Title February 2022

Je! Yuda atahukumiwa na Mungu kwa dhambi yake ya usaliti?

Je! Yuda atahukumiwa na Mungu kwa dhambi yake ya usaliti? Na wakati ulikua mpango wa Mungu Bwana Yesu afe kwaajili ya ukombozi?.

Jibu: Ndio Yuda atahukumiwa kama mkosaji..Kwasababu Bwana Yesu huyo huyo alisema..

Marko 14:21 “… lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu; ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa”.

Hapo Bwana anasema ingekuwa heri kwake kama asingalizaliwa, maana yake mtu atakayemsaliti atakuwa na kosa kubwa sana. Haijalishi maandiko yametabiri au la!.

Sasa swali la msingi ni kwanini iwe ni kosa ilihali imeshatabiriwa na maandiko lazima yatimie?

Ili tuelewe vizuri hebu tusome tena unabii mwingine uliootolewa na Bwana ambao haujatimia bado lakini utakuja kutimia siku za mwisho.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Huo ni unabii Bwana alioutoa ambao bado haujatimia, lakini umeelenga baadhi ya watu, kwamba siku ile watamfuata Bwana na kumwambia maneno hayo, na Bwana atawakana sawasawa na alivyotabiri.

Sasa hebu tujiulize!.. Hao ambao watatimiza unabii wa kukanwa na Bwana siku ya mwisho, watakuwa hawana hatia au makosa, kwasababu tayari walikuwa wameshatabiriwa hayo?.

Kama jibu ni hapana!..basi hata Yuda anayo hatia ya kumsaliti Bwana hata kama unabii umetabiri hayo..

Kumbuka Bwana hakuwatajia jina la atakayemsaliti..alisema tu mmoja wenu atanisaliti akaishia hapo!!..hakuendelea zaidi kumtaja mtu jina, Ndio maana wanafunzi wake wote walikuwa na wasiwasi kuwa unabii unawazungumzia wao.

Marko 14:18 ” Nao walipokuwa wameketi chakulani, wakila, Yesu alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu, naye anakula pamoja nami, atanisaliti.

19 Wakaanza kuhuzunika, wakamwambia mmoja mmoja, Je! Ni mimi?

20 Akawaambia, Ni mmoja wa hao Thenashara, ambaye achovya pamoja nami katika kombe”.

Tofauti ya Yuda na mitume wengine 11 waliosalia ni Kwamba Yuda hakuwa anazingatia unabii wa kumsaliti Bwana hivyo baada ya kuusikia haukumshtua, aliendelea kuishi atakavyo.

Lakini wakina Petro na mitume wengine, waliingiwa na hofu na kauli hiyo ya Bwana, hivyo hata kama kulikuwa na roho ya usaliti ndani yao iliyoanza kuingia basi waliipambana nayo iondoke na hatimaye wakaishinda, lakini Yuda ilimshinda na ikamvaa..

Umeona?

Ni sawasawa tu na Bwana alivyosema..“watakuja wengi siku ile na nitawaambia siwajui”.Na watu leo wanalipuuzia neno hilo wala hawaogopi, bado wanaendelea na uzinzi, bado wanaendelea na ulevi, uasherati, uuaji, usengenyaji, wizi n.k unategemea vipi watu wa namna hii wasitimize huo unabii wa Bwana katika siku ya mwisho???

Hii ni tahadhari kwetu, kwamba tujitakase, ili tusiutimize unabii huo, kadhalika lengo la Bwana kutoa unabii wa yeye kusalitiwa ni tahadhari ya mitume wasije kumsaliti.
Je umeokoka????..au ni mkristo jina tu!
Maandiko yanasema..

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

MKAMCHUKUE SALAMA.

Kama Bwana anawajua walio wake tangu asili kwanini tunahubiri injili? (Warumi 8:29).

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je sisi wakristo tunaruhusiwa kufanya 40 za marehemu?

Je sisi wakristo tunaruhusiwa kufanya 40 za marehemu, au kufanya maziara ya makaburi baada ya mazishi?

Historia ya sherehe ya 40 ni ya kipagani na si ya kikristo. Asili yake ni katika Taifa la Misri, ambapo Watu waliokuwa mashuhuri (yaani wafalme au watu maarufu), baada ya kufa walikuwa wanapakwa dawa maalumu kwa muda wa siku 40, (Kila siku unapakwa mara moja na kisha unaachwa!, na kesho tena kurudiwa, na kesho kutwa mpaka siku 40 zitimie).

Na baada ya siku hizo kuisha ndipo mwili wa marehemu unafungwa katika sanda, na kisha kuwekwa kwenye sanduku Fulani maalumu, ambapo mwili ule utakaa mamia ya miaka bila kupotea kabisa kwa kuoza!. Ndicho Yusufu alichomfanyia baba yake Yakobo..

Mwanzo 50:1 “Yusufu akamwangukia babaye usoni, akamlilila, akambusu.

2 Yusufu akawaagiza watumishi wake waganga, kwamba wampake baba yake dawa asioze. Waganga wakampaka dawa Israeli.

3 SIKU ZAKE AROBAINI ZIKAISHA, maana hivyo hutimizwa siku za kupaka dawa. Wamisri wakamlilia siku sabini”.

Sasa hizo zilikuwa ni desturi za wamisri, na si waIsraeli, Yusufu alitumia desturi hiyo ya wamisri kwasababu sehemu kubwa ya Maisha yake aliishi Misri, hata mke wake alikuwa Mmisri, na hata jina lake alibadilisha na Farao na kuwa la KiMisri. Lakini baada ya sheria kuja kwa mkono wa Musa, hizo taratibu zilikufa!!!..na wala hakuna mahali popote Mungu aliwaagiza Israeli wazipake maiti dawa kwa siku 40 baada ya hapo!..

Kulikuwa na taratibu za kupata Mwili wa marehemu Marhamu (yaani Perfume), lakini si kwa kipindi cha siku 40 mfululizo!, na ni Marhamu iliyokuwa inapakwa na si Dawa!

