Category Archive Mafundisho

NDOA TAKATIFU NI MKE MMOJA/MUME MMOJA.

Ndoa za wake wengi ni za ibilisi!..ndoa za wake wengi ni za ibilisi!!… ndoa za wake wengi ni za ibilisi!!!. Hali kadhalika ndoa za waume wengi ni za ibilisi, kama tu zilivyo za jinsi moja (zote ni zao la ibilisi).

Zipo hoja kuwa kwasababu Daudi, Sulemani na manabii wengine wakale walioa wake wengi, basi hata leo ni halali kuoa wake wengi.. tena zipo hoja zifananishazo wanyama wa porini na wa kufungwa na uhalali wa kuoa wake wengi.

Hoja zote hizi ni za ibilisi… Ndugu, usiongeze wake, wala wala usiongezee waume.

Bwana YESU alipokutana na yule mwanamke Msamaria kisimani hakumwambia akawalete WAUME ZAKE!.. Ingawa alikuwa ana wanaume wengi (na Bwana alilijua hilo), lakini alimwambia nenda “kamlete mumeo”… ikimaanisha kuwa ndoa halali na takatifu ni ya mume mmoja na mke mmoja.

Sasa Kristo alikuwa anamjua Sulemani, na Daudi..

Yohana 4:15 “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.

16  Yesu akamwambia, NENDA KAMWITE MUMEO, uje naye hapa.

17  Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume;

18  kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli”.

Bwana YESU kabla ya kukutana na huyu mama, alikuwa anamjua Daudi pamoja na Sulemani na idadi ya wake wake waliooa!.. Lakini tunaona hakumwambia huyu mwanamke Msamaria, kwamba akawalete waume zake!!.. Bali alimwambia kamlete mumeo! (maana yake mmoja tu).. bado huoni tu, kuwa ndoa za mitara ni batili na za ibilisi!.

Na tena biblia inasema hapo Mwanzo Mungu alimwumba mwanaume na mwanamke, na si mwanaume na wanawake, au mwanamke na wanaume (soma Mwanzo 1:27 na Mathayo 19:4).

Huoni kuwa ndoa hizo za wake wengi zitakukosesha maji ya uzima!.. Na pia fahamu kuwa ndoa za wake wengi sio zile tu zinazohusisha mtu kuwa na wake wengi katika boma moja kwa wakati mmoja…la! Hata zile za kuacha na kuoa mwingine ilihali yule wa kwanza bado yupo hai.. hiyo ni mitara! Ndicho kilichokuwa kwa huyu mwanamke Msamaria.

Huyu mwanamke msamaria alikuwa na wanaume watano kulingana na darubini ya kimbingu! Ingawa haishi nao, lakini alikuwa nao watano, na anayeishi naye ni wa 6, vile vile kuna watu leo hii wamecha wake zao na kuoa wengine, na kuacha tena na kuoa wengine, (hawa hawana tofauti na wale waliooa wake wawili na kuishi nao wote kwa pamoja).

Na madhara ya ndoa za mitara ni “KUKOSA MAJI YA UZIMA”..

Yapo maji ya Uzima tuyanywayo hapa Duniani, na yapo yale tutakayoyanywa katika mbingu mpya na nchi mpya.

Maji ya Uzima duniani ni YESU KRISTO, tumpatapo yeye tunapata uzima wa milele (Yohana 4:14), lakini ukijiunganisha na hizi ndoa za mitara hawezi kuingia ndani yako!.. vile vile maji ya uzima baada ya maisha haya tutayanywa kutoka katika ule mto wa maji ya Uzima katika mbingu mpya na nchi mpya.

Ufunuo 22:1 “Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo,

2  katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.

3  Wala hapatakuwa na laana yo yote tena. Na kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo ndani yake. Na watumwa wake watamtumikia;

4  nao watamwona uso wake, na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao.

5  Wala hapatakuwa na usiku tena; wala hawana haja ya taa wala ya nuru ya jua; kwa kuwa Bwana Mungu huwatia nuru, nao watatawala hata milele na milele”.

Neema ya Bwana YESU itufunike.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAFUNDISHO YA NDOA.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.

NDOA NI NINI?

KUWA NA  MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.

Rudi Nyumbani

Print this post

FUNDISHO LA BWANA JUU YA KUZALIWA MARA YA PILI.

Jina la BWANA wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia neno la Mungu wetu ambalo ni Taa na Mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Hebu tuangalie uzito wa kuzaliwa mara ya pili kupitia maneno ya BWANA WETU YESU KRISTO.

Yohana 3:1 “Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.

2  Huyo alimjia usiku, akamwambia, RABI, TWAJUA YA KUWA U MWALIMU, UMETOKA KWA MUNGU; KWA MAANA HAKUNA MTU AWEZAYE KUZIFANYA ISHARA HIZI UZIFANYAZO WEWE, ISIPOKUWA MUNGU YU PAMOJA NAYE.

3  Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

4  Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5  Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, MTU ASIPOZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO, HAWEZI KUUINGIA UFALME WA MUNGU”.

Hapa Nekodemo anataja vigezo vya Mtu kuwa na MUNGU kuwa ni “Ishara azifanyazo”…na anamthibitisha Bwana kwa ishara hizo, lakini Bwana anamrekebisha, kuwa “MTU asipozaliwa mara ya pili hawezi kuurithi ufalme wa Mungu (maana yake hawezi kuwa na MUNGU)”… Je! na sisi leo tunalijua hilo??????….Je unalijua hilo??? .

Nikodemo anaona ISHARA ni tiketi ya kuwa na MUNGU,… Bwana YESU anataja KUZALIWA MARA YA PILI ndio TIKETI.. Sasa tuchukue ya nani tuache ya nani?.. Bila Shaka maneno ya BWANA YESU ni hakika, na tena ndio uzima.

Ndugu haijalishi tutakuwa na uwezo wa kufanya miujiza mingi na mikubwa kiasi gani, kama HATUJAZALIWA MARA YA PILI (Maana yake kwa maji na kwa Roho) hatuwezi kuwa na Mungu, kutembea naye wala hatutamwona siku ile.

Mtu anapozaliwa mara ya pili anakuwa kiumbe kipya, maana yake yale maisha ya kwanza ya dhambi yanakuwa hayapo tena maishani mwake.

Kuzaliwa kwa maji ni Ubatizo wa Maji mengi na kwa jina la Bwana YESU na kuzaliwa kwa Roho ni ubatizo wa Roho Mtakatifu (Matendo 2:37-38), mambo haya ndiyo yanamkamilisha mtu baada ya kutubu.

Na anayetuzaa mara ya si mtu bali ni Mungu mwenyewe, na Mungu ni Roho (sawasawa na Yohana 4:24), na tunapozaliwa na Roho, basi tunakuwa watu wa rohoni.

