Category Archive Maana ya maneno

Ukaufu ni nini? (Kumbukumbu 28:22).

Swali: Ukaufu ni nini na Koga ni nini kama tunavyosoma katika Kumbukumbu 28:22?


Jibu: Turejee.

Kumbukumbu 28:22 “Bwana atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto, na kwa upanga, na kwa UKAUFU, na kwa KOGA; navyo vitakufukuza hata uangamie”

“Ukaufu” ni ugonjwa wa mazao unaotokana na utandu (fangasi), tazama picha juu. Ugonjwa huu unaposhambulia zao la nafaka basi linapata mabaka mabaka na kisha kunyauka na mwishowe kutozalisha chochote.

Sasa hapo Bwana alikuwa anasema na watu wake  Israeli (ambao ni sisi pia) kwamba tutakapomwacha Bwana na kufuata miungu mingine na kuiabudu basi tutakuwa tumefungua milango ya laana juu ya maisha yetu,  kwani tutapigwa kwa magonjwa ya mwilini lakini pia mazao ya mashamba yetu yatapiwa kwa magonjwa.. na pia tutapigwa kwa misiba na majanga ya nchi.

Mfano wa magonjwa ya mwilini ni hayo yaliyotajwa hapo (Kifua kikuu, homa na kuwashwa).. na mfano wa magonjwa yatakayoshambulia mimea yetu hata tusipate chakula ni hayo yaliyotajwa hapo (Koga na UKAUFU),

Koga ni utandu mweupe unaoshambulia mimea ambao nao pia ukikamata zao la chakula, basi zao lile linadhoofika na hatimaye kufa. (Tazama picha chini).

koga ni nini

Lakini pia mfano wa majanga nchi yatakayotupata ikiwa tutamwacha Bwana ni hayo yaliyotajwa hapo juu (hari ya moto na upanga)..Hari ya moto inayozungumziwa hapo ni vipindi vya ukame na jua kali na upanga unaozungumziwa hapo ni vita (au umwagaji damu).

Na sio kwa mambo hayo tu, bali pia kwa mambo mengine mengi yaliyotajwa hapo katika Kumbukumbu 28 na yasiyotajwa… yote yatatupata ikiwa tutamwacha BWANA MUNGU WETU, na kujitumainisha katika mambo mabaya…

Kumbukumbu 28:58 “Kama hutaki kutunza kufanya maneno yote ya torati hii yaliyoandikwa katika kitabu hiki, upate kulicha jina hili la fahari na utisho, Bwana, MUNGU WAKO;

59 ndipo atakapofanya Bwana mapigo yako yawe ya ajabu, na mapigo ya uzao wako, mapigo makubwa kwa kweli, ya kudumu sana, na magonjwa mazito ya kudumu sana.

60 Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe.

61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa”.

Lakini kinyume chake, ikiwa tutamtii Bwana MUNGU WETU, na kwenda katika njia zake, basi tutafanikiwa sana kufungua milango ya Baraka nyingi, wala hatutapatwa na hayo yote (Saswasawa na Kumbukumbu 28:1-14)

Bwana atusaidie na kutuneemesha.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAGONJWA YAKUPATAYO MARA KWA MARA.

Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

ATAANGAMIZWA NA KUTENGWA NA WATU WAKE.

Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?

Rudi Nyumbani

Print this post

Hadhari ni nini kibiblia? (Mithali 1:4)

Hadhari ni nomino ya kitenzi tahadhari. Neno Lenye maana ya “uangalifu”.

>Kwamfano mwalimu anayesahisha mitihani ya wanafunzi tunasema huwa na hadhari kubwa katika usahishaji.

  • Kula bila hadhari ya usafi huweza sababisha magonjwa.

