Category Archive Mafundisho

IJUE FAIDA YA KUFUNGA PAMOJA NA WANYAMA WAKO.

(Masomo maalumu yahusuyo mifungo na maombi).

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze Biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na Mwanga wa njia yetu (Zab 119:105).

Biblia inatufundisha sehemu kadhaa FAIDA za kufunga (yaani kujizuia kula na kunywa kwa kitambo) kwamba kwa kufanya hivyo tunafungua milango mingi, ambayo isingeweza kufunguka kwa maombi ya kawaida tu.

Mathayo 17:20  “Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

21  [LAKINI NAMNA HII HAITOKI ILA KWA KUSALI NA KUFUNGA”.

Lakini JE UNAJUA FAIDA ZA KUIFUNGISHA NA MIFUGO YAKO PIA? AU KAZI YAKO, AU BIASHARA YAKO?. Si watu tu wanaopaswa kufunga hata wanyama pia.. Utauliza hilo limekaaje?, hetu turejee biblia kidogo nyakati zile za Nabii Yona alipokwenda kuhubiri katika mji wa Ninawi.

Biblia inaonyesha kuwa Mfalme wa Ninawi alipiga mbiu kuwa wanadamu na wanyama wote walioko Ninawi wafunge wasile wala wasinywe (Zingatia hilo: si wanadamu tu bali hata wanyama wa kufungwa).

Yona 3:6 “Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu. 

7 Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu ASIONJE KITU, WALA MNYAMA WALA MAKUNDI YA NG’OMBE, WALA MAKUNDI YA KONDOO; WASILE, WALA WASINYWE MAJI;

 8 bali na wafunikwe nguo za magunia, MWANADAMU NA MNYAMA PIA, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake. 

9 Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe?  10 Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende”.

Unaona alichofanya Mfalme wa Ninawi??…Na matokeo yake tunaona baadaye Mungu anawataja wanyama kuwa wamestahili rehema kwa mfungo huo..Maana yake wanyama nao pia wasingefungishwa huenda wangepona watu tu  lakini wanyama wangepigwa (wangekufa!!)..Maana yake uchumi wao watu wa Ninawi ungeharibika, hata baada ya wao kupokea msamaha!!.

Yona 4:10 “Bwana akamwambia, Wewe umeuhurumia mtango, ambao hukuufanyia kazi, wala kuuotesha; uliomea katika usiku mmoja, na kuangamia katika usiku mmoja;

 11 na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi YA MIA NA ISHIRINI ELFU, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; TENA WAMO WANYAMA WA KUFUGWA WENGI SANA?

Nataka uangalie hayo maneno ya mwisho ya Bwana… “TENA WAMO WANYAMA WA KUFUGWA WENGI SANA?”

Kumbe hata wanyama pia wanaweza kuingizwa kwenye mkondo wetu wa BARAKA AU LAANA!.. Mfalme wa Ninawi aliliona hili, alijua siku ile ya gharika ya Nuhu hata wanyama waliangamizwa na dunia, na yeye akajua dhambi zimewachafua si tu watu, bali hata na wanyama wao wa kufungwa, hivyo nao pia ni lazima watakaswe kwa toba na  kwa kufunga, na utaona aliwavisha mpaka hao wanyama mavazi ya magunia!.

Ni vizuri kulijua hili ndugu, kuwa unapofunga fanya hivyo pia kwa wanyama wako (inaweza isiwe mara kwa mara lakini weka desturi hiyo)!!!

Unapofunga hebu pia funga pia na shamba lako, usinyeshee chochote siku hiyo, usiweke mboleo siku hiyo, wala usilipalilie, kama unafuga kuku, usiwalishe siku hiyo, usilishe ng’ombe wako siku hiyo, usilishe mbuzi zako siku hiyo, vile vile usifungue biashara yako siku hiyo, fanya hivyo kwa Imani  na utaona matokeo makubwa sana baada ya hapo!.

Wengi hawaoni matokeo katika kazi zao kwasababu wanasahau kufunga biashara zao, badala yake wanafunga tu wao, pasipo kujua kuwa vifungo pia havipo tu katika mwili, bali pia katika biashara na mifugo, hivyo nayo pia inapaswa ifungishwe.

Bwana akubariki.

Maran atha

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

NINI MAANA YA KUTUBU

Je tunaruhusiwa kutumia vidonge wakati wa kufunga?

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Rudi nyumbani

Print this post

HAZINA YAKO ILIPO, NDIPO UTAKAPOKUWAPO NA MOYO WAKO.

Hakuna namna utautenganisha “Moyo” na “hazina”.. vitu hivi vinaenda pamoja!.(ni sawa na miguu na mwili,..mahali miguu ilipo na mwili upo, miguu haiwezi kuwa mahali pengine na mwili mahali pengine) Vile vile Moyo wa mtu na hazina yake, vinaenda pamoja…Pale mtu alipojiwekea hazina, ni lazima (akili yake yote na fikra zake na hisia zake na mawazo yake yatakuwa huko).

Ndio maana mtu aliyejiwekea hazina kubwa ya mali za kidunia, halafu mali zile zikapotea zote ghafla, ni rahisi mtu huyo kuchanganyikiwa au kupoteza maisha maisha kabisa!.

Kwanini?..Kwasababu Moyo wake wote (fikra, mawazo, akili, malengo, uzima, hadhi) vilikuwepo katika mali zile, na sasa hana tena!, hata maisha kwake yanakuwa hayana maana tena!. Ndivyo ilivyo, kwamba Moyo siku zote unafuata hazina ilipo!, na unaishi kutokana na hazina mtu alizonazo. Ndivyo moyo wa mtu ulivyoumbwa!..

Vile vile mtu anayejiwekea hazina mbinguni, ni lazima fikra zake, mawazo yake, akili yake, malengo yake yote yatakuwa kule mbinguni hazina yake ilipo.

Sasa Bwana Yesu alitufundisha kanuni ya kuielekeza Mioyo yetu mbinguni, kwamba si kwa kuomba tu! Bali kwa kujiwekea hazina kule mbinguni,..kwanini?…kwasababu tutakapojiwekea hazina kule juu mbinguni basi mioyo yetu (yaani fikra, fahamu, akili, mawazo na hisia) zitaelekea kule Mbinguni, bila shuruti!.

