Title November 2018

JE! UNAMPENDA BWANA?

Bwana Yesu alisema “MTU AKINIPENDA  ATAZISHIKA AMRI ZANGU (Yohana 14:15)” lakini tunaona hiyo pekee haitoshi kwasababu kama  ingekuwa inatosha Bwana asingemwambia tena Mtume Petro mahali pengine  maneno haya…

Yohana 21:15 “ Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia , Naam ,Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu.
16 Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu.
17 Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.

Kwahiyo tunaona licha ya kuzishika amri zake, kuna mambo mengine matatu ya yatakayokamilisha upendo wetu kwa Kristo.  Nayo ni (1) KULISHA WANA-KONDOO WAKE, (2) KUCHUNGA KONDOO ZAKE (3) KULISHA KONDOO ZAKE.

KUZISHIKA AMRI:

Kuzishika Amri za Mungu ni kuzielewa, kuzipenda na kuziishi, na sio kuzikariri  na yeyote aziishie amri za Mungu  amri hizo zinapaswa zisiwe nzito kwake, Maagizo ya Mungu yanapaswa yawe ni mepesi kwake kuyashika kwasababu Roho wa Mungu anakaa ndani yake, hivyo Nira ya Kristo kwake inakuwa ni laini, na mzigo unakuwa mwepesi,hajisikii uzito wala hajilazimishi kuzitimiza sheria za Kristo ndani yake..

Hatatumia nguvu nyingi kujizuia kutenda dhambi, hivyo anakuwa anazitimiza pasipo kujiweka katika utumwa, hawi chini ya utumwa wa sheria, kwasababu Nia ya Mungu sio sheria zake ziwe mzigo mzito kwetu, nia yake sio tuzishike amri zake kwa uchungu na mateso na utumwa ..hapana na ndio maana alisema katika..

Kumbukumbu 30: 10 “ukiwa utaifuata sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa kuyashika maagizo yake, na AMRI ZAKE zilizoandikwa katika chuo hiki cha torati; ukimwelekea Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote.

11 Kwa maana maagizo haya nikuagizayo leo, SI MAZITO MNO KWAKO, WALA SI MBALI.

12 Si mbinguni, hata useme, Ni nani atakayetupandia mbinguni akatuletee, aje atuambie tusikie, tupate kuyafanya?

13 Wala si ng’ambo ya pili ya bahari, hata useme, Ni nani atakayetuvukia bahari, akatuletee, aje atuambie, tusikie, tupate kuyafanya?

Unaona ili kuzishika Amri za Mungu,  ni lazima Kuwepo na wepesi ndani yako ambao Mungu ameuweka, ili Sheria zake zisiwe nzito mno kwako. Hivyo kwa kuishi maisha kama hayo ya kutimiza sheria za Mungu pasipo utumwa. Huko ndiko kuzishika Amri za Mungu. Na huko ndiko kumpenda Bwana. Lakini kufanya hivyo pekee hakutoshi kuonyesha upendo wetu kwa Bwana. Lipo jambo lingine la ziada la kufanya ili kutimiza upendo wetu kwake.

Na jambo hilo si lingine zaidi ya kulitazama kundi la Mungu kwa kulilisha na kulichunga.Ndio maana Bwana alimwuliza Petro mara tatu swali lile lile? Je! wanipenda?

 NINI MAANA YA KULISHA KONDOO WAKE:

Kama neno lenyewe lilivyo “kondoo wake”  ikiwa na maana kuwa sio kondoo wa mtu Fulani, bali ni kondoo wa Kristo. Hivyo mtu hawezi kujiamulia tu, njia au namna ya kuwalisha,  kwa lugha nyingine Petro aliambiwa yeye ni  mchungaji aliyeajiriwa kuwachunga na kuwalisha kondoo, hivyo kondoo hata mmoja asipolishwa inavyopaswa ataulizwa na aliyemwajiri, kwasababu kondoo sio wake, bali ni wa mtu mwingine.

Kondoo wanawakilisha watu wa Kristo waliomwamini yeye, na wachache wanaohitaji kumwamini.. hao ndio kondoo wa Kristo, biblia inasema tuwalishe hao, na chakula chao sio nyasi bali ni NENO LA MUNGU lisilochanganywa na chochote..  Kazi kubwa ya mchungaji ni kwenda huku na huko kutafuta mahali penye nyasi zinazowafaa kondoo.. Kadhalika Sisi kama wakristo tuliookolewa tunalo jukumu la kuwaongoza wenzetu, au kuongozana sisi kwa sisi mahali panapopatikana Neno la Uzima.

Ukimwona ndugu yako anahangaika huku na kule, ni wajibu wako kama mkristo kumwelekeza kwa upendo mahali ambapo anaweza kuishibisha nafsi penye Neno la Uzima. Huko ndiko kumpenda Kristo. Maadamu ndani yetu kuna nuru kidogo ambayo haimo ndani yao.

KUCHUNGA KONDOO WAKE.

Kama neno lilivyo “kondoo wake” ikiwa na maana kuwa “sio kondoo wa  mtu fulani” bali ni kondoo wa Yesu Kristo, hivyo hatuwezi kujichagulia njia ya kuwachunga..Tunapokea maagizo kutoka kwake namna ya kuwachunga.

Sasa Bwana Yesu alisema “Tujihadhari na mbwa mwitu wakali” na pia alisema “tujihadhari na mbwa mwitu wanaokuja na mavazi ya kondoo”…Sasa dhumuni la mbwa mwitu kuvaa mavazi ya kondoo ni ili na yeye aonekane kama kondoo ili asitumie nguvu nyingi kuwakamata kondoo. Sasa hao Bwana ndio aliosema tujichunge nao sana, na tukiisha kujihadhari nao, tuwachunge na ndugu zetu dhidi yao.. HUKO NDIKO KUCHUNGA KONDOO WAKE.

Sasa hawa mbwa-mwitu ndani ya mavazi ya kondoo ni wakina nani?

Mathayo 7: 15 “Jihadharini na manabii wa uongo, WATU WANAOWAJIA WAMEVAA MAVAZI YA KONDOO, WALAKINI KWA NDANI NI MBWA-MWITU WAKALI. Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?”

Unaona, Manabii wa uongo ndio mbwa-mwitu ndani ya mavazi ya kondoo.  Na manabii wa uongo sio tu manabii, hapana bali hata waalimu wa uongo, wachungaji wa uongo, watumishi wa uongo, wainjilisti wa uongo, maaskofu wa uongo, mashemasi wa uongo, wapendwa wa uongo, waimbaji wa uongo n.k hawa wote kwa pamoja wanaunda kundi linalojulikana kama manabii wa uongo.

Yaani watu wote ambao kwa nje wanajulikana kama ni wakristo lakini ndani katika maisha yao ya siri sio wakristo hata kidogo, ni watu wa ulimwengu huu, walevi, watukanaji, vuguvugu, waasherati, walaji rushwa n.k…Na bado wanahubiri na kushuhudia na kuimba. Wengine wanajiita PAPA wakiwapoteza watu waabudu sanamu Mungu alizozikataa.Hiyo ndio roho  ya mpinga-kristo.

Hao ndio Bwana, aliotuonya tulichunge kundi lake dhidi yao, ikiwa tumeona mtu ajiitaye mkristo halafu ni mwasherati au mlevi au mwabudu sanamu,tunapaswa tujihadhari naye Hatupaswi kuwashauri watoto wa kiroho(kondoo wa Kristo) kuambatana nao, ni lazima tutawachunga kondoo wa Mungu dhidi yao..Na zaidi ya yote tutawafundisha hila za hao manabii wa uongo, na Roho ya Mpinga Kristo inavyotenda kazi, Biblia inasema

1Wakoritho 5: 9 “Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.

10 Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.

11 Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba MSICHANGAMANE NA MTU AITWAYE NDUGU, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.

12 Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?

13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. NINYI MWONDOENI YULE MBAYA MIONGONI MWENU.”

Hivyo tunapoona ndugu yetu, anapotea na uongo wa adui ni jukumu letu sisi,  kumwokoa, hatuwezi tukasema tunampenda Kristo na tukaacha kulipenda na kundi lake, Popote pale tulipo katika hatua yoyote ile ya kiroho, ni wajibu wetu kuwasaidia walio chini yetu..

Hata katika familia jukumu la kulea watoto sio la wazazi peke yake, lakini utakuja kukuta kwamba hata watoto wana jukumu la kuleana wao kwa wao..kaka au dada anawalea wadogo zake na hao wadogo wanawalea walio wadogo zaidi. Na katika familia ya Mungu ni hivyo hivyo, ndio jukumu tulilopewa kulishana na kuchungana.

Kuchunga kondoo wa Kristo sio jukumu la mchungaji kanisani tu au muhubiri bali ni jukumu la Kila Mkristo.

Bwana atusaidie sote tuweze kumpenda yeye kweli kweli, KWA KUZISHIKA AMRI ZAKE na KULICHUNGA KUNDI dhidi ya mbwa mwitu wakali lake na KULILISHA chakula cha Neno la Uzima.

Mungu akubariki.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine…

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MAFUNUO YA ROHO.

ITAFAKARI VEMA KAZI YA MUNGU

SADAKA ILIYOKUBALIKA.

JE! MUNGU ATAIANGAMIZA DUNIA TENA BAADA YA GHARIKA YA NUHU?

MANENO HAYA YANA MAANA GANI? “..KWA SABABU HAMTOI ROHO KWA KIPIMO. (YOHANA3:34)”

NI KWA JINSI GANI MUNGU ANAPATILIZA MAOVU YA BABA ZETU SAWASAWA NA KUTOKA 20:5-6?

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.


Rudi Nyumbani

Print this post

KITENDAWILI CHA SAMSONI

Waamuzi 14: 13”……… Basi wakamwambia, Haya, tega kitendawili chako, ili tupate kukisikia. 14 Naye akawaambia, KATIKA HUYO MWENYE KULA KIKATOKA CHAKULA, KATIKA HUYO MWENYE NGUVU UKATOKA UTAMU

Kitendawili hichi Samsoni alisukumwa kukisema baada ya kukutana na tukio la ajabu katika safari yake alipokuwa akishuka kwenda Ufilisti yeye pamoja na wazazi wake kwa ajili ya kumchumbia binti aliyekuwa amemwona huko katika kijiji kimoja kilichoitwa Timna.

Sasa wakati akiwa njiani alikutana na Simba mwenye nguvu ambaye alitaka kumrarua, lakini Samsoni alipomwona alinyanyuka na kumshambulia kama biblia inavyosema jinsi alivyo mpasua haraka sana ni kama vile mtu anavyompasua mbuzi, Samsoni hakutumia silaha yoyote mkononi, ni kitendo kilichochukua sekunde chache tu, na shughuli yote ilikuwa imekwisha, akaendelea na safari yake.,

Hilo lilikuwa jambo la kawaida kwake halikumwingia sana moyoni mwake, lakini jambo lililomshangaza ni baada ya kurudi kutoka huko Timna yeye pamoja na wazazi wake na kukuta ule mzoga wa simba umezungukwa na nyuki wengi sana na ndani yake kuna Asali.

Ni jambo la kushangaza! Hata sisi sote tunajua Moja ya wadudu walio wasafi na hawatui katika vitu vilivyo na uozo au uchafu wowote ni NYUKI. Nyuki huwa utawakuta sana sana kwenye maua, mazuri, na kwenye miti yenye matunda na yenye harufu wakitafuta vimelea vizuri vingi tofauti tofauti kwa ajili ya kutengeneza asali yenye ubora ule tunaouna..

Na kamwe haijajawahi kutokea nyuki kutua kwenye mizoga na miozo, tena cha kushangaza zaidi ndani ya muda ule mfupi kwenye mzoga wa Yule Simba walikuwa tayari wameshatengeneza asali nyingi, na wakati nyuki kutengeneza asali iliyotayari kulika tunajua inachukua sio chini ya miezi 6 na kuendelea.

Hivyo Samsoni kuona jambo lile ilimshtusha sana, mpaka kugundua kuwa lipo somo kubwa ndani yake anapaswa ajifunze, na baada ya kutafakari kwa utulivu sana ndipo akatunga kitendawili kile na kuwapelekea wafilisti.

Akawaambia: “Katika huyo mwenye kula kikatoka chakula, Katika huyo mwenye nguvu ukatoka utamu.(Waamuzi 14:14)”

Samsoni akijua kabisa hakuna hekima yoyote ya kibinadamu inayoweza kukitegua kitendawili kile isipokuwa Mungu au yeye peke yake awafunulie. Na ndio maana ukisoma hiyo habari utaona wale wafilisti walipoona muda wao waliopewa wa kurudisha majibu unakaribia kuisha na bado majibu hawana, wakatumia hila ya kumshawishi Yule binti wa kifilisti aliyekuja kumchumbia amulize Samsoni tafsiri ya kitendawili kile..Na baada ya Yule binti kumbembeleza sana ndipo Samsoni akawafunulia tafsiri yake. Lakini alikasirika sana kwasababu walitumia hila kupata majibu na tafsiri yake ilikuwa ni hii:

Wakamwambia:,NI KITU GANI KILICHO TAMU KULIKO ASALI? NI KITU GANI KILICHO NA NGUVU KULIKO SIMBA?

