Category Archive Uncategorized

MUNGU HAONI SHIDA KUMUHAKIKISHIA MWOVU ULINZI.

Baada ya Kaini kumuua ndugu yake, na Mungu, kumlaani kwa laana ile ya kwamba atakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani, utaona alimwomba Bwana ampunguzie adhabu yake, na baada ya kupunguziwa kwa kutiwa alama, haikuishia hapo,  bado Mungu alimuhakikishia usalama mwingine wa juu Zaidi.  Tusome;

Mwanzo 4:14 “Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.

15 Bwana akamwambia, KWA SABABU HIYO YE YOTE ATAKAYEMWUA KAINI ATALIPIZWA KISASI MARA SABA. Bwana akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga”.

Unaona hapo kwenye mstari  wa 15, Bwana akimuhakikishia ulinzi wa kipekee sana. Jambo ambalo si rahisi mtu mwovu kufanyiwa na mtu yeyote, kwasababu hakuna tendo lolote la kishujaa alilotenda Kaini mpaka alipiziwe kisasi mara saba, kwa yeyote atakayemuua,ni heri ingekuwa ni mara moja, lakini mara saba, hiyo angepaswa afanyiwe mtu mwenye haki.

Tengeneza picha diktekta, ambaye ameshutumiwa kwa mauaji wa maelfu ya watu, kama vile HITLER wa ujerumani, leo hii, unasikia Mungu anasema mtu yeyote atakayemuua Hitler atalipizwa kisasi mara saba, unaweza kudhani Mungu anafurahishwa na maovu. Ndivyo ilivyokuwa kwa Kaini, Mungu haoni shida kumuhakikishia mwovu ulinzi na mafanikio. Hilo tunapaswa tulijue.

Lakini afadhali ingeishia kwa Kaini tu, Tabia yake ya uuaji iliendelea mpaka kwa uzao wake. Utaona yupo mmoja aliitwa, Lameki, yeye alikuwa muuaji kuliko hata baba yake, anasema alimuua mtu kwa kumtia jeraha tu, alimuua mtu kwa kumchubua tu, akiwa na maana mtu aliyemkosea  kwa jambo dogo sana alikuwa  radhi kumuua, bila kujali chochote.

Huku akitumia kivuli kile kile cha baba yake, cha usalama aliohakikishiwa na Mungu, tena na Zaidi, anasema kama ikitokea mtu atataka kumlipizia kisasi kwa uuaji wake, basi akumbuke kuwa Mungu atamlipizia sio tu mara saba, bali mara saba sabini.

Mwanzo 4:23 “Lameki akawaambia wake zake, Sikieni sauti yangu, Ada na Sila; Enyi wake za Lameki, sikilizeni usemi wangu; Maana nimemwua mtu kwa kunitia jeraha; Kijana kwa kunichubua;

24 Kama Kaini akilipiwa kisasi mara saba, Hakika Lameki atalipiwa mara sabini na saba”.

Unaona? Walikuwa wanajiamulia kufanya mauaji tu kama vile kuchinja kuku, kwasababu walijua hakuna laana yoyote itakayowapata,. Hiyo ndio sababu ulimwengu wa kipindi kile ulizidi kuwa mwovu kupitiliza, mpaka ikafikia hatua ya Mungu kusema, mwisho wa kila mwanadamu umefika.

Mwanzo 6:5 “Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.

6 Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.

7 Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya…….

11 Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia ikajaa dhuluma.

12 Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani.

13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia.

Lakini siku moja ilipofika Gharika kubwa ilishuka ikauangamiza ulimwengu wote, wakapona tu watu 8, yaani Nuhu pamoja na familia yake. Na adhabu yao haikuishia tu, pale, bado huko kuzimu walipo sasa hivi, wanaendelea na mateso makali yasiyokuwa ya kawaida.

Ndugu yangu, fahamu kuwa Mungu anaweza kukuahidia ulinzi, na usalama, na afya na amani, na furaha, angali bado upo katika dhambi zako, hilo sio jambo gumu  kwake kukupa, liweke tu akilini, angali ukiwa unafanya uchawi wako bado Mungu anaweza kukuhakikishia Maisha ya heri hapa duniani, angali unaua watu, unauza madawa ya kulevya unauza pombe, unazini nje ya ndoa.. Bado Mungu atakuhakikishia ustawi wa mambo yako.

Hivyo usishangae kwanini waovu hawakumbwi na madhara yoyote, tena Zaidi ndio wanafanikiwa na kustarehe kama ulivyokuwa uzao wa Kaini, jinsi ulivyokuwa na mafanikio makubwa duniani, kuliko hata ule uzao wa Sethi lakini mwisho wao ulikuwa ni gharika.

Huu si wakati wa kustarehe katika dhambi, kisa tu hatuoni dhara lolote mbele yetu, tujue kuwa sisi watu wa kizazi hichi ndio tupo katika hatari kubwa ya kukumbana na ghadhabu kali ya Mungu, inayokaribia kuja duniani hivi karibuni, kuliko hata vizazi vingine vya nyuma vilivyotangulia.

Kwasababu maovu tunayoyafanya sasa hivi, yamezidi hata yale ya wakati wa Nuhu, licha ya kwamba sisi tumeshaufahamu ukweli wote na kuiona njia..

Bwana Yesu alisema.

Mathayo 11:23 “Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.

24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.

Ndugu, Tubu dhambi zako, usipumbazwe na ulinzi wa Mungu, angali upo bado katika dhambi, hizi ni  siku za mwisho, mwisho wa dunia upo karibu sana, dalili zote zimeshatimia, Jiulize UNYAKUO ukipita leo, utakuwa wapi ndugu yangu? Utamweleza nini Kristo siku ile ya hukumu, utamwambia mimi sikusikia injili? Na wale wa Sodoma na Gomora ambao sasahivi wapo kuzimu waseme  nini?

Tafakari Maisha yako, duniani hapa tunapita, na vitu vyote vinapita,. Mgeukia Kristo ayabadilishe Maisha yako leo ili akufanye kuwa kiumbe kipya, kisha uishi  Maisha ya kama mtu anayemsubiria Kristo kweli kweli, na sio kama mtu wa kidunia, acha kudhani kuwa Mungu haioni maovu unayotenda.

Bwana atusaidie sote.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI.

USIOMBE MAOMBI YASIYOKUWA NA MAJIBU NA WALA USIMTUKANE MUNGU.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

UZAO WA NYOKA.

UFUNUO: Mlango wa 1

Rudi nyumbani

Print this post

USIJITUMAINISHE JUU YA SIRA YAKO ANGALI UPO KATIKA DHAMBI.

