Category Archive Mithali

Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. 

Mstari huu unaeleza uhalisia wa mambo kwa ujumla wake katika maisha ya wanadamu hapa duniani.

Tunafahamu kwamba maskini wengi hutumia maombi kupata kitu, huwa wanyenyekevu pale wanapotaka kupewa kitu, kwasababu hawana. 

Lakini matajiri hawawezi kujishusha (japo si wote) kauli zao huwa ni za lazima na zenye amri. Kwani mali zake humpa kiburi. Hivyo waombe ya nini?

Sasa biblia haitufundishi tuwe matajiri ili tuwe wakali (wenye sauti) hapana, bali inatutahadharisha matokeo ya mafanikio yoyote. Jinsi yanavyoweza kumpotezea mtu unyenyekevu wake.

Bwana akunyanyuapo, ndio uwe wakati wako wa kujishusha. Kwasababu mali, fedha, mafanikio visipowekewa mipaka yake vinaweza kuyaharibu maisha ya mwaminio kwa sehemu kubwa. (1Timotheo 16:10)

Lakini pia katika eneo la kiroho. Kuna maneno haya Bwana Yesu aliyasema.

Mathayo 5:3

[3]Heri walio maskini wa roho;  Maana ufalme wa mbinguni ni wao. 

Ikiwa na maana watu walio maskini rohoni, ni wale wanaojiona kila siku wana haja na Mungu, bado hawajafika. Na hivyo humlilia Mungu sikuzote kwa unyenyekevu ili Bwana ayaongoze maisha yao.

Lakini wale wanaojiona wamefika wanajua kila kitu hawawezi kufanya hivyo. Ndio wale mafarisayo enzi za Bwana Yesu ambao hata kuomba kwao kulikuwa ni kwa majivuno (Luka 18:9-14). Hawawezi kujishusha, maneno yao ni ya ukali, wala hawaoni shida kumwita hata  Bwana wao Beelzebuli.

Hata kama tutakuwa tumepiga hatua kubwa kiasi gani rohoni, Bwana hataki tujidhani kuwa sisi tumefika, sisi ni matajiri, bali tumtegemee yeye sikuzote haijalishi wewe ni mtumishi mkubwa au uliyeokoka leo. 

Unyenyekevu kwa Bwana unapaswa uwe ni uleule. Usiende mbele za Mungu kama mtumishi wa Mungu, nenda kama mtoto wa Mungu mfano tu wa yule ambaye kaokoka leo. Jinyenyekeze kama vile ndio umeokoka leo. Kwasababu kumjua Bwana itatuchukua milele.

Lakini tukijiona ni matajiri tutaishia katika anguko hili alilolisema katika..

Ufunuo 3:17-19

[17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. 

[18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. 

[19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu. 

Hivyo katika utajri wowote (wa kiroho /kimwili). Bwana atupe unyenyekevu kama wa maskini. Ndio kiini cha mstari huo.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Tajiri na maskini hukutana pamoja; BWANA ndiye aliyewaumba wote wawili.

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 25:13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; 

SWALI: Nini maana ya Mithali 25:13

Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao;  Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao. 


JIBU: Kwa wanaoishi maeneo ambayo kuna misimu ya theluji, wanafahamu kuwa vipindi hivyo vya baridi vinapofika, huwa kunakuwa na upepo-baridi unaovuma.

Sasa kwa mujibu wa vifungu hivyo, anasema, Kama upepo huo ukivuma kipindi cha mavuno, ambacho kimsingi ni wakati wa kiangazi,na sio baridi, kingekuwa ni shangwe kubwa sana kwa wavunaji.

Kwa namna gani?

Kazi ya uvunaji inafanyika wakati wa jua kali, kwasababu mazao pia wakati huo yanakuwa yamekauka. Lakini pia mfano jua lile likapoozwa na upepo wa baridi, huuburudisha sana moyo wa mvunaji.

Vivyo hivyo anafananisha na wajumbe waaminifu wanaotumwa kupeleka habari fulani anasema; 

“Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao; Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao”. 

Mjumbe wa kwanza mwaminifu aliyetumwa ni Bwana wetu Yesu Kristo. Alimburudisha Baba moyo wake, kwasababu yote, na kusudi alilopewa kulifanya la kutukomboa sisi alilitimiza lote.