Kwa lugha rahisi tunayoweza kuielezea kitendawili hicho kwa sasa ni hii “CHAKULA KITAMU KULIKO VYOTE MFANO WA ASALI, HUWA KINATOKA KWA WANYAMA WAKALI NA WENYE VITISHO KAMA SIMBA”…Pia haijabadili maana tukisema “HAZINA KUBWA ZA MAFANIKIO YOTE, HAZIPATIKANI PENGINEPO ISIPOKUWA KATIKA MAZINGIRA YA MAJARIBU MAZITO, AU VITISHO AU MAADUI WAKALI”.

Samsoni hakutazamia kuwa katika yule Simba aliyekuwa anataka kumrarua ndani yake kuna ASALI. Hakutazamia kuwa kutoka kwa Yule adui yake ambaye alikuwa anataka kummeza huyo huyo ndiye atakayeweza kumtolea chakula chake cha kila siku.. Na ndio maana ukisoma habari za Samsoni maisha yake kuanzia huo wakati na kuendelea hakuwahi kuwaogopa maadui zake walipokuja kushindana naye..Ilifika wakati alikuwa anajiona salama zaidi kwenda kulala katikati ya hema za wafilisti [maadui zake] zaidi hata ya alipokuwa nyumbani kwao Israeli ni kwasababu gani? Ni kwasababu alijua kuwa “ katika huyo mwenye kula, ni lazima kitoke chakula tu, na katika huyo mwenye nguvu utatoka utamu nao”.

Ujasiri huo huo aliokuwa ndani ya Samsoni tunaweza kuuona pia ukijidhihirisha ndani ya Manabii wa Mungu miaka mingi baadaye baada ya kufa Samsoni. Ule ujasiri tunauona tena juu ya huyu nabii aliyeitwa ELISHA. Tunasoma habari zake katika 2Wafalme 6. Siku moja mfalme wa Shamu alikasirika sana baada ya kuona siri zake zinafichuliwa na Elisha huko Israeli, Kila alipopanga njama dhidi ya waisraeli Elisha alifunua siri zao na mikakati yao.

Hivyo huyu mfalme wa Shamu akaamua siku moja kupanga majeshi yake yote kuenda kuuhusuru huo mji aliokuwa anaishi Elisha, Na walipoamka asubuhi kumbe jeshi lote la Shamu limewazunguka kama tunavyosoma habari Yule mtumishi wake Elisha aliogopa sana kwasababu alijua siku hiyo ndio mwisho wake umefika, Lakini Elisha alimwambia usiogope simba hawa..Ndipo Yule kijakazi akafunguliwa macho yake na kuona jeshi kubwa la malaika limewazunguka kuwapigania na kuwashindania.

Vivyo hivyo ilitokea wakati huo huo hilo jeshi la shamu liliuzunguka tena mji wa Samaria ili kutaka kuungamiza mji wote na vitu vyao vyote, Elisha naye akiwa humo humo ndani, Hao washami waliuzingira mji wote kwa muda wa siku nyingi, kiasi kwamba hakukuwa hata na mtu wa kuingiza na kutoa chakula mle mjini, matokeo yake kupelekea chakula kupungua sana na uchumi wa mji kuporomoka kwa kiwango kikubwa, njaa ilikuwa kali kiasi kwamba hata mavi ya njiwa yalikuwa ni chakula kinachouzwa kwa kugombaniwa na kwa bei ya juu sana.. Kichwa cha punda nacho kiliuzwa kwa bei ya juu sana, watu walikuwa wanakufa kwa njaa na Elisha naye yupo ndani yake.

Mfalme wa Israeli alipoona Elisha ndiye wakati wa nyuma aliwaombea rehema hao hao maadui zao waliokuja kuwahusu wasiangamizwe, akakasirika sana na kutuma mtu aende kumuua lakini Elisha, hakuwa na wasiwasi wowote wala hofu yoyote, kwasababu alilitambua lile neno kama la Samsoni:

KATIKA HUYO MWENYE KULA, KITATOKA TU CHAKULA, NA KATIKA HUYO MWENYE NGUVU NI LAZIMA UTOKE UTAMU”.

Hivyo Elisha akasubiri mpaka dakika ya mwisho, hakudhubutu kufungua kinywa chake na kumkufuru Mungu kwamba kwanini Mungu amewaacha mpaka wamefikia hatua hiyo? kama walivyokuwa wananung’unika wana wa Israeli kule jangwani. Bali yeye alitulia kimya mpaka Yule mjumbe aliyetaka kuja kumuua alipofika.Na ndipo Neno la BWANA likamjia Elisha na kumwambia Yule mtu.

2Wafalme 7: 1 “Elisha akasema, Lisikieni neno la Bwana; Bwana asema hivi, Kesho panapo saa hii, kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, langoni pa Samaria.

2 Basi yule akida, ambaye mfalme alikuwa akitegemea mkono wake, akamjibu yule mtu wa Mungu, akasema, Tazama, kama Bwana angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akamwambia [Elisha], Angalia, wewe utaliona kwa macho yako, lakini hutakula.”.

Unaona? Watu hawakusadiki maneno yale, ni sawa leo hii mtu aseme bei ya gari lililokuwa linauzwa milioni 20 sokoni, kuanzia kesho na kuendelea litakuwa linauzwa kwa shilingi elfu 50…Kwa namna ya kawaida hilo haliwezi kuwezekana, na ndio maana hata Yule mjumbe kutoka kwa mfalme akamdhihaki Elisha na kumwambia hata kama MUNGU angefungulia madirisha ya ngano kutoka mbinguni hilo jambo lisingewezekana..hata kama magari yote ulaya yangetupwa Tanzania kama nguo za mitumba, hilo jambo lisingewezekana unaona?.

Lakini hawakujua kuwa Mungu si wanadamu..Hawakujua kuwa Yule SIMBA aliyekuwa anataka kupambana nao kumbe ndiye aliyewaletea ASALI NYINGI..Wale waliowahusuru pande zote ndio waliowaletea wao chakula.

Angalia jambo Mungu alilofanya. Kumbuka wale nao wasingeweza kuwazunguka wayahudi siku hizo zote bila kuwa na chakula, na nyara, na wanyama wengi na maghala ya nafaka pamoja nao. HIVYO KITU ALICHOFANYA BWANA NI KUWASIKILIZISHA SAUTI YA VITA USIKU WA MANANE, NA VISHINDO VIZITO VYA FARASI NA TETEMEKO la nchi kiasi kwamba wale Washami wakayeyuka mioyo wakidhani kuwa Israeli imekwenda kukodi mataifa jirani ili waje kuwasaidia..Hivyo jambo la haraka haraka ambalo wangeweza kufanya ni kuondoa maeneo yale kwa kasi sana wao kama wao pasipo kuchukua kitu chao chochote.

WALIACHA MAGHALA YAO YA CHAKULA, NYARA ZAO, HAZINA ZAO, FEDHA ZAO, WANYAMA WAO WENGI SANA.

Na asubuhi ilipofika wayahudi walishangaa wasione mtu, hivyo wakaenda kuchukua zile nyara zao zote, chakula siku ile kikawepo kingi kiasi kwamba bei ya chakula ilishuka ghafla na kuuzwa kwa bei ile ile Elisha mtu wa Mungu aliisema. Hivyo njaa iliyoikumba mji ilikoma ndani ya siku moja. Na uchumi wa Israeli wote kunyanyuka ndani ya siku moja.

Ni kwasababu gani? Ni kwasababu Elisha alijua katika huyo mwenye kula, kitatoka tu chakula, na katika huyo mwenye nguvu ni lazima utoke utamu”.

Nataka nikutie moyo wewe uliyeamua kuchukua uamuzi wa kumfuata Kristo kwa gharama zozote zile, usitishwe na majaribu yatakapokujia, usitishwe na hila za maadui, usitishwe na vikwazo, fahamu tu huko ndiko utajiri wako ulipo, huko ndiko chakula chako kilipo.. Wana wa Israeli walipokuwa wanapita katika hali ngumu kwa kitambo tu badala ya kuusubiria wokovu wa Mungu wao moja kwa moja walianza kumnung’unikia kana kwamba Mungu anawatesa..

Na ndio maana Mungu hakupendezwa nao kwasababu walikosa ufahamu kuwa mara nyingine kwa kupitia njia zile ndio Mungu alikuwa anawaletea hazina zao. Wakristo tunaomsubiria Bwana tukijifunza kanuni hizi hatutakuwa watu wa manung’uniko tunapokutana na vikwazo, na maadui badala yake ndio tutafahamu kuwa wakati wa mbaraka wetu ndio umekaribia.

Yusufu alipopelekwa katika gereza la wafalme mahali ambapo alikuwa anasubiria wakati wowote kukatwa kichwa, kama tu vile alivyomtabiria Yule muokaji wa mfalme kuwa atakatwa kichwa si zaidi yeye aliyekuwa anashutumiwa kwa kulala na mke wa mfalme..alifahamu kabisa yupo pale kusubiria siku ya kukatwa kichwa, lakini hakunung’unika na kulalamika akisema ni kwa nini Mungu mimi ninateseka huku muda wote huu angali ninalicha jina lako? Hakudhubutu kusema vile, yeye aliungojea tu kwasababu alitambua kuwa

katika huyo mwenye kula, kitatoka tu chakula, na katika huyo mwenye nguvu ni lazima utoke utamu”. Na tunasoma Kutoka kwa Farao ulitoka utamu.

Na kweli ulipofika wakati, Yule Yule aliyekuwa anamtazamia amuue, alikuja kumfanya kuwa waziri wake mkuu.

Hivyo kaka/dada uliyekombolewa kwa damu ya Bwana Yesu, usihangaike huku na kule jaribu linapotokea mbele yako, wala usilione ni kubwa, tulia na utauona wokovu wa Bwana katikati ya hatari, utiwe nguvu katika jaribu lolote unalopitia siku moja Mungu atakuthibitisha kwasababu huko ndiko kutokako utamu wa maisha yako ya sasa na ya baadaye.
Amen!

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

UKOMA NA UJANE ULIO NDANI YAKO, UMEUPATIA TIBA?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

USIACHE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU

NINI MAANA YA HUU MSTARI “NIMEVIPIGA VITA VILIVYO VIZURI, MWENDO NIMEUMALIZA, IMANI NIMEILINDA”?

NI LAANA IPI HIYO MUNGU ALIMAANISHA ATAIPIGA DUNIA NAYO KATIKA MALAKI 4:5-6?

JE! MWANADAMU WA KWANZA KUUMBWA NI YUPI MZUNGU MWAFRIKA AU MCHINA?


Rudi Nyumbani

Print this post

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

Ukisoma biblia kuna maneno  mtume Paulo aliyasema ambayo kwamfano yangetamkwa leo mbele za watu wengi, kimsingi yangeonekana kama ni kufuru. Jaribu kuwazia heshima Mungu aliwayowapa  mitume wake  12, hata kabla hawajaanza  kutumika  Mungu aliwaandaa kwa muda wa miaka 3,ukizingatia maandalizi yao hayakuwa kama haya ya kwetu, wao walipewa nafasi ya juu sana ya kipekee ya kuishi, kula, kulala na mkuu wa uzima mwenyewe kwa muda wa miaka mitatu na nusu.

Watu ambao Kristo mwenyewe alisema wamesha kuwa safi kwa lile Neno alilokuwa anawafundisha (Yohana 15:3), watu ambao Yesu aliyewatawaza mwenyewe na kuwatia mafuta wawe misingi ya Kanisa lake takatifu lililohai, Watu waliokuwa wamejaa Roho wa Mungu wenye sifa, na vyeo, walioheshimiwa na kuogopwa na kila mtu katika kanisa la Kristo mitume 12 wa Bwana.


Lakini ilifika wakati  siku moja mkristo mmoja aliyechipukia chini asiyejulikana sana ambaye hata hakuwepo siku ya Pentekoste anasimama kwa ujasiri na kuyaeleza makanisa  hakuna kitu cha ziada alichokiona wanacho zaidi yake yeye, licha ya kuwa na sifa nyingi katikati ya watakatifu lakini bado anasema wote wao ni mamoja kwake,. Habari Hiyo Tunaisoma katika..

 Wagalatia 2:6 “Lakini wale wenye sifa ya kuwa wana cheo; (walivyokuwa vyo vyote ni mamoja kwangu; Mungu hapokei uso wa mwanadamu); nasema, hao wenye sifa hawakuniongezea kitu; 

7 bali, kinyume cha hayo, walipoona ya kuwa nimekabidhiwa injili ya wasiotahiriwa, kama vile Petro ya waliotahiriwa;

 8 (maana yeye aliyemwezesha Petro kuwa mtume wa waliotahiriwa ndiye aliyeniwezesha mimi kwenda kwa Mataifa); 

9 tena walipokwisha kuijua ile neema niliyopewa; Yakobo, na Kefa, na Yohana, wenye sifa kuwa ni nguzo, walinipa mimi na Barnaba mkono wa kuume wa shirika; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara;”

Unaweza ukajiuliza  ni kwanini mtume Paulo alisema vile?, unadhani ni kwa kuonyesha kiburi chake kwa kufanikiwa kwake au vinginevyo?, jibu ni hapana lakini aliuzungumza ukweli wote katika Kristo, kwamba Mungu hapokei uso wa mwanadamu yoyote na ndivyo ilivyo. Kama biblia inavyosema katika

Matendo 10:34 “… Hakika natambua ya kuwa Mungu hana upendeleo; 

35 bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.”

