JE KUJIUA NI DHAMBI?

by Admin | 1 November 2019 08:46 pm11

Je Kujiua ni dhambi?

Ili kufahamu kuwa kujiua ni dhambi au la! Hebu tutafakari mstari ufuatao.

1Wakorintho 6:19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.

Mstari huu unatosha kutupa jibu la swali letu! Hebu tafakari ni sahihi kutumia vibaya mali ya mwingine?..Mtu akikuambia chukua kiatu changu hichi kivae ukitunze akakupa na mashari na wewe ukasema kwasababu umeshakabidhiwa basi una mamlaka ya kukitumia utakavyo na kukiharibu je mwenye kiatu atakuwa na hatia kukulipisha?

Ndivyo ilivyo na miili hii tuliyonayo Biblia inasema hapo juu kwamba SIO MALI YETU WENYEWE. Na hivyo kama sio mali yetu wenyewe hatuna mamlaka yoyote ya KUIUA. Je kujiua ni dhambi? Jibu ni ndio! kujiua ni dhambi kubwa sana mbele za Mungu, kwasababu mtu anayejiua anakuwa anaitumia mali ya Mungu isivyopaswa.

Na sio tu kujiua, bali hata kuichora chora au kuivalisha mavazi yasiyoipasa…Mwanamke akivaa mavazi ya mwanamume hapo ameitumia isivyopaswa mali ya Mungu, na kadhalika mwanamume naye vivyo hivyo..na mwanamke anayetoboa masikio baada ya kuujua ukweli, na anayevaa hereni na bangili wanaitumia mali ya Mungu isivyopasa..Mungu atawahukumu watu wote wasiotumia vyema miili waliyopewa.

1Wakorintho 3:16 “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi”.

Je unautunza mwili wako? Je Roho Mtakatifu anakaa ndani yako? Je una uhakika wa kwenda mbinguni?

Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

MAVAZI YAPASAYO.

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/11/01/je-kujiua-ni-dhambi/