Lakini swali ni kwanini leo katika Ukristo, sherehe hii imeingizwa kana kwamba ni sherehe ya kiimani?

Sherehe hii ya 40, ilikuja kubadilika kutoka katika kupaka dawa mwili wa marehemu mpaka kuadhimisha marehemu. ilikuja kuingizwa baada ya kundi dogo la watu ambao si wakristo, walipolilinganisha tukio la Bwana Yesu kuwatokea watu kwa siku 40, baada ya kufufuka kwake, na jinsi alivyopaa baada ya siku hizo 40.

Hivyo kwa kulinganisha huko wakazalisha hoja kwamba, mtu anapokufa roho yake kabla haijakwenda kuzimu au paradiso, inakuwa inazunguka na kuwatokea wengi kwa siku 40, na baada ya siku 40, ndipo aidha inapaa kwenda juu au inapelekwa chini kuzimu.

Hivyo kulingana na baadhi ya madhehebu wanaamini kuwa ndani ya hizo siku 40 baada ya kifo ndio wakati sahihi wa kuwaombea marehemu, ili waishie katika hatima nzuri, maana yake wasipoombewa katika hizo siku 40, basi kama marehemu alikufa katika dhambi basi hatakwenda mbinguni, bali motoni, na ndugu zake walio hai watakuwa hawajamfanyia wema.

Lakini je jambo hilo lina uhalisia wowote kibiblia?

Jibu ni la! Halina uhalisia wowote kibiblia, maandiko yanathibitisha kuwa mtu anapokufa, saa ile ile anashuka kuzimu kama amekufa katika dhambi, au anaingia paradiso kama amekufa katika haki (Soma Luka 16:22-23 na Waebrania 9:27). Hakuna siku 40 za mangojeo..Na Zaidi ya yote!, Bwana Yesu hakuwa Marehemu kipindi anawatokea watu kwa siku 40!, alikuwa tayari ameshafufuka na kuwa hai, wala hakuwa “Mzimu”.. Mizimu inabakisha mifupa yao makaburini, lakini Bwana Yesu hakukuwa na kitu kilichobaki katika kaburi lake Zaidi ya zile “SANDA!”.

Kwahiyo sherehe ya 40, ni ya kipagani!, wakristo hatupaswi kuiadhimisha, kwasababu Kristo hayupo katika hizo sherehe.

Sasa unaweza kuuliza, ikitokea umealikwa na ndugu wanaofanya sherehe hizo na wewe uhudhurie!..

Kama umealikwa na ndugu zako, ambao bado macho yao hayajafumbuliwa kulitambua hilo, unaweza kuhudhuria ila usishiriki hata kidogo ibada zao! (Kwasababu ni ibada za wafu), Na lengo la wewe kwenda kule isiwe kula!, bali liwe kuwahubiria na kuwaonesha pendo la Kristo! Katika hekima yote!!. Ili wanapotoka pale wamjue Kristo na uweza wake na ukweli kuhusu yatakayojiri baada ya kifo!..

Na vile vile wakristo hatuna ruhusa ya kufanya maziara katika makaburi ya Marehemu kwa lengo la kuwafanyia Ibada, kwamba kubadilisha hatima yao kule walipo!, au kupata baraka kutoka kwao!.. Hapana!. Tunapaswa kufanya maziara katika makaburi kwa lengo tu! La usafi!, na heshima yetu sisi tuliosalia, kuonesha ustaarabu wetu!, mbele za watu walio nje!.. Sawasawa tu na unavyofanya usafi katika viunga vyako na bustani zako, au uwanja wako.

Kwa maelezo marefu kuhusu nini kitatokea baada ya kifo, unaweza kufungua hapa >> Nini kitatokea baada ya kifo!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

CHAPA YA MNYAMA

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

Zeri ya Gileadi ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda.

SWALI: Bwana alimaanisha nini katika mstari huu;

Amosi 6:5 “ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi”

Je! alimkosa Daudi, kwa namna alivyokuwa anamsifu?


JIBU: Jibu ni la! Mstari huo haumaanishi kuwa Mungu anachukizwa na watu wanaomsifu kwa ala, na vyombo vingi vya muziki, hapana, kinyume chake anasisitiza sana tufanye hivyo, tena hiyo pia ilikuwa ni sababu nyingine iliyomfanya Mungu ampende Daudi..

Daudi kwa uvuvio wa Roho aliandika maneno haya;

Zaburi 150:3 “Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;

5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya”.

Umeona? Kuonyesha kuwa Mungu anapendezwa sana na kufisiwa kwa ala na midundo mbalimbali ya miziki.

Lakini sasa kwanini kwenye mstari huyo wa Amosi, anaonekana kama anawakemea watu wanaofanya hivyo?

Kumbuka hapo, anasema ninyi “mnaoimba nyimbo za upuzi”. Ikiwa na maana, wanachokiimba  hakimtukuzi Mungu, kinamfano wa ki-Mungu lakini ni cha kidunia, na pia hawamuiimbi Mungu katika Roho na Kweli, yaani, matendo yao, yapo mbali na Mungu halafu wanajifanya wanamwimbia yeye katika ustadi wa ala mbalimbali..

Ndicho walichokifanya wana Israeli hicho kipindi, walikuwa wanafanya maasi mengi, lakini wanajifanya wanajua kumtukuza Mungu kwa nguvu kama Daudi..Matokeo yake, Mungu akawazira kwa sifa zao za kinafki, akawapa adhabu ya kuchukuliwa utumwani Babeli..

Ukisoma mistari ya mbele kidogo Bwana anasema;

Amosi 6:8 “Bwana MUNGU ameapa kwa nafsi yake, asema Bwana, Mungu wa majeshi; Naizira fahari ya Yakobo, nachukizwa na majumba yake; kwa sababu hiyo nitautoa huo mji, pamoja na wote waliomo ndani yake.

9 Hata itakuwa, wakisalia wanaume kumi katika nyumba moja, watakufa”.

Umeona, mfano wa Kanisa la Kristo lililopo sasa.