Mtume Paulo alionyesha kuwa sio cheo, wala maono,wala karama wala sifa yoyote ile itokayo kwa Mungu au kwa mwanadamu ndiyo kiashiria cha mtu huyo kuwa analo daraja kubwa mbele za Mungu, na kwamba hakuna yeyote atakayeweza kuwa juu yake kisa tu kaitwa  na Mungu.. Ilifikia wakati Mtume Paulo kwa neema za Mungu alizopewa alijishuhudia katika Roho kuwa kati ya waliomtangulia hakuna aliyetenda kazi zaidi yake yeye. ( 1Wakorintho 15:10), Leo  tunaweza kujifunza machache juu ya matukio ya mitume yaliyorekodiwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume.

MATENDO YA MITUME:

Ndugu kitabu cha Matendo ya mitume, unajua ni kwanini kiliitwa vile?. Kilitwa vile kwasababu Ule ulikuwa ni uwanja wa mapambano katika roho kati ya mitume wa Kristo wote waliokuwepo kwa wakati ule, Kila mmoja akionyesha matendo ya Imani yake katika mashindano yaliyokuwa yamewekwa mbele yake.Lakini kama ukichunguza kwa makini utaona mwanzoni kabisa mwa sura za mwanzo za kitabu kile,

Ulikuwa unaweza kusoma habari za watu wengi na watakatifu wengi, na ushujaa wao wote waliokuwa wanaufanya, pamoja na habari za mitume mbalimbali wa Kristo, utaona kulikuwa na watu 500 waliotokewa na Kristo baada ya kufufuka kwake  kama alivyotokewa mtume Paulo,Ambao Bwana alifanya makusudi kujidhihirisha kwao ili wakawe mashuhuda wa kutangaza habari ya kufufuka kwake, utawaona pia wale watu 120 waliokuwako siku ile ya Pentekoste, utamwona Filipo,akitenda kazi ya Mungu kwa bidii, kadhalika utaona  habari ikirudi tena kwa Yohana, Utamwona Barnaba, utamwona Stephano, utamwona Petro, utawaona wakina Prisila na Akila, utamwona Anania, Apolo, utamwona nabii Agabo, Marko, Sila, luka, na wengineo.

Na kila mmoja ambaye habari zake zilisikika,  Mwandishi aliyevuviwa na Roho aliyekiandika  kitabu kile cha matendo ya mitume aliziweka habari zake, hakukuwa na upendeleo wowote. Na ndio maana ukichunguza mwanzoni walianza wengi kwa moto, habari za kila mmoja zikawa zinagusiwa, mara huyu, mara  Yule, lakini ukizidi kuendelea mbele kuanzia sura ya 13…mpaka ya mwisho kabisa wa sura ya 21 utaona ni Paulo tu peke yake ndiye anayezungumziwa kana kwamba hakukuwa na wengine wanaofanya ziara au wanaotenda kazi ya Mungu.

Sio kana kwamba hawakuwepo, walikuwepo, lakini aliyeonekena anapiga mbio zaidi ndio habari yake iliyopewa uzito mkubwa zaidi kuandikwa. Ni kama leo tu kwamfano  ukiangalia kwenye TV labla wanariadha wanaoshiriki katika michezo ya kukimbia umbali wa km 40, utaona kwa pale mwanzo  kamera haimlengi mtu Fulani mmoja maalumu, bali watu wote, kwasababu bado haijajulikana mshindi atakuwa ni nani, hivyo Yule anayeonekana inaongoza wenzake kamera itamchukua,

Kadhalika akipitwa tu kidogo kamera itahahamia kwa mwingine hivyo hivyo. Lakini ukiangalia wakishafika labda km ya 30 kuelekea 40 hapo wameshaachana nafasi kubwa sana, utaona kamera inamchukua tu Yule wa kwanza peke yake mpaka anapokwenda maliza. Kana kwamba ni yeye tu ndiye anayeshiriki michezoni lakini ukweli ni kwamba huko nyuma kuna umati wa mamia ya watu nao pia wanapiga mbio isipokuwa wameachwa nyuma sana.

Na ndivyo ilivyokuwa katika kitabu cha matendo ya mitume, Walianza wengi, lakini aliyemaliza ni mmoja. Naye si mwingine zaidi ya Mtume Paulo. Sio kana kwamba yeye alikuwa na kitu cha ziada sana zaidi ya wale wengine hapana, walikuwepo watu 500 waliotokewa na YESU kama yeye, na wengi wao walikuwepo siku ya Pentekoste na pengine hata kabla ya hapo, Bwana alitazamia na wao pia wapige mbio lakini kilichomtofautisha Mtume Paulo na wengine ni kwamba yeye alikuwa akimwomba Mungu neema na akionyesha bidii katika Bwana.

Lakini mambo hayo yanatufundisha nini?. Hayo yalitendeka katika kanisa la kwanza, lakini pia  lilikuwepo kanisa la pili na la tatu na la nne mpaka la mwisho la saba ambalo ndilo hili tunaloishi mimi na wewe, na kila kanisa linao mitume wake [watumishi wa Mungu],  nao pia kitabu cha matendo yao kinaandikwa mbinguni wanarekodiwa wanaopiga mbio,

Lakini swali je! Ni nani atakayemaliza na ushindi kwa Laodikia?.. Ni William seyomor, mwanzilishi wa kanisa la Pentekoste, ni Billy Granham? ni Oral Robert, ni WILLIAM BRANHAM mjumbe wa Kanisa la LAODIKIA? Ni TL Osborn Ni Hellen white? Ni Kulola, ni Kakobe, ni mchungaji wako, mwalimu wako wa madarasa ya jumapili? au ni WEWE?..

Hakika unaweza ukawa ni wewe.

Wote wanaodai walitokewa  na YESU na kupewa huduma kubwa wawe ni mamoja kwako, kwasababu wapo sio tu kutokewa , bali pia kuishi naye na kulala naye lakini bado walipitwa katika mbio, wanaodai wameonyeshwa maono makubwa sana watakuwa ni wainjilisti wa kimataifa wawe ni mamoja kwako, walio na sifa kubwa katika taifa na kanisa kuwa ni watumishi wa Mungu wawe ni mamoja kwako, wanaojulikana kuwa ni wajumbe wa makanisa na manabii wa vizazi wawe ni mamoja kwako Mungu hapokei uso wa mwanadamu.

Tujifunze kwa Mtume Paulo mtu ambaye hapo mwanzo aliuharibu uzima wake kuliko watu wote, lakini baada ya kutubu kwake alisimama na kuanza upya na kushinda kuliko wote  waliomtangulia yeye alisema maneno haya:

1Wakorintho 9: 23 “Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine. 

24 Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate. 

25 NA KILA ASHINDANAYE KATIKA MICHEZO HUJIZUIA KATIKA YOTE; BASI HAO HUFANYA HIVYO KUSUDI WAPOKEE TAJI IHARIBIKAYO; BALI SISI TUPOKEE TAJI ISIYOHARIBIKA. 

26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa; 

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Alisema pia..

2 Timotheo 2: 4 “Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari. 

5 HATA MTU AKISHINDANA KATIKA MACHEZO HAPEWI TAJI, ASIPOSHINDANA KWA HALALI. 

6 Yampasa mkulima mwenye taabu ya kazi kuwa wa kwanza wa kupata fungu la matunda. 

7 Yafahamu sana hayo nisemayo, kwa maana Bwana atakupa akili katika mambo yote.”

Je! Mambo ya dunia bado yanakusonga na huku bado unataka ufanikiwe zaidi ya hao mashujaa wa imani Hilo wingu kubwa la mashahidi lililotutangulia lililonenwa katika Waebrania 12 wanapaswa wawe mamoja kwetu?. Weka kando mizigo yote ya dhambi chini, tubu dhambi zako anza kumwangalia Bwana kwasababu ushindi hakika utaupata kama ukishindana kihalali.

Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu, 

2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.”

Ubarikiwe sana.

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

SIKU ZA MAPATILIZO.

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.

MARIAMU

Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?

JE! KUSHIRIKI AU KUJIHUSISHA KWENYE MICHEZO NI DHAMBI?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

JE! NI DHAMBI KWA KIJANA ALIYEOKOKA KUVAA SURUALI ZA KUBANA (MODEL), KUNYOA MITINDO?


Rudi Nyumbani

Print this post

JINA LAKO NI LA NANI?

Bwana Mungu alipowaumba Adamu na Hawa, tunafahamu hakuwaumba wote kwa wakati mmoja, bali alianza kumuumba Adamu kwanza kisha Hawa baadaye, Ndoa ya Adamu na Hawa  ndio ndoa ya kwanza  kabisa kufungishwa, na ilifungishwa na Mungu mwenyewe.

Lakini jambo la kujifunza mara tu baada ya mtu wa kwanza kuumbwa Bwana Mungu, alimpatia jina “Adamu” na baadaye alipomfanya Hawa kutoka katika ubavu wa Adamu hakumpatia jina lolote lile badala yake Adamu ndiye aliyekuja kumpatia jina mkewe na kumwita Hawa..kwasababu alisema yeye ndiye mama wa wote walio hai (Mwanzo 3:20), Lakini jina hilo Hawa halikutoka kwa Mungu bali kwa Adamu. Kwanini Mungu hakumpa Hawa jina hilo tutakuja kuona sababu tutakavyozidi kusoma.

Lakini hebu tutazame kwa ufupi nguvu iliyopo katika jina, katika maisha ya kawaida ukilitaja jina la Raisi wa nchi ni tofauti na jina la Waziri wa nchi, na ni tofauti na jina  la mbunge au balozi, kila jina lina nguvu yake na heshima yake. Jina lenye cheo kikubwa ndilo lenye  nguvu zaidi na heshima kubwa zaidi.

Barua ikiandikwa kwa jina la Raisi itaheshimika zaidi kuliko  ikiandikwa kwa jina la Balozi.  Kadhalika biashara yenye jina kubwa ni raisi kupata mapato mengi kuliko, yenye jina lisilojulikana, Kwahiyo unaweza ukaona kuwa jina la mtu au kitu au bidhaa linaweza likabeba nguvu kubwa sana ndani yake.

Sasa Bwana Mungu alimpatia jina mtu wa kwanza, akamwita ADAMU, jina hilo lilikuwa na nguvu ya kutosha na heshima ya kutosha ya kuweza kutiisha na kumiliki fahari  na milki zote za mwilini na za rohoni Bwana Mungu alizompa Mwanadamu. Na ndio maana tunaona mwanamke hakupewa jina lingine lolote na MUNGU,  lilikuwa ni jina moja tu walilopewa na Mungu Adamu na Mkewe, liwapasalo wao kufanyia mambo yote. Tunaweza tukasoma jambo hilo katika kitabu cha Mwanzo..

Mwanzo 5:1-2 “Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya; 

2 mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki AKAWAITA JINA LAO ADAMU, siku ile walipoumbwa.”

Unaona hapo? Akawaita jina lao ADAMU!!, hakumuita mwanamume peke yake ADAMU bali pia alimwita mwanamke ADAMU. Ikiwa na maana kuwa ni Jina moja tu walilopewa liwapasalo wao kutawala na kumiliki milki zote za ulimwengu huu. Heshima yao na nguvu yao ilikuwa ndani ya hilo jina.  Jina Hawa lilitoka kwa Adamu tu kama utambulisho kwa mkewe, lakini mbele za Mungu jina lao lilikuwa ni moja tu nalo ni ADAMU!

Lakini tunaona baada ya Adamu na mkewe kuasi kwa kutokutii maagizo ya Mungu, na kula matunda  waliyoagizwa wasiyale, heshima yao ilishuka, wakafukuzwa  kutoka katika ile bustani ya Edeni. Na hapo ndipo jina lao likashuka thamani. Nguvu ya lile jina ikashuka. Hata simba akawa hamwogopi tena mwanadamu, baadhi ya wanyama badala ya kumwogopa na kumkimbia mwanadamu, wakaanza kutafuta  kumla, ardhi badala imzalie Adamu na mkewe vyakula vizuri ikaanza kumzalia michongoma na miiba n.k

Hivyo Heshima ya mwanadamu ikapotea, na Bwana Mungu kwa kulijua hilo na kwa kumuhurumia mwanadamu, akamleta Adamu wa pili, ambaye angempa jina lisiloweza kuharibika, ili kwa jina hilo aweze kurudisha heshima na milki zote ambazo mwanadamu wa kwanza kazipoteza,

 Adamu huyu wa pili naye pia anaye mke wake aliyetwaliwa kutoka ubavuni mwake lakini mke wake sio wa mwilini bali wa rohoni.  Na Adamu huyu wa pili ni YESU KRISTO ambaye mkewe wake NI KANISA LAKE TEULE ALILOLITOA KUTOKA UBAVUNI MWAKE PALE KALVARI, walipomchoma mkuki ubavuni kulitoka MAJI na DAMU, ikifunua kuwa kanisa lake linazaliwa kwa DAMU YAKE iliyomwagika pale Kalvari na Linazaliwa kwa MAJI..Haleluya..

2Wakorintho 11: 1 “Laiti mngechukuliana nami katika upumbavu wangu kidogo! Naam, mchukuliane nami. 

2 Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; KWA KUWA NALIWAPOSEA MUME MMOJA, ILI NIMLETEE KRISTO BIKIRA SAFI. 

3 Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo”.

Unaona hapo? Na kama vile Mungu hakumpa mkewe Adamu jina lingine vivyo hivyo na Mke wa Bwana Yesu Kristo hakupewa jina lingine lolote isipokuwa jina la Yesu.

Matendo 4: 12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, KWA MAANA HAPANA JINA JINGINE CHINI YA MBINGU WALILOPEWA WANADAMU LITUPASALO SISI KUOKOLEWA KWALO”.

