibitika kuwa ni kweli. Kitabu hichi kimejaa historia zinaeleza visa vya dunia ya kwanza kugharikishwa na maji, kinasema baadhi malaika wa Mungu  ambao walikuwa ni waangalizi wa huku ulimwenguni, ambao idadi yao ilikuwa ni 200 waliwaona binti za wanadamu, kisha wakawatamani, , hivyo wakashauriana washuke duniani wajitwalie wake, waishi nao, na kweli wakafanya hivyo  wakashuka duniani wakawapa mimba wanawake, ndio wakazaa wale majitu ambayo tunayasoma katika Mwanzo 6

Zaidi ya yote, malaika hawa kwa kuwa walikuwa na ujuzi, wakawafundisha wanadamu, kubuni silaha za chuma, kufanya uharibifu, wengine wakawafundisha wanadamu kufanya uchawi, na wengine kusoma nyota za mbinguni. Pamoja na hayo watoto wao waliowazaa wakawa wakatili kupita kiasi, ndio wale wanefili, wakawa wanaharibu kila kitu ikiwemo mimea, wanyama, mpaka wanadamu. Urefu wa majitu hayo ulikuwa ni futi 4500, sawa na Jengo la ghorofa 415. Jambo ambalo ni ngumu kusadikika,  Hakuna kiumbe cha namna hiyo kinaweza kuzaliwa na mwanamke. Japo wanefili kweli walikuwa ni wakubwa lakini sio kwa kiwango hicho.

Baadaye baadhi ya malaika wa mbinguni wakampelekea Mungu habari zao,  lakini Mungu akakataa kuwasamehe, akawafunga katika vifungo vya giza, ndio hapo Mungu akamwambia Henoko kuwa atakwenda kuiangamiza dunia kwa gharika.  Hii ndio habari ambayo inafahamika sana

Zipo habari nyingine katika kitabu hicho ambazo kiuhalisia hazina uhalisia wowote  na maandiko.

Tunapaswa tujue vitabu hivi vimejaa hadithi nyingi za kutungwa, ambazo ni sumu kwa Mkristo, na ndio maana huwezi kuziona vikijumuishwa katika biblia yenye vitabu 66 vilivyovuviwa na Roho Mtakatifu, kwasababu vinakinzana na misingi ya kweli ya maandiko.

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 22:29 “Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.

30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni”.

Unaona? Hakuna andiko lolote linaloonyesha kuwa malaika wanaoa, au wanazaliana, malaika hawakuumbiwa viungo vya uzazi kama tulivyonavyo sisi, hawahitaji kuzaliana, wao tayari walishaumbwa, ndivyo walivyo na idadi yao tayari ipo kamili, Lakini kusema walishuka duniani, ni fundisho la uongo ambalo wakristo wengi wanaliamini mpaka leo, na chanzo chake walikitoa katika hichi kitabu cha Henoko.

Waliowaona binti za wanadamu wakawatamani, walikuwa ni watakatifu wa Mungu, ambao hao hawakujichanganya na mambo ya ulimwengu tangu mwanzo, bali walitumia sehemu kubwa ya maisha yao, kuliita jina la Bwana na kumwabudu Mungu soma Mwanzo 4:26 utalithibitisha hilo ndio ule  uzao wote wa Sethi (Wakina Henoko, Methusela, Na Nuhu).. Lakini binti za wanadamu walikuwa ni watu wa kidunia tu, ambao walitokea katika ule uzao wa Kaini..hao ndio tangu mwanzo walikuwa na ujuzi mkubwa, na hodari na pia wakatili ukisoma pale Mwanzo 4:16-23 utaona ni jinsi gani, uzao wa Kaini ulivyokuwa hodari, wenye ujuzi mwingine, lakini pia mwovu kwa uuaji, kama Baba yao alivyokuwa.

Baadaye sasa walipojichanganya mbegu ndipo Mungu akakasirika, akaghahiri na kuuangamiza ulimwengu wote, ni sawa na leo hii, Mungu aone, watakatifu wake wote, wanaiga na kufanya mambo ya ulimwengu, wanawake wanavaa vimini, wanatembea nusu uchi barabarani, wanaume watakatifu wanakuwa mashoga n.k. kiasi kwamba huwezi kuona tofauti yoyote kati yao na ulimwenguni, hapo kinachofuata ni Mungu kuuteketeza ulimwengu, ndivyo ilivyokuwa kwa watu wa kipindi kile. Watakatifu walijitofautisha kabisa na wana wa ulimwengu..