Sasa swali, tunajiwekeaje hazina juu mbinguni?.. yeye mwenyewe (Bwana Yesu) alitufundisha kanuni katika Luka 18:18-22

Luka 18:18 “Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele?

19  Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu.

20  Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako.

21  Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu

22 Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, NAWE UTAKUWA NA HAZINA MBINGUNI; kisha, njoo unifuate”.

Na tena anarudia maneno kama hayo hayo katika Luka 12:32-34

Luka 12:32  “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.

33  Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, AKIBA ISIYOPUNGUA katika mbingu, mahali pasipokaribia mwivi, wala nondo haharibu.

34  KWA KUWA HAZINA YENU ILIPO, NDIPO ITAKAPOKUWAPO NA MIOYO YENU”.

Umeona?.. Kumbe kanuni ya kujiwekea hazina mbinguni ni kumtolea Mungu!..

Kwanini?.. Kwasababu tunapomtolea Mungu vile tulivyo navyo, mawazo yetu yatakuwa siku moja kwenda kupata thawabu mbinguni!, fikra zetu zitakuwa siku moja kwenda kuona miji mizuri tuliyoandwaliwa, mawazo yetu yatakuwa siku moja kwenda kuvikwa taji……hivyo muda wote tutakuwa tunafakari tu yaliyo ya juu na huko ndiko mioyo yetu itakapokuwepo!.

Ndio maana utaona watu wanaojitoa kwa Mungu kuanzia miili yao, mpaka mali zao, muda wote wanawaza unyakuo utakuwa lini?, muda wote wanawaza Kristo anakuja lini?.. ni kwanini wanakuwa hivyo?, si kwamba wanajilazimisha kuwa hivyo, ni kwamba tayari mioyo yao ipo mbinguni kwasababu wamejiwekea hazina huko.

Hii ni kanuni rahisi kabisa ya kuhamisha mioyo yetu kutoka kutafakari MAMBO YA CHINI na kuanza kutafakari MAMBO YA JUU!.

Ukitaka uwe mtu wa kutafakari mambo ya mbinguni sana, mtolee Mungu kuanzia muda wako, akili yako, mwili wako, ufahamu wako na hata vitu vyako!.. Hapo moyo wako wenyewe tu utaanza kuelekea mbinguni bila hata kutumia nguvu nyingi!,. Utajikuta tu unaanza kutamani kumwona Yesu, utajikuta unatamani ile siku ya mwisho ifike n.k

Laakini kinyume chake usipofanya hivyo na ukajitumainisha katika kujiwekea hazina katika mambo ya ulimwengu, basi fahamu kuwa moyo wako utaelekea tu katika mambo ya ulimwengu hata kama hupendi!.

Wakolosai 3:2 “Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

UKIMBIE UASHERATI (USIJIUNGAMANISHE NA miungu)

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu libarikiwe.

Karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na mwanga wa njia yetu.

Kuna mambo makuu mawili ambayo yanaweza KUMUUNGANISHA MTU MOJA KWA MOJA NA USHIRIKA WA MAPEPO.

Na mambo hayo ni SADAKA NA UASHERATI. Haya mambo mawili yanaenda pamoja, ndio maana wanaoenda kwa waganga utaona wanaambiwa watoe sadaka, au wafanye zinaa, lengo la zile sadaka si kuimairisha maisha ya wale wanaozitaka (waganga), wala lengo la ile zinaa si kuwafurahisha hao waganga bali ni kumuunganisha yule mtu na madhabahu ile!.  

Sasa nataka tuangalie mfano mmoja wa kwenye biblia wa watu waliojiunganisha na madhabahu za mashetani kwa njia hizo mbili; (MATOLEO PAMOJA NA UASHETANI). Na hao si wengine Zaidi ya Wana wa Israeli walipokuwa katika safari yao ya kwenda Kaanani.

Tusome,

Hesabu 25:1 ”Basi Israeli akakaa Shitimu, KISHA WATU WAKAANZA KUZINI PAMOJA NA WANAWAKE WA MOABU; 

2 kwa kuwa waliwaalika hao watu WAENDE SADAKANI, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao. 

3 IKAWA ISRAELI KUJIUNGAMANISHA NA BAAL-PEORI; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli.

4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli.

 5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baalpeori”

Mstari wa 3 hapo unasema hao watu kajiunganisha na “Baali-peori” ambaye ni mungu wa wamoabi, na njia waliojiunganisha nayo ni UASHERATI na SADAKA!

Na adui njama aliyoitumia ni KUALIKA!.. walioalikwa tu! Lakini kumbe walikuwa wameshaandaliwa “wanawake wa kuzini nao” na kwa tamaa zao wakaingia kwa wanawake hao na kuzini, pasipo kujua kuwa kwa kitendo hiko tayari walikuwa wameshajiungamanisha na miungu yao, na hivyo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli na Mungu akapigo kwa pigo kuu.

Ndugu, (kaka, dada,mama, baba) jihadhari na uasherati, jihadhari na Mialiko isiyo rasmi inayohusisha jinsia mbili tofauti.. Mtego wa shetani si wewe ufanye tu dhambi ya uzinzi, bali lengo lake ni wewe kukuunganisha na miungu na madhabahu ya huyo unayekwenda kuzini naye.

Na madhara ya kuunganishwa na mtu huyo ni kwamba zile “laana” na “hukumu” anazozibeba na wewe unazibeba..Ndicho kilichowatokea wana wa Israeli walipozini na wanawake wa Moabu, Taifa la Moabu lililaaniwa na wote waliozini na wale wanawake walibeba zile laana.

Ndivyo maandiko yanavyosema katika 1Wakorintho 6:15…

1Wakorintho 6:15  “Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!

16  Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja”.

Sasa inawezekana ulifanya hayo pasipo kujua, na hivyo ulijiungamanisha na madhabahu za kuzimu. Suluhisho la kwanza si kwenda kuombewa!… bali ni wewe kutubu! Kwa kumaanisha kutofanya machukizo hayo tena. Na baada ya kutubu, hatua inayofuata ni ubatizo sahihi na kisha kudumu katika Imani huku ukijitenga na uovu na vichocheo vyake vyote.

1Wakorintho 6:18 “Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).

Rudi nyumbani

Print this post

MWAGA DAMU YAKO KWA AJILI YA BWANA.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tena tujifunze maneno ya uzima.