Hivyo jina la bibi-arusi(mke) wa Yesu Kristo linalojulikana mbinguni ni moja tu nalo si lingine zaidi ya YESU. Ndilo alilopewa na Baba,  Yohana 17: 6 “Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika”.

Ukisoma Yohana 1:25-26 utaona tena jambo hilo:

 “Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua; lakini mimi nalikujua, na hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma. Nami naliwajulisha JINA LAKO, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.”

Hivyo malaika au mapepo wakimwona bibi-arusi wa Kristo popote  pale ni sawa na wamemwona Yesu Kristo mwenyewe, Sasa Katika hilo Jina bibi-arusi wa Kristo anaokolewa,  hilo hilo anabatiziwa, anaponywa magonjwa yake, anafanya miujiza yote na zaidi ya yote amepewa mamlaka ya kufanya chochote  atakacho kwa jina hilo.

Wakolosai 3.17 “na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote KATIKA JINA LA BWANA YESU, MKIMSHUKURU MUNGU BABA KWA YEYE”.

SASA BIBI-ARUSI WA KRISTO NI NANI?

Bibiarusi wa Kristo ni mtu yeyote aliyemwamini na kumkubali Yesu Kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yake, aliyetubu dhambi zake zote kwa kumaanisha kuziacha, na kusafishwa kwa DAMU yake na kusafishwa kwa MAJI ambalo ni Neno lake, ambao ni UBATIZO wa Maji MENGI katika Jina LAKE, yule anayeishi maisha matakatifu na ya kujichunga wakati wote huyo ndiye bibi-arusi wa Bwana Yesu au mke wa mwanamkondoo.

Je! wewe ni bibi-arusi wa Kristo? Kumbuka huwezi ukamiliki chochote kama jina lako halijabadilishwa, je! mbinguni unajulikana kama nani? Adamu na Mkewe walijulikana kama ADAMU, Kadhalika Kristo na wateule wake wanajulikana kwa jina moja nalo ni Jina la Yesu, je! na wewe ni miongoni mwa kundi  lililobadilishwa jina na kupewa jina la Yesu?? kama hujazaliwa mara ya pili na kuwa bibi-arusi wa Kristo huwezi kuwa na jina hilo. Heshima yako katika ulimwengu wa roho bado haipo,hofu itakusumbua,  magonjwa yatakutesa, nguvu za giza zitakutesa, mauti itakuandama, na mambo yote mabaya yatakuwa sehemu yako. Kwasababu haupo chini ya Jina moja lililoadhimishwa na Mungu kwa ukombozi.

Wafilipi 2: 9 “Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, AKAMKIRIMIA JINA LILE LIPITALO KILA JINA;  ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;”

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.”

Ni maombi yangu kuwa huyu Bwana Yesu, asikupite leo hii, kama hujampokea Yeye umpokee leo, ayageuze maisha yako, na akuingize katika milki ya watu wa Mungu, na kwa jina lake akulinde, upate ushindi angali muda bado upo. Kwasababu jina hilo ni ngome IMARA. Kumbuka Jina la YESU linakaa ndani yako na sio ulimini mwako. Likiwepo humo basi lolote utakalolitamka kwa ulimi wako litafanikiwa sawa na mapenzi yake. Lakini ikiwa hautaokolewa au upo vuguvugu jina la YESU halina nguvu yoyote ndani yako.

Ubarikiwe sana.

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine na Mungu atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! MWANADAMU WA KWANZA KUUMBWA NI YUPI MZUNGU MWAFRIKA AU MCHINA?

NI RAHISI KWA NGAMIA KUPENYA KATIKA TUNDU LA SINDANO, JE! NI SINDANO IPI HIYO INAYOZUNGUMZIWA?

JE! MABALASI BWANA ALIYOYATUMIA KUGEUZIA MAJI KUWA DIVAI, YALITUMIKA TU KWA KAZI HIYO?

LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.

UKOMA NA UJANE ULIO NDANI YAKO, UMEUPATIA TIBA?

MKUMBUKE MKE WA LUTU


Rudi Nyumbani

Print this post

TUNAYE MWOMBEZI.

Maombolezo 3:22 Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.
23 NI MPYA KILA SIKU ASUBUHI; Uaminifu wako ni mkuu.
24 Bwana ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini.

Jina la Bwana na mwokozi wetu YESU KRISTO lihimidiwe milele. Leo ni siku mpya ambayo Bwana aliibuni tangu zamani kwa ajili yangu mimi na wewe ili tuiishi, tulipoamka asubuhi leo tumebahatika kupewa neema ya kusikia sauti nzuri ya milio ya ndege ikimsifu Mungu kwa furaha mitini, Tukikumbuka kuwa Leo tu ya tarehe hii yenyewe zaidi ya watu 151,600 watakufa ulimwenguni kote hiyo ni kulingana na takwimu za sensa ya dunia, lakini mimi na wewe Bwana ametukirimia neema zake za kipekee, sio tu kuamka salama bali pia kupata nafasi ya kufungua simu zetu na kuingia mitandaoni na kutazama yaliyojiri huko, mpaka unapokutana na ujumbe huu..

Unadhani utakuwa umefanya jambo gani jema mbele za Mungu mpaka uifikie siku ya leo?. Jaribu kufikiri juu ya hilo, je! Ni utakatifu wako?, je! Ni kwasababu unayo afya? Je! Ni kwasababu wewe ni kijana?.

Utagundua ni huruma tu za Bwana kwamba hatuangamii..Mungu anatuhurumia ndugu yangu, rehema zake ikishaitwa tu LEO asubuhi zinakuwa mpya tena kana kwamba hazikuwepo jana na juzi, zinakuwa mpya kama vile leo ndio mara ya kwanza kuachiliwa juu yetu..Mara nyingi tunamkosea Mungu wetu kwa namna zote lakini REHEMA zake ni nyingi kwa watu wote. Yaani Kwa waliookolewa na kwa wale ambao hawajaokolewa, wote rehema za Mungu zinakaa juu yako kwasababu yeye mwenyewe alisema anawaangazia jua na kuwanyeshea mvua yake wote waovu na wema.

Hivyo kwa sisi TULIOOKOLEWA pale tunapokaribia kuzama katika maji ya mauti kutokana na mapungufu yetu au madhaifu yetu na majaribu mazito hakika tunaye mwombezi wetu naye ni YESU KRISTO Bwana wetu, yeye pekee ndiyo hiyo hizo REHEMA YA MUNGU KWETU, na HURUMA yake Mungu kwetu. Biblia inasema katika

1Yohana 2:1 Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki…

Unaona yeye Bwana kila ikiitwa Leo anatupelekea dua zetu kwa Baba, hakika sifa na heshima na utukufu tunamrudishia yeye kwa upendeleo huu wa ajabu..Na kama sio yeye leo hii sisi tunaoitwa watakatifu tungeshaangamia siku nyingi. Siku ile tungewezaji kusimama kwa hoja yetu?. Hakika Wana AMANI tele wote walio katika Kristo YESU siku zote. Haleluya.

Lakini kwa ambaye hajaokolewa naye pia rehema za Mungu zipo juu yake: Lakini ni kwasababu gani haangamii?. Sio kwamba Bwana YESU yupo anamwombea juu mbinguni hapana?, yeye hilo halimuhusu kwasababu wakati Bwana angali akiwa hapa duniani hakudhubutu kufanya jambo kama hilo kwa yeyote Yule asiyeupande wake bali yeye mwenyewe alisema katika Yohana 17: 9 “Mimi nawaombea hao; SIUOMBEI ULIMWENGU; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako;”.

Unaona hapo mtu mwenye dhambi haombewi lolote na Bwana YESU, ni mtu aliye katika hukumu siku zote akisubiria siku ile kusimama mbele ya kiti cheupe cha enzi cha Mungu ahukumiwe kisha atupwe katika lile ziwa la moto, lakini kama ni hivyo basi ni kwanini haangamii?.Ni kwanini mpaka leo anaishi, anapumua, ana afya, anafanikiwa, angali YESU hamwombei juu mbinguni?. Ni kwanini mpaka leo shetani hatamwangamiza?

Ni kwasababu moja tu ambayo hiyo tunayoisoma katika,

Ezekieli 33: 11 Waambie, Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sikufurahii kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli?

Ezekieli 18: 23 Je! Mimi ninafurahia kufa kwake mtu mwovu? Asema Bwana MUNGU; si afadhali kwamba aghairi, na kuiacha njia yake, akaishi?

Unaona ni kwasababu gani huangamii ewe mtu mwovu?..Ni kwasababu Rehema za Bwana zimekushikilia mpaka sasa ili UTUBU. Unafahamu kabisa maisha unayoishi nje ya Kristo huna raha nayo,unastahili kwenda kuzimu, lakini bado unazidi kuishi hivyo!, unafahamu kabisa uzinzi na ukahaba unaoufanya utakupeleka jehanum lakini bado unazidi kudumu katika mambo kama hayo, unafahamu kabisa ukiwa nje ya YESU KRISTO hutaweza kusalimika, hutaweza kuikwepa hukumu ya Mungu, lakini ni kwanini unaendelea kufanya hivyo?. Idadi kubwa ya watu wanaokufa leo haumo katikati yao, unadhani hao waliokuwa na dhambi nyingi sana kuliko wewe?.

Siku ya leo ni mpya, rehema za Bwana zipo juu yako, zikikuvuta utubu, lakini usipofanya hivyo leo, ipo siku mauti itakukuta kwa ghafla na kule uendapo utaufichia wapi uso wako? utakuwa ukijutia siku zile zote neema ya Mungu ilipokuwa inakupigia kelele masikioni kila siku asubuhi utubu lakini hukutaka. Yatakuwa ni majuto makubwa kiasi gani?

Ndugu kwa haya maneno machache, ikiwa Kristo hayupo ndani yako leo, fanya uamuzi wako binafsi sasa. Unachopaswa kufanya ni wewe mwenyewe utubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kabisa kuziacha, uamue kabisa kuanzia sasa unaanza maisha mapya ndani ya Kristo YESU. Kumbuka toba ni kugeuka na sio kuongozwa sala Fulani tu. Wewe peke yako chukua uamuzi wa kugeuka hiyo ni bora zaidi ya sala yoyote unayoweza kuongozwa, na ikiwa toba yako imetoka moyoni kweli kweli na sio kidesturi za kidini au kimazoea. Basi uwe na uhakika Bwana amekusamehe.

Lakini hiyo peke yake haitoshi, Biblia inasema “aaminiye na KUBATIZWA ataokoka (Marko 16:16)”. Hivyo unaukamilisha wokovu wako kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na uwe katika jina la YESU KRISTO..hapo utakuwa na uhakika wa kupata ondoleo la dhambi zako, na kisha kuanzia huo wakati Bwana atakupa Roho wake MTAKATIFU akulinde mpaka siku ya ukombozi wa mwili wako, yaani unyakuo (Matendo 2:38).

Kumbuka ubatizo sahihi ni muhimu, ikiwa ulibatizwa ulipokuwa mchanga, au ulibatizwa kwa kunyunyiziwa maji, au ulibatizwa kidini tu, au kimazoea na haukutubia dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha siku ulipobatizwa, basi ni sharti ukabatizwe tena kwa ubatizo wa maji tele na kwa jina la YESU KRISTO, na sio kwa jina la Baba na mwana na Roho Mtakatifu kama inavyofanyika kimakosa kwa watu wengi, bali kwa jina lake Yesu Kristo ili upate ondoleo la dhambi zako, Hiyo ni kulingana na vifungu hivi vya maandiko (Mdo 2:38, mdo 8:16, ,mdo 10:48, na mdo 19:1-5).

Hivyo ukiwa utazingatia hayo yote, na kuyaishia maisha matakatifu Bwana akubariki kwa kuwa hapo utakuwa umezaliwa mara ya pili. Na ndio kuanzia huo wakati wewe nawe unakuwa na MWOMBEZI mbinguni, ambaye hapo kwanza haukuwa naye..Naye si mwingine zaidi ya BWANA YESU KRISTO kuhani wetu mkuu aliyetupatanisha sisi na Mungu kwa damu yake. Utukufu na heshima na enzi vina yeye milele na milele AMINA.

Ikiwa utatenda dhambi pasipo kujijua, au dhambi ya kutokukusudia au dhambi ya madhaifu yeye yupo siku zote kukuombea mbele za BABA, akulinde na Yule mwovu kwa Kuwa Kristo ameshakuwa mtetezi wako basi mbele za Mungu ukiwa chini hiyo neema hauhesabiwa kuwa na hatia makosa yako yanasitiriwa kwasababu rehema zake hazitakoma juu yako milele na milele. Na hatuhesabiwi haki kwa matendo ya sheria bali kwa Neema;

Ndio lile neno lililosemwa na manabii hapo linatimia..

Warumi 4:6 “uheri wake mtu yule ambaye Mungu amhesabia kuwa na haki pasipo matendo,

7 Heri waliosamehewa makosa yao, Na waliositiriwa dhambi zao.

8 Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi.”

Hivyo ubarikiwe wewe uliyechagua uamuzi huu bora wa kumwamini YESU KRISTO.

Tafadhali “share” habari hizi kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.

UZAO WA NYOKA.

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

JE! KUSHIRIKI AU KUJIHUSISHA KWENYE MICHEZO NI DHAMBI?

JE! NI DHAMBI KWA KIJANA ALIYEOKOKA KUVAA SURUALI ZA KUBANA (MODEL), KUNYOA MITINDO?