Yeremia 48:11 “MOABU AMESTAREHE TANGU UJANA WAKE, NAYE AMETULIA JUU YA SIRA ZAKE, WALA HAKUMIMINWA KUTOKA CHOMBO KIMOJA KUTIWA CHOMBO KINGINE, wala hakwenda kufungwa; kwa hiyo ladha yake anakaa nayo, wala harufu yake haikubadilika.

12 Basi, tazama, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo nitampelekea wamiminao, nao watammimina, nao watamwaga vyote vilivyomo vyomboni mwake, na kuzivunja chupa zake vipande vipande.

Unajua sira ni nini?

Sira ni yale makapi yanayosalia baada ya pombe kuchachushwa, ni  mchanganyiko wa maganda ya mbegu na wadudu waliokuwa wanaichachusha pombe hiyo. Kwa kawaida pombe kama divai inapomalizika kuchachushwa, wanachofanya ni kuimimina kwenye vyombo vingine kwa ajili ya matumizi na kuiacha Sira chini.. kwasababu yenyewe inakuwa kama  topetope au urojo urojo fulani hivi.

Lakini makapi haya huwa yanathamani kubwa sana kwa wachachushaji, kwasababu pombe inayokaa muda mrefu juu ya Sira, huwa inaubora tofauti na ile ambayo, imekaa kwa muda mfupi. Kwa jinsi itakavyokaa sana juu ya sira basi ladha ya divai ndivyo inavyokuwa nzuri sana, vilevile mwonekano wake na harufu yake inakuja Zaidi, Lakini ile ambayo imechachushwa tu na saa hiyo hiyo au baada ya kipindi kifupi ikaondolewa na kupelekwa katika vyombo vingine huwa haina uzuri saa kama ile iliyodumu muda mrefu juu ya sira.

Wanaotengeneza divai, za ghali kama vile zinazoitwa champagne, huwa zinaachwa muda mrefu juu ya sira, hata miezi 4 na Zaidi, hivyo ubora wake unakuwa wa juu Zaidi kulinganisha na divai nyingine za kawaida. (Soma pia Isaya 25:6)

Sasa tukirudi katika mstari huo tuliousoma hapo juu, biblia inasema..

“Moabu amestarehe tangu ujana wake, naye ametulia juu ya sira zake, wala hakumiminwa kutoka chombo kimoja kutiwa chombo kingine…”

Moabu katika historia ni taifa ambalo, tangu lilipozaliwa halikupitia migogoro kabisa, au kama lilipitia basi ni midogo midogo sana ambayo haikulisababishia taifa hilo madhara makubwa, ukilinganisha na mataifa mengine, Moabu haikuwa na majanga, wala vita, wala njaa wala shida shida, lakini pamoja na kwamba ilijaliwa hivyo haikujua ni kwanini Mungu aliwaacha wawe vile, kinyume chake yenyewe iliendelea tu kufanya maovu na matendo yasiyompendeza Mungu kwa muda mrefu.

Na ndio maana hapo inafananishwa na divai ambayo imekaa juu ya sira yake kwa muda mrefu, divai ambayo haikuharakishwa kumiminwa miminwa kwenye vyombo vingine, ikiwa na maana kuwa haikuchukuliwa utumwani, haikupitishwa katika matatizo, iliendelea kubakia katika ustawi wake kwa muda mrefu..

Ikawa inadhani kuwa kamwe haitakaa ukumbane na mabaya, yenyewe imebarikiwa tu, ikafikiria  hao wengine wanaoadhibiwa kama Israeli wana laaana na mikosi kutoka kwa Mungu.

Lakini tukisoma mistari inayofuata inasema hivi..

Moabu amestarehe tangu ujana wake, naye ametulia juu ya sira zake, wala hakumiminwa kutoka chombo kimoja kutiwa chombo kingine, wala hakwenda kufungwa; kwa hiyo ladha yake anakaa nayo, wala harufu yake haikubadilika.

12 Basi, tazama, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo nitampelekea wamiminao, nao watammimina, nao watamwaga vyote vilivyomo vyomboni mwake, na kuzivunja chupa zake vipande vipande.

Umeona, kuna wakati ulifika, wakaldayo walikuja na kuwaangamiza na kuwachukua utumwani na kuwaharibu kabisa, na uzuri wao ukapotea ghafla, jambo ambalo hawakutazamia kama lingekaa liwapate, kama wengine.

Ndugu yangu, leo hii unatenda dhambi lakini huoni chochote, unazini Bwana hakuadhibu kwa lolote, unafanya mambo yako machafu kwa muda mrefu sasa, unakwenda kwa waganga, hauumwi, kinyume chake unazidi kustawi, unaendelea kufanya anasa na ulevu, unasema mbona hakuna dhara lolote linalonipata, hujiulizi ni kwa nini? Unachodhani ni kuwa wewe ni spesheli sana kwake sio?  embu soma mstari huu tena ujifunze jambo..

Sefania 1:12 “Kisha itakuwa wakati ule, nitauchunguza Yerusalemu kwa taa; nami NITAWAADHIBU WATU WALIOGANDA JUU YA SIRA ZAO; wasemao katika mioyo yao, Bwana hatatenda mema, wala hatatenda mabaya”.

Umeona, Mungu utafika wakati atakuchunguza kwa taa, wewe ambaye umetulia juu ya Sira yako, huangaishwi angaishwi, unafanikiwa angali upo katika dhambi, unayesema, Mungu hawezi fanya jambo lolote hata nikiwa mwovu kiasi gani.

Jiangalie, hukumu ipo, utakufa ghafla, na moja kwa moja utajikuta upo jehanamu kama yule Tajiri wa Lazaro, ambaye hapa duniani alikuwa akijitumaisha katika Maisha yake ya anasa tu, hajali kama kuna kuzimu, au hukumu, hajali kama kuna kiama chake mbeleni.. Na wewe ndipo utakapojikuta huko kama hutatubu, ukilia na kuomboleza, ukisema laiti ningelijua, laiti ningelijua..

Wakati huo utakuwa umeshachelewa ndugu. Leo hii ukiona Mungu hafanyi chochote juu ya dhambi zako, sio kwamba anayafurahia hayo Maisha unayoishi, anakutazama tu, yamkini siku moja utatubu, lakini ikifikia wakati haoni badiliko lolote la wewe kumgeukia yeye, atakujia na kukuondoa duniani kama alivyofanya kwa Wamoabu.