Kulikuwa na aina nne za wito ambao Bwana aliwaitwa mitume wake.

  1. Wito wa kawaida: Ambapo Bwana alipowaona mitume aliwaambia nifuate. Lakini hakukuwa na vigezo vyovyote, nyuma yake, au majumu Fulani ya lazima ya kuyafanya.(Yohana 1:35-51)
  2. Wito wa uanafunzi: Baadaye akaja kuwafanya kuwa wanafunzi wake, hapo ndipo aliwakuta na kuwaambia waache vyote kisha wamfuate, na akatoa na vigezo vyake, kwa wale wote waliotaka kuwa wanafunzi wake (Luka 14:25-35), Hivyo Bwana alikuwa nao wengi zaidi ya wale 12
  3. Wito wa kitume: Baadaye akawachagua mitume kati ya wanafunzi wake wengi. Yaani watu ambao atawatuma kwa kazi maalumu. Ndio hapo wakapatikana 12
  4. Wito wa mashahidi: Lakini mwisho akawachagua mashahidi wake, Huu ndio wito wa juu sana na wa mwisho, ambao Bwana aliwakusudia mitume wake, akawapa siku ile aliyokuwa anapaa.

Matendo 1:8  Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi

Sasa nini maana ya kuwa SHAHIDI? Kuwa shahidi maana yake ni kuwa tayari kupitia mateso au kumwaga damu yako kwa ajili ya kumtetea Yule anayekutuma. Hivyo mtu yoyote aliyemwaga damu yake, kwa ajili ya Yesu huyo ni SHAHIDI. Hivyo mitume walijua kabisa hatma yetu ni kumwaga damu tu, huko mbeleni. Na watu kama hawa wanakuwa na nafasi ya juu sana, mbele ya Kristo siku ile watakapofika mbinguni, kwasababu wanakuwa wamepitia sehemu ya mapito yaleyale aliyoyapitia Bwana wao hapa duniani.

Leo tutatazama aina nne(4), za mashahidi wa Kristo. Na wewe pia utajipima upo wapi kati ya hawa na kama haupo popote basi, ufanye bidii uwe katika wingu hili la Mashahidi wa Yesu.

Aina nne (4), za Mashahidi wa Yesu.

1) Wanaoteswa na kupigwa na kuuliwa kwa ajili ya Bwana au injili:

2Wakorintho 11:23  “Wao ni wahudumu wa Kristo? (Nanena kiwazimu), mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi. 24  Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja. 25  Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini”.

Hata sasa, wapo watu wanateswa kwa namna mbalimbali, wengine wanamwaga damu kwa mapigo, watu kama hawa ni mashahidi wa Bwana. Sawa tu wale mitume wake.

2) Wanaooponza/ wanaohatarisha maisha yao kwa ajili ya Bwana au injili.

Hili ni kundi la pili ambalo linamwaga damu pia. Ijapokuwa haitaonekana kwa nje lakini rohoni Mungu anawaona kama wamemwaga damu kwa ajili ya ushuhuda wake. Kwamfano tukiangazia kile kisa cha Daudi ambapo wakati Fulani alitamani kunywa maji ya kisima kilichokuwa katikati ya maadui zake wafilisti. Lakini tunaona mashujaa wake watatu waliposikia, waliondoka kisirisiri, wakahatarisha maisha yao, kwenda katika marago ya wafilisti, na kuyachukua yale maji na kumletea Daudi, lakini Daudi hakuyanywa alisema ile ni damu yao na sio maji tena.

2Samweli 23:14 Naye Daudi wakati ule alikuwako ngomeni, na jeshi la Wafilisti wakati ule walikuwako Bethlehemu.  15 Daudi akatamani, akasema, Laiti mtu angeninywesha maji ya kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango!  16 Basi hao mashujaa watatu wakapenya jeshi la Wafilisti, wakateka maji kutoka kile kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango, wakayachukua, wakamletea Daudi; walakini yeye hakukubali kuyanywa, akayamimina mbele za Bwana.  17 Akasema, Hasha, Bwana, nisifanye hivi; je! Si damu hii ya watu hao waliohatirisha nafsi zao? Kwa hiyo hakukubali kuyanywa. Hayo ndiyo waliyoyafanya wale mashujaa watatu.

Umeona? Maji yamekuwa damu kwasababu ya hatari waliyoingia watu wale. Vivyo hivyo na wewe ujitoapo sadaka kwa ajili ya Bwana, unapohatarisha hata kazi yako, muda wako, ujana wako, ili tu umfanyie Mungu jambo. Ndugu hilo linakuwa sio jambo la kawaida bali ni damu yako unayoimwaga kwake.

Kulikuwa na Yule mwanamke alikwenda kumtolea Bwana sadaka ya senti mbili, lakini maandiko yanasema ndio iliyokuwa riziki yake yote, hajui kama kesho ataiona, pengine hata jana yake hakula. Si ajabu kwanini Bwana aliona ametoa zaidi ya wengine wote. Kwasababu kilichokuwa anakitoa ni uhai wake, na sio sadaka ya kawaida.

Jiulize nguvu zako unazozisumbukia daima unazimalizia kwa nani, je! Ni kwenye kujenga tu, ni  kuwekeza, ni kuvaa ni kula? Au ni nini? Vipi kwa Mungu wako, unampa sehemu ndogo tu, ni kweli utapata thawabu? Lakini je! Ulishawahi kufikiria kutenda jambo linalokugharimu wewe kwa Bwana wako? Damu yako unaimwaga wapi?. Watakatifu wa kanisa la kwanza, waliweza kuuza mali zao za thamani na kumtolea Bwana, na sisi tunafanya nini kwa Bwana?.

3) Wanaoondoa viungo vyao vinavyowakosesha kwa ajili ya Kristo.

Hili nalo ni kundi lingine la wanaomwaga damu. Ukisoma Marko 9:43-49, kuna maneno Bwana Yesu alisema, kuhusiana na viungo vyetu. Akasema ikiwa kimojawapo kinakukosesha kikate, ili usikose uzima wa milele. Unajua sikuzote kiungo kikatwapo, ni lazima damu imwagike. Ukiuondoa mguu wako, yapo maumivu, lakini pia ipo damu itakayokutoka.