Katika biblia neno hili utalisoma kwenye vifungu hivi;

Danieli  2:13 Basi ile amri ikatangazwa, na hao wenye hekima walikuwa karibu na kuuawa; watu wakamtafuta Danielii na wenzake ili wauawe.  14 Ndipo Danieli kwa busara na HADHARI akamjibu Arioko, akida wa walinzi wa mfalme, aliyekuwa ametoka ili kuwaua wenye hekima wa Babeli;  15 alijibu, akamwambia Arioko, akida wa walinzi wa mfalme, Mbona amri hii ya mfalme ina ukali namna hii? Ndipo Arioko akamwarifu Danielii habari ile

Mithali 1: 1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.  2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu;  3 kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili.  4 Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na HADHARI;

Yoshua 22:24 au kama sisi tumefanya jambo hili kwa HADHARI sana, tena makusudi, huku tukisema, Katika siku zijazo wana wenu yamkini wakanena na wana wetu, na kusema, Ninyi mna nini na Bwana, yeye Mungu wa Israeli?

Sisi pia kama watakatifu, tuwe na hadhari, katika maisha ya ulimwenguni. Tunaishi ulimwenguni lakini hatupaswi kufungwa nira na huo kwa jinsi isivyo sawasawa. Kwasababu watu wanaokosa jambo hili husongwa na anasa, udanganyifu wa mali na shughuli za ulimwengu huu, na tamaa ya mambo mengine hatimaye hawazalishi kitu.

Shalom.

Je! Umeokoka? Unatamani leo kupokea msamaha wa dhambi? Ikiwa jibu ni ndio basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya kumkaribisha Yesu moyoni mwako.>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

AGANO LA MOYO LENYE NGUVU

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?

Rudi Nyumbani

Print this post

Heshima ni nini kibiblia?

Heshima ni kitendo cha kumpa mtu hadhi yake, au uthamani wake anaostahili. Kwa kawaida kila mwanadamu anastahili heshima. Na hivyo kama mwamini huna budi kujua jinsi ya kuigawanya heshima kulingana na mtu husika. Kwasababu ukosefu wa heshimu, kwanza ni zao la kiburi (Mithali 15:33), lakini pia hukuondolea Baraka na kibali  popote pale uendapo. Lakini pia ukitoa heshima isiyompa mtu ni kosa pia.

Warumi 13:7  Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima

Heshima kwa Mungu ipo wapi?

  1. Ipo katika kuliamini na kuliishi Neno lake: Si katika kulipamba jina lake, na huku hufanyi anayokuambia. Alisema. Luka 6:46  Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo? 47  Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake.
  2. Ipo katika uaminifu katika  utoaji: Mithali 3:9 Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote
  3. Ipo katika ibada :  Anayestahili kuabudiwa, kusujudiwa, kupigiwa magoti, kuhimidiwa ni Mungu tu peke yake, na wala si mwanadamu au kiumbe kingine pamoja naye, heshima hii inamuhusu yeye peke yake. Ufunuo 4:11 “ Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa”

Heshima kwa Wazazi ipo wapi?

  1. Kuwasaidia. Biblia inasema kuwaheshimu wazazi ni pamoja na kuwasaidia kimahitaji (Mathayo 15:1-7)
  2. Kuwasikiliza na kushika maagizo yao: Mithali 1: 8 Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

Heshima kwa Viongozi wako wa kiroho ipo wapi?

Kutii maelekezo yao.

Waebrania 13:17  Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.

Heshima kwa watoto ipo wapi?.

Kutowakwaza,

Waefeso 6:4  Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.

Heshima kwa Viongozi wa nchi.

Kutenda agizo lao.

Warumi 13:1  Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. 2  Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu

Heshima kwa Mabwana ipo wapi?

Kuwatumikia kwa uaminifu na adabu. (Waefeso 6:5-8)

Hivyo kwa hitimisho, ni kwamba kila mwanadamu anastahili heshima, haijalishi, tajiri, au maskini, mrefu au mfupi, mgonjwa au mzima, mwenye elimu au asiye na elimu, bwana au mtumwa, ameokoka au hajaokoka. Wote ni agizo tuheshimiane.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

CHUJIO HILI NI LA AJABU SANA!

JIWE LILILO HAI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuapiza ni nini? (Mathayo 5:21-22)

Mathayo 5:21  Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu akiua, itampasa hukumu. 22  Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto.

