Title April 2024

NI MAJIRA YAPI YA NEEMA WEWE UPO?

Kuna wakati wa kukokotwa-kokotwa, lakini kuna majira ya  kuachwa ufanye maamuzi mwenyewe, na usipofanya unakufa. Mtu aliye mchanga kiroho, ni rahisi Mungu kuchukuliana naye katika mambo yasiyofaa kutokana na uchanga wake kwa siku zile za awali, lakini haiwezi kuwa hivyo siku zote, kwa jinsi siku zinavyokwenda, kusukumwa sukumwa hakutakuwepo, ni kuwa makini sana!.

Ukitafakari habari ya Mke wa Lutu, unaweza kupata picha halisi jambo hili lilivyo, yeye alidhani ataendelea kuvutwa-vutwa tu nyakati zote, lakini walipofikishwa mahali Fulani, nje kidogo ya mji wameshaijua njia, waliambiwa wajiponye wenyewe nafsi zao, lakini yeye akageuka nyuma, na wakati ule ule akawa jiwe la chumvi.

Mwanzo 19:15 Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu. 

16 AKAKAWIA-KAWIA; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, KWA JINSI BWANA ALIVYOMHURUMIA, wakamtoa wakamweka nje ya mji. 

17 Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, JIPONYE NAFSI YAKO USITAZAME NYUMA, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea.

Hatari tuliyonayo sisi tuliopo katika siku hizi za mwisho, katika kanisa hili la Laodikia (Ufunuo 3:14-21), ni kwamba tunafahamu mambo mengi, na tumeshaona mifano mingi kwenye maandiko na kwenye historia, lakini geuko la dhati ndani ya wengi halipo, tukifikiri  tutalinganishwa na wale watu wa zamani. Neema kwako wewe haifanyi kazi katika kukokotwa tena, bali katika kukimbia. Ilifika wakati Yesu hakuwaambia tena wanafunzi wake “nifuate”, aliwaambia na “ninyi mnataka kuondoka?”

Halikadhali, kama umeshaokoka, jichunge sana, dhambi usiifanye rafiki kwako, ukidhani kila kosa tu utakalolifanya upo msamaha, acha hayo mawazo, unajitafutia kuwa mke wa lutu. Neno la Mungu linasema;

Waebrania 6:4  Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5  na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6  wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

7  Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; 8  bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.

Ni kusimama imara, sio tena kumbelezewa injili, sio tena kukumbushwa-kumbushwa wajibu wako wewe kama mkristo, na kuambiwa kaombe, nenda ibadani, mtafute Mungu, acha anasa, soma biblia. Ni wakati wa kujitambua kuwa sasa umeshatolewa nje ya mji, changamka, zama ndani ya Kristo. Acha kuwa vuguvugu utatapikwa, zama hizi ni zama za uovu. Wokovu wa mawazo mawili sio sasa, neema hiyo haipo kwetu mimi na wewe siku hizi za mwisho. Injili ya maneno laini, isikupumbaze, fanya Imara uteule wako na wito wako.

Ufunuo 22:10  Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11  Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa

12  Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

Kimbia, usiangalie nyuma.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! “majira na sheria” mpinga-kristo atakayokuja kubalisha ni kupindua siku ya sabato na kuwa jumapili?

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

UMEJIANDAAJE KWA NYAKATI ZA KUWA PEKE YAKO?

WAKATI ULIOKUBALIKA NALIKUSIKIA

Rudi Nyumbani

Print this post

Ni uchafu gani unaozungumziwa katika Wagalatia 5:19?

Jibu: Turejee,

Wagalatia 5:19  “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, UCHAFU, ufisadi,

20  ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21  husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.

Dhambi zote ni “uchafu” lakini zipo dhambi ambazo ni “chafu Zaidi”, hizo ndizo zinazoitwa “Uchafu” Mfano wa hizo ni zile zilizotajwa katika Mambo ya Walawi 18 na 20(Dhambi za kulala na mnyama na ndugu wa karibu).

Walawi 18:23 “Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; NI UCHAFUKO”.

Walawi 20:12 “Na mtu mume akilala na mkwewe mwanamke wote wawili hakika watauawa; wamefanya yaliyo UCHAFUKO; damu yao itakuwa juu yao”.

Utaona dhambi nyingine zimetajwa tu kama ni “Machukizo” mfano lakini hizi zimetajwa kama “Uchafuko” maana yake zimezidi machukizo.. Ni uchafu mkuu mbele za Mungu.