Hivyo hakuna sababu ya mkristo kuamini, moja kwa moja vyanzo ambavyo havipo katika biblia, kwasababu vingi kati ya hivyo vinakasoro nyingi na vimejaa hadithi nyingi zilizotungwa na wanadamu lakini sio kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu.

Kwamfano kwasasa Kanisa Katoliki, limeamua kuchukua baadhi ya hivi vitabu vya Apokrifa na kuviongezea kwenye biblia takatifu yenye vitabu 66, kufikia 73. Vitabu vyenyewe ikiwemo Yudithi, Baruku, Yoshua bin Sira, Wamakabayo 1&2,  Hekima.

Vitabu hivi vinakinzana na misingi ya imani, kwamfano, vinafundisha kwenda toharani, yaani mtu mwenye dhambi anaweza kwenda mbinguni tena, lakini baada ya kupitishwa mahali panapoitwa toharani ili kutakaswa,.,Fundisho lingine ni kuwa Mungu, anasikia maombi ya wafu, mambo ambayo ni uongo, biblia inasema, mtu ameandikiwa kuishi mara moja na baada ya kifo ni hukumu (Waebrania 9:27).

Kwahiyo, vitabu vya Aprokifa, sio vya kuviamini, kama uaminivyo biblia, iwe ni kitabu cha Henoko, au kingine chochote kile nje ya vitabu 66 vya biblia sio vya kuiamini vinamakosa mengi na wakati mwingine vimejaa uongo mwingi, ambao unapotosha kabisa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi nyumbani

Print this post

KOIKOI ANGANI AJUA NYAKATI ZAKE ZILIZOAMRIWA.

Yeremia 8:7 “Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za Bwana”.

Koikoi, mbayuwayu na korongo ni ndege wa ajabu sana, ni ndege wenye uwezo wa kusoma majira ya dunia, Na hiyo imewasaidia sana, kuishi maisha ya salama salmini huku duniani, pasipo kukumbana na changamoto zozote  zisizo na maana.

Hawa ni ndege ambao kikikaribia kipindi cha baridi wanahama wote waeneo yao wanayoishi kwa muda, na kusafiri umbali mrefu sana, kwenye pembe ya pili ya dunia kutafuta msimu tulivu aidha wa vuli au  wa joto ulipo wakatulie, kisha baadaye hali ya baridi ikishakwisha wanarudi katika makazi yao ya awali kuendelea na maisha yao ya kawaida.

Kumbuka baridi tunayoizungumzia ni ile baridi haswaa, ya kutengeneza barafu iliyopo huko nchi za ulaya, ambayo hata mtu wa kawaida akikaa nje masaa machache tu anageuka kuwa jiwe la barafu, haijalishi atavaa masweta makubwa kiasi gani.. Baridi ya namna hiyo watu wanaoishi huko wanatumia muda wao mwingi kuwepo ndani, na hata kazi zao wanazifanyia ndani katika nyumba zilizojengwa kitaalamu kuhifadhi joto ndani, kwani nyumba za kawaida kama hizi zetu, kule hazijengwi kwasababu zinapitisha baridi, kiasi kwamba ukibaki ndani yake, ukakaa huko mpaka asubuhi ukiamka umeganda. Huku kwetu Afrika hatuna baridi ya namna hiyo.

Sasa, ndege hawa, wanaelewa kabisa kwa namna ya kawaida hawawezi kuishi katika mazingira hayo ya baridi kali, kwasababu hata viota vyao vitaganda.. Sasa ili kulitatua hilo tatizo inawagharimu wahame kwa muda, ndio hapo wanasafiri maelfu ya kilometa wanakuja mpaka huku kwetu Afrika, au nchi nyingine zenye joto, wanakaa  huko mpaka msimu wa baridi  utakaposhakwisha kule Ulaya ndio wanarudi sasa, kuendeleza maisha yao ya sikuzote.

Sasa Mungu ametumia mfano wa ndege hawa wasio na akili, kutushangaa sisi wanadamu wenye akili timamu kwanini hatujui hukumu zake alizoziweka hapa duniani..anasema..

“Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za Bwana”

Hii ikiwa na maana tunashindwa kujua wakati wa neema ni upi, na wakati wa hukumu za Mungu ni upi.. Sisi tupo tu hatujui majira yetu, tunadhani wakati wote, hii neema ya wokovu itaendelea kuwepo, tunadhani wakati wote, hali itakuwa kama ilivyo sasa hivi, utahubiriwa injili kama unavyohubiriwa sasa hivi..

