Title May 2022

Nyakati za kuburudishwa ni zipi? (Matendo 3:19).

Nyakati za kuburudishwa ni kile kipindi cha utawala wa miaka elfu moja.

Kipindi hicho ni kipindi ambacho dunia itarejeshwa na kuwa kuwa nzuri zaidi hata ya Edeni, ni kipindi ambacho tutatawala na Kristo kama wafalme baada ya kuonekana wadhaifu nyakati nyingi, ni kipindi ambacho tutaishi kama malaika wasioumwa wala wasiozeeka wala kufa.

Hicho kitakuwa ni kipindi cha kufutwa machozi kwa wateule, na kipindi cha kutawala pamoja na Kristo (kwa ufupi kitakuwa ni kipindi cha kuburudika).

Matendo 3:18 “Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo.

19 Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, ZIPATE KUJA NYAKATI ZA KUBURUDISHWA;

20 apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani;

21 ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu”.

Umeona?..Kristo sasahivi yupo juu mbinguni, lakini atakuja tena kutoka huko aje aifanye dunia kuwa kama Edeni na hata zaidi ya pale, na kuwaburudisha wato wote waliojikana nafsi sasa, wanaochekwa sasa kwaajili ya jina lake, walioua kuacha uzinzi, ulevi, uvaaji mbaya, utukanaji n.k kwaajili ya jina lake.

Na nyakati hizo zimekaribia sana, kinachosubiriwa ni kondoo wa mwisho kuingia ndani ya zizi, ili majira hayo yaanze.

Lakini swali jepesi ni je!.. Umempokea Yesu leo?..je utakuwepo katika hiyo miaka ya kuburudishwa au utakuwepo katikamahali pa mateso majira hayo yatakapoanza?.

Ni heri ukatubu leo, na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu kama bado hujatubu wala kubatizwa ubatizo sahihi wala kupokea Roho.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:

Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Nini maana ya Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu;?

Nini maana ya Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu&?

NJIA MOJAWAPO YA KUPATA MSAADA KUTOKA KWA BWANA.

Rudi nyumbani:

Print this post

Kusubu ni nini? Miungu ya kusubu ni ipi?

Kusubu kibiblia ni kitendo cha kuyeyusha dhahabu au  fedha au ‘kito’ chochote kwa lengo la kuunda kitu kingine kipya.

Neno hilo utalisoma sehemu nyingi katika biblia kwa mfano hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utakutana nalo;

Mambo ya Walawi 19:4

[4]Msigeuke kuandama sanamu, wala msijifanyizie miungu ya kusubu mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

Maana yake msaifanye sanamu za kuyeyusha,

Kumbukumbu la Torati 27:15

[15]Na alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga, au ya kusubu, machukizo kwa BWANA, kazi ya mikono ya fundi, akaisimamisha kwa siri. Na watu wote wajibu, waseme, Amina.

Soma pia..

2Nyakati 24:4, 28:2, Waamuzi 17:3, Hesabu 33:52, 1Wafalme 7:23.

Maana yake ni ipi kiroho?

Hata sasa watu wengi, wanajiundia sanamu zao za kusubu rohoni bila wao kujijua…kwa kugeuza maumbile ya vitu vyema na kuvitumia isivyopasa..mpaka kuviabudu.

Kwa mfano fedha si mbaya lakini leo hii watu wameigeuza fedha kuwa mungu wao..kiasi kwamba kwao Mungu si kitu zaidi ya fedha, maisha yao yote ni kuhangaikia mali, kana kwamba hiyo ndio itakayowafikisha mbinguni, kaacha kumtumikia Mungu, hata muda na ibada hana, dai lake ni “Natafuta pesa’’ Sasa hizo ndio sanamu za kusubu..

Wengine biashara kwao zimeshageuka na kuwa sanamu za kusubu, wengine wanadamu., wengine muvi, wengine magemu, wengine mipira.

Tunapaswa tujilinde sana kwasababu sanamu za namna hii zinamtia Mungu WIVU, na wivu ni mbaya kuliko ghadhabu..

Ni heri Mungu akukasirikie kwa makosa mengine kuliko kwa kukuonea wivu.

kwasababu adhabu ya wivu ni mbaya sana kuliko ya hasira..

Mithali 27:4

[4]Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika;

Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu.

Tujilinde mioyo yetu na ibada za sanamu. Mungu hakuwahurumia wana wa Israeli walipotengeneza ndama ya kusubu na kuiabudu kule jangwani. Japokuwa yeye ndiye aliyewaokoa kwa mkono hodari.

Vivyo hivyo na wewe ukisema umeokoka, epuka kugeuza kitu chochote kuwa Mungu wako. Usiruhusu kamwe chochote kuchukua sehemu ya Mungu yako.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Shetri ni nini kama tunavyosoma katika Marko 3:38?

Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).

Zeri ya Gileadi ni nini?

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

UTARATIBU WA KUTOA FUNGU LA 10 UPOJE?.

Haya ni maswali 8 maarufu yahusuyo Zaka.

 1. Ni nani anayepaswa kutoa fungu la 10?,

 2. Je fungu la 10 tunatoa katika faida au mtaji?

 3. Je tunapopewa zawadi tunazitolea fungu la 10?,

 4. Je fedha ya mkopo inatolewa fungu la 10?.

 5. Je Kama mshahara wangu ni milioni moja lakini kutokana na makato ya serikali kama kodi, na pspf, najikuta napokea sh.laki 7 tu, je zaka natoa kutoka katika hiyo laki 7 au kutoka katika ile milioni.?

 6. Je kama nimepokea mshahara ambao haupo katika mfumo wa kifedha, mfano napewa ng’ombe au kuku, namtoleaje zaka huyo?

7. Je!. Tunaweza kuweka deni la fungu la 10? Yaani badala ya kutoa.kila.siku, tukakusanya na hatimaye tukaja kulipa mwisho wa mwezi au mwaka?

8. Je! Fungu la 10 linapaswa lipelekwe wapi kimaandiko?.Na je kuna ulazima wowote wa kulipa zaka?


Tukianza na swali la kwanza.

1. Ni nani anayepaswa kutoa fungu la 10?(Zaka).

Jibu: Kila mtu aliyeokoka ana wajibu wa kutoa fungu la 10. Haijalishi umri wake, jinsia yake?, au hali yake ya kiuchumi.

Maana yake kama unafanya kazi ya mikono au haufanyi, ni lazima kutoa fungu la 10 (yaani kulipa zaka).

2. Fungu la 10 tunatoa katika faida au mtaji?

Fungu la 10 linatolewa katika faida na si mtaji. Mfano una mtaji wa laki moja, na kazi unayoifanya imakupa faida kwa siku sh. Elfu kumi. Hapo zaka utatoa kutoka katika hiyo faida uliyoipata na si. Kutoka katika mtaji ulionao (maana yake kiasi cha zaka unachopaswa utoe hapo kwa siku ni sh. Elfu moja).

3. Je tunapopewa zawadi tunazitolea fungu la 10?

Kama zawadi hiyo uliyopewa utaifanya kuwa mtaji, basi hutaitolea zaka, lakini utatoa katika faida huo mtaji utakayoizalisha. Lakini kama zawadi hiyo matumizi yake ni kama ya mshahara wa kawaida..yaani katika kujihudumia kwa chakula, makazi au malazi, basi utaitolea zaka.

Na vile vile kama hufanyi kazi yoyote, au bado hujapata kazi, chochote kitakachofika mkononi mwako kwaajili ya mahitaji yako, hicho utakitolea zaka.

4. Je fedha ya mkopo, tunaitolea zaka?

Kama mkopo uliochukua ni kwa lengo la mtaji wa biashara, hupaswi kuutolea zaka, bali utatoa zaka katika faida utakayoipata kutoka katika mkopo huo.

Lakini kama mkopo ulioupokea ni kwa lengo la kujihudumia kimaisha kama chakula, mavazi au malazi (Huo ni kama mshahara, hivyo unapaswa uutolee zaka).

 5. Kama mshahara wangu ni milioni moja lakini kutokana na makato ya serikali kama kodi, na pspf, najikuta napokea sh.laki 7 tu, je zaka natoa kutoka katika hiyo laki 7 au kutoka katika ile milioni moja.?

Jibu: Zaka utatoa kutoka katika hiyo milioni moja na si kutoka katika hiyo laki 7, maana yake kiasi cha zaka hapo kitakuwa ni sh. Laki moja kila mwezi.

6. Je kama nimepokea mshahara/Zawadi ambayo haupo  katika mfumo wa kifedha, mfano napewa ng’ombe au kuku, namtoleaje zaka huyo?

Jibu: Kama ng’ombe huyo utamfanya kuwa mtaji, hautamtolea zaka, isipokuwa faida utakazozipata kutoka katika shughuli hiyo, utaitolea zaka (maana yake kama utafanya biashara ya kuuza maziwa, faida utakayoipa kupitia maziwa hayo, utalipa zaka).

Lakini kama utamtumia kwaajili ya kitoweo, hapo huna budi kutafuta thamani ya ngombe huyo na kutoa sehemu ya 10, maana yake kama ng’ombe ana thamani ya milioni moja basi utatoa laki moja kama zaka, au kama hutaweza kupata thamani hiyo, basi utaitoa sehemu ya 10 ya nyama kama zaka.

7. Je!. Tunaweza kuweka deni la fungu la 10? Yaani badala ya kutoa kila siku, tukakusanya na hatimaye tukaja kulipa mwisho wa mwezi au mwaka mwaka?

