Title June 2023

Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)

SWALI: Mjombakaka ni nani kwenye maandiko?


JIBU: Neno hilo tunalipata kwenye vifungu hivi;

Walawi 11:29 Tena katika vitu vile vitambaavyo, vitambaavyo juu ya nchi, hivi ni najisi kwenu; kicheche, na panya, na mjombakaka, kwa aina zake,

Katika agano la kale, Mungu alitoa maagizo ya wanyama wanaopaswa kuliwa na wale wasiopaswa kuliwa. Na mmoja wa viumbe vilivyokatazwa kuliwa alikuwa ni mjombakaka.

Mjombakaka kama lilivyotumika hapa kwenye maandiko ni Kobe, na aina zake zote.

Walioorodheshwa katika vifungu hivyo ni wanyama wasio na mabawa, tofauti na wale wa kwenye Mambo ya walawi 11:20-23 wenye mabawa, ambao wote kwa pamoja wamewekwa katika kundi la viumbe najisi ambavyo haviruhusiwa kushikwa au kuliwa, kwasababu “vinatambaa” yaani matumbo yao yakiburuta chini.

Lakini Mungu aliruhusu visiliwe sio kwasababu za kiafya kama wengi wanavyodhani. Hapana, kwani hata sasa zipo jamii nyingi zinakula baadhi ya wanyama hao na wanaishi bila matatizo yoyote ya kiafya, bali walikatazwa kutokana na tabia walizobeba, ambazo zinafunua jambo la kiroho ambalo mtu akiwa nalo, basi anaweza kuonekana najisi mbele za Mungu.

Kwamfano, walikatazwa kula wanyama wasiocheua, kama nguruwe. Mnyama asiyechuwa hana sifa ya kuhifadhi chakula na kukirejesha tena mdomo kukitafuna kisha kukimeza tena kama ng’ombe. Kufunua kuwa tukiwa watu tusioweza kukumbuka fadhili za Mungu alizotutendea nyuma, tukiwa watu wa kusikia tu Neno halafu baada ya hapo ndio imeisha hatulitendei kazi, sisi mbele za Mungu tunaonekana kama viumbe najisi.

Halikadhalika na hapa, wanyama hawa walionekana najisi, kwasababu wanatambaa, matumbo yao yanagusa chini. Nyoka alipolaaniwa aliambiwa kwa matumbo atakwenda. Ikiwa na maana haikuwa ni mapenzi ya Mungu viumbe vyake vitambae, tengeneza picha mwanadamu angekuwa anatembea huku tumbo lake likiburuta chini, angekuwa mdhaifu kiasi gani.?

Vivyo hivyo rohoni, hatupaswi kutambaa, bali kukimbia. Mashindano tuliyowekwa mbele yetu sio hata ya kutembea, bali kukimbia kabisa,

1Wakorintho 9:24 “ Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate”.

Hivyo hupaswi kuwa mlegevu, ukijiona upo katika ukristo ule ule miaka nenda miaka rudi, huna jambo jipya uliloliongeza katika ufalme wa Mungu, au uliloliongeza ni dogo kulinganisha ni muda uliodumu kwenye wokovu wako basi ujue kuwa unatambaa na hivyo Mungu anakuhesabu kama mmoja wa wanyama najisi.

Hivyo tujitahidi tusiwe wakristo wa namna hii, onyesha bidii kwa Mungu, itende kazi ya Mungu kwa karama uliyowekewa ndani yako. Kila siku jiulize ni jambo gani jipya nimeliongeza kwa Mungu wangu. Kwasababu ukumbuke kuwa kila mmoja atatolea hesabu talanta yake aliyopewa na Mungu siku ile. Je wewe umeongeza nini kwenye ufalme wa Mungu?

Bwana atupe nguvu ya kulitendea kazi Neno lake.

Shalom.

Angalia chini maana ya wanyama wengine kibiblia.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Lumbwi ni nini katika biblia?

JINSI UNAJISI UNAVYOMGHARIMU MTU.

Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

HAKUONA MAHALI PA KUTUA KWA WAYO WA MGUU WAKE.

Nyamafu ni nini?

Naivera ni nini? Kwanini Daudi aliihitaji alipomtafuta Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

USHUJAA WA ROHONI HAUANGALII UZOEFU WAKO.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Nakukaribisha tuyatafakari maneno ya uzima ya Bwana wetu.

Leo nataka tujifunze asili ya ushujaa wa rohoni, ambao wakati mwingine tunadhani mpaka tuwe na uzoefu ndio tuweze kufanya makuu kwa Mungu. Wakati Fulani Taifa la Israeli liliingia katika hali mbaya ya njaa isiyokuwa ya kawaida, mpaka kufikia hatua ya baadhi ya watu kuchinja watoto wao na kuwala (2Wafalme 6:28-29),  Na hiyo ilikuwa ni kwasababu ya kuzungukwa na maadui zao wenye nguvu kwa muda mrefu walioitwa washami. Hivyo wakashindwa kuingiza au kutoa chochote ndani ya mji kwa muda usiokuwa mchache.