JIBU: Katika vifungu hivi tunaona Bwana Yesu anatoa mtazamo mpya kuhusiana na dhambi ya uuaji. Hapo mwanzo ilidhaniwa kuwa pale mtu anapochukua hatua ya kumchinja ndugu yake, au kumpiga mpaka kufa kama alivyofanya Kaini, ndio umehitimu kuwa muuaji. Lakini Bwana Yesu anasema..

Kitendo  tu cha kumwonea hasira ndugu yako, kumfyolea, na kumwapiza, tayari ni kosa la uuaji.

Sasa alikuwa na maana gani kwa maneno hayo matatu. “Hasira, kufyolea na kuapiza?”

Hasira kwa ndugu, huzaa mambo kama kinyongo, uchungu, na wivu. Kwahiyo kama mtu akiwa na mambo kama hayo  kwa ndugu yake, mbele ya Kristo amestahili kuhukumiwa.

Lakini pia akimfyolea. Kumfyolea ni kumwita mwenzako mjinga wewe, au mpumbavu wewe. Ukilenga mtu asiye na akili, Kwa urefu wa tafsiri hii fungua hapa>> RACA Hilo nao ni kosa lililostahili kuketishwa kwenye mabaraza ya wazee, utoe hesabu.

Lakini mbaya zaidi kumwapiza. Hichi ni kitendo cha kumtamkia kabisa maneno ya  laana. Kana kwamba ni mtu mwovu sana aliyepindukia. Kwamfano kumwita ndugu yako mwana-haramu wewe, au kumwita ‘shoga wewe’, kumwita msenge(neno lenye maana mtu anayeshiriki uovu kinyume na jinsia yake), kumwita pepo, kafiri wewe, n.k. maneno ambayo hayawezi kutamkika, ni sawa na tusi kwa mwenzako. Huko ndio kuapiza.

Adhabu yake Kristo anaifananisha na kutupwa katika jehanamu ya moto.

Hivyo hatupaswi kudhani kuwa, kuua ni mpaka tumwage damu, lakini twaweza kufanya hivyo tokea moyoni mwetu hadi vinywani mwetu, kabla hata hatujafikia kwenye kitendo chenyewe.

Tujazwe Roho Mtakatifu, tuwezi kuzishinda tabia hizi mbaya za mwili.

Katika agano la kale ilikuwa sio tu kumpiga mzazi wako, ilikupasa kifo (Kutoka 21:15), lakini pia kumwapiza huku, adhabu yake ilikuwa ni moja tu na hilo kosa la kwanza yaani kifo.

Kutoka 21:17 “Yeye amwapizaye baba yake au mama yake, sharti atauawa”

Shalom.

Je! Umeokoka? Fahamu kuwa usipomwamini Kristo, na kupokea msamaha wake wa dhambi, hauna uzima wa milele ndani yako. Kwasababu kamwe hutakaa umpendeze Mungu kwa nguvu zako au matendo yako mwenyewe. Na sababu ya Yesu kufa msalabani kwa ajili yako kukusaidia, kupokea msamaha wa dhambi, lakini pia nguvu ya kushinda mambo mabaya kwa Roho wake Mtakatifu tuliopewa. Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu akuokoe leo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo ya wokovu, Bwana akubariki >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Amen

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bwana alimaanisha nini kusema “atazamaye mwanamke kwa kumtamani” amezini naye?

Je ni sahihi kumwita mtu “Mkuu”?

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

UFANYE MOYO WA MUNGU UWAELEKEE WATU WAKE.

Rudi Nyumbani

Print this post

SAFINA NI NINI?

Kwa kiyahudi huitwa ‘Tevat’, ni chombo cha majini kilichotumika mahususi kwa ukombozi. Ni mfano wa meli iliyotumika kuokoa watu/wanyama kutoka katika maangamizi fulani. Kwamfano katika biblia tunaona Nuhu aliagizwa atengeneze safina, ambayo ataingia yeye pamoja na familia yake, na wanyama wa nchi.

Ukisoma Mwanzo 6-8, utapata kufahamu vipimo vya safina hiyo vilivyokuwa na vigezo vyake, japokuwa biblia haijatueleza mahususi umbo la chombo kile kilivyokuwa.