Biblia inasema saa ya wokovu ni sasa, na wakati uliokubali ni leo, usingojee siku Fulani ukasema hiyo ndio itakuwa siku yako ya wokovu, haitakaa ije kamwe. Mpe Yesu Kristo Maisha yako leo ayaokoe, Tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kisha tafuta mahali ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO ili upate ondoleo la dhambi zako, na Kisha mwenyewe Mungu atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu ili akae na wewe siku zote za Maisha yako.

Hata kama ikitokea Maisha yako yamefikia ukingo leo, basi unaouhakika wa kuurithi uzima wa milele.

Ikiwa utapenda kuokoka, na unahitaji msaada huo basi unaweza, kutafuta kanisa la kiroho lililokaribu na wewe, wakusaidie au ukawasiliana na sisi kwa namba zetu hizi +255693036618 /+255789001312 kwa ajili ya Sala ya Toba na maagizo mengine.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE! ULEVI NI DHAMBI?.

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?

UFUNUO: Mlango wa 15

Rudi nyumbani

Print this post

ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.

Shalom, karibu tujifunze Neno la Mungu. Biblia inatuambia..

 “Ondoa takataka katika fedha, Na chombo kitatokea kwa mtakasaji; (Mithali 25:4)

Tunapoiona dhahabu au madini mengine yote, yanang’aa sana, mpaka kufikia kiwango cha kuuzwa kwa thamani kubwa sana, hatupaswi kudhani, huko chini yanapochimbwa yanatoka kama yalivyo. Hapana, mengi ya hayo yanakuwa yamechanganyikana na mawe mengine au uchafu mwingi tofauti tofauti, kiasi kwamba unaweza kukutana na mwamba mkubwa sana, na ndani yake kukawa na kiwango kidogo sana cha dhahabu au fedha.

Hivyo, ili kuitapata dhahabu yenyewe safi, inawagharimu wafuaji wafanye kazi ya ziada, na kazi yenyewe ndio hiyo ya kutenganisha madini hayo kutoka katika hizo takataka nyingine, Zipo takataka ambazo unaweza kuziondoka kwa kuzichuja tu au kupepeta, lakini zipo ambazo itakuhijitaji utumie moto ili kuzitenganisha, kwasababu inakuwa zzimechanganyikana na dini lenyewe hadi ndani.

Hivyo wanachokifanya ni kwenda kuyachoma mawe hayo, kwa joto kali sana mpaka yayeyuke, na yakishayeyuka na kuwa kama uji uji,  ndipo sasa uchafu unajitenga na dhahabu yenyewe.  Kwa kupanda juu, hapo ndipo yule mfuaji anapoondoa uchafu ule,  na atarudia tena hizo hizo hatua kwa jinsi atakavyoweza, na kwa jinsi anatakavyozidi kuondoa takatakata hizo zote hata zile ndogo, ndivyo, mnga’o wa fedha hiyo unavyozidi kuja.. hatimaye, inatokea ikiwa nzuri sana yenye kunapendeza, tayari kwa matumizi yenye thamani.

Mithali 25:4 “Ondoa takataka katika fedha, Na chombo kitatokea kwa mtakasaji;”.

Hivyo na sisi pia kama wakristo, tunapookoka tunakuwa hatuna tofauti na fedha/dhahabu iliyochimbwa katikati ya miamba, tumetolewa huko tukiwa na mambo mengi ya kidunia  ambayo yameshikamana sana na sisi,

Sasa tunapookoka, kanuni ni ile ile inatugharimu tuingizwe katika moto, ili tuwe safi kabisa, Na moto huo anayetuingiza Mungu, na pia tunajiingiza sisi wenyewe.

Hapo ndipo utaona pale tunapokuwa wakristo tu, Mungu anaruhusu tupitishwe katika majaribu mbali mbali ya moto ili tuwekwe safi. Ndio maana biblia inasema;

1Petro 1:6 “Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;

7 ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo”.

Yakobo 1:2 “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;

3 mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi”.

Unaona, ni jambo la kawaida Mungu, kuwapitisha watoto wake katika majaribu ya namna mbalimbali, lengo sio kuwaangamiza, bali kuwaimarisha Zaidi.

Pia Neno la Mungu linatuambia na sisi wenyewe, tunapaswa tuondoe takataka katikati ya kila kitu tunachokifanya katika maisha yetu ya ukristo ili Mungu aweze kutufanya kama vile anavyotaka, iwe ni katika  huduma zetu, au  shughuli zetu n.k..

Tukitaka tumwone Mungu katikati ya Maisha yetu, tuondoe mambo ambayo hayampendezi, tuondoke uzinzi, tuondoe usengenyaji, tuondoke kuchat chati kusikokuwa na maana mitandaoni, na kutazama muvi muvi zisizotujenga, tuondoe mizaha, tuondoe unafki, tuondoe rushwa, tuondoe uvaaji mbovu,  n.k. Mambo kama haya tukiyazingatia basi Mungu, atatuletea ule mng’ao tunaostahili kuwa nao sisi kama wakristo, na tutakuwa wa thamani nyingi mbele zake na mbele za ulimwengu.

2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.

Kumbuka mambo kama haya kuyaondoa, haihitaji kuwa mlegevu legevu, inahitaji kujiingiza wewe mwenyewe katika moto wako, (kujinyima, kukataa na kuepuka) kila kitu ambacho unaona hakimpendezi Mungu. Hata kama nafsi yako inakitamani vipi, unakipinga. Unakubali kuonekana wa ajabu, lakini moyo wako uwe salama, na faida yake utaiona baadaye.

Vilevile hata katika Maisha yetu ya huduma, ili Kristo atende kazi vema, na ukuu wake uthibitike tunapaswa tuondoe mambo yote  maovu katikati ya kanisa, tusiwe radhi na wazinzi na wapotoshaji katikati yetu, na Mungu atajifunua miongoni mwetu.

Mithali 25:4 “Ondoa takataka katika fedha, Na chombo kitatokea kwa mtakasaji;

5 Mwondoe asiye haki mbele ya mfalme, Na kiti chake cha enzi kitathibitika katika haki”.

Bwana atusaidie sote, Na atubariki.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

Fuawe ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 41:7

NYAYO TUNAZOPASWA KUZIFUATA.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Mwandishi wa kitabu cha Warumi alikuwa ni Paulo au Tertio?

SWALI: Je! Mwandishi wa kitabu cha Warumi alikuwa ni Paulo au Tertio? kulingana na mstari huu;

Warumi 16:22 “Mimi Tertio, niliyeandika waraka huu, nawasalimu katika Bwana”.


