by Nuru ya Upendo | 30 December 2025 08:46 pm12
Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu
Wimbo ulio bora 2:15
15 : Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.
Kitabu cha wimbo ulio Bora ni kitabu kinachoeleza asili ya upendo wa Kristo kwetu na jinsi tunavyopaswa kuuitikia.
Kuwa urefu wa masomo yaliyo nyuma ya kitabu hiki fungua hapa >>> NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.
Lakini kwenye mstari huu, tunaona ni kama vile mtu kwa lugha ya picha anaona mbweha “ Wadogo” wamevamia shamba lake la mizabibu inayochanua na hivyo hawapuuzii kwasababu ya udogo wao, bali anatoa tamko la kukamatwa na kuondolewa…ili shamba lake linalochanua liwe salama.
Kimsingi mbweha si mnyama anayekula nyama tu, bali hula pia mizazibu, na mingine kuiharibu.
Hii ni kufunua nini katika hali zetu za rohoni..
Adui akishaona mahusiano Yetu na Kristo yanazaa matunda, huinua vitu Vidogo vidogo ili kuharibu mahusiano wakati mwingine unaweza usione kama vina madhara sana au vina nguvu sana, lakini katika eneo la kiroho kitu kidogo kina nguvu sawa na kitu kikubwa…
Hivi ndio vinavyoitwa mbweha wadogo..
Mambo Kama haya ni kama vile kuendekeza vishawishi vya dhambi kwenye maisha yako.
Kwa mfano wewe ni binti halafu kila siku unaona wanaume wanazungumza na wewe maneno ya mizaha, sasa kama usipokemea tabia hiyo, ukaona ni kawaida, tabia hizo ndogo ndogo ndizo zinazopelekea mtu baadaye kuanguka kwenye dhambi za uzinzi.
Samsoni, alipoona ushawishi wa delila unaendelea, badala aukatishe yeye akapuuzia mwisho wa siku akatekwa..
Hao ni mbweha wadogo wanaoharibu shamba lako, kila kichocheo na kishawishi kiwe kidogo kiasi gani usikipuuzie.
Wakati mwingine kuendekeza uvivu wa kiroho, yaani kupuuzia maombi, kupuuzia ibada, kidogo kidogo hupelekea kupoa kiroho, na hatimaye unajikuta kabisa umerudi duniani..mpaka unajiuliza nimefikaje hapa? Ni kwasababu uliendekeza uvivu wa kiroho..ulisema. nitaomba kesho, nikesha kesho, nitamtumikia Mungu mwezi ujao..mwishowe ukawa hivyo ulivyo leo…
Angalia ni eneo lipi la maisha yako limevamiwa na hawa mbweha wadogo, kisha chukua hatua za haraka kurekebisha.
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi wa kitabu cha wimbo uliobora.
Nini maana ya Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, (Wimbo 2:7)
Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?
Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/12/30/wale-mbweha-wadogo-waiharibuo-mizabibu/
Copyright ©2026 Wingu la Mashahidi unless otherwise noted.