Lakini pia wakati Musa anazaliwa, tunaona wazazi wake walimtengeneze a naye kisafina kidogo, akafichwa ndani yake, ili kunusuriwa na maangamizi ya Farao.

Kutoka 2:1 Mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaondoka akaoa binti mmoja wa Lawi. 

2 Yule mwanamke akachukua mimba akazaa mwana, na alipoona ya kuwa ni mtoto mzuri akamficha miezi mitatu. 

3 Na alipokuwa hawezi kumficha tena, akampatia kisafina cha manyasi akakipaka sifa na lami, akamtia mtoto ndani yake, akakiweka katika majani kando ya mto.

Jambo la muhimu kufahamu ni kuwa safina hizo ilikuwa ni lazima zipakwe LAMI ndani na nje. Lami hizo ni mfano wa gundi nzito zilizopakwa, lengo lake likiwa ni kuzuia maji yasiweze kupenya sehemu yoyote ndani ya Safina, (Mwanzo 6:14, Kutoka 2:3). Safina zilikuwa na sifa kama za “nyambizi” tulizonazo sasa, ambazo hazihathiriwi na maji mahali popote ziwapo juu au chini ya maji.

Safina inamwakilisha nani ?

Ni Kristo Yesu, yeye ndiye mwokozi wetu dhidi ya ghadhabu ya Mungu juu ya ulimwengu huu kwa wenye dhambi. Na DAMU yake ndiyo ile LAMI. Inayonyunyizwa kwetu sisi. Mtu yeyote ambaye hajamwamini Yesu, ni dhahiri kuwa ghadhabu ya Mungu ipo juu yake, hawezi kuiepuka. Kwasababu amekataa msamaha wa dhambi, tuliopewa bure kwa kifo chake pale msalabani.

Je! Unaichezea neema? Kumbuka ulimwengu huu unafikia mwisho. Kristo amekaribia kurudi, kuwanyakua watu wake. Je! Bado upo kwenye dhambi? Ikiwa utataka kuupokea wokovu leo bure, basi uamuzi huo ni bora kwako, Hivyo waweza, fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa sala hiyo ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.

Mvinje ni mti gani? (Mwanzo 6:14)

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya sulubu/ sulubisha?

Neno sulubu huzaa kusulibisha/kusulubisha,

Maana ya Sulubu, ni kuadhibisha kwa kuning’iniza kwenye mti wa msalaba, au nguzo iliyonyooka, kwa kufungwa au kugongelewa miguu na mikono, na kuacha hapo mpaka ufe.

Hii ni aina ya adhabu ya kifo, ambayo ilitumika zamani, kwenye falme zilizokuwa na nguvu na katili kama Rumi.

Watu walioshitakiwa kwa makosa makubwa ikiwemo uhaini, au uuaji, uvunjaji amani, hawakupewa adhabu ya kawaida ya kifo kama vile kukatwa kichwa na kufa mara moja,. Bali walipewa adhabu kali kama hii, lengo lake ni kumfanya Yule mshitakiwa kupitia mateso makali ya muda mrefu kabla ya kufa, kwasababu, baada ya kuning’inizwa kwake pale msalabani itamchukua siku tatu mpaka wakati mwingine wiki hadi kufa. Hivyo kipindi chote hicho unatakuwa unateseka tu pale mtini.

Hiyo ndio adhabu waliyoichagua kwa mwokozi wetu Yesu Kristo, ambaye hakuwa na hatia yoyote, wala kosa, jambo ambalo hata mtawala yule Pilato alilishuhudia kuwa hakukuwa na uovu wowote ndani yake. (Luka 23:4). Lakini kwasababu ilipasa maandiko yatimie ili sisi tupate ukombozi mkamilifu, ndio maana ilimpasa Yesu aadhibiwe vikali, ili mimi na wewe tupokee ONDOLEO LA DHAMBI. Kwa kifo chake.

