Category Archive Mafundisho

VAA MAVAZI, USIVALIE MAVAZI.

Je hayo mavazi uvaayo ni kwa lengo gani?.. ili uonekane na nani?.. 

1 Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi”.

Sasa kuvaa mavazi si vibaya, hata hivyo tunapaswa tuvae mavazi, (hilo ni agizo la Bwana tangia Edeni, Bwana Mungu alipowafanyia mavazi ya ngozi wazazi wetu wa kwanza).

Lakini hapo katika 1Petro 3:3 hasemi “kuvaa mavazi”..bali na anasema “kuvalia mavazi”.

Kuna tofauti ya “kuvaa” na “kuvalia”.

Kuvalia maana yake “hayo mavazi yamelengwa kwa kusudi maalumu la kutazamwa na watu”

Kwamfano makahaba (wanawavalia mavazi ya kikahaba wateja wao ili miili yao iuzike vizuri). vile vile wahuni wanawavalia mavazi wahuni wenzao ili watazamwe na wao.

Kijana wa kiume anayevaa suruali ya kubana huyo hajavaa mavazi bali “amevalia mavazi”…. amewavalia mavazi aina fulani ya watu (wahuni wa kike), ili wamtazamapo wamtamani.

Dada anayevaa suruali ya aina yoyote ile, anakuwa hajavaa mavazi bali kavalia mavazi (kamvalia mtu),

Na lengo lake si lingine zaidi ya kutaka kutamaniwa, na Neno la Mungu linasema “yeyote amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye nafsini mwake”

Kwahiyo mwanamke anayetazamwa na kutamaniwa kwa uvaaji wake, naye pia kazini na yule aliyemtamani (hiyo ni kulingana na Neno la Mungu).

Kama unavyokuwa makini na kile kinachoingia ndani yako (yaani chakula)...vile vile ongeza umakini kwa kila unachojivika nje.

Usiwe mwepesi wa kwenda na kila fasheni inayoingia…kiasi kwamba kila mtindo unaoingia unaupokea, ni lazima uchague kama unavyochagua chakula.

Ni lazima uwe na uchaguzi unaokufaa kama vile ulivyo na uchaguzi wa baadhi ya vyakula vikufaavyo.

Jiulize je hilo vazi la mgongo wazi kama umevaa au umevalia,?…

Hilo vazi linaloonyesha kitovu na mapaja je umevaa au umevalia?

Hiyo kaptura kijana uliyoivaa na kutembea nayo barabarani umevaa kwa lengo gani?..je unamvalia nani?

Jisitiri, na pia jiheshimu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

LISIMAMISHE JIWE.

Jina la Mkuu wa Uzima (YESU KRISTO, Mwamba wa Milele), libarikiwe.

Lipo jiwe Yakobo aliloliweka chini ya kichwa chake kabla ya kulala na baada ya kuamka alilisimamisha likanyanyuka.

Jiwe hili lilibeba ufunuo wa YESU KRISTO, ambao napenda tuutazame leo.

Kipindi Yakobo anamkimbia Esau ndugu yake, alifika mahali fulani ambapo ni pa kawaida, lakini baadaye pakawa si pa kawaida.

Kabla ya kulala, alitwaa jiwe na kuliweka chini ya kichwa chake kama mto, huenda aliliona tu ni kama jiwe la kawaida lakini baada ya kuamka aligundua limebeba ufunuo mkubwa.

Mwanzo 28:10 “Yakobo akatoka Beer-sheba, kwenda Harani.

11 Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale.

12 Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake.

13 Na tazama, BWANA amesimama juu yake, akasema, Mimi ni BWANA, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka; nchi hii uilalayo nitakupa wewe na uzao wako……………

16 Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli BWANA yupo mahali hapa, wala mimi sikujua.

17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni.

18 Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake.

19 Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.

20 Na jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi”.

Unaona?..baada ya Yakobo kuamka usingizini aliona jiwe lile halipaswi tena kuwa kama Mto wa kulalia bali nguzo inayosimama.

Je na wewe jiwe hii umelisimamisha au unaendelea kulilalia tu.

Na Jiwe hilo si mwingine zaidi ya Bwana YESU.

1 Petro 2:4 “Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima”.

Jiwe hilo lililofungua ufahamu wa Yakobo na akamwona Mungu na Malaika wake usiku ule na hilo akalifanya kuwa NGUZO.

Akalifanya kuwa Nguzo ya nadhiri zake, akalifanya kuwa nguzo za hekalu la Mungu.

Je na wewe jiwe hili (YESU) umelisimamisha katika maisha yako au umelilaza?.

Kama jiwe hili limelala chini yako basi matokeo yake kwa nje ni tufani na maangamizi ya ibilisi, lisimamishe kuanzia leo.

Mitume wa Bwana YESU walijua umuhimu wa kulisimamisha Jiwe Bwana YESU katika ile tufani ilipotokea baharini..

Marko 4:35 “Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo.

35 Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye.

37 Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji.

38 Naye mwenyewe alikuwapo katika shetri, amelala juu ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?

39 Akaamka, akaukemea upepo, akaiambia bahari, Nyamaza, utulie. Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu”

Ukiwa Yesu uliye naye ni yule wa kidini tu, yule wa kurithi kwa wazazi….basi fahamu kuwa ni Jiwe lililolala chini yako.

Ukiwa ukristo wako ni ule wa mazoea tu, usio na hofu na Mungu, basi jua kuwa unalo jiwe lililo lala.

Ikiwa ukristo wako ni ule wa ndoto na maono tu, na hutaki kujifunza Neno la Mungu basi fahamu ya kuwa jiwe lako limelala.

Yakobo baada ya kuona maono yale hakuendelea kulifanya lile jiwe kuwa Mto badala yake alilisimamisha mbele yake, lakini utaona wakristo wa leo baada ya kuona maono mawili matatu ya kiMungu, basi hata Neno la Mungu halisomwi tena, wanabaki tu kuendelea kuishi kwa ndoto na maono, jambo ambalo ni hatari sana.