Vivyo hivyo na sisi, tumewekwa kuwa wajumbe wa Bwana, wa kuenenda  kuihubiri injili ya Kristo kwa kila kiumbe, ulimwenguni kote. Yatupasa tuwe waaminifu, mfano wa Bwana na mitume wake, ili moyo wa Kristo wetu ufurahi.

Na thawabu ya kuuburudisha moyo wa Bwana ni sisi kupewa mamlaka kubwa kule ng’ambo tufikapo, kwa mfano ambao Bwana Yesu aliutoa katika vifungu hivi;

Luka 19:12-26

[12]Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi. 

[13]Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja. 

[14]Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale. 

[15]Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake. 

[16]Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.

[17]Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi. 

[18]Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida. 

[19]Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.

[20]Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso. 

[21]Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda. 

[22]Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda; 

[23]basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake? 

[24]Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi. 

[25]Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi. 

[26]Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho. 

Je na sisi tunaweza kuwa mbele za Bwana Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; ?

Bwana atusaidie.

Je! Umeokoka?

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

WALIYATWAA MAVAZI YAKE, WAKAFANYA MAFUNGU MANNE,

Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 11:17 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake

Nini maana ya Mithali 11:17 inaposema;

Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake; Aliye mkali hujisumbua mwili wake.


JIBU: Mwenye rehema ni mtu wa huruma, mwenye kusamehe, mwenye kuachilia hata kama tendo alilofanyiwa linastahili adhabu kwa yule mwingine.

Biblia inasema mtu kama huyo huipa faida nafsi yake. Huitendea mema nafsi yake. Ambayo huipata kwanza hapa hapa duniani, kwasababu Bwana alisema kipimo kile tupimacho ndicho tutakachopimiwa na watu.

Marko 4:24 Akawaambia, Angalieni msikialo; kipimo kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa, na tena mtazidishiwa.

Maana yake ni anajijengea wigo mpana wa yeye naye kukutana na rehema nyingi mbeleni.

Vilevile anapata faida katika ulimwengu ujao, Bwana  alisema..

Mathayo 5:7 Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema.

Lakini anasema pia, mtu mkali hujisumbua mwili wake. Mtu mkali ni kinyume cha mtu mwenye rehema, ni mtu asiye na huruma, mwenye visasi, asiyejali, mkorofi, akiudhiwa anarudisha Maudhi, akikosewa kidogo, analipiza mara mbili, maneno yake hayana staha, kugombeza wengine kwake ni jambo la kawaida n.k.

Sasa matokeo ya mtu wa namna hii ni kuadhibiwa na Mungu, aidha hapa hapa duniani, au kule aendapo.

Bwana alisema…auaye kwa upanga, atauwa kwa upanga, ukimtendea mtu kwa ukali na wewe ukali utakurudia, ukimpiga mwingine kwasababu kakuudhi kidogo, na wewe utapigwa mahali fulani kwasababu ulimuudhi mwingine.. (hicho huitwa kisasi cha Mungu).

Hivyo tendea mema nafsi yako,lakini pia mwili wako, kwa kumpenda Bwana.Na kuwa mwema.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.(Opens in a new browser tab)

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

(Opens in a new browser tab)NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.(Opens in a new browser tab)

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?(Opens in a new browser tab)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 6:30 Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha

SWALI: Je!  Mithali 6:30 inamaana gani?

Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha, iwapo aona njaa;  31 Lakini akipatikana, atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake.

JIBU: Chukulia mfano mtu hajala siku tatu, halafu akaona kuna duka lipo wazi pale jirani, na mwenyewe ametoka, akashawishika kuingia haraka  na kubeba mkate, ili akale. Lakini mwenye duka aliporudi na kuona mkate umeibiwa, alianza kumfuatilia, mwishowe akamkuta amejificha mahali Fulani anakula akiwa katika hali mbaya.

Kibinadamu, atakapoona hali halisi ya mwizi, huwenda ataishia kukasirika tu, au kumgombeza, au kwenda kumwajibisha, kwa mambo madogo madogo. Kwasababu anaona alichokifanya ni kwa ajili ya kusalimu maisha yake tu, ale asife, lakini sio kwa lengo la kuchukua vya watu, akauze, au kuleta hasara kwa wengine.