Hivyo hali ikiwa mbaya sana, mfalme akafunga mji, hawajui cha kufanya, watu wamepaniki, wanakula vita visivyopaswa kulikwa, kiasi kwamba hata ‘mavi ya njiwa’ tu yalikuwa yanauzwa kama chakula. Tengeneza picha taifa kubwa kama hilo, linakumbwa na janga la njaa kali namna hiyo, hadi askari wake wazoefu wa vita, wanatetemeka na kujificha ndani ya mji, kwasababu walijua wakitoka tu ni kifo. Na ndicho maadui zao walichokuwa wanakisubiria kwao, aidha watoke wawaue, au wafe na njaa ndani. Hivyo hali ilikuwa ni ya kutisha sana. Lakini tunaona siku moja Nabii Elisha, akapewa unabii na Mungu, na kuambiwa kuwa chakula kitapatikana na kuuzwa kwa bei ya chini kiasi ambacho hakijawahi kuuzwa hapo kabla siku ya kesho yake, ni sawa ni uambiwe siku ya kesho, gunia la mahidi, linauzwa kwa  Tsh1, wakati unatambua kuwa halipungui wastani wa bei ya Tsh,70,000. Ndivyo ilivyokuwa kwa Israeli, Mungu alipompa Elisha unabii huo akaambiwa siku ya kesho yake, chakula kitauzwa kwa bei ile.

Sasa kulikuwa na wakoma wanne(4), waliokuwa nje ya mji, wakoma hawa walitengwa na taifa, kwasababu ilikuwa ni kuwa watu walioathirika na ugonjwa huu watengwe mbali na makazi ya watu  wao wasije kuleta maafa hayo ndani ya jamii, ni sawa na ugonjwa wa Ebola tunavyouona sasa, ndivyo ilivyokuwa ukoma kwa wakati ule.

Tengeneza picha watu hawa walikuwa ni wagonjwa, hawana wa kuwatazama, na zaidi sana wamekuwa dhaifu kwa njaa kali. Lakini tunaona walishauriana jambo kisha wakafanya maamuzi, ambao ndio ulikuwa ukombozi wa taifa la Israeli; Tusome hapo;

2Wafalme 7:1 Elisha akasema, Lisikieni neno la Bwana; Bwana asema hivi, Kesho panapo saa hii, kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, langoni pa Samaria. 

2 Basi yule akida, ambaye mfalme alikuwa akitegemea mkono wake, akamjibu yule mtu wa Mungu, akasema, Tazama, kama Bwana angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akamwambia, Angalia, wewe utaliona kwa macho yako, lakini hutakula

3 Basi walikuwapo watu wanne wenye ukoma, penye lango la mji; wakasemezana, Mbona tunakaa hapa hata tufe? 

4 Tukisema, Tutaingia mjini, mjini mna njaa, nasi tutakufa humo; nasi tukikaa hapa, tutakufa vile vile. Haya! Twende tukaliendee jeshi la Washami; wakituhifadhi hai tutaishi; wakituua, tutakufa tu. 

5 Basi wakaondoka kabla ya mapambazuko, ili waende mpaka kituo cha Washami; na walipofika mwanzo wa kimo cha Washami, kumbe! Hapana mtu. 

6 Kwa maana Bwana alikuwa amewasikizisha Washami kishindo cha miendo ya magari, na kishindo cha farasi, kama kishindo cha jeshi kubwa; wakaambiana, Tazama, mfalme wa Israeli amewaajiri wafalme wa Wahiti, na wafalme wa Wamisri, waje wapigane nasi. 

7 Kwa hiyo wakaondoka, wakakimbia kungali giza bado, wakaziacha hema zao, na farasi zao, na punda zao, na kimo chao vile vile kama kilivyokuwa, wakakimbia wapate kujiponya nafsi zao. 

8 Basi wale wenye ukoma walipofika mwisho wa kituo, waliingia katika hema moja, wakala, na kunywa, wakachukua fedha, na dhahabu, na mavazi, wakaenda wakavificha; wakarudi, wakaingia katika hema ya pili, vile vile wakachukua vitu, wakaenda, wakavificha. 

9 Ndipo wakaambiana, Mambo haya tufanyayo si mema; leo ni siku ya habari njema, na sisi tunanyamaza; mkingoja hata kutakapopambazuka, madhara yatatupata; basi twende tukawaambie watu wa nyumba ya mfalme. 

10 Basi wakaenda, wakawaita mabawabu wa mji; wakawaambia, Tulifika kituo cha Washami, na tazama, hapana mtu ye yote huko, wala sauti ya mtu, ila farasi wamefungwa, na punda wamefungwa, na hema zao kama walivyoziacha. 

11 Na mabawabu wakaita wakawaambia watu wa nyumba ya mfalme.

Ni nini kimejificha hapa?