Lisimamishe jiwe, lisimamishe jiwe.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

AINA TATU ZA UTAKATIFU

Zipo aina tatu za Utakatifu, na leo tutaangalia moja baada ya nyingine, na tutajua ni upi unaotufaa sisi.

Aina hizi za utakatifu ni kama ifuatavyo.

1.UTAKATIFU WA MWILINI

2. UTAKATIFU WA ROHONI

3. UTAKATIFU WA MWILINI NA ROHONI.

 1.UTAKATIFU WA MWILINI.

Ni ile hali ya kuuweka mwili katika viwango vya kumpendeza MUNGU, ikiwemo kuvaa vizuri kiasi kwamba mtu akikutazama basi anaona ushuhuda wa Kristo katika uvaaji wako na mwonekano wako.

Vile vile utakatifu wa mwilini unahusisha, kujilinda na matendo yote ya mwili yanayotajwa katika Wagalatia 5:19-20…ikiwemo uasherati, ulevi, kujichua, kujichubua na mengineyo.

Mtu anaweza kuwa na utakatifu huu wa mwilini na ule wa rohoni akaukosa. Anaweza kuwa na mwonekano mzuri sana wenye ushuhuda lakini akaukosa ule wa rohoni.

Sasa utakatifu wa rohoni ni upi?.

             2. UTAKATIFU WA ROHONI.

Utakatifu wa rohoni ni ule unaohusisha, matendo yote ya rohoni yanayompendeza MUNGU.

Ikiwemo kuomba, kutoa sadaka (Mathayo 6:4), kumwabudu Mungu katika roho, kujifunza na kutafakari Neno la Mungu, vile vile upendo, uvumilivu, utu wema, kiasi.

Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.

Mtu akiwa na matunda hayo basi kibiblia ni mtakatifu rohoni.

Sasa ni rahisi sana mtu kuwa mtakatifu mwilini na asiwe mtakatifu rohoni, lakini ni jambo la Nadra sana kukuta mtu mtakatifu rohoni na mwilini akawa si mtakatifu.

Watu wengi wenye utakatifu rohoni halafu nje mwonekano wao hauna ushuhuda, wengi wao ni watu wanaovaa viatu vinavyowabana, huwa wanajua kabisa kuwa mionekano yao haina ushuhuda kwasababu ya Roho Mtakatifu aliye ndani yao, isipokuwa kuna mazingira yanayowafanya wabaki katika hiyo hali.

Na mazingira hayo yamegawanyika katika sehemu mbili.

Sehemu ya kwanza: Viongozi wao wa kiroho wanawachanganya.

Wengi wanaotamani kubadili mionekano yao ya nje, wanapowatazama viongozi wao wa kiroho kuwa ndio watu wanaoongoza katika kuvaa ovyo, wanachanganyikiwa na kubaki kufikiri kwamba wao wana makosa na viongozi wao wapo sawa, hivyo wanabaki katika hali ya ubumbuazi wa kiroho, wanashindwa kujua nini cha kufanya na wanaishia kupokea yale viongozi wao wanayoyasema na kuyatenda.

Dada/kaka kama upo katika hili kundi, basi sikia sauti ya Roho Mtakatifu leo. KAMILISHA UTAKATIFU WAKO WA MWILINI, ni kweli matendo yako ya rohoni ni mema na mazuri, sasa umebakisha hilo moja tu la Rohoni, ondoa hayo mapambo ya kidunia mwilini mwako, ondoa hizo hereni, ondoa hiyo mikufu, ondoa hizo bangili, ondoa hizo rangi usoni, ondoa huo mtindo wa nywele na uvaaji usio na ushuhuda, na utapanda viwango vingine vya kiroho.

Usichanganywe na miujiza inayofanywa na viongozi wako wa kiroho, hata kama ndiye aliyekuleta kwa Kristo, basi asikuogopeshe na kukufunga usilifuate Neno la Mungu.

Hata kama ana hubiri vizuri, usiogope, hata kama aliwahi kukuombea ukapona, bado uasiogope..Neno la MUNGU ni nyundo na upanga ukatao kuwili, na Bwana alisema wengi watakuja siku ile na kusema walitoa pepo na kufanya miujiza kwa jina lake lakini atawafukuza.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Sehemu ya pili: Wazazi na Ndugu.

Wazazi na ndugu ni sehemu kubwa na kuuzia utakatifu wa mwilini kwa mtu, kwani wengi wanapoona na kusikia ushauri wa ndugu, bali ule ushauri unaweza kuwa mzito sana zaidi hata ya mtu mwingine yeyote.

   3. UTAKATIFU WA MWILINI NA ROHONI.

Utakatifu wa mwilini na rohoni ni ile hali ambapo mtu anakuwa na ushuhuda wa ndani roho yake na nje ya mwili wake. Na huu ndio utakatifu Mungu anaouhitaji kwetu.

1 Wakorintho 7:34 “….. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho….”

Utakatifu wa mwilini na rohoni ndio msingi wa sisi kumwona Mungu sawasawa na ile Waebrania 12:14.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”.

Timiza utakatifu wako Mteule wa MUNGU..

2 Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”

VIWANGO VYA UTAKATIFU.

Katika kuwa watakatifu wa mwilini na rohoni ni lazima viwango vyetu viwe juu zaidi ya watu wasio wa Kristo.

Mathayo 5:20 “Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”.

Maana yake ni kwamba kama kumcha Mungu basi ni lazima tuwazidi wa imani nyingine, kama kuvaa kwa staha ni lazima tuwazidi watu wengine wote wasio wa Imani n.k.

Bwana YESU atusaidie sana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

MMOJA APANDA, MWINGINE ATIA MAJI.