Yohana 3:6 “Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho”

Na kuwa mtu wa rohoni, si kuona maono, au mapepo, bali ni kuzaliwa katika Roho, na Maji. Na sifa kuu ya mtu wa rohoni ni kuushinda ulimwengu (dhambi na mambo mengine ya kidunia).

1Yohana 5:4  “Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu”.

Soma pia 1Yohana 3:9 na 1Yohana 5:18.

Hivyo ukiona tamaa za kidunia bado zinakusumbua kuna uwezekano kuwa bado hujazaliwa mara ya pili, kwasababu wote waliozaliwa mara ya pili wanayo nguvu ndani yao ya kuushinda ulimwengu na ndio watu wa rohoni.

Je ishara ni uthibitisho wa mtu kuwa na Mungu??..jibu ni ndio!, lakini si uthibitisho wa kwanza… bali uthibithsho wa kwanza wa mtu kuwa na Mungu ni KUZALIWA MARA YA PILI. Kwasababu wapo watakaotenda miujiza na kufanya ishara nyingi lakini wasimwone Bwana siku ile sawasawa na Mathayo 7:22.

Kwahiyo kilicho cha msingi kuliko vyote ni “KUZALIWA MARA YA PILI (kuwa kiumbe kipya)”  na mengine ndio yafuate.

Wagalatia 6:15 “Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya“.

1Petro 1:23 “Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Rudi Nyumbani

Print this post

Matangamano ni nini? (Isaya 13:10)

Jibu: Turejee…

Isaya 13:10 “Maana nyota za mbinguni na MATANGAMANO havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze

 “Matangamano” ni “Mkusanyiko wa nyota” unaoonekana na kutengeneza umbile Fulani. Wanajimu baadhi wameyataja matangamano hayo kwa maumbile ya wanyama mbali mbali, kwamfano lipo kundi moja wamelitaja kuwa na umbile kama la N’ge, lingine kama Dubu, lingine kama Simba, lingine mapacha n.k

Kwamfano kundi la nyota lenye umbile kama la Ng’e jinsi linavyoonekana mbinguni kwa macho ya damu na nyama ni kama linavyoonekana kwenye picha hapo juu.. Lakini kwa jinsi lilivyounganishwa na wanajibu mpaka kuleta umbo kama la Ng’e ni kama inavyoonekana hapa chini..

Matangamano ni nini?

Na makundi haya ya nyota, sasa yanatumika kwa unajibu (ambayo ni elimu ya shetani asilimia mia) kwaajili ya utambuzi wa majira na nyakati za watu, Elimu hii kwa jina lingine inaitwa FALAKI, Fungua hapa kwa maelezo Zaidi >>>Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).

Elimu hii wanajimu wanaitumia kutabiri mambo yajayo juu ya mtu, ndio hapo mtu anaenda kusomewa nyota yake na kufanyiwa utabiri, jambo ambalo kiuhalisia ni elimu ya giza, mtu yule anakuwa haambiwi mambo yajayo bali anapangiwa mambo yajayo na ibilisi, akidhani ndio katabiriwa.

Sasa Elimu hizi za Falaki pamoja na ibada zote za jua na mwezi na sayari, Bwana Mungu kazilaani, na siku za mwisho Jua, na mwezi vitatiwa giza, na Nyota zote za mbinguni zitaanguka na Matangamano yote yatazima.. kuonyesha kuwa mambo hayo yaliyotukuka kwa wanadamu si kitu mbele za Mungu, na Bwana atawaadhibu waovu pamoja na ulimwengu, ndivyo maandiko yasemavyo.

Isaya 13:9 “Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.

10 Maana nyota za mbinguni na MATANGAMANO havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.

11 Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali”.

Kuhusiana na unabii wa kufutwa kwa Mwezi, nyota na sayari zote siku za mwisho pitia maandiko haya Yoeli 3:15, Marko 13:24,  Mathayo 24:29, na Ufunuo 6:12.

Kwahiyo ndugu usiende kusoma gazeti kwa lengo la kutafuta utabiri wa nyota, ni machukizo kwa Bwana, usiende kwa waganga ili wakakusafishie nyota, kinyume chake ndio unaenda kuharibu maisha yako, badala yake mfuate Bwana YESU naye atayasafisha maisha yako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MKUU WA GIZA.

UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?

MKUU WA GIZA.

Kwanini Mungu aliupenda ulimwengu?

AGIZO LA UTUME.

Rudi Nyumbani

Print this post

FAHAMU KANUNI ZA KUZISUBIRIA AHADI ZA MUNGU?

Mungu anaweza kuahidi, lakini kama hujui kanuni za kusubiria ahadi za Mungu unaweza usipokee lolote. Kila mmoja wetu amestahili kupokea lolote analo mwomba Mungu endapo ameomba sawasawa na mapenzi yake (yaani sio kwa matumizi mabaya). Yawezekana wewe umeomba Bwana akupe kazi, akupe mke/mume bora, akuponye ugonjwa wako, aikuze  karama yako n.k.

Sasa mahitaji kama hayo na mengine yoyote. Mungu alisema kwenye Neno lake, atatupatia (1Yohana 5:14). Na hivyo inakuwa kwake ni ahadi ambayo lazima aitimize. Kwahiyo wewe unachopaswa kufanya ni kusubiri tu. Kuzingojea hizo ahadi za Mungu kwasababu ni lazima zije. Jifunze tu kungojea.

Maombolezo 3:25 Bwana ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo.  26 Ni vema mtu autarajie wokovu wa Bwana Na kumngojea kwa utulivu

Sasa unazingojea katika mazingira gani?. Hapo ndipo unapopaswa ujue.

Embu tuangalie kwa mtu mmoja ambaye aliahidiwa jambo na Mungu. Na hivyo alikuwa katika mazingira gani, mpaka akalipokea. Mtu mwenyewe si mwingine zaidi ya Simeoni.

Tusome.

Luka 2:25  Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, NAYE NI MTU MWENYE HAKI, MCHA MUNGU, AKIITARAJIA FARAJA YA ISRAELI; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.

26  Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.

27  Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,

28  yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,

29  Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;

30  Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako,

31  Uliouweka tayari machoni pa watu wote;

Wengi wetu tukimtafakari Simeoni, tunatengeneza picha ya mtu Fulani, mzee aliyekuwa anamngoja Mungu tangu ujana wake hadi uzee atimiziwe ahadi yake. Lakini biblia haituelezi katika picha hiyo, inatueleza alikuwa ni “mtu mwenye haki mcha Mungu”. Na tazamio lake lilikuwa ni kuona mkombozi anakuja duniani, Mungu akasikia kiu yake, ndipo akamwambia utamwona.

Ni jambo gani unapaswa ujue?

