Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;

by Admin | 22 November 2021 08:46 pm11

SWALI: Nini maana ya huu mstari..

Mithali 15:27

[27]Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;

Bali achukiaye zawadi ataishi.


JIBU: Mstari huo ni mgumu kueleweka kidogo kwasababu kiswahili kilichotumika hapo ni kile cha zamani..

Ukiangalia tafsiri nyingine..mstari huo unamaana hii.. Atamaniye kupata vingi kwa njia isiyohalali huifadhaisha nyumba yake mwenyewe bali achukiaye rushwa ataishi.

Jambo ambalo ni kweli..kwamfano Mtu anayejiingiza katika biashara ya madawa ya kulevya kwa tamaa tu ya kupata fedha nyingi..hajui kuwa mwisho wake ni kujibomoa yeye mwenyewe na pamoja nyumba yake yote.

Habakuki 2:9

[9]Ole wake yeye aipatiaye nyumba yake mapato mabaya, ili apate kukiweka kioto chake juu, apate kujiepusha na mkono wa uovu!

Mwingine utakuta anatoa rushwa ili bidhaa zake zisilipishwe kodi..lakini hajui mwisho wake utakuwa mbaya siku moja.

Lakini kinyume chake biblia inasema atakayeyakwepa hayo yote ataishi..

Sikuzote tamaa ya  za haraka haraka mwisho wake huwa ni mitegoni..

Mhubiri 4:6

[6]Heri konzi moja pamoja na utulivu,

Kuliko konzi mbili pamoja na taabu;

na kujilisha upepo.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kama utapenda uwe unafikiwa na masomo ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP basi bofya hapa ujiunge moja kwa moja  >>>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Maana ya huu mstari ni ipi? Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;bali nguvu za ngombe zaleta faida nyingi’.

UMEDI NA UAJEMI ZILITAWALAJE?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

HUANGUA MAYAI YA FIRA, NA KUSUKA WAVU WA BUIBUI;

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/11/22/atamaniye-faida-huifadhaisha-nyumba-yake-mwenyewe-bali-achukiaye-zawadi-ataishi/