Jibu: Ndio! Lakini kama kuna ulazima wa kufanya hivyo. Mfano unaweza ukawa unapata faida ndogo, ambayo mahesabu ya zaka yake yanakuwa ni chini ya sh.50, sasa huwezi kutoa sh 40 au 20 au 10 kama zaka kila siku, kwasababu hata matumizi ya hizo sarafu hayapo!.Kwahiyo suluhisho ni kufanya mahesabu ya kiasi kinachopatikana kwa wiki au mwezi, na kulipa kwa pamoja.

Vile vile hakuna ratiba maalumu ya kimaandiko ya wakati wa kulipa zaka..maana yake kama mtu atachagua kulipa kila mwisho wa wiki, hafanyi dhambi, mwingine kila mwisho wa mwezi hakosei, mwingine kila mwisho wa miezi mitatu pia afanyi makosa, ilimradi analipa kiasi chote kwa uaminifu. (Lakini ni vizuri zaidi kulipa mapema, ili kuzuia mlundikano wa madeni..lakini kila mtu anao ustaarabu wake, ambao yeye anauwezo wa kuumudu).

8. Je fungu la 10 linapaswa lipelekwe wapi?..kwa mayatima, kanisani, kwa mtumishi wa Mungu au wapi?.

Ili kupata kupata jibu la swali hili kwa urefu unaweza kufungua hapa >>>> NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

Bwana atubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

JE! KUNA UMUHIMU WOWOTE WA KULIPA ZAKA?

Kwanini Mungu anajifanya kama hajui mambo?

KITABU CHA UKUMBUSHO

Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi.

ZIKUMBUKE FADHILI ZA MUNGU

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya ampokeaye Nabii atapata thawabu ya Nabii? (Mathayo 10:41).

Je! Ni thawabu gani inayozungumziwa hapo?.

Jibu: Ili tuelewe vizuri, labda tuanzie kusoma kuanzia mstari wa 40

Mathayo 10:40 “Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma.

41 Ampokeaye nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki”

Sasa swali, ni thawabu gani inayozungumziwa hapo?..Jibu la swali hili tutalipata katika mstari unaofuata wa 42

Mathayo 10:42 “Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia, HAITAMPOTEA KAMWE THAWABU YAKE”.

Kumbe thawabu inayozungumziwa hapo ni THAWABU KUTOKA KWA MUNGU kwa jinsi sisi tunavyowakaribisha watumishi wake!. Yaani kiwango utakachompimia Mtu wa Mungu,(yaani kumbariki) na jinsi utakavyomchukulia,  ndicho na Mungu pia atakachokupimia wewe!..

Kama umempokea Mtumishi wa Mungu, kama mtu wa heshima sana, na ukambariki sana.. Ndivyo Mungu na yeye atakavyokuchukulia wewe kama mtu wa Heshima sana, na mwenye kustahili thawabu nyingi.

 Lakini kama umempokea kama mtu wa kawaida, kwamba ni mtu mzuri tu!..basi na Mungu naye atakuchukulia wewe kama mtu mzuri tu, na kukupa thawabu kama hiyo hiyo uliyompimia huyo mtu wa Mungu.. Na kama umemlaani mtumishi wa Mungu, na Mungu naye atakulaani.

Bwana Yesu sehemu nyingine alisema maneno haya..

Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, NDICHO WATU WATAKACHOWAPA VIFUANI MWENU. KWA KUWA KIPIMO KILE KILE MPIMACHO NDICHO MTAKACHOPIMIWA”.

Unaona hapo?..anamalizia hapo kwa kusema, KIPIMO MPIMACHO NDICHO MTAKACHOPIMIWA!!..

Mfano wa Mwanamke aliyepata thawabu ya Nabii ni yule mwanamke wa Sarepta aliyemkaribisha Nabii Eliya na kumpikia chakula, ale..kwakuwa alimpokea yule kama Nabii na kumpa chakula, kama mtu wa heshima sana, Mungu naye akampa heshima kwa kulizidisha pipa lake la unga siku zote wakati Israeli yote ina njaa. (1Wafalme 17:9-16)

Kwahiyo na sisi tujitahidi siku zote kupima kipimo kizuri kwa watu wote, hususani walio watumishi wa Mungu, ili na sisi tupimiwe kipimo kilicho kikubwa na Mungu

Bwana atajalie tuwe miongoni mwa watu wa kubariki, ili na sisi tubarikiwe.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

Rudi nyumbani

Print this post

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

Kuna majira yakupasa uisikie sauti ya Mungu, kuliko hasara utakayoingia, ili kuiponya nafsi yako.