Gharama aliyoilipa ni kubwa sana, kusulubiwa uchi wa mnyama, bila nguo, kudhalilishwa na kupigwa, na kuharibiwa mwili wote. Ni kwasababu mimi na wewe tupokee msamaha wa dhambi, tuepushwe na hukumu ya milele ya jehanamu ya moto.

Ndio maana maandiko yanasema..

Waebrania 2:3  sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia.

Je! Umempokea Yesu maishani mwako?

Ikiwa ni la! Basi waweza kufanya hivyo sasa, kwa kubofya hapa ili upate mwongozo wa sala hiyo. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kulaumu/ Lawama ni nini kibiblia?

Je! wakristo tunalaumiwa?

JIBU: Ni mashtaka au maneno  Fulani yanayotolewa dhidi yako, yanayolenga kutoridhishwa na mwenendo, au maneno au tabia yako.

Tunaweza tukawa watoto wa Mungu, na bado siku ile ya mwisho tukalaumiwa na Mungu.  Utauliza ni kwa namna gani?

Ni kweli deni letu la mashtaka limeondolewa pale msalabani kwa Kifo cha Yesu Kristo. Na kwamba mtu anapomwamini tu Yesu Kristo haukumiwi, bali anaingia uzimani. Tafsiri yake ni kuwa hana lawama la hukumu ya jehanamu (Wakolosai 1:21-22)

Lakini, kumbuka wewe “unahesabiwa” kuwa mwenye haki. Lakini kiuhalisia “huna haki ndani yako”. Yaani kwa asili wewe huna kitu chochote kizuri ndani yako mbele za Mungu, na kimsingi huo sio mpango Mungu aliokusudia kwa mwamini. Mungu anataka amwokoe mtu wake, na wakati huo huo awe mkamilifu kama yeye.

Ndio hapo hatupaswi kuichukulia NEEMA ya Mungu kama fursa ya sisi kupumzika katika dhambi, au kupuuzia matendo ya haki. Au kutokuonyesha bidii yoyote ya Kufanana na Kristo.

Maandiko yanasema watu wengi wataonekana kuwa na lawama, mbele za Kristo, kwa kushindwa tu kurekebisha baadha ya mienendo yao, walipokuwa hapa duniani.

Kwa mfano maandiko haya yanaeleza baadhi ya mienendo, hiyo; moja wapo ni  kukaa katika  Mashindano, au manung’uniko ndani ya wokovu hupelekea utumishi wako,kulaumiwa .

Wafilipi 2:14  “Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,  mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu”

Vilevile kutofikia upendo  na  Utakatifu, ni zao la lawama.

1Wathesalonike 3:12  Bwana na awaongeze na KUWAZIDISHA KATIKA UPENDO, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;

13  apate kuifanya imara mioyo YENU IWE BILA LAWAMA KATIKA UTAKATIFU mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.

Tufanye nini ili tuweze kuepuka lawama, na tuwe na ujasiri, mbele za Kristo siku ile?

Ni kuitendea kazi neema ya Kristo maishani mwetu. Kwa kumtii yeye, na kumfuata kwa mioyo yetu yote, nguvu zetu zote, akili zetu zote na roho zetu zote, Ambayo inafuatana pia na bidii katika kujitenga na maovu, Ndipo itakuwa rahisi sisi kuyashinda,kwasababu ataiachilia nguvu yake ya ushindi itende kazi ndani yetu, na hivyo tutajikuta tunakaa mbali na mambo ya kulaumu.

1Wathesalonike 5:22  jitengeni na ubaya wa kila namna.

23  Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu MHIFADHIWE MWE KAMILI, BILA LAWAMA, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.

Hivyo ndugu uliyeokoka, tambua kuwa kila mmojawetu atatoa hesabu yake mbele za Mungu, siku ile. Hatuna budi sasa kuishi kama watu wanaotarajia TAJI bora, na sio watu wasio na mwelekeo wowote. Bwana asije akaona “neno ndani yetu”, mfano wa yale makanisa 7  tunayoyasoma katika Ufunuo 2&3, ambayo Yesu aliyapima akaona mapungufu. Hivyo tuishi kama watu wenye malengo, sio tu wa kukombolewa, bali pia wa kukamilishwa.

