Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?

by Admin | 2 February 2023 08:46 am02

JIBU: Wapo wanaofikiri kwamba shetani amefungwa, atakuja kufunguliwa kipindi Fulani huko mbele, lakini pia wapo wanaodhani, shetani anaishi mahali Fulani kuzimu( aidha chini ya bahari, au kwenye sayari fulani), ambapo huko kuna amesimika utawala wake unaofanana na huu wa duniani.

Lakini ukweli ni kwamba shetani hajafungwa, wala hayupo katika eneo Fulani rasmi la mwilini, ambalo unaweza kwenda ukakutana naye.

Ikumbukwe kuwa ibilisi anafanya kazi katika ulimwengu wa roho, alipoasi mbinguni, alitupwa chini duniani, akaanza kazi yake ya kuudanganya ulimwengu mpaka akafanikiwa kuuteka ukawa chini ya milki yake, Tunalithibitisha hilo katika maneno aliyomwambia Bwana Yesu.

  Luka 4:5 Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja.

6  Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo.

7  Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako. 8  Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke

Hivyo shetani yupo anazunguka zunguka duniani hana makao rasmi, Alimwambia hivyo Mungu.

Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.  7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo”.

Atakuja kufungwa kipindi ambacho utawala wa miaka 1000 wa amani wa Yesu Kristo kuanza, na baadaye atafunguliwa kidogo, lakini kwasasa hajafungwa yupo duniani ndio chanzo cha maovu yote, wala hana eneo Fulani rasmi kwamba amejijengea  anaishi huko na mapepo yake, hapana bali wanafanya kazi katika ulimwengu wa roho, wakijigawanya tu katika vitengo mbalimbali, wengine katika anga, wengine, katika mataifa, wengine katika familia moja moja, na wengine katika kila huduma/au kanisa la Kristo lilipo, wengine katika uchawi n.k.

Hivyo, sisi tutamshinda na kumpinga tu kwa kulishika Neno la Mungu, na kudumu katika maombi daima.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

POPOBAWA NI KWELI YUPO?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

MATESO YA KUZIMU.

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2023/02/02/shetani-anaishi-wapi-je-amefungwa-au-yupo-kuzimu/