JIBU: Paulo katika maneno yake ya utangulizi alishatupa  mwangaza kuwa yeye ndiye aliyekiandikia kitabu hicho, kiwaelekee watakatifu wote waliokuwa Rumi. Tusome;

Warumi 1:1 “PAULO, MTUMWA WA KRISTO YESU, ALIYEITWA KUWA MTUME, NA KUTENGWA AIHUBIRI INJILI YA MUNGU;

2 ambayo Mungu amekwisha kuiahidi kwa kinywa cha manabii wake katika maandiko matakatifu;

3 yaani, habari za Mwanawe, aliyezaliwa katika ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili,

4 na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu;

5 ambaye katika yeye tulipokea neema na utume ili mataifa yote wapate kujitiisha kwa imani, kwa ajili ya jina lake;

6 ambao katika hao ninyi mmekuwa wateule wa Yesu Kristo;

7 KWA WOTE WALIOKO RUMI, WAPENDWAO NA MUNGU, WALIOITWA KUWA WATAKATIFU. Neema na iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo”.

Lakini baadaye karibia na mwishoni mwa waraka huu tunakuja kumwona mtu mwingine aliyeitwa Tertio akijitokeza na kusema ameuandika waraka ule. Sio kwamba mtume Paulo hakuhusika hapana, Jibu ni kwamba Tertio alikuwa ni mwandishi wa mtume Paulo, aliyekuwa anamwandikia nyaraka zake. Aidha kwa kuandika kile alichokuwa anaambiwa au kwa kunakili kile alichoandikiwa na Paulo, japo hakuna sehemu nyingine katika biblia Tertio anaonekana akitajwa.

Na kulikuwa na sababu ya mtume Paulo kutokutumia mkono wake mwenyewe kuandikia waraka huu, pengine Tertio alikuwa ni mwandishi  mwaminifu anayejulikana sana  na watakatifu waliokuwa Rumi kwa umahiri na ufanisi wa kazi zake zilizothibitishwa. Hivyo mtu akiona waraka ulionakiliwa na yeye, basi ilikuwa ni rahisi kuamini uhalisia wa yule mwandishi husika. Kwasababu wakati huo walikuwepo pia watu waliojifanya ni mitume, na kutoa kopi zao wakidai kuwa ni za mitume, ili tu kuwachanganganya watu.

Na ndio maana mtume Paulo ili kuthibitisha nyaraka zake, sehemu nyingine alikuwa anatia sahihi yake mwishoni, soma(2Wathesalonike 3:17), na pia na hapa aliona  ni vema amtumie huyu Tertio kuuandika kwa warumi, iwe kama sahihi yake.

Hivyo waraka huu uliandikwa na Paulo, lakini aliyeunakili ni Tertio.

Hii ni kutufundisha kuwa, si kila kazi ya Mungu, hata kama tutaiona  ni nyepesi kiasi gani, tuifanye sisi mwenyewe, wakati mwingine tutahitaji tushirikiane na viungo vingine vya Kristo, ili kuleta ufanisi Zaidi wa kazi hiyo kwa watu wake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA FILEMONI.

Kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?

SWALI: Kitabu cha Henoko ndio kitabu kipi hicho, Je! Sisi kama wakristo tunapaswa kukiamini?


JIBU: Kitabu cha Henoko ni moja ya vitabu vya Apokrifa ambavyo viliandika kati ya miaka 200 kabla ya Kristo(KK), na  miaka 400 baada ya Kristo(WK). Vitabu hivi  vinaaminiwa na baadhi ya wakristo kuwa  vilihifadhiwa kwa siri, kutokana na kuwa vilikuwa na siri za ndani sana kuhusu Mungu na historia ya ulimwengu kwa ujumla, kiasi kwamba havikuweza kujumuishwa moja kwa moja kwenye biblia yenye vitabu 66 ambayo tunayo hivi sasa.

Lakini si kweli, vitabu hivi havikujumuishwa katika biblia takatifu kwasababu vilikuwa na siri za Mungu hapana badala yake vilionekana kujaa habari nyingi za kutungwa, ambazo zinakinzana na misingi ya imani ya Kikristo.

Sasa tukirudi katika hichi kitabu cha Henoko, kiligunduliwa kwenye miaka ya 1700 huko Ethiopia, baadaye kikasafirishwa mpaka Uingereza kwa ajili ya kutafsiriwa katika lugha nyingine, Kitabu hichi kilijulikana kama Henoko wa  Kwanza (1Henoko), kwasababu kulikuja kuwa pia na matoleo mengine yaliyofuata baadaye.

Vipande vya nyaraka vya kitabu hichi pia viligunduliwa huko Israeli mnao mwaka 1947, kwenye mapango yalikuwa katika fukwe za bahari ya chumvi (dead sea), Na kwenye mapango hayo kulionekana pia machapishi ya vitabu vyote vya agano la kale isipokuwa tu kitabu cha Esta, inasadikika ni vitabu ambavyo vilikuwa vimehifadhiwa huko na watu wa kale ambao waliishi kabla hata ya Kristo kuja duniani.

Sasa kitabu hiki kinamueleza Henoko ambaye alikuwa ni mtu wa saba kutoka Adamu kama tunavyosoma katika biblia Mwanzo 5:18-24…Henoko hakuonja mauti kama ilivyokuwa kwa wanadamu wengine, bali alinyakuliwa kama Eliya. Hiyo imekuwa ikawafanya watu wengi waamini kuwa mtu huyu alipewa siri nyingi za rohoni na kuziandika kwa ajili ya watu wa baadaye.

Hivyo kitabu hichi kilipogunduliwa, kilidhaniwa  kuwa mwandishi wake  ni Henoko, japo hilo jambo halikuthibitika kuwa ni kweli. Kitabu hichi kimejaa historia zinaeleza visa vya dunia ya kwanza kugharikishwa na maji, kinasema baadhi malaika wa Mungu  ambao walikuwa ni waangalizi wa huku ulimwenguni, ambao idadi yao ilikuwa ni 200 waliwaona binti za wanadamu, kisha wakawatamani, , hivyo wakashauriana washuke duniani wajitwalie wake, waishi nao, na kweli wakafanya hivyo  wakashuka duniani wakawapa mimba wanawake, ndio wakazaa wale majitu ambayo tunayasoma katika Mwanzo 6

Zaidi ya yote, malaika hawa kwa kuwa walikuwa na ujuzi, wakawafundisha wanadamu, kubuni silaha za chuma, kufanya uharibifu, wengine wakawafundisha wanadamu kufanya uchawi, na wengine kusoma nyota za mbinguni. Pamoja na hayo watoto wao waliowazaa wakawa wakatili kupita kiasi, ndio wale wanefili, wakawa wanaharibu kila kitu ikiwemo mimea, wanyama, mpaka wanadamu. Urefu wa majitu hayo ulikuwa ni futi 4500, sawa na Jengo la ghorofa 415. Jambo ambalo ni ngumu kusadikika,  Hakuna kiumbe cha namna hiyo kinaweza kuzaliwa na mwanamke. Japo wanefili kweli walikuwa ni wakubwa lakini sio kwa kiwango hicho.