JE! MBINGUNI KUTAKUWA NA KULA NA KUNYWA?. KWANINI, TUIMBE, JE! KUNA ULAZIMA WOWOTE WA KUFANYA HIVYO?


Rudi Nyumbani

Print this post

MJUE SANA YESU KRISTO.

Moja ya jukumu la muhimu sana la kufanya baada ya kuzaliwa mara ya pili, ni kuzidi kumjua Yesu Kristo kwa undani, kwasababu Agano jipya lote linamuhusu Yesu Kristo, kiini chote cha biblia kinamuhusu Yesu Kristo, Agano la kale lilimuelezea Yesu Kristo kimafumbo lakini agano jipya limemwelezea kwa uwazi wote, Ukristo utakuwa haujakamalika kwa namna yoyote kama tutashindwa kumwelewa vizuri Yesu Kristo.

Tukishindwa kumwelewa Bwana Yesu , ni nani, kwanini alikuja duniani, anatendaje kazi, anataka nini kwetu, na sisi tunahitaji nini kutoka kwake, yuko wapi sasa hivi, anafanya nini n.k basi hatutaweza kumwelewa pia yule anayempinga yeye (Mpinga-Kristo) ni nani na anatoka wapi? Kadhalika Hatutaweza kujua mpinga-Kristo anatendaje kazi.

Kwasababu ni wazi kuwa huwezi kumjua adui ya mtu kabla hujamjua huyo mtu mwenyewe, hakuna mtu anayeweza kufahamu maadui wa mtu asiyemjua, sharti kwanza amjue huyo mtu anapotokea na maisha yake ndani nje yalivyo ndipo aweze kuwatambua na maadui zake. Vivyo hivyo hatutaweza kumjua Mpinga-Kristo kama hatutamjua Yesu Kristo vizuri kwa undani.

Miaka mingi, sana kabla ya mwanadamu wala wanyama kuumbwa, Bwana Mungu alikuwa peke yake, alikuwa hana cheo chochote kwasababu katika hali ya kawaida, ili mtu awe na cheo sharti awepo mtu aliye chini yake.

Sasa Mungu kabla ya kuumba wanadamu wala malaika, kulikuwa hakuna mtu chochote chini yake wala juu yake, hivyo alikuwa hana cheo chochote, alikuwa ni yeye kama yeye tu! na alikuwa pia hana jina, kwasababu jina kazi yake ni utambulisho kwa wasio kujua, hivyo yeye wakati huo alikuwa hana bado wasio mjua wala wanaomjua, hivyo alikuwa ni yeye kama yeye,Na ndio maana alimwambia Musa jina lake ni “MIMI NIKO AMBAYE NIKO”..sasa hilo sio jina kama ukilitafakari kwa makini, bali ni sentensi inayojaribu kuelezea uwepo wa Mungu. Hapo ni Bwana alikuwa akijaribu kumweleza Musa nafasi yake aliyokuwepo nayo kabla ya uumbaji wa kitu chochote kile.

Sasa ulipofika wakati wa uumbaji alipoanza kuumba malaika, ndipo hapo akaanza kuitwa Mungu, kwasababu maana ya Neno Mungu ni “mtengenezaji/au muumbaji” ndipo vikawepo viumbe chini yake vilivyoumbwa na yeye, viumbe hivyo vikaanza kumwita yeye Mungu, lakini kabla ya hapo alikuwa haitwi Mungu. Kwasababu hata katika maisha ya kawaida, Mtu hawezi akaitwa Baba kabla hajapata watoto, siku atakapopata watoto ndipo hapo atakapoitwa Baba au Mama, na ndivyo ilivyokuwa kwa Mungu hakuitwa Mungu, mpaka siku alipoumba.

Na ulipofika wakati wa mwanadamu kuumbwa, ambao aliwaita watoto wake, Cheo chake kilizidi kubadilika na Kuwa Baba, hivyo akawa na vyeo viwili yaani Baba pamoja na Mungu mwenyezi, kwasababu sisi wanadamu tuliomwamini yeye, Mbele za Mungu wetu ni kama watoto wake, Malaika sio watoto wa Mungu, bali sisi wanadamu ndio tunaoitwa watoto wa Mungu..

Waebrania 1:5 “Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?” .

Hivyo ulipofika wakati wa Yeye kujidhihirisha kama Baba ni pale alipowatoa wana wa Israeli kutoka Misri akafunua jina lake kama YEHOVA,(Kutoka 6:1-6) Kwahiyo jina la Baba likawa ni YEHOVA, lakini ndio yule yule Mungu mwenyezi na ndio yule yule Baba Yetu. Aliwaokoa wana wa Israeli kama watoto wake kutoka katika mikono ya Farao kwa jina lake Yehova.

Kutoka 4:22 “Nawe umwambie Farao, Bwana asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu; nami nimekuambia, MPE MWANANGU RUHUSA AENDE, ili apate kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako”.

Hosea 11: 1 “Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, NIKAMWITA MWANANGU ATOKE MISRI”.

Unaona Sasa kwasababu Israeli ni Mzaliwa wa Kwanza, ni lazima awepo mzaliwa wa pili, na huyo sio mwingine zaidi ya watu wa mataifa, Hivyo watu wa Mataifa nao pia waliingizwa katika neema hii ya kuitwa wana wa Mungu..

Warumi 9:23 “tena, ili audhihirishe wingi wa utukufu wake katika vile vyombo vya rehema, alivyovitengeneza tangu zamani vipate utukufu;

24 ndio sisi aliotuita, si watu wa Wayahudi tu, ILA NA WATU WA MATAIFA PIA?

25 Ni kama vile alivyosema katika Hosea, Nitawaita watu wangu wale wasiokuwa watu wangu, Na mpenzi wangu yeye asiyekuwa mpenzi wangu.

26 Tena itakuwa mahali pale walipoambiwa, NINYI SI WATU WANGU, HAPO WATAITWA WANA WA MUNGU ALIYE HAI”.

Lakini kama tunavyojua agano la kwanza halikuweza kumkamilisha mwana wa kwanza (wana wa Israeli) kuwa mkamilifu, kadhalika lisingeweza pia kumkamilisha mwana wa pili (yaani watu wa mataifa) kuwa wakamilifu, hivyo Bwana Mungu mwenyezi akatengeneza njia nyingine ya kuwakamilisha wana wake wote wawili (yaani wayahudi na watu wa mataifa), ambayo katika hiyo watakuwa wakamilifu kweli kweli…. Na ndio hapo akauvaa mwili yeye mwenyewe YEHOVA na kuwa mwanadamu, ili kuwa kipatanishi kati ya wanadamu na nafsi yake mwenyewe.


Akauvaa mwili akazaliwa kama mwanadamu, akatembea kama mwanadamu akaishi kama mwanadamu, akajinyenyekeza kama mwanadamu, hakufanya vile kwa wazi bali alifanya kama siri mpaka utakapofika wakati wa kufunuliwa kwa siri hiyo, kwamba Yesu Kristo alikuwa ni Yehova mwenyewe katika mwili wa kibinadamu, na ndio maana Malaika Gabrieli alimwambia Bikira Mariamu amwite jina lake YESU, sasa tafsiri ya jina Yesu kwa kiebrania ni YEHOVA-MWOKOZI, kwahiyo ni yule yule YEHOVA KATIKA MWILI WA KIBINADAMU, Isipokuwa Jina lake limeongezeka na kuwa YEHOVA-MWOKOZI hivyo amekuja kwa kuokoa. Siri hiyo hawakufunuliwa watu wote isipokuwa wale ambao Bwana alipenda kuwafunulia. Na ndio maana Mtume Paulo aliileza siri hiyo kwa ujasiri katika..

1 Timotheo 3: 16 “Na bila shaka SIRI YA UTAUWA NI KUU. Mungu alidhihirishwa KATIKA MWILI, Akajulika kuwa na HAKI KATIKA ROHO, Akaonekana na malaika, AKAHUBIRIWA KATIKA MATAIFA, AKAAMINIWA KATIKA ULIMWENGU, AKACHUKULIWA JUU katika utukufu”.

Unaona hapo Mtume Paulo anamzungumzia Yesu Kristo, Mungu katika mwili, lakini anasema ni SIRI?

Sasa unaweza ukajiuliza kama Yesu alikuwa ni Mungu katika mwili kwanini aliruhusu watu wamwite yeye mwana wa Mungu? au aruhusu kujulikana kama mwana wa Adamu? Au mwana wa Daudi?.

Bwana Mungu, alipouvaa mwili wa kibinadamu, alijishusha kuwa mdogo sana, sasa mtu hawezi kujishusha na kuwa mdogo na bado atafute kuitwa mkubwa, bila shaka atakuwa ni mnafki. Ndio maana aliwaambia wanafunzi wake, mimi mnaniita Bwana na ndivyo nilivyo lakini sikuja kutumikiwa bali kutumika, na akawaambia mtu akitaka kuwa mkubwa kuliko wote basi awe mtumishi wa wote, hivyo yeye alikuwa kielelezo namba moja cha maneno hayo,

Ili kuelewa vizuri hebu jaribu kutafakari mfano huu, kulikuwa na tajiri mmoja mwenye mali nyingi sana, na mwenye makampuni mengi na wafanya kazi wengi sana, na wengi wa wafanyakazi wake walikuwa hata hawamjui kwa sura kutokana na ukuu wake, wengi walikuwa wanamsikia tu, lakini yule tajiri akaona kuna kasoro Fulani katika moja ya makampuni yake yaliyopo katika moja ya majimbo yake, akasikia kwamba kwenye moja ya hilo kampuni lake, wafanya kazi wananyanyaswa hawalipwi mishahara yao kwa wakati, na kuna ubadhilifu wa fedha mahali Fulani, sasa yule tajiri akaona njia pekee ya kwenda kutafuta suluhisho la hilo tatizo na kujua ukweli wa Mambo sio tu kutuma mawakili wake, bali akaona njia pekee ni kujibadilisha na kutoka kwenye ukurugenzi wake, na kusafiri mpaka kwenye hiyo nchi ambapo kampuni lake lipo na kwenda kujifanya kama nayeye anatafuta ajira ndani ya hilo kampuni, na akishapata naye awe kama mmoja wa watumwa wadogo wa lile kampuni walioajiriwa,..

Sasa kwasababu yeye yupo pale sio kwa kutafuta ukubwa bali kwa kutafuta chanzo cha tatizo, hivyo hawezi kuanza kujitangaza kwamba yeye ndiye Mmiliki wa lile kampuni, hapana bali atafanya mambo yake kwa siri siri, atajifanya mtumwa, na zaidi ya yote, atazitii zile sheria ambazo yeye ndiye aliyezipitisha katika enzi zake, kama vile sio yeye aliyezipitisha, atakipa heshima kile cheo cha mkuu wa makampuni kama vile sio chake, mpaka utakapofika wakati wa yeye kuondoka labda ndio atawaambia moja wa wafanyakazi wake kwamba YEYE NDIYE MKUU WA MAKAMPUNI YALE. Hapo ni baada ya kile alichokuwa anakitafuta kukipata.

Na ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu Kristo, yeye alikuwa ni Mungu katika mwili, isipokuwa katika SIRI asingeweza kujiita Mungu kwa namna yeyote ile, alikubali kuitwa mnazareti, alikubali kuitwa mwana wa Mungu, alikubali kuitwa mwana wa Yusufu, alikubali kuitwa mwana wa Daudi , n.k ingawa yeye hakuwa mwana wa Yusufu wala mwana wa Daudi.. kwasababu yeye mwenyewe mahali Fulani aliwauliza mafarisayo…

Mathayo 22:41 “Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo?

42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.

43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema,

44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?

45 Basi, DAUDI AKIMWITA BWANA, AMEKUWAJE NI MWANAWE?

46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena.”

Unaona hapo Bwana anawauliza mafarisayo kama yeye ni mwana wa Daudi, inakuwaje tena Daudi anamwita Kristo Bwana? Kwahiyo unaweza ukaona Bwana Yesu Kristo, kujidhihirisha kama mwanadamu, au kama mwana wa Mungu, au kama mwana wa Yusufu haimaanishi kwamba yeye ni mwanadamu au yeye ni mtoto kweli wa Daudi au yeye ni mtoto kweli wa Yusufu, au yeye ni wa ulimwengu huu.

Hivyo Baada ya Mungu kumaliza kazi ya upatanisho kwa njia ya msalaba pale Kalvari, alirudi katika enzi yake kama Mungu Mkuu, lakini akaituma Roho yake kama Roho Mtakatifu, ambaye ndio yeye mwenyewe lakini katika mfumo wa Roho, kwa namna ya kawaida huwezi kumtenganisha Mtu na Roho yake, mahali mtu alipo ndipo na Roho yake ilipo, huwezi ukasema mtu na Roho ni vitu viwili tofauti hapana ni kitu kimoja, na ndivyo ilivyo kwa Mungu wetu, ni yeye yule aliyekuwa kama Baba mbinguni, kisha akajidhihirisha kama mwana duniani, na sasa yupo pamoja nasi kama Roho Mtakatifu.

