Ayala, Paa na Kulungu ni wanyama gani?

Ayala, Paa na Kulungu ni wanyama gani?

Ayala ni mnyama jamii ya swala, ambaye anapatikana sana maeneo ya nchi za barini, wana pembe ndefu zilizotawanyika kama mashina ya miti (Tazama picha juu).

Paa ni jamii ya swala wenye mistari meupe, (Maarufu kama Gazelle kwa lugha ya kiingereza). Paa wanapatikana zaidi maeneo ya ukanda wa joto, kama Afrika. (Tazama picha chini). Na pia kwenye biblia kuna watu waliitwa Paa.

paa

Matendo 9:36  “Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa”.

Na Kulungu pia ni jamii ya swala, ambao nao pia wanapatikana nchi za ukanda wa baridi kama Ulaya. (Tazama picha chini).

kulungu

Wanyama hawa kwa pamoja tunawasoma wametajwa katika biblia katika kitabu cha Isaya..

1Wafalme 4: 22 “Na vyakula vya Sulemani vya siku moja vilikuwa kori therathini za unga wa mzuri, na kori sitini za ngano.

 23 na ng’ombe kumi walionona, na ng’ombe ishirini za malisho, na kondoo mia, pamoja na ayala, na paa, na kulungu, na kuku walionona”.

Sasa kwanini biblia iwataje wanyama hawa?

Kwanza ni wanyama ambao kimwonekano ni wazuri, na wepesi, na pia wana-mbio sana, (soma Habakuki 3:19, Isaya 35:6, Zaburi 18:33, 2Samweli 22:34, na 2Samweli 2:18). simba ni rahisi kumkamata punda milia lakini si swala… Sasa katika roho vijana wanafananishwa jamii ya hawa wanyama wa swala. Vijana wana nguvu na pia kimwonekano ni wazuri kuliko wazee, na pia ni wepesi wa kufanya mambo..

Na ndio maana biblia inatoa maonyo haya..

Wimbo 2: 7 “Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe”.

Maana yake usiwe mwepesi kuruka huko na huko kama kulungu kuzichochea tamaa za mwili, waasherati wote biblia imesema hawataurithi uzima wa milele.

2Timotheo 2:22  “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi”.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Hayawani ni nini katika biblia?

Katika biblia Neno “Mshenzi” linatajwa.Kwanini liwekwe?

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

Nyinyoro ni nini?

Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Yoram Emmanuel wumi
Yoram Emmanuel wumi
10 months ago

Amina

Gerald anthony
Gerald anthony
10 months ago

Amina sana kwa somo hili zuri ambalo lmenisaidia mimi binafsi kuielewa biblia zaid na kuweza kupambanua mambo mengi ya kibiblia. Mungu akubariki sana mtumishi.

Letcia Alphoncr
Letcia Alphoncr
1 year ago

Atukuzwe Mungu kwa kaz njema mnayofanya,ninakua,nataman azidi kunikuza zaid,kwa masomo haya mmefanya nitafute kumjua Mungu sana ndyo kiu