Siri nayotaka uone ambayo imejificha nyuma ya hawa wakoma wanne, ni kwamba, pindi tu walipoamua kufanya uamuzi, wa kujitoa muhanga kwa ajili ya maisha yao, na kuanza mwendo, kuelekea kambi ya maadui, kumbe kule kwenye kambi ya washami, wanasikia kama JESHI kubwa sana la maaskari linawafuata. Hivyo wakakimbia kwa kasi sana, na kuacha kila kitu nyuma. Lakini wale maaskari wa kiisraeli waliokuwa wazoefu wakati huo wamejifungua ndani ya mji hawadhubutu kuchukua hatua..

Watu waliokuwa dhaifu na wagonjwa, ndio waliowafukuza washami na kuleta ukombozi Israeli. Watu wanne tu, waligeuka kuwa jeshi la maaskari elfu rohoni.

Hiyo ni kutufundisha nini?

Na sisi pia pale tunapoamua kufanya jambo kwa ajili ya Mungu, bila kujali hali zetu au udhaifu wetu, tufahamu kuwa jeshi la shetani linaogopa na kutetemeka kushinda hata sisi tunavyoweza kudhani. Daudi alijijua kuwa yeye si mtu wa vita, hajazoea vita, hawezi kutumia upanga wala mkuki, lakini yeye ndiye aliyesimama, kinyume na Goliathi, na kulifuka jeshi lake lote.

Hivyo, hupaswi kujidharau, ikiwa umeokoka leo, au jana, usiseme mimi sina uzoefu, au sijui biblia vizuri, kama kushuhudia watu wenye dhambi ambao wengine wameshindwa, wewe nenda, usisubiri mpaka mchungaji wako afanye hivyo, hujui kuwa wakati huo ndio Mungu kakuchagua kuwa sababu ya ukombozi kwa wengine.

Hivyo, popote unapojiona hukidhi vigezo, fahamu kuwa rohoni ndio unakidhi. Unajiona hustahili, jua tu kwa Mungu unastahili, kuwa na imani, chukua hatua, usingoje ngoje. Tumia karama uliyopewa ndani yako kuujenga ufalme wa Mungu. Popote pale unapojiona unafaa, basi tumia nafasi hiyo kumtangaza Kristo kwa wengine. Na hakika rohoni shetani atatoweka kama jeshi la washami.

Bwana akubariki.

Shalom.

Je, umeokoka? Kama bado basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo huo wa kumwalika Yesu maishani mwako.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).

MAHANAIMU (Jeshi la Mungu)!

Yerusalemu ni nini?

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

MAGONJWA YAKUPATAYO MARA KWA MARA.

Rudi nyumbani

Print this post

WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.

Karibu tujifunze biblia.

Leo tutajifunza moja ya taratibu illiyokuwa inaendelea katika Hekalu la Mungu ambayo haikuwa inampendeza Mungu.

Tusome,

Marko 11:15  “Wakafika Yerusalemu, naye akaingia ndani ya hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza na kununua ndani ya hekalu, akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao wauzao njiwa;

16  WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU”.

Maandiko haya ni maarufu tunapoyasoma husuani mahali hapo Bwana alipowafukuza waliokuwa wanauza njiwa na waliokuwa wanabadili fedha.

Lakini tukizidi kujifunza, tutaona sio kundi hilo tu Bwana alilolifukuza na kuliadhibu. Bali kulikuwa na kundi lingine pia ambalo lilikuwa linapandisha harufu mbaya mbele za Mungu.  Na kundi hilo ni lile la watu waliokuwa WANACHUKUA CHOMBO NDANI YA HEKALU.

Sasa kuchukua Chombo kunakozungumziwa hapo si “KUIBA VYOMBO VYA HEKALUNI au KUHAMISHA CHOMBO NDANI YA HEKALU” Hapana! Bali ni KUPITA au KUKATISHA na Chombo ndani ya Hekalu, Na chombo ni kitu chochote cha kubebea bidhaa au kurahisisha kazi kama makapu, au matenga au baiskeli.

Sasa mahali hekalu lilipojengwa lilikuwa linatengenisha sehemu mbili, sehemu ya kwanza ni Bethsaida (mahali palipokuwa na soko kubwa la kondoo) na Sehemu ya juu ya “Mji wa juu”. Hivyo watu waliotoka Mjini kuelekea Bethsaida sokoni walianza tabia ya kukatiza katika ukumbi wa hekalu kama njia ya mkato (shortcut) ya wao kufika Bethsaida.

Kwahiyo kulikuwa na kundi kubwa la watu wanaokatiza pale wakiwa na vyombo vyao kila siku, Kwaufupi paligeuzwa kuwa njia, mtu yeyote alipita, wezi wezi walikatiza, wahuni walipita, wasengenyaji walikatiza na stori zao za kuwasema wengine, waliotaka kwenda sokoni kuweka vimeza vya Kamari walikatika kila ziku na meza zao, matapeli ndio shortcut yao  hiyo n.k

Tabia ambayo Bwana Yesu hakupendezwa nayo!. Hivyo akasimama pia katika maingilio na matokeo ya Hekalu akawazuia wote waliokuwa wanakatiza!.. Huenda pia nao walitandikwa na kile kikoto!!.