Kungojea ahadi za Mungu sio tu kusema  ‘Bwana naomba hiki au kile’. Hapana, ni pamoja na kutembea katika haki na kumcha Mungu. Simoni alikuwa hivyo, hakuwa mtu anayetarajia jibu lake, huku anaendelea na udunia kama wengine, huku anaendelea ni anasa kama wanadamu  wengine, huku anaendelea ni uzinzi kama wapagani.

Alidumu muda wote, kuyalea maono aliyoonyeshwa na Mungu, katika hofu ya Kristo. Ndipo wakati ulipofika akaona alichokuwa akikitarajia.

Palilia maono yako uliyomwomba Mungu akutimizie/ au aliyokuonyesha, kwa kutembea ndani ya Kristo. Mche Mungu, kuwa mtu wa rohoni uliyejazwa Roho kama Simoni, tembea katika usafi wa Kristo, kataa udunia, na maisha ya kipagani, kuwa mwombaji.

Ni hakika hilo ulilomwomba Bwana utaliona tu, baada ya wakati Fulani, haijalishi ni gumu/zito kiasi gani, au limepitiliza muda kiasi gani. Utalipokea tu, katika ubora ambao hukuutegemea.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

PALE AHADI ZA MUNGU ZINAPOKUJARIBU.

ZIJUE TABIA ZA AHADI ZA MUNGU KWA MWAMINIO.

KANUNI JUU YA KANUNI.

Rudi Nyumbani

Print this post

USIPENDE USINGIZI USIJE UKAWA  MASKINI.

Mithali 20:13 “Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula”.

Usingizi unaozidi unachelewesha utekelezaji wa majukumu ya muhimu. Kwamfano Mwanafunzi anayelala kupita kiasi ni lazima atakuwa mchelewaji wa shule, vilevile mfanyakazi alalaye kupita kiasi ni lazima atakuwa mchelewaji wa kazini, mfanya biashara anayealala kupita kiasi ni lazima atachelewa kuanza biashara  yake.

Upo usemi usemao “biashara ni asubuhi” maana yake kwa mtu anayefanya biashara labda ya kuuza duka, asubuhi ndio wakati wa kufungua bishara maana watu wengi wanawahi kutafuta bidhaa asubuhi Zaidi ya mchana, hivyo alalapo sana hatapata zile faida za asubuhi, na hivyo yupo hatarini kufilisika.

Atapanga kweli kuwahi kuamka mapema kesho, lakini ifikapo asubuhi kitanda kinakuwa na nguvu kuliko maamuzi yake, atajiongezea muda wa kulala, na mwisho wa siku atashtukia kumeshapambazuka na jua linawaka..na hayo ni matokeo ya kusema “bado kulala kidogo”.

Mithali 6: 9 “Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaondoka lini katika usingizi wako?

10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi!

11 Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha”.

Sasa biblia ni kitabu kilichojaa hekima ya kumwongoza mtu hata katika maisha ya kawaida Zaidi yay ale ya rohoni…. ni kitabu kilichojaa mafunzo mengi mema yahusuyo kanuni za kimaisha na kitabu cha Mithali kimejaa mafunzo hayo.

Hivyo biblia inatufundisha wakristo tuwe na kiasi katika kulala, kwani usingizi unaozidi una matokeo mabaya.. Si kila changamoto inasababishwa na “wachawi”….. nyingine zinatokana na tabia zetu wenyewe.., na hivyo biblia inatufundisha jinsi ya kuepukana nazo, kwamba ni kubadili tu mienendo.

Maana yake ni kwamba, tukitaka kuepukana na “umasikini”  kanuni sio tu “kufunga na kuomba” bali pia ni KUTOUPENDA USINGIZI!. Ukifunga na kuomba na huku unaendekeza usingizi kupita kiasi hakuna matokeo yoyote utakayoyaona.

Maana yake kama ni mfanyakazi basi usiwe mtu wa kupenda kulala mno..Ni kweli hatuwezi kuacha kulala kabisa, lakini kusizidi mipaka, kwani usingizi uliozidi ni zao la ibilisi.

Mithali 19:15 “Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa”

Lakini pia kiroho hatupaswi kulala kabisa, kwani usingizi wa kiroho matokeo yake ni mabaya kuliko ule wa kimwili.. Matendo yote ya giza mtu ayafanyayo ni matokeo ya usingizi wa kiroho..

Mtu anayefanya uzinzi, uasherati, anayelewa pombe, anayeiba, anayetukana, anayesengenya…huyo macho yake yamefumba kwa usingizi mzito.

Je na wewe umo miongoni mwa waliolala kiroho? Basi huu si wakati wa kuendelea kulala, bali wa kuamka na kuyaacha matendo ya giza.

Warumi 13:11 “Naam, tukiujua wakati, kwamba SAA YA KUAMKA KATIKA USINGIZI imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini

12  USIKU UMEENDELEA SANA, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.

13  Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu”

Waefeso 5:14 “ Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza

15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;

16  mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu”.

Bwana atubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.

NYOTA YA ASUBUHI.

Nini maana ya usijiongezee hekima mno? (Mhubiri 7:16b)

Rudi Nyumbani

Print this post

USIPINDUE MAMBO

Masomo maalumu kwa wahubiri.

Isaya 29:16 “NINYI MNAPINDUA MAMBO; Je! Mfinyanzi ahesabiwe kuwa kama udongo; kitu kilichofinyangwa kimnene yeye aliyekifinyanga, Hakunifinyanga huyu; au kitu kilichoumbwa kimnene yeye aliyekiumba, Yeye hana ufahamu?”

Kama Mtumishi/Mhubiri jihadhari na MAPINDUZI yasiyo na msingi!.

USIIPINDUE INJILI YA KRISTO KWASABABU YA TAMAA YA FEDHA.

Unapoanza kuwadanganya watu wa wenye nia ya kumtafuta Mungu, ili tu upate fedha kutoka kwao!.. unapoanza kuwatumainisha watu wa Mungu mambo ya uongo ili tu uwatoe fedha!.. Hiyo ni ishara mbaya na hatari kubwa sana kwako!. Bwana ataenda kukupindua nawe pia!.

Tito 1:11 “Hao WANAPINDUA watu wa nyumba nzima, wakifundisha yasiyowapasa kwa ajili ya mapato ya aibu”.

Ukilipindua Neno la Mungu na kuanza kufanya biashara katika nyumba ya Mungu (ambayo ni wewe mwili wako sawasawa na 1Wakorintho 3:16) kwa kuanza kufanya uasherati na uzinzi na ukahaba fahamu kuwa Bwana naye atakupindua (Soma 1Wakoritho 6:19).