Tuna vyombo vingi vya kisasa vya kumsifu Mungu, tuna magitaa, tuna maspika yenye nguvu, tuna mapiano, vinanda vya kisasa, matarumbeta n.k. jambo ambalo ni zuri kumsifu Mungu kwa namna hiyo. Lakini angalia kinachoimbwa sasa, na staili za uchezaji, ni ‘upuuzi’ sawasawa na maneno ya Bwana. Huwezi tofautisha nyimbo ya ki-Mungu na nyimbo za wasanii wa kidunia.

Na hata kama tutaimba maneno ya kumsifu Mungu, lakini angalia matendo yetu nyuma ya pazia, yapo mbali kabisa na wokovu na utakatifu.

Hivyo unabii huo unatuhusu sisi, tunapaswa tujirekebishe, ili Bwana asituzire kwa kutupa adhabu kama alivyowapa wana wa Israeli kwa kuwapeleka utumwani Babeli.

Biblia inasema tumwabudu Mungu katika uzuri wa utakatifu, Na Sio katika vinywa tu, na midundo, Ili tupokee baraka alizozikusudia katika kufanya hivyo.

1Nyakati 16:29 “Mpeni Bwana utukufu wa jina lake;…. Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu”;

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Kinubi ni nini katika biblia? (1Samweli 16:16, 23)

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.

Rudi nyumbani

Print this post

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Maana inayojulikana ya Unafiki ni ile hali ya kutoa maneno, au kuonyesha hisia au vitendo kwa nje tu, ambavyo kiuhalisia ndani ya mtu huyo havipo.

Kwamfano mtu anaweza kuwa anakuchukia, lakini kwa nje akawa anaonyesha kama kukujali na kukuchekea. Huo ndio unafiki.

Pengine unaweza ukawa unafahamu aina hiyo moja ya unafiki, lakini Leo tutaona aina mbalimbali za unafiki ambazo zinazungumziwa kwenye biblia, na namna gani ya kuzikwepa, kwasababu moja ya dhambi ambazo zinamchukiza Mungu sana ni unafiki, na inawapeleka watu wengi kuzimu pasipo wao kujua.

  1. Aina ya kwanza ni pale unapoijua elimu ya dunia hii kuliko elimu ya Mungu.

Hilo Bwana Yesu aliliweka wazi kabisa akasema..

Luka 12:54 Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya?

Ikiwa Geografia ipo kichwani, kanuni za fizikia umezitunza mpaka unafahamu ni kwanini jani linaanguka chini na haliendi juu, unajua ukiumwa unaweza kwenda kutumia mwarobaini ukapona..Lakini unashindwa kujua kwa Mungu yupo, au hizi ni siku za mwisho. Ukweli ni kwamba Mungu anakuona kama ni mnafiki, na mwisho ukifika hatahangaika kukupa neema ya kumtambua bali utaishia kupotea kwasababu anajua wewe unajiweza, lakini hutaki tu.

  2. Ni pale unapoona matatizo ya wengine sana, kuliko matatizo yako mwenyewe;

Bwana alisema;

Mathayo 7:3 “Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii?

4 Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?

5 Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako”.

Hali hii inakufanya, uwaone wengine wote ni wakosaji, au hawastahili, na matokeo yake Mungu anakuona na kukuhukumu vilevile kama unavyowahukumu wao, Soma habari ya Yule farisayo aliyejihesabia haki zaidi ya mtoza ushuri( Luka 18:9-14) utalithibitisha hilo. Hivyo, hatuna budi, kujiuhubiria kwanza sisi, ndio tuende na kwa wengine.

3. Pale unaposali au unapotoa sadaka, lengo lako likiwa ni utazamwe na watu, kuwa wewe ni mtoaji au mwombaji mzuri, huo Bwana anauona pia ni unafiki.

Alisema:

Mathayo 6:1 “Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.

2 Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu”.

4. Pale unapoufahamu ukweli lakini unawazuia wengine wasiujue ukweli huo kwa makusudi.

Mathayo 23:13 “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie.”

Hii inawahusu sana sana viongozi wa dini, kwamfano pengine wanajua ubatizo sahihi ni wa kuzamishwa katika maji mengi, lakini hawawafundishi kondoo wao hilo, wanajua, hizi ni siku za mwisho na Yesu yupo mlangoni kurudi, kwamba watu waache dhambi wamgeukie Mungu, kinyume chake wanawahubiria mafanikio tu miaka yote, ili tu wapate fedha. Huo Bwana anauona kama ni unafiki, mbaya sana, na adhabu yake ni ziwa la moto.

5. Unafiki ni pamoja, na kujifanya msafi lakini, ndani ni mchafu:

 Mathayo 23:27 “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote.

28 Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani mmejaa unafiki na maasi”.

Hili bado lipo kwa viongozi wa imani, unakuwa askofu au mchungaji, unavaa kanzu nyeupe, unaitwa baba, lakini unafumaniwa na skendo za uzinzi,  unakunywa pombe kichini chini, unapenda mambo ya ulimwenguni. Kwa Bwana ni heri tujionyeshe kuwa sisi ni wakosaji, kuliko kujificha nyuma ya kivuli cha utakatifu ni hatari sana.

6. Unafiki ni pale unapojua unapaswa umtumikie Mungu, lakini hufanyi hivyo kwa kutoa udhuru:

Soma Mathayo 24:45-51, utaona anazungumzia habari ya Yule mtumwa mwaminifu, ambaye alifanya vyote alivyoagizwa na Bwana wake bila udhuru, lakini mwingine, akajisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia akaanza kuwapiga wafanyakazi wake. Bwana Yesu anasema atakaporudi, atamweka fungu lake pamoja na wanafiki. Epuka udhuru na uvivu katika kumtumikia Mungu.

Mathayo 24:50 “bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51 atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.

7. Na mwisho, unafiki ni pale unaposisitizia watu wayatimize yale maagizo, madogo, lakini yale ya msingi, na yenye kuokoa, huna habari nayo.

