Category Archive maswali na majibu

Mishale ya moto ya mwovu inayozungumziwa kwenye Waefeso 6:16 ni ipi?

Waefeso 6:16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu

Waefeso sura ya 6, inaeleza mapambano ambayo yapo rohoni kati ya sisi na ufalme wa giza, na namna ambavyo tunapaswa tusimame kushinda vita hivyo, kwa kuvaa zile silaha zote za haki zinazotajwa pale. Kama vile chapeo ya wokovu, dirii ya haki, kweli kiunoni, upanga wa Roho,  na ngao ya Imani,.

Lakini pia katika vifungu hivyo tunaelezwa mojawapo ya silaha ya adui, nayo ni “mishale ya moto”. Swali Je hii mishale ya moto ni ipi?

Mishale ni silaha zilizotumika zamani, za kumshambulia adui kwa mbali, na hivyo ili kuziboresha waliweka moto kwa mbele ili zitakapomfikia adui basi zilete madhara zaidi ya yale tu ya  kutoboa, bali kuunguza kama sio kumuharibu kabisa adui.

Tofauti na silaha kama rungu, au upanga ambavyo vinahitaji uso kwa uso kutumika. Kwa mbali havina matokeo.

Tukirudi katika ulimwengu wa sasa mishale ya vita  ni makombora, Kwanini hapo shetani anaonekana akirusha mishale kutokea mbali? Ni kwasababu kwa karibu hamwezi mwamini, kwani nguvu zilizo ndani yake ni nyingi kuliko alizonazo.

Ifuatayo ni mishale ya moto ya adui.

1) Ulimi:

Shetani hutumia sana ulimi kuleta, aidha udanganyifu,  mafarakano, vita n.k. Ndio maana maandiko yanasema;

Yakobo 3:5 Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum.

7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu.

8 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.

9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.

10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo.

Hawa alidanganywa na Nyoka kwa ulimi, Mafundisho ya uongo, huanzia katika maneno. Hivyo sisi kama watoto wa Mungu ni lazima tuijue silaha hii na kuidhibiti kwanza sisi wenyewe ndani yetu, kuhakikisha hatutumiki kama warusha mishale, kwa kusema yasiyopasa, lakini pia kusimama kwa imani kuhakikisha, tunakuwa thabiti kiimani, kwa kupuuzia, au kutokuweka moyoni kila Neno linalosemwa kinyume chetu, sambamba na kuwa makini kwa kupima kila neno tunaloambiwa kama kweli ni la Mungu au la!.

Mkristo usipojua silaha hii ya adui, utajikuta kila kukicha unaishi kwa machungu ya maneno ya watu, huna raha, una mashindano,  au utajikuta unaanguka katika mikono ya manabii wa uongo, na hatimaye shetani anakuwa amekupata.

2) Mshale wa moto pia ni Majaribu.

1Petro 4:12 Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.

13 Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia

Majaribu yote hutoka kwa Yule mwovu, lengo lake ni kumwangusha mwamini ili amwasi Mungu, hata wakati ule Bwana Yesu anakaribia kusulubiwa, alimwombea Petro ili imani yake isitindike, kwasababu alijua wataingia kwenye majaribu makubwa, kwa upungufu wa maombi yao. Vivyo na sisi yatupaswa tuwe waombaji ili tuizime mishale ya majaribu mbalimbali ya adui tusiyojua pembe ipi yanatokea.  Na pia tunapojikuta ndani ya hayo majaribu, yatupasa kuishikilia imani yetu hasaa, kwa kuamini kuwa Bwana yupo pamoja nasi kutengeneza njia ya kutokea.

3) Mishale mingine ni vitisho, hofu , mashaka

Shetani akijua kuwa hana nguvu ya kumshinda mwamini moja kwa moja,  hivyo hupenda kuinua ujasiri wake kama silaha, na akiwa mbali anajua akirusha mishale yake kisha Yule mtu akiiogopa basi anamwangusha. Ndio hapo huleta vitisho, mfano wa kipindi kile cha wana wa Israeli walipopewa agizo la kwenda kumjengea Mungu nyumba Yerusalemu, tunasoma baada ya kipindi kifupi maadui zao wakainuka, na kuwasemelea kwa mfalme, hatimaye marufuku ikatoka, wasiendeleze ujenzi, hivyo mahali pa Mungu pakabaki gofu tu la msingi kwa muda mrefu, kisa hofu ya utalawa mpya. Lakini baada ya muda mwingi sana, tunaona Mungu akawaamsha  mioyo Hagai pamoja na Zekaria, na kuwaambia  Israeli kwanini wameacha kuijenga nyumba ya Bwana.  (Hagai 1:1-9), walipogundua makosa yao, kwa kuruhusu hofu, Ndipo walipoamka kwa ujasiri tena na kuijenga, Mungu akawafanikisha sana.