Sasa tabia kama hiyo pia inaendelea katika nyumba za Mungu leo (Makanisani), utakuta kuna miingiliano ya watu wanaokatiza katiza na wanaozunguka zunguka!, wasio na fikra habari na mambo ya kiMungu… Wengi wa hao hawapiti kwa lengo la kumsogelea Mungu bali kwasababu ya shughuli zao, na biashara zao na ajenda zao, wanaouza chakula wanaingia wanavyotaka, wanaouza viatu wanaingia wanavyotaka, watoto wanaotaka kucheza kutoka huko nje basi eneo la kanisa ndio ukumbi wao n.k.. ni muhimu kuwa makini sana!!

Ni lazima, kuifanya Nyumba ya Mungu kuwa nyumba ya Mungu… kama tu sisi hatupendi watu wakatize kwenye maeneo ya Nyumba zetu, tena tunawaza wakati mwingine tuzungushe uzio vipi kwa Mungu??. Kama tu sisi tunapenda watu waziheshimu nyumba zetu vipi kwa Mungu?..

Na pia nyumba ya Mungu si jengo tu bali pia miili yetu, maandiko yanasema miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu (1Wakorintho 3:16, na 1Wakorintho 6:19). Ikiwa na maana kuwa pia miili yetu sio NJIA YA KILA MTU KUKATIZA!!!!.. (Maana yake si chombo cha zinaa wala kuchezewa).

1Wakorintho 6:15  “Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!

16  Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.

17  Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye.

18  Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe”.

Itunze na kuiheshimu nyumba ya Mungu (Mwili wako mwenyewe pamoja na Jengo unalokusanyikia).

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NI NANI ALIYEKUPA MAMLAKA HII UYATENDE HAYA?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?

Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?

KAA MAJANGWANI.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 27:6 “Jeraha utiwazo na rafiki ni amini;

SWALI: Nini maana ya mstari huu Mithali 27:6 “Jeraha utiwazo na rafiki ni amini; Bali kubusu kwa adui ni kwingi sana”


JIBU: Rafiki anayezungumziwa hapo ni rafiki wa kweli ambaye humwazia mema mwenzake, Hivyo inapotokea umeumizwa kwa maneno ya Ukweli aliyokuambia, ni bora kuliko kusifiwa na watu ambao nyuma yake ni maadui zako.

Ukweli unaomiza, ni kimelea cha upendo sahihi wa ki-Mungu. Bwana Yesu alikuwa ni mtu anayewaeleza ukweli watu wote, hususani wale mafarisayo kwa mambo ya kinafiki waliyokuwa wanayafanya kinyume na Neno la Mungu,(Mathayo 23) jambo ambalo makutano walishindwa kufanya kinyume chake walikuwa wanawasifia tu masokoni kila walipowaona, lakini matokeo yake ikawa ni wao kumchukia  Yesu badala ya kumpenda.

Mtume Paulo alilikemea kanisa la Galatia, kwa tabia yao ya kurudia mafundisho manyonge kiwepesi, ambayo walikuwa wameshayaacha huko nyuma mpaka akawakemea na kusema hamna akili, ni nani aliyewaloga?. Wao walitegemea kuambiwa mambo ya faraja wakati wote, lakini haikuwa hivyo wakati huu, bali lilikemewa sana na Paulo, na ndio maana akasema maneno haya;

Wagalatia 4:16  Je! Nimekuwa adui wenu kwa sababu nawaambia yaliyo kweli?

Lakini alikuwepo Yuda ambaye alimsaliti Bwana wake kwa kumbusu, akijifanya kama anampenda kumbe, anamundia njia ya kumsaliti.

Maana yake ni kuwa, ukikaa na ndugu, ambaye anakueleza ukweli unaokupasa hata kama ni kwa kukumea au kukurapia, na unakuumiza mpende huyo kuliko makundi ya watu wanaokusifia wakati wote hata pale unapokosea. Ukikaa katika fundisho ambalo unakemewa dhambi na mambo yako mabaya na mwenendo usiostahili, ni heri hapo kuliko kubaki katika mafundisho ambayo yanakusifia na kukufariji wakati wote.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inamaana gani inaposema ‘tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao’?

VITA DHIDI YA MAADUI

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

USIWE ADUI WA BWANA

Haini ni mtu gani? Mithali 13:2

Rudi nyumbani

Print this post

ORODHA YA MITUME.

Hii ni Orodha ya Mitume 12 wa Bwana YESU.