Na jina lake ni lake ni YESU KRISTO (YAANI YEHOVA-MWOKOZI). Ana nafsi moja tu, Na hatujapewa jina lingine litupasalo sisi kuokolewa kwalo isipokuwa jina lake YESU KRISTO, kwa jina hilo tunapata msamaha wa dhambi, na kufunguliwa vifungo vyetu, kwa jina hilo tunabatiziwa, kwa jina hilo tunatolea pepo, kwa jina hilo la Yesu tunatenda mambo yote ya mwilini na rohoni. Na wala hapana wokovu kwa mwingine yoyote isipokuwa kwa Mungu wetu (YESU KRISTO, MUNGU MKUU BWANA WA UTUKUFU).

Kwahiyo Mtu akimkataa Yesu Kristo, amemkataa Mungu mwenyewe, mtu akimpinga Yesu Kristo amempinga Mungu mwenyewe.

Kaka/Dada leo hii umefahamu kuwa Yesu ndiye Mungu, mtazamo wako juu yake upoje? Yeye ndiye atakayeketi katika kiti chake cha enzi na kuhukumu mataifa yote. Jifunze sana kumjua huyu kwasababu yeye ndio Njia pekee ya kuufikia uzima wa milele sio kuwa na dini wala dhehebu au kujiunga na mojawapo ya hayo, njia pekee ya kuupata uzima wa milele ni kumwamini yeye na kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi na maisha ya kale, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina lake hilo “Yesu Kristo” kulingana na ( Matendo 2:38. Mdo 8:16, mdo 19:5 na Mdo 10:45) Na Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu. Ni maombi yangu kwamba Bwana atakukirimia neema yake kuyapata hayo na kuzidi kumfahamu sana yeye..

Waefeso 4: 13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;

14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.

15 Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo”.

Ubarikiwe!

Tafadhali “share ” ujumbe huu kwa wengine.

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

TUZIJARIBU HIZI ROHO.

MAISHA YETU NI MILKI YA YESU KRISTO.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

UMEPATA UHAKIKA WA KUTOKUINGIA HUKUMUNI KATIKA SIKU ILE?

JE! ADAMU ALIWASALIANA NA MUNGU KWA LUGHA IPI PALE BUSTANINI?

JE! KUCHORA TATTOO NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani

Print this post

DALILI ZIPI ZITAMTAMBULISHA MTU KUWA AMEFANYIKA KIUMBE KIPYA?

Mtu anapozaliwa mara ya pili, siku hiyo hiyo anafanyika kuwa kiumbe kipya, na mtu aliyezaliwa mara ya pili ni lazima awe ametubu dhambi zake kwanza kwa kumaanisha kuziacha kabisa, kisha akabatizwe kwa maji na kwa Roho. (Yohana 3:1-5), Ndipo awe na uhakika kuwa amezaliwa mara ya pili na kafanyika kiumbe kipya.

Lakini hiyo peke yake haitoshi kukupa uhakika huo kwasababu biblia pia inasema katika Yakobo 2:17 “Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake…haizai” 

Hii ikiwa na maana kuwa siku ile unapofanyika kuwa kiumbe kipya ni lazima matendo yaambatanayo na huko kuwa kiumbe kipya yajidhihirishe ndani yako.

Wapo watu wanaodhani mioyoni mwao kuwa siku ile walipotubu na kubatizwa katika ubatizo sahihi ilitosha wao kukubaliwa na Mungu na huku wakiendelea kuishi katika maisha yao ya kale. Kumbuka ndugu nyakati hizi za mwisho biblia ilishatabiri kutakuwa na makundi mawili ya waaminio, Ukisoma katika Mathayo 25 utaona habari ya wale wanawali 10, ambao wote walikuwa kweli ni mabikra, na wote walikuwa wanamngojea Bwana arusi aje kuwachukua waende pamoja Arusini, lakini tofuati yao ilikuwa ni kwamba watano walikuwa ni werevu na watano wao walikuwa wapumbavu.

Wale warevu walibeba mafuta ya ziada katika katika vyombo vya pembeni pamoja na taa zao, lakini wale wapumbavu hawakubeba mafuta ya ziada isipokuwa yale tu yaliyokuwa katika taa zao. Na Bwana arusi alipokuja usiku wa manane wale wapumbavu taa zao zilikuwa zinakaribia kuzima, hivyo ikiwalazimu waende kutafuta mafuta ili waweze kwenda kumlaki Bwana arusi, lakini waliporudi wakakuta wenzao wameshaingia karamuni na mlango umefungwa.

Mfano huo unaonyesha aina mbili za wakristo watakaokuwepo katika siku hizi za mwisho, angali sisi sote tukifahamu kuwa unyakuo upo karibuni kutokea siku yoyote, lakini ni wazi kuwa wapo watakaoenda na Bwana na wapo watakaoachwa. Kumbuka hapo wote ni wakristo [wanawali] wote walizaliwa mara ya pili, lakini wapo waliodumisha mafuta ya Roho mtakatifu ndani yao na wapo ambao waliyazimisha.. Na hawa walioyazimisha ndio watakaoachwa na watakaopitia dhiki kuu ya mpinga-Kristo siku ile ikifika.

Mtu unapokuwa kiumbe KIPYA. Ni lazima uwe MPYA kweli kweli kama neno lenyewe linavyosema KIUMBE KIPYA. Kuanzia huo wakati ulipotubu na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la YESU KRISTO na kupokea Roho Mtakatifu wa Mungu ndani yako, safari ndio inaanza na sio imeisha.  

kuanzia huo wakati ni kuanza maisha yako UPYA tena, yaani kuyasahau (kuyaaga) mambo yote ya nyuma uliyokuwa unayafanya na kuyatenda na kumwishia Kristo siku za maisha yako yaliyobaka hapa duniani, ulikuwa ni mwasherati ulikuwa ni mtukanaji, ulikuwa ni mwizi, ulikuwa unakwenda disco, ulikuwa unatazama Pornography, ulikuwa unafanya mustarbation, ulikuwa unasengenya, ulikuwa ni mla rushwa, ulikuwa ni mshirikina, ulikuwa ni mvaaji vimini na suruali, ulikuwa ni mtembeaji uchi, ulikuwa ni mwabudu sanamu, ulikuwa unasikiliza miziki ya kidunia, n.k.. Kuanzia huo wakati na kuendelea ni kuyasahau na kukaa nayo mbali, sasa hiyo ndiyo dalili itakayokuthibitisha kuwa kweli wewe umefanyika kiumbe kipya.

Lazima ufikie hatua inayokuonyesha kuwa jana yako ni tofuati na leo yako.

Neno la Mungu linasema

2Wakorintho 5:17 Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; YA KALE YAMEPITA TAZAMA! YAMEKUWA MAPYA.

Unaona hapo je! ya kale yako yamepita? Mtume Paulo kabla ya kuokolewa kwake alikuwa ni mwuaji, mtukanaji, mpinga-kristo,n.k. lakini baada ya kuzaliwa mara ya pili na kufanyika kiumbe kipya alisema maneno haya..

Wafilipi 3:11 “ili nipate kwa njia yo yote kuifikia kiyama ya wafu.

12 Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu.

13 Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ILA NATENDA NENO MOJA TU; NIKIYASAHAU YALIYO NYUMA, NIKIYACHUCHUMILIA YALIYO MBELE;

14 nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu”.

Unaona Imani ni lazima iambatane na matendo yake, unasema umekuwa kiumbe KIPYA je! Yale ya kale bado yapo ndani yako? Huo upya ulio nafsini mwako upo wapi Kama bado kuupenda ulimwengu kuko ndani yako?. Bwana YESU akirudi leo kulichukua kanisa lake, kuwachukua wale wanawali werevu na wewe utakuwa mmoja wapo?.

Utajisikiaje siku hiyo, utakapoona umeachwa na mkristo mwenzako uliyekuwa unamwona kila siku ambaye yeye alijikana nafsi yake ameenda na Bwana katika utukufu milele na wewe umebakia hapa chini?. Ni hali mbaya sana ambayo hakuna mtu yeyote atatamani aipitie.

Lile neno linalosema kutakuwa na kilio na kusaga meno, halitakuwa kwa mtu asiyemjua Kristo, hapana yao itakuja huko baadaye, lakini zaidi litakuwa kwa Yule mkristo aliyejidhania kuwa angekwenda kwenye unyakuo lakini badala yake ameachwa.

Na alibaki kwasababu gani?. Ni kwasababu hajakamilishwa katika wokovu wake, aliiishi mguu mmoja nje, mwingine ndani, leo wa Mungu kesho wa ulimwengu huu, Anasema amezaliwa mara ya pili lakini bado hataki kuacha baadhi ya mambo ya kidunia,Ni heri kuwa moto au baridi kuliko kuwa vuguvugu biblia inasema hivyo.

Kama yanavyosema maandiko: Mungu hadhihakiwi, apandacho mtu ndicho atakachovuna. Ni maombi yangu sisi sote (mimi na wewe) tusiwe katika hilo kundi kubwa la wanawali wapumbavu ambalo limeenea katika ukristo wa sasa. Badala yake tuwe miongoni wa wale wanawali werevu, tukiwa na mafuta ya ziada katika chupa chetu ili taa zetu zisizime wakati wowote hata Bwana ajapo.

Tufanyike viumbe vipya kweli kweli kila siku, yale tuliyoyaacha baada ya kutubu na kubatizwe tusitamani yaingie akilini mwetu hata kidogo. Tuishindanie Imani tuliyopewa mara moja tu na Bwana wetu, Tuishindanie hiyo hata ajapo. Naye atatupa TAJI YA UZIMA.

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

18 Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho.”

DUNIA INAPITA NA MAMBO YAKE.

AMEN.

Tafadhali sambaza ujumbe huu wa Mungu kwa ndugu zako nao wapone, na Bwana atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.

MNARA WA BABELI

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “HERI WALIOTASA, NA MATUMBO YASIYOZAA, NA MAZIWA YASIYONYONYESHA”?

NIFANYAJE ILI NI NIJUE KUWA UAMUZI NINAOUFANYA NI MAPENZI YA MUNGU?


Rudi Nyumbani

Print this post

TAWI LIZAALO HULISAFISHA ILI LIZIDI KUZAA.

Yohana 15.1 “Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.

 2 KILA TAWI NDANI YANGU LISILOZAA HULIONDOA; NA KILA TAWI LIZAALO HULISAFISHA, ILI LIZIDI KUZAA 

3 Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia.

 4 Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.

 5 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote. 

6 Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea.

 7 Ninyi mkikaa ndani yangu,”.

Kama wewe ni mkulima, au kama ulishawahi kujihusisha na shughuli yeyote ya kilimo, unaweza ukaelewa kwa undani uhusiano uliopo kati ya shina, matawi na matunda, utagundua kwamba mti hauwezi kuzaa matunda pasipokuwepo na shina, na kama shina halina matawi basi pia haliwezi kuzaa matunda. Kwahiyo ili matunda yawepo ni lazima liwepo shina pamoja na matawi.

Biblia inasema Bwana wetu Yesu Kristo ni mzabibu (shina), na Baba yake ndiye mkulima, na sisi ndio watu wake ndio matawi, kila tawi lisilozaa huliondoa na kila tawi lizaalo hulisafisha ili lizidi kuzaa.

Sentensi hii inaonyesha wazi kabisa huyu mkulima, yupo kwaajili ya kutafuta faida, yaani kupata matunda, utagundua kuwa sio mkulima wa kupanda tu na kuondoka bali utagundua ni mkulima ambaye yupo kimaslahi zaidi, na anafanya juu chini kuhakikisha anapata anachokitafuta.

Sasa ili kupata anachokitafuta ndio hapo tunaona anauchunguza mti wake siku baada ya siku kutafuta matawi yanayozaa ili aendelee kuyasafisha na yale yasiyozaa ayaondoe, na utaona hashughuliki na shina (yaani Yesu Kristo) bali utaona anashughulika na matawi (yaani wafuasi wa Yesu Kristo).

Sasa kama wewe ni mkulima utagundua kuwa ili kuufanya mti usiendelee kuwa mrefu kwenda juu huwa wanakata lile tawi la juu kabisa linalokua kwenda juu, na matokeo yake ni kwamba ule mti utaendelea kutanuka badala ya kuendelea kwenda juu, vivyo hivyo watu wakitaka mti uzidi kuwa mrefu kwenda juu, huwa wanaondoa yale matawi ya pembeni, na matokeo yake ule mti utaendelea kwenda juu sana lakini hautataanuka.

Kwanini wanafanya hivyo?..Ni kwasababu endapo yale matawi ya pembeni yakiachwa na kuendelea kuwepo ule mti hautaendelea kukua kwenda juu kwasababu nguvu yote au chakula chote cha ule mti kitaenda kwenye yale matawi yaliyopo pembeni na hivyo kudhoofisha ukuaji wa matawi ya juu, na vivyo hivyo kama wanataka mti upanuke kwa mapana, wanapaswa waondoe matawi ya juu ili chakula chote kisiende kwenye yale matawi yaliyopo juu na badala yake kiende kwenye yale matawi ya pembeni ili utanuke kwa kasi.

Kadhalika wakulima wa mazao ya biashara kama kahawa wanaelewa kwamba, wakitaka mmea kama mti wa kahawa uzae sana, huwa  wanakwenda kukata kile kikonyo cha juu kabisa cha mti wa mkahawa, ili usiendelee kwenda juu, na pia wanaondoa yale matawi madogo madogo ambayo yameota kwenye shina, ambayo hayazai, na kuacha yale matawi yenye matunda tu, na lengo la wao kufanya hivyo sio kwasababu hawapendi ule mkahawa uwe na matawi mengi, hapana! Bali wanajua endapo wakiyaacha yale matawi madogo yasiyozaa yaendelee kuwepo basi kuna hatari ya kuvuna kahawa chache kwasababu nguvu yote ya chakula badala iende kwenye yale matawi yanayozaa, inaishia kwenda kwenye yale matawi madogo madogo yasiyozaa, hivyo kusababisha matunda hafifu kutoka kwenye yale matawi makubwa yanayozaa. Hivyo utamkuta mkulima amekata matawi yote madogo madogo kama ni 20 au mia na kubakiwa tu na matawi matano au kumi makubwa yanayozaa.