Vivyo hivyo na sisi, tumepewa agizo la kuhubiri injili, ikiwa itapingwa, au tutatishiwa kuuawa au kufungwa, ikiwa tutapitishwa kwenye miiba au miamba hatupaswi kuogopa mishale hiyo, bali tusimame kwa imani kama akina Shedraki na Danieli, wakiwa katika matanuru ya moto, na matundu ya simba hawakutetereka. Bali walimtumaini Mungu anayewaokoa, na hatimaye kweli ikawa vile.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba ipo kweli mishale mingi ya moto, ya adui lakini hiyo mitatu ndio mikuu. Na tukiweza kusimama kwa imani basi shetani pande zote anakuwa ameshindwa kabisa kabisa, (Akiwa karibu na vilevile akiwa mbali) linda kinywa chako /puuzia/ pima maneno unayoyasikia, vilevile kuwa mwombaji ili usiingie majaribuni/ uyashinde majaribu, Lakini zaidi sana kamwe usiogope vitisho vya adui, kwasababu hawezi kufanya lolote kwa ihari yake mwenyewe.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

TUZIDI KUWA HODARI KATIKA BWANA.

Print this post

Tofauti kati ya dhehebu na dini ni ipi?

Dini ni mfumo au utaratibu wa kumwabudu Mungu. Kwamfano ukienda mahali ukaona watu wamekusanyika na kukubaliana kuabudu kitu Fulani, ni lazima utaona tu utaratibu, au mwongozo au miiko wamejiwekea ya kuifuata na kuishika, ili ibada yao iwe na matokeo. Sasa huo utaratibu ndio unaitwa dini.

Hata imani yetu ndani ya Kristo, inasukumwa na dini. Hatumwabudu tu Mungu kama tunavyotaka bali Mungu aliweka utaratibu na njia ya kuifuata.

Lakini Dhehebu, ni “aina ya dini”. Ambayo huzalika ndani ya imani ile ile moja. Kwamfano utaona wakristo imani yao ni moja kwa Kristo Yesu, na msingi wa kuegemea ni biblia ile ile moja takatifu. Lakini ndani yao kuna michipuko mingi tofauti tofauti ya kitaratibu na ufanyaji ibada, kulingana na walivyoielewa biblia. Ndio hapo utaona wengine wanajiita wapentekesto, wengine wakatoliki, wengine wasabato, n.k. Sasa hii yote ni michupuko, ambayo mengine inakaribiana sana na uhalisia, na mengine inakwenda mbali na kweli ya Mungu.

Lakini cha kumshukuru Mungu ni kuwa biblia imeshaeleza asili ya dini ya kweli inapaswa iweje….

Yakobo 1:26 Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai. 27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.

Kwamba ni lazima itakuwa ya kimatendo zaidi. Yaani utafunzwa utakatifu, na kujitoa.

Swali lingine je! Dhehebu linampeleka mtu mbinguni?

Hapana, kwasababu Yesu hakuja kuleta dhehebu jipya duniani. Kwani alipokuja alikuta tayari yapo madhehebu mengi yamesha-zaliwa kama tu ilivyo sasa, mfano Mafarisayo, na masadukayo. Lakini hakuwahi kutetea lolote kati yao. Bali alisisitiza watu kumwamini yeye, kama ndio njia ya kweli na uzima mtu asipofanya hivyo hawezi  kumwona Baba (Yohana 14:6).

Ikiwa na maana haijalishi una dhehebu zuri kiasi gani. Ukikosa shabaha ya Ukristo, bado mbinguni huendi. Waamini wengi wanashikilia zaidi dini, jambo ambalo ni jema, lakini dini ni kisaidizi cha imani. Sio imani yenyewe, ni sawa na shule na elimu, tunaweza kusema shule ni kisaidizi cha elimu, lakini sio elimu yenyewe.

Hivyo ni busara kuchukua tahadhari ya dhehebu unalotaka kumwabudia Mungu, kwasababu ukweli ni kwamba madhehebu mengine hayana ubora wa kumfanya mtu awe mkristo kamili.

Kwamfano dhehebu lisilo, patana na imani katika Kristo Yesu tu, au lisilofundisha utakatifu, au lisilo amini juu ya vipawa vya Roho Mtakatifu, au linalochanganya ibada ya Mungu na sanamu, bali linasisitiza mambo ya mwilini tu, hilo halikujengi, bali linakupoteza.

Lifananishe  kwanza na biblia yako, huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, kisha ndio ufanye maamuzi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE NI YESU YUPI UNAYE? WA KIDINI AU WA UFUNUO!

Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?

Print this post

Ipi tofauti ya Falme, Mamlaka na Wakuu wa giza (Waefeso 6:12)

Jibu: Turejee..

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya FALME na MAMLAKA, juu ya WAKUU WA GIZA HILI, juu ya MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”.

Hapa kuna vitu vinne, vilivyogawanyika katika sehemu mbili.. Kundi la kwanza ni “FALME na MAMLAKA” na kundi la pili ni “WAKUU WA GIZA na JESHI LA MAPEPO” jumla mambo manne (4)

Sasa hebu tuanze na kundi la kwanza la FALME na MAMLAKA.

Mwandishi (ambaye ni Paulo, Mtume wa Bwana YESU) alitumia mfumo wa Tawala za dunia, kutoa picha ya tawala za ufalme wa giza.

Katika Dunia tunajua kunakuwa na Falme za wanadamu… Kwamfano kuna Falme za kiafrika, falme za kiarabu, Falme za kiasia n.k,

Sasa kwa vizazi vyetu nyakati hizi mfano wa Falme ni hizi SERIKALI tulizonazo (ambapo kila nchi inayo serikali yake), lakini zamani za kale Falme zilibaki kuitwa falme..Kwamfano kwenye Biblia utaona kulikuwa na Ufalme wa Umedi na Uajemi, Ufalme wa Babeli, Ufalme wa Uyunani, Ufalme wa Rumi n.k.. Hizi zote zilikuwa ni falme na ziliongozwa na Wafalme.. kwahiyo katika ulimwengu kulikuwepo na Falme Nyingi, zenye wafalme wengi, lakini dunia ni moja.

