Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.
NAFASI YAKO NI IPI KATIKA MWILI WA KRISTO?
Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?
Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?
Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?
ANTIPA SHAHIDI WANGU, MWAMINIFU WANGU.
Kama kichwa cha waraka Huu kinavyosema… “Waraka wa pili wa Paulo Mtume kwa Wakorintho”
Kutuonyesha kuwa Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hichi..
Tunaweza kukigawanya katika sehemu kuu tatu (3)
1) Utendaji kazi wa Mungu, na wajibu wa watakatifu katika huduma na maisha yao ( sura ya 1-7)
2) Utoaji bora kwa mkristo.(Sura ya 8-9)
3) Utetezi wa huduma ya Paulo (10-13)
1) Utendaji kazi wa Mungu, na wajibu wa watakatifu katika huduma na maisha yao ( sura ya 1-7)
Katika sura hizi, Mtume anagusia maeneo kadha wa kadha, kama ifuatavyo.
i) Faraja ya Mungu
Paulo anatoa shukrani zake kwa jinsi Mungu anavyoweza kuwafariji watu wake katikati na dhiki na majaribu mazito. Akimtaja Mungu kama ni ndio mtoa faraja yote, katika dhiki zetu. (1-3-7)
2 Wakorintho 1:3-4
[3]Na ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema, Mungu wa faraja yote;
[4]atufarijiye katika dhiki zetu zote ili nasi tupate kuwafariji wale walio katika dhiki za namna zote, kwa faraja hizo, tunazofarijiwa na Mungu.
ii) Nafasi ya kutubu.
Sehemu inayofuata Paulo anaeleza sababu ya kutofika Korintho haraka, kama ilivyodhaniwa. Ni ili asilete tena huzuni zaidi kama akiwakuta bado hawajakamilika. Na hiyo ni kutokana na kuwa hawakuwa na mabadiliko ya haraka kwa agizo lake la kwanza, hivyo hakutaka afanye ziara ya ghafla bali wayatengeneze kwanza wao wenyewe ili ziara yake kwao, safari hii iwe ya raha na sio ya hukumu.(1:23-2:4)
iii) Wajibu wa kusamehe. (2:5-11)
Paulo anawahimiza wakorintho kusamehe kwa wale watu wanaoleta huzuni ndani ya kanisa, Hususani waliomnenea vibaya utume wake. Anahimiza kuliko kusimamia adhabu ziwapasazo ambazo wana haki kweli ya kuzipokea. Kinyume chake wawasamehe ili wawapate tena wasipotee kabisa katika huzuni zao.
IV) Utukufu wa agano jipya.(sura ya 3-5)
Paulo Anaeleza jinsi gani, agano jipya utukufu wake ulivyo mbali na ule wa agano la kale. Kwasababu utukufu wa agano jipya umekuja Katika Roho atoaye uhuru.
Paulo anaeleza kwasababu hiyo hatupaswi kulegea kwa kuenenda kwa hila au kulichanganya Neno la Mungu na uongo. Au kwa kutohubiri injili. Bali kufanya yote bila kujali utu wetu wa nje kuchakaa. Tukijua kuwa ule wa ndani unafanywa upya siku baada ya siku na kwamba ipo siku tutasimama mbele ya kiti hukumu kutoa Hesabu ya mambo yetu yote tuliyoyatenda katika mwili.
Paulo anaeleza kwamba kama Kristo alivyopewa huduma ya upatanisho sisi pia tumepewa Neno Hilo hilo ndani yetu. Kuupatanisha ulimwengu na Mungu kupitia Yesu Kristo. Akionyesha kuwa ni wajibu wetu sote kuhubiri injili.
V) Maisha ya ukamilifu (sura ya 6-7)
Paulo anawasihi Wakoritho waikunjue mioyo yao na waishi maisha ya ukamilifu na ya uangalifu wasiwe kwazo la namna yoyote ili utumishi wao usije laumiwa siku ile ya Bwana
Lakini pia anawapa onyo wasiwe na ushirika na wasioamini.
