NI KIJIJI CHA AINA GANI UPO?

NI KIJIJI CHA AINA GANI UPO?

Yapo makazi ambayo si rafiki sana kwaajili ya uponyaji wa maisha yako!.

Kuna mahali/vijiji/mitaa ambayo ukikaa ni ngumu kupokea chochote kutoka kwa Mungu, isipokuwa Mungu mwenyewe amekuambia uishi hapo!. Lakini kama hakuna msukumo wowote wa KiMungu kuishi hapo, basi kuwa makini na mahali utakapopachagua!, kama ni mtaa, mji au kijiji.

Utauliza kwa namna gani?

Utakumbuka yule kipofu aliyepelekwa kwa Bwana ili aponywe!, biblia inasema “Bwana Yesu alimtoa nje ya kijiji kabla ya kumponya” na hata baada ya kumponya alimzuia asirudi kile kijiji alichokuwepo!.

Marko 8:22 “Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse.

23  Akamshika mkono yule kipofu, AKAMCHUKUA NJE YA KIJIJI, akamtemea mate ya macho, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu?

24  Akatazama juu, akasema, Naona watu kama miti, inakwenda.

25  Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, naye akatazama sana; akawa mzima, akaona vyote waziwazi.

26  Akampeleka nyumbani kwake, akisema, HATA KIJIJINI USIINGIE”

Umeona?..sababu ya Bwana kumtoa huyu kipofu nje ya kijiji si kwasababu ya ghasia ya watu!, hapana bali ni kutokana na hali ya kiroho ya mahali pale, maana yake mazingira ya kile kijiji yalikuwa ni magumu kwa yule mtu kupokea uponyaji! (Maana yake ukinzani uliokuwepo pale ulikuwa ni mkubwa sana), Ndio maana Bwana akamtoa kwanza nje ya kijiji kabla ya kumponya!

Hali kama hiyo inaendelea hata leo!, ipo mitaa ambayo ina vita vikali vya kiroho kuliko mingine, vipo vijiji vilivyo vizito kuliko vingine, na sisi kama wana wa Mungu ni lazima tuongozwe na roho mahali pa kwenda na mahali pa kuishi.

Aina ya vijiji/mitaa ifuatayo kuwa makini nayo!

1. Yenye watu wengi wasio na hofu ya Mungu.

Ukiona mtaa/kijiji hakuna hofu ya Mungu, maana yake watu wa mahali hapo ni watu wasiojali, na hata kuidharau injili, na kuipinga kazi ya Mungu, kuwa makini na huo mtaa au hicho kijiji. Kwasababu mitaa inayoikataa Injili mara nyingi inakuwa chini ya vifungo vya laana (Mathayo 10:14-15), na mwisho wake huwa inaharibiwa na Mungu aidha kwa mapigo ya magonjwa au majanga au hali za kiuchumi!.

2. Yenye kiwango kikubwa cha ushirikina na uasherati.

Uchawi na uasherati ni ibada kuu mbili za shetani. Mahali palipojaa kiwango kikubwa cha uasherati na ushirikina fahamu kuwa hiyo ni kambi ya adui asilimia zote. Kuwa makini na mahali hapo!. Kama Roho wa Bwana amekuongoza uishi, basi ishi hapo na utafanikiwa, maana ni mapenzi yake!..lakini kama sio, basi usiishi hapo, ili ubaki salama na familia yako!, (mara nyingi adui anatumia mitaa/vijiji kuharibu watoto au ndoa), hivyo kuwa makini!

Ufunuo 18:4 “Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.

Aina za dhambi

UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments