MWAMBA WENYE IMARA

by Admin | 17 July 2020 08:46 am07

Mwamba wenye Imara, kwako nitajifichaa…” Ni wimbo wa kenye kitabu cha Tenzi, ambao unafahamika sana…lakini historia ya wimbo huu ni haujulikani na wengi.

Wimbo huu uliandikwa na Mhubiri mmoja wa kanisa la kiprotestant aliyejulikana kwa jina la “Augustus Montague Toplady” , mwenye asili ya nchi ya Uingereza. Mhubiri huyu siku moja alipokuwa anasafiri katika ziara zake za kuhubiri katika kijiji kimoja huko kaskazini mwa Uingereza mwaka huo wa 1763 kilichoitwa “Blagdom”..alipokuwa safarini alikumbana na “Dhoruba kubwa sana ya kuogopesha”.. na hakuwa na mahali pa kujificha…lakini karibu na eneo alilokuwepo palikuwa na MWAMBA MKUBWA, ambao ulikuwa na mwanya mdogo wa kujificha. Na ndipo alipokimbilia chini ya mwamba ule kwenye ule upenyo mdogo na kujificha, mpaka dhoruba ile kali ilipopita..

Sasa akiwa katikati ya upenyo wa mwamba ule, huku anatetemeka kwa baridi, ndipo kichwani ukamjia mistari ya huu wimbo…”mwamba wenye imara…kwako nitajificha..”  Akilinganisha tukio hilo la dhoruba ya mvua kubwa na dhoruba ya kimaisha, ikamsukuma kuimba Yesu ni mwamba wake wa kujifichia..mpaka leo wimbo huo umekuwa Baraka kwa zaidi ya miaka 200.

Huo ni ujumbe wa Mungu kutuonyesha kuwa palipo na dhoruba basi kuna Mwamba…Hivyo hatupaswi kuogopa tunapopitia dhoruba, tunapoona juu kumefunga, maisha yamekwama, vita ni vingi, matatizo ni mengi…tunapofikia mahali tunaona kesho hatapafika, tunapoona mwaka huu hautaisha…Huo ndio wakati wa kumtazama Bwana aliye mwamba wetu..kwake huyo tutajificha…

Mwamba huu hautoi tu hifadhi wakati wa  dhoruba, bali pia unatoa maji baridi  na uvuli wakati wa jua kali..na huo sio mwingine zaidi ya YESU KRISTO, kama mhubiri huyu Augustus alivyoimba..

1Wakorintho 10: 4 “wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo”.

Je upo chini ya mwamba leo?..kama haupo..je wakati wa dhoruba utajificha wapi?…wakati wa tufani utakimbilia wapi?..je wakati wa jua kali utapata wapi uvuli? Na maji ya kunywa?…hivyo mkabidhi Kristo leo maisha yako naye atakuwa mwamba kwako.

Lakini kama umeshamkabidhi tayari muda mrefu..basi usitishwe na dhoruba zinazokuja mbele yako, wala usitishwe na vipindi vya hari ya jua kali na ukame…upitiapo hali kama hizo..mwamba upo karibu nawe..Ukumbuke msalaba, na mkumbuke mwokozi, mshukuru, na jinyenyekeze chini yake…na utaona maajabu baada ya kipindi kifupi… Hivyo imba wimbo huu uliovuviwa nguvu za Roho Mtakatifu kukufariji na kukutia moyo..

Mwamba wenye imara, kwako nitajificha
Maji hayo na damu, yaliyotoka humo
Hunisafi na dhambi, hunifanya Mshindi.

Kwa kazi zote pia, sitimizi sheria
Nijapofanya bidii, nikilia na kudhii
Hayaishi makosa, ni we wa kuokoa

Sina cha mkononi, naja msalabani
Nili tupu nivike, ni mnyonge nishike
Nili mchafu naja, Nioshe mi sijafa.

Nikungojapo chini, nakwenda kaburini
Nipaapo mbinguni, nakukuona enzini
Roho yangu na iwe, rahani mwako wewe

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

TENZI ZA ROHONI

WAKATI WA JUA KALI NDIO WAKATI WA KAZI:

USIHUZUNIKE.

WAKATI WA BWANA KUKUVUSHA, NI LAZIMA ARUHUSU JESHI LA ADUI KUNYANYUKA.

USIFIKIRI FIKIRI.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/07/17/mwamba-wenye-imara/