Tusogee mbele zaidi..

Chini ya kila Falme (au serikali) kunakuwa na Mamlaka, kwamfano katika Serikali ya nchi ya Tanzania, kuna Mamlaka mbalimbali, kuna Mamlaka ya mapato (TRA), Mamlaka ya Maji safi na maji taka, Mamlaka ya mawasiliano, Mamlala ya Hali ya hewa, Mamlaka ya Elimu, Mamlaka ya bandari n.k, hivi vyote ni viungo vya Serikali kwaajili ya kuwahudumu walio chini ya Serikali/Ufalme.

Kwahiyo tunaweza kurahisisha kwa kusema mfano huu, “Vyanzo vya maji vyote vilivyopo katika UFALME wa Tanzania vipo chini ya MAMLAKA ya maji ya maji ya nchi hiyo”… au Ukusanyaji wa kodi za wananchi katika Ufalme/serikali ya Tanzania upo chini ya MAMLAKA ya Ukusanyaji mapato (TRA)….Au jukumu la Ulinzi wa raia na mali zao la Ufalme wa Tanzania lipo chini ya Mamlaka ya ulinzi na usalama kupitia chombo chake maalumu kiitwacho Polisi….Umeona huo muunganiko wa Ufalme na Mamlaka?.

Na kawaida kila Mamlaka inayo Wakuu wake na jeshi.. Ndio hapo utasikia “Mkuu wa mamlaka ya mapato” au Mkuu wa mamlaka ya mawasiliano,  na jeshi zima la mamlaka hiyo ni wafanya kazi wote waliopo chini ya mamlaka hiyo..

Na katika ULIMWENGU wa giza ni hivyo hivyo, kuna FALME na pia kuna MAMLAKA mbalimbali… Zipo mamlaka za uuaji na utekaji (mfano wa hizo ni zile zilizoruhusiwa kumkamata Bwana YESU (Soma Luka 22:53),

zipo mamlaka za uharibifu wa ndoa, zipo mamlaka za uharibifu wa huduma, zipo mamlaka za uharibifu wa familia, kazi n.k n.k,

Na kila mamlaka ya giza inayo Mkuu wake/Kiongozi ambaye ni Pepo (hao Ndio wanaoitwa wakuu wa giza)..  Hapa ndipo tunapofika katika kundi la Pili la WAKUU WA GIZA na MAJESHI YA MAPEPO.

Sasa kama kuna kiongozi au mkuu, ni wazi kuwa kuna Jeshi chini yake, (hakuna kiongozi/mkuu asiye  na jeshi la watu chini yake la kuliongoza)

hivyo mapepo yote yaliyosalia yanayofanya kazi chini ya Wakuu wa giza ndio wanatengeneza kundi la majeshi ya mapepo wabaya.

Kwahiyo Biblia inaposema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama bali juu ya FALME NA MAMLAKA NA WAKUU WA GIZA NA MAJESHI YA PEPO WABAYA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, imemaanisha kuwa tunapambana na wakuu wa giza (Wakuu wa mapepo) na majeshi yao ambayo yanatumia Mamlaka na Ufalme wa giza kupambana nasi.

Kwahiyo ufalme wa giza, imesimama katika ngazi zake, kuonyesha kuwa vita vyetu si virahisi kama tunavyovichukulia, kupambana na falme si kazi ndogo! Inahitaji msuli wa kutosha wa kiroho, maana yake ni lazima mtu uwe umesimama kwelikweli, umezama kweli kweli kwenye ufalme wenye nguvu kuliko huo wa giza.

Na hakuna ufalme mwingine wenye nguvu kuuzidi ufalme wa giza, zaidi ya UFALME WA MBINGUNI, ambao Mkuu wa Ufalme huo ni YESU KRISTO (Mwamba Mgumu). Huyo ndiye mwenye nguvu za kuuvunja nguvu zote za falme za giza, na hana namba mbili yake!..

Je unaye YESU moyoni na maishani?.. Kama hujaokoka fahamu kuwa upo chini ya ufalme wa giza na mamlaka za giza hata kama ni tajiri, au una afya au una mafanikio mengine yote, bado upo chini ya utawala wa giza, wanaweza kukufanya chochote kwa wakati wowote, na wanaweza kukutumia vyovyote watakavyo, Mgeukie YESU leo na uhame kutoka katika huo ufalme wa giza.

Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;

14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;

15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.

16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.

17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.

18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote”.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je mkristo anaweza akawa na mapepo?

Je! tunaweza kuwaamuru Malaika kama tunavyoyaamuru mapepo?

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe. Akawapa ruhusa.

Print this post

Fahamu maana ya Warumi 7:25 je tunatumikia sheria ya dhambi?

SWALI: Naomba kufahamu Warumi 7:25 ina maana gani?

Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.

JIBU: Katika sura yote ya saba, mtume Paulo, anaeleza kwa kina mapambano yaliyo ndani ya mwamini.  Kwamba nia yake kutoka ndani ni kuitii sheria ya Mungu, lakini mwili wake kwa nje ni kikwazo kikubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kabisa kutimiza maadhimio yake.