Kwamfano kuhimiza sana utoaji wa sadaka, ambao kimsingi Bwana mwenyewe alisema tufanye hivyo, lakini pale inapokuwa imezidi kila ibada ni sadaka tu, sadaka tu, mpaka ya mchicha, na tunasahau mambo makuu kama Utakatifu, kumcha Mungu na upendo. Huo ni unafiki mkubwa kwa Bwana..

Mathayo 23:23 “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache.

24 Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia”.

Bwana atusaidie tujiepusha na hizo aina saba (7) za unafiki, kwasababu zitatupelekea jehanamu ikiwa zipo ndani yetu.

Lakini swali ni Je! Tunazikwepaje? Jibu ni kwa kumaanisha kumfuata Yesu kwa mioyo yetu yetu.  Kwa jinsi tunavyomkaribia yeye ndivyo anavyotukaribia na sisi, kutusaidia kuwa kama yeye. Hivyo tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kutoka katika moyo wako, kisha nenda kabatizwe ikiwa hukufanya hivyo, kumbuka ubatizo sahihi ni kwa jina la YESU KRISTO sawasawa (Matendo 2:38). Kisha Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu, ikiwa utapenda upate msaada huo wa wokovu, basi wasiliana nasi kwa namba zinazoonekana chini;

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

MAMA UNALILIA NINI?

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

YESU ANA KIU NA WEWE.

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

Deraya ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 59:17

Jibu: Tusome,

Isaya 59:17 “Akajivika haki kama DERAYA KIFUANI, na chapeo cha wokovu kichwani pake, akajivika mavazi ya kisasi yawe mavazi yake, naye alivikwa wivu kama joho”.

Deraya ni jina lingine la “DIRII”. Dirii ni vazi la chuma, askari walilokuwa wanalivaa kipindi wapo vitani, vazi hilo lilikuwa linafunika eneo la kifua na tumbo!, hivyo hata mkuki ukirushwa kwa bahati mbaya ukafika maeneo ya tumbo au kifua, basi usingeweza kupenya kwasababu ya vazi hilo gumu la chuma, lililopo kifuani. (Unaweza kusoma pia 2Nyakati 26:14).

Lakini hii Deraya au Dirii, inafunua nini kiroho?, au inawakilisha nini katika roho?

Tusome tena hiyo Isaya 59:17.. “Akajivika haki kama DERAYA KIFUANI, na chapeo cha wokovu kichwani pake”

Umeona hapo?..kumbe Deraya au Dirii inafananishwa na HAKI, na chepeo yaani Helmet inafananishwa na Wokovu.. Sawa sawa na Waefeso 6:14..

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na KUVAA DIRII YA HAKI KIFUANI”

Haki inayozungumziwa hapa, sio ile HAKI inayotokana na Matendo yako!, bali ni ile inayotokana na IMANI THABITI YA KUMWAMINI BWANA YESU.

Tunapopata Ufunuo wa Yesu ni nani?, na kujua kuwa kwa kupitia yeye tumepata ondoleo la dhambi, na yeye ndiye vazi letu mbele za Mungu, na kwamba tunahesabiwa haki bure! Kwa njia ya yeye, basi tunakuwa na Amani, na HAKI hiyo ni silaha tosha ya kumshinda shetani, ambayo kiroho ndio Dirii au Deraya.

Warumi 5:1 “BASI TUKIISHA KUHESABIWA HAKI ITOKAYO KATIKA IMANI, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,

2 ambaye kwa yeye tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo mnasimama ndani yake; na kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu”.

Je! Umemwamini Yesu?, kama bado basi kiroho huna dirii kifuani mwako, na adui shetani, ana uwezo wa kukudhuru wakati wowote, na kukumaliza kabisa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

UMEITIMIZA HAKI YOTE?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

UMEITIMIZA HAKI YOTE?

Rudi nyumbani

Print this post

MKAMCHUKUE SALAMA.

Je unajua sababu kuu ya Yuda kujinyonga?.. Jibu ni kwasababu alishuhudia jambo ambalo lilikuwa ni tofauti na mategemeo yake!

Matazamio ya Yuda hayakuwa kumtoa Bwana Yesu auawe!.. Yuda lengo lake kuu lilikuwa ni KUPATA PESA!, Hivyo alichojua ni kwamba katika kumsaliti Bwana Yesu, Makuhani watamchukua na kisha watamwadhibu kwa viboko tu! Na kisha watamwonya asiendelee kuhubiri na hatimaye watamwachia, na yeye ataendelea kuwa mtume wa Bwana Yesu, hakujua kuwa USALITI WAKE utampelekea Bwana KUHUKUMIWA AFE!. Alijua hata kama Bwana atakuja kufa, lakini si kwa kupitia usaliti wake!, alijua atakuja kufa kwa njia nyingine. Ndio Maana utaona baada tu ya hukumu kupita ya Bwana kuuawa!, alijuta majuto makuu..

Mathayo 27:1 “Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua;

2 wakamfunga, wakamchukua, wakampeleka kwa Pilato aliyekuwa liwali

3 Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, ALIPOONA YA KUWA AMEKWISHA KUHUKUMIWA, ALIJUTA, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema, NALIKOSA NILIPOISALITI DAMU ISIYO NA HATIA.

4 Wakasema, Basi, haya yatupasani sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe.

5 Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga”.

Umeona?.. Wazee wa makuhani walimficha Yuda nia yao hiyo ya kumwua!, walikuja kuiweka wazi baada ya kumkamata Bwana Yesu!, kwasababu walijua endapo wangemfuata Yuda na kumwambia moja kwa moja kwamba wanataka kumwua!, Yuda angekataa!!!..kamwe asingeweza kumtoa Bwana Yesu auawe!!

Sasa ili tuzidi kulithibitisha hilo kuwa lengo la Yuda si kumpeleka Bwana asulubiwe!, bali aadhibiwe tu na kuachiwa.. tusome mistari ifuatayo…

Marko 14:42 “Ondokeni, twendeni zetu; tazama, yule anayenisaliti amekaribia.