Kuna mfalme mmoja wa Yuda anaitwa Amazia, Huyu mfalme siku moja alijikuta anaingia katika vita na maadui zake (Waedomi), Hivyo alichokifanya ni kupanga vikosi vya wanajeshi yake, ili kwenda kushindana nao. Lakini bado aliona majeshi yake hayatoshi, hivyo akaenda kwa ndugu zake, waliokuwa upande wa Israeli, ili awaajiri wanajeshi wao kwa fedha nyingi sana..

Hivyo akawaajiri wanajeshi takribani Laki moja (100,000).

Lakini tunaona alipokuwa anakaribia kwenda vitani, nabii wa Mungu alimfuata, akamwambia, achana na hao askari uliowaajiri, kwasababu mimi sipo nao..Nenda mwenyewe na jeshi lako vitani.

Likawa ni jambo gumu kwake, kwasababu tayari anapunguza nguvu, na kama hiyo haitoshi, tayari alishalipa fedha nyingi sana kwa ajili ya majeshi hayo..Amewekeza fedha zake nyingi katika vita na haziwezi kurudishwa.

Lakini kwasababu Amazia alikuwa anamcha Mungu, alitii sauti ya Mungu, akawa tayari kuipokea hasara, hiyo. Akaenda vitani na jeshi lake dhaifu, na Bwana akamsaidia kushinda, tena kwa ushindi mnono.

2Nyakati 25:6 “Akaajiri pia watu mashujaa mia elfu wa Israeli kwa talanta mia za fedha.

7 Lakini mtu wa Mungu akamjia, akasema, Ee mfalme, usiwaache jeshi la Israeli waende nawe; kwa kuwa Bwana hayupo pamoja na Israeli, yaani, wana wote wa Efraimu.

8 Lakini ukitaka kwenda, haya, jitie nguvu upigane; Mungu atakuangusha mbele ya adui; maana MUNGU ANAZO NGUVU ZA KUSAIDIA, NA KUANGUSHA.

9 Amazia akamwambia mtu wa Mungu, Lakini tuzifanyieje zile talanta mia nilizowapa jeshi la Israeli? MTU WA MUNGU AKAJIBU, BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO”.

Ni mara ngapi, watu wengi wanashindwa kumfuata Yesu, kisa hasara watakazoingia kwa uamuzi huo?

Niliwahi kuzungumza na mtu mmoja, anasema anampenda Mungu kweli, lakini anamiliki bar tena sio moja bali kadha wa kadha, na anasema ndipo anapopatia rizki. Nikamwambia hana budi kuacha biashara hiyo, kwasababu Mungu anaouwezo wa kumpa kitu kingine bora kuliko hicho, ikiwa tu atamtii Kristo. Lakini jambo hilo likawa bado ni gumu kwake kulipokea, akaendelea na biashara yake.

Mwingine pia tulimshuhudia akawa yupo  tayari kuokoka, lakini madai yake ni kuwa hana kazi, anatumia njia ya kujiuza ili apate pesa za kulipa kodi, na bili za maji na umeme.. Anasema kabisa nikiokoa najua hii kazi nitaacha, na sitakuwa na chanzo chochote cha mapato, nitaishije mjini?

Ndugu ikiwa na wewe ni mmojawapo wa watu wanaoshindwa kuacha kazi za ibilisi, kisa tu, umewekeza pesa nyingi katika hizo, au unahofia utakuwa maskini, au ukifanya kazi nyingine utapata kipato kidogo.. Nataka ukumbuke hilo andiko hapo juu kuwa “Bwana anazo nguvu za kusaidia, na kuangusha”.. Na “tena, Anaweza kukupa Zaidi sana kuliko hizo”

Anaweza kukupa mara dufu ya hivyo. Na hata kama hatokupa basi anaweza kukufanya uishi kwa raha na amani kuliko hata hapo ulipokuwepo. Bwana Yesu anasema,..Itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima, kisha upate hasara ya nafsi yako?. Amazia, alikubali kuingia hasara akijua kabisa Mungu kweli atampa Zaidi ya vyote alivyovipoteza.

Ni heri ukampa Yesu Maisha yako ayaokoe, kipindi hichi cha kumalizia, watu wengi wamenaswa kwenye vitanzi hivi…Wakiangalia mitaji yao yote imelalia kwenye michezo ya kamari, imelalia kwenye madawa ya kulevya, imelalia kwenye biashara za pombe na sigara, imelalia kwenye mavazi ya kikahaba na kidunia.

Achana nayo, mwamini Mungu anayekuita. Utakuwa salama, na atakusaidi kumudu Maisha yako..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

Kwanini wakristo wengi ni maskini?

ORODHA YA WAFALME WA ISRAELI.

JAWABU LA MAISHA YA MTU.

APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).

ENZI NA MAMLAKA AMEZIFANYA KUWA MKOGO

Uru wa Ukaldayo ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

Jina la Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo libarikiwe.. Karibu katika kujifunza Neno la Mungu wetu, ambalo ni Taa iongozayo miguu yetu na Mwanga wa Njia yetu. (Zab. 119:105).