Viungo vinaweza vikawa ni wazazi, marafiki, ndugu, kazi, mazingira n.k. Ikiwa mzazi anakukosha usisimame vema na Mungu, anakukataza usimwabudu Bwana,au usihubiri huna budi kutomtii kwasababu hiyo, ni kweli utakutana na maumivu, damu itatoka, lakini umemtii Kristo.

Ndicho alichokifanya mfalme mmoja aliyeitwa ASA, yeye alimcha Mungu, na alipoona mama yake anamletea habari za ibada za masanamu, akamwondoa kwenye kiti cha umalkia, japokuwa ni fedheha kubwa alionyesha lakini aliona ni heri kumtii Kristo zaidi ya mwanadamu (1Wafalme 15:11-13)

Hata leo, watu ambao, wameachwa, na viongo vyao vya karibu, au wameviondoa, kwasababu ya Kristo, visiwaghasi, labda ni kazi, ndugu, rohoni wanaonekana kama wamemwaga damu zao kwa ajili ya ushuhuda wa Kristo, na hivyo ni mashahidi wa Bwana. Ndugu usiopoge maumivu, mpende Bwana zaidi ya chochote.

4) Wanaoomboleza kwa ajili ya kanisa, na injili.

Yesu alipokuwa anaomba, kwa maomboleza na dhiki nyingi kwa ajili yetu muda mfupi kabla ya kusulibiwa, maandiko yanasema jasho lake, likageuka kuwa matone ya damu.

Luka 22:41  “Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, 42  akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. 43  Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu. 44  Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchini.]

Hivyo na wote, waombolezao kwa ajili ya haki, machozi yao si bure, wanaokesha kuliombea kanisa, na kazi ya Mungu, wanaowaombea wengine kwa machozi na huzuni, wanadumu madhabahuni kwa Bwana muda mwingi mfano wa Ana (Luka 2:36). Rohoni wanamwaga damu, japo wanaweza wasilijue hilo. Na hivyo ni mashahidi wa Kristo duniani. Thawabu yao mbinguni ni sawasawa na wale waliokatwa vichwa kwa ajili ya Bwana.

Swali ni je! Mimi na wewe tunasimama wapi? Paulo anasema ninakufa kila siku, je! Na sisi tunafanya hivyo kwa Bwana wetu? Bwana atusaidie tuwe maaskari wake kwelikweli, ili siku ile ajivunie sisi mbele za Mungu na malaika zake.

Fanyika shahidi mwaminifu wa Bwana.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU

MAMBO YA KUJIFUNZA KWA KLOPA NA MKE WAKE!

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

Rudi nyumbani

Print this post

UMEJIANDAAJE KWA NYAKATI ZA KUWA PEKE YAKO?

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tuyatafakari maneno ya neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Sisi kama wakristo hatuna budi kutambua kuwa yapo majira mbalimbali tutapishana nayo angali tukiwa hapa duniani katika safari yetu ya imani. Leo tutaona mojawapo ya majira ambayo, huna budi kupishana nayo sehemu Fulani katika maisha yako. Na watakatifu wengi wanapofikia hatua hii, huwa wanavunjika moyo, na wengine kudhani Mungu amewaacha. Lakini la! Ni moja ya mapito ambayo Bwana anayaruhusu kwasababu zake maalumu.

Na majira hayo ni ya kuondolewa msaada, au usaidizi, au ukaribu, au faraja ya  ndugu, ya marafiki, au ya wapendwa. Yategemea na pito la mtu mwenyewe. Na sio kwamba ni wabaya, hapana, ni Mungu tu peke yake kaamua kufunga milango hiyo. Ili abaki yeye na Mungu wake tu, katika chumba cha siri cha rohoni.

Tujifunze kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Ambaye, alikuwa mashuhuri sana, na kila mahali alipokwenda alizingirwa na makutano mengi, wakati mwingine alijificha ili watu wasimwone, kwasababu walikuwa wanamsonga sana, hata nafasi ya kula ilikosekana, maelfu ya watu walitamfuata popote alipokwenda.

Lakini kuna majira, hata wale waliokuwa karibu naye (yaani mitume) walimkimbia akabaki yeye peke yake, na hilo aliliona mapema akawaambia wanafunzi wake, ili wasije wakajisikia vibaya.

Yohana 16:32  Tazama, saa yaja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanyika kila mmoja kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu; walakini mimi si peke yangu, kwa kuwa Baba yupo pamoja nami.

33  Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.

Na ilikuja kutokea hivyo (Soma Marko 14:27-51). Kwasababu ilikuwa ni sehemu ya pito la mwana wa Mungu.

Halikadhalika yupo mtume Paulo, kama tunavyojua yeye ndio alikuwa kama askofu-kiongozi wa makanisa ya mataifa. Alikuwa na marafiki wengi, alikuwa na wapendwa wengi waliomsapoti na kumfariji, katika utumishi wake. Lakini upo wakati alijikuta peke yake. Mpaka akaandika sehemu ya waraka huo na kumtumia Timotheo. Jambo ambalo huwezi dhani linawezekana kwa askofu wa makanisa.

2Timotheo 4:16  “Katika jawabu langu la kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu, bali wote waliniacha; naomba wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo. 17  Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu, ili kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu, hata wasikie Mataifa yote; nami nikaokolewa katika kinywa cha simba. 18  Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina”

Hivyo, hii sio bahati mbaya, ijapokuwa tunazungukwa na wapendwa, na familia, na watoto, na marafiki, lakini kuna wakati Bwana atataka ubaki peke yako na yeye. Na hivyo katika kipindi hicho utakachojikuta, upo mbali nao, au huoni msaada wowote kutoka kwao kama ilivyokuwa kule mwanzo, au hawakuulizii tena, huna mtu wa kucheka naye, kuimba naye. Usijione mpweke, bali mtazame Kristo, elekeza mawazo yako kwake, kwasababu kuna jambo anataka kukufundisha.

Na wakati huo ukiisha, utaona tena anakurejeshea, faraja yako, wapendwa wako, rafiki zako, ndugu zako, na safari inaendelea. Kama alivyofanya kwa Ayubu.

Ayubu 42:10 “Kisha Bwana akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; Bwana naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza.  11 Ndipo wakamwendea nduguze wote, waume kwa wake, nao wote waliojuana naye hapo zamani, wakala chakula pamoja naye katika nyumba yake; nao wakamlilia na kumtuza moyo katika habari za huo uovu wote Bwana aliouleta juu yake; kila mtu akampa kipande cha fedha, na pete ya dhahabu kila mmoja”.