Huwezi kufanya kazi zote peke yako..

Aliyeunda injini ya gari, alihitaji mwingine mwenye ubobezi katika utengenezaji wa matairi, lakini pia alimhitaji mbobezi wa umeme wa magari, hivyo ili gari lisimame na kuanza kutembea limegharimu mikono na ujuzi wa wataalamu wengi.

Vile vile, mtumishi wa Mungu mmoja hawezi kufanya mambo yote peke yake, kuna wakati wengine watahusika tu.

Katika biblia kuna mahali Filipo alihubiri na kubatiza, lakini lakini Petro na Yohana waliwaombea hao waliobatizwa ili wajazwe Roho Mtakatifu.

Matendo 8:12 ”Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake.

13 Na yeye Simoni mwenyewe aliamini akabatizwa, akashikamana na Filipo; akashangaa alipoziona ishara na miujiza mikubwa inayotendeka.

14 Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana;

15 ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu;

16 kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.

17 Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu”

Umeona? mmoja Anabatiza wengine wanaombea ujazo wa Roho Mtakatifu..

Mambo yote yanakamilika namna hiyo katika ushirikiano na umoja wa Roho, na ndivyo kanisa la kwanza lilivyoenenda, hakukuwa na mashindano wala wivu katikati yao, tofauti na leo ambapo kila mtu anajiona bora kuliko mwingine.

Maandiko yanazidi kutuonyesha kuwa hata Paulo, hakupanda na kuwagia yeye, bali matunda yake yalipaliliwa na wengine.

1 Wakorintho 3:6-7 “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.

7 Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye”.

Kama mtumishi wa Mungu, Je unaweza kuruhusu watumishi wengine wawajenge wale uliowatafuta wewe?…

Kumbuka si kila mtumishi ni wa kweli!…wengi ni wa uongo, lakini je inapotokea umehakiki kuwa kweli yule ni mtumishi wa Mungu, je waweza kuruhusu yule uliyemvua wewe ajengwe na mtumishi mwingine kama wewe?.

Kama hilo jambo gumu basi msaada wa haraka kutoka kwa Bwana unahitajika kwasababu ndivyo Mitume walivyofanya na sisi tunapaswa tufuate hivyo vielelezo.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAFUNUO YA ROHO.

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

Washami ni watu gani katika biblia?

Rudi Nyumbani

Print this post

UCHAWI UNA GHARAMA, JIFUNZE KUMTOLEA MUNGU.

(Masomo maalumu yahusuyo faida za matoleo).

Jifunze kutoa sadaka!!, jizoeze kutoa sadaka, jitaabishe kutoa sadaka!!.

Utoaji si agizo la washirika bali hata viongozi (wachungaji, waalimu, wainjilisti na watu wote wanaoujenga mwili wa Kristo), pasipo kujali Umri wala kipato. Hili ni agizo la Bwana YESU lenye baraka na laana nyuma yake (soma Mathayo 25:31-46).

 Sadaka inayotolewa katika misingi ya Neno la Mungu, inafanya mambo makubwa zaidi ya yale tuyajuayo.

Sadaka inayotolewa katika msingi wa Neno la Mungu, inameza sadaka nyingine zilizotolewa na upande wa ibilisi.

Ile fimbo ya Musa ilibidi aitoe na kuitupa, ndipo ilipoweza kumeza zile fimbo nyingine za wachawi wa Farao.

Sasa zile fimbo zilizomezwa, laiti zingeendelea kuwepo zingeleta madhara mengine kwani zilikuwa ni za kichawi, na zilitumika na wachawi kwa shughuli za kichawi.

Sasa ilimgharimu Musa kuitoa fimbo yake kwanza ili imeze zile nyingine. Vile vile iliwagharimu wachawi kutoa fimbo zao za gharama ili wahindane na Musa.

Vile vile kuna mambo mengine yanahitaji tu matoleo yatatuke..(Kasome Waamuzi 20:20-40).

Sasa wale waganga wa Misri walizigharimia zile fimbo zao, hazikutokea tu… huenda walizinunua kwa fedha na kuzifanyia matambiko mengi.

Kitabu cha Matendo ya Mitume kinatuonyesha jinsi waganga wanavyougharimia uganga wao.

Matendo 19:17 “Habari hii ikajulikana na Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawaingia wote, na jina la Bwana Yesu likatukuzwa.

18 Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao.

19 Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu

Hapo anasema gharama ya vile vitabu vya uganga vilivyochomwa ilikuwa ni elfu 50.

Sasa tukisema elfu 50, kwenye vichwa vya wengi inadhaniwa ni shilingi za kitanzania, zinazotosha tu gharama ya nauli kutola mkoa mmoja hadi mwingine..La!.

Kujua thamani halisi ya vipande vya fedha elfu 50…rejea kile kiasi Yuda alichoongwa ili amsaliti Bwana YESU, maandiko yanasema alipewa kiasi cha vipande 30 tu vya fedha na vipande hivyo vilitosha kununulia shamba (ambalo hatujui ni hekari ngapi) lakini tunajua ni hekari nyingi maana zilitumika kama eneo la makaburi..soma Mathayo 27: 3-7.

Sasa piga hesabu kama vipande 30 vya fedha ya Yuda vimenunua shamba, na hapo vitabu vya waganga gharama yake ni vipande vya fedha elfu 50..gawanya hapo uone waganga waliugharimia uganga wao kiasi gani…

Utaona hapo ni zaidi ya mashamba 1,600 na kama shamba moja litauzwa tu kwa gharama ya shilingi za kitanzania milioni moja…basi jumla yake vile vitabu vyote ni zaidi ya BILIONI MOJA.

Kwahiyo wale waganga waligharimia mabilioni kuusimamisha uganga wao!!!…..

Halafu wewe na mimi kuigharimia injili  kidogo tu tunaona tabu!!!!…..Fikiri mara mbili…fikiri mara mbili!!!.

