Amali ni nini?(Mhubiri 4:4).

by Admin | 13 January 2025 08:46 am01

Amali ni nini (Mhubiri 4:4)

Jibu: Turejee…

Mhubiri 4:4 “Tena nikafikiri amali zote, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.

Amali ni “kazi ya tabu/kuchosha”.. Mtu anayefanya kazi yenye kuchosha mwili na akili, kazi yake hiyo inaitwa “Amali”.

Hivyo mstari huo wa Mhubiri 4:4 unaweza kueleka hivi….

Mhubiri 4:4 “Tena nikafikiri KAZI ZOTE ZA TABU, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.

Maana yake kazi nyingi za kuchosha zinatokana zinahusisha mambo maovu ikiwemo Tamaa, Uchungu, Wivu, uchoyo, hasira na visasi.

(Ingawa pia si zote, yaani si wote wenye kufanya kazi za taabu/kuchosha wapo juu ya misingi hiyo, wapo wengine nia zao ni njema kabisa wana amani na Bwana anawatunza na kuwaonekania.. lakini wengi wao msingi wao ni uovu).

Mhubiri 4:8 “Kuna mtu aliye peke yake, wala hana wa pili wake; naam, hana mwana wala ndugu; hata hivyo amali yake haina mwisho, wala macho yake hayashibi utajiri. Basi asema, Ni kwa ajili ya nani nafanya kazi, na kujinyima nafsi yangu mema? Hayo nayo ni ubatili, naam, ni taabu kubwa”.

Lakini kama mtu atakuwa na Amali na akamcha Bwana ana heri, kwani tabu yake si bure kama maandiko yasemavyo, ila kwa mwenye kumweka Bwana pembeni, amali yake itakuwa bure.

Mistari mingine yenye kutaja Amali ni pamoja na Mhubiri 5:19, na Mhubiri 8:15.

Ikiwa kazi yako ya mikono, inakulemea akili na nguvu na huoni faida yake basi kimbilia kwa Bwana YESU naye atakutia mizigo sawasawa na ile Mathayo 11:28.

Zaburi 127:2 “Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema, Na kukawia kwenda kulala, Na kula chakula cha taabu; Yeye humpa mpenzi wake usingizi”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/01/13/amali-ni-ninimhubiri-44/