Hivyo weka akiba ya wakati huo, kwasababu hutaukwepa ikiwa wewe ni mwana wa Kristo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.

RABI, UNAKAA WAPI?

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

JE UTII WAKO KWA MUNGU UMETIMIA?.

Rudi nyumbani

Print this post

SADAKA INAKOMESHA LAANA!

Karibu katika mfululizo ya masomo yahusuyo matoleo!

(Ifahamu Nguvu iliyopo katika Sadaka)

Tangu Adamu aanguke ardhi ilianza kulaaniwa; kila siku laana ilikuwa inajiongeza juu ya laana, ndio maana utaona Mungu alimwambia Adamu ardhi imelaaniwa kwaajili yake yeye na uzao wake (Mwanzo 3:17), lakini ukizidi kusoma utaona tena ardhi inalaaniwa mara ya pili kwa Kaini (Mwanzo 4:11).

Na desturi hiyo iliendelea juu ya wanadamu, (Maana yake kila kukicha ardhi ilikuwa inalaaniwa juu ya wanadamu, kutokana na maasi).

Lakini tunasoma alipozaliwa Nuhu maandiko yanamtaja kama mwana wa Faraja, atakayeikomesha laana iliyo juu ya ardhi.

Mwanzo 5:28 “Lameki akaishi miaka mia na themanini na miwili, akazaa mwana. 

29 Akamwita jina lake Nuhu, AKINENA, HUYU NDIYE ATAKAYETUFARIJI KWA KAZI YETU NA KWA TAABU YA MIKONO YETU KATIKA NCHI ALIYOILAANI BWANA”

Sasa unaweza kujiuliza ni wakati gani ambao Nuhu alileta faraja katika Nchi aliyoilaani Bwana?

Tusome Mwanzo 8:20-22.

Mwanzo 8:20 Nuhu akamjengea Bwana madhabahu; akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu. 

21 Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, SITAILAANI NCHI TENA BAADA YA HAYO KWA SABABU YA WANADAMU, MAANA MAWAZO YA MOYO WA MWANADAMU NI MABAYA TANGU UJANA WAKE; WALA SITAPIGA TENA BAADA YA HAYO KILA KILICHO HAI KAMA NILIVYOFANYA. 

22 Muda nchi idumupo, majira ya kupanda, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma”

Umeona hapo? Baada ya Nuhu kumjengea Bwana madhabahu na kumtolea Bwana sadaka nzuri na ya kumridhisha, ndipo akaikomesha ile laana yote iliyokuwa inaendelea juu ya ardhi, kukawa hakuna tena kulaaniwa kwa nchi baada ya hapo!, ndio maana mpaka leo tunaona misimu ya mvua ipo, misimu ya kiangazi cha mavuno ipo, majira ya kuvuna na kupanda bado yapo, kama isingelikuwa ile sadaka Nuhu aliyoitoa huenda leo tungekuwa dunia ingekuwa mahali pabaya.

Lakini siri ya KUIKOMESHA HIYO LAANA!, Nuhu alifahamu ni kwa NJIA YA MATOLEO TU!..Na ni kanuni gani Nuhu aliyoitumia kutoa sadaka mpaka kufikia kuvunja misingi ya laana ya ardhi?

1.Alijenga Madhabahu.

Na sisi ni lazima tujenge madhabahu kwanza, na Madhahabu ya sasa, Agano jipya si ile ya mawe bali ni MIOYO YETU, Hiyo inapaswa iwe misafi kabla ya kufikiri kumtolea BWANA sadaka. Kwasababu maandiko yanasema sadaka ya mtu mbaya ni machukizo kwa Bwana (Mithali 15:8).

2. Kutoa vilivyo safi.

Baada ya Nuhu kutoka kwenye safina alitwaa wanyama walio safi tu na kumtolea Mungu, Na sisi ni lazima tumtolee Mungu vitu vilivyo visafi, hatupaswi kumtolea Mungu vitu vilivyopatikana kwa njia haramu kama ukahaba, dhuluma, rushwa, wizi, utapeli, na njia nyingine zote zinazofanana na hizo.

Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili.”

3. Kutoa katika KILA kilicho safi!

Hii ni kanuni ya mwisho na ya muhimu sana, Ni lazima kutoa katika “KILA” kilicho safi, na si katika “BAADHI ya vilivyo safi”. Nuhu hakutoa tu Ng’ombe pekee yake kama sadaka, na kuwahifadhi mbuzi kwaajili ya chakula chake na biashara yake,  au hakutoa kondoo pekee yake, na kuwaacha kuku na mbuzi…bali alitoa katika vyote vilivyo safi, ikiwemo kondoo, mbuzi, ng’ombe, njiwa, kuku na vinginevyo.. kila kimoja kwa sehemu yake..Hiyo ikafanya sadaka yake kumridhisha Mungu, na hivyo kufuta laana zote zilizokuwepo juu ya nchi, ambapo mpaka leo tunakula matunda yake.

Na wewe una vitu gani vilivyo safi mbele za Mungu?, je katika vyote unavyovifanya huwa unafikiri kumtolea Mungu katika hivyo?, Je katika zawadi unazopewa ulishawahi kufikiri kumtolea Mungu sehemu ndogo katika hiyo?, au unafiki ni sehemu ya mshahara tu ndio Mungu anaitaka?!

Je katika mifugo yako yote ulishawahi kufikiri kumtolea Mungu sehemu ya hiyo? Usimtolee Mungu kuku na kuacha Mbuzi!.. Jaribu siku moja kumtolea mbuzi na kuku kwa pamoja, na uone matokeo yake, (Mungu ameruhusu tumjaribu kwa njia hiyo, Malaki 3:10).

Utaona laana zinavyoondoka juu yako!!.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).

Kwanini Nuhu alimlaani Kaanani badala ya mtoto wake Hamu,

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

Rudi nyumbani

Print this post

UWE KIKOMBE SAFI 

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tuyasikilize maagizo ya Mungu.

Kuna wakati Bwana alipokutana na mafarisayo alisema maneno haya;

Mathayo 23:25-26

[25]Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang’anyi na kutokuwa na kiasi.