Kuna tofauti ya kusamehewa makosa, na kuondolewa Dhambi.. Watu wengi sana wanasamehewa makosa yao na Mungu..lakini bado wanakuwa hawajaondolewa dhambi, Kusamehewa  ni kitu kingine na kuondolewa ni kitu kingine..

Mtu wa kidunia, ambaye hata hamwamini Kristo anaweza kufanya kosa fulani, labda la kuiba na akastahili kufungwa, mtu huyo anaweza kumlilia Mungu, na Mungu akamsamehe kosa hilo na kumwepushia mbali adhabu ya kufungwa, lakini hiyo haimaanishi kuwa ndio kashapata ondoleo la dhambi zake zote.

Utakumbuka wale watu waliomsulubisha Bwana msalabani.. Bwana Yesu aliwaombea Msamaha.. Lakini kwa kuowaombea kule msamaha, haikumaanisha kuwa tayari wameshaokoka na kwamba wakifa wanaenda mbinguni. La! bado walikuwa wana dhambi, ya asili, ambayo hiyo haiondoki kwa kuombewa au kutamkiwa bali kwa mtu mwenyewe kuamua kuchukua hatua ya kufanya maamuzi..

Ingekuwa inaondoka kwa kutamkiwa tu, basi kazi ya wokovu ingekuwa ni rahisi sana, BWANA YESU Asingetuambia tujikane nafsi, asingetuambia tukabatizwe, ANGETUTAMKIA TU DUNIA NZIMA KUWA, TUMESAMEHEWA DHAMBI, na sisi tungekuwa tumestarehe.

Lakini haikuwa hivyo, bali kulikuwa na kanuni maalumu, Na kanuni hiyo ndio ile tunayoisoma katika.. Matendo 2:38, ya KUTUBU NA KUBATIZWA!.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Kwahiyo wale Makuhani, na Maaskari waliomsulubisha Bwana hawakupata Ondoleo la Dhambi, kwasababu formula la kupata ondoleo la dhambi, ili kupata uzima wa milele, na kuokoka na ghadhabu ya Mungu ya ziwa la Moto, ndio hiyo ya kutubu na kubatizwa.

Wao walichokipata ni msamaha tu, wa lile tendo walilolifanya la kumsulubisha Bwana, lakini kama kulikuwa na uzinzi walioufanya juzi, au uuaji walioufanya wiki iliyopita, au wizi walioufanya mwaka uliopita, ambao hawakuutubia, bado walikuwa na hatia ya dhambi hizo, Hivyo walisamehewa kosa hilo moja tu, la kumsulubisha Bwana aliyekuwa mwenye haki, lakini makosa mengine yalibaki pale pale.

Maana yake ni kwamba, kama Bwana Mungu alikuwa amepanga kuwaadhibu kwa kosa hilo la kumsulubisha Bwana Yesu, basi alighairi kwa kuwa waliombewa msamaha. Lakini Msamaha huo walioupata sio Ule wa kuepukana na ziwa la Moto, au wa kuwapatia uzima wa Milele..bali wal lile kosa tu!

Msamaha uletao uzima wa milele, na utuepushao na ziwa la Moto, ni ule tuupatao kwa sisi wenyewe kuamua kutubu dhambi zetu zote kwa kumaanisha kuziacha, na kubatizwa katika ubatizo sahihi, kama ishara ya kufa na kufufuka na Kristo katika upya wa roho, na kupokea Roho Mtakatifu. (Msamaha huu ndio utuleteao uzima wa Milele, na ndio wa muhimu).

Je na wewe umepokea msamaha upi?..Umepata msamaha tu!, au Msamaha kamili..

Inawezekana kila siku unaamka asubuhi na kuomba toba!, ni kweli Bwana ni Mwingi wa Rehema atakusamehe, lakini kama USIPOPATA  MSAMAHA KAMILI WA ONDOLEO LA DHAMBI ambao huo unakuja kwa wewe kuamua kutubu, kwa kumaanisha kuacha Dhambi zako zote.

Kama bado hujapata Msamaha kamili, basi utafute leo kwa bidii.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

NINI MAANA YA KUTUBU

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Rushwa inapofushaje macho?

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Mkristo kutembea na walinzi (Bodyguards),ni sawa?

SWALI: Je Mkristo kutembea na walinzi (Bodyguards), katika huduma ni sawa? Kama sio mbona Bwana Yesu alitembea na mitume wake?


JIBU: Tufahamu kuwa mitume hawakuwa walinzi wa Bwana Yesu, Bali waliitwa kwa kazi ya kumshuhudia Yesu duniani.