Jenga ufalme wa Mungu, kwani shetani anajenga ufalme wake kwa kasi na gharama.

Bwana atusaidie.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

UCHAWI WA BALAAMU.

Kupiga ramli ni nini katika biblia?

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

UJIO WA BWANA YESU.

Rudi Nyumbani

Print this post

IHUBIRI INJILI, KILA MAHALI KWASABABU AKUZAYE NI MUNGU.

Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe.

Upo umuhimu wa kuhubiri injili mahali popote na katika mazingira yoyote kwasababu ni agizo la Bwana mwenyewe (Mathayo 28:18-20).

Wapo wanaoamini kuwa injili ya mitaani na masokoni hazina faida yoyote kwasababu watu wanakuwa hawapo katika utulivu.

Na pia wapo wanaoamini kuwa injili  za kwenye mikutano au makanisani ndizo zilizo bora kwasababu watu wanakuwa katika utulivu.

Lakini nataka nikuambie Injili zote zina umuhimu, (Za watu walio katika utulivu na utayari wa kusikiliza na za ambao hawako katika utayari)... na Mitume wa Bwana YESU walihubiri zote (katika masinagogi na masokoni).

Matendo 17:17 “Basi katika sinagogi akahojiana na Wayahudi na waliomcha Mungu, na wale waliokutana naye sokoni kila siku”.

Na hata Bwana wetu YESU alifanya hivyo pia..

Luka 8:1 “Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye”

Lakini leo nataka nikupe umuhimu wa injili za mitaani (za watu wasio na utayari wa kusikia).

Kikawaida ni ngumu kumsimamisha mtu barabarani na kumwambia asimame asikilize… Wengi wanakuwa hawana utayari huo.

Lakini anapopita au anapokuwa ameketi na wewe kukaa mbali naye kidogo na kulazimisha asikie kile anachokisema pasipo hata ridhaa yake, kuna vitu vitaingia ndani yake hata kama hataki.

Kwani lile Neno atakalolisikia hata kama ni moja, litakuwa mbegu njema ndani yake ambayo itachupuka kwa wakati wake.

Kwahiyo ni heri kusikia hata hilo moja kuliko kutokusikia kabisa, kwasababu wengine hata kanisani hawaendi kabisa, wengine ni wa imani nyingine, hawajawahi na wala hawana mpango wa kwenda kanisani wala kusogea mahali penye mahubiri….na wengine wanaamini wapo sahihi katika njia zao, hivyo hawahitaji kusikia kingine chochote, wameridhika na kutosheka na wanavyovijua au walivyo navyo.

Hivyo ukisema uwasubiri, au uombe ridhaa ya kuzungumza nao, hawafungui huo mlango!…sasa kundi hili linasaidikaje?…je kwa kuliacha tu?…au kusubiri au kuliombea tu!…

Jibu: Linasaidika kwa kusikia kwa lazima!.

Ezekieli 2:7 “Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana”

Umeona?..ni lazima wasikie kwa lazima…Kwani atakapolisikia lile neno, pengine alishakwisha kusikia mengine kama hayo 99 na hivyo hilo moja lilikuwa limesalia kufikia hatua yake ya kutafakari zaidi na kutubu…na kupitia hilo neno moja basi ataenda kukata shauri la kumpokea Bwana YESU au kuachana na mwenendo anaouendea.

Vile vile huenda hilo la kwako ndilo Neno lake la kwanza kati ya maneno 99 yanayomngojea mbele ili aokoke. Kwahiyo unaposema na kuhubiri, unakuwa umeianza safari nyingine ndani ya maisha yake, ambayo inaweza kukamilika pengine baada ya miezi au miaka baadae…

Tatizo kubwa linalotukumba wahubiri ni kuona mtu hakati shauri pale pale tunapohubiri, pasipo kujua kuwa kazi za Roho Mtakatifu ndani ya mtu hatuwezi kuzitafsiri kwa akili.

Wapo ambao wanaosikia Neno kwa mara ya kwanza, wengine ndio mara ya pili na wengine ni mara yao ya mia na ya kuokoka.

Ni wachache sana, ambao wamepewa Neema wanaweza kukata shauri la uhakika siku ile ile wanapolisikia Neno, huwa wengi wanakuwa ni mashamba yenye magugu mengi, ambao inawachukua muda kutengenezeka, wanahitaji kusikia mara nyingi, ndio maana Bwana Mungu alikuwa anawatuma manabii wake kupiga kelele katika miji na vijiji, mara nyingi sana, kwasababu ya ugumu wa mioyo.

Isaya 58:1 “Piga kelele, usiache, Paza sauti yako kama tarumbeta; Uwahubiri watu wangu kosa lao, Na nyumba ya Yakobo dhambi zao”.

Kazi ya kuhubiri si nyepesi, ni mapambano mengi na uvumilivu mwingi, na endelevu mpaka mmoja atubu, ndio maana maandiko yanasema mmoja anapopatikana basi malaika wanashangilia.

Luka 15:10 “Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye”

Swali ni je! UMEOKOKA???.

Pengine ni wewe ndiye unayeisikia injili muda mrefu na hutaki kubadilika, hutaki kuacha udunia, hutaki kuacha kuvaa suruali mwanamke, hutaki kuacha kuvaa vimini, hutaki kuacha ukahaba na ulevi, na kiburi na usengenyaji na wivu… nataka nikutahadharishe jambo moja kuwa Injili ya kurudia rudia kwako si mfano wa yale matangazo yanayojirudia kwenye redio au Tv, bali ni ushuhuda!.

Mathayo 24:14 “Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja”.

Kama umeisikia mara kwa mara na unaendelea kuidharau, utakutana nayo mbele ya kile kiti cha hukumu, na hiyo itakuhukumu, hiyo ni kulingana na biblia.