Ukilipindua Neno la Mungu kwa kuiharibu nyumba yake (kama jengo) kwa kuanza kufanya biashara ndani yake na kufanya yasiyofaa Bwana YESU atazipindua meza zako (soma Mathayo 21:12)

Ukilipindua Neno la Mungu juu ya utakatifu wa mwilini na rohoni (sawasawa na 1Wathesalonike 5:23) na kuanza kufundisha/ kuhubiri kuwa Mungu haangalii mwili bali anaangalia roho tu peke yake ni kupindua maandiko ambako matokeo yake ni Mungu kuyapindua maneno yako na wewe kwa ujumla.

Mithali 22: 12 “Macho ya Bwana humhifadhi mwenye maarifa; Bali HUYAPINDUA MANENO YA MTU HAINI”

Ukilipindua Neno la Mungu na kuanza kuhubiri kuwa  YESU KRISTO bado sana arudi, au kwamba hakuna mwisho wa dunia, huko ni kupindua mambo ambako matokeo yake ni mabaya kama ya Fileto na Himenayo.

2Timotheo 2:17 “na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto,

18  walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata KUIPINDUA imani ya watu kadha wa kadha”.

Kama Mhubiri Ni heri KUPINDUA ulimwengu kwa mambo ya kweli ya INJILI kama walivyofanya Mitume wa kanisa la kwanza  kuliko kuigeuza/kuipindua injili kwa faida zetu wenyewe.

Matendo 17:6 “na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa WALIOUPINDUA ULIMWENGU WAMEFIKA huku nako”

Siku ya Mapinduzi makuu inakuja, ambapo Bwana ataipindua dunia yote kama alivyoipindua miji ya Sodoma na Gomora (soma Kumbukumbu 29:23) na kipindi cha gharika ya Nuhu (Soma Ayubu 12:15).

Ezekieli 21:27 “NITAKIPINDUA, NITAKIPINDUA, NITAKIPINDUA; hiki nacho hakitakuwa tena, hata atakapokuja yeye ambaye ni haki yake; nami nitampa”

Hegai 2:22 “nami nitakipindua kiti cha enzi cha falme, nami nitaziharibu nguvu za falme za mataifa; nami nitayapindua magari, na hao wapandao ndani yake; farasi na hao wawapandao wataanguka chini; kila mtu kwa upanga wa ndugu yake”.

Usipindue Mambo yaliyonyooka, bali pindua yale yaliyopotoka.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIJANA NA MAHUSIANO.

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

IMANI “MAMA” NI IPI?

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

Rudi Nyumbani

Print this post

SIFA ZA MAMBA YULE MKUBWA WA AYUBU.

Katika Ayubu 41, tuona Mungu akieleza kwa urefu sifa ya mnyama mamba.

Ametumia taswira ya mamba huyu tunayemwona, kumwelezea mamba wake wa  rohoni, ambaye hasaa Ayubu alionyeshwa habari zake kwa urefu kupitia sura hii.

Na ndio maana kuna sifa nyingine ukizisoma hapo, huwezi kuziona kwa mamba huyu tuliye naye sasa, lakini Mungu hupenda kutumia mifano halisi walau tupate taswira wa kile alichokimaanisha. Ndio maana akaweka sifa chache kwenye mambo wetu huyu ili tumwelewe.

Sasa katika sura hii, Mungu anaanza kwa kumwonyesha Ayubu jinsi anavyomtofautisha sana mnyama mamba na viumbe vingi mbalimbali vilivyopo duniani, kuanzia vya kwenye maji kama vile samaki, mpaka vile vile vya angani kama  vile ndege, hadi wanyama wa kufugwa kama ng’ombe na wale wa mwituni kama vile simba.. Hawa wote hakuna aliyelinganishwa naye.

Mungu anamwonyesha ukali  mwingi alionao, nguvu alizonazo, ugumu ulio katika ngozi yake, kiasi cha mkuki wowote kushindwa kupenya kwenye ngozi yake, zaidi sana ujasiri alioumbiwa. Kwa ufupi kulingana na habari hii hakuna mnyama aliyeweza kulinganishwa na huyu duniani kote.

Sasa embu soma hizi sifa, na mwishoni utamjua mamba huyo ni nani, na uzao wake ni upi. (Zingatia maneno yaliyoandikwa kwa herufi kubwa)

Ayubu 41

1 Je! Waweza wewe KUMVUA MAMBA KWA NDOANA? Au, kuufunga ulimi wake kwa kamba?  2 Je! Waweza kutia kamba puani mwake? Au kutoboa taya yake kwa kulabu?

3 JE! ATAKUSIHI SANA? Au, atakuambia maneno ya upole?  4 Je! Atafanya agano pamoja nawe, UMTWAE KUWA MTUMISHI WAKO milele?

5 Je! UTAMCHEZEA kama ndege? Au, kumfunga kwa ajili ya wasichana wako?  6 Je! Vikosi vya wavuvi watamfanyia biashara? WATAMGAWANYA kati ya wafanyao biashara?

7 Je! Waweza kuijaza ngozi yake na vyuma vyenye ncha, Au kichwa chake kwa vyusa?  8 Mwekee mkono wako; Vikumbuke vile vita, wala usifanye tena.

9 Tazama, kumtamani ni bure; Je! Hatambwaga chini huyo atakayemtazama?  10 HAPANA ALIYE MKALI HATA AKATHUBUTU KUMWAMSHA; Bali ni nani awezaye kusimama mbele yangu mimi?  11 Ni nani aliyetangulia kunipa hata nimlipe? Kila kilicho chini ya mbingu nzima ni changu.

12 Sitanyamaa kusema habari za via vyake, Wala nguvu zake kuu, wala umbo lake zuri.  13 Ni nani AWEZAYE KUMBAMBUA MAGAMBA YAKE? NI NANI ATAKAYEPENYA DIRII YAKE MARADUFU?  14 Ni nani awezaye kuifungua milango ya uso wake? Meno yake yatisha kandokando yake.

15 Magamba yake yenye nguvu ndiyo fahari yake, Yamefungamana pamoja kama kwa kufungwa kwa muhuri.  16 Jinsi yalivyoshikamana Hata upepo hauwezi kupita kati.  17 Yamefungamana pamoja; Yameshikamana, hata hayawezekani kutengwa.

18 Kwa kuchemua kwake mwanga humemetuka, Na macho yake yanafanana na makope ya alfajiri.  19 MIENGE IWAKAYO HUTOKA KINYWANI MWAKE, NA MACHECHE YA MOTO HURUKA NJE.  20 MOSHI HUTOKA KATIKA MIANZI YA PUA YAKE, Kama nyungu ikitokota, na manyasi yawakayo.

21 Pumzi zake huwasha makaa, Na miali ya moto hutoka kinywani mwake. 22 Katika shingo yake hukaa nguvu, Na utisho hucheza mbele yake.  23 Manofu ya nyama yake hushikamana; Yanakazana juu yake; hayawezi kuondolewa.