Warumi 7:19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu

Na ni kweli huo ndio uhalisia wa kila mtu. Na ndio maana mwishoni mwa sura hiyo anahitimisha kwa kueleza hali hiyo, Lakini katika vifungu hivyo, wengi wanatafsiri vibaya wakidhani  Paulo anatetea udhaifu wa mwili hapana.. Kinyume chake alianza kwanza kueleza uhalisia wa kibinadamu, ili atoe suluhisho halisi la namna ya kushinda, ambalo ndio tunalisoma katika sura inayofuata ya nane (8)

Ambapo sasa kwenye sura ya nane(8) inayofuata, anaeleza namna ambayo Kristo anatusaidia kuishinda hiyo hali, kwa sheria nyingine  mpya ya Roho ambayo anaiweka ndani yetu.

Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti. Maana yake ni kuwa, Roho Mtakatifu, anatuweka huru katika huo utumwa wa mwili unaotupelekesha.

Inahitaji tu kutii, kwa kumfuata Roho Mtakatifu, kisha yeye mwenyewe atatupa nguvu ya kushinda mambo yote ya mwilini. Lakini sio kwa kutegemea  nguvu zetu tu wenyewe.

Warumi 8: 5 Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.

7 Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii. 8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.

9 Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.

10 Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.

Hivyo ukiishi kwa kumtii Roho Mtakatifu, basi huwezi tumikishwa tena na  mwili,

Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.

Hitimisho:

Warumi 7:25, Paulo analenga hasaa sababu ya sisi kushindwa kutimiza sheria ya Mungu, Ni kwasababu ipo sheria nyingine (ya dhambi iliyojificha ndani yetu) ambayo ni ngumu kutoka kwa namna ya kibinadamu, hivyo anataka hilo tulijue ili tufahamu kuwa kwa nguvu zetu wenyewe hatuwezi kuishinda, Lakini kwa Yesu Kristo atupaye Roho wake ndani yetu, tukienenda kwa kumtii huyo, basi sheria hiyo ya dhambi tutaishinda kabisa kabisa.

Ni wito wa kila mwamini kujifunza kutembea katika Roho.

Je! Unafahamu namna ya kutembea katika Roho kama sio. Basi tutumie ujumbe kwa namba uzionazo chini ya somo hili tukutumie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

Print this post

Kwanini Nyaraka za Paulo kwa makanisa tuzifanye kuwa nyaraka zetu leo?

Swali: Nyaraka za Paulo tunaona ni barua kwenda kwa makanisa yaliyokuwepo wakati huo, kama Korintho, Efeso, Kolosai na Galatia na nyingine kwenda kwa watu waliokuwepo wakati huo, kama Timotheo, Tito na Filemoni sasa iweje nyaraka hizo zituhusu na sisi na hata ziwe ni neno la MUNGU?, na kuzitumia hizo kufundishia sasa?


Jibu: Swali zuri lakini ili tuweze kupata majibu yaliyojitosheleza, hetu tutafakari mifano ya kawaida iliyopo,

Alikuwepo mwanasayansi mmoja  wa kijerumani maarufu ambaye sasa ni marehemu ajulikanaye kama Albert Einstein (Mgunduzi wa kanuni ya kutengeneza bomu la Nyuklia), huyu wakati wa vita vya pili vya dunia alimwandikia waraka Raisi wa Marekani aitwaye Roosevelt, kwamba atengeneze silaha ya Nyuklia, kabla Adolf Hitler hajaitengeneza, na katika waraka huo alimpa pia hiyo fomula/kanuni ya kutengeneza silaha hiyo. (Waraka huo uliandikwa mwaka Agosti 2,1939).

Na matokeo ya waraka huo ni Raisi Roosevelt kuunda bomu la Nyuklia, na kwenda kulifanyia majaribio katika miji miwili ya nchi ya Japani (Mji wa Heroshima na Nagasaki).

Lakini ajabu ni kwamba baada ya wakati huo, sehemu za waraka huo zilizobeba kanuni za utengenezaji wa nyuklia zilivuja na kufikia mataifa mengine, na mataifa hayo kama Urusi hayakulaza damu bali nayo pia yakaunda mabomu ya nyuklia yenye kanuni ile ile, zilizokuwepo ndani ya ule waraka.

Na cha ajabu zaidi ni kwamba miaka mingine mingi mbele mataifa mengine kama Ufaransa, Pakistani,India, na mengine machache yakaichukua kanuni hiyo hiyo ya kuunda bomu la Nyuklia na kutengeneza mabomu yao,

Na cha kushangaza zaidi na zaidi ni kwamba mataifa mengine mengi leo yanafanya jitihada kuunda mabomu yao kupita kanuni ile ile ya mwanasayansi huyo Albert Einstein aliyetokea miaka mingi huko nyuma kupitia waraka wake aliomwandikia Raisi wa Marekani.

Sasa swali la kujiuliza, ni hili; kulikuwa kuna haja gani ya Mataifa kama Urusi, Ufaransa, na mengineyo kufuatilia waraka Einstein aliomwandikia Raisi Roosevelt na hata kuzitumia kanuni/fomula alizoziandika ndani yake kutengeneza mabomu yao??..

Tulitegemea waraka wa Einstein kwenda kwa Raisi huyo, uishe matumizi baada ya kusomwa na kutumika na Raisi huyo wa Marekani, lakini ajabu ni kwamba mpaka sasa una matokeo katika ulimwengu wetu, ingawa uliandikwa miaka mingi iliyopita.