Baadaye baadhi ya malaika wa mbinguni wakampelekea Mungu habari zao,  lakini Mungu akakataa kuwasamehe, akawafunga katika vifungo vya giza, ndio hapo Mungu akamwambia Henoko kuwa atakwenda kuiangamiza dunia kwa gharika.  Hii ndio habari ambayo inafahamika sana

Zipo habari nyingine katika kitabu hicho ambazo kiuhalisia hazina uhalisia wowote  na maandiko.

Tunapaswa tujue vitabu hivi vimejaa hadithi nyingi za kutungwa, ambazo ni sumu kwa Mkristo, na ndio maana huwezi kuziona vikijumuishwa katika biblia yenye vitabu 66 vilivyovuviwa na Roho Mtakatifu, kwasababu vinakinzana na misingi ya kweli ya maandiko.

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 22:29 “Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.

30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni”.

Unaona? Hakuna andiko lolote linaloonyesha kuwa malaika wanaoa, au wanazaliana, malaika hawakuumbiwa viungo vya uzazi kama tulivyonavyo sisi, hawahitaji kuzaliana, wao tayari walishaumbwa, ndivyo walivyo na idadi yao tayari ipo kamili, Lakini kusema walishuka duniani, ni fundisho la uongo ambalo wakristo wengi wanaliamini mpaka leo, na chanzo chake walikitoa katika hichi kitabu cha Henoko.

Waliowaona binti za wanadamu wakawatamani, walikuwa ni watakatifu wa Mungu, ambao hao hawakujichanganya na mambo ya ulimwengu tangu mwanzo, bali walitumia sehemu kubwa ya maisha yao, kuliita jina la Bwana na kumwabudu Mungu soma Mwanzo 4:26 utalithibitisha hilo ndio ule  uzao wote wa Sethi (Wakina Henoko, Methusela, Na Nuhu).. Lakini binti za wanadamu walikuwa ni watu wa kidunia tu, ambao walitokea katika ule uzao wa Kaini..hao ndio tangu mwanzo walikuwa na ujuzi mkubwa, na hodari na pia wakatili ukisoma pale Mwanzo 4:16-23 utaona ni jinsi gani, uzao wa Kaini ulivyokuwa hodari, wenye ujuzi mwingine, lakini pia mwovu kwa uuaji, kama Baba yao alivyokuwa.

Baadaye sasa walipojichanganya mbegu ndipo Mungu akakasirika, akaghahiri na kuuangamiza ulimwengu wote, ni sawa na leo hii, Mungu aone, watakatifu wake wote, wanaiga na kufanya mambo ya ulimwengu, wanawake wanavaa vimini, wanatembea nusu uchi barabarani, wanaume watakatifu wanakuwa mashoga n.k. kiasi kwamba huwezi kuona tofauti yoyote kati yao na ulimwenguni, hapo kinachofuata ni Mungu kuuteketeza ulimwengu, ndivyo ilivyokuwa kwa watu wa kipindi kile. Watakatifu walijitofautisha kabisa na wana wa ulimwengu..

Hivyo hakuna sababu ya mkristo kuamini, moja kwa moja vyanzo ambavyo havipo katika biblia, kwasababu vingi kati ya hivyo vinakasoro nyingi na vimejaa hadithi nyingi zilizotungwa na wanadamu lakini sio kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu.

Kwamfano kwasasa Kanisa Katoliki, limeamua kuchukua baadhi ya hivi vitabu vya Apokrifa na kuviongezea kwenye biblia takatifu yenye vitabu 66, kufikia 73. Vitabu vyenyewe ikiwemo Yudithi, Baruku, Yoshua bin Sira, Wamakabayo 1&2,  Hekima.

Vitabu hivi vinakinzana na misingi ya imani, kwamfano, vinafundisha kwenda toharani, yaani mtu mwenye dhambi anaweza kwenda mbinguni tena, lakini baada ya kupitishwa mahali panapoitwa toharani ili kutakaswa,.,Fundisho lingine ni kuwa Mungu, anasikia maombi ya wafu, mambo ambayo ni uongo, biblia inasema, mtu ameandikiwa kuishi mara moja na baada ya kifo ni hukumu (Waebrania 9:27).

Kwahiyo, vitabu vya Aprokifa, sio vya kuviamini, kama uaminivyo biblia, iwe ni kitabu cha Henoko, au kingine chochote kile nje ya vitabu 66 vya biblia sio vya kuiamini vinamakosa mengi na wakati mwingine vimejaa uongo mwingi, ambao unapotosha kabisa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi nyumbani

Print this post

KOIKOI ANGANI AJUA NYAKATI ZAKE ZILIZOAMRIWA.

Yeremia 8:7 “Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za Bwana”.

Koikoi, mbayuwayu na korongo ni ndege wa ajabu sana, ni ndege wenye uwezo wa kusoma majira ya dunia, Na hiyo imewasaidia sana, kuishi maisha ya salama salmini huku duniani, pasipo kukumbana na changamoto zozote  zisizo na maana.

Hawa ni ndege ambao kikikaribia kipindi cha baridi wanahama wote waeneo yao wanayoishi kwa muda, na kusafiri umbali mrefu sana, kwenye pembe ya pili ya dunia kutafuta msimu tulivu aidha wa vuli au  wa joto ulipo wakatulie, kisha baadaye hali ya baridi ikishakwisha wanarudi katika makazi yao ya awali kuendelea na maisha yao ya kawaida.

Kumbuka baridi tunayoizungumzia ni ile baridi haswaa, ya kutengeneza barafu iliyopo huko nchi za ulaya, ambayo hata mtu wa kawaida akikaa nje masaa machache tu anageuka kuwa jiwe la barafu, haijalishi atavaa masweta makubwa kiasi gani.. Baridi ya namna hiyo watu wanaoishi huko wanatumia muda wao mwingi kuwepo ndani, na hata kazi zao wanazifanyia ndani katika nyumba zilizojengwa kitaalamu kuhifadhi joto ndani, kwani nyumba za kawaida kama hizi zetu, kule hazijengwi kwasababu zinapitisha baridi, kiasi kwamba ukibaki ndani yake, ukakaa huko mpaka asubuhi ukiamka umeganda. Huku kwetu Afrika hatuna baridi ya namna hiyo.