Ndugu yangu, fahamu kuwa neema hii inakwenda kuisha siku sio nyingi, Dhiki kubwa ambayo haijawahi kutokea tangu dunia iumbwe na wala haitakaa iwepo itakwenda kutokea ulimwenguni kote..Dalili zote zinaonyesha, pengine katika wakati wetu huu tunaoishi tutayashuhudia hayo..Haya majira ya neema ndio yanaishia hivyo, muda huu tulionao ni wa nyongeza tu, dunia ingepaswa iwe imeshakwisha tangu zamani, lakini kwasababu tu ile nuru ndogo ya jioni ipo ndio maana unaona mambo bado yapo hivi..

Tumeshafikia wakati ambao Yesu hatuhubirii  tena injili ya kutuvuta kwenye wokovu, kama ilivyokuwa zamani bali anatuhubiria injili ya kuthibitisha ulichokiamini. Sikiliza anavyosema..

Ufunuo 22:10 “Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.

12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.

Unaona, hiyo yote ni kwasababu ya unafki tulionao sasa, kwasababu kama tunaweza kuyatambua majira ya nchi, kwamba huu ni msimu wa masika na hivyo tunaanza kuyaandaa mashamba yetu kabla ya mvua kunyesha, au tunahama mabondeni mapema mafuriko yasitukute, inakuwaje basi, tunashindwa kuzitambua siku hizi kuwa ni siku za mwisho? Korona inakufundisha nini? Vimbunga vinakufundisha nini, Hili wimbi la manabii wa uongo unaloliona leo hii limezuka duniani kwa ghafla linakufundisha nini? . Bado tu huoni, hizo ni dalili za wazi kabisa ambazo zinatutambulisha kuwa tukio la unyakuo lipo karibu?

Yesu alisema..

Luka 12:54 “Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya”?

Itakuwa ni ajabu sana tukishindwa akili na akina koikoi. Tujitathimini sana, tuamke katika usingizi huu mzito, hukumu ya Mungu juu ya ulimwengu wote ipo karibu. Kama upo nje ya safina, anza safari upesi, mkimbilie Kristo kwa kumaanisha kabisa kwa moyo wako wote akuokoe, kwasababu hatuna muda mrefu hapa duniani,

 mbingu na nchi zitapita lakini maneno ya Bwana Yesu hayatapita milele.

Mbingu ipo,lakini pia kuzimu ipo, uchaguzi ni wa wako,

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

WAENDEE WANA WA ISAKARI, UWE SALAMA.

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

SWALI: Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi?

Kwanini kuna mahali Bwana Yesu anawaita wale aliowaita mitume, na sehemu nyingine anawaita wanafunzi, tofauti yao ni ipi? Au ni kitu kimoja?


JIBU: Si kila mwanafunzi ni mtume, lakini kila mtume ni lazima awe mwanafunzi wa Yesu.

Mwanafunzi ni mtu ambaye anaketi chini kufundishwa, kupewa ujuzi au utashi au maarifa ya kumsaidia kuishi au kufanya jambo Fulani, Na Bwana Yesu naye alikuwa na watu wa namna hiyo hiyo,

Lakini kumbuka si wote waliomfuata waliitwa wanafunzi wake, isipokuwa wale tu waliokidhi vigezo vyake alivyoviweka, na vigezo vyenyewe ndio hivi;

Luka 14:25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,

26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia?

29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,

30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.”.

Lakini Mtume maana yake ni “aliyetumwa”,   Wale walioitwa na Bwana Yesu na kuandaliwa kwa jukumu Fulani maalumu waliitwa mitume, ambao walikuwa kumi na mbili tu kwa wakati ule. Na kusudi lenyewe waliloitiwa lilikuwa hili;

Mathayo 28:19 “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa Dahari”.

Mitume pia waliendelea kuitwa na Kristo hata baada ya yeye kuondoka duniani.. Mfano utawaona  mitume  kama  Paulo,  Barnaba, na Epafrodito (Wafilipi 2:25)

Hata kwa wakati huu wa sasa, watumishi wote wa Mungu wanaofanya kazi kama waliyoifanya mitume, Yesu anawatambua kama mitume wake, hawa ni Zaidi ya wanafunzi, kwasababu hawawi wakristo tu peke yake, bali Zaidi wanajitaabisha kwa ajili ya ufalme wa mbinguni.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.

Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?

USITAFUTE KUKANWA NA BWANA SIKU ILE.

Rudi nyumbani

Print this post