24 MOYO WAKE UNA IMARA KAMA JIWE; Naam, imara kama jiwe la chini la kusagia.  25 Anapojiinua, mashujaa huogopa; Kwa sababu ya woga wao huvunjwa moyo.  26 Mtu AKIMPIGA KWA UPANGA, HAUMWINGII; Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha.

27 Yeye huona chuma kuwa kama nyasi, Na shaba kama mti uliooza.  28 Mshale hauwezi kumkimbiza; Na mawe ya teo kwake hugeuka kuwa kama makapi.  29 Marungu huhesabiwa kama mabua; Naye hucheka mshindo wa mkuki ukitupwa.

30 Pande zake za chini ni kama vigae vikali; Hutandika malazi kama kuweka chombo cha kupuria nafaka juu ya matope.  31 Yeye huchemsha kilindi mfano wa nyungu; Hufanya bahari kuwa kama mafuta.

32 Hufanya mapito yake kung’aa nyuma yake Hata mtu angedhani kilindi kina mvi.  33 JUU YA NCHI HAPANA ALIYEFANANA NAYE, ALIYEUMBWA PASIPO OGA.  34 Yeye hutazama kila kitu kilicho juu; Ni mfalme juu ya wote wenye kiburi.

Mamba huyu si mwingine zaidi ya BWANA YESU KRISTO.!

Hakuna ufalme, au mwanadamu, au mamlaka iliyoweza au inayoweza kuutetemesha ufalme wa Kristo, zaidi dunia nzima humuhofu. Yeye sio samaki, yeye ni zaidi ya mamba.

Lakini pia anao uzao wake tofauti na uzao wa viumbe vingine. Na watoto wake watafanana na yeye, ndio wale waliomwamini. Ndio maana ukimpokea Kristo kwa kuzaliwa mara ya pili, unakuwa mtu mwingine kabisa duniani, kwasababu asili yake  inakaa ndani yako.

Ndugu, utaishi kinyonge hapa duniani, mapepo yatakusumbua, dunia itakusumbua kwasababu wewe ni dhaifu, na utaendelea kuwa dhaifu tu kama visamaki vingine vinavyovuliwa-vuliwa tu ovyo na ndoano. Lakini ukimpokea Kristo maishani mwako. Wewe ni mtu mwingine.Rohoni unaogopeka mno.

Embu leo tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, mwambie Yesu naufungua moyo wangu, ingia ndani yangu, na hakika ataingia, na kukusamehe dhambi zako zote, kama hakikisho la uzima wa milele . Atakufanya kiumbe kipya, hakikisha tu unamaanisha kusema kimatendo kuanzia leo YESU ni wangu, mimi ni wake. Hilo tu, kisha nenda ukabatizwe ikiwa hukubatizwa. Baada ya hapo asili yako itabadilishwa. Uwe mamba, umiliki na kutawala sio samaki.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Neno “Via” linamaanisha nini katika biblia?

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

Yesu kuvishwa taji la miiba kichwani, kulifunua nini?

Rudi Nyumbani

Print this post

MIMI NA WEWE TU KAZI YA MUNGU.

Waefeso 2:10

MAANA TU KAZI YAKE, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno ya uzima.

Mimi na wewe kama vile maandiko yanavyosema hapo, ni  “kazi ya Mungu”..Hivyo ni lazima kujua kama ni  kazi ya Mungu basi ni lazima pia tumekusudiwa kutimiza jukumu fulani hapa duniani.

Kwamfano unapoona gari, unasema lile ni kazi ya mtu sio mbuzi.. Na kama ni kazi yake, basi kuna wajibu fulani nyuma yake ambao liliumbiwa lifanye. Na wajibu wenyewe ni kumsafirisha mtu au vitu kwa haraka na wepesi.

unapoona nyumba, tunasema ni kazi ya mtu,  imejengwa kuwa makao ya kupumzika, haijajengwa tu, bila kusudi lolote duniani.

hata unapoona kiota, ile ni kazi ya ndege kakijenga sio kiwe tu pale kama takataka, bali aishi ndani yake.

Vivyo hivyo na sisi ni kazi ya Mungu tuliumbwa kutimiza kusudi fulani. Hivyo ni lazima ujue, na kusudi lenyewe ni KUTENDA MATENDO MEMA.

Sisi ni vyombo mahususi, Mungu alivyovikusudia kudhihirisha matendo mema, ambayo aliyaumba tangu mwanzo yatendwe, hakuna chombo chochote chenye uwezo wa kufanya hivyo isipokuwa mwanadamu.

Waefeso 2:10

MAANA TU KAZI YAKE, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Sasa wewe kama mtu usipojua wajibu wako hapa duniani, utakuwa hatarini kuangamizwa. Ni sawa na TV isiyoonyesha kitu, gari lisilotembea, pasi isiyotoa moto. ni wazi kuwa vitatupwa kama sio kuwekwa kwenye karakana.

Na wewe vivyo hivyo, fahamu kuwepo kwako duniani ni kutenda matendo mema. ndio kusudi lako

Sasa, si matendo mema, ilimradi matendo mema…hapana…yapo matendo mema, lakini yasiwe na nguvu mbele za Mungu, hayo ndio yale ambayo mataifa huyafanya..lakini matendo mema tunayoyazungumzia hapa ni yale yaliyo ndani ya YESU KRISTO. Ndio maana hapo anasema tuliumbwa katika Kristo Yesu, sio katika Adamu, au Ibrahimu, au nabii fulani bali Kristo Yesu..maana yake matendo ya Yesu, (au kwa namna nyingine tabia za Yesu) ambayo hakuna mwingine awezaye kuyatenda isipokuwa mtu huyo amezaliwa mara ya pili.

Hivyo leo tutatazama aina ya matendo hayo mema ambayo wewe kama mwana wa Mungu huna budi kuyadhirisha uwapo duniani.

  1. UPENDO

Upendo wa Kristo, sio kama upendo wa kiulimwengu, ule ambao, unawapenda wakupendao hapana..mbele za Mungu hapo bado hujafanya tendo la upendo, huo ni mwanzo tu.

bali ni ule wa kupenda wanaokuudhi, lakini sio kupenda tu, unafikia hatua ya kuwaombea, na unapofikia kilele chake unaweza hata kuutoa uhai wako kwa ajili yao.

Mathayo 5:43-48

[43]Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

[44]lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

[45]ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

[46]Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

[47]Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

[48]Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.

Huu unaitwa upendo wa agape. Mimi na wewe lazima tufanye bidii tuudhihirishe. Ndio ulioumbiwa tangu mwanzo uuonyeshe kwa wengine. Epuka mafundisho ya piga adui zako, kumbuka wewe ni kazi ya Mungu, kuonyesha upendo.