Sasa, ndege hawa, wanaelewa kabisa kwa namna ya kawaida hawawezi kuishi katika mazingira hayo ya baridi kali, kwasababu hata viota vyao vitaganda.. Sasa ili kulitatua hilo tatizo inawagharimu wahame kwa muda, ndio hapo wanasafiri maelfu ya kilometa wanakuja mpaka huku kwetu Afrika, au nchi nyingine zenye joto, wanakaa  huko mpaka msimu wa baridi  utakaposhakwisha kule Ulaya ndio wanarudi sasa, kuendeleza maisha yao ya sikuzote.

Sasa Mungu ametumia mfano wa ndege hawa wasio na akili, kutushangaa sisi wanadamu wenye akili timamu kwanini hatujui hukumu zake alizoziweka hapa duniani..anasema..

“Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za Bwana”

Hii ikiwa na maana tunashindwa kujua wakati wa neema ni upi, na wakati wa hukumu za Mungu ni upi.. Sisi tupo tu hatujui majira yetu, tunadhani wakati wote, hii neema ya wokovu itaendelea kuwepo, tunadhani wakati wote, hali itakuwa kama ilivyo sasa hivi, utahubiriwa injili kama unavyohubiriwa sasa hivi..

Ndugu yangu, fahamu kuwa neema hii inakwenda kuisha siku sio nyingi, Dhiki kubwa ambayo haijawahi kutokea tangu dunia iumbwe na wala haitakaa iwepo itakwenda kutokea ulimwenguni kote..Dalili zote zinaonyesha, pengine katika wakati wetu huu tunaoishi tutayashuhudia hayo..Haya majira ya neema ndio yanaishia hivyo, muda huu tulionao ni wa nyongeza tu, dunia ingepaswa iwe imeshakwisha tangu zamani, lakini kwasababu tu ile nuru ndogo ya jioni ipo ndio maana unaona mambo bado yapo hivi..

Tumeshafikia wakati ambao Yesu hatuhubirii  tena injili ya kutuvuta kwenye wokovu, kama ilivyokuwa zamani bali anatuhubiria injili ya kuthibitisha ulichokiamini. Sikiliza anavyosema..

Ufunuo 22:10 “Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.

12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.

Unaona, hiyo yote ni kwasababu ya unafki tulionao sasa, kwasababu kama tunaweza kuyatambua majira ya nchi, kwamba huu ni msimu wa masika na hivyo tunaanza kuyaandaa mashamba yetu kabla ya mvua kunyesha, au tunahama mabondeni mapema mafuriko yasitukute, inakuwaje basi, tunashindwa kuzitambua siku hizi kuwa ni siku za mwisho? Korona inakufundisha nini? Vimbunga vinakufundisha nini, Hili wimbi la manabii wa uongo unaloliona leo hii limezuka duniani kwa ghafla linakufundisha nini? . Bado tu huoni, hizo ni dalili za wazi kabisa ambazo zinatutambulisha kuwa tukio la unyakuo lipo karibu?

Yesu alisema..

Luka 12:54 “Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya”?

Itakuwa ni ajabu sana tukishindwa akili na akina koikoi. Tujitathimini sana, tuamke katika usingizi huu mzito, hukumu ya Mungu juu ya ulimwengu wote ipo karibu. Kama upo nje ya safina, anza safari upesi, mkimbilie Kristo kwa kumaanisha kabisa kwa moyo wako wote akuokoe, kwasababu hatuna muda mrefu hapa duniani,

 mbingu na nchi zitapita lakini maneno ya Bwana Yesu hayatapita milele.

Mbingu ipo,lakini pia kuzimu ipo, uchaguzi ni wa wako,

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

WAENDEE WANA WA ISAKARI, UWE SALAMA.

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

SWALI: Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi?

Kwanini kuna mahali Bwana Yesu anawaita wale aliowaita mitume, na sehemu nyingine anawaita wanafunzi, tofauti yao ni ipi? Au ni kitu kimoja?


JIBU: Si kila mwanafunzi ni mtume, lakini kila mtume ni lazima awe mwanafunzi wa Yesu.

Mwanafunzi ni mtu ambaye anaketi chini kufundishwa, kupewa ujuzi au utashi au maarifa ya kumsaidia kuishi au kufanya jambo Fulani, Na Bwana Yesu naye alikuwa na watu wa namna hiyo hiyo,

Lakini kumbuka si wote waliomfuata waliitwa wanafunzi wake, isipokuwa wale tu waliokidhi vigezo vyake alivyoviweka, na vigezo vyenyewe ndio hivi;

Luka 14:25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,

26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia?

29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,

30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.”.

Lakini Mtume maana yake ni “aliyetumwa”,   Wale walioitwa na Bwana Yesu na kuandaliwa kwa jukumu Fulani maalumu waliitwa mitume, ambao walikuwa kumi na mbili tu kwa wakati ule. Na kusudi lenyewe waliloitiwa lilikuwa hili;

Mathayo 28:19 “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa Dahari”.

Mitume pia waliendelea kuitwa na Kristo hata baada ya yeye kuondoka duniani.. Mfano utawaona  mitume  kama  Paulo,  Barnaba, na Epafrodito (Wafilipi 2:25)

Hata kwa wakati huu wa sasa, watumishi wote wa Mungu wanaofanya kazi kama waliyoifanya mitume, Yesu anawatambua kama mitume wake, hawa ni Zaidi ya wanafunzi, kwasababu hawawi wakristo tu peke yake, bali Zaidi wanajitaabisha kwa ajili ya ufalme wa mbinguni.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.

Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?

USITAFUTE KUKANWA NA BWANA SIKU ILE.

Rudi nyumbani

Print this post

Fumo ni nini kama tunavyosoma katika biblia? (Hesabu 25:7)

Fumo ni mkuki, lakini katika biblia Neno mkuki linatumika kwa namna mbili, upo mkuki wa kuchomea, na pia upo mkuki wa kurusha.

Ule mkuki wa kuchomea ndio unaoitwa Fumo, ambao askari wanaubeba, na kuchoma maadui zao pale wanapowakaribia,  na kwa kawaida unakuwa ni mizito kidogo na mrefu na wenye ncha kali. Lakini ule mwingine wa kurusha wenyewe kibiblia unajulikana kama mkuki tu hivyo hivyo, isipokuwa wenyewe ni mwepesi kidogo na umetengenezwa hivyo ili utakaporushwa uweze kufika mbali zaidi adui alipo. Zote hizi ni silaha za kivita.

Hivyo unaweza kukutana na haya maneno mawili kwenye biblia yakakuchanganya.. kwa mfano baadhi ya vifungu vinayatajwa maneno yote mawili ni kama vifuatavyo.