Warumi 2:16 “katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu”.

Sasa endelea kusitasita na kuwa hivyo ulivyo mpaka ile siku…haya yote unayoyasoma na kuyasikia, utayathibitisha siku ile.

Bwana atusaidie..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

IMANI NI NINI?

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

TUSIWE WAVIVU WA KUSIKIA.

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

Rudi Nyumbani

Print this post

VIGEZO VYA NEEMA YA MUNGU.

Tangu mwanzo mwanadamu alikuwa akijaribu kujiokoa kwa njia yake mwenyewe ikiwemo kuonyesha matendo yake mazuri, na mwenendo wake mkamilifu lakini hakuweza. Pengine aliweza kushinda wizi kikamilifu lakini uongo ukamshinda, aliweza kushinda uzinzi wote, lakini tamaa zikamtawala, aliweza kushinda ibada za sanamu na vinyago, lakini kusamehe kukamshinda. Alipoweza kushinda kimoja, nyuma yake kulikuwa na elfu vinavyo mhukumu.

 

Na hiyo ilimfanya asikidhi vigezo vya kuingia mbinguni, kwasababu watakaoiona mbingu na Mungu ni watakatifu asilimia mia wasio na doa lolote. Ndio maana maandiko yanasema wote wameoza,wamepotoka hakuna amtafutaye Mungu. Bali tunahesabiwa haki bure kwa neema ya Bwana Yesu Kristo.

 

Warumi 3:11  Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu. 12  Wote wamepotoka, wameoza wote pia; Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja.

 

Ndio sababu ya Yesu kuja duniani, ili kwa kupitia kumwamini yeye tuipokee hiyo neema ya kuitwa watakatifu, bila kuonyesha kwanza kipimo chochote kwa Mungu. 

Maana yake ni kuwa mimi na wewe tunapomwamini Yesu Kristo, ni moja kwa moja tunaitwa watakatifu, tuliosamehewa dhambi zetu, na kuondolewa pia. 

 

Ikiwa umemwamini leo Yesu Kristo, moja kwa moja Mungu hakuhesabii tena dhambi yoyote kama mkosaji. Ijapokuwa utakuwa hujakamilika bado.  Hii ndio maana ya neema, yaani kukubaliwa kusikostahili. Ilikupasa kwanza uwe na matendo makamilifu asilimia 100 kama Bwana Yesu, ndio uitwe mtakatifu uliyestahili kumwona Mungu. Lakini sasa kwa kuupokea ukombozi wa Yesu Kristo, dhambi zako, zimefuta unaitwa mtakatifu, kabla hata ya ukamilifu wa utakatifu wenyewe kukufikia. Ndio maana sisi tulio ndani ya Kristo hatuna budi kuwa na amani, na furaha wakati wote. Kwasababu ule mzigo mzito wa kujitahidi sisi wenyewe kuingia mbinguni umeondolewa na Yesu Kristo Bwana wetu, kwa kifo chake pale msalabani.

 

 

Lakini sasa, katika nyakati hizi za mwisho suala hili la neema limetafsirika vibaya, kama tu nyakati zile za zamani, na hapo yatupasa  tuwe makini sana. Ni sawa na taifa litangaze neema kwa nchi yake na kusema, sasa huduma zote za maji ni bure, hakuna kulipia bili,matumizi ni kama unavyotaka. halafu uone watu wanatumia fursa hiyo kwenda kufungulia  mabomba yatiririshe maji kwenye mitaro na mabarabarani, kila mahali kuwe ni maji tu,  Bila shaka utasema hawa watu wamerukwa na akili, hawana sifa ya kupewa huduma hiyo tena.

 

Ndivyo ilivyo kwa jambo linaloitwa neema, tusijipojua kanuni zake, tutajikuta badala ya kupokea wokovu, tunapokea maangamizi. Badala ya kukazana kumpendeza Mungu, tunastarehe katika dhambi,  Na ndicho kinachoendelea sasa kwa sehemu kubwa miongoni watu na madhehebu.

 

Yafuatayo ni mambo ambayo ujiepushe nayo kwa nguvu zote, wewe uliyeipokea neema ya Mungu.

 

  1. Kuipokea neema bure,

2 Wakorintho 6:1

[1]Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.

Ukisoma vifungu vichache vya nyuma anasema mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya, ya kale yamepita tazama yamekuwa mapya.

 

Mtu ambaye hataki geuko, baada ya kusamehewa dhambi zake, huyo ni mtu ambaye ameipokea neema bure, haithamini, ameitwa mtakatifu, halafu hataki kuishi maisha matakatifu, anaendelea na maisha yake yale yale ya kale.. Mtu kama huyo asijidanganye neema hiyo ni batili. Mtu yeyote aliyeokoka  wakati huo huo una wajibu wa kuanza kupiga hatua za mabadiliko, na unapaswa uithamini sana hiyo zaidi ya vyote, kwasababu ni Mungu ndiye akutakasaye baada ya hapo.

 

Lakini pia mtu ambaye amekaa muda mrefu hamzalii Mungu matunda, anahesabika kama aliyeipokea neema ya Mungu bure, na hivyo mwisho wake unakuwa ni kukatwa.

 

Tito 2:11  Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa;12  nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; 

 

Je! Umeitii neema hii inayokufundisha kukataa machafu ya duniani?. Leo yapo madhehebu yanayosema, ukiokoka umekoka milele, kazi yako imeisha, hata usipoonyesha  bidii nyingine yoyote kwa Mungu,huwezi potea. Ndugu yangu kuwa makini sana na imani hizi. Neema haipokelewi bure.

 

  1. Kuipungukia Neema

Epuke pia  kuipungukia neema.

 

Waebrania 12:15-17

[15]mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo. 

[16]Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kimoja. 