2Wakorintho 6:3  TUSIWE KWAZO LA NAMNA YO YOTE KATIKA JAMBO LO LOTE, ILI UTUMISHI WETU USILAUMIWE; 4  bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa Mungu; katika saburi nyingi, katika dhiki, katika misiba, katika shida;

5  katika mapigo, katika vifungo, katika fitina, katika taabu, katika kukesha, katika kufunga;

6  katika kuwa safi, katika elimu, katika uvumilivu, katika utu wema, katika Roho Mtakatifu, katika upendo usio unafiki;

7  katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu; kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto;

8  kwa utukufu na aibu; kwa kunenwa vibaya na kunenwa vema; kama wadanganyao, bali tu watu wa kweli.

Bwana akubariki.

Hivi ni baadhi ya vifungu vingine utakavyokutana na Neno hilo pia (1Timotheo 3:1-7, Luka 1:5-6)

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

Mtakatifu ni Nani?

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

MUNGU MWENYE HAKI.

Rudi nyumbani

Print this post

Rubani ni nani katika biblia? (Ezekieli 27:8)

Swali: Je zamani marubani wanaoendesha ndege walikuwepo kama tunavyosoma katika Ezekieli 27:8?


Jibu: Turejee mstari huo..

Ezekieli 27:8 “Wakaao Sidoni na Arvadi ndio waliovuta makasia yako; wana wako wenye akili, Ee Tiro, walikuwa ndani yako, ndio WALIOKUWA RUBANI ZAKE”.

“Marubani” wanaozungumziwa hapo si Marubani wanaorusha ndege kwamaana kipindi hicho ndege zilikuwa hazijavumbuliwa…bali marubani wanaozungumziwa hapo ni wana-maji (manahodha)..Kwasababu asili ya neno hilo rubani si mwana-anga, bali ni mwana-maji.

Isipokuwa kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda na kumavumbuzi mengi kuibuka, basi maneno mengi yanakuwa yanapata maana Zaidi ya moja.

Kwamfano katika biblia yametajwa magari (Mwanzo 45:21)..sasa magari ya zamani si sawa na haya sasahivi, ingawa yote ni magari… vile vile katika biblia kuna mahali pametajwa “Risasi” (Kutoka 15:10) lakini Risasi hiyo si sawa na hii inayojulikana sasa.. Vile vile pametajwa neno “Ufisadi“ (2Petro 2:7).. Lakini ufisadi huo wa biblia ni tofauti kabisa na huu unaofahamika sasa. N.k

Kwahiyo tukirudi katika Rubani, anayetajwa hapo katika Ezekieli 27:8, ni rubani mwana-maji, na si mwana-anga. Ndio maana ukiendelea mbele Zaidi katika mstari wa 29 utaona biblia imeweka sawa…

Ezekieli 27:29 “Na wote wavutao kasia, wana-maji, na RUBANI ZOTE WA BAHARINI, watashuka katika merikebu zao, na kusimama katika nchi kavu”.

Hapo anasema “Rubani zote za baharini” ikiashiria kuwa ni wana-maji na si wana-anga.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Risasi inayotajwa kwenye Ezekieli 27:12 ni ya namna gani?

Ufisadi una maanisha nini katika biblia?

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

Rudi nyumbani

Print this post

Neno kupomoka linamaana gani kwenye biblia?(Hesabu 16:22)

Hesabu 16:20 Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,  21 Jitengeni ninyi mkaondoke kati ya mkutano huu, ili nipate kuwaangamiza mara moja.  22 Nao WAKAPOMOKA kifudifudi, wakasema, Ee Mungu, Mungu wa roho za wenye mwili wote, je! Mtu mmoja atafanya dhambi, nawe utaukasirikia mkutano wote?

Soma pia

Yoshua 5:13 Ikawa hapo Yoshua alipokuwa karibu na mji wa Yeriko, akavua macho yake na kuangalia, na tazama, mtu mume akasimama kumkabili mbele yake, naye alikuwa na upanga wazi mkononi mwake; Yoshua akamwendea, na kumwambia, Je! Wewe u upande wetu, au upande wa adui zetu? 