[26]Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi.

Tengeneza picha ya kikombe. Kiuhalisia ili kifae Kwa matumizi ni lazima kiwe kisafi pande zote, yaani nje na ndani. Huwezi kutumia kikombe ambacho nje ni kisafi lakini ndani kina matope, vilevile huwezi tumia kikombe ambacho ndani ni kisafi lakini nje kina matope,. Bado uchafu ni ule ule..Hivyo ili kifae Kwa matumizi hakina budi kisafishwe kotekote ndani na nje.

Leo hii tunakosa shabaha kudhani, ni upande mmoja tu Mungu anautazama. Ndivyo walivyofanya mafarisayo Kwa nje walionekana wanyenyekevu, wafanya ibada, Wana staha, waalimu wazuri wa torati lakini ndani walijaa wivu, mashindani, majivuno, tamaa n.k.

Lakini vilevile wapo watu ambao Kwa ndani wanadai Wana upole, Upendo, amani, lakini Kwa nje, hawana ushuhuda wowote, Hawa ndio wale ambao wanasema Mungu anaangalia vya rohoni haangalii vya nje.

Ndugu ili utumiwe na Bwana, safisha kikombe kotekote. Rohoni na Mwilini 

Sasa haya ni baadhi ya mambo ambayo unapaswa uyafanye kotekote. Tukiangazia mifano kwa Bwana Yesu.

1) KUMPENDEZA MUNGU.

Yesu aliishi maisha ya kumpendeza Mungu, lakini alijua kwamba kabla ya kumpendeza Mungu ni lazima niwapendeze kwanza wanadamu. Hivyo akafanya bidii kuwa na sifa njema katika jamii pia, na kwa Mungu.

Luka 2:52

[52]Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

Umeona? Hakuwa mtu wa kusema Mimi ni Mungu tu, lakini alitafuta sifa nzuri pia Kwa wanadamu ili Mungu wake atukuzwe, hivyo aliishi vizuri na wanadamu, alikuwa mtiifu, mwaminifu, mwenye utu, mwenye adabu kwa watu. Vivyo hivyo na wewe kama mkristo kama sifa zako nje zinavuma vibaya.. hata kama ni mtu mzuri kiibada hapo ni sawa na umesafisha kikombe Kwa ndani lakini nje ni kichafu. Hivyo bado hujakamilika. Safisha pande zote, mbinguni na ulimwenguni.

2) UPENDO

Maandiko yanasema, Mpende Bwana Mungu wako Kwa moyo wako wote, na Kwa Roho yako yote na Kwa nguvu zako zote..lakini kabla hayajasema maneno hayo, Mungu alitangulia kusema kwanza mpende jirani Yako,ili Upendo wako kwake ukamilike.

1 Yohana 4:20-21

[20]Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.

[21]Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.

Kabla hujampenda Mungu mpende mwanadamu. Safisha kikombe nje na ndani.

3) USAFI

Mungu anatutaka tuwe wasafi moyoni moyoni.(Mathayo 5:8)..Lakini usafi wa ndani unakamilishwa na ule wa nje.

Soma

2 Wakorintho 7:1

[1]Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.

Umeona kumbe Kuna uchafu wa mwili na pia wa roho. Ule wa Roho ndio wivu, kiburi, uongo n.k. lakini ule wa mwili ndio ulevu, uvaaji mbovu, uchoraji mwili, utukanaji, mazungumzo mabaya.n.k

Ikiwa unajiita Mtakatifu halafu unatembea na vimini barabarani, Binti unatembea na suruali, na nguo za mgongo wazi, huna tofauti na yule mhudumu wa pale bar.Fahamu kuwa huo usafi wako wa roho ni kazi bure. Kijana unatembea na suruali za milegezo, unafuga Rasta na viduku, huna tofauti na yule msanii wa kidunia.halafu unasema wewe ni msafi wa moyo fahamu kuwa hapo unayo dosari mbele za Bwana.

UWE KIKOMBE SAFI.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA.

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?

Rudi nyumbani

Print this post

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

Mathayo 9:14  “Wakati ule wanafunzi wake Yohana wakamwendea, wakasema, Kwa nini sisi na Mafarisayo twafunga, BALI WANAFUNZI WAKO HAWAFUNGI?

15  Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kuomboleza, muda bwana arusi akiwapo pamoja nao? Lakini siku zitakuja WATAKAPOONDOLEWA BWANA ARUSI; NDIPO WATAKAPOFUNGA”.

Wanafunzi walipokuwa na Bwana Yesu katika mwili, chochote walichokihitaji walikipata kirahisi kwasababu Neema walikuwa naye katika mwili, walipohitaji uponyaji Kristo alikuwepo kuwaponya, walipohitaji kuona ishara na miujiza kama ile ya mikate mitano kulisha elfu tano, waliiona kirahisi.

Kila walichokihitaji walikipata, kwasababu Mtenda miujiza walikuwa wanamwona dhahiri na kumshika. Lakini ulipofika wakati wa Kristo kuchukuliwa juu, mambo yalibadilika!!, ile hali ya kusubiria kufanyiwa mambo na Bwana ikapotea, ikawabidi waanze kutafuta wenyewe namna ya kufanya mambo!. Ni kama tu kifaranga cha kuku kilichoachwa na mama yake, kikawaida kinaanza kujitafutia chenyewe, kitatembea huku na kule kama mama yake kutafuta chakula.

Ndicho kilichowatokea Mitume Bwa Yesu, ulipofika wakati wanakutana na wagonjwa na yule Bwana Yesu wa kukimbiziwa  wagonjwa hayupo!!!.. ndipo ufahamu wa kutafuta nguvu alizokuwa nazo Bwana Yesu ukawajia!.

Ndipo wakaanza kutafiti ni vitu gani vilivyokuwa vinampa nguvu Bwana Yesu, kufanya miujiza ile na kuishi maisha yale!, ndipo wakaanza kutafakari maisha yake na kugundua kuwa muda mwingi Bwana aliutumia KUFUNGA na KUKESHA MILIMANI KUOMBA.