Kulala na Mnyama, ni uchafu, vile vile kulala na mama mkwe au baba mkwe ni uchafu..na wachafu wote hawataurithi uzima wa milele sawasawa na maandiko hayo.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

Ninyi ni chumvi ya dunia, Andiko hilo lina maana gani?

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

Rudi Nyumbani

Print this post

Tirano alikuwa nani na darasa lake lilikuwaje? (Matendo 19:9)

Swali: Huyu Tirano tunayemsoma katika Matendo 19:9 alikuwa ni nani, na darasa lake lilikuwaje?


Jibu: Tuanzie kusoma mstari ule wa 8 hadi ule wa 11 ili  tuweze kuelewe vizuri..

Matendo 19:8  “Akaingia ndani ya sinagogi, akanena kwa ushujaa kwa MUDA WA MIEZI MITATU, akihojiana na watu, na kuwavuta katika mambo ya ufalme wa Mungu.

9  Lakini wengine walikaidi, wakakataa kuamini, wakiitukana ile Njia mbele ya mkutano; basi, akaondoka akawaacha, akawatenga wanafunzi, akahojiana na watu kila siku katika DARASA YA MTU MMOJA, JINA LAKE TIRANO.

10  Mambo haya yakaendelea kwa MUDA WA MIAKA MIWILI, hata wote waliokaa Asia wakalisikia neno la Bwana, Wayahudi kwa Wayunani.

11  Mungu akafanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida”.

Baada ya Paulo kuingia Efeso, aliingia katika sinagogi moja la wayahudi ili kuhubiri habari za BWANA YESU, na wachache walioamini na kuitii injili, lakini wengi walikaidi na hata kuitukana kabisa injili mbele ya watu wote..

Mtume Paulo alipoona kuwa wameikataa injili, aliliacha sinagogi hilo (la wayahudi) ambalo pengine lingekuwa ndio sehemu bora kwa watu kujifunzia habari za Bwana YESU, lakini kutokana na ubishi na ugumu wa watu wa sinagogi (wayahudi).. Paulo aliondoka pamoja na wale wachache walioamini (wanafunzi)..na kuhamia kwenye darasa lingine la mtu mmoja wa mataifa aliyeitwa TIRANO. (na kipindi ambacho Paulo alihudumu katika Sinagogi la wayahudi mpaka alipoondoka na kuhamia kwenye darasa la Tirano ni muda wa miezi 3)

Kumbuka hapo biblia inaposema “darasa la Tirano” inamaanisha “jengo” lililokuwa maalumu kwaajili ya kufundishia la mtu aliyeitwa Tirano.

Sasa swali huyu Tirano alikuwa nani?

Biblia haijaeleza kwa kina huyu Tirano alikuwa ni nani, lakini ni wazi kuwa alikuwa ni mmoja wayunani aliyeamini injili na hivyo akatoa darasa lake hilo liweze kutumika kama mahali pa kufundishia watu injili.. Kama tu Petro alivyoalikwa nyumbani kwa Simoni mtengeneza ngozi kule Kaisaria (Matendo 9:43).

Na mpaka atoe darasa hilo, maana yake hapo kwanza inawezekana alikuwa ni mwalimu wa Falsafa za Kiyunani (kwani wayunani walikuwa ni watu wasomi na wenye kutafuta elimu sana).

Na baada ya Paulo kuhama kutoka kwenye lile Sinagogi na kuhamia kwenye darasa hilo la Tirano, injili ilipata mafanikio makubwa sana, kwani baada ya miaka miwili tu, Watu wote wa Asia waliisikia injili na kuitii..

Matendo 19:10 “Mambo haya yakaendelea kwa MUDA WA MIAKA MIWILI, hata wote waliokaa Asia wakalisikia neno la Bwana, Wayahudi kwa Wayunani.

11  Mungu akafanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida”.

Ikifunua kuwa kuna mambo au mifumo ndani ya masinagogi (au madhehebu) ambayo inazuia kutembea kwa Roho Mtakatifu, zipo tabia ambazo zinazuia injili kusambaa, ipo mienendo inayokinzana na nguvu za Roho Mtakatifu kutembea.. na mojawapo ya hiyo ni tabia ya kupingana na Neno la Mungu (kama ilivyokuwa kwa hawa wayahudi ndani ya Sinagogi)..walikuwa wanashindana na Paulo kutwa kuchwa.