Kwahiyo Utaona kwamba sababu pekee ya mataifa mpaka leo hii kuitumia kanuni ya mwanasayansi huyo aliyetokea miaka mingi huko nyuma ni kwasababu alichokigundua Albert Einstein ni kitu cha Kweli chenye manufaa na tija si tu kwa wakati wake tu, au Taifa lake tu bali hata kwa mataifa mengine na kwa vizazi vingi vijavyo.

Na ni hivyo hivyo Nyaraka za Mtume Paulo na za Mitume wengine… kwa jicho la nje zitaonekana kama zimeandikwa kwaajili ya makanisa yale ya wakati ule, au kwaajili ya watu wa wakati ule, lakini kwa jicho la rohoni ni ujumbe kwetu zaidi hata ya watu wa wakati ule.

Kwasababu yaliyoandikwa katika nyaraka za Mitume wa kwenye Biblia ni maneno ya kweli yanayoishi katika vizazi vyote, na tena kwa jinsi muda unavyozidi kwenda ndivyo yanavyohitajika zaidi kwasababu yaliyokuwa yanatendeka zamani, sasa hivi yamezidi mara nyingi sana.

Vita vya kiroho walivyokuwa wanapigana watu wa kanisa la Korintho, Galatia, na mengineyo nyakati hizo ndizo tunazopambana sasa, tena wakati huu zimezidi zaidi, kwahiyo tunahitaji fomula na kanuni za wanasayansi wetu wa kiroho (Mitume na manabii wa kwenye Biblia) kutengeneza silaha zetu za kiroho sasa, na kupambana hivi vita mpaka tushinde.

Lakini tukibaki na kusema zile nyaraka zilikuwa ni za wakorintho tu peke yao na wagalatia tu peke yao, na kwamba sisi hazituhusu tutamalizwa vizuri na shetani, ni sawa na Taifa la Urusi liseme ule waraka wa Einstein aliomwandikia Raisi wa Marekani, kuhusu utengenezaji wa Nyuklia uliwahusu Wamarekani peke yao, wangekuwa na akili hiyo, leo wangeisha, au wangetawaliwa!.

Na sisi ni lazima tuiamini Biblia, kuwa ni Neno la MUNGU linaloishi kwa nyakati zote na vizazi vyote, hakuna wakati litaisha matumizi, au litapitwa na wakati, Mafunuo yaliyokuwemo ndani ya Biblia yana nguvu na Uwezo, kwani waliofunuliwa wamefunuliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu na si kwa akili zao.

Mwisho; Je umempokea YESU kwelikweli au kidini?.. kama maisha unayoishi ni ya uvuguvugu bado hunaye YESU, unamhitaji YESU aingie maishani mwako, unahitaji kujikana nafsi na kubeba msalaba na kumfuata YESU, Fanya mageuzi na acha kuishi maisha ya uvuguvugu, kwani tunaishi nyakati za hatari na muda umeenda sana, na parapanda inalia muda wowote, na mambo yote yatapita.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?

Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu,

Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.

Kibiblia, hekima, ni uwezo wa  kupambanua , kuhukumu na kufanya maamuzi yenye matokeo makamilifu ya Ki-Mungu duniani.

Kwamfano, biblia inatuambia kwa hekima Mungu aliziumba mbingu na nchi (Mithali 8:22-31)

Sulemani alimwomba Mungu hekima ya kuchunga na kufanya hukumu kwa watu wake Israeli, na Mungu akampa, Danieli alipewa hekima ya upambanuzi wa ndoto na maono yote ya siri,

Kwa ufupi hekima ya ki-Mungu ni zaidi ya maarifa, elimu, au akili, ni uwezo wa juu sana ambao unazidi upeo wa ki-binadamu.

Lakini inapatikanaje?

Kumbuka Biblia inaitaja hekima pia kuwa ni mtu. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

1Wakorintho 1:24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.

Na kama Ndio hekima mwenyewe..Basi ndani yake matunda yote ya hekima yapo.

Wakolosaia 2:3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.

Hivyo ili mtu kuiona hekima tafsiri yake ni kuwa anapaswa amwone YESU. Na kumwona Yesu ni kumpokea kama Bwana na mwokozi wa maisha yako (Warumi 10:9), pamoja na kumtii kutembea katika njia zake.

Yesu anapatikana wapi?

Katika mahubiri, Mahubiri yanapatikana wapi? Kila mahali, kwenye njia kuu, viwanja, kwenye mikutaniko ya watu, mastendi, masokoni, mitandaoni n.k.

Anapazaje sauti?

Anapaza sauti kupitia watumishi wake mbalimbali Aliowatuma kumuhubiri.

Hivyo, hilo andiko linalosema,

Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.

Unaweza kuelewa sasa analenga injili, inayohubiriwa kila mahali duniani kote. Ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kusema hajawahi kuisikia injili, kwasababu kila mahali inahubiriwa kwa nguvu. Kuonyesha kuwa hekima haijajificha ipo sikuzote, bali ni watu ndio wanaikwepa.

Mtu yeyote anayemwamini Kristo basi tayari amefungua mlango wa ufahamu mkubwa sana unaoweza kufungua mambo yote katika hii dunia.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Kati ya Exegesis na Eisegesis. Ni ipi namna  bora ya kutafsiri maandiko?