Na wao ikawabidi wabadilike na kuanza kuwa WAFUNGAJI NA WAOMBAJI kama Bwana Yesu ili baadhi ya mambo yawezekanike kama yalivyowezekanika kwa Bwana, vinginevyo baadhi ya mambo yasingeenda sawa, Ndio maana utaona akina Petro walipokuwa na Bwana ni kama walikuwa wanavutwa vutwa katika suala la uombaji (Utaona kuna mahali Bwana Yesu alikuja kuwaamsha Zaidi ya mara 2 waombe lakini wakarudi kulala).

Marko 14:34  “Akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa mkeshe.

35  Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akiomba ya kuwa, ikiwezekana, saa hiyo imwepuke. 36  Akasema, Aba, Baba, yote yawezekana kwako; uniondolee kikombe hiki; walakini, si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.

37  AKAJA AKAWAKUTA WAMELALA USINGIZI, AKAMWAMBIA PETRO, JE! SIMONI, UMELALA? Hukuweza kukesha saa moja? 14.38  Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu.

39  Akaenda zake tena, akaomba, akisema neno lilo hilo.

40  AKAJA TENA AKAWAKUTA WAMELALA, maana macho yao yamekuwa mazito, wala hawakujua la kumjibu.

41  Akaja mara ya tatu, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike; yatosha, saa imekuja; tazama, Mwana wa Adamu anatiwa mikononi mwao wenye dhambi”.

Hapa tunaona akina Petro wakiwa wanavutwa vutwa katika suala la uombaji, lakini tunaona mambo yanabadilika baada ya Bwana Yesu kuondoka, walianza kufunga na kukesha katika maombi mengi,.. Kuna mahali Petro anaonekana kufunga kwa kuomba mpaka anazimia kwa njaa.

Matendo 10:9  “Hata siku ya pili, walipokuwa wakisafiri na kuukaribia mji, Petro alipanda juu darini, kwenda kuomba, yapata saa sita ya mchana;

10  AKAUMWA NA NJAA SANA, AKATAKA KULA; LAKINI WALIPOKUWA WAKIANDAA, ROHO YAKE IKAZIMIA,

11  akaona mbingu zimefunuka, na chombo kikishuka kama nguo kubwa, inatelemshwa kwa pembe zake nne hata nchi”

Hii ikifunua nini?

Kristo mpaka sasa hayupo nasi katika Mwili, hivyo na sisi pia tupo katika Nyakati za KUFUNGA na KUOMBA.

Ndugu Hizi ni nyakati za “Kufunga na kuomba”. Bwana Yesu alisema mambo mengine hayawezekaniki isipokuwa kwa kufunga na kuomba/kusali.

Mathayo 17:21 “[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga]”

Je Unataka kumwona Mungu katika maisha yako?..Funga na kuomba!..je  unataka kuongezeka viwango vya kumjua Mungu?..Funga na kuomba!…Je Unataka Neema iongezeke juu yako! Na mambo mengine mengi yaliyo mazuri uyaone??, basi funguo ni Mifungo na Maombi. (Na kumbuka hapa biblia inazungumzia Maombi na sio maombezi). Usifunge na kwenda kutafuta kuombewa na mtumishi!.. Bali funga na omba mwenyewe!.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Kwanini maombi kwa Marehemu si sahihi kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.

Je unajua kuwa roho ya mpinga-kristo imeshaanza kutenda kazi na inaendelea kutenda kazi hata sasa?

1 Yohana 4:3 “Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; NA SASA IMEKWISHA KUWAKO DUNIANI”.

Andalizi la mwisho la Mpinga Kristo kabla ya chapa yake kuanza kufanya kazi ni hili “MUNGU HAANGALII MWILI BALI ROHO”.

Roho ya Mpinga-kristo inawaandaa sasa watu na hiyo saikolojia, kwamba waamini Mungu haangalii mwili bali roho tu.

Na kwanini anafanya hivyo?.. ni ili iwe vyepesi kwake siku ile  kuwatia watu CHAPA mwilini (Usoni na mikononi)

Kwasababu asipowaandaa na hiyo saikolojia itakuwa kwake ni ngumu sana kuwashinikiza waipokee chapa katika vipaji vya nyuso na katika mwili siku zile baada ya unyakuo wa kanisa kupita.

Kwahiyo anaanza na saikolojia ndogo tu kwamba kuvaa hereni sio kosa, kutoboa pua sio kosa, kujichora tattoo na hina sio kosa na kupaka lipstick midomoni na wanja machoni sio dhambi.. ( kwamba Mungu hawezi kumhukumu mtu kwa vitu vinavyowekwa mwilini)

Ndugu usidanganyike,  je! Umewahi kujiuliza kwanini Mungu atawahukumu watu wote watakaoipokea  ile chapa ya mnyama  katika VIPAJI vya nyuso zao na katika MIKONO yao siku ile?..

Kama Mungu haangalii mwili kwanini chapa ya 666 itiwe katika mwili na Mungu awahukumu wale wote watakaoipokea chapa hiyo?, maana maandiko yanasema watu wote watakaoipokea chapa hiyo katika vipaji vya nyuso zao au katika mikono basi watahukumiwa katika lile ziwa la moto (Ufunuo 14:9-10).

Sasa kama tu alama ya kishetani katika kipaji cha uso au katika sehemu ya mkono, inaweza kuwa sababu ya mtu kukataliwa na Mungu milele!, vipi hizo tattoo unazochora mwilini, vipi hizo hina unazozipaka na  wanja unaoupaka machoni?, vipi hizo lipstick unazopaka mdomoni na rangi unazopaka kwenye kucha?… Vipi hizo hereni unazozining’iniza masikioni?.

Kama tu leo ni ngumu kuelewa kuwa kupaka wanja ni kosa kibiblia, utashawishikaje siku ile kuamini kuwa kuandikwa alama ya 666 kwenye kipaji cha uso wako ni kosa?..nataka nikuambie kuwa siku ile utaipokea tu chapa kama kawaida.  Kama tu leo kutoboa masikio na kuweka hereni na kutoboa pua na kuweka pini huoni shida, utaonaje shida siku ile utakapotobolewa  katika mkono wako na chipu kuwekwa mwilini mwako?.

Tafakari sana dada!!… tafakari sana kaka!! Tafakari sana Mama, tafakari sana Baba…Usiwe mwepesi kuiga mambo yanayoendelea na kuonekana ulimwenguni, hususani yanayofanywa na watu wengi!…(Mengi ya hayo yanaongozwa na roho ya mpinga kristo)…Ni kweli unajipenda, na ni vizuri kufanya hivyo, ni kweli unapenda uonekane vizuri na maridadi mbele za watu, ni vizuri pia kufanya hivyo lakini vipi na roho yako? Je itaendelea kubaki salama?.