Walikuwa wanaikejeli injili, hata kama wanaona kinachohubiriwa ni kweli kabisa..

Na hata katika madhehebu na makanisa leo ni hivyo hivyo, utakuta mtu au kiongozi anaweza kuiona kweli lakini bado akashindana nayo na kuipinga!..Kiongozi anaweza kuona jambo Fulani sio sawa lakini bado akalipalilia, na kushindana na ile kweli, watu wanaweza kufunuliwa maandiko lakini bado wakawa hawabadiliki wapo vile vile, bado maisha yao ni yale yale NA KWA MATENDO YAO WANAITUKANA INJILI (ingawa midomo yao inakiri).. mambo hayo yanazuia injili kusambaa na kutembea kwa Roho Mtakatifu.

Bwana atusaidie tuzidi kutembea katika kweli yake.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

Sinagogi kufumakana maana yake nini? (Matendo 13:43).

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Rudi Nyumbani

Print this post

UTAJUAJE UFAHAMU WAKO UMECHUKULIWA?

Swali: Utajuaje ufahamu wako umetekwa au ni viashiria gani vitakavyotambulisha kuwa ufahamu umetekwa na adui?


Jina la Bwana YESU libarikiwe.

Kabla ya kujipima kama ufahamu umechukuliwa au la!..Ni vizuri kwanza tukajua kibiblia mtu mwenye ufahamu anatafsiriwaje?

Turejee kile kitabu cha Ayubu 28:28.

Ayubu 28:28 “Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, NA KUJITENGA NA UOVU NDIO UFAHAMU

Kwahiyo kumbe Mtu anayeweza kujitenga na Uovu ndiye mwenye ufahamu…maana yake kinyume chake yule asiyeweza kujitenga na uovu hana Ufahamu…au kwa lugha nyingine “UFAHAMU WAKE UMETEKWA”.

Na hapo neno linasema “kujitenga na uovu” na sio  “kujizuia na uovu”… maana yake “unakaa nao mbali”... Kama ni ulevi mtu anakaa nao mbali, kuanzia mazingira ya kulewa mpaka makundinya walevi (wote anajitenga nao).

Kama ni uasherati na uzinzi, mtu anakaa nao mbali kuanzia mawasiliano, mavazi, makundi…vile vile anajitenga na mazingira yote yanayochochea hiyo dhambi ikiwemo mazungumzo na mitandao.

Kama ni usengenyaji, mtu anajitenga na mazingira hayo na makundi yote..

Kama ni utukanaji vivyo hivyo, Kama ni wizi/ufisadi au utukanaji na hasira ni hivyo hivyo..

Lakini kinyume chake mtu asiyeweza kujitenga na hayo yote basi UFAHAMU WAKE UMECHUKULIWA (UMETEKWA)!!...Upo chini ya Milki ya mkuu wa giza. Anatumikishwa na mamlaka za giza.

Haijalishi kama ni mchungaji, au askofu, au Nabii, au Mtume, au mwimbaji wa kwaya, au Papa, au Raisi wa nchi, au mtu mwingine yoyote mwenye kuheshimika katika jamii au kanisa.

Mtu asiyeweza kujiepusha na UOVU  ufahamu wake haupo (Umefungwa na kamba za kuzimu)., haijalishi ana uwezo mkubwa kiasi gani wa kupambanua mambo ya kimwili, haijalishi ana elimu kubwa kiasi gani na anategemewa na watu wengi kiasi gani katika kutatua mambo…bado ufahamu wake haupo!.

UTAURUDISHAJE UFAHAMU WAKO?.

Hakuna mtu ambaye kwa nguvu ake ana uwezo wa kuurudisha ufahamu wake!… Isipokuwa kwa msaada wa Mungu tu…Na msaada huu unaanza pale tunapoamua kufanya mageuzi katika maisha yetu kwa kutubia dhambi zetu na kumkiri Mwokozi YESU.

Ambapo kama tutatubu kwa kumaanisha kweli basi atatupa kipawa cha Roho wake mtakatifu ambaye kupitia huyo basi ataurejesha ufahamu uliochukuliwa na ile nguvu ya kuushinda uovu na kujitenga nao itakuwa juu yetu.

Faida ya kwanza ya ufahamu wa mtu kurudi ndani yake ni UZIMA WA MILELE lakini pia UZIMA WA MAISHA ya duniani, kwani ufahamu wa roho ndio unaofungua kufahamu mambo mengine yote.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

JE! UNATAKA UITWE MSOMI NA MUNGU?