Pamoja na hilo katika sura ya saba, Paulo anaeleza furaha yake kwa Wakorintho Kwa kuitii toba..kufuatana na waraka aliowaandikia hapo kabla wa huzuni ( Ambao haupo miongoni mwa nyaraka hizi zilizo kwenye biblia). Ambapo walipousoma walitubu na kugeuka, kwelikweli. Kuonyesha utii wa toba. Ambao unapaswa uonekane ndani ya makanisa hata sasa.
2) Utoaji bora kwa mkristo.(8-9)
Katika sura ya 8-9
Paulo anahimiza michango kwa ajili ya watakatifu walio Yerusalemu, Akitolea mfano watakatifu wa Makedonia jinsi walivyoweza kutoa kwa ukarimu hata katika umaskini wao, vivyo hivyo na wao anawahimiza wawe na moyo huo huo. Akiwaonyesha jinsi Bwana wetu Yesu alivyotupa kielelezo cha kukubali kuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.
2 Wakorintho 8:9
[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.
Kwasababu utumishi wa namna hiyo sio tu unawapata watakatifu rizki lakini pia huleta matunda ya shukrani kwa Mungu.
2 Wakorintho 9:12
[12]Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu;
3) Utetezi wa huduma yake (Paulo). Sura ya 10-13
Katika sura hizi Paulo anaitetea Huduma yake dhidi ya watu wengine wanaojitukuza mbele za watu, kana kwamba ni mtume wa kweli kumbe ni mitume wa uongo, ambao huwashawishi watu kwa majivuno ya nje na ukali, lakini si ya kazi.
2 Wakorintho 11:20
[20]Maana mwachukuliana na mtu akiwatia utumwani, akiwameza, akiwateka nyara, akijikuza, akiwapiga usoni.
Hivyo Paulo anawaeleza kwa upana uthabiti wa huduma yake, tangu asili ya kabila lake, mateso aliyopitia, akionyesha mpaka kusimama vile, hakukutokea hivi hivi tu, bali katika masumbufu mengi, anawaeleza pia maono aliyoyafikia mpaka kunyakuliwa mbingu ya tatu, hiyo yote ni kuwaonyesha wakorintho kama wanataka kuamini kwa watu wanaojisifia basi yeye anawazidi wao, lakini hatumii njia hiyo, bali ya udhaifu ili asihesabiwe zaidi ya vile watu wavionavyo Kwake.
Salamu za mwisho.
Anahimiza wakoritho wanie Mamoja, watimilike na wafarijike.
Hivyo kwa ufupi mambo haya makuu tunaweza kuyapata katika waraka huu;
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)
Fahamu maana ya 2 Wakorintho 8:9 alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.
Rudi Nyumbani
Swali: Je ni sahihi kusema waraka fulani wa Mtume Paulo ni kwaajili ya kanisa fulani tu?…Mfano waraka wa Wakorintho uliwahusu Wakorintho tu peke yao hivyo si vitu vyote vya kuchukua huko…
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)
Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
Biblia inasema nini kuhusu mtu ‘Mwenye kujipendekeza (Mithali 29:5)
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Arkipo ni mmoja wa wahudumu wa agano jipya. Ambaye alikuwa na ushirika wa karibu na mtume Paulo katika kazi ya kuieneza injili.
Paulo alipokuwa anamwandikia waraka Filemoni, anamtaja Arkipo kama ASKARI mwenzake.
Filemoni 1:1-2
[1]Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na Timotheo aliye ndugu yetu, kwa Filemoni mpendwa wetu, mtenda kazi pamoja nasi,
[2]na kwa Afia, ndugu yetu, na kwa Arkipo askari mwenzetu, na kwa kanisa lililo katika nyumba yako.
Lakini pia katika waraka ambao Paulo aliundika kwa Wakolosai tunaona katika salamu zake za mwisho, anatoa agizo maalumu kwa mtu huyu kwa kumwambia, aiangalie sana huduma Ile aliyopewa na Bwana ili aitimize.
Wakolosai 4:17
[17]Mwambieni Arkipo, Iangalie sana huduma ile uliyopewa katika Bwana, ili uitimize.
Kuonyesha kuwa alikuwa na sehemu ya huduma kwa hawa watakatifu wa Kolosai. Ijapokuwa biblia haijatueleza ni huduma ya namna gani.
Lakini ni kwanini amwambie vile?