  1. SIMONI-aliyeitwa PETRO.
  2. ANDREA- Ndugu yake Simoni Petro.
  3. YAKOBO- Mwana wa Zebedayo.
  4. YOHANA- Mwana wa Zebedayo.
  5. FILIPO.
  6. BARTHOLOMAYO-  Au jina lingine Nathanaeli (Yohana 1:45)
  7. THOMASO.
  8. MATHAYO- Mtoza Ushuru.
  9. YAKOBO- Mwana wa Alfayo
  10. THADAYO- Aliyeitwa jina lingine “Yuda mwana wa Yakobo” (Luka 6:16)
  11. SIMONI – Mwenyeji wa Kana (Mkananayo) ambaye aliitwa jina lingine “Simoni Zelote (Matendo 1:13 na Luka 6:15)
  12. YUDA- Mwenyeji wa Keriothi (Iskariote)-Ndiye aliyemsaliti Yesu.

Orodha hii inapatika katika Kitabu cha Mathayo 10:2-4, na kitabu cha Marko 3:18, na Luka 6:13-16.

Katika Vitabu hivyo panaonekana Mitume kutajwa kwa jina Zaidi ya Moja katika injili nyingine, kwamfano Mtume aliyeitwa Thadayo (Mathayo 10:3),  kitabu cha Luka 6:16 anaonekana akitajwa kama “Yuda wa Yakobo”, Hiyo ni kuonyesha kuwa Mtume huyo alikuwa  anajulikana kwa jina Zaidi ya moja. Vile vile Mtume anayeonekana kuitwa Nathanaeli katika Yohana 1:45 ndio huyo huyo anayekuja kuoenakana akiitwa kwa jina la Bartholomeo katika Mathayo 10:3.

Lakini pia baada ya Yuda kumsaliti Bwana na kwenda kujinyonga, maandiko yanaonyesha kuwa Mtu aliyeitwa Mathiya alichukua nafasi yake na kuhesabiwa miongoni mwa mitume 11 wa Bwana Yesu.

Matendo 1:26 “Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja”.

Hiyo ndiyo Orodha ya Mitume 12 wa Bwana Yesu Kristo, ambao Bwana aliwaweka kuwa kama Mashahidi wa kufufuka kwake (Matendo 10:39-42 na Matendo 1:22), na baada ya hawa Bwana alinyanyua mitume wengine mfano wa hawa, ambao miongoni mwao alikuwa Mtume Paulo.

Na Mitume wanatajwa katika Agano jipya tu na wao ndio walioweka msingi wa Imani kwa kanisa, katika Agano la kale walioweka msingi wa kumjua Mungu kama Yehova ni Manabii, hivyo kwa muunganiko wa Mafunuo waliopewa Mitume wa agano jipya na Manabii wa agano la kale, kanisa la Kristo linajegwa juu ya Msingi wao.

Waefeso 2:20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”.

Je unajua jinsi Bwana alivyowachagua Mitume wake? na ni kigezo gani aliitumia?.. kufahamu zaidi fungua hapa >>JINSI BWANA ALIVYOWACHAGUA MITUME WAKE.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

Orodha ya mistari ya biblia kuhusu watoto

ORODHA YA IMANI POTOFU- Sehemu ya 1

YEZEBELI ALIKUWA NANI

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Sulemani alienda mbinguni?

JIBU: Jibu ni ndio.

Kosa alilolifanya Sulemani la kushawishiwa na wake zake kuwajengea madhabahu miungu, (1Wafalme 11:3:13) maandiko hayatuthibitishii kuwa lilikuwa ni endelevu, kana kwamba alimwacha Mungu moja kwa moja, hapana, au alitenda dhambi isiyosameheka kabisa hapana. Ni wazi kuwa Sulemani alitubu, kwa kosa lile, tunaposoma kitabu cha Mhubiri ambacho alikiandika katika uzee wake, kinatupa picha ya mambo mengi ambayo aliyatenda au aliyadhania kuwa ni sawa lakini mwisho wake akagundua ni ubatili ni sawa na kuufuata upepo. Na ndio maana mwisho kabisa akahitimisha, kuwa jumla ya yote yampasayo mtu ni kumcha Bwana na kuepukana na uovu. Kuonyesha kuwa Sulemani aligundua usahihi upo wapi, kabla hajafa.

Lakini pia asingetajwa katika vizazi vya ukoo wa  Bwana Yesu kama angekuwa ni mmojawapo wa waliopotea. Hivyo hatuwezi kusema kuwa Sulemani alikwenda kuzimu, hata kama hakuna maandiko ya moja kwa moja yanayoonyesha mahali alipotubu.

Kikubwa tujifunze katika kosa alilolifanya. Maandiko yanasema kutii ni bora kuliko dhabihu. Kama Sulemani angetii agizo la Bwana la kutokuoa wanawake wa-kimataifa, hayo yote yasingemkuta. Lakini alidhani kwa hekima zake kuwa nyingi asingeweza kudanganyika. Ndio alikuwa mjanja mwanzoni katika ujana wake, lakini sekunde za mwisho za uzee wake shetani alimpiga mweleka. Zipo dhambi ambazo shetani anakuandalia uzitende baadaye, lakini maandalizi yake anayatengeneza sasa.  Tii kila agizo la Mungu, hata kama ni dogo kiasi gani, hata kama litaonekana ni jepesi kulishinda kiasi gani sasa, wewe tii, kwasababu Mungu anaona mbele wewe unaona hapa. Simama katika Neno, sio katika mitazamo yako, ndipo utakapoweza kumshinda shetani, ikiwa wenye hekima kama hawa walinaswa katika tundu bovu wewe ni nani usinasike pindi unapolipuuzia Neno la Mungu linalokusemesha moyoni mwako uache hiyo tabia au hiyo dhambi?.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SHAMBA HUWA HALIMTAMBUI WALA KUMSUBIRIA MKULIMA.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?