43 Basi alipokuwa katika kusema, mara Yuda alifika, mmoja wa wale Thenashara, na pamoja naye mkutano, wana panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani, na waandishi, na wazee.

44 Na yule anayemsaliti alikuwa amewapa ishara, akisema, Nitakayembusu, huyo ndiye; MKAMATENI, MKAMCHUKUE SALAMA.

45 Basi alipokuja, mara akamwendea, akasema, Rabi, akambusu.

46 Wakanyosha mikono yao wakamkamata”.

Hapo mstari wa 44, unasema.. “MKAMATENI, MKAMCHUKUE SALAMA”.. Maana yake halikuwa lengo lake Bwana apate madhara Makubwa kama yale!, ya kusulubiwa!.. Lakini ilikuja kinyume na matarajio yake!.. Badala wale wakuu wa makuhani wamwonye tu na kumwachia, wakahimiza asulubiwe!.. Ikawa ni kinyume na makubaliano yao na YUDA!, Na Yuda kuona vile akajuta kuchukua fedha zao, akawarudishia, kwasababu hawakukubaliana hayo!.

Ni kitu gani nataka tuone hapo?

Kuna mambo au maamuzi ambayo unaweza kuyachukua sasa, ambayo utaona kama madhara yake ni madogo mbeleni, lakini kumbe ni makubwa sana!.

Siku zote unapoingia mkataba na dhambi, madhara yake ni makubwa sana mbeleni!.. Leo hii dhambi inaweza kukushawishi kuwa ulifanyalo ni dogo tu!, halitakuletea shida kubwa mbeleni.. lakini siku itakapofika litakuletea matokeo makubwa tofauti na ulivyotegemea.

Maandiko yanasema kuwa “..mshahara wa dhambi ni mauti (Warumi 6:23)” na si “mshahara wa dhambi ni huzuni”.. maana yake Unapoingia mkataba na dhambi leo, fahamu kuwa mwisho wake ni Mauti!.

Umeshaokoka halafu unasema ngoja “nikazini tu mara moja” kwa matarajio kwamba utatubu tu! na hakutakuwa na madhara yoyote!.. Nataka nikuambie hata Yuda, alisema hivyo hivyo, alijua bado anazo siku nyingi sana za kuendelea kuwa mtume wa Bwana Yesu, hakujua ile siku ndio ilikuwa siku ya mwisho ya utume wake! Na lile busu ndio lilikuwa busu lake la mwisho!, milele hatamwona Bwana!.. mwisho wake ulikuwa ni MAUTI (Kujinyonga)..

Ndugu usiyapime matokeo ya dhambi kwa uzoefu!.. ile dhambi ambayo unaona kama haina matokeo makubwa.. maandiko yanasema matokeo yake ni MAUTI!

Leo hii unapomsaliti Bwana na kwenda kufanya uasherati, au kujiuza mwili wako, au kuiba au kutapeli, au kufanya anasa, au kuua, au kujilipiza kisasi, ukiwa na mategemeo kuwa utatubu tu! Na utarudiana na Bwana kama kawaida!!..nataka nikuambie “KUWA MAKINI SANA!!”.. Huo uzinzi unaopanga kwenda kuufanya pengine ndio unaweza kuwa mwisho wa mahusiano yako wewe na Bwana!, pengine ndio njia panda yako ya kuzimu!.. Laiti! Yuda angelijua masaa machache mbele ni nini kitakwenda kutukia, asingelimbusu Bwana!, laiti Samsoni angejua masaa machache mbele hatakaa amwone tena mama yake na Baba yake kwa macho yake, asingemfunulia siri Delila!

Kamwe usiipime nguvu ya dhambi kwa uzoefu!.. Mhubiri mmoja alisema “kamwe usimwogope shetani bali iogope dhambi” hiyo ni kweli kabisa!!.. Kwasababu maandiko hayajasema mshahara ya shetani ni mauti, bali yalisema “mshahara wa dhambi ni Mauti”

Bwana Yesu atusaidie, kila siku tuweze kujitenga na dhambi.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kwanini Yesu aliwaambia wale wakoma wakajionyeshe kwa makuhani?

UTAONA MAMBO MAKUBWA KULIKO HAYA.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

DHAMBI YA MAUTI

Rudi nyumbani

Print this post

Upole ni nini?

Upole ni kitendo cha kutokuonyesha madhara, kwa mtu au kiumbe kingine, huwa unaambatana na utulivu . Upole unakuwa na maana Zaidi pale ambapo unaouwezo wa kuleta madhara kwa kiumbe kingine lakini hutumii uwezo huo, kumdhuru, Kwamfano ni kitu gani kinachomtafautisha nyoka na ng’ombe.

Nyoka ni kiumbe kidogo, dhaifu, hakina miguu, wala mikono, tofauti na ng’ombe, ambaye ni mkubwa, mzito,na mwenye pembe kiasi kwamba ukiwekwa naye katika mapambano ni rahisi kuuliwa naye. Lakini kwanini wewe itakuwa ni rahisi kumkimbilia ng’ombe na sio nyoka?.

Ni kwasababu ng’ombe ni mpole, si rahisi kutumia uweza wake wa pembe, na nguvu zake kukudhuru . Lakini ukimkaribia tu nyoka muda huo huo, atakuuma na utakufa.

Vivyo hivyo na katika wanadamu. Wapo ambao ni wapole lakini wapo ambao si wapole.

Katika biblia ipo mifano ya watu wawili ambao walishuhudiwa kuwa ni wapole. Wa kwanza ni Bwana wetu Yesu Kristo. Na wa pili ni Musa.

YESU KRISTO:

Bwana Yesu mwenyewe alisema.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Alikuwa ni mpole mfano wa mwanakondoo. Na kwasababu ya upole huo, ilimpelekea mpaka Roho Mtakatifu kushuka juu yake kipekee sana kama HUWA (Njiwa). Kumbuka sikuzote njiwa hatui sehemu isiyo na utulivu, wala hawezi kutua juu ya mnyama mkali kama vile mbwa mwitu, Bali anatua juu ya mnyama mpole kama vile kondoo, na ndio maana Bwana Yesu alitambulika kama mwanakondoo wa Mungu.