[17]Maana mwajua ya kuwa hata alipotaka baadaye kuirithi baraka, alikataliwa (maana hakuona nafasi ya kutubu), ijapokuwa aliitafuta sana kwa machozi.

Kuipungukie neema Ni tabia ya kuishusha thamani neema, na kuilazimisha  itende kazi hata katika kiwango ambacho si chake.

 

Hii hasa huja kwa watu ambao wanazoelea kufanya dhambi mara kwa mara wakiamini kuwa kwasababu Mungu hawahesabii makosa basi hata wakifanya kosa lolote hawawezi kupotea.

Ndugu, neema si kuhalalisha maisha ya dhambi. 

Biblia inasema..

Warumi 6:1  Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? 2  Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi?

3  Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

4  Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

Usitende dhambi za mazoelea, ukadhani neema itakuwa sikuzote kukufunika. Ukiifanyia jeuri neema, itaondoka kwako.

 

Waebrania 6:4  Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5  na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, 6  wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

 

  1. Kuibadili neema ya Mungu.

 

Yuda 1:4  Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.

 

Neema ya Mungu inaweza badilishwa ikamaanishwa kivingine kabisa. Kwamfano utaona leo hata mashoga, wanavyama vyao wakisema sisi tupo chini ya neema. Walevi nao, wenye dhambi nao wanasema neema ya Yesu ipo duniani sasa, kumwokoa kila mtu.

 

Hivyo watakuambia maneno kama usihukumu usije ukahukumiwa. Na wana amani na ujasiri katika hayo wanayoyafanya na wengine wanajiita maaskofu na wachungaji, wakihalalisha kila kitu kiovu kufanyika kwa kivuli cha neema.

 

Hao ndio waibadilishao neema ya Bwana Yesu kuwa ufisadi, hilo Neno ufisadi ni zaidi ya uasherati, Ni pamoja na matendo yote maovu kupita kiasi. Lakini neema ya Yesu,.haikuja kufunuki dhambi, bali ilikuja kuondoa dhambi ndani ya mtu. Usiwe mmojawapo aibadilishaye neema ya Mungu.

 

Hivyo kwa vifungu hivyo itoshe kusema kuwa NEEMA tunaipokea bure, lakini ili iweze kufanya kazi lazima tujue sifa zake,  kisha tuzikubali, vinginevyo tutajidanganya na kuangamia.  Ni sawa na mtu akupe gari bure, lakini usipoliweka mafuta, na kujua kuliendesha linakuwa halina tofauti na mdoli wa gari.

Lakini ukiithamini neema, itakutunza, itakuhifadhi na kuyaficha makosa yako yote, Hivyo utaendelea kuonekana mkamilifu asilimia mia mbele za Mungu, na hata ukifa, ni moja kwa moja mbinguni.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

Print this post

IFUATE KANUNI SAHIHI YA MUNGU

Zipo kanuni za ki-Mungu tunaweza kuzifuata na zikaleta matokeo kabisa halisi, lakini zisiwe na manufaa kwetu katika suala la wokovu.  Sasa kabla ya kuangalia ni kwa namna gani? 

chukulia mfano wa kawaida.

Mwanamke yeyote anaweza kubeba ujauzito katika mazingira mbalimbali, kwamfano anaweza akatwezwa nguvu (akabakwa), na akapata ujauzito, lakini pia anaweza kwenda kujiuza kama kahaba na bado akapata ujauzito, vilevile anaweza akasubiri aolewe kwanza katika ndoa halali ndipo apokee ujauzito na likafanikiwa vilevile tu, kuleta kiumbe duniani, kama angefanya hayo kabla ya ndoa, au atokapo nje ya ndoa yake.

Sasa unaweza jiuliza, katika njia zote hizo ambazo angepata ujauzito ni ipi iliyo halali inayokubalika mbele za Mungu na wanadamu. Bila shaka ni hiyo njia ya mwisho ambayo ni ya kuolewa kwanza, ndipo apokee ujauzito kutoka kwa mume wake mmoja wa halali. Na ndio mtoto huyo hujulikana kama halali sio haramu.

Lakini cha ajabu ni kuwa ijapokuwa njia halali ipo lakini feki pia huleta matokeo yaleyale mfano wa halali. Kwasababu gani? Kwasababu kanuni ya kupata mtoto, si kanuni ya uhalali. Hivyo ni vitu viwili tofauti, 

Hata Ibrahimu, alikuwa na watoto wengi, alitangulia Ishmaeli, kisha baadaye wakazaliwa na watoto wengine sita kwa suria mwingine, mbali na Isaka. Wote walikuwa wanadamu, viumbe wa Mungu, wenye akili na nguvu na baraka, wasio na hatia. Lakini lilipokuja suala la urithi, ndipo kubaguliwa  kulipokuja, Watoto wote wa masuria walifukuzwa wakapewa zawadi tu bali Isaka alipewa vyote.

Mwanzo 25:5-6

[5]Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo. 

[6]Lakini wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake, waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu. 

Hii ni kutufundisha nini hasaa katika maisha yetu ya wokovu.

Zipo kanuni nyingi sana za kiroho ambazo mtu yeyote, hata ambaye  hajamwamini Yesu anaweza zitumia na zikatoa matokeo yaleyale sawa tu na mtu ambaye ameokoka.

Kwamfano, kufanya miujuza na ishara kwa jina la Yesu. Watu hawajui kuwa jambo hili huhitaji imani tu, katika jina lake. Hivyo wale wafikiao kiwango hicho haijalishi ni mwizi, ni mpagani, anaweza pokea muujiza na akafanya pia muujiza sawa tu na yule aliyeokoka.

Kwasababu gani? kwasababu amefanikiwa kufuata kanuni ambayo ni Imani.

Akijua lile neno linalosema  ‘yote yawezekana kwake yeye aaminiye’’ (Marko 9:23). Ndio maana walikuwepo watu wengi wasiokuwa wayahudi kipindi kile cha Yesu walipokea miujiza mikubwa, zaidi ya wayahudi kwasababu tu ya ukubwa wa imani zao. Na sio haki zao.

