Mabibi wastahiki walikuwa ni watu gani? (Esta 1:18).

by Admin | 31 December 2023 08:46 am12

(Mada maalumu kwa wanawake)

Jibu: Mabibi Wastahiki ni “wanawake wa heshima”.. kundi hili la wanawake lilihusisha wake za Wafalme, Maliwali au Maakida au Majumbe..

Wakati mfalme Ahasuero alipowafanyia maakida wake na maliwali wake karamu, biblia inatuambia kuwa Malkia Vashti (mke wa mfalme), yeye naye aliwafanyia wanawake (ambao ni wake wa hao maakida na maliwali) karamu.

Esta 1:2 “siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni;

3 mwaka wa tatu wa kumiliki kwake, ikawa aliwafanyia karamu maakida wake wote na majumbe wake; wakuu wa Uajemi na Umedi, watu wenye cheo na maakida wa majimbo, wakihudhuria mbele zake. 

4 Akawaonyesha utajiri wa ufalme wake mtukufu, na heshima ya enzi yake bora siku nyingi, maana siku mia na themanini……………………..

9 Tena Vashti, malkia, naye akawafanyia karamu WANAWAKE NDANI YA NYUMBA YA KIFALME YA MFALME Ahasuero”.

Sasa hao wanawake waliokuwa wake za “maliwali na maakida” ndio waliojulikana kama “mabibi wastahiki”.. wakiongozwa na Malkia Vashti.

Lakini tunachoweza kujifunza ni kuwa ile karamu ya hawa wanawake haikuwa na utukufu wowote, kwani iliishia kuleta aibu kubwa katika ufalme wote wa Uajemi. Kwani Malkia Vashti alikosa utii kwa Mfalme alipoitwa, na Zaidi sana alionyesha dharau hizo mbele ya Mfalme na waliwali wake wote.

Na huenda pia kiburi hicho kilichochewa na jopo la wale wanawake wengine wastahiki waliohudhuria karamu hiyo ya Malkia Vashti. Hiyo ikifunua kuwa hakuna cha maana walichokuwa wanakizungumza au kukipanga katika hiyo karamu Vashti aliyowaandalia, huenda yaliyokuwa yanazungumziwa kule ni UMBEA TU na kusema mapungufu ya waume zao!

Hiyo ikamfanya Vashti apoteze umalkia wake, na hata hao wanawake wengine ambao wastahiki kuzidi kutawaliwa na waume zao.

Esta 1:16 “Basi Memukani akajibu mbele ya mfalme na maakida, Huyu Vashti, malkia, hakumkosa mfalme tu peke yake, ila na maakida wote, na watu wote pia walioko katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero. 

17 Kwa maana tendo hilo la malkia litajulikana na wanawake wote, hata waume zao watadharauliwa machoni pao, itakaponenwa ya kuwa mfalme Ahasuero aliamuru Vashti, malkia, aletwe mbele yake, bali hakuja. 

18 Hata na leo hivi mabibi wastahiki wa Uajemi na Umedi waliokwisha kuzisikia habari za tendo lake malkia watawaambia vivi hivi maakida wote wa mfalme. Hivyo kutatokea dharau nyingi na ghadhabu tele.

 19 Basi mfalme akiona vema, na itoke kwake amri ya kifalme, nayo iandikwe katika sheria za Waajemi na Wamedi isitanguke, ya kwamba Vashti asifike tena mbele ya mfalme Ahasuero; na umalkia wake mfalme ampe mwingine aliye mwema kuliko yeye.

 20 Basi mbiu ya mfalme atakayoipiga itakapotangazwa katika ufalme wake wote, nao ni mkubwa, wake wote watawaheshimu waume zao, wakubwa kwa wadogo.

 21 Basi neno hili likawapendeza mfalme na maakida; naye mfalme akafanya sawasawa na neno lake Memukani.

 22 Kwa maana alipeleka nyaraka katika majimbo yote ya mfalme, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake, ya kwamba kila mwanamume atawale nyumbani mwake, na kuitangaza habari hii kwa lugha ya watu wake”.

Tabia kama hii inaendelea mpaka leo kwa baadhi ya wanawake walioolewa!, ambao baada ya kuolewa wanawaona waume zao kama si kitu tena, na hata kupoteza UTII kwao!. Pasipo kujua kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kujipotezea nafasi zao ndani ya familia zao, kwani badala ya kuwa kichwa Mungu anawaweka kuwa wa mwisho.

Neno la Mungu linasema wanawake na wawatii waume zao.

1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;

2  wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.

3  Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, NA KUWATII WAUME ZAO”

Soma tena Waefeso 5:24 na Tito 2:5 utaona jambo hilo hilo, sasa mwana-mama unatolea wapi kiburi!!!. Badilika, na anza kuwa mtii, ikiwa haupo ndani yako, na hiyo ni kwa faida yako na familia yako. Kitabu cha Esta, huenda kingepaswa kiitwe kitabu cha Vashti, lakini kwa kiburi chake, umalkia wake akapewa Esta.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ESTA: Mlango wa 5, 6 & 7

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

NI KIJIJI CHA AINA GANI UPO?

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2023/12/31/mabibi-wastahiki-walikuwa-ni-watu-gani-esta-118/