JIBU: Haya ni maneno ya kiyunani, yanayoeleza namna tofauti ya kutafsiri maandishi.

1) Eksejesisi (exegesis).

Ni namna ya kutafsiri maandiko kwa kuzingatia mtazamo wa awali uliokusudiwa na mwandishi, kwa kuzingatia muktadha, hali ya kihistoria, matamshi na matumizi ya lugha.

2) Eisojesisi ( Eisegesis).

Ni namna ya kutafsiri Maandiko kwa namna ya mtazamo wa mtu mwenyewe, kwa kulileta andiko liendane Na wazo lake binafsi,. Namna hii haitilii maanani sana kusudio La kwanza la mwandishi, bali lile aliaminilio kuwa ni sahihi Kwake. (Mfano wa hii ni ile namna ya kusema nimefunuliwa)

Kwa ufupi eksejesisi ni Kuliruhusu andiko lijitafsiri lenyewe huku Eisojesisi ni lilete andiko litafsiri ninachokitaka au kiamini.

Je ipi inakubaliwa na Mungu?

Ijapokuwa Eksejesisi,(tafsiri ya awali) ndio msingi hasaa wa kusimamia katika kuyaelewa maandiko lakini eisojesisi pia Mungu huitumia kusema na sisi katika nyakati Fulani.

La kuzingatia ni kwamba kabla hujaipokea namna nyingine.. Ifahamu kwanza asili ya kwanza ya andiko hilo, ilikuwa ni nini.

Kwamfano Bwana Yesu aliposema.

Mathayo 11:28

[28]Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

Katika Eksejesisi hiyo mizigo inayozungumziwa hapo na Bwana Yesu sio umaskini, Mateso, madeni, familia, majukumu,n.k. hapana, bali mizigo ya dhambi. Ndicho Bwana Yesu alichomaanisha na kusudi la kwanza lililomfanya kuja duniani lilikuwa ni hilo kumkomboa mwanadamu kutoka katika dhambi zake.

Lakini pia Bwana anaweza tumia andiko hilo kulenga na mizigo mingine, kwasababu ni ukweli usiopingika alisema pia tumtwike yeye fadhaa zetu zote.

1 Petro 5:7

[7]huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

Hivyo namna zote Mungu anaweza kutumia kutujenga. Kwasababu Neno lake ni pana na njia zake hazichunguziki, katika kuwajenga, kuwafariji na kuwaponya watu. Isipokuwa hatari inakuja mtu kukosa kulipambanua vizuri Neno na matokeo yake kutegemea zaidi mtazamo (alioupokea), na kuacha biblia yenyewe kujieleza.

Hii ndio Imekuwa chumbuko la mafundisho mengi ya uongo, na potofu, kwamfano mtu atasema chapa ya mnyama (ufunuo 13) Ni ugonjwa wa Korona (covid-19). Wakati si kweli.

Au mtu atasema Yesu alitengeneza matope kwa mate yake akampaka mtu machoni akaona,(Yohana 9:6-7) hivyo na sisi kufanya kwa namna hiyo si kosa. Kumbe lile lilikuwa ni “ingilio la Mungu” la wakati husika lakini sio agizo la kudumu. Kwani agizo la daima ni kutumia jina la Yesu kutenda/kuamuru jambo lolote.(Kol 3:17)

Hivyo ili kubaki katika upande sahihi ni vema ukajifunza eksejesisi, (kufahamu muktadha wa kimaandiko), na ndio pale esiojesisi inapokuja Basi unaeweza Kuligawanya vema Neno la Mungu. Bila kuleta uharibifu/ madhara yoyote, katika imani au kwa kile unachowafundisha wengine.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

Je! Petro na wenzie walitambuaje kuwa wale walikuwa ni Musa na Eliya?

Swali: Katika kitabu cha Mathayo 17:4 Mtume Petro na wenzie waliwezaje kufahamu kuwa wale ni Musa na Eliya?


Jibu: Turejee habari hiyo kuanzia ule mstari wa kwanza..

Mathayo 17:1 “Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;

2 akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.

3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.

4 Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya”.

Biblia haijaeleza kama Musa na Eliya walijitambulisha katika maono yale, ikiwa na maana kuwa kuna njia nyingine iliyowafanya Petro na wenzie kujua kuwa wale ni manabii Musa na Eliya na si wengine.

Sasa njia Pekee iliyomfanya Petro na wenzie kufahamu kuwa wale walikuwa ni Musa na Eliya na si wengine, ni UFUNUO WA ROHO MTAKATIFU.

Kama vile ufunuo wa Roho Mtakatifu ulivyomjia Petro kumhusu YESU.

Mathayo 16.15 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”.

Umeona hapo?, aliyemwambia Petro kuwa YESU ni KRISTO tena ni MWANA WA MUNGU aliye juu sio YESU mwenyewe!, bali ni ufunuo wa alioupokea kutoka kwa Baba.

Na hiyo sio ajabu kwani walikuwa wameenda mlimani kuomba.. ni kawaida kwa watumishi wa MUNGU kupokea mafunuo ya mambo yaliyopo, au yajayo wanapokuwa katika maombi, hususani kama hayo ya mlimani.

Kwahiyo Mtume Petro na wenzie walipata ufunuo wa ujio au uwepo wa manabii hao wawili wakiwa katika maombi, utaona jambo kama hilo lilishatokea tena kwa Petro wakati yupo kwa Yule Simoni mtengenezaji wa ngozi wa kule Yafa, wakati ambapo Roho Mtakatifu alimfunulia alipokuwa katika maombi kuwa kuna watu watatu wanamwulizia, hivyo aende nao asiogope!, na kweli ikawa hivyo..