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Karibu katika kuyatafakari maneno ya uzima.

Sulemani, mtoto wa Daudi, katika kitabu chake cha mhubiri, kilichojawa na utafiti wa hali ya juu wa mambo mengi ya kimaisha yamuhusuyo mwanadamu, Tunaona mwishoni kabisa mwa utafiti wake alihitimisha kwa maneno haya;

Mhubiri 12:11 “Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; HAKUNA MWISHO WO WOTE WA KUTUNGA VITABU VINGI; NA KUSOMA SANA HUUCHOSHA MWILI. 

13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili. 

13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu”.

Sulemani alikuwa ni mtafiti sana, na kama kusoma na kutunga vitabu, basi alitunga vingi sana, na katika vyote (viwe Vya ki-Mungu na visivyo wa ki-Mungu ) alijaribu kutafuta siri, na mwongozo sahihi wa mwanadamu. Lakini tunaona akapata jawabu, ambalo ni rahisi sana kwa wote. Na jawabu lenyewe ni hili “kumcha Mungu na kuzishika amri zake”.

Akasema unaweza ukakesha kusoma vitabu vingi sana katika huu ulimwengu, na matokeo ya kusoma sana, ni kudhoofika, Na bado usipate ukweli mwingine zaidi ya ule ule “kumcha Mungu na kuzishika amri zake”. Ndio maana akahitimisha kwamba Mtu akizingatia sana hilo, laweza kuzidi usomaji mwingi tuuona hapa duniani.

Sasa kumcha Mungu na kuzishika amri zake maana yake ni nini?

Kumbuka biblia nzima inazungumzia habari za Yesu Kristo mwokozi wetu. Hivyo hapo ni sawa na kusema “Kumcha Yesu na kuzishika amri zake”. Hiyo Ni zaidi ya kuwa na maarifa ya vitabu milioni moja, au elimu za shahada elfu,. Ikiwa na maana yule mtu aliyemwamini Yesu, kisha akawa anaishi kwa kulifuata Neno lake, na kuitimiza amri yake kuu, ambayo alisema ni UPENDO. Huyo ni zaidi ya Msomi yoyote aliyewahi kutokea duniani. Au mtunzi yoyote mwenye hekima aliyewahi kuandika vitabu vingi. Ni mtu aliyemaliza kusoma vitabu vyote.

Yohana 13:34  Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.

35  Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.

Hivyo, usisumbukie maarifa  mengi, ukadhani kuwa ndio utamwelewa Mungu, sumbukia Kristo moyoni mwako, sumbukia upendo wa agape moyoni mwako. Kwasababu huko kote utakapokwenda kutakurudisha hapo hapo, ndicho alichokigundua sulemani katika usomaji wake mwingi, hakuna jipya ndani yake Ni kujisumbua tu, ndio maana biblia inasema, yapo mambo mengi aliyoyafanya Yesu na kama yangeandikwa basi vitabu vyote visingetosha duniani.

Yohana 21:25  Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa.

Umeona? Vitabu visingetosha kuandika mambo yote ya Yesu, kwasababu maudhui yake ndio yaleyale, tunayoyasoma katika maneno machache ya kwenye biblia. Ambayo ni wokovu na Upendo wa Mungu. Tukiyatimiza hayo ni sawa na kusoma vitabu vyote duniani.

Hivyo mimi na wewe tuanze kuweka juhudu, kimatendo, kutendea kazi Neno lake, zaidi ya kuhangaika kutafuta maarifa mengi. Kwasababu anasema mwenyewe chanzo cha maarifa ni kumcha yeye, na sio chanzo cha kumcha yeye ni maarifa.

Kumbuka pia asemapo kusoma kwingi huuchosha mwili, hamaanishi uwe mjinga usiwe msomaji kabisa hapana, Lakini anakupa shabaha ni wapi uweke juhudi zako nyingi ili ufanikiwe kuwa na Maarifa ya kweli ya kisomi, Usije ukawa unaufuata upepo.

Tumia nguvu nyingi kuyatendea kazi yale yaliyopo kwenye biblia tu, zaidi ya mihangaiko mingi huku na kule, na elimu nyingi za kidunia.  Utaitwa Msomi na Mungu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Uchaji ni nini kama tunavyosoma katika 1Timotheo 2:10?

NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?

Rudi Nyumbani

Print this post

Je ile habari ya mtini kunyauka inajichanganya?