Paulo anasisitiza kuwa huduma hiyo amepewa na Bwana, (ikiwa na maana si mwanadamu)..huwenda alidhani alichokirimiwa hakikuwa na msukumo kwa Bwana, ni yeye tu mwenyewe ameanza kukitenda..Au watu wamekipuuzia au kukiona cha kawaida, hivyo na yeye pia akakiona cha kikawaida, hakitakiwi kutiliwa mkazo sana.
Au Pengine Arkipo alipitia kuvunjwa moyo, au mashaka fulani, na hiyo ikampelekea kutowajibika vya kutosha katika nafasi yake.
Hivyo Paulo anamtia moyo kwa kumwambia huduma hiyo ni ya Mungu, hivyo hakikisha unaitimiza.
Ni lipi la kujifunza kwa Arkipo.
Hata sasa kila mtu aliyeokoka ni askari wa Bwana. Na hivyo amepewa huduma ndani yake, kufuatana na karama aliyokirimiwa ambayo anapaswa aiangalie na kuitimiza.
Kama askari wa Bwana ni lazima tufahamu kuwa tutakumbana na vita na kuvunjwa moyo, na kutaabishwa, na dhiki, na kupungukiwa, na taabu za namna mbalimbali lakini pia Raha katika huduma.
Kwa vyovyote vile Hatupaswi kupoa, au kulegea, au kuvinjika moyo. Bali tubakie tufahamu kuwa ipo siku tutatolea hesabu uwakili wetu.
Kama askari ya Kristo Timiza huduma yako
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mhunzi ni nani? (Isaya 54:16)
Mwandishi wa kitabu cha Filemoni ni nani?
Mwandishi wa kitabu cha Filemoni ni nani?
Kuwanda ni kufanya nini?
Aristarko ni mmoja wa wahudumu wa injili katika agano jipya. Paulo anamtaja kama mtenda kazi pamoja naye (Filemoni 1: 24), wengine wakiwa ni Luka, dema, na Marko.
> Aristarko ni mmoja wa watu walioamini injili mahali palipoitwa Thesalonike, Paulo alipokuwa anahubiri, ambao kwa mioyo yao wenyewe wakaamua kuambatana na Paulo katika ziara zake za kuhubiri injili kwenye mataifa mengine.
Matendo ya Mitume 20:4
[4]Watu hawa wakafuatana naye, Sopatro Mberoya, mwana wa Piro, na Aristarko na Sekundo, watu wa Thesalonike; na Gayo mtu wa Derbe, na Timotheo; na Tikiko na Trofimo watu wa Asia.
> Kati ya watendakazi wa Paulo waliovamiwa na kundi la mataifa ( Paulo aliwaita hayawani wakali) kule Efeso, mmojawapo alikuwa ni Aristarko. Ijapokuwa biblia haituambii kama walipigwa au kuwajibishwa vikali…Lakini ni wazi kuwa walipitia dhiki na hwenda ilikuwa ni kupigwa kwelikweli.
Matendo ya Mitume 19:29
[29]Mji wote ukajaa ghasia, wakaenda mbio wakaingia mahali pa michezo kwa nia moja, wakiisha kuwakamata Gayo na Aristarko, watu wa Makedonia waliosafiri pamoja na Paulo.
> Aristarko anatajwa pia na Paulo kama mfungwa mwenza. Kuonyesha kuwa si tu alishiriki mapigo, bali pia na vifungo pamoja na Paulo, tangu kwenye safari yake akiwa kama mfungwa kuelekea Rumi, mpaka Rumi kwenyewe alipokuwa mfungwa kwenye nyumba yake mwenyewe.
Matendo ya Mitume 27:2
[2]Tukapanda katika merikebu ya Adramitio iliyokuwa tayari kusafiri mpaka miji ya pwani za Asia, tukatweka; Aristarko, Mmakedonia wa Thesalonike, akiwa pamoja nasi.
Wakolosai 4:10
[10]Aristarko, aliyefungwa pamoja nami, awasalimu; na Marko, mjomba wake Barnaba, ambaye mmepokea maagizo kwa habari yake; akifika kwenu mkaribisheni.
Kwa ufupi, tunaweza jifunza mengi