Matendo 10:17 “Hata Petro alipokuwa akiona shaka ndani ya nafsi yake, maana yake ni nini maono hayo aliyoyaona, wale watu waliotumwa na Kornelio, wakiisha kuiulizia nyumba ya Simoni, wakasimama mbele ya mlango,

18 wakaita; wakauliza kwamba Simoni aitwaye Petro anakaa humo.

19 Na Petro alikuwa akiyafikiri yale maono. Roho akamwambia, Wako watu watatu wanakutafuta.

20 Basi ondoka ushuke ufuatane nao, usione tashwishi, kwa maana ni mimi niliyewatuma.

21 Petro akawashukia wale watu, akanena, Mimi ndiye mnayemtafuta. Mmekuja kwa sababu gani?”

Kwa namna hiyo hiyo, huenda Petro na wenzake walipokea ufunuo kuwa wale ni Musa na Eliya, labda walipokea ufunuo huo muda mchache kabla hawajawatokea, au wakati ule ule walipotokea.

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa tuwapo katika uwepo wa MUNGU kama katika maombi, ni rahisi kupokea ufunuo wa Roho Mtakatifu kwani tunakuwa tupo katika roho, na mtu anapokuwa katika roho anayatambua mambo yote ya rohoni pasipo kuambiwa!

Hivyo ni muhimu sana kuwa waombaji, na wasomaji wa Neno la MUNGU, endapo akina Petro wangekuwa si watu wa kusoma maandiko, ni dhahiri kuwa wasingemjua Musa wala Eliya na hiyo ingezuia Roho kuwafunulia watu hao, kwani Roho Mtakatifu anamfunulia mtu kitu ambacho kinahusiana na Neno la MUNGU.

Je na wewe ni mtu wa kudumu uweponi mwa MUNGU? Je KRISTO YESU?..Je unao uhakika kwamba akirudi unaenda naye?

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini Eliya afunge Mbingu miaka mitatu na nusu? (1Wafalme 17:1)

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

Je! Tutatambuana tukifika mbinguni?

Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?

Kwanini Mungu alimchagua Musa, na si mtu mwingine?

Print this post

Yesu aitwaye Yusto alikuwa ni nani? (Wakolosai 4:11).

Swali: Je huyu Yesu anayetwaja katika Wakolosia 4:11 alikuwa ni nani, na je ni kwanini aitwe hilo jina tukufu?


Jibu: Turejee..

Wakolosai 4:11 “Na YESU AITWAYE YUSTO; hao ni watu wa tohara. Tena hao peke yao ni watendaji wa kazi pamoja nami kwa ajili ya ufalme wa Mungu; nao walikuwa faraja kwangu”.

Katika Biblia Kristo mwokozi wetu hakuwa wa kwanza kuitwa jina YESU, bali walikuwepo watu wengine kadhaa kabla yake walioitwa kwa hilo jina, kwani lilikuwa ni jina linalojulikana Israeli yote,

Na tafsiri ya jina YESU ni  (YEHOVA-MWOKOZI), kama vile ilivyokuwepo YEHOVA-YIRE ambayo tafsiri yake ni YEHOVA mpaji n.k

Kwahiyo YESU ni jina lililokuwepo hapo kabla, kama tu Simeoni aliyeitwa Petro, hakuwa wa kwanza kuitwa Simeoni, au Yuda aliyemsaliti Bwana YESU hakuwa wa kwanza kuitwa Yuda, kwani hata mtoto wa Yakobo,  aliitwa Yuda, na ndio ukoo Bwana YESU aliotokea.

Sasa ni kitu gani kilichomtofuatisha YESU mwokozi wetu na maYesu wengine?.. si kitu kingine bali ni kiunganishi cha mwisho cha jina hilo,.. Aliyetufia anajulikana kama YESU KRISTO,  maana yake YESU MTIWA MAFUTA na MUNGU…

Wengine wanaitwa “Yesu wa Yusto”, wengine “Bar-YESU” (soma Matendo 13:6) lakini ni mmoja tu anaitwa “YESU KRISTO”.. Huyu kwa jina lake hili ndio tunapata ondoleo la dhambi na wokovu (Matendo 4:12).

Na kwa jina la YESU KRISTO, Tunafunguliwa na kuponywa magonjwa yetu, na ziadi sana ndio kwa jina hili tunapaswa tuhubiri na kuhubiriwa ili tupate ukombozi.

Lakini katika hizi siku za mwisho shetani amewanyanyua maYesu wengi wa uongo, ambao na si Yule wa uzima.

2Wakorintho 11:3 “Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.

4 MAANA YEYE AJAYE AKIHUBIRI YESU MWINGINE AMBAYE SISI HATUKUMHUBIRI, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!”

Yesu mwingine, (asiye KRISTO) anahubiriwa sasa na manabii na watumishi wa uongo, ambaye yeye hahitaji utakatifu.. ukiona unahubiriwa kwa jina la YESU lakini injili hiyo haikupeleki kuwa msafi mwilini na rohoni, badala yake unazidi kuwa wa kidunia, fikiri mara mbili ni Yesu gani uliyempokea, kwahiyo hatuna budi kujipima.