Swali: Mathayo 21:19 inasema “mtini ulinyauka mara (maana yake muda ule ule uliolaaniwa)”.. lakini katika Marko 11:20 biblia inasema “mtini ulinyauka kesho yake, na sio siku ile ile ulipolaaniwa”.. Je mwandishi yupi yupo sahihi na yupi hayupo sahihi?.


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kujua kuwa biblia haijichanganyi mahali popote na wala haijawahi kujichanganya mahali popote, isipokuwa pambanuzi zetu, fahamu zetu na tafakari zetu ndizo zinazojichanganya pale tunaposoma pasipo kutafakari kwa kina.

Sasa turejee habari hizo moja moja na kisha tuzitafakari tena..

Mathayo 21:18 “Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.

19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; akauambia, Yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele. MTINI UKANYAUKA MARA.

20 WANAFUNZI WALIPOONA, WALISTAAJABU, WAKISEMA, JINSI GANI MTINI UMENYAUKA MARA?

21 Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng’oka, ukatupwe baharini, litatendeka”.

Hapa tunaona mtini ulinyauka “Mara”.. Lakini turejea kitabu cha Marko ni kama tunasoma habari tofauti…

Marko 11:12 “Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa.

13  Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini.

14  Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia”

Turuke mpaka mstari wa 19-23..

“19  Na kulipokuwa jioni alitoka mjini.

20  NA ASUBUHI WALIPOKUWA WAKIPITA, WALIUONA ULE MTINI UMENYAUKA TOKA SHINANI.

21  PETRO AKAKUMBUKA HABARI YAKE, AKAMWAMBIA, RABI, TAZAMA, MTINI ULIOULAANI UMENYAUKA.

22  Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu.

23  Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake”

Hapa tunasoma “MTINI ULINYAUKA SIKU INAYOFUATA na si muda ule ule”.. Sasa swali? habari ipi ni sahihi kati ya hizo mbili?

Jibu ni kwamba habari zote ni sahihi, waandishi wote wote wapo sahihi, hakuna hata mmoja aliye mwongo..…

Sasa kwa ufupi ni kwamba mtini haukunyauka muda ule ule Bwana alipoulaani, bali mpaka kufikia kesho yake ndio ulikuwa umekwisha nyauka kabisa..…Sasa swali, kama ni hivyo kwanini Mathayo aseme ulinyauka MARA?…

Jibu la swali hili ni kwamba…si kila mahali panapotumika neno “Mara” panamaanisha “dakika ile ile, au sekunde ile ile, au muda ule”… Hapana!.. Bali neno “Mara” linaweza kumaanisha kipindi fulani cha muda/wakati… ili tuelewe vizuri, tusome habari ifuatayo..

Marko 1:26 “Yule pepo mchafu akamtia kifafa, akalia kwa sauti kuu, akamtoka.

27  Wakashangaa wote, hata wakaulizana, wakisema, Nini hii? Ni elimu mpya! Maana kwa uweza awaamuru hata pepo wachafu, nao wamtii!

28  Habari zake ZIKAENEA MARA KOTEKOTE KATIKA NCHI ZOTE kandokando ya Galilaya”

Hapo biblia inasema habari za Bwana YESU zikaenena “MARA KOTE KOTE KATIKA NCHI ZOTE”… Sasa swali??…Je zilienea sekunde ile ile, au muda ule ule, aliotoa Pepo?..Jibu ni la!...bali ni baada ya kipindi Fulani cha wakati labda masaa kadhaa mbele au siku moja mbele au siku kadhaa???… Kwani isingewezekana ndani ya sekunde ile ile muujiza ulipotokea, habari zifike Galilaya yote ambayo ilikuwa na vimiji vidogo vidogo Zaidi ya 400 kulingana na historia na miji hiyo ikiwemo Nazareti, Kapernaumu, korazini na Bethasaida, Na tena si Galilaya tu!, na hata nje ya Galilaya, maana hapo anasema taarifa zilifika miji yote ya kandokando ya Galilaya (maana yake nje ya Galilaya).

Kwa mantiki hiyo basi tutakuwa tumeelewa kuwa Mathayo alipotumia neno “kunyauka Mara” hakumaanisha sekunde ile ile, bali alimaanisha kuwa ni kwa kipindi Fulani cha masaa kadhaa, (haraka sana, ambako sio kwa kawaida kwa desturi ya miti kunyauka)… kwa maana kikawaida mpaka mti unyauke unachukua siku kadhaa, na huo ni kama umekatwa…sasa ule haukuonekana kama umekatwa, lakini ulinyauka kabisa (Hivyo ni muujiza).