Lakini sehemu ya pili ya mstari huo anaendelea kusema kama “akipatikana atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake”.

Maana yake ni kuwa kama “atapatikana na kosa”, basi atalipa mara saba. Atagharimikia vyote alivyoviiba mara saba. Sasa kauli hiyo haimaanishi kwamba mwizi huyo huyo aliyeiba kwa ajili ya kujishibisha tumbo lake ndio atalipa mara saba, hapana, vinginevyo mstari huo ungekuwa unajipinga unaposema “watu hawamdharau mwizi akiiba kwa kujishibisha”, bali  anamaanisha kama akipatikana na hatia tofauti na hiyo..mfano aliiba vitu ili akauze, aliiba fedha ili akajiendeleze kwenye mambo yake, alete hasara kwa wengine. Huyo atalipa gharama zote mara saba.

Ndio maana utaona adhabu nyingi za wezi huwa ni kubwa sana zaidi ya vile walivyoviiba, wanapigwa faini kubwa, wengine mpaka wanauliwa, kwa wizi tu mdogo. Hapo ni sawa na wamelipa mara saba.

Je! Hili linafunua nini rohoni?

Kama njaa ya mwilini, inaweza kumfanya mwizi asihesabiwe kosa. Kwasababu watu wanaelewa umuhimu wa kunusuru uhai kwa chakula, vipi kuhusu rohoni. Hata kuna wakati Daudi alikula mikate ya makuhani ambayo  hawakupaswa watu wengine kula, lakini kwasababu alikuwa na njaa yeye na wenzake haikuhesabiwa kwake kuwa ni kosa (1Samweli 21).

Vivyo hivyo rohoni, Mungu anatufundisha sio kwamba tuwe wezi, hapana, lakini anataka tuthamini sana roho zetu, pale zinapokuwa hazina kitu, zina njaa. Iweje mtu unakaa hadi unakufa kiroho halafu unaona ni sawa kuwa hivyo hivyo kila siku. Hufanyi jambo Fulani la kujinasua katika hiyo hali yako mbaya rohoni, unaendelea tu hivyo hivyo. Tafuta kwa bidii chakula cha kiroho usife ndugu. Jibidiishe.

Iba muda wako wa kufanya mambo mengine ili ukipate chakula cha kiroho. Ni kweli ulipaswa kuwepo mahali Fulani pa muhimu, embu ghahiri muda huo, nenda kasome biblia, nenda kaombe, nenda kasikilize mahubiri yatakayokujenga. Ulipaswa uwepo kazini, lakini kwasababu ibada ile ni muhimu embu usione shida kughahiri.

Huna biblia Iba hata pesa yako ya matumizi ya muhimu kanunue, acha uonekane mjinga nenda kanunue biblia au vitabu vya rohoni vikujenge. Tafuta ile MANA iliyofichwa.

Siku hizi ni za mwisho. Na Bwana alishatabiri duniani kutakuwa na njaa, sio ya kukosa chakula au maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Mungu ya kweli. Usipojiongeza katika eneo la ukuaji wako kiroho.  Ni ngumu kuvuka hizi nyakati mbaya  za manabii wengi wa uongo, na mafundisho ya mashetani. Usipoyajenga maisha yako ya kiroho, shetani akusaidie kuyajenga kwake.

Amosi 8:11 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana”

Penda biblia, penda kujifunza, penda maombi zaidi ya vingine.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.

NJAA ILIYOPO SASA.

(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

(Opens in a new browser tab)KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.(Opens in a new browser tab)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; 

SWALI: Nini maana ya Mithali 16:30

Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;  Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya. 

JIBU: Mstari huo haumaanishi mtu anayefumba macho yake, Huwa anaishia kuwaza mawazo mabaya, hapana kama ni hivyo basi,  tungekuwa tunafanya makosa kufumba macho tunapoomba.

