Je tunaruhusiwa kutumia vidonge wakati wa kufunga?

by Admin | 16 May 2022 08:46 pm05

Je ni tunaruhusiwa kunywa dawa wakati wa kufunga, au kuonja chakula wakati wa kupika kwaajili ya wengine?

Jibu: Unapofunga unakuwa unajizuia kula chakula au kunywa chochote, kwa lengo Fulani la kiroho. Lakini hatufungi kwa sheria au kanuni Fulani maalumu (biblia haijatupa kanuni yoyote maalumu), wala agizo la Sharti ya kufunga. Isipokuwa imesema tu “mambo mengine hayatoki isipokuwa kwa kufunga na kuomba”.

Mathayo 17: 21 “Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga”

Lakini tukirudi kwenye swali, je tunaruhusiwa kunywa dawa wakati wa kufunga?

Jibu ni NDIO! Kama kuna ulazima huo, kwasababu “Vidonge sio chakula” huwezi kula vidonge ukashiba, au ukakata njaa. Vidonge kazi yake ni kutibu tatizo Fulani lililopo ndani ya mwili (yaani vimetengenezwa kwa lengo la matibabu). Kwahiyo mtu anaweza kuwa amefunga na huku anatumia dawa.

Vile vile kuonja ladha ya chakula, kama kimekolea chumvi, au viungo hakubatilishi mfungo!..Kwamfano unaweza kuwa umefunga, lakini unalo jukumu la kupika chakula kwa wengine ambao hawajafunga! Mf.watoto, katika mazingira kama hayo, unalazimika kuonja chakula kama kimeiva, au kimekolea chumvi..(lakini kwa kiwango kidogo tu! Cha kuishia kwenye ulimi).

Ukionja kwa namna hiyo hufanyi dhambi, wala hakuharibu mfungo wako.. Kwasababu hapo umeonja na hujala. Lengo lako ni kuonja kama chakula hicho kipo sawa au la!.. Ungekuwa umeonja kwasababu unayo njaa, hapo ingekuwa ni tatizo, lakini hujaonja kwa lengo hilo.

Kwasababu ingekuwa hilo ni tatizo, basi hata mswaki asuhuhi, ingekuwa si ruhusa kupiga!..kwa maana ile dawa ya meno, tunapoiweka mdomoni, tayari tunaionja, hata kama hatutaki, vile vile tusingepaswa tusikie hata harufu ya chakula, lakini hayo mazingira hatuwezi kuyaishi.. Ni lazima tusafishe vinywa vyetu kila siku, na pia tutakutana na mazingira tofauti tofauti mahali tunapoishi..

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba kutumia dawa wakati wa mfungo si kosa, wala kuonja chakula kwakiwango kidogo kinachoishia ulimini si dhambi.

Lakini Zaidi ya yote, mfungo kwa mkristo unapaswa uwe ni jambo la mara kwa mara, inasikitisha mtu anayejiita ni mkisto lakini hana rekodi yoyote ya kungunga angalau wiki moja mfululizo.

Mkristo wa namna hii nguvu zake za kiroho zipo chini sana, kuna mambo katika Maisha yake, hawezi kuyapokea kwasababu Bwana Yesu mwenyewe alisema “kuna mambo hayawezekaniki isipokuwa kwa kufunga na kuomba”.

Bwana atusaidie tuwe waombaji na vile vile wafungaji!

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

Je mama mjamzito anaruhusiwa kufunga?

Je! ni halali kwa mtu wa Mungu kutumia njia za uzazi wa mpango,ikiwamo mipira?

Je sisi wakristo tunaruhusiwa kufanya 40 za marehemu?

Easter ni nini?..Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/05/16/je-tunaruhusiwa-kutumia-vidonge-wakati-wa-kufunga/