by Devis | 4 October 2020 08:46 pm10
Kuhusu Huduma ya Wingu la Mashahidi – Nuru ya Upendo wa Kristo
Wingu la Mashahidi ni huduma ya kiinjilisti iliyo chini ya Kanisa la NURU YA UPENDO WA KRISTO, yenye lengo kuu la kusambaza habari njema za wokovu alioletwa na Bwana wetu Yesu Kristo kwa watu wote kupitia mitandao ya kijamii na mtandao wa intaneti.
Biblia Takatifu ndio kitabu pekee kilichovuviwa na Roho Mtakatifu, chenye mamlaka ya kuwakomboa na kuwakamilisha wanadamu. Mafundisho yote katika tovuti na huduma hii yanategemea maandiko hayo.
Tunaamini kuwa wokovu unapatikana kwa mmoja tu: YESU KRISTO – kwa kumwamini, kubatizwa kwa jina lake, na kupokea Roho Mtakatifu kulingana na Matendo 2:38.
Tunaamini kuwa tupo katika nyakati za mwisho, na tunatazamia kurudi kwa Bwana Yesu Kristo kupitia tukio la unyakuo.
Huduma hii haina uhusiano wowote na dhehebu la “Mashahidi wa Yehova.”
Jina “Wingu la Mashahidi” limetokana na andiko la Waebrania 12:1:
“Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu.”
Kama walivyokuwa mashahidi wa zamani, mimi na wewe pia tunaweza kuwa sehemu ya wingu hilo, kwa kuishi maisha ya ushuhuda na kushiriki habari njema za wokovu kwa watu wote.
Huduma ya Wingu la Mashahidi inawakaribisha watu wote waliookoka kutoka kote ulimwenguni wenye imani moja katika Kristo Yesu, ili kushirikiana katika kueneza injili kwa kila mtu.
📍 Tunapatikana Tegeta, Tanzania.
Kwa maswali, maombi, au msaada wa kumpokea Yesu Kristo maishani mwako:
📞 +255789001312
📞 +255693036618
Au tuandikie kwenye kisanduku cha maoni kilicho chini ya ukurasa.
Source URL: https://wingulamashahidi.org/kuhusu-sisi/
Copyright ©2025 Wingu la Mashahidi unless otherwise noted.