Nchi ya Nodi ambayo Kaini alikimbilia ndio nchi gani kwasasa?(Mwanzo 4:16).

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inamaana gani inaposema ‘tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao’?

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema ‘tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao’? Mhubiri 3:11


JIBU:

Mhubiri 3:11 “Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho”

Mwanadamu alivyoumbwa ni tofauti na wanyama au viumbe hai vingine.  Kwani vyenyewe tangu vilipoumbwa mpaka sasa havibadiliki, wala haviendelei, kimaarifa, kiuelewa, au kiujuzi.. Lakini sisi wanadamu kila siku ndani yetu kuna kiu  ya kujua zaidi na zaidi, kufahamu zaidi na zaidi, kutafuta zaidi na zaidi, kutokuridhika hata kama tumepata.. Na hiyo ndiyo inayotupelekea kupiga hatua mpya kila leo. Sasa hiyo hali isiyokoma ndani yetu ndio inayoitwa UMILELE.

Na Mungu ameiruhusu iwepo ndani ya mwanadamu, kuvumbua, mambo mapya, tangu zamani hata sasa, na anafanya bidii kutafuta akidhani labda atafikia ukomo anaoutazamia, lakini kila kunapokucha ndipo anapogundua kuwa bado sana kuyaelewa mambo ya Mungu. Wanadhani pengine kwa kugundua ndege, ndio itawafikisha mbinguni, lakini kumbe, ndio wanaona anga halina mwisho.

Maana yake ni kuwa, hata milele yote ya maisha, au ya maarifa, au ya uvumbuzi kamwe hatutakaa tummalize Mungu. Yatosha sisi kukaa katika pendo lake, kuyatenda mapenzi yake katika Kristo Yesu,. Lakini tusipoteze nguvu zetu kumtafiti Mungu, ni heri tutumie hizo kuutafiti utukufu wake ili tumwabudu kuliko kuzitafiti njia zake, au kanuni zake alizojibunia, tutapoteza muda.

Sulemani alisema..

Mhubiri 8:17 basi, niliiona kazi yote ya Mungu, ya kuwa haitafutikani na mwanadamu kazi inayofanyika chini ya jua; kwa sababu mwanadamu na akijisumbua kadiri awezavyo kuitafuta, hata hivyo hataiona; naam, zaidi ya hayo, mwenye hekima ajapodhania ya kuwa ataijua, lakini yeye hataweza kuiona.

Dumu katika mapenzi yake Mungu, tunayojifunza kupitia biblia, kwani hilo ndio FUNGU letu tulilowekewa.

Ndio maana ya hilo Neno; Mhubiri 3:11 “Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho”

Je! Umeokoka? Je! Unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho, na Kristo yupo mlangoni kurudi? Umejiandaaje? Tubu mgeukie Bwana akuponye.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)

USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

SWALI: Biblia ilimaanisha nini iliposema Kaini ‘Akatoka mbele ya uso wa Bwana’. Kutoka kule kulimaanisha nini?


JIBU: Tunaona baada ya Kaini kumuua ndugu yake Habili kwa wivu, ambao ulizuka baada ya sadaka yake kukataliwa na ya ndugu yake kukubaliwa. Mungu alimsemesha, na kumweleza laana yake itakayompata baada ya pale. Lakini mwisho wa maneno yale, Tunaona Kaini anaonekana akitoka mbele ya uso wa Bwana. Maana yake ni nini?

Tusome.

Mwanzo 4:9 “Bwana akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu? 

10 Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.  11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;  12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. 

13 Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.  14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua. 

15 Bwana akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. Bwana akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga.  16 Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni”

Alitokaje?

Kutoka mbele ya uso wa Bwana hapo, sio Kuahirisha mazungumzo yaliyokuwa yanaendelea baina yake yeye na Mungu hapana. Bali ni kumwacha Mungu moja kwa moja. Yaani kwa ufupi mkataba wake na Mungu aliumalizia pale. Hakuna cha dhabihu tena wala sadaka, wala kumwomba Mungu, wala kujihusisha na tendo lolote la kiibada. Akaanza kujishughulisha na mambo ya kidunia tu, na sayansi, na utafiti na uvumbuzi, na akafanikiwa sana katika bidii yake hiyo, yeye na uzao wake wote, wakawa watu hodari duniani, lakini waovu sana (Soma Mwanzo 4:20-22). Na hawa ndio waliopelekea gharika kuletwa duniani.

Tofauti na uzao wa Adamu kwa Sethi, wao waliendelea kuwepo mbele ya uso wa Bwana, wakitaka fadhili na rehema kwa Mungu daima,wakiliitia jina lake.