Shetani amewafunga wengi macho siku hizi za mwisho wasiyaelewe maandiko! Na kuwaaminisha kuwa Mungu haangalii mwili bali anaangalia roho.

Dada usidanganyike! Kwasababu udanganyifu upo leo.. na utaendelea kuwepo mpaka wakati wa chapa ya mnyama.

Tupa hereni zote, kachome mawigi, ondoa pistick, na wanja machoni.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

JE CHANJO YA KORONA NI ALAMA YA MNYAMA?

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Rudi nyumbani

Print this post

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu lililo hai (Zab.119:105)

Je unaijua nguvu ya kinywa chako? Biblia inasema kuwa MAUTI na UZIMA huwa katika uwezo wa ULIMI. Na mtu awezaye kuutumia vizuri ulimi wake atakula matunda yake.

Mithali 18:21 “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”.

Sasa ULIMI una matunda mawili tu!, ambayo ni “Uzima na Mauti”. Maana yake mtu anaweza kuutumia ulimi wake ukamletea UZIMA, lakini pia anaweza kuutumia na ukamletea MAUTI.

Yule kijana aliyempelekea Daudi habari za kifo cha Sauli, kinywa chake mwenyewe kilimletea “Mauti” (2Samweli 1:16) hali kadhalika Mfalme Yehoshafati alipokuwa katika hatari ya kufa, kwa kinywa chake mwenyewe alijiokoa. (2Nyakati 18:31).

Lakini leo nataka tuangalie faida za kutumia ULIMI katika eneo la  MAOMBI.

Wengi tumezoea kuomba kimoyomoyo, jambo ambalo ni zuri lakini si wakati wote linafaa!!.. kuna mazingira ni lazima utumie kinywa chako kutoa maneno dhahiri yanayosikika!..Kuna ngome zinahitaji kusikia sauti ndipo zitii!, Kuna ngome zinahitaji kuamrishwa na kukemewa ndipo zitii (Kuta za Yeriko zilihitaji kelele nyingi ili zianguke)….Hali kadhalika katika imani inahitajika sauti ya kinywa ili kuthibitisha wokovu mtu alioupata…

Warumi 10:9  “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

10  Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.

Kwa hiyo si kila wakati maombi ya ukimya yanafaa… Ni lazima ujifunze kubadili gear unapoingia katika maombi ya vita, hata motokaa haisaifiri kwa gear moja tu, ikienda hivyo itakwamaa mahali Fulani.

Sasa biblia inatufundisha kuwa “Mauti na Uzima” huwa katika uwezo wa kinywa. Maana yake ni kwamba tukitumia vizuri ndimi zetu wakati wa kuomba tunauwezo wa kuvihuisha vitu vingi vilivyokufa, na pia kuviua baadhi ya vitu visivyofaa maishani mwetu.

Tunaviuaje vitu visivyofaa?.. Tunaviua kwa “kuvitamkia kifo” kwa mfano ule ule wa Bwana Yesu alivyoutamkia ule Mtini, na ukafa wakati ule ule.

Mathayo 21:18  “Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.

19  Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; AKAUAMBIA, YASIPATIKANE MATUNDA KWAKO TANGU LEO HATA MILELE. MTINI UKANYAUKA MARA.

20  Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema, Jinsi gani mtini umenyauka mara?

21  Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng’oka, ukatupwe baharini, litatendeka.

22  Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea”.

Mstari wa 19 unasema “..akauambia, yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele, mtini ukanyauka mara.” Hapo Bwana Yesu aliuua huo mtini kwa kutumia kinywa chake. (Aliutumia ulimi wake na akala matunda yake), na anatuambia tukiwa na Imani tunaweza kufanya kama hayo na hata Zaidi ya hayo.

Hivyo na sisi ni lazima tujifunze kutumia Ndimi zetu kuua baadhi ya vitu ambavyo shetani kavipanda katika maisha yetu.

Unapoamka kusali Ua kazi za giza katika siku yako, unapotembea zihukumu kazi za giza kwa kutumia kinywa chako.. kwasababu unapotamka na kuamini moyoni mwako basi fahamu kuwa ni lazima yatokee hayo uliyoyasema.

Zitamkie mauti kazi za shetani katika utumishi wako, katika familia yako, katika watoto wako, katika shughuli zako, katika vitu vyako unavyomiliki, Usiishie tu kuomba kimya kimya pasipo kutoa maneno yoyote.. Paza sauti kwasababu kuna nguvu Mungu kaiweka katika ulimi wa mwanadamu.

Wachawi na mawakala wote washetani wanajua nguvu iliyopo katika ulimi, ndio maana wanautumia kuleta madhara makubwa katika maisha ya watu.. sasa na watu waliookoka ni lazima kutumia ulimi kutangua maneno yote yaliyonenwa au yanayonenwa kinyume na maisha yetu ya kiroho na kimwili.

Vile vile ni lazima tutumie Ndimi zetu kutamka UZIMA wa vitu vilivyokufa katika maisha yetu. Nabii Ezekieli aliambiwa aitabirie mifupa mikavu ili iweze kuwa na uhai tena, na katika maono yale aliitabiria mifupa ile kwa kinywa chake na ikarudia uzima na likaamka jeshi kubwa sana (soma Ezekieli 37:1-8).

Sehemu zote Bwana Yesu alipoenda kuponya wagonjwa alitumia kinywa chake kutamka, na sisi ni lazima tutumie vinywa vyetu kutamka uzima juu ya vitu viliyokufa ndani yetu. Ikiwa ni huduma, ikiwa ni karama, ikiwa ni shughuli unayoifanya, ikiwa ni watoto, au kitu kingine chochote kilicho chema ni sharti kipate uzima kupitia kinywa chako!. Fanya hivyo daima, usiache hata siku moja hata kama unaona kwa nje ni pakavu, endelea kwasababu vita vya kiroho si vita vya kimwili, na ukiwa na bidii kufanya hivyo mwisho utakula matunda ya ulimi wako.

Mithali 18:21 “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

Rudi nyumbani

Print this post