Vivyo hivyo hata katika kuomba. Mtu yeyote aombaye hupokea. Ni kanuni ya asili ya rohoni, haijalishi ni nani.

Mathayo 7:8

[8]kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. 

Watu hawajui hata kufanikiwa kwa shetani hutegemea maombi, na yeye pia huenda mbele za Mungu kuomba na hupewa..hajiamulii tu mambo yake ovyo ovyo bila idhini ya Mungu, kwasababu hii dunia si yake… utauliza kwa namna gani, ? unamkumbuka shetani kipindi cha Ayubu, yeye naye alikwenda kujihudhurisha mbele za Mungu, ndipo akaleta uharibifu. Akapeka haja zake akasikiwa, dua zake na magoti yake.

Ayubu 1:6

[6]Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao. 

Watu wengi wanapoona wanamwomba Mungu wanajibiwa wanadhani, ndio wamekubaliwa na Mungu. Kumbe unaweza kuomba kama mwana-haramu usiyekuwa na urithi wa uzima wa milele, bali haki ya kupokea tu unachokiomba.

Unaweza ukafanya miujiza kama mwana-haramu. Lakini usiende mbinguni.

Mathayo 7:22-23

[22]Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? 

[23]Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu. 

 Unaweza ukamwamini Yesu, na kumuhofu,  lakini ukaamini kama mashetani.

Yakobo 2:19

[19]Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka. 

unaweza ukawavuta watu kwa Kristo na wakaokoka, lakini ukawa mtu wa kukataliwa kama tu Paulo alivyosema katika; 

1 Wakorintho 9:27

[27]bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa. 

Sasa kanuni sahihi ya Mungu ni ipi ili tuonekane kamili na halali?

Kanuni Mungu anayoitazama kwetu ni Wokovu uliokamilishwa kwa matendo yake.

Angalia mwishoni pale kwenye Mathayo 7:23 Bwana Yesu alichokisema;

“ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Umeona je unaishi maisha gani?. hicho ndio kipimo cha ki-Mungu, 

Alisema pia.

Yakobo 2:24

[24]Mwaona kwamba mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake. 

Hakikisha maisha yako yanaendana na ukiri wako, wa imani yako, usiishi tu kama mtu ambaye hajaamini ukijitumainisha, kuona maombi yako yanajibiwa, karama yako inafanya kazi, imani yako inatenda kazi..hizo ni kanuni za kupokea lakini sio kanuni za uhalali wa kuurithi uzima wa milele. Ishi kama mtu ampendezaye Bwana wake kimwenendo, ndipo hayo mengine yakifuata huna hasara.

Nyakati hizi za mwisho, adui anaweka uzito kwenye mioyo ya watu wasipende kutafuta maisha matakatifu, kinyume chake wabakie tu kwenye miujiza, uponyaji, utabiri…Siku ile hivyo vitu havitafuata na wewe ndugu, bali matendo yako.

Ufunuo wa Yohana 14:13

[13]Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao. 

Tuanze sasa kujipima mienendo yetu. Kisha tutumie nguvu nyingi hapo kujirekebisha, sawasawa na imani tuliyoipokea, ili tuwe wana halali waliozaliwa kweli ndani ya Kristo, watakaorithi uzima wa milele.

Wokovu wa kweli hufunuliwa kwa mwenendo mzuri. Tuitazame sana kanuni hii.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KANUNI JUU YA KANUNI.

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI AU KUTOA TALAKA?

Print this post

KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU. 

Nehemia 8:10

[10]Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa BWANA wetu; wala msihuzunike; KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU.

Ni habari ya kutafakarisha, lakini zaidi sana ya kuwafariji watu wote wampendao Mungu. Tukisoma katika biblia ile habari ya Ezra na Nehemia, katika juhudi zao wa kuwarejesha Israeli katika ibada na njia za Mungu Yerusalemu.

Tunaona wakati ule ukuta wa Yerusalemu ulipomalizwa kujengwa baada ya kurudi kwao utumwani Babeli, Ezra hakuwaacha tu hivi hivi, wafurahie kukamilika kwa majengo, bali alitaka wakamilishwe na mioyo yao hivyo, alikichukua kitabu cha Torati na kuanza kuwasomea wayahudi wote tangu asubuhi mpaka adhuhiri, ili wajue ni nini Bwana anataka kwao (Nehemia 8).

Na waliposikia waliona makosa yao mengi sana, na hukumu nyingi za Mungu, alizowatamkia kufuatana na makosa yao, yaliyowapelekea mpaka wakachukuliwa mateka. Ikumbukwe kuwa kitabu hicho cha torati hakikuwahi kusomwa tangu zamani walipochukuliwa utumwani, ndio ilikuwa mara yao ya kwanza kukisoma baada ya miaka mingi kupita.

Hivyo wayahudi kusikia vile wakaanza kulia sana na kujuta na kuomboleza. Lakini tunaona kuna jambo lilifanyika la kitofauti.

Nehemia, alitambua wazo la Mungu…Hivyo akawazuia watu kulia na kuomboleza kwa ajili ya makosa yao. Kinyume chake akawaambia leo ni siku takatifu kwa Bwana, hivyo mle ,.mnywe, mtoe sadaka, mfurahi mbele za Mungu wenu kwasababu “furaha ya BWANA ni nguvu zenu” 

Hivyo watu wakasheherekea, badala ya kulia, Sio kwamba Nehemia alisheherekea makosa yao, hapana, bali alipewa kujua kwamba  furaha ya mtu kwa Mungu wake, ndio chanzo cha nguvu ya kumtumikia yeye. 

Ndio hapo baada ya wayahudi kujua makosa yaowakimfurahia Mungu, siku hiyo, na wakapokea nguvu nyingi za kuishika sheria ya Mungu. 