14 Akasema, La, lakini nimekuja sasa, nili amiri wa jeshi la Bwana. Yoshua AKAPOMOKA kiusouso hata nchi, naye akasujudu, akamwuliza, Bwana wangu aniambia nini mimi mtumishi wake?

Neno hilo utalisoma pia katika vifungu hivi baadhi; Hesabu  16:4, 16:45,

Ni Kiswahili cha zamani cha Neno kuporomoka.  Yaani kuanguka chini, kwamfano maji yanayoelekea chini kwa wingi tunasema maporomoko ya maji, au udongo unaoanguka kutoka milimani kwa wingi tunasema maporomoko ya udongo.

Hivyo, katika vifungu anaposema Musa na Haruni wakapomoka kifudifudi, anamaanisha wakaanguka chini kifudi fudi mbele za Mungu kumlilia Bwana rehema.

Je! Na sisi tuombapo rehema au  tumtakapo Bwana kwa jambo Fulani muhimu ni lazima tupomoke chini ili tusikiwe ?

Jibu lake ni kwamba sio takwa kufanya hivyo. Kwasababu Mungu anaangalia moyo, kupomoka kwetu kunapaswa kuwe moyoni. Lakini pia si vibaya kuomba kwa namna hiyo, na ni vema, kwasababu pia ni ishara moja wapo ya unyenyekevu wa moyo. Ni sawa tu na tunapopiga magoti, au kunyosha mikono juu wakati wa kumwomba Mungu, kama ishara ya unyenyekevu mbele zake.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Ni kwanini tunambariki Mungu? Je! Mungu huwa anabarikiwa?

LAANA YA YERIKO.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Kuwatema farasi, maana yake ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Kuna tofauti gani kati ya “Mwivi” na “Mwizi”?

Swali: Kwanini katika biblia lisitumike neno “Mwizi” na badala yake linatumika neno “Mwivi”…Mwivi ni nini?


Jibu: Mwivi na Mwizi ni Neno moja, lenye maana moja.. isipokuwa ni lugha mbili za nyakati mbili tofauti.

Kiswahili kilichotumika katika kutafsiri biblia ni Kiswahili cha zamani, kilichoitwa “kimvita” ambacho ndicho kimebeba maneno ambayo hatuyaoni katika Kiswahili cha sasa, na mojawapo ya maneno ndio kama hayo “Mwivi na wevi” ikimaanisha “mwizi na wezi”. Ndio maana katika biblia yote huwezi kukuta neno Mwizi, badala yake utakuta mwivi (Soma Kutoka 22:2, Ayubu24:14, Zaburi 50:18, Mithali 6:30, Yoeli 2:9, Luka 12:39 n.k )

Maneno mengine ya kimvita (Kiswahili cha zamani) ambayo mengi ya hayo hayatumiki sasa ni pamoja na “jimbi” badala ya “Jogoo”“Kiza” badala ya “Giza”….”Nyuni” badala ya “ndege”…. “Kongwa” badala ya “Nira” na mengine mengi.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba “Mwivi” na “Mwizi” ni Neno moja, lenye maana ile ile moja (ya mtu anayeiba).

Lakini mbali na hilo, maandiko yanatufundisha kuwa Bwana YESU atakuja kama “Mwivi”..

Ufunuo 16:15 “(Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake)”

Je umewahi kujiuliza ni kwanini aje kama Mwivi na si Askari?.. Kwa upana juu ya hilo basi fungua hapa >>ANAKUJA KAMA “MWIVI” NA SI KAMA “ASKARI” FANYIKA CHOMBO CHA THAMANI.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KAMA MWIZI USIKU WA MANANE.

Nini maana ya Mithali 6:30 Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha

OKOA BADALA YA KUANGAMIZA!

Nini maana ya ELOHIMU?

Wale waliowekewa tayari ufalme ni akina nani?. (Mathayo 20:23).

Rudi nyumbani

Print this post