Na ndio maana utaona wakati Fulani walijaribu kumtetea kwa silaha zao, Lakini Bwana Yesu alimkemea Petro, na kumwambia sikushindwa kuwaagiza Malaika wa Baba yangu kuja kunipigania,(Mathayo 26:52) hiyo ni kuonyesha kuwa kazi ya ulinzi ni ya Malaika sio ya wanadamu. Na pia hakuwaita, ili wamlinde, bali wajifunze kwake.

Kitendo cha mkristo, au askofu kutembea na askari wenye silaha, mikononi mwao wenye lengo la kumlinda, kama vile walindwavyo wanasiasa au watu mashuhuri, hiyo si sawa. Kwasababu hizo sio nyendo za Bwana wetu Yesu Kristo,alipokuwa hapa duniani.

Ndio upo wakati ambapo huduma itakuwa kubwa, na hivyo kutahitajika kuwekwe mipaka ya watu kukufikia, ili huduma itendeke kwa utaratibu, Lakini hiyo bado haikufanyi uwaajiri walinzi, bali  unapaswa uwaweke watendakazi wenzako katika shamba la Bwana walio chini yako, hiyo ndio kazi yao, kama Kristo alivyofanya kwa mitume wake, hakuwaweka  maakida wa kirumi, au watoza ushuru, au watu mataifa kuwa wahudumu wake.

Yohana 12:20 “Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.

21 Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu.

22 Filipo akaenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu”.

Hivyo kibiblia sio sahihi, mtu wa Mungu kuwaajiri maaskari wa ulinzi, kumlinda. Ni vizuri Zaidi akawachagua watakatifu wenzake ambao atakuwa anahudumu nao, kila aendapo.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Wale mamajusi walikuwa ni wakina nani?

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?

Mshipi wa dhahabu matitini ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Talanta ni nini katika biblia.

Katika agano la kale Talanta kilikuwa ni kipimo cha uzito cha juu zaidi ya vyote (kilitumiwa hususani katika  kupima madini ya  dhahabu na fedha)..Talanta moja ina uzito wa Kg 34.2.

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi..

Kutoka 25:39, 38:25, Samweli 12:30, 1Wafalme 10:10.

Lakini katika agano jipya haikutumika tu kama kipimo cha uzito bali pia kama cha fedha.

Ambapo biblia inatuambia..Talanta 1 ilikuwa na thamani ya sh5,000 ya wakati ule.

Hivyo kulingana na mfano ule wa yule mtumwa ambaye alisamehewa deni lake lililokuwa kubwa sana la talanta 10,000, ambayo tukiibadili katika pesa ya sasa si chini ya Tsh. Bilioni 6…Tunaona yeye  akashindwa kumsaheme mdeni wake aliyekuwa na deni dogo..la Tsh. Laki 1.

Kama tunavyosoma habari Matokeo yake ikawa ni kukamatwa  na kwenda kutupwa gerezani kwa watesaji. (Mathayo 18: 21-35)

Mfano mwingine ni habari ya yule mtu aliyesafiri, kisha akawaita watumwa wake na kuwapa talanta wafanyie biashara.mmoja akampa tano, mwingine mbili, mwingine moja. (Mathayo 25:14-30)

Hivyo katika vipimo vyote viwe ni vya kifedha au vya kiuzito bado ni vipimo vikubwa na  vya  juu sana.

Lakini tunaona jambo lingine katika kitabu cha Ufunuo..juu ya ile ghadhabu ya Mungu atakayoishusha juu ya dunia nzima siku za mwisho.

Anasema mawe yatakayoporomoka kutoka mbinguni yatakuwa ni makubwa kama talanta..Tengeneza picha jiwe moja lenye uzito wa kg 34.2 linaanguka juu yako ..ni mawe yenye uwezo wa kuvunja fuvu la kichwa..

Ufunuo wa Yohana 16:20-21

[20]Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.

[21]Na mvua ya mawe kubwa sana, ya MAWE MAZITO KAMA TALANTA, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno.

Si ajabu watu wataomba wafe haraka..Ili tu kujisitiri na hiyo ghadhabu kali ya Mungu mwenyezi juu ya waovu wote.

Ufunuo wa Yohana 6:14-17

[14]Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake.

[15]Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,

[16]wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.

[17]Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama?

Ni mambo ya kutisha sana yanayokuja huko mbeleni

Jiulize unyakuo ukikupita leo, tumaini lako litakuwa ni nini… Ni majuto na vilio vya kusaga meno, ukijua kabisa hata baada ya kufa huko kwa mateso, ni safari ya moja kwa moja hadi kuzimu.

Ni heri ukampa Kristo maisha yako leo maadamu neema ipo..Unyakuo ni wakati wowote, usipumabazwe na huu ulimwengu…achana nao kwasababu Bwana Yesu anasema siku hiyo wao itawajia kwa ghafla tuwala hawatatambua lolote kwasababu wapo gizani..Na sisi tusiwe kama wao gizani ..dalili zote zimeshatimia, tunachosubiria hapa ni unyakuo basi! Hakuna mtu asiyejua hilo. Injili tuliyonayo sio ya kubembelezewa tena wokovu, ni kujionea hali halisi na kuamka usingizini mwenyewe ..