Hatushangai ni kwanini Mungu alimtukuza namna ile,kwanini leo hii watu wote wanamkimbilia Kristo, ni kwasababu alikuwa mpole sana rohoni. Sio kwamba alikuwa mnyonge, hawezi kuangamiza, au kuharibu watu, kumbuka Anaitwa pia “Simba wa Yuda”, Tunajua tabia za simba sio upole. Lakini yeye alikuja katika upole.. Hiyo ndio sifa kuu ya mtu mpole.

MUSA:

Mtu mwingine tunamsoma katika biblia aliitwa Musa. Utajiuliza ni kitu gani cha kipekee alichokuwa nacho Musa, mpaka kikamfanya awe karibu sana na Mungu kwa namna ile?

Ni kwasababu ya Upole wake, Tunasoma;

Hesabu 12:3 “Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi”.

Musa aliwazidi watu wote waliokuwa duniani kwa upole. Na hiyo ikamfanya awe karibu sana na Mungu, kuliko wanadamu wote walioishi duniani wakati huo.

Hata sasa, kanuni ya Mungu ni hiyo hiyo, Tukitaka tumkaribie Bwana sana, hatuna budi kuwa Wapole.

Tunakuwaje wapole?

Kwanza ni Kwa kujishusha: Unapokubali kuonekana wewe ni dhaifu, ni hatua nzuri sana ya kuelekea upole, Lakini unapotaka kujiona wewe ni Hodari wa mambo yote, ni ngumu kuwa  mpole. Usipokubali kuchungwa, , ujue kuwa utabikia kuwa mbuzi sikuzote na si mwanakondoo

Pili Kwa kuzizuia hasira zetu: Hatuna budi, kuwa watu wa kuvizuia sana vinywa vyetu. Hasira huwa ndio chimbuko la ugomvi na vita. Hivyo ukiweza kudhibiti hasira zako hata kama utaudhiwa kiasi gani, hujibu, basi upole taratibu utaanza kujengeka ndani yako.

Tatu Kwa kusoma Neno na kuomba: Hii ni tiba kubwa sana, ukitaka ujue hesabu soma kitabu cha hisabati, halikadhalika ukitaka uwe na upole, usikwepe biblia. Kwasababu hiyo ndio itakukumbusha, misingi ya kuwa mpole kama Kristo alivyokuwa. Vilevile kusali, kunaukaribisha uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yako, na hatimaye utafikia kiwango hicho.

Bwana atusaidie sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Furaha ni nini?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

TUMAINI NI NINI?

Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?

Rudi nyumbani

Print this post

DORKASI AITWAYE PAA.

Matendo 9:36 “Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa.

37 Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani.

Bwana Yesu asifiwe..

Ulishawahi kujiuliza kulikuwa na umuhimu gani, biblia kueleza tafsiri ya jina la mwanafunzi huyu aliyeitwa Tabitha?. Ukishaona mahali Fulani tafsiri ya jina la mtu inatolewa basi ujue kuna jambo Mungu anataka tujifunze, kwa huyo.

Mfano wa mtu mwingine kama Tabitha alikuwa ni Petro, Ukisoma Yohana 1:42, Bwana Yesu anafunua tafsiri ya jina lake.

Yohana 1:42 “Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).”

Unaona, kulikuwa na sababu ya Bwana kueleza tafsiri ya lile jina kwamba ni Jiwe/mwamba , ikiwa na maana kuwa zipo tabia, ambazo alikuwa  nazo, au atakuja kuzionyesha zinazomwakilisha JIWE KUU mwenyewe ambaye ni Yesu Kristo..

Jambo hilo utalithibitisha mbeleni kidogo, katika Ufunuo alioupata kutoka kwa Mungu, kuhusiana na Bwana wetu Yesu Kristo, tusome;

Mathayo 16:15 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni”.

Umeona akiwa anamaanisha kuwa juu ya mwamba(yaani Ufunuo alioupata kuhusiana na Yesu ni nani), ndio Bwana Yesu atalijengea kanisa lake hapo. Kwahiyo utaona kutolewa tafsiri ya jina lake tangu kule mwanzoni ni kwasababu ya matendo au funuo alizokuwa anazipata kuhusiana na Yesu Kristo, kama msingi wa Kanisa.

Sasa tukirudi kwa Tabitha naye, tafsiri ya jina lake linatolewa, kwamba ni PAA.

Paa, ni aina ya swala. Mwanzoni nilitafakari sana kwanini aitwe swala, asiitwe labda simba, au au kifaru, au dubu, majina yenye sifa, lakini badala yake anaitwa swala.

Je swala anatabia gani nzuri?

Swala ni mnyama ambaye ni mwepesi sana, miguu yake ipo haraka mno, na ni mwepesi wa kurudia juu, kiasi kwamba akikimbia, katika nyasi ndefu au uwanda tambarare, hata simba hawezi kumkamata, mnyama pekee pirini ambaye anaweza kumkimbiza swala (Paa). Ni duma tu peke yake, tena kumpata kwake ni kwa shida sana.

Hivyo hiyo inamfanya, awe salama muda mwingi, akiwa porini.

Katika biblia mashujaa wa Bwana vitani walifananishwa na Paa, Kwamfano mmoja wa mashujaa wakuu wa Daudi aliyeitwa Asaheli alisifika kuwa mwepesi wa miguu kama swala hawa..

2Samweli 2:18 “Na wana watatu wa Seruya walikuwako huko, Yoabu, na Abishai, na Asaheli; na Asaheli alikuwa mwepesi wa miguu kama kulungu”.

“Kulungu, Paa, na Ayala” ni jamii hiyo hiyo moja ya Swala.

Soma pia,

1Nyakati 12:8 “Na wa Wagadi wakajitenga kumfuata Daudi ngomeni huko nyikani, waume mashujaa, watu waliozoea vita, walioweza kutumia ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kama nyuso za simba, nao walikuwa wepesi kama kulungu juu ya milima;

Soma tena;

2Samweli 22:34 “Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu; Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.

35 Ananifundisha mikono yangu vita; Hata mikono yangu yaupinda upinde wa shaba”.

 

Wimbo 8:14 “Ukimbie, mpendwa wangu, Nawe uwe kama paa, au ayala, Juu ya milima ya manukato”.

Sasa mpaka hapo utapata picha ni kwanini Tabitha, aliitwa Paa, ni kwasababu miguu yake ilikuwa ni mepesi katika kutenda matendo mema. Mpaka akasifika katika mji mzima wa Lida, jinsi gani alikuwa tayari kwenda kuwashonea mitume nguo, na kanzu, Pamoja na watakatifu wengine,bila kuombwa wala kuulizwa, Jinsi gani alivyokuwa mwepesi wa kumtolea Mungu. Bila kusukumwa sukumwa, au kukumbushwa kumbushwa, yeye mwenyewe kama swala, alikimbia kutekeleza majukumu yake ya kiutumishi, Zaidi ya watu wote waliokuwa katika ule mji wa Lida.

Hatimaye akafa, lakini watu walimwona kama hastahili kuondoka mapema, watu waliliona pengo  lake lilivyo kubwa, hadi wakati ule Petro, alipokwenda katika mji huo, kulikuwa na maiti nyingi lakini hakuitwa kwa mojawapo ya maiti hizo bali ya Dorkasi tu;

Matendo 9:36 “Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa.

37 Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani.

38 Na kwa kuwa mji wa Lida ulikuwa karibu na Yafa, nao wanafunzi wamesikia ya kwamba Petro yuko huko, wakatuma watu wawili kwake, kumsihi na kusema, Usikawie kuja kwetu.

39 Petro akaondoka akafuatana nao. Alipofika, wakampeleka juu orofani wajane wote wakasimama karibu naye, wakilia na kumwonyesha zile kanzu na nguo alizozishona Dorkasi wakati ule alipokuwa pamoja nao.

40 Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, ondoka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi”.

Hii ni kutufundisha kuwa, ili Mungu awe naye mwepesi kama Swala kutuhudumia, basi na sisi tuonyeshe wepesi wetu kwake. Je sisi nasi ni wepesi wa kutenda matendo mema kama Tabitha? Je tu wepesi kutoa mali zetu na vitu vyetu kwa ajili ya utumishi wa Bwana? Au tu wabinafsi, au mpaka tukumbushwe, au mpaka tulazimishwe, au mpaka tuvutwe vutwe?

Wakati mwingine kwanini, majibu ya maombi yetu yanachelewa?, Ni kwasababu sisi wenyewe sio wepesi kwa Bwana, tunamfanya yeye naye awe mzito.

Tuifanya miguu yetu mepesi, ili wakati wa haja zetu Bwana naye awe mwepesi kutusaidia, kama alivyofanya kwa Dorkasi.

Habakuki 3:19 “YEHOVA, aliye Bwana, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

Ayala, Paa na Kulungu ni wanyama gani?

Kwanini wakristo walipomuona Petro akigonga walisema “Ni malaika wake”?

MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA?.

USIPUNGUZE KUTUMBUIZA!

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI UPIGE MISHALE CHINI?

Ahimidiwe Bwana wetu Yesu Kristo, utukufu na heshima vina yeye milele na milele.Amen

Wakati fulani mfalme wa Israeli aliyeitwa Yehoashi alimfuata Elisha ili kumjulia hali kabla hajafa.

Kama tunavyosoma habari ile  Elisha alimwambia achukue mshale kisha aurushe upande wa mashariki kupitia dirishani. Na alipofanya vile Elisha alimwambia huo ni mshale wa ushindi dhidi ya maadui zake washami..

Hivyo mfalme alipoona vile jinsi alivyopewa maagizo mepesi na yenye uhalisia wa ushindi  kwa tendo la kutupa mishale, hakuwa na shaka yoyote kusikia pengine Elisha atampa maagizo mengine kama hayo, ya kurusha mishale mingine mingi Zaidi ili kuwapiga maadui zake walio karibu naye.

Lakini mambo yalikuwa ni kinyume na mtazamo wake kwani Elisha alimwagiza apige mishale yake ardhini badala ya kuirusha juu, kama alivyofanya hapo kwanza, tendo hilo  likaweka ukakasi kwake “kutupa mishale ardhini”!? pengine alidhani ni mishale inayomrudia yeye.

Tusome..

2 Wafalme 13:14-19

[14]Basi Elisha alikuwa ameshikwa na ugonjwa wake uliomwua; naye Yehoashi mfalme wa Israeli akatelemka amtazame, akamlilia mbele yake, akasema, Baba yangu! Baba yangu! Gari la Israeli na wapanda farasi wake!

[15]Elisha akamwambia, Twaa uta na mishale; naye akatwaa uta na mishale.

[16]Akamwambia mfalme wa Israeli, Weka mkono wako katika uta; naye akaweka mkono wake juu yake. Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.

[17]Akasema, Lifungue dirisha linaloelekea mashariki; akalifungua. Basi Elisha akasema, Piga; akapiga. Akasema, Mshale wa BWANA wa kushinda, naam, mshale wa kushinda Shamu, kwa maana utawapiga Washami katika Afeki hata utakapowaangamiza.

[18]Akasema, Itwae mishale; akaitwaa. Akamwambia mfalme wa Israeli, Piga chini; akaipiga nchi mara tatu, akaacha.

[19]Yule mtu wa Mungu akamkasirikia, akasema, Ingalikupasa kupiga mara tano au mara sita; ndipo ungaliipiga Shamu hata kuiangamiza; bali sasa utaipiga Shamu mara tatu tu.