  1.  UTAKATIFU

Yesu alisema haki yenu isipozidi ya waandishi na mafarisayo, hamtaingia kamwe katika  ufalme wa mbinguni.

Mathayo 5:20

[20]Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

Mafarisayo walikuwa hawana Roho Mtakatifu, hivyo mambo yote waliyatimiza kwa nguvu lakini haikusaidia kuondoa tamaa za mwili. walikuwa hawazini lakini mioyo yao ilikuwa na tamaa. Lakini Yesu alitoa  mizizi ya uzinzi, ndani ya mtu kwa Roho wake mtakatifu anayempa.

Ndio maana kwanini unapaswa ujazwe Roho, lakini pia utembee kwa Roho Mtakatifu ili uweze kuushinda mwili, vinginevyo hutaweza kwa nguvu zao, utafanya kinafiki. Biblia inasema..

Wagalatia 5:16-17

[16]Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

[17]Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

Ni lazima ujifunze utii wa Neno la Mungu, kwa kujikana nafsi, na kumfuata Yesu, wakristo wengi hawajikani nafsi, wanakiri wokovu lakini gharama zake hawataki kuingia, wamesilibiwa kweli msalabani lakini hawataki kufa, hawataki kuvunjwa vunjwa miguu yao wafe,. Ukiingia kwa Kristo kubali kufa ili akuhuishe,  ndivyo utakavyoweza kuushinda ulimwengu, kubali kusema bye! bye! kwa ulimwengu. Utaona tu jinsi gani utakavyoweza kuishi maisha matakatifu bila shida yoyote. Roho Mtakatifu huwa anapata nguvu ya kumbadilisha mtu pale ambapo anakubali kujikana kweli nafsi. lakini kama hataki, Mungu kidogo, udunia kidogo, utaendelea kuwa vilevile tu kama mafarisayo na waandishi, ambao vikombe vyao havijasafishwa kwa ndani.

Wewe ni kazi ya Mungu umeumbwa uwe mtakatifu kama yeye alivyo mtakatifu. Kubali tu kuongozwa na Roho kwa kujikana nafsi.

1 Petro 1:16

[16]kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

3) KUHUBIRI HABARI NJEMA.

Yesu alipokuja duniani, alitambua kuwa vinywa vyetu viliumbwa mahususi, kuwafundisha na kuwaekeza wengine njia iliyo sahihi. Ndio maana mapema tu, alianza kuhubiri na kufundisha katikati ya vijiji na miji, habari za ufalme..Huoni hayo ni matendo mema?

Warumi 10:15

[15]Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!

Halikadhalika hatuna budi kufahamu agizo la sisi kuhubiri, ndilo tuliloumbiwa na Mungu tangu mwanzo tulifanye..ndio agizo kuu. Jambo ambalo lipo kwa wakristo tu. Ni mpango ambao Mungu amekusudia kuutumia kuzungumza, kuponya, kufungua watu kupitia watu hao hao.

Sasa ikiwa wewe umeokoka halafu, huna habari ya kuwashuhudia wengine Injili, fahamu kuwa wewe, sio kazi ya Mungu, uliyeumbwa katika Kristo Yesu. Bali ni kazi ya mwingine.

Amka sasa, ondoa woga na uvivu wa kuwatangazia wengine Kristo, usiwe chombo kibovu, anza kuwatangazia wengine wokovu, uwezo huo upo ndani yako, kushuhudia hakuhitaji elimu yoyote ya biblia au vifungu elfu vya kwenye maandiko, ni kueleza ushuhuda wa maisha yako matendo makuu Kristo aliyokutendea, ushuhuda huo unatosha kumgeuza mwingine, kabla hujafikiria kutoa vifungu anzia kwanza hapo. Ndicho alichokifanya yule kichaa aliyetolewa pepo, Yesu alimwambia nenda kwenu kawashuhidie watu matendo makuu Mungu aliyokutendea, na  kwa kupitia ushuhuda wake taifa zima la Dekapoli likamwamini Kristo, mwanamke msamaria, kusikia tu habari zake zinafichuliwa akaenda kuwaleza watu, samaria yote ikaamini. Hakuna haja ya kuwa na hofu, anza sasa kuwashuhudia ndugu zako.

Wewe ni kazi ya Mungu, umeumbwa ili uhubiri.

4) IMANI

Vilevile Matendo ya imani, tuliumbiwa sisi tangu mwanzo tuyadhihirishe, na ndio maana hatumwoni Mungu kwa macho, tofauti na malaika, kwasababu tumetengenezwa kwa namna hii, haiwezekani wewe kumpendeza Mungu pasina imani.

Waebrania 11:6

[6]Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.

Lakini imani yetu, haina budi kuzidi ile ya watu wa kidunia, ya kwetu huzaliwa na Neno la Mungu, nguvu ya Mungu iliyo katika msalaba wa Yesu.

tukiumwa tunaamini hakika, Yesu alishayachukua magonjwa yetu, huzuni zetu, umaskini, hatuna mashaka kwasababu Yesu alishayamaliza yote. Hatupaswi kuwa na hofu ya maisha, Yesu mwokozi wetu ameshayamaliza.

Kuwa mtu wa imani, liweke Neno la Mungu kwa wingi ndani yako. Mtegemee Kristo, amini kazi zake. Usiishi kwa kuona.

5) MAOMBI

Maombi ni mawasiliano. Sisi kama kazi yake anatazamia, tuwe watu wa kumtegemea kwa asilimia mia, maombi yapo ya aina mbalimbali, sifa ni moja ya maombi, ibada ni aina ya maombi,

Ndio maana Yesu alipokuja duniani, maombi yalikuwa ni sehemu ya maisha yake. Aliomba zaidi ya watu wa kidini, alikesha, akawataka na mitume wake wafanye vile, alisema ombeni nanyi mtapewa, ombeni bila kukoka, dumuni katika sala. (Mathayo 26:41, Wakolosai 4:2)

Wewe ni manukato ya Mungu, Mungu anataka kusikia harufu yako nzuri. Na harufu yenyewe ni Maombi yako.

Ufunuo 5:8  Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu

Vilevile fahamu maombi ni mahali ambapo unampa Mungu nafasi ya kukukarabati wewe kama chombo chake uweze kuzifanya kazi zake vyema. Vilevile Haiwezekani mwanadamu uliyeumbwa kwa mfano wa Kristo kwa wokovu uepuke maombi. Ukifa kimaombi, ni umekufa kiroho, huwezi kuzitenda kazi za Mungu.

6) UMOJA.

Jambo lingine ambalo Mungu anatazamia alione kwako, ni wewe kudhihirisha umoja wa Roho ndani ya mwili wa Kristo. (Waefeso 4:3)

Yesu alisema .

Yohana 17:11, 21

[11]Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. … [21]Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA.