Lakini tukirudi kwenye swali!, Je huyu Yesu aitwaye Yusto alikuwa ni nani?..

Huyu Yesu aitwaye Yusto, alikuwa ni mmoja wa wafuasi wa Bwana wetu YESU KRISTO, ambaye alishirikiana na akina Paulo (watumishi wa MUNGU) kuhubiri injili, na alikuwa ni Myahudi (ndio maana Biblia inasema hapo alikuwa ni mtu wa tohara, maana yake aliyetahiriwa).

Maana ya jina Yusto ni “mwenye haki”.. na aliitwa “Yesu aitwaye Yusto”, kumtofautisha na YESU KRISTO. Huyu hakusimama kutaka aabudiwe, bali kinyume chake alikuwa anamhubiri YESU KRISTO.

Je umempokea Bwana YESU KRISTO?. Kama bado unasubiri nini?

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE BWANA YESU ALIMTOKEA YUDA BAADA YA KUFUFUKA KWAKE?.

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

YESU MNAZARETI,  ANWANI YA MSALABA.

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Print this post

Je YESU KRISTO alikuwa na wadogo zake?

Swali: Je YESU alikuwa na dada na kaka (ndugu wa kike na kiume), kama watu wengine?


Jibu: Ndio! Bwana wetu YESU KRISTO alikuwa na ndugu wengine wa kike na kiume, waliozaliwa na Mariamu mamaye!, maandiko yanathibitisha hilo katika Mathayo 13:55-56 na Marko 6:3.

Mathayo 13:54 “Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii?

55 Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? NA NDUGUZE SI YAKOBO, NA YUSUFU, NA SIMONI, NA YUDA?

56 NA MAUMBU YAKE WOTE HAWAPO HAPA PETU? Basi huyu amepata wapi haya yote?”

Kulikuwa na sababu ya kuanza na “Mwana wa seremala (Yusufu) na  kisha Mariamu mamaye na kumaliza na akina Yakobo, Yusufu, Simeoni na Yuda na maumbu (yaani wadada)”.. Ikimaanisha kuwa iliyokuwa inatajwa hapo ni familia, na si ukoo.

Ikimaanisha kuwa Marimu baada ya kumzaa Bwana YESU hakuendelea kuwa Bikira, bali alizaa watoto wengine pamoja na Yusufu mumewe, na watoto hao walikuwa wakike na kiume kama walivyotajwa hapo juu.

Ipo imani kuwa Mariamu hakuendelea kuzaa watoto wengine baada ya kumzaa Bwana YESU na kwamba watoto hao waliotajwa hawakuwa watoto waliozaliwa na Mariamu bali walikuwa ni ndugu wengine kama watoto wa mjomba, au baba mdogo ambao walikuwa karibu sana na Mariamu na Yusufu..

Hoja hii ni dhaifu na haina ukweli, kwani kusingekuwa na sababu ya MUNGU kuruhusu Mariamu achumbiwe na YUSUFU kama hawakuwa na mpango wowote wa kukutana na kuzaa watoto huko mbeleni,.. Malaika angeweza kumtokea Mariamu hata kabla hajachumbiwa, na hilo lingeweza labda kutufanya tuamini kuwa Mariamu aliendelea kuwa bikira mpaka anakufa!.

Lakini kitendo cha mpango wa MUNGU kuingilia kati wakati ambao tayari Mariamu kashachumbiwa, na kuonyesha kuwa hao tayari wamekusudiwa kuwa mume na mke na kuzaa watoto, na hata hivyo kipindi ambacho Yusufu amekusudia kumwacha Mariamu kwasababu ya ujauzito wake, bado kulikuwa na nafasi ya Malaika kumruhusu Yusufu amwache Mariamu, na kumruhusu akaoe mwanamke mwingine, ili Marimu abaki bikira maisha yake yote.

Lakini tunaona Yule Malaika hakumruhusu Yusufu amwache mkewe, ikifunua kuwa Yule ataendelea kuwa mke na ataendelea kutumika kama mwanamke mara baada ya kumzaa Bwana YESU.

Kwahiyo Bwana YESU alikuwa na ndugu wengine na Mariamu hakupaa, wala hakufa bikira, bali alikuwa na watoto wengine, na kati ya hao (yaani Yuda na Yakobo) ndio walioandika vitabu vya Yuda na Yakobo vya agano jipya katika Biblia.

Lakini pamoja na kuwa Bwana YESU alikuwa na ndugu wengine katika mwili, bado alisema kuwa ndugu zake hasa ni wale wayafanyayo mapenzi ya Baba yake.

Luka 8:19 “Wakamwendea mama yake na ndugu zake, wasiweze kumkaribia kwa sababu ya mkutano.

20 Akaletewa habari akiambiwa, Mama yako na ndugu zako wamesimama nje wakitaka kuonana nawe. 21 Akawajibu akasema, Mama yangu na ndugu zangu ndio hao walisikiao neno la Mungu na kulifanya”.

Je umempokea YESU?, Je Umefanyika kuwa ndugu yake Bwana kwa kulishika Neno lake na kulifanya?

YESU ANARUDI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni halali kubatiza watoto wadogo?

HUYU SI YULE SEREMALA, MWANA WA MARIAMU?

Je! Tutatambuana tukifika mbinguni?

JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?

Ipi tofauti kati ya Sheria na kanuni kibiblia.

Print this post