Mwanzo 4:25 “Adamu akamjua mke wake tena; akazaa mwana mwanamume, akamwita jina lake Sethi; maana alisema, Mungu ameniwekea uzao mwingine mahali pa Habili; kwa sababu Kaini alimwua.  26 Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. Hapo ndipo watu walipoanza kuliitia Jina la Bwana”.

Mpaka sasa makundi haya mawili yapo duniani. Lipo ambalo halina habari na Mungu,(Ambao ndio uzao wa Kaini rohoni) bali mambo ya kidunia tu, na limefanikiwa sana katika hayo, ni jepesi katika uvumbuzi na utafiti, lakini  Mungu kwao ni kama historia za mababu wa kale, ni kama vile mashariki na magharibi zilivyo mbali. Lakini sisi hatupaswi kufanana wa watu hao. Bali kama Watoto wa Adamu kwa Sethi. Furaha yetu ipo katika Bwana. Tegemeo letu ni yeye, na nguvu zetu ni yeye, haijalishi tutakosa vyote au tutapata vyote. Yeye ndiye atakayekuwa urithi wetu milele.

Je! Wewe upo kundi lipi?   Uthibitisho ni maisha yako ulipoyaelekeza.

Hizi ni nyakati za mwisho. Kristo anarudi. Tubu mgeukie Bwana, mtafute yeye.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Bustani ya Edeni ipo nchi gani?

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

Rudi nyumbani

Print this post

UMEONDOLEWA DHAMBI?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na mwanga wa njia yetu. (Zab. 119:105).

Kuna tofauti ya Msamaha wa dhambi na Ondoleo la dhambi.

Mtu anapokukosea  labda amekutukana au kukuibia na akikuomba msamaha unaweza kumsamahe  (ukamwachilia kabisa moyoni mwako) lakini kumsamehe kwako hakumfanyi yeye kuacha ile tabia.. Maana yake ni kwamba kama ile tabia haitaondoka ndani ya huyo mtu basi ni wazi kuwa atarudia lile kosa siku nyingine. Atapumzika siku mbili au tatu na baadaye atarudia lile kosa. Sasa mtu kama huyu kapata msahama lakini si ondoleo la ile tabia.

Vile vile kwa Mungu tunaweza kupata msamaha wa makosa yetu na dhambi zetu, lakini kama hatutapata Ondoloe la dhambi hizo (Maana yake kama ule mzizi wa dhambi ndani yetu hautang’olewa) basi tutabaki vile vile, kila mara tutarudia makosa yale yale. Na mzizi wa dhambi ni lazima uondoke maishani mwetu kwasababu ndicho kitu kilichomleta Bwana Yesu duniani.

Bwana Yesu hakuja tu kuleta msamaha wa dhambi bali pia ondoleo la dhambi..Kwasababu msamaha wa dhambi ulikuwepo hata kabla ya Bwana Yesu kuja duniani, watu waliomba msamaha mbele za Mungu na wakasamehewa makosa yao, lakini Ondoleo la dhambi halikuwepo, Dhambi hazikuondolewa katika kumbukumbu za Mungu (zilifunikwa tu) na vile vile hazikuondolewa ndani ya mtu, bado watu waliendelea kurudia makosa yale yale, baada ya Bwana Yesu kuja watu ndipo wakapata ondoleo la dhambi, ndani yao (utumwa wa dhambi ukakoma kwa wale wote waliompokea).

Sasa tunapataje ondoleo la dhambi?.. kiasi kwamba dhambi haitupelekeshi tena wala kututawala?

Kwanza ni kwa kutubu mbele za Mungu, na kukiri kwamba sisi ni wakosaji, (hapa unatubia makosa yako yote ambayo umeyafanya kwa kujua, na kwa kutokujua mbele za Mungu, kwa tendo hilo Bwana atakusamehe ikiwa toba hiyo imetoka kweli ndani ya moyo na kwamba umekusudia kubadilika kabisa..)

Sasa hatua inayofuata ili Dhambi zako ziondolewe (ule mzizi wa dhambi ndani yako uondoke) baada ya kutubu ni wewe kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi…  Hiki ni kipengele cha muhimu sana ambacho si cha kupuuzia hata kidogo..

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, NANYI MTAPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU

Ubatizo sahihi unakamilisha toba na hivyo mtu anayefanya hayo Mungu anampa zawadi ya Roho Mtakatifu pamoja na Ondoleo la dhambi, jambo ambalo ni muhimu sana.

Mtu huyu kama toba yake imetoka ndani ya moyo kabisa basi ule uzinzi uliokuwa unamsumbua mara kwa mara unakufa, anajikuta anaushinda uasherati na haurudii tena, kwasababu dhambi imeondolewa ndani yake, zile tabia zilizokuwa zinamwendesha mara kwa mara zinaondoka ndani yake kwasababu ule mzizi wa dhambi umeondolewa ndani yake n.k n.K

Na kumbuka ni muhimu sana kubatizwa ubatizo ulio sahihi, kwasababu si kila batizo zinaondoa dhambi.. nyingine utabatizwa lakini utabaki vile vile. Na ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 19:10)!.

