Categories
Kansa Uncategorised

njoni kwangu

ninyi nyote msumbukao

Categories
Kansa

Ameponywa kansa iliyokuwa katika hatua ya Nne.



Hakuna mtu angependa kupokea aina ya taarifa niliyoipokea mimi kwenye simu kutoka kwa daktari wangu.

Daktari Alisema Shirley umetafunwa na kansa sana sio tu kwenye matiti yako bali mpaka kwenye mifupa yako, na viungo vyako vya ndani,na mpaka kwenye tezi zako.

Kwa kweli nililia sana nikajiuliza, hii inawezakanikaje kwani nimekuwa nikimtumikia Mungu maisha yangu yote, nashindwa kuelewa ni kwanini?

Kwa kitambo nimekuwa nikisikia maumivu ya kifua, na kujihisi mdhaifu na vibaya, lakini huwa ni mara chache sana ninakwenda kwa daktari lakini baada ya kuona maumivu yanadumu  kwa muda mrefu hayaishi ndipo nilipoamua kwenda kuangalia afya yangu. Kilichofuata nilichukuliwa vipimo kadha wa kadha, na baadaye ndipo niligundulika kuwa ni Kansa hatua ya nne (stage 4). Hatua hii haitibiki na hivyo niliambiwa nina siku 90 tu za kuishi

Maswali mengi yalianza kupita ndani ya kichwa cha Mume wangu, akiwaambia watu, Itakuwaje kama Shirley akifa leo, watoto wetu watakuwa katika hali gani, mimi nitaenda wapi? Mimi nitafanya nini? Haiwezekani nahitaji maandiko kwasababu hapo ndipo pekee ninaweza kupata faraja..Nilimfuata mke wangu na kumuuliza je! Ni repoti ya nani tunapaswa kuiamini?,Daktari au Mungu? Neno la Mungu linatuambia tutaishi hatutakufa na pia linatuambia hakuna silaha itakayorushwa kinyume chetu itakayofanikiwa, na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

Lakini siku iliyofuata maumivu yalizidi kuongezeka.

Mpaka nikakiri kutembea kwake kumekuwa kwa shida kutokana na mauvivu yaliyo sehemu ya juu ya paja langu, na uvimbe ambao upo katika ziwa langu la kuume, ulio mkubwa kiasi cha nusu ngumi, kwakweli mawazo mengi yalikuwa yanapita kichwani mwangu yakinishawishi ni heri nife kuliko kuishi.

Lakini mimi na mume wangu tuliikataa roho ya hofu, badala yake tulijifunza kuishi kwa imani na bila kutamka neno hata moja la mashaka.

Nilikuwa nikisema kwa ujasiri, sijawahi kuona mahali popote kwenye maandiko,kama kuna mtu alishamfuata Yesu Kristo ili amponywe na akaondoka bila kuponywa, nilianza kufahamu sasa Imani sio tu kuamini kuwa Mungu anaweza kukuponya lakini pia ni kuamini kuwa Mungu atakuponya.

Hivyo niliendelea kutafuta ongozo wa Mungu, nakumbuka siku moja usiku niliamka nikamwona Yesu kwenye pembe ya mwisho wa kitanda changu, na nilipomwangalia hivi niliona, huruma yake, niliona upendo, niliona tumaini,na saa hiyo hiyo Nilianza kuhisi jasho linatiririka sehemu ya nyuma ya goti langu la kulia, ilikuwa sio hali ya kawaida ndipo nikamuuliza Bwana ulikuwa unataka nitoke jasho?

Siku tatu baadaye nilipata jibu pale nilipokwenda kumwona daktari mpya wa masuala ya kansa,Yule daktari akaniambia nina neno moja la kukwambia kabla huaondoka “kwamba unahitaji kutoka jasho”

Alianza kuingia katika tiba ya kusababisha jasho litoke, nilianza kutumia mabafu ya moto na kufanya mazoezi mengi, pamoja na kula  vyakula vya asili, huku marafiki zangu na familia yangu wakifunga na kuomba kwa ajili ya uponyaji wa kiungu, na mume wangu pia akiniombea na kuniwekewa kila mara.

Mume wangu mara kwa mara alikuwa akisema maneno haya  “mtaweka mkono juu ya wagonjwa nao watapata afya, akiamrisha ugonjwa uondoke kwa jina la YESU”

Na wiki tatu mbeleni nilipata ndoto “nilikuwa nimesimama karibu na dirisha la kioo, na ghafla akaona mbele yake semi-trailer kubwa nimejaa mizigo mingi ikija kuelekea upande nilipokuwepo,sikuwa na la kufanya zaidi ya kulia YESU! YESU! YESU!..muda kidogo Lilisimama mbele yangu na kupiga tu kile kioo kilichokuwa mbele yangu..Ndipo nikasikia Roho akizungumza ndani yangu na kusema kuwa lile gari nililolizuia ndio kansa iliyokuwa mwilini mwangu.

Kwa miezi mengine miwili mbeleni niliendelea na matibabu, huku nikiamini Mungu ameshaniponya, Na Kwa jinsi siku zilivyokuwa zinaendelea kwenda ndivyo9 habari njema zilikuwa zinazika zile habari mbaya na siku  ya mwisho nilipokwenda kwa ajili ya vipimo vya siku 90, hatimaye nilipata majibu ya maombi niliyokuwa ninayasubiria kwa muda mrefu.

Daktari aliniambia vipimo vinaonyesha hakuna uvimbe wowote kwenye titi lako na vile vile hakuna dalili yoyote ya kansa katika mwili wako. Kwa kweli ninaamini kuwa kuwa mtu aliyekatika hatua ya NNE ya kansa, halafu kansa imeondoka, huo ni muujiza.

Nilikuwa ninaruka ruka kwa furaha nikimshukuru Mungu sana, kuwa yeye ndiye mrejezi wangu, huku nikishangilia kwa furaha sana

Mume wangu anasema alijisikia uhuru mkubwa sana ndani ya nafsi yake, jinsi Mungu alivyompa nafasi tena ya kuendelea kuwa na mke wake mpaka mwisho wa maisha yao ya hapa duniani.

Tokea huo wakati Agosti 2012, mpaka sasa Shirley hajawahi kuwa na dalili yoyote ya kansa.

Shirley anasema: Nimeponywa leo kwasababu nimeliamini na kulipokea Neno lake, na nililifanya kuwa sehemu ya maisha yangu…Alimalizia na kusema:

Yeye hatazami uso wa mwanadamu, kama alinifanyia na mimi atakufanyia na wewe.

Haleluya!, Hata na wewe msomaji, unaweza ukawa na tatizo pengine kubwa kushinda la Shirley, usikate tamaa Huyu Yesu anayezungumzwa na mabilioni ya watu duniani, yupo kweli kukuhudumia na wewe. Mwamini tu, nawe atakutendea muujiza wako.

×

Powered by WhatsApp Chat

× Karibu tukuhudumie..