1Samweli 17:45 “Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana”.

Ayubu 41:26 “Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii; Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha”.

Vifungu vingine ambavyo utakutana na hili neno “Fumo” Ni kama vifuatavyo;

Hesabu 25:7 “Naye Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona jambo hilo, akaondoka hapo katikati ya mkutano, akashika fumo mkononi mwake;

8 akamwandama huyo mtu wa Israeli na kuingia ndani ya hema nyuma yake, naye akawachoma wote wawili kwa fumo lake, yule mume wa Israeli na huyo mwanamke kati ya tumbo lake. Basi pigo likazuiwa kwao wana wa Israeli”.

1Samweli 17:7 “Na mti wa fumo lake ulikuwa kama mti wa mfumaji; na kichwa cha mkuki wake kilikuwa shekeli mia sita za chuma uzito wake; na mtu aliyemchukulia ngao yake akamtangulia”.

1Samweli 26:12 “Basi Daudi akalitwaa lile fumo, na lile gudulia la maji, kichwani pa Sauli; nao wakaenda zao, wala hapana mtu aliyeliona jambo hili wala kulijua, wala kuamka; maana wote walikuwa wamelala; kwa kuwa usingizi mzito kutoka kwa Bwana umewaangukia”.

Soma pia 2Samweli 1:6, Ayubu 39:23,

Halikadhalika na sisi  kama wakristo rohoni ni lazima tuwe na FUMO zetu na MIKUKI yetu mikononi mwetu, ili tuitwe askari kamili wa  Kristo, hizo ndio zile silaha za mkono wa kuume zinazozungumziwa katika 2Wakorintho 6:7… Kwa hizo, ndivyo tutakavyoweza kumpiga shetani, tukizikosa, tujue kuwa shetani hatoweza kutuogopa, na silaha yenyewe ni ufahamu wa kuyatambua mamlaka tuliyopewa katika jina la YESU na DAMU yake. Na kuyatumia..

Yeye mwenyewe alisema..

Luka 10:19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.

Kila mmoja wetu ambaye anasema ameokoka anapaswa ajue kuwa mamlaka hayo amepewa, Hivyo simama kama shujaa, hubiri, haribu kazi za shetani, wafungue watu, mwaribu shetani na kazi zake zote katika maombi. Kwasababu Fumo zetu na mikuki yetu ipo  mikononi mwetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

NYAYO TUNAZOPASWA KUZIFUATA.

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

Rudi nyumbani

Print this post

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya huu mstari?

Wakorintho 3:17 “Basi ‘Bwana’ ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru”.


JIBU: Kauli hiyo kinyume chake ni kuwa, kama  Roho wa Bwana hayupo basi mahali hapo hapana uhuru wowote, kwa mujibu wa biblia.

Lakini ni uhuru wa aina gani Roho Mtakatifu analeta.

kibiblia Roho Mtakatifu alikuja kuleta Uhuru wa aina mbili.

  • Uhuru wa kutuondoa katika utumwa wa dhambi na mateso.

  • Uhuru wa kututoa katika utumwa wa sheria.

1). Tukianzana na uhuru wa kutuondoa katika utumwa wa dhambi;

Siku ile Bwana Yesu alipoanza huduma yake ya kuhubiri alisema maneno haya..

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Umeona hiyo ni kuonyesha kuwa Roho Mtakatifu aliposhuka juu ya watu wake na katika kanisa alikuwa na kazi ya kuwatoa watu katika vifungo vya dhambi na mateso ya  ibilisi, yaani waliokuwa wanasumbuliwa na mapepo, waliokuwa wanateswa na magonjwa, na hofu, na mauti, na shida  vyote hivyo vilikuja kuondolewa na Roho Mtakatifu mwenyewe,

na pia ukizidi kusoma tena katika Isaya 61:3-4 utaona unabii huo wa Roho Mtakatifu unaendelea kusema..

“…kuwafariji wote waliao; 3 kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe”.

Unaona anafanya pia kazi ya kuwatoa watu katika huzuni zao, kuwafariji,kuwapa mataji ya utukufu na sifa. huo ni Zaidi ya Uhuru, ambao hakuna mtu yeyote hapa duniani angeweza kuutoa.

2). Uhuru wa sheria;

Pia alikuja kutukomboa sisi tuliokuwa chini ya sharia, tutoke katika laana ya sheria..

Wagalatia 4:3 “Kadhalika na sisi, tulipokuwa watoto, tulikuwa tukitumikishwa na kawaida za kwanza za dunia.

4 Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria,

5 kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana.

6 Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.

7 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu”.

Roho Mtakatifu alikuja kututoa katika utumwa wa sheria, ili tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Yesu Kristo na sio kwa matendo yetu tena. Kwasababu hapo mwanzo tulijitahidi sana kumpendeza Mungu kwa kushika sheria, lakini sheria ilituzidi nguvu, kwasababu ya udhaifu wa miili yetu. Hivyo tangu enzi za agano la kale, hakuwahi kuonekana hata mmoja aliyeweza kumpendeza Mungu kwa matendo yake mwenyewe, haijalishi walijitahidi kiasi gani.

Hivyo ili Mungu kutuokoa,  alimtuma mwanawe Yesu Kristo duniani, ili yeye peke yake atende mema, pasipo kufanya dhambi yoyote, kisha Mungu amuhesabie haki yeye peke yake kwa matendo yake, na ndipo sasa sisi  tutakaomwamini Yesu baadaye tuhesabiwa haki kama vile yeye, kwa njia ya matendo yake na sio yetu..

Kwahiyo, ikiwa wewe umemwamini Yesu, na ukampokea Roho wake, basi ujue Mungu haangalii matendo yako, kama ndio kipimo cha yeye kukubali, bali anamwangalia mwana wake YESU KRISTO uliyemwamini, na hivyo unahesabiwa haki, kama vile hujawahi kumkosea Mungu, kwasababu VAZI la Yesu linakufunika mbele yako.

Huoni kama huo ni uhuru mkubwa sana? Unahesabiwa haki kwa kumwamini tu!  Lakini ikumbukwe kuwa hiyo haimaanishi kuwa tuendelee kutenda dhambi kisa tu hatuhesabiwi haki kwa matendo yetu, hapana, hata kwa namna ya kawaida, huwezi kwenda kupeleka mkono kwenye tundu la nyoka akung’ate kila saa, kisa tu dawa ya kutibu sumu ipo, hapana, vinginevyo utakuwa mwendawazimu, bali utachukua tahadhari kubwa sana, kwa kuzidi kukaa mbali na nyoka, kwasababu unajua sumu yake sikuzote ni kifo..