Je unataka usiendelee kuwa mtumwa wa dhambi?.. Tumia kanuni hiyo ya Matendo 2:27-37. Na Mungu ni mwaminifu atafanya sawasawa na Neno lake.

Maran atha.

Ikiwa hujabatizwa bado na unahitaji msaada wa kupata ubatizo sahihi, basi waweza kuwasiliana nasi kwa namba zetu na tutakusaidia kwa hilo.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.

NINI MAANA YA KUTUBU

Dameski ni wapi kwasasa?

BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.

Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mikononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?

Rudi nyumbani

Print this post

JE UNAMTUMIKIAJE BWANA?

Mafunzo maalumu kwa Wanawake.

Karibu tujifunze Biblia,

Je Bwana alishakufanyia muujiza wowote katika maisha yako?..Na ukaufurahia?.. Je baada ya hapo ulimfanyia nini Bwana?.. Je uliishia kushukuru tu na kuendelea na mambo yako? Au kuna lingine la ziada ulilifanya?, kama hukufanya chochote au hukujua nini cha kufanya basi leo fahamu yakupasayo kufanya!

Hebu tujifunze kwa baadhi ya wanawake katika biblia ambao hawakuwa Mitume, wala Waalimu, wala Maaskofu wala wachungaji lakini walikuwa wakimtumikia Bwana Yesu.. na kisha tutazame walikuwa wakimtumikia kwa namna gani?

Mathayo 27:55  “Palikuwa na wanawake wengi pale wakitazama kwa mbali, HAO NDIO WALIOMFUATA YESU TOKA GALILAYA, NA KUMTUMIKIA.

56  Miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo na Yusufu, na mama yao wana wa Zebedayo”.

Hawa wanawake walikuwa wakifuatana na Bwana Yesu kila mahali.. Lakini je! Walikuwa wanafuata naye kumtazama uso?, au kumsikiliza tu anayoyahubiri?..Jibu ni La! Biblia inatuambia walikuwa pia WAKIMTUMIKIA!!.. Sasa swali wakimtumikia kwa nini?..tusome mistari ifuatayo..

Luka 8:1  “Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye,

NA WANAWAKE KADHA WA KADHA ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3  na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, WALIOKUWA WAKIMHUDUMIA KWA MALI ZAO”.

Umeona hapo?.. Walikuwa wakimhudumia kwa MALI ZAO!. Ikiwa na maana kuwa gharama kubwa za kuipeleka Injili zilikuwa zinabebwa na hawa WANAWAKE!..  hata ule mkoba ambao Yuda alikuwa anaushika, huenda sehemu kubwa ilijazwa na hawa wanawake!.

Na kwanini wanawake hawa walipata msukumo huo mkuu wa kumhudumia Bwana kwa mali zao?.. Jibu ni kwasababu walitendewa miujiza na Bwana, walitolewa pepo waliokuwa wanawatesa, waliponywa magonjwa  yao yaliyokuwa yanawatesa, walipewa wokovu ndani yao ambao uliwapa Amani na tumaini la maisha..Hivyo wakaona si sawa kumtazama Yesu kwa uso tu na kumshukuru kwa maneno tu!, bali pia kwa vitendo.

Ndipo wakaona wavunje vibweta vyao ili Bwana akaende miji mingi Zaidi kuhubiri, wakaona watoe hazina zao ili wanafunzi wa Bwana wasipungukiwe wanapokwenda kuhubiri miji na miji. Na hivyo wakawa mashujaa wa Imani ambao mpaka leo tunawasoma.

Na sio hao tu, bali pia tunamwona na Mkwe wake Petro, (Mama yake mkewe) ambaye alikuwa anaumwa homa, biblia inasema baada ya Bwana kumponya, alinyanyuka na kuanza KUMTUMIKIA BWANA!.

Mathayo 8:14 “Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwe wa Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa.

15  Akamgusa mkono, homa ikamwacha; NAYE AKAONDOKA, AKAWATUMIKIA”

Je na wewe Mama unamtumikia nani?, Na wewe binti unamtumikia nani?…Je umemtumikia Bwana kwa kipi tangu alipokuponya?, tangu alipokufungua?, tangu alipokuinua?, tangu alipokupa wokovu bure?.. Je unamtumikia kwa maneno tu, au pia na vitendo?.

Ni kweli wewe sio Mchungaji, wala Mwalimu, wala Mhubiri, wewe ni kama tu Mariamu Magdalena, au Susana..basi fanya kama hao!.. Na kumbukumbu lako litadumu kama la hao wanawake lilivyodumu, Bwana atakuheshimu na kukuona wewe ni mtumishi wake kama tu walivyo Mitume kwasababu na wewe pia unamtumikia kwa mali zako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

WANNE WALIO WAONGO.

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Rudi nyumbani

Print this post