Sasa hiyo hatua yote ya kupunguza matawi yasiyozaa ndiyo inayoitwa KUUSAFISHA MTI. Unaweza kutazama mfano wa picha chini.

Sasa tukirudi kwenye ule mfano Bwana Yesu aliosema kwamba kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa na lile lizaalo hulisafisha alikuwa ana maana kuwa, Kila mtu aliyekuwa ndani yake yeye asiyeonyesha dalili yote ya kuzaa matunda, Baba yake atamwondoa na sababu ya kumwondoa sio kwasababu anamchukia au hapendi awepo ndani ya Yesu Kristo, hapana!  Sababu pekee ya kumwondoa ni kwasababu ile nguvu au kile chakula ambacho kinatumika kwa mtu asiyezaa matunda kingeweza kutumika kwa mtu anayezaa matunda ili azae mengi zaidi na zaidi. Na ndio maana mahali pengine Bwana Yesu alisema..

Mathayo 25.29 “Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa”.

Nilikutana na ndugu mmoja mwislamu wakati Fulani, nikamwambia Bwana Yesu alisema kuwa mwenye kitu atapewa lakini asiye na kitu atanyang’anywa hata kile alicho nacho, Yule ndugu alihuzunika sana kusikia ile sentensi, alisema kwanini iwe hivyo, sio vizuri? Ina maana kwamba Yesu hana upendo kwanini amnyang’anye Yule asiyekuwa nacho hata kile kidogo alichokuwa nacho?. Nikajaribu kumweleza kuwa Bwana Yesu hazungumzii mambo haya ya  mwilini bali ya rohoni lakini bado alihuzunika. hivyo ndivyo ilivyo kwamba Bwana yupo kwa ajili ya faida, anachotaka kutoka kwetu ni matunda, sio nyuso zetu!! Na tutakuja kuyaona hayo matunda ni yapi muda mfupi baadaye.

Kwahiyo utaona kuwa, kuna hatari kubwa sana ya kutokuzaa matunda, hatari hiyo ni kwamba ile Neema na Baraka za Mungu juu yako za kumzalia Mungu matunda zinaondolewa kwako na kupewa mtu mwingine anayezaa, ndio hapo utakuta mwanzoni ulikuwa una hamu sana ya kumtafuta Mungu ghafla ile hamu inakufa, anaenda kuongezewa Yule mtu ambaye alikuwa anaonyesha bidii kidogo, anaongezewa nguvu mara mbili zaidi ya kumtafuta Mungu, utaanza kuona ile nguvu ya kuomba ambayo ilikuwa ndani yako ulikuwa una uwezo wa kuomba hata nusu saa, ghafla unajikuta hamu yote ya kuomba imekufa unaacha anaenda kuongezewa Yule ambaye kwa unyoofu wa moyo kila siku anajitahidi angalau aombe nusu saa, anaongezewa nguvu anaanza kuomba lisaa, masaa au hata mkesha, ukiona umepoa ghafla  fahamu tu kuwa umeondolewa kutoka katika lile shina, au upo hatarini kuondolewa.

Sasa ni Matunda yapi Bwana anayoyahitaji kutoka kwenye mashina (yaani mimi na wewe)?

Matunda ambayo Bwana anayahitaji yanatoka katika kitabu cha

Wagalatia 5:22 “Lakini TUNDA LA ROHO ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.”

Unaona hayo ndio matunda Bwana anayoyahitaji kutoka kwetu, anategemea katika kipindi chote tunachokaa ndani yake yeye kama mzabibu mkuu, anategemea kutuona tunazaa, upendo ndani yetu, tunazaa fadhili, tunazaa utu wema, tunazaa upole, tunazaa kuwa na kiasi na uvumilivu, tunazaa amani..hata baadaye tuwahubirie wengine habari njema za wokovu.

Lakini atakapokuja na kutukuta hatuzai hayo matunda ya haki badala yake  tunazaa, kutokusamehe, tunazaa wivu, tunazaa uasherati, tunazaa matusi, tunazaa kutokujiheshimu, tunazaa kiburi, tunazaa kuupenda ulimwengu kuliko kumpenda Mungu, na bado tunasema sisi ni wakristo tupo ndani yake, bado tunasema sisi ni matawi yake, nataka nikwambie ndugu Kristo hana matawi ya namna hiyo, hii Neema iliyopo na wewe leo inayokulilia ugeuke utubu ili uzae matunda ya haki, itaondolewa kwako na kupewa watu wengine waliostahili. Ndivyo biblia inavyosema..

Mathayo 3.8 “Basi, toeni matunda yapatanayo na toba; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumwinulia Ibrahimu watoto. 

9 Na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa PENYE MASHINA YA MITI; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”

Na pia inasema “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao HAPANA MTU ATAKAYEMWONA BWANA ASIPOKUWA NAO; Waebrani 12:14”

Itii sauti ya Roho wa Mungu leo inayokuambia utubu uache dhambi zako na umgeukie Muumba wako leo kwa moyo wako wote! Itafika wakati hutaisikia tena ndani yako,siku hiyo injili kwako itakuwa ni kama upuuzi tu!.. Hujawahi kukutana na mtu hata umwelezeje hataki kusikiliza injili?? itii sauti ya Mungu inayokuambia leo, uache uasherati!, Uache uvaaji mbaya kama wanawake wa ulimwengu huu wasiomjua Mungu, uache sigara na pombe!, uache usengenyaji Mtii Mungu leo, kisije hicho kidogo alichowekeza ndani yako akakiondoa na kumpa mwingine, acha kudanganyika kwamba utatubu tu siku moja!! Hakuna kitu kama hicho hiyo ni sauti ya shetani mwenyewe ikizungumza ndani yako. Na acha kuamini injili za kwamba Mungu ni upendo tu! Mungu ni upendo tu! Hawezi kutufanya chochote…Yeye mwenyewe kasema mara kadhaa na sio sehemu moja kwamba “yeye asiye nacho hata kile kidogo alicho nacho atanyang’anywa” ikiwa na maana kwamba hatakuachia hata hicho kimoja ulicho nacho..

Mathayo 25: 28 “BASI, MNYANG’ANYENI TALANTA HIYO, MPENI YULE ALIYE NAZO TALANTA KUMI. 

29 Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa”.

Je! Sentensi hiyo haikuogopeshi?? Tubu leo ukabatizwe upokee kipawa cha Roho Mtakatifu. Ili ufanyike Tawi lizaalo.

Bwana akubariki.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa ndugu zako wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

VIUMBE VINATAZAMIAJE KUFUNULIWA KWA WANA WA MUNGU?

NINI MAANA YA MSIMWITE MTU BABA DUNIANI?

KAINI ALIPATIA WAPI MKE?


Rudi Nyumbani

Print this post

NGUVU YA MUNGU YA UUMBAJI

Katika kitabu cha mwanzo tunasoma, baada ya Bwana Mungu kuumba mbingu na nchi na viumbe vyote alistarehe siku ya saba, biblia inasema hivyo katika..

Mwanzo 2: 1 “Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote.

2 Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya.

3 Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.

4 HIVYO NDIVYO VIZAZI VYA MBINGU NA NCHI ZILIPOUMBWA. Siku ile Bwana Mungu alipoziumba mbingu na nchi”.

Lakini kuna mambo kadhaa ya kujiuliza kuhusu uumbaji wa Mungu, Jambo la kwanza la kujiuliza ni kwanini Mungu hakuumba vitu vyote ndani ya dakika moja? Maana anao huo uwezo na badala yake akachukua siku saba kukamilisha uumbaji wake?

Swali la pili la kujiuliza, Ni hapo aliposema… “HIVYO NDIVYO VIZAZI VYA MBINGU NA NCHI ZILIPOUMBWA” Hivyo vizazi vilivyoumbwa ni vipi?

Na yapo maswali mengine mengi sana ya kujiuliza juu ya kitabu cha mwanzo, lakini leo tuyatazame haya mawili kwa msaada ya Bwana. Kwasababu tukiweza kumwelewa Mungu katika uumbaji wake tutaweza kumwelewa Mungu katika uumbaji wake anaotufanyia sisi kila siku katika maisha yetu, kwasababu Mungu ni yeye yule  jana, leo na hata milele hatabadilika. Njia alizozitumia kuumba mwanzo ndizo hizo hizo zinazoendelea leo katika uumbaji na utengenezaji wa maisha yetu.

Ni wazi kuwa Mungu anao uwezo wa kuumba kitu kufumba na kufumbua lakini, tunaona hakuutumia huo uwezo wake katika uumbaji wa Mbingu na nchi pamoja na uumbaji wa wanadamu na viumbe.. Hakuiumba dunia kufumba na kufumbua, bali ilimchukua muda kidogo katika utengenezaji, kwanini alifanya hivyo..kwasababu ndivyo ilivyompendeza.

Kwahiyo tunaweza kujifunza kuwa sio mpango wa Mungu, mambo kuzuka haraka haraka, sio mpango wa Mungu kwamba jambo ameliahidi leo na leo leo litimie kama lilivyo, ingawa huo uwezo anao, lakini hautumii sana na ndio maana tunasoma pale mwanzo baada ya Bwana Mungu kuiumba dunia, hakuiumba pamoja na miti wala bustani siku ile ile bali aliiumba kwanza yenyewe pamoja na mbegu kisha akizinyeshea mvua, ndipo baada ya kipindi Fulani zile mbegu zikaota, zikawa miche midogo ya miti, pengine ilichukua miezi kadhaa kuwa mikubwa, pengine miaka, lakini baada ya kipindi Fulani ndipo ikatokea misitu mikubwa..Lilikuwa ni jambo la pole pole, ingawa Mungu hakushindwa kuiumba dunia ikiwa na misitu tayari kwa dakika moja.

Kadhalika alipoviumba vizazi vya nchi (yaani wanadamu na wanyama) hakutokeza mamilioni ya wanadamu ndani ya siku moja, au mamilioni ya wanyama ndani ya siku moja, bali alimwumba mwanadamu mmoja kama mbegu duniani, akamwekea ndani yake vizazi vyake, vizazi vyote vya wanadamu akaviweka ndani ya mtu mmoja , ili kwamba baada ya muda Fulani labda baada ya miaka 1,000 au 2,000 ndipo wanadamu wawe wameijaza dunia yote.

Kwahiyo unaweza kuona kwamba mpango wa Mungu, wa wanadamu kuijaza dunia yote, ulikuwepo Edeni lakini haukutimia ile ile siku ya kwanza Mungu alipomuumba mwanadamu, hivyo unaweza ukaona jambo ni lile lile kwamba sio mpango wa Mungu kutimiza kusudi lake lote katika ile siku ya kwanza aliyozungumza.

Kadhalika sio mpango wa Mungu, leo tuzaliwe kesho tuwe na watoto, haitawezekana kwasababu nguvu ya Mungu ya uumbaji haiendi kasi hivyo, inapasa kwanza mwanadamu akamilike kwa miaka kadhaa ndipo awe na uwezo wa kupata mtoto.

Na vivyo hivyo, katika maisha yetu, sio mpango wa Mungu leo tukapande mbegu shambani na leo leo tukavune, sio mpango wa Mungu kutupa mali kwa haraka haraka, ingawa anao uwezo wa kufanya hivyo, ila ni mara chache chache sana na kwa watu wachache tena kwa ajili ya utukufu wake, lakini mpango wa Mungu hasa ni kuchuma kidogo kidogo.

Mithali 13: 11 “Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa”..

Kwahiyo tukitaka Bwana aumbe jambo jipya katika maisha yetu tunapaswa tuwe watu wenye subira na wavumilivu.

Kadhalika tukitaka Bwana atuponye, sio lazima atuponye siku hiyo hiyo tuliyomwomba, wakati mwingine itachukua muda, wiki, miezi au wakati mwingine hata miaka, lakini mwisho wa siku atatuponya. Mtu akipata jeraha tunajua hawezi kupona siku ile ile, itamchukua wiki, au miezi, au wakati mwingine miaka jeraha lile kupona, na kufunga, na ngozi kurudia kama ilivyokuwa..Sasa ile hatua ya kidonda kupona taratibu taratibu kwa namna ambayo hatuwezi kuona, ndio ile ile nguvu ya uumbaji iliyokuwa pale Edeni, Bwana Mungu alipoziumba mbingu na nchi, na ndio hiyo hiyo nguvu inayoponya maisha yetu leo.

Nguvu hii ya uumbaji ipo taratibu sana haiwezi kuonekana kwa macho lakini baada ya kipindi Fulani inaleta matokeo, ndio hiyo hiyo inayolisogeza jua na mwezi, huwezi kuona jua likisogea kwa macho isipokuwa baada ya masaa Fulani ukitazama juu utaona limehama kutoka pale lilipokuwepo kwanza.

Vivyo hivyo huwezi kuona mti ukikua kutoka hatua moja hadi nyingine kwa kuudadisi kwa macho, ukifanya hivyo hutaona chochote, utasubiri na kusubiri pasipo kuona chochote ila mfano ukiondoka na kurudi baada ya siku kadhaa utashtukia tu umeongezeka urefu, hivyo ndivyo nguvu ya Mungu ya uumbaji inavyotenda kazi.