Tengeneza taa yako. Maanisha kuishi maisha wokovu, kwasababu watakaoachwa pia ni wale wanawali wapumbavu, wakristo vuguvugu (Mathayo 25).

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.

Ratli/ Ratili ni nini katika biblia?

ANGALIA JINSI USIKIAVYO:

KWA KUWA WASEMA MIMI NI TAJIRI.

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

Wahiti ni watu gani?

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

KWA KUWA WASEMA MIMI NI TAJIRI.

Hebu tusome Habari ifuatayo kwa utaratibu halafu tutafakari Pamoja…

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona”.

Hayo ni maneno ya Bwana Yesu aliyowaambia watu wa kanisa la Laodikia, ambalo kanisa hilo kiroho ni sisi wakristo wa siku hizi za mwisho.

Utaona anawashutumu watu wa kanisa hilo na kuwaambia kuwa WANAJIOTA KUWA NI MATAJIRI, kumbe ni MASKINI. Lakini Pamoja na hayo utaona anawashauri wakanunue kwake DHAHABU ili wawe matajiri!!!

Sasa swali la kujiuliza hapo, ni lini MTU AKINUNUA DHAHABU ANAKUWA TAJIRI??.. Ni heri angesema NJOO  NIKUPE DHAHABU BURE!, Lakini yeye anasema NJOO UNUNUE!..Maana yake unatoa kitu ili uipate hiyo dhahabu.

Na kama wewe ni mtafakariji mzuri wa Maandiko utaona Bwana Yesu alichokuwa anakimaanisha hapo, ni kwamba ukainunue dhahabu hiyo kwake, kwa bei ya chini, na kisha ukaiuze kwa bei kubwa ILI UPATE FAIDA UWE TAJIRI. (Ndicho alichokuwa anakimaanisha hapo!).

Sasa tatizo ndio liko hapo, kutoa gharama kuinunua hiyo dhahabu iliyosafishwa kwa Moto. Ingekuwa ni bure wengi wangeenda kuichukua tu!.. lakini Bwana anaiuza!..na inahitajika gharama kuinunua. Sasa swali gharama hiyo ni ipi?

Gharama hiyo tunaisoma katika mfano mmoja Bwana alioutoa katika kitabu cha Mathayo Mlango wa 13.

Tusome..

Mathayo 13:45 “Tena ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara, mwenye kutafuta lulu nzuri;

46 naye alipoona lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza alivyo navyo vyote, akainunua”.

Lulu, ni kama dhahabu tu kwa gharama, kwasababu zinakaribiana thamani!.. Kwahiyo ni sawa  kusema “ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara aliyeona dhahabu nzuri au lulu nzuri akaenda akauza alivyonavyo vyote, akainunua”

Sasa kumbuka huyu ni mfanya biashara, lengo lake ni apate faida awe Tajiri, hivyo katika pitapita zake akakutana na lulu mahali Fulani ambayo inauzwa kwa bei ya chini, na yeye anajua soko la mahali inapouzwa kwa bei ya juu.. na akaona endapo akienda kuinunua kwa bei hiyo ya chini na kwenda  kuiuza kwenye soko la juu atapata faida nyingi sana…sasa kwa busara akaenda kuuza shamba lake, na vyote alivyonavyo ili aipate fedha ya kutosha kuinunua hiyo lulu inayouzwa kwa bei ya chini… Lengo la kwamba atakapoenda kuiuza kwa bei ya juu itamrudishia fedha ya kutosha ya kununua vyote alivyovipoteza na Zaidi sana kubakiwa na faida nyingi.

SASA UMEONA GHARAMA HIYO?

Maana yake kama hatakubali kuuza vyote alivyonavyo ili apate fedha za kuinunua hiyo Lulu hataweza kuinunua na ataendelea kuwa maskini hivyo hivyo hata kama anajiona hana mahitaji yoyote…

Ndicho Bwana Yesu alichokuwa anamaanisha hapo katika hiyo Habari ya dhahabu.. Kwamba mtu yeyote akitaka kuwa Tajiri basi aende kwake akanunue dhahabu hiyo, kwa bei ya chini, ili akaiuze kwa bei ya juu, na kubakiwa na faida ambayo ndio utajiri wenyewe.

Sasa mfano huo kiroho inamaanisha nini?

Tukitaka kuupata ufalme wa mbinguni ambao ndio unaofananishwa na Dhahabu na Lulu. Hatuna budi kuacha vyote tulivyonavyo vinavyozuia sisi kuupata  huo uzima wa milele (Hiyo Ndio maana ya kuuza vyote na kwenda kuinunua lulu/dhabahu).