Yaani kwa namna nyingine, Mungu kuwakemea makosa yao,lengo lake lilikuwa sio awahukumu, au wainamishe vichwa vyao wakidhani kuwa wao ni kichefu-chefu kwake. Hapana..Bali anawapenda na hivyo anatarajia wajue nia ya makemeo yake.

Nehemia 8:10 Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.

11 Hivyo Walawi wakawatuliza watu wote, wakasema, Nyamazeni, kwa maana siku hii ni takatifu; wala msihuzunike. 

12 Na watu wote wakaenda zao kula na kunywa, na kuwapelekea watu sehemu, na kufanya furaha nyingi, kwa sababu walikuwa wameyafahamu maneno yale waliyohubiriwa

 

Ni hata sasa, unaposoma biblia na kuona inakushitaki, inakuambia usiibe, usisengenye, amchukiaye ndugu yake ni sawa na muuaji, wazinzi wote sehemu yao ni katika lile ziwa la moto, inapokukemea maovu yako ya siri.. Usiinamishe kichwa na kusema “mimi sifahi mbele za Mungu, mimi ni mkosefu sistahili kuitwa mwana wake”..Ukaacha kukisoma kabisa, ukawa unalia tu, umenyong’onyea, na kujihisi wewe ni wajehanamu tu, Mungu hakupendi, ameshakuacha, ona sasa unamkosea kosea kila siku… Fahamu kuwa hilo sio kusudi la Mungu.

Kusudi la Mungu sio usome biblia, ujawe na hisia za Mungu kukuhukumu, au kukulaumu, au kukushitaki, bali kusudi la Mungu ni ujue  upendo wake uliozidi sana kwako, kiasi cha yeye kuonyesha hisia zake kwako namna ambavyo unapaswa uwe kama yeye.

Hivyo ukitoka kuonywa na kukemewa, unapaswa utoke kwa kufurahi moyoni  na kuruka-ruka, na hapo ndipo utapokea nguvu ya kuishinda hiyo dhambi. Lakini ukitoka kinyonge na mashaka utashindwa kwasababu furaha ya Bwana ndio chanzo cha nguvu zetu. Ukilipenda hilo katazo, utalitenda, usipolipenda kamwe huwezi litenda.

Mtunga Zaburi alisema,

Zaburi 119:52

[52]Nimezikumbuka hukumu zako za kale, Ee BWANA, nikajifariji.

Bwana anataka tuone upendo wake kwetu katika makemeo yake, tufarijike tupokee nguvu ya kushinda. Pengine umetoka kufanya dhambi fulani ya makusudi na Roho Mtakatifu akakumbusha kuwa watu wa namna hii, huangukia katika mtego mbaya wa shetani bila kunasuka, Sasa hapo usianze kupoteza ladha na Mungu wako, au biblia, ukauchukia wokovu, kabisa,  maanisha kutubu, jifunze kutokana na makosa, kisha furahia mwambie Bwana asante kwa kunipenda,

hata wachezaji wa mpira, wafungwao kipindi cha kwanza, wanapotulia na kujihamasisha tena, hupokea nguvu ya kucheza vema kipindi cha pili, lakini wajilaumupo, hufanya vibaya zaidi

Na sisi pia tuiamshe furaha ya Bwana daima.Kila tusomapo Neno lake, tufurahi kwasababu ni barua ya upendo wa Mungu kwetu Ili tuweze kuwa na nguvu.

Kwasababu furaha ya Bwana ndio nguvu yetu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SHUKURU KWA KILA JAMBO.

Furaha ni nini?

Fahamu maana 1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;

 

Print this post

USI..USI..USI.

Usi!.. Usi!.. Usi! na sio Msi!… Msi!.. Msi!..

Amri za Mungu zinasema Usiue, Usizini, Usiibe … na sio Msiibe, Msiue, Msizini… Ikifunua kuwa Mungu anaongea na mtu mmoja mmoja… Anasema na Mimi kivyangu, lakini pia anasema na wewe kivyako… Na hatuambii wote kwa pamoja.

Kutoka 20:13 “Usiue. 

14 Usizini. 

15 Usiibe. 

16 Usimshuhudie jirani yako uongo. 

17 Usiitamani nyumba ya jirani yako…”

Siku ya Hukumu, hatutahukumiwa kwa pamoja, kila mtu atasimama peke yake, na kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe..

Wagalatia 6:5 “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe”.

Na tena kila mtu atatoa habari zake mwenyewe na si pamoja na mwenzake..

Warumi 14:12 “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu”

Sasa kama ni hivyo kwanini Boss wako akukoseshe?..kwanini Rafiki akukoseshe, kwanini wanadamu wakukoseshe??… Na ilihali utasimama peke yako siku ile.

Kumbuka unapofanya uzinzi, siku ile hutakuwa na yule aliyefanya naye uzinzi, badala yake utasimama wewe kama wewe (kwasababu ile amri  inakuhusu wewe, na Mungu alikuwa anazungumza na wewe kivyako na si wewe pamoja na mwenzako)..

Kama unaiba, siku ile hutasimama na aliyekushawishi ukaibe, au uliyekuwa unashirikiana naye katika wizi.. wewe utakuwa peke yako, na yeye peke yake….kwasababu Amri ya Usiibe, uliambiwa wewe, nimeambiwa mimi na si wewe pamoja na mimi… Hivyo kila mtu atatoa habari zake mwenyewe.

Kama unaua, ni hivyo hivyo, kama uwaheshimu wazazi ni hivyo hivyo, na amri zote ni hivyo hivyo..

Hukumu ya Mungu inatisha!.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! sisi kama watakatifu tunaowezo wa kuamuru hukumu?

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe;

CHUKUA MZIGO WA MWINGINE.

Rudi Nyumbani

Print this post