Na sisi vivyo hivyo maadamu tunahesabiwa haki kwa kumwamini Yesu Kristo ni jukumu letu sote, tukae mbali na dhambi, kwa kadiri tuwezavyo, katika utakatifu wote ili tupate kumzalia Mungu matunda. Na hiyo ndio ishara ya kuamini kwetu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa Roho Mtakatifu ametuletea uhuru mkubwa sana hapa duniani.  kiasi kwamba mtu yeyote atakayempokea, atakuwa HURU KWELI KWELI. Jambo ambalo watu wengi hawalifahamu, wakidhani kwa Mungu ni utumwa.

Swali ni je wewe umeshampokea ndani yako? Kama jibu ni la, unasubiri nini? Kumbuka Pasipo Roho Mtakatifu huwezi kwenda katika unyakuo, na haji ndani yako isipokuwa  kwanza umemwamini  Yesu Kristo, kwa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa na kuwa tayari kuyaacha mambo yako maovu uliyokuwa unayafanya huko nyuma. Na pili kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele, na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, Na hapo ndipo Mungu atakapokupa kipawa cha Roho Mtakatifu ndani yako bure.

Hivyo ikiwa utapenda kumkaribisha Yesu maishani mwako, basi tafuta mchungaji yoyote, au mtumishi yoyote aliyesimama katika Imani, akusaidie, au wasiliana nasi kwa namba hizi: +255693036618 / +255789001312

Mungu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

2Wathesalonike 3:13 inasema..

“Lakini ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema”.

Unajua mpaka biblia inakuambia usikate tamaa, inamaanisha kuwa si kitu chepesi kukishikilia wakati wote. Si kitu ambacho unaweza ukaona faida yake moja kwa moja pale unapokifanya.. Lakini katika yote hayo bado inakuambia usikate tamaa.

Ili jambo lolote liwe wema, ni lazima malipo yake yasilingane na huduma iliyotolewa. Kwamfano mtu anapokwenda kuwasaidia yatima au maskini, huo ni wema, kwasababu hawana cha kumlipa hata baada ya kuwapa mahitaji yao, au pale anapowasomesha ndugu, huo nao ni wema, kwasababu pesa hizo ungeweza kuzitumia katika mambo yake mengine lakini ameona vema, ujinyime yeye uwape wengine maarifa.. Au unapowapa wengine chakula au mavazi bila kuwachaji pesa au kuwadai kitu chochote huo ni wema.. Au unapowapa wengine maarifa ya ufalme wa mbinguni bila malipo yoyote huo nao ni wema mkuu sana n.k.

Lakini katika hayo, kuna wakati akili inaweza kukujia, ukajisikia kuchoka na kusema nimeshasaidia watu sana mbona sioni faida yoyote ya kufanya hivyo? Au mbona sioni nikirudishiwa fadhila yoyote kutoka kwao? Wacha nipunguze wema wangu, nianze kujijali mimi mwenyewe. Au nitafute mambo yangu mwenyewe.

Katika mazingira kama hayo, biblia inasema.. usichoke kutenda wema..Kwasababu ni mbegu nzuri sana ambayo unaipanda leo, lakini siku moja utavuna matunda yake ukiwa mvumilivu.

Wagalatia 6:9 “Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho”.

Hata kama utaona wale uliowatendea mema wamekutangulia,wewe umekuwa daraja kwao la kufika juu, au wengine wamekudharau kwa ukarimu wako, bado usichoke katika kutenda kwako, kwasababu hicho unachokipanda thamani yake ni kubwa kuliko fedha au dhahabu. Utakuja kujua vizuri utakapovuka kule ng’ambo.

Katika biblia, tunamwona, mtu mmoja aliyeitwa Mordekai, yeye alikuwa ni mlinda mlango wa mfalme, lakini siku moja baadhi ya watumishi walipanga njama ili wamuue mfalme. Mordekai alipopata habari, kwasababu alikuwa ni mtu mwema, hakukaa kimya bali alikwenda kutoa taarifa ya njama hizo, na hatimaye mfalme akanusurika kifo, lakini biblia inatuonyesha akasahaulika, muda mrefu ukapita, wala hakuna aliyekumbuka wala kujali wema wake.

Siku moja akiwa katika hatihati ya kuuliwa na adui yake aliyeitwa Hamani, biblia inatuambia usiku huo huo mfalme alikosa uzingizi kabisa, ndipo akaanza kupitia vitabu vya kumbukumbu za taarifa za kifalme, ndipo akakutana na tukio la wema alilofanyiwa na Mordekai, mfalme akauliza je mtu huyu alitendewa fadhila gani?, wakasema, hakutendewa lolote. Ndipo akatoa maagizo kwamba avikwe mavazi yake ya kifalme anayoyavaa yeye, kisha apandishwe kwenye farasi ambaye yeye mwenyewe ndiye anayempanda, kisha wamzungushwe mji mzima, huku akipigiwa mbiu, ili atukuzwe mbele ya watu wote, kwasababu mfalme AMEMUHESHIMU biblia inasema hivyo;. Soma Esta 6

Sasa mambo hayo yanafunua na ya rohoni pia. Ukiwa ni mtenda wema, ipo Heshima ya kipekee sana, itokayo kwa Mungu mwenyewe, italetwa juu yako, siku ile ikifika. Atakugawia ule utukufu wake mwenyewe,.. Biblia inasema..

Warumi 2:6 “atakayemlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake; 7 wale ambao KWA SABURI KATIKA KUTENDA MEMA WANATAFUTA UTUKUFU NA HESHIMA NA KUTOKUHARIBIKA, watapewa uzima wa milele; 8 na wale wenye fitina, wasioitii kweli, bali wakubalio dhuluma, watapata hasira na ghadhabu; 9 dhiki na shida juu ya kila nafsi ya mwanadamu atendaye uovu, Myahudi kwanza na Myunani pia; 10 BALI UTUKUFU NA HESHIMA NA AMANI KWA KILA MTU ATENDAYE MEMA, Myahudi kwanza na Myunani pia”;

Unaona? hivyo, usichoke kutenda mema, kumbuka wema mkuu ni pamoja na kuwakumbuka walio katika dhambi na kuwavuta kwa Bwana. Pia kuwafariji na kuwaombea wale waliowadhaifu katika Imani. Swali ni je! Katika maisha yako, ni mema mangapi, ulishawahi kufanya kwa ajili ya Mungu?

Bwana atusaidie, tuyatimilize yote.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

FAHAMU UWIANO MUNGU ANAOHITAJI KUUONA KWETU.

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

Rudi nyumbani

Print this post