Tukishaacha vyote yaani Ulevi wetu, uongo wetu, wizi wetu, anasa zetu, kiburi chetu, uasherati wetu, umaarufu wetu, ujuzi wetu ambao unatuletea kiburi, ujuaji wetu, na biashara zetu haramu, kama za madawa ya kulevya, au uuzaji wa pombe, au utapeli au rushwa n.k Tunapoviacha hivi vyote, na kumfuata Yesu hapo ni sawa na tumeuza vyote, na katika viwango vya kimbinguni tumejipatia credit tosha za kuupata Ufalme wa mbinguni (ambao ndio unaofananishwa na ile lulu au dhahabu safi).

Mathayo 19:20 “Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena?

21 Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.

22 Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.

23 Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni”.

Umeona gharama za kuinunua ile DHAHABU ILIYOSAFISHWA KWA MOTO!!!.. Suluhisho ni kuacha vyote, kuvitoa ndani ya moyo wako..

Luka 14:33 “Basi, kadhalika kila mmoja wenu ASIYEACHA VYOTE ALIVYO NAVYO, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Unaacha vyote na kumfuata Yesu kama ulivyo.. Bwana Yesu anawapenda watu wanyenyekevu, ambao wameamua kabisa kuanza moja katika Maisha yao, ambao wamejikana nafsi, ambao wamedhamiria kabisa kuzaliwa upya.. Leo Bwana anakuita, anataka akutumie kama chombo kipya, hivyo vua ujuzi wako leo, vua kiburi chako, acha dhambi zako, na mambo yote yanayokusonga  na mfuate…naye atakupenda!, na kukupa zawadi ya Roho wake Mtakatifu atakayekusaidia katika kushinda dhambi, na kukufanya kuwa mtumishi wake..

Usijione kuwa ni Tajiri, na huna haja ya kitu!.. (usiojione kuwa humhitaji Yesu kwa sasa) bado unamuhitaji sana, bado unaihitaji ile Dhahabu.. nenda kainunue kwa Bwana, kwasababu inapatikana kwa bei ya chini.. na ukiinunua na kwenda kuifanyia biashara, yaani kuwafundisha wengine Habari za ufalme wa mbinguni, utakuwa Tajiri sana katika ufalme wa mbinguni.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

GHARAMA YA UFALME WA MBINGUNI.

VIACHENI VYOTE VIKUE HATA WAKATI WA MAVUNO.

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

NUNUA MAJI YA UZIMA.

Je! Ni kweli Yesu alirejesha kila kitu kama pale Edeni?

Rudi nyumbani

Print this post

Babewatoto ni nani katika biblia?(Isaya 34:14).

Babewatoto ni jina lingine la mapepo yanayotembea usiku (yenye mfano wa ndege wa angani).

Hawa wametajwa mara moja tu katika biblia..

Isaya 34:14 “Na hayawani wa nyikani watakutana na mbwa-mwitu, na beberu anamwita mwenziwe; naam, babewatoto anakaa huko na kujipatia raha”.

Bwana alitoa unabii juu watu wote wa ulimwengu waliomwacha yeye, kuwa makao yao yatakuwa ni makao ya hayawani wa porini na ya mapepo hayo (Babewatoto).

Utaona unabii kama huo Bwana aliutoa pia kwa Babeli kwamba utaanguka na makao yake yatakuwa ukiwa na hayawani wa mwituni watakaa huko na MAJINI yatacheza huko.

Jambo ambalo lilikuja kutimia kama lilivyo..ulipofika wakati wa unabii huo kutimia, Babeli ilikuja kuanguka na mahali pale ambapo palisifika kwa uzuri na bustani zinazoelea leo hii tunapozungumza ni jangwa, hayawani wa porini wanapita na majini wanakaa huko.

Isaya 13:19 “Na Babeli, huo utukufu wa falme, uzuri wa kiburi cha Wakaldayo, utakuwa kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.

20 Hautakaliwa na watu tena kabisa, wala watu hawatakaa ndani yake tangu kizazi hata kizazi. Mwarabu hatapiga hema yake huko, wala wachungaji hawatalaza makundi yao huko.

21 Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na MAJINI watacheza huko”.

MAJINI yanayozungumziwa hapo ni mapepo yenye maumbile kama ya Mbuzi-mwitu.

Hiyo ikifunua kuwa tukimwacha Mungu haijalishi tulikuwa tumestawi kiasi gani, Bwana ataushusha utukufu wetu na makao yetu yatakuwa ni makao ya majini (mapepo) na babewatoto.
Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:

Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au

Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

MAJINI WAZURI WAPO?

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

Makao ambayo Yesu alikwenda kutuandalia ni yapi?

Rudi nyumbani

Print this post