Kwahiyo kwa hitimisho ni kuwa mtini mpaka kufikia asubuhi ndio ulionyesha kunyauka na wanafunzi walishagaa hiyo asuhubi hivyo biblia haijichanganyi mahali popote..

Je unaliamini Neno la Mungu?.. Na je umeokoka?…Kama bado ni nini kinachokusubirisha usimpokee Bwana YESU??.. Fahamu kuwa tunaishi katika siku za mwisho na YESU yu mlangoni.. hivyo usiyachezee maisha yako wala mtu mwingine yoyote asiyachezee..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MTINI, WENYE MAJANI.

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?

Rudi Nyumbani

Print this post

Je biblia inajichanganya katika ile habari ya binti wa Yairo?

Swali: Je biblia takatifu inajichanganya katika habari ile ya binti wa Yairo?.. kwamaana katika Marko na Luka inaonyesha kuwa Binti alikuwa katika kufa! (Marko 5:23) Lakini katika Mathayo 9:18 inasema binti alikuwa amekwishakufa, sasa habari ipi ni sahihi kati ya hizo mbili?


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa biblia haijichanganyi mahali popote, isipokuwa pambanuzi zetu, na tafakari zetu ndizo zinazochanganyikiwa. Sasa ili tuelewe vizuri, turejee mistari hiyo..

Marko 5:21  “Hata Yesu alipokwisha kuvuka kurudia ng’ambo katika kile chombo, wakamkusanyikia mkutano mkuu; naye alikuwa kando ya bahari.

22  Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona, akaanguka miguuni pake,

23  akimsihi sana, akisema, BINTI YANGU MDOGO YU KATIKA KUFA; nakuomba uje, uweke mkono wako juu yake, apate kupona, na kuishi

24  Akaenda pamoja naye; mkutano mkuu wakamfuata, wakimsonga-songa.”…..

Turuke mpaka mstari ule wa 35 na 36 ili tuimalizie habari hii kama ilivyoelezewa na Marko..

35  Hata alipokuwa katika kunena, WAKAJA WATU KUTOKA kwa yule mkuu wa sinagogi, WAKISEMA, BINTI YAKO AMEKWISHA KUFA; kwani kuzidi kumsumbua mwalimu?

36  Lakini Yesu, alipolisikia lile neno likinenwa, akamwambia mkuu wa sinagogi, Usiogope, amini tu”

Katika kisa hiki ni kweli tunaona taarifa zinaanza na binti kuwa katika HALI YA KUFA, na zinaishia na BINTI KUFA.. Lakini tukirejea katika kitabu cha Mathayo tunaona habari nyingine ambayo inaonekana kama ni tofauti kidogo..

Turejee…

Mathayo 9:18  “Alipokuwa akiwaambia hayo, tazama, akaja jumbe mmoja, akamsujudia, akisema, BINTI YANGU SASA HIVI AMEKUFA; lakini njoo, uweke mkono wako juu yake, naye ataishi.

19  Akaondoka Yesu, akamfuata, pamoja na wanafunzi wake”……….

Hapa tunasoma kuwa Jumbe-Yairo anamwambia Bwana kuwa Binti yake amekwisha kufa, na si yu katika kufa!, hivyo aende kumwekea mikono afufuke.. sasa swali je! Biblia inajichanganya?

Jibu ni la!.. kama tulivyosema, biblia haijichanganyi, isipokuwa ni pambanuzi zetu.

Sasa ili tukiweke hiki kisa vizuri; ni kwamba Yairo alipotoka nyumbani mwake kumfuata Bwana YESU, binti yake alikuwa hajafa bado!, ila alikuwa katika hali ya kufa,..na alipokutana na Bwana akamwomba aende amwekee mikono ili apone, sawasawa na Marko alivyorekodi hapo katika Marko 5:23, tukio ambalo halijarekodiwa na Mathayo..

Lakini alipokuwa katika kumsihi Bwana kuna watu baadhi waliotokea nyumbani kwake na kumpa taarifa kuwa binti yake amekwisha kufa!…Sasa Yairo aliposikia kuwa mwanae kafariki hakukata tamaa, bali aliendelea kumsihi Bwana kuwa aende kumwekea mikono ili afufuke hata kama amekwisha kufa!, Na Bwana YESU aliposikia hayo akaahidi kwenda naye.

