Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Mathayo 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja KUITANGUA TORATI AU MANABII; La!, SIKUJA KUTANGUA, bali KUTIMILIZA.

18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie”.

JIBU: BWANA aliposema hakuja kuitangua torati wala manabii bali kuitimiliza…alikuwa ana maana kuwa yeye hakuja kuondoa neno lolote la torati lililosemwa bali alikuja kulifanya kuwa IMARA ZAIDI..kwa mfano torati iliposema usizini, haikuishia pale tu katika mwili…lakini Bwana Yesu alipokuja alisema amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye nafsini mwake…si umeona hapo.. hajaiondoa amri ile bali ndio ameikolezea..Ikiwa na maana sio tu kwenda kuchukua hatua ya kuzini ndio iwe kosa hapana bali kitendo cha kumtamani tu tayari ni kosa, hivyo haupaswi kutamani kabisa ili kuitimiliza torati… 

Kadhalika Torati pia ilisema usiue..lakini Yesu alisemaje? amchukiaye ndugu yake ni sawa na muuaji..umeona na hapo pia sio tu Kuua ndio iwe kosa, hapana! bali hata hilo wazo la kumchukia tu ndugu yako halitakiwi liwepo ndani ya mtu. Torati ilisema pia ikumbuke siku ya sabato uitakase, lakini Bwana Yesu alisema ..Yeye ndiye BWANA wa Sabato (Marko 2:28), ikimaanisha kuwa ukimpata Yesu umeishika sabato yako, kwasababu ndani ya moyo wako kila wakati unakuwa ndani ya pumziko lako na kila siku unakuwa katika ibada na sio tena siku moja maalumu. 

(Mathayo 11:28)…Unaona hapo? Hajaiondoa lakini ameifanya ieleweke zaidi. Na ndivyo ilivyo pia kwa maneno mengine yote yote ya torati Bwana hakuyaondoa bali aliyafanya kuwa imara zaidi. 

Ubarikiwe sana .jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa njia ya maelezo unaweza kufungua video chini

[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=RxbUfwts4fg[/embedyt]


Mada zinazoendana:

UTIMILIFU WA TORATI.

JE! VITABU VYA BIBLIA VILIWEZAJE KUKUSANYWA PAMOJA?

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?

USIMFANYIE JEURI ROHO WA NEEMA.

JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

TAFUTA KUMJUA MUNGU ZAIDI YA SHETANI

NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
lucas mhula
lucas mhula
2 years ago

Amen naomba kutumiwa hiyo video