Zaidi sana mtu mwenye hekima huwa anapoona jambo la kutisha ovu, au lenye aibu Ndio anayekuwa wa kwanza kufumba macho yake asiruhusu kuona kinachoendelea.. kama vile walivyofanya watoto wa Nuhu.(Mwanzo 9:23)

Hali kadhalika anaposema mtu aikazaye (aifumbaye), midomo yake. Haimaanishi mtu asiyezungumza-zungumza, Huwa anaishia kuyazungumza maneno yasiyofaa. Kama ni hivyo biblia isingesema;

Mithali 21:23

[23]Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu. 

Lakini je? Vifungu hivyo vilimaanisha Nini?

Hapo anaposema afumbaye macho yake ni kuwaza yaliyopotoka,..alimaanisha afumbaye macho asitazame kweli (ambayo ni Neno la Mungu), linapomfundisha au kumwonya. Mtu huyo lengo lake ni kuendelea katika mawazo yake mabaya ya dhambi. Mfano aambiwapo kuishi na mke ambaye si wako ni uzinzi, na wazinzi sehemu Yao ni Katika ziwa la moto, lakini hataki kuliona au kulisikia Hilo andiko, jibu lake ni kuwa anataka kuendelea katika matendo yake ya giza.

Ndicho kilichokuwa Kwa waliompinga Yesu., Ndio maana akasema  maneno haya; 

Mathayo 13:15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, 

Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Vilevile anaposema “Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya”

Anamaanisha, aizuiaye midomo yake kusema maneno ya uzima, ya staha, ya kujenga, ya adabu, ya maarifa, ya busara n.k.. Mwisho wake utakuwa ni kunena maneno mabaya tu.

Bwana alisema..

Luka 6:45

[45]Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake. 

Vivyo na hivyo na sisi, hatuna budi tujipime na kujichunguza…macho yetu hutazama Nini, vinywa vyetu vimejawa na maneno gani.? Lakini fahamu kuwa huwezi kushinda jicho lako, au ulimi wako ikiwa Kristo hajaumbika ndani yako.

Je! Unataka msaada Kwa Yesu Kristo? Kama jibu ni Ndio, basi unachopaswa kufanya cha kwanza ni kuyaachilia maisha yako kwake. Ili akusamehe dhambi zako. Ndipo akupe nguvu ya kushinda dhambi.

Hivyo bofya hapa Kwa ajili ya Mwongozo wa Sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

NI WAKATI UPI UTAUONA USO WA KRISTO?

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya  Mithali 21:1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana;

SWALI: Nini maana ya  Mithali 21:1

“Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo”.


JIBU: Kuna mithali inayosema “maji hufuata mkondo”. Ikiwa na maana, palipo na mfereji kule kule unapoelekea ndipo maji nayo huelekea. Mfano ukielekeza mrefeji shambani mwako, basi maji yale yataelekea huko si kwingineko, ukielekezea mfereji nyumbani mwako, basi maji yatakuja ndani mwako. Kamwe maji  hayajiamulii  pa kuririkia.

Vivyo hivyo na Mungu, ndivyo anavyofananisha mamlaka yake juu ya wafalme na wakuu wa dunia hii. Kwamba mashauri yao, hawajiamulii tu peke yao kwa kujitakia. Kwamfano utakumbuka kuna wakati  Mungu alimnyanyua Moyo Koreshi mtawala wa Uajemi ili awape ruhusu wayahudi warudi katika nchi yao wakamjengee nyumba.

Ezra 1:1 Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia, akisema,  2 Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi;  3 Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya Bwana, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu.  4 Na mtu awaye yote aliyesalia mahali po pote akaapo hali ya ugeni, na asaidiwe na watu wa mahali pake, kwa fedha, na dhahabu, na mali, na wanyama, zaidi ya vitu vitolewavyo kwa hiari ya mtu, kwa ajili ya nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu

Mungu huyo  huyo ndiye aliyemfanya mfalme Nebukadreza kuwa na moyo mkatili ili awachukue watu wake utumwani kwasababu ya makosa yao.(Yeremia 27:6, 43:10)

Mungu anaweza kuwatumia watawala kuadhibu taifa, au kuwabariki watu wake. Hii ni kuonyesha kuwa hakuna tawala yoyote katika hii dunia inamilikiwa na fikra za mwanadamu asilimia 100, bali mengi ya mashauri ya wakuu hutoka juu mbinguni, au yameruhusiwa na Mungu. Wao ni kama maji tu yanayofuata mkondo wa kusudi la Mungu.

