by Nuru ya Upendo | 11 December 2025 08:46 pm12
Kibiblia ni neno lenye maana ya wale funza, ambapo hutokea palipo na mzoga, au uozo. Hivyo popote ukutanapo na Neno hilo, huashiria/humaanisha, uharibifu au maiti, au kaburi,
Kwamfano ukisoma;
Ayubu 17:14 Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu;
Buu kama lilivyotumika hapo ni kaburi, Ayubu akimaanisha katika hatua aliyofikia, kaburi, na uharibifu ni kama familia yake (baba yake, mama yake na dada yake), kama tunavyojua familia ni kitu cha karibu sana na mtu, ndivyo Ayubu alivyojiona katika hali aliyokuwa amepitia.
Maana yake, kifo kilikuwa karibu na yeye zaidi hata ya familia yake.
Sehemu nyingine inasema;
Ayubu 25:6 iuze mtu, aliye mdudu! Na mwanadamu, ambaye ni buu!
Mwandishi akimaanisha mwanadamu ni sawa na mzoga, (yaani mwili wenye uharibifu usio na umilele).
Neno hili utalisoma pia katika vifungu hivi;
Kutoka 16:20,24, Kumbukumbu 28:39, Ayubu 7:5.
Katika maeneo mengine kwenye biblia linatajwa moja kwa moja kama funza. (Isaya 66:24)
Hii ni hatma ya kila mwanadamu asiye na Mungu, yeye ni buu, haijalishi atakuwa na afya leo, anapesa zote ulimwenguni, anacheo kikubwa au elimu, maisha yake bila Yesu Kristo kumwokoa, ni buu tu (maiti, kaburi, )..atakufa na kuishia jehanam ya moto. Lakini akiokoka, hata ajapokufa, ataishi, siku ya ufufuo ikifika, atafufuliwa na kubadilishwa mwili wake na kupewa mwili mwingine wa utukufu, kisha Kwenda kuishi na Kristo milele na milele mbinguni.
Ikiwa haujaokoka, bado na upo tayari kufanya hivyo leo, basi basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba upokee msamaha wa dhambi leo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Msikwao ni mtu gani Na nini tunajifunza katika neno hilo? (Zaburi 69:8).
Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?
Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/12/11/buu-mabuu-humaanisha-nini-kwenye-biblia/
Copyright ©2025 Wingu la Mashahidi unless otherwise noted.