Lakini alipokuja mtu mwingine kutoka nyumbani mwake kumpa hizo hizo taarifa kuwa binti yake kashafariki hivyo asizidi kumsumbua mwalimu… (maana yake alikuwa anarudia rudia kumwambia, sasa hiyo kauli ya asizidi kumsumbua Marko 5:35) ndio iliyomfanya Bwana YESU amwambie ASIOGOPE!, kwani ndiyo inayokatisha tamaa, na yenye kuua Imani ya Jumbe (Marko 5:36).

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa Mwandishi wa kitabu cha Marko alianzia kuelekezea tukio kuanzia mwanzo kabla ya binti kufa, na kutaja kuwa watu walikuwepo Zaidi ya mmoja waliokuja kumpa taarifa Yairo za kifo cha mwanae (Marko 5:35),

Lakini mwandishi wa kitabu cha Mathayo alianzia kuelezea tukio katikati wakati ambao tayari binti amekwishakufa na hakuelezea kabla ya kufa kwake…..Hivyo hakuna mkanganyiko wowote hapo, na wala mahali pengine popote katika biblia.

Je umeokoka?.. Je unafahamu kuwa tunaishi katika majira ya siku za mwisho?, na Kristo yupo mlangoni?. Kama bado hujampokea unangoja nini?.. Mpokee leo na ubatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU KRISTO, upate ondoleo la dhambi zako nawe utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

USIFE NA DHAMBI ZAKO!

ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!

MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 2)

Je biblia inajichanganya kwa habari za Yohana kuwa Eliya?

Rudi Nyumbani

Print this post

MWANAMKE UKITAKA KIBALI, USIWE MTU WA KUPENDA VITU. (Esta 2:17)

(Masomo maalumu kwa wanawake).

Kama wewe ni mwanamke na unatamani kupata kibali cha ndoa, au kupata mtu sahihi wa atakayekupenda, basi kuwa kama Esta, ambaye alikuwa na tabia ya kutokupenda-penda vitu!… Wengi wanadhani ubikira ndicho kigezo cha juu ya kupata kibali… Nataka nikuambie sivyo!.. walijitokeza mabikra wengi mbele ya Mfalme Ahasuero, lakini ni mmoja tu aliyechaguliwa..

Sasa ni kigezo gani cha juu kilichompa Esta umalkia??….Turejee maandiko tutapata majibu..

Esta 2:15 “Hata ilipowadia zamu yake Esta, binti Abihaili, mjomba wake Mordekai, ambaye alimtwaa kuwa binti yake, ili aingie kwa mfalme, YEYE HAKUTAKA KITU, ila vile vilivyoagizwa na Hegai, msimamizi wake mfalme, mwenye kuwalinda wanawake. Naye huyu Esta alikuwa amepata kibali machoni pa wote waliomwona.

16 Basi Esta alipelekwa kwa mfalme Ahasuero, katika nyumba ya kifalme, mwezi wa kumi, ndio mwezi wa Tebethi, mwaka wa saba wa kumiliki kwake.

17 MFALME AKAMPENDA ESTA KULIKO WANAWAKE WOTE, NAYE AKAPATA NEEMA NA KIBALI MACHONI PAKE KULIKO MABIKIRA WOTE; BASI AKAMTIA TAJI YA KIFALME KICHWANI PAKE, AKAMFANYA AWE MALKIA BADALA YA VASHTI”.

Esta hakuwa na tabia ya kupenda-penda vitu (kwa ufupi hakuwa na tamaa) na wala hakuwa na mambo mengi!!.. aliingia kwa mfalme yeye kama yeye, katika uhalisia wake!.. wakati wengine walitaka waingie kwa mfalme na marashi yao, na mitindo yao, na wapambe wao, ili wakubalike, Esta yeye hakutaka hayo yote, aliona ni ulimbukeni, aliingia yeye kama yeye, isipokuwa vitu vichache ambaye yule msimamizi aliyeitwa Hegai alimshauri.

Hata leo ni hivyo hivyo, Biblia bado ni Neno la Mungu lililo hai, kupitia hilo tunajifunza kanuni nyingi.. kama wewe ni binti!, au mwanamke!.. ukitaka kibali na Neema.. basi KUWA WEWE!!!... Usianze kujibadili maungo yako, au sauti, au chochote kile katika mwili wako ambacho umeumbwa katika ualisi wake, vile vile usiwe mtu wa tamaa ya vitu (kila unachokiona unakitamani)..