Umeona, hakujua kuwa ile ya kupiga chini ndio mishale ya ushindi, kinyume chake akawa na hofu matokeo yake akapiga michache tu (yaani mitatu)..

Ni jambo la kawaida hata leo, Mungu anawaagiza watakatifu wake warushe mishale mingi mahali ambapo ni  kinyume na matarajio yao..lakini mashaka yanawaingia, wanaona kama wanafanyakazi bure, na kupoteza nguvu.

Ndugu yangu vita vya kiroho  ukivitazama kwa jicho la mwilini ni rahisi sana kukata tamaa, kwasababu unaweza ukajiona kama unapoteza tu nguvu zako na muda..kama vile kupiga mishale chini..

Unapokuwa katika maombi, usitazamie kuona badiliko lolote la nje labda  mbingu imekuwa  ya blue, au usikie mapanga yakipigwa na malaika katika anga la kwanza hapana..zaidi sana utaona  ni kama siku nyingine tu ya kawaida, umeomba bure, umeuchosha mwili bure. Lakini katika roho umeangusha ngome nyingi sana za ibilisi, tena na kwa jinsi unavyozidi kudumu zaidi na zaidi katika kuomba ndivyo unavyomfukuza shetani mbali nawe kabisa kabisa .

Hivyo hupaswi kukata tamaa au kuacha kuomba kwasababu hiyo mishale ya ardhini ndio yenye mapigo ya Mungu kuliko ile ya juu.

Unaposhea Neno la Mungu na wengine mtandaoni unaweza usione Matokeo yoyote ya kile unachokifanya, lakini wewe endelea Shea sana kwasababu hiyo ndio mishale ya ushindi unayoidharau wewe.

Unapohubiri mitaani au masokoni, unaweza ukaona kama unawapigia tu watu makelele, au watu hawakusikilizi, lakini hiyo ndio mishale ya ushindi katika vita vyako.

Njia za Mungu sio njia zetu. Wewe utarusha juu, yeye atataka urushe chini..huwezi kumpangia kanuni ya vita.

Hivyo tufanyapo jambo lolote la ki-Mungu tusipime-pime sana au kuchunguza-chunguza sana kwa jicho la nje, kwasababu ukifanya hivyo itakuwa ni rahisi kukata tamaa…bali tufanye kile alichotuagiza kwa bidii kana kwamba tunapoteza nguvu zetu bure, na matokeo yake tutakuja kuyaona baadaye katika ulimwengu wa roho.

Ongeza michale yako ya chini.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

Rudi nyumbani

Print this post

Kitambi kilichopo kwenye Ini ndio kilikuwaje?

Jibu: Tusome,

Walawi 3:3 “Naye atasongeza katika sadaka hiyo ya amani, dhabihu kwa Bwana itakayofanywa kwa njia ya moto; yaani, mafuta yafunikayo matumbo, na mafuta yote yaliyo juu ya matumbo,

4 na figo zake mbili, na mafuta yaliyoshikamana nazo, yaliyo karibu na kiuno, na HICHO KITAMBI KILICHO KATIKA INI, pamoja na hizo figo; hayo yote atayaondoa”.

Kulingana na lugha yetu, tumezoea kutafsiri neno “kitambi” kama “tumbo lililotoka nje”..yaani unapotaja kitambi tu!, basi picha ya kwanza kujitengeneza akilini ni “mtu mwenye tumbo kubwa” lakini kiuhalisia neno kitambi tafsiri yake sio tumbo.. bali ni “kitu chochote ambacho kimevimba au kimejaa na kutengeneza mduara”. Pulizo lililojaa upepo au lililojaa maji limetengeneza kitambi! Kwa ule ujazo na ule mduara.

Kadhalika “Ini” linacho “kitambi” na kitambi chenyewe ndio ule mduara wake.. Na ini linatabia ya kuongezeka ukubwa na kupungua kama vile tumbo lilivyo, mtu leo utamwona yupo kawaida kesho atakuwa na kitambi, kadhalika wachunguzi wanasema Ini nayo linakua, hata likipunguzwa baada ya kipindi Fulani linaota tena na kuwa kubwa, (kitambi chake kinaongezeka..)

Bwana alimwagiza Haruni na wanawe kulitwaa Ini, Pamoja na kitambi chake hicho, Pamoja na figo na mafuta yaliyo yaliyoshikamana na viungo hivyo, na kuviteketeza juu ya madhahabu kuwa harufu ya kupendeza kwa Bwana.(Maagizo hayo Bwana aliwapa wakati watu watakapotaka kuleta sadaka za amani mbele za Bwana)

Na kwanini Bwana alivihitaji viungo hivyo vya ndani vichache tu! na si viungo vyote kama miguu, nyama n.k? bali alihitaji tu FIGO na INI?

Ni kwasababu viungo hivyo viwili yaani FIGO, Pamoja na INI vinahusika katika kuchuja sumu inayoingia Mwilini. Mtu au Mnyama akiondolewa FIGO au INI anamuda mfupi sana wa kuishi, kwani atakufa kwa sumu itakayoingia mwilini mwake kwa njia ya chakula au maji!..kwani vyakula tunavyokula vinayo sumu nyingi lakini ini, inavunja vunja ile sumu ya kukibakisha kile chakula salama.

Ikifunua kuwa na sisi tunapomtolea Mungu sadaka za amani kama hizo, basi sehemu ya roho zetu inayohusika na upambanuzi wa roho za uadui, Bwana anaziongoza yeye, tunajikuta tunakuwa na uwezo mkubwa wa kupambanua mabaya na kuyashinda, kadhalika mambo yote mabaya ambayo ni sumu kwetu, tunakuwa tunauwezo wa kuyapambanua.. kama vile Figo na Ini zilivyokuwa na uwezo huo.

Hivyo kuna umuhimu pia mkubwa sana wa kumtolea Bwana, hususani tunapomtolea kwa hiari na si kwa kulazimishwa, kuna baraka nyingi sana za kiroho.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

UTAWALA WA MIAKA 1000.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

Rudi nyumbani

Print this post