MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

by Admin | 19 October 2019 08:46 pm10

Uthibitisho wa kwanza wa mtu kuwa na Roho Mtakatifu ni Utakatifu atakaouonesha, na Utakatifu kwa ujumla ndio tunda la Roho. Na uthibitisho wa Pili ndio karama aliyo nayo…. Na Mtu Mtakatifu ni lazima aoneshe vitu 9 vifuatavyo..pamoja na vingine vingi, lakini hivi 9 ndio msingi wa UTAKATIFU WA MTU.

  1. UPENDO
  2. FURAHA
  3. AMANI
  4. UVUMILIVU
  5. UTU WEMA
  6. FADHILI
  7. UAMINIFU
  8. UPOLE
  9. KIASI

Tabia hizi 9 zinapatikana kutoka katika kitabu cha Wagalatia..

Wagalatia 5:22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. 

Mtu Mwenye Roho Mtakatifu lazima awe navyo hivi vyote kwa pamoja! hapaswi kukosa hata kimoja..kwasababu vyote kwa pamoja ndio vinaitwa TUNDA LA ROHO, na si MATUNDA YA ROHO…Ikiwa na Maana ni lazima viende kwa pamoja.

Ubarikiwe.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?

EPUKA KUTOA UDHURU.

JE! NI SAHIHI KUJIPA CHEO MFANO MIGHTY PROPHET, CHIEF APOSTLE N.K?

BIBLIA INAKATAZA KUAPA KABISA, LAKINI KWANINI WATU WANAAPA MAHAKAMA?


Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/10/19/matunda-9-ya-roho-mtakatifu/