Ukiwa mtu wa namna hiyo ni rahisi sana kupata kibali.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mistari ya biblia kuhusu kibali.

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

ESTA: Mlango wa 4

Rudi Nyumbani

Print this post

Ipi tofauti ya Ulawiti na Ufiraji (1Wakorintho 6:9)?

Ulawiti na Ufiraji vina tofauti gani, kulingana na 1Wakorintho 6:9?


Jibu: Turejee…

1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, WALA WAFIRAJI, wala WALAWITI”

“Ulawiti” ni kitendo cha mwanaume kumwingilia mwanaume mwingine kinyume na maumbile… Na “Ufiraji” ni kitendo cha Mwanaume kumwingilia mwanamke kinyume na maumbile.

Mambo haya yote mawili ni machukizo makuu mbele za Mungu, na “wafiraji na walawiti” hawataurithi uzima wa milele sawasawa na maandiko hayo.

Kama wewe ni mwanaume na una mke jiepushe na Ufiraji!.. na kama wewe ni mwanamke na una mume kataa ufiraji, kama mwenzako anataka kukuacha kwasababu hiyo ya wewe kuukataa ufiraji, hapo yupo huru kuondoka!.. na wewe upo huru kuoa au kuolewa na mwingine mwenye kufanana na wewe, (asiyefanya mambo hayo na aliyeokoka)!

1Wakorintho 7:15 “Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika Amani”.

Neno “Ulawiti” limeonekana mara moja tu katika biblia na ni tendo baya kuliko ufiraji (Maana humu ndio wamo mashoga, jamii za wale watu wa Sodoma na Gomora).. Kwa ujumla Mkristo hapaswi kulawiti/kulawitiwa… kufira/kufirwa. Wote wafanyayo hayo, wana roho nyingine ndani yao, na sehemu yao itakuwa katika lile ziwa la moto.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mshahara wa Mbwa ni upi? Kama tunavyousoma katika Kumbukumbu 23:18

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

MSIWE NA UCHUNGU NAO!

Hapo ndipo, atakapompa Mungu Baba ufalme wake.

Fahamu maana 1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya usijiongezee hekima mno? (Mhubiri 7:16b)

Swali: Kwanini biblia ikataze kujiongezea hekima, kwani kuna ubaya gani katika kuongeza hekima?

Jibu: Turejee..

Mhubiri 7:16 “Usiwe na haki kupita kiasi; Wala usijiongezee hekima mno; Kwani kujiangamiza mwenyewe?”.

Hekima inayozungumziwa hapo si hekima ya KiMungu, ambayo hiyo tumeagizwa tuitafute sana..

Yakobo 1:5 “Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa”.

Tena maandiko yanasema mtu aonaye hekima (hiyo ya kiMungu), biashara yake ni Zaidi ya fedha..

Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu.

14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.

15 Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye”.

Kwahiyo hekima iliyozungumziwa hapo katika Mhubiri 7:16b ambayo mtu akiwa nayo nyingi inamharibu si hekima ya kiMungu, bali ni HEKIMA YA KIDUNIA.. Ambayo hiyo kwa Mungu ni upuuzi sawasawa na 1Wakorintho 3:18

1Wakorintho 3:18 “Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.

19  Maana HEKIMA YA DUNIA HII NI UPUZI MBELE ZA MUNGU. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao.”

Umeona?.. kumbe hekima ya dunia ni upuuzi mbele za Mungu na hiyo mtu akijiongezea sana itamwangamiza!!!.

Sasa mfano wa hekima ya kidunia ni ile inayosema “mwanadamu asili yake ni nyani”.. sasa hii ni elimu/hekima ya kidunia..ambayo imetukuka miongoni mwa wasomi wengi wakubwa, kiasi kwamba mtu aliyezama sana katika hiyo hekima, anajiangamiza mwenyewe, kwani atafikia hatua ya kusema hakuna MUNGU.

Ndio maana hapo biblia inasema “usijiongezee mno”… Maana yake usizame sana katika kuzitafuta, kwani zimejaa upotofu mwingi na ukweli kidogo…

Bwana atusaidie.

Kwa maarifa Zaidi kwanini biblia iseme “usiwe na haki kupita kiasi” fungua hapa >>>>>USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini Mungu alimkataa Sauli? (1Samweli 15:23)

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?.

Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

Rudi Nyumbani

Print this post