Ndio jambo ambalo Mungu alimwambia Mfalme Nebukadreza kwamba “aliye juu ndiye anayetawala”(Danieli 5:21) lakini yeye alidhani ni uongo, mpaka siku alipoondolewa kwenye ufalme wake kwa miaka 7, na kurudishwa baadaye.

Hivyo, jambo hili, sio tu la viongozi wa kidunia, lakini pia hata wa kanisani. Ikiwa kanisa ulilopo linasimamia kweli na utakatifu na Kristo Yesu ndio kiini cha fundisho lao, basi waheshimu sana viongozi wako, kwasababu si kila shauri linalotoka kwenye vinywa vyao, ni wao wamefikiria. Wao ni kama maji tu yaliyomwagwa kwenye mfereji, ili kukuongoza wewe. ukishandana nao, au ukipuuzia kuongozwa nao, wakati mwingine unapingana na maamuzi ya Mungu wako bila kujijua.

Waheshimu viongozi wako wanaokulea kiroho, kama vile unavyowaheshimu watawala ya kidunia.

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;

Maelezo ya Mithali 28:20

“Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele; Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa”.


Mstari huo unatufundisha jinsi pupa (kutaka vya haraka), inavyokinzana na neno “Uaminifu”. Ikiwa na maana mtu ambaye anataka wingi kwa muda mfupi, ni lazima tu atatumia njia isiyo ya haki, ili avipate anavyovitaka. Kwamfano viongozi wa nchi au waajiriwa wenye tamaa ya mafanikio ya haraka, wanaotaka mwezi  huo huo wajenge, au wawe na miradi mikubwa, mwisho wa siku huwa wanatumia njia za wizi, ili kufikia mafanikio yao.  Hiyo ndio sababu inayowafanya wapoteze uaminifu katika kile walichokabidhiwa.

Na hatma ya hawa watu, ni kukutana tu na matatizo, aidha kufungwa, au kufukuzwa kazi, au kutozwa faini, n.k.. na kuangukia hasara tu sio faida.

Ndio maana ya hili Neno

Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele; Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.

Kwasababu mafanikio na pupa,  havipatani kabisa. Bali achumaye kidogo-kidogo ndiye atakayefanikiwa(Mithali 13:11)

Yusufu alirekodiwa kuwa ni mwaminifu katika kazi yake. Na hivyo, akabarikiwa na Bwana mpaka akapewa nafasi ya uwaziri-mkuu wa taifa kubwa la Misri (Mwanzo 39:1-6). Danieli alirekodiwa kuwa muaminifu na hivyo akadumu katika falme zote mbili zilizotawala dunia wakati ule, yaani Babeli pamoja na Umedi na Uajemi (Danieli 6:4).

Lakini pia Neno hili linatafsirika rohoni.

Katika kazi ya Bwana, palipo na UAMINIFU, basi mwishowe Mungu huwa anabariki utumishi wa mtu huyo. Alisema maneno haya;

Luka 16:10  “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia. 11  Basi, kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu, ni nani atakayewapa amana mali ya kweli? 12  Na kama hamkuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?

Umeona? Lakini ukikosa uaminifu, ndio utataka utumie njia zisizompendeza Mungu ili uone matokeo unayoyatarajia haraka, ndio hapo utaona mhubiri anatumia njia za undanganyifu kutengeneza shuhuda za uongo, ili watu wajue kuwa anao-upako wajae kwenye kanisa lake. Mambo kama haya hatma yake ni , uangamivu. Wengine, wanahubiri injili ya kisiasa, au vichekesho, wengine wanapachika staili za kidunia madhabahuni na kwenye kwaya, hawahubiri tena kweli, wala hawakemei dhambi, wakihofia watu kukimbia makanisa yao. Wanapoteza uaminifu ili wapate watu wengi kanisani. Hii ni hatari kubwa!

Hawajui kuwa ndani ya uaminifu, zipo Baraka. Na Mungu anaona, Mungu atamnyanyua tu mtu huyo.

Hivyo tupende kusimamia kweli, turidhike na nafasi zetu, tupinge mambo ya giza, TUWE WAAMINIFU katika yote na hakika tutaona Baraka za Bwana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE.