Ndivyo Mungu, anavyotenda kazi hatuwezi kumchunguza kwa akili za kibinadamu, tunachopaswa kufanya ni kumuamini tu, na kisha kuiachia ile nguvu yake ya uumbaji itende kazi, kwa uvumilivu wote pasipo kunung’unika.

Leo Bwana akikuahidia kukuponya unachopaswa kufanya ni kumwamini, usiangalie umekaa na ugonjwa siku ngapi au miezi mingapi au miaka mingapi, usijaribu kumdadisi Mungu jinsi gani anaponya…wewe mwamini tu, na kusubiri, kwa uvumilivu wote, na kushukuru kwasababu ile nguvu yake ya uumbaji inatenda kazi ndani yako kwa namna ambayo wewe huwezi ukajua. Itafika wakati utajikuta tuu, unaanza kuona unafuu kidogo kidogo, na hatimaye kupona kabisa, ukiona umeombewa na bado hali yako bado iko vile vile..sio wakati wa kuhama kanisa hili kwenda lile au mtumishi huyu kwenda yule, sio wakati wa kupanic huku na kule, tulia mahali ulipo mngoje Bwana, kwasababu Bwana anatenda kazi kwa namna usioijua wewe.

Vivyo hivyo na riziki nyingine za ulimwengu huu kama mali, sio za kuzihangaikia huku na huko, kwenda kwenye maombi haya na yale pale unapoona hakuna mabadiliko, tulia mahali ulipo tekeleza wajibu wako Bwana atakupa kidogo kidogo, kwanza yeye alisema “hata tusitie shaka” BWANA Mungu hakuijaza dunia hii watu ndani ya siku moja, ilichukua maelfu ya miaka vivyo hivyo hawezi kukujaza wewe mali nyingi ndani ya siku moja, atakupa kidogo kidogo mpaka utakapojaa kiwango anachokitaka yeye. Ndivyo nguvu yake ya uumbaji inavyotenda kazi.

Na zaidi sana na lililo kuu ni “KUWA MKAMILIFU”…Huwezi kuzaliwa mara ya pili leo na leo leo kuwa mkamilifu kwa kiwango kile Mungu anachotaka, Baada ya kuzaliwa mara ya pili Bwana anatutakasa kidogo kidogo ule uchafu uliopo ndani yetu ambao tulikuwa tunautumikia tulipokuwa kwenye dhambi, anauondoa mpaka tunakuwa wakamilifu kwa viwango vile anavyotaka yeye. Siku baada ya siku tunadumu katika ushirika, fundisho la mitume, kuumega mkate, na kusali ili tukue viwango vya kumzaliwa Mungu matunda.(Matendo 2:42)

Dada/Kaka..Je! umeiruhusu hii nguvu ya Mungu ya uumbaji itende kazi ndani yako leo?..Nguvu ambayo itakutengeneza na kukuumba upya uwe mtakatifu katika vile viwango vya kwenda mbinguni?, biblia inasema waasherati, wazinzi, walevi, waabudu sanamu, watukanaji sehemu yao ni katika lile ziwa la moto, na inasema pia katika “Waebrania 12:14 kwamba hakuna mtu atakayemwona Mungu asipokuwa Mtakatifu” Je wewe unao? Una uhakika kwamba Kristo akija leo utakwenda mbinguni? Kama huna huo uhakika ni wazi kuwa atakapokuja utaachwa..na kukumbana na dhiki kuu na siku ya Bwana inayowaka kama moto,na maandiko yanasema katika 2 Petro 1:10 kwamba tujitahidi kuufanya imara uteule wetu na wito wetu,..

Ndugu tunaishi katika siku za hatari ambazo Kristo yupo mlangoni kurudi, siku sio nyingi waovu wote wa huu ulimwengu wataomboleza na kujuta watakapojua kwamba Kumbe Kristo alikuwa ni Kweli, na wakati huo watakuwa wameshachelewa, ni maombi yangu usiwe mmoja wao. Tubu leo ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kukamilisha maagizo ya Bwana Yesu Kristo naye Bwana ataanza kuyaumba upya maisha yako, kwa kupitia Roho wake Mtakatifu.

Bwana Yesu akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine na Bwana atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KISASI NI JUU YA BWANA.

MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!

SEHEMU ISIYO NA MAJI

MTUME PAULO ALIKUWA ANA MAANA GANI KUSEMA “KWA SABABU HIYO, TUKIACHA KUYANENA MAFUNDISHO YA KWANZA YA KRISTO, TUKAZE MWENDO ILI TUUFIKILIE UTIMILIFU;?

NITAMJUAJE NABII WA UONGO?


Rudi Nyumbani

Print this post

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

Mwanzoni kabla sijaokoka nilidhani ndani ya moyo wangu kuwa Mungu hataweza kunihukumu mimi, nilidhani ndani ya moyo wangu kuwa ijapokuwa ninamuudhi Mungu sasa lakini mwisho wa siku ataniokoa tu, kwasababu mimi sina dhambi nyingi zaidi ukilinganisha na watu kama wauaji, na wachawi, nilidhani kuwa pombe nilizokuwa ninakunywa kwa kiasi sizingeweza kuniletea madhara makubwa kiasi cha kutupwa jehanum kama wale wanaokuwa walevi wa kupindukia, uasherati niliokuwa ninafanya na disco nilizokuwa ninakwenda zisingekuwa ni kosa kubwa sana kunifanya mimi niangamizwe kabisa mfano wa wale wanaoigiza mikanda ya ngono.

Nilidhani kuwa matusi niliyokuwa ninatukana Mungu atayafumbia macho siku ile kwasababu Mungu ni wa rehema atanirehemu, kadhalika usengenyaji niliokuwa ninauzungumza niliona pia ni hali tu ya kibinadamu kwamba kila mtu huwa anafanya hivyo, kila kitu niliona kama si dhambi sana, nusu nusu maadamu mimi simdhulumu mtu, siui, wala siendi kwa waganga, isitoshe mimi ni mkristo na nina dhehebu langu, ninawapa kitu maskini hiyo inatosha,Mungu kunihurumia katika siku ile .

Sikuwa najali sana habari za Mungu, niliona kukaa hapo katikati ni sawa tu niliona kama YESU ni kitu cha ziada katika maisha yangu lakini sio msingi wa maisha yako. Hayo yote yalikuwa ndani ya moyo wangu Mpaka siku Bwana alipokuja kuniokoa kwa neema zake, na kunifungua macho ndipo nilipogundua kuwa nilikuwa katika hali ya HATARI SANA pasipo kujijua.

Biblia ipo wazi kabisa inasema;

Mithali 14: 12 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti. 

Ni wazi kila mtu ndani ya nafsi yake ataona kuwa kile anachokifanya au anachokiamini kuwa ni sawa hata kama watu wengine watakiona vipi, mwingine ataona kuwa kushika amri kumi tu za Mungu inatosha, hakuna haja ya kumjua Kristo YESU, mwingine ataona kunywa pombe huku upo kwenye dini yako ni sawa tu!. Mungu atasema Mungu haangalii nje anaangalia vya ndani hivyo kuvaa vimini, na suruali kwa mwanamke wa kikristo sio tabu, Mwingine atasema mimi naamini hakuna ziwa la moto bali tukifa tunapotea tu, mwingine atasema tukifa tunakwenda kwanza toharani kisha mbinguni baadaye, mwingine atasema kusaidia tu yatima na wajane na kuishi maisha ya kujitunza hiyo inatosha kukupeleka mbinguni. Mwingine atasema mambo ya Mungu yametungwa hakuna kitu kama hicho fanya biashara tengeneza pesa enjoy maisha siku ukifa umepotea hakuna maisha baada ya kifo..n.k. Kila mtu akiwa na mawazo yake mwenyewe moyoni akijitumainisha kuwa ni sawa..Biblia inaendelea kusema.

Yeremia 17: 9 “MOYO HUWA MDANGANYIFU KULIKO VITU VYOTE, UNA UGONJWA WA KUFISHA; NANI AWEZAYE KUUJUA?

10 Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.”

Unaona hapo, shetani ni mdanganyifu, lakini MOYO wako ni mdanganyifu zaidi ya shetani. Kwasababu shetani naye hakuwa na mtu wa kumdanganya kabla yake bali moyo wake ndio uliomdanganya, vivyo hivyo na wewe pia kinachokudanganya kwanza ni moyo wako kisha baadaye shetani atakusaidia kufanya hivyo. Na ndio maana biblia inazidi kusisitiza na kusema katika Mithali 4: 23 LINDA MOYO WAKO KULIKO YOTE UYALINDAYO; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

Kaka/Dada haijalishi ni kitu gani unachokiamini kuwa ni sawa, haijalishi unajiona upo katika njia iliyonyooka kiasi gani, haijalishi ni sifa gani umeipata mbele za watu kwa matendo yako mema na ya kiasi, lakini Neno la Mungu na kanuni za Mungu zitabakia kuwa pale pale, Biblia inasema katika,

Yohana 14: 6 Yesu akamwambia, MIMI NDIMI NJIA, NA KWELI, NA UZIMA; MTU HAJI KWA BABA, ILA KWA NJIA YA MIMI.

Usidhani kuwa dini inatosha, yupo aliyekuwa mtu wa dini na kushika amri zote lakini hakuwa na uzima ndani yake unaotoka kwa YESU KRISTO peke yake. Tunamsoma huyo katika

Mathayo 19: 16 “Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ILI NIPATE UZIMA WA MILELE?

17 Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri.

18 Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo,

19 Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.

20 Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena?

21 Yesu akamwambia, UKITAKA KUWA MKAMILIFU, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; KISHA NJOO UNIFUATE.

22 Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.

23 Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.

24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.

Kadhalika aliwaambia mafarisayo na masadukayo wale washika dini maneno haya:

Yohana 8:24 “kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu.”

Unaona hapo? Usikubali kuuruhusu moyo wako kukudanganya kuwa YESU hana umuhimu sana katika maisha yako, usiruhusu kuona njia zako kuwa ni sawa mbele za Mungu na huku bado haujasafishwa dhambi zako katika damu ya YESU KRISTO. Leo hii unaweza ukawa na ujasiri mwingi na kiburi kingi cha kujiona hivyo, lakini ngoja siku utakayokaribia kufa hapo ndipo utajiona kuwa wewe si kitu, unahitaji uzima ndani yako na wakati huo utakuwa umeshachelewa.

Ni maombi yangu usitumainie akili zako kukuongoza popote katika njia za uzima, usitumainie nguvu zako, usitumainie elimu yako, usitumainie matendo yako, usitumainie uzuri wako, usimtumainie mwanadamu, usitumainie kile unachoamini bali tumainia kile Mungu anachosema kuwa kitakuokoa hiyo ndio salama yako ndugu. Siku ile kutakuwa na majuto makubwa sana pindi utakapogundua moyo wako ulikudanganya, kuupinga wokovu unaopatikana katika YESU KRISTO peke yake.

Huu ni wakati wa kubadili mwelekeo wa njia zako, na kukubali kuitii INJILI, Bwana Yesu anasema

Yohana 6:44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho.

Unaona hapo wote walio nje ya neema wapo katika giza, na wewe usitie moyo wako ugumu ukaipinga hiyo sauti inayokuita UOKOKE, kwasababu hiyo ni sauti ya neema ili umwendee akupe uzima wa milele, sio wote watakoikubali isipokuwa wale waliochaguliwa na Mungu tangu kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu. Leo hii uwe nawe mmojawapo kwa kuitii, Inawezekana ulisharudi nyuma, au haukutambua umuhimu wa YESU maishani mwako, leo anza upya.

Mithali 28: 13 Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.

Tubu sasa kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako mbele zake YESU KRISTO, Kisha baada ya kufanya hivyo hatua inayofuata upaswa ukabatizwe katika UBATIZO SAHIHI kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako. Kumbuka wale wote walio nje ya Kristo hawana ondoleo la dhambi zao, hata iweje. Hivyo ili kuukamilisha wokovu wako unapaswa ukabatizwe kwa maji mengi na uwe ni kwa jina la YESU KRISTO, kama ulibatizwa ubatizo mwingine nje ya hapo pasipo kujua ni batili unapaswa ukabatizwe tena, kisha Bwana mwenyewe atakupa Roho wake mtakatifu kuanzia huo wakati na kuendelea atakayekupa uwezo wa kushinda dhambi. Na hapo utakuwa umeuokolewa mwenye tumaini la uzima wa milele. Kisha Damu ya YESU Kristo ndipo itaanza kunena mema juu ya maisha yako.

Hizi ni siku za mwisho YESU KRISTO yupo mlangoni kurudi, usiruhusu njia za udanganyifu wa mali zikakusonga usiufuate uzima ulio kwa BWANA YESU.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Ukiwa umetubu na unautahitaji wa kubatizwa, unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hizi 0789001312.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NJIA YA MSALABA

NJIA YA BWANA INATENGENEZWA WAPI?

UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?

JE! NI HALALI KWA MTU WA MUNGU KUTUMIA NJIA ZA UZAZI WA MPANGO?

JE! NI DHAMBI KWA MKRISTO KWENDA HOSPITALI AU KUTUMIA MITI SHAMBA ANAPOUGUA?

NINI MAANA YA MTU AKIJA KWANGU NAYE HAMCHUKII BABA YAKE HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU?


Rudi Nyumbani

Print this post