Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

SWALI: Naomba kufahamu maana ya huu mstari;

Mithali 17:17 “Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu”.


JIBU: Huu mstari unaeleza rafiki wa kweli anapaswa aweje, pia rafiki ambaye atazidi  kuwa kama ndugu anapaswa aweje?

Anasema ‘Rafiki hupenda sikuzote’, Ndio.. hii ni tabia ya rafiki wa kweli, hupenda nyakati zote, ziwe ni nzuri , au ni mbaya, kwamfano, rafiki ambaye siku umemfurahisha anakupenda, lakini siku pia umemuudhi anakupenda, siku umempa anakupenda, lakini siku umemnyima bado anakupenda zaidi. Rafiki ambaye wakati mnawasiliana anakupenda, lakini wakati mlipopotezana kimawasiliano kwa muda mrefu bado anakupenda.

Huyo ndio rafiki wa kweli..

Lakini hapo anaposema “Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu” ..Maana yake ni kuwa Yule ambaye anakuwa na wewe bega kwa bega, katika wakati wa shida zako, na taabu zako, na misiba yako huyo si rafiki tena bali ni ndugu..

Unamwona anakujali, wakati unaugonjwa wa hali ya juu, unamwona, anakushika mkono wakati umefilisika, unamwona unakufariji sana wakati wa msiba wako, unamwona anatafuta kila mbinu, kukusogeza mahali wakati upo katikati ya mateso. Huyo ni rafiki aliyefanyika ndugu.

Kwasababu kama hapo inavyosema ‘ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu’..Maana yake ili mtu aitwe ndugu, ni lazima awe amezaliwa mahususi kwa ajili ya siku za shida zako.

Je! Na sisi tunapoitana ‘ndugu’ na ‘rafiki’ tunatambua wito wetu katika hayo?

Lakini tunamwona mmoja ambaye, ni zaidi ya rafiki, ni pia ni zaidi ya ndugu, ambaye sio tu amekuwa karibu na sisi katika shida zetu, na mateso yetu na hukumu zetu.. Lakini pia aliyatoa maisha yake yote, pamoja na uhai wake, ili kufa kwa ajili yetu.

Yohana 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”

Hivyo basi, hatuna budi na sisi kuuthamini upendo mkuu namna hii, kwa kukubali kukombolewa na yeye, ili tuoshwe dhambi zetu. Kumbuka hakuna ukombozi nje ya Yesu Kristo, vilevile hakuna uwezekano wowote wa sisi kumpendeza Mungu kwa matendo yetu wenyewe. Na ndio maana ilimpasa aje, ili atukomboe, kutoka dhambini.

Waebrania 2:3 “sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”;

Ikiwa upo tayari kumkabidhi Bwana Yesu maisha yako, basi waweza wasiliana nasi kwa namba zetu hizi, +255693036618/ +255789001312 kwa ajili ya mwongozo huo, bure, na hakika Bwana atayaokoa maisha yako, na kukufanya kuwa mpya tena.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

RAFIKI MWEMA.

JIRANI YANGU NI NANI?

KAMA VILE UMEME UTOKAVYO MASHARIKI UKAONEKANA HATA MAGHARIBI.

Mretemu ni mti gani?

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments