Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

by Admin | 30 March 2020 08:46 pm03

SWALI: Nini maana ya  “Tusitweze unabii”?


JIBU: Tusome..

1Wathesalonike 5:19 “Msimzimishe Roho;

20 msitweze unabii;

21 jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;

22 jitengeni na ubaya wa kila namna”.

Maana ya neno “kutweza” ni kudharau au kupuuzia jambo fulani…Hivyo biblia inaposema msitweze unabii maana yake ni “msiudharau/msiupuuzie unabii”..Na unabii unaozungumziwa hapo ambao haupaswi kutwezwa (maana yake haupaswi kudharauliwa/kupuuziwa)..ni unabii wa kurudi kwa Bwana mara ya pili.. ambao Mtume Paulo aliwaonya Wakristo hao waliopo Thesalonike mwanzoni kabisa mwa sura hiyo ya tano(5). Tusome..

1 Wathesalonike 5:1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Huu ndio unabii wa kwanza ambao haupaswi kupuuziwa hata kidogo, na haukuandikwa kwa Wathesalonike tu peke yao, bali hata kwetu sisi, kwasababu ndio tunaoishi ukingoni mwa nyakati kabisa kuliko vizazi vyote vilivyotangulia. Ukisoma sura yote ya 5 hiyo ambayo ndio ya mwisho kabisa ya kitabu hicho cha 1Wathesalonike utaona jinsi biblia inavyotuonya kwa msisitizo mkubwa kujiweka tayari na siku hiyo ya kurudi kwa pili kwa Kristo, Kwamba siku hiyo inakuja kama mwivi na tusilale usingizi kama wengine walalavyo, na TUSIUUPUUZIE WALA KUUDHARAU HUO UNABII…Kwasababu ni kweli siku hiyo yaja na Mungu hawezi kusema uongo…wote wanaoudharau huo unabii siku hiyo itawajia kama mwivi na kutakuwa na maombolezo makubwa na majuto makubwa, watatamani warudishwe dakika tano nyuma warekebishe mambo yao, lakini itashindikana.

Na hautwezwi kwa midomo tu bali matendo pia…Mtu ambaye hajajiweka tayari kwa kumwamini Yesu Kristo na kutubu dhambi zake kwa kumaanisha kuziacha, na kuishi kulingana na Neno la Mungu, ingawa kila siku anasikia injili lakini anapuuzia mtu huyo ANAUTWEZA UNABII, hali kadhalika mtu ambaye kila siku anasikia habari za kurudi kwa Kristo mara ya pili na anadhihaki na kudharau na kuwaona wanaomgoja Bwana ni watu waliorukwa na akili, na wanaopoteza muda wao, au wamepoteza dira ya Maisha, huyu naye anafanya dhambi hiyo hiyo ya kuutweza unabii ambapo siku moja atajuta majuto makuu na hatapata nafasi ya kurekebisha mambo yake, na mambo hayo yatakuwa hivi karibuni, moja ya hizi siku hii dunia itakuwa si dunia tena..

Vilevile Na unabii mwingine wowote wa kwenye biblia sio wa kuudharau kabisa, kwasababu kila alilolisema Bwana lazima litatimia.

Hivyo kama hujaokoka, saaa wokovu ni sasa, sio baadaye wala kesho..Tubu sasa na Kristo atakusamehe bure kama alivyoahidi.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/03/30/biblia-inamaanisha-nini-inaposema-tusitweze-unabii/