Maana ya Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”

Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.

Nini maana ya Mithali 27:6 “Jeraha utiwazo na rafiki ni amini;

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

THAWABU YA UAMINIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu Maana ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.

Maelezo ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,  Ni upumbavu na aibu kwake.


Hekima inatufundisha tusiwe watu wa kujibu au kuzungumza kabla hatujasikia habari yote au taaarifa yote na kuitafakari kwanza..Kwamfano mwenzako anazungumza jambo Kisha wewe ukaingilia kati na kutaka kujibu, hoja ambayo haijakamilika..Matokeo yake hapo ni Nini kama sio kutoa majibu yasiyosahihi?. Au ambayo hayajakamilika?

Ndio hapo anasema ni upumbavu na aibu kwake. 

Hii imeathiri hata kusambaa Kwa taaarifa za uongo. Mtu atasikia jambo, kwasababu Hana taaarifa nalo vizuri, atatoka muda huo huo na kwenda kumpasha mwingine, na yule mwingine atampasha mwingine..Hivyo taaarifa za uongo huzagaa Kwa upesi sana. Ndivyo ambavyo hata waandishi wa habari ambao hawawi makini wanavyosambaza habari ambazo bado hawajazifanyia uchambuzi yakinifu. Na matokeo yake husababisha matatizo makubwa katika jamii. 

Mafarisayo na wayahudi walimpinga Yesu kwasababu walikuwa ni watu wa kupokea tu taaarifa ambazo hawazitafiti, walisikia Yesu anatokea Nazareti, wakahitimisha amezaliwa Nazareti, wengine wakamwita Msamaria. Lakini kama wangesubiri kutuatilia Kwa ukaribu mawazo Yao yangebadilika, na wasingekuwa wapumbavu kama tunavyowasoma kwenye biblia.

Hata wakati alipokuwa anazungumza nao, hawakutaka kusikiliza mpaka mwisho ni Nini Bwana anataka kuwaambia, kwamfano Kuna wakati aliwaambia, mtu akilishika Neno lake hataonja mauti milele. Lakini wao Hawakutaka ufafanuzi alimaanisha Nini.. hapo hapo wakarukia na kumwita ana Pepo;Kwa kauli Ile.

Yohana 8:52-53

[52]Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.

[53]Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?

Wakati mwingine aliwaambia livunjeni hili hekalu,nami nitalisimamisha baada ya siku tatu. Wakairukia hiyo kauli bila kusubiria maelezo  yake , ndio ikawa habari ya mji mzima Kuna mtu kasema anaweza kulijenga Kwa siku 3 hekalu lililojengwa Kwa miaka 46. Kumbe hawakujua Kristo anazungumzia habari ya mwili wake.(Yohana 2:20)

Biblia inatuasa tuwe wepesi wa kusikia, na si wa kusema; Ina faida nyingi.

Yakobo 1:19

[19]Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

HAUWEZI KURUKA MADARASA YA MUNGU!

KUOTA UPO UCHI.

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Maana ya Mithali 19:15 ‘Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;

Rudi nyumbani

Print this post

Hii ni Maana ya Mithali 18:18 Kura hukomesha mashindano;

Fahamu Maana ya;

Mithali 18:18 Kura hukomesha mashindano;  Hukata maneno ya wakuu.


Kupiga kura ni Moja ya njia ambayo ilitumika kuleta suluhisho lenye utata, na wakati mwingine kuchagua viongozi/wamiliki. Pitia hapa ujue zaidi kuhusu kura zilivyopigwa zamani za biblia…>> Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo;

Na Mungu wakati mwingine aliingilia kati na kuleta majibu yake sahihi kwa kupitia njia hiyo. Kwamfano wakati ule Yona anamkimbia Mungu, Hali ilipochafuka kule baharini, utaona wale watu walipiga kura, ili kujua sababu ya mambo yale ni nani na Ile kura ikamwangukia Yona.

Mitume wa Bwana baada ya kuomba, kuhusu mrithi wa nafasi ya Yuda wakapiga kura katika ya wale wanafunzi wawili, nayo ikamwangukia Mathiya, na likawa kweli ni chaguo la Mungu.(Matendo 1:15-19),

Hata wakati wa nchi ya Israeli kugawanywa . Kura zilitumika kuamua nani akae wapi, na nani arithi wapi (Hesabu 26:55).