Lengo la kufikia umoja ni ili ulimwengu umwamini Kristo. Mahali ambapo tunashindwa kupaelewa sisi kama kazi ya Mungu ndio hapo, yaani kila mtu anataka awe kivyake, au wazo lake liwe bora, tukidhani ndio tuliombwa tuishi hivyo..

halitawezekana, endapo hutatambua nafasi zetu katika mwili wa Kristo ni ipi, kama Mungu hajakupa uongozi, kwanini ung’ang’anie nafasi hiyo?

kuwa katika utumishi wa chini, hakukufanyi karama yako kudidimia, Mungu alimtoa Daudi mazizini, vivyo hivyo yule aliyemkusudia atamwinua tu popote lakini sio kugombani au kumwonea wivu mwenzako awapo kwenye nafasi fulani, hivyo ili tuufikie umoja wa Roho ni kukubali kujishusha kwa kuongozwa, na kufundishwa, na kuridhika na ulichokirimiwa na Bwana.

Tukizangatia matendo hayo. Basi tutakuwa ni vyombo bora, vinavyostahili kutumika kwa kazi rasmi za Mungu ambazo bado hazijafuniliwa..Zitafunuliwa katika huo ulimwengu ujao, Huko ambako jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.

Jiulize je! Wewe ni chombo kamilifu cha Kristo?

2 Timotheo 2:20-21

[20]Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina.

[21]Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, KIMETENGENEZWA KWA KILA KAZI ILIYO NJEMA.

Hayo ndio matendo yetu mema, yatokayo kwa Kristo Yesu, sio ulimwengu. Fanya bidii kuyatoa ndani yako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SI SHETANI BALI NI WEWE. (CHAGUA MEMA)

Ni kama machungwa katika vyano vya fedha.

“Vya Kaisari mpeni kaisari”  ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?.

Rudi Nyumbani

Print this post

VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu, (Mkuu wa Uzima na Mfalme wa wafalme), YESU KRISTO libarikiwe. Karibu tujifunze Neno la Mungu wetu lililo taa na Mwanga wa njia zetu (Zab. 119:105).

Kiashiria cha Kwanza ni UTAKATIFU:

kwamba Roho Mtakatifu yupo ndani yako (au umebatizwa na Roho Mtakatifu) ni UTAKATIFU, angalia maisha yako, je dhambi imekuwa hafifu kiasi gani, ukijilingalisha na kipindi cha nyuma.. Ukiona kuna nguvu kubwa ndani yako ya kushinda dhambi, basi tambua kuwa si wewe, bali ni uwepo wa nguvu za Roho Mtakatifu ndani yako.

Kiashairia cha Pili ni KARAMA:

Karama maana yake ni ile shauku/msukumo  wa kumtumikia Mungu katika eneo Fulani, ambao unakutofautisha na mwingine.. Ukiona una shauku kubwa ya kumtumikia Mungu, na ukiangalia shauku hiyo huioni kwa mwingine aliye karibu na wewe, au ukijaribu kumweleza mwingine ni kama hakuelewi, basi fahamu kuwa hiyo shauku si wewe, bali ni Nguvu/msukumo wa Roho Mtakatifu ndani yako. (ndio maana zinaitwa karama za roho, 1Wakorintho 12:1)

Kiashiria cha Tatu ni KUCHUKIWA/KULAUMIWA BILA SABABU:

Si kila lawama ni ishara mbaya: Ukiona kila unalolifanya la KiMungu linazua lawama, au shida mahali ulipo..basi hiyo pia ni ishara nyingine ya uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yako..

1Petro 4:14 “MKILAUMIWA kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia”.

Kiashiria cha Nne: KUPUNGUA KWA HOFU NDANI YAKO.

Ukiona hofu imeisha ndani yako, kiasi kwamba wakati  wengine wana wasiwasi kuhusiana na mambo Fulani wewe huna wasiwasi hata kidogo, na unajihisi kabisa kuwa Mungu yupo na wewe, basi fahamu kuwa kuna uwepo wa Nguvu za Roho Mtakatifu ndani yako, na si wewe kwa akili zako (kwasababu kwa akili za kawaida, hakuna mtu mwenye akili timamu asiyetishwa na misukosuko ya maisha).

Kiashiria cha Tano: FURAHA.

Ukiona kuna furaha isiyoelekeza ndani yako kila unapofikiria habari za YESU, na wakati mwingine unatamani kumweleza mwingine, na ukijaribu ni kama haoni kama unavyoona, basi fahamu kuwa si wewe hisia zako, bali ni nguvu za Roho Mtakatifu ndani yako, Wagalatia 5:22.

Kiashiria cha Sita: MFULULIZO WA MAFUNUO.

Ukiona kila unapotembea unamwona YESU katika neno lake, au unauona uweza wa YESU, ambao unakuletea changamko Fulani, na msisimko wa kipekee, ambao huoni kwa mwingine, basi tambua kuwa ni kazi za Roho Mtakatifu hizo ndani yako.. kwani kwa kawaida macho yaliyofumbwa hayawezi kumwona YESU popote wala kuuona uweza wake.

Vile vile ishara hii inaambatana na kupata ufahamu wa maandiko kwa namna ya kipekee sana.

SASA UFANYE NINI UNAPOGUNDUA KUWA ROHO MTAKATIFU YUPO NDANI YAKO?

  1. USIMZIMISHE ROHO (1Wathesalonike 5:19)

Kumzimisha Roho Mtakatifu ni kitendo cha kumfanya Roho Mtakatifu aondoke ndani yako na kukaa mbali nawe aidha kwa muda kwa muda au moja kwa moja.. na vitu vinavyomzimisha Roho Mtakatifu ni dhambi za makusudi…kama uzinzi, wizi, ibada za sanamu na kupenda mambo ya kidunia.

Mambo haya mtu akiyafanya Roho Mtakatifu anaondoka ndani yake, na ile nguvu ya kushinda dhambi inaondoka ndani yake, vile vile ile nguvu ya kushinda hofu pia inaondoka ndani yake.

  1. USIMHUZUNISHE ROHO (Waefeso 4:30)

Kumhuzunisha Roho sawasawa na Waefeso 4:30, ni kitendo cha kumfanya Roho Mtakatifu asifurahiwe na wewe, na matokeo ya kumhuzunisha Roho Mtakatifu kwa muda mrefu, ni kuondoka ndani ya mtu.

Mambo yafuatayo yanaweza kuwa sababu ya Roho Mtakatifu kuhuzunika ndani yetu..

1. Tabia ya kukosa Imani…kama vile Bwana YESU alivyohuzunishwa na wanafunzi wake mara kadhaa, pale walipokuwa wanapungukiwa na Imani, mpaka kufikia hatua ya kuwaambia mara kwa mara “Imani yenu iko wapo”

Vile vile na sisi tunapopungukiwa na Imani katika mazingira tukutanayo hiyo Roho Mtakatifu anaugua ndani yetu, hivyo hatuna budi kuwa watu wa Imani daima.