Hivyo kupiga kura ilikuwa ni mojawapo ya njia kuleta jibu lisilokuwa na upendeleo. Au lililoegemea upande Fulani mmoja. Na kwa kufanya hivyo malalamiko mengii yalikomeshwa kwasababu maamuzi hayakuamuliwa na upande wowote ule.

Ndio maana ya hili andiko

Mithali 18:18

[18]Kura hukomesha mashindano;  Hukata maneno ya wakuu.

Hata kipindi Cha sasa njia ambayo hutumiwa kuchagua viongozi wengi ulimwenguni Huwa ni ya  kura.  Isipokuwa hii siyo ya kurusha SHILINGI, au kete angani  inayomwangukia mmojawapo ndio anakuwa kiongozi..hapana Bali ni kuruhusu Kila mmoja kutia maoni yake..Kisha zinahesabiwa na yule mwenye nyingi hupewa. Na hivyo hakuna malalamiko. 

Tofauti na Ile mtu atawadhwe tu Moja Kwa moja kuwa kiongozi, Hiyo huleta ukakasi mwingi.

Hivyo ni kutufundisha kua Bwana anaouwezo wa kuingilia kura zipigwazo na kuleta majibu yake sahihi..hususani pale anaposhirikwa Kwa maombi, na kama hakusema Kwa njia nyingine ya Moja Kwa moja.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

MKUU WA ANGA.

Mzushi ni nani kibiblia? (Tito 3:10).

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Biblia inakataza kuapa kabisa, lakini kwanini watu wanaapa mahakamani na katika vifungo vya ndoa?

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

Nini maana ya Mithali 27:21  inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 19:15 ‘Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;

Fahamu Maana ya Mithali 19:15 “Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa”.


Mara nyingi Sulemani kwa hekima ya Roho aliongozwa kuona uhusiano uliopo kati ya uvivu na umaskini. Kama tu kinyume chake, sehemu nyingine alivyoweka uhusiano kati ya bidii na utajiri(Mithali 10:4). Vivyo hivyo uvivu na umaskini havipishani.

Na kama anavyosema hapo, uvivu humpeleka mtu katika usingizi, lakini sio usingizi tu bali ule mzito, Kwasababu gani? Ni kwasababu mwili haupo katika hali ya kujishughulisha, na hivyo utalala tu, na Bado utaendelea kulala siku baada ya siku.. Na matokeo yake kutokuzalisha chochote kinachoonekana, hatimaye, umaskini unaingia.

Hivyo mstari huo unalenga Nyanja mbili. Ya kwanza ni ule uvivu wa mwilini, na ya pili ni ule uvivu wa rohoni.

Uvivu wa mwilini:

Mungu katuumbia kufanya kazi, watu wote (ikiwemo watakatifu). Maana yake ni kuwa ikiwa huna huduma yoyote ya madhabahuni Bwana amekuitia, ambayo inakufanya utumike muda wote hapo. Ni sharti ufanye kazi. Mtume Paulo alilionya kanisa juu ya watu ambao hawafanyi kazi kwamba ni sharti wajishughulishe ili wapate na kitu cha kuwagawia na wengine (2Wathesalonike 3:10)

Uvuvu wa rohoni:

Lakini pia Uvuvi wa rohoni. Mtakatifu anapokuwa mvivu, kusoma Neno, yaani muda wa Neno anakwenda kutazama filamu, anakwenda kijiweni kucheza drafti,.Anakuwa  mvivu kuomba, Unapofika huo muda tu anaona usingizi ni bora kuliko kuomba,.Au Mtakatifu hataki kushuhudia habari za Kristo kwa wengine, anasema jua kali. Sasa mtu huyo anajiandaa kuwa maskini kiroho. Yaani atakuwa katika wokovu usiokuwa na matunda, ukuaji wake wa kiroho utakuwa hafifu, Neema ya Mungu haitatenda kazi kwa wingi juu yake, na hivyo atakosa mema mengi ya Mungu katika safari yake wa wokovu hapa duniani.

Uvuvi wowote, una hasara, kwahiyo tuuweke katika orodha ya maadui zetu wa imani.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post