Na Imani chanzo chake ni kusikia Neno la Mungu, (ambayo tafsiri yake ni kusoma na kujifunza biblia). Neno la MUNGU linapokaa kwa wingi ndani yetu pamoja na maombi basi viwango vyetu vya Imani vinakuwa na hivyo tunakuwa katika hali ya kumpendeza Roho Mtakatifu.

2. Tabia ya uvivu wa kiroho.. Ukiwa mlegevu kutenda yakupasayo, Roho Mtakatifu anaugua kwasababu hutumii kile ulichopewa,

Kama viashiria hivyo havipo ndani yako basi huenda Roho MTAKATIFU bado hajaingia ndani yako, au amesogea pembeni, na hiyo si kwasababu wewe ni mbaya, au una kasoro, au wengine ni bora kuliko wewe mbele zake, LA!..bali ni kwasababu bado hujafungua mlango, au ulikuwa hujui jinsi ya kuufungua mlango..kwasababu yeye anatamani aingie ndani yako Zaidi hata ya wewe unavyotamani.

Sasa swali la msingi, unaufunguaje mlango ili aingie ndani yako?

Kanuni ni rahisi sana, isiyogharimu hata theluthi ya senti moja.. na kanuni  yenyewe ni kukiri tu makosa yako, kwamba wewe ni mwenye dhambi na hivyo unahitaji msaada wake (kutubu) kwa kumaanisha kabisa kuacha mambo yote mabaya.., na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU, kama bado ulikuwa hujabatizwa, baada ya hapo yeye mwenyewe ataingia ndani yako, na utaona matunda hayo na mengine Zaidi ya hayo..

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39  Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”

Kama haujabatizwa na utahitaji msaada huo, basi waweza wasiliana nasi kwa namba zilizoanishwa hapa chini na tutakusaidia juu ya hilo.

Ubarikiwe sana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FAHAMU VIASHIRIA VYA MTU ALIYESAMEHEWA DHAMBI ZAKE.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

IMANI “MAMA” NI IPI?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

UJIO WA BWANA YESU.

Rudi Nyumbani

Print this post

JE! NI CHEMCHEMI IPI INATOKA NDANI YAKO, YA MITO AU YA KISIMA?

Mtu yeyote aliyeokoka, ndani ya moyo wake kunatokea chemchemi ya maji  yaliyo hai (Mithali 4:23). Na maji hayo huwa hayakauki, kwasababu yanatoka kwenye chanzo chenyewe  halisi ambacho ni Yesu Kristo,

Na Kama vile tunavyojua maji hufanya kazi zisizopungua nne.

  1. kukata kiu,
  2. kumeesha,
  3. kusafisha,
  4. na kugharikisha pale yanapozidi,

Ndivyo ilivyo kazi ya maji haya  katika moyo wa mtu, hukata kiu ya mambo maovu(Ufunuo 21:6, Yohana 4:14), humeesha mambo mema ya Mungu , husafisha moyo wa mtu, lakini pia  hugharikisha kazi za Yule  mwovu.

Ndio maana maandiko yanasema pepo limtokapo mtu hupitia mahali pasipo na maji, ni kwanini? Ni kwasababu eneo lenye maji  rohoni, haliwezi pepo hawezi kukaa anaona gharika, na mafuriko makubwa hawezi kusogelea hapo. Na eneo lenye maji ni moyo wa mtu aliyeokoka.

Luka 11:24  Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika; asipoona, husema,

25  Nitairudia nyumba yangu niliyotoka

26  Hata afikapo, akaiona imefagiwa na kupambwa, ndipo huenda akachukua pepo wengine saba, walio waovu kuliko yeye mwenyewe, wakaingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza

Sasa wengi wetu hatujui kuwa hayo maji, yanakuwa kama maji ya “KISIMA” tu, ambayo hutulia pale pale, ni neema ya bure ambayo kila mwamini amepewa. Lakini ili ayafanye maji hayo kuwa “MITO” yaani yatiririke mbali. Si jambo la kusema tu nimeokoka. Bali kitu cha ziada lazima kifanyike kwenye maisha ya mtu.

Kama tunavyojua mito, huenda mbali kuwasaidia, hata watu wasiojua chanzo chake kilianzia wapi, Kwamfano mamilioni ya  wakazi wa mji wa Kilimanjaro, kutegemea maji yanayotiririka kutoka katika mlima wa Kilimanjaro, Na ni wazi wengi wao hawajui chanzo ni mwamba gani. Lakini wananufaika. Hata Pale Edeni Mungu alitoa mto katikati ya bustani, lakini haukuishia pale bali ulitoka mpaka nje ya bustani, kuyanufaisha mataifa. (Mwanzo 2: 10-14)

Vivyo hivyo ili na wewe yale maji uliyoyapokea siku ulipookoka, kama chemchemi ya kisima, unataka yatoke nje, huna budi kufanya jambo lingine la ziada.

Ndio maana mitume walishindwa kulitoa lile pepo sugu, wakijiuliza kwanini, ndipo   Bwana Yesu alisema maneno haya

Mathayo 17:21  [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]

Ni nini hiyo haitoki?

Ni maji yaliyo ndani yako. Kubadilika na kuwa mito, ni lazima uingie gharama za kuwa mwombaji. Si kuomba tu bali Kuomba bila kukoma. Mwombaji yoyote huuvutia uwepo wa Mungu maishani mwake. Maombi ni ‘pump ‘ya Mungu inayoyavuta yale maji nje! Yakawasaidie wengine. Huwezi kuwa mtu wa mafunuo kama huna desturi ya kuomba, huwezi kuwasaidia wengine rohoni, hata kuwaombea wasaidike, kama wewe si mtu wa kuomba. Unatazamia mumeo aache pombe, halafu sio mwombaji, utapona tu wewe peke yako, lakini hutaweza kumponya mwingine. Unatazamia familia yako iokoke, halafu wewe mwenyewe huingii gharama za mifungo na maombi, yasiyo koma, mara kwa mara, zitakuwa ni ndoto tu, labda Mungu awaguse kwa njia zake mwenyewe, lakini sio kwa matamanio yako.

Na si tu katika eneo la kuwasaidia wengine, bali hata katika maeneo ya maisha yako ambayo unataka uone maingilio Fulani ya Mungu makubwa. Huna budi kuyatoa hayo maji yaende kuponya hayo maeneo.

Maandiko yanasema imetupasa kumwomba Mungu sikuzote bila kukata tamaa (Luka 18). Hiyo ndio njia pekee itakayoleta majibu.

Yohana 7:38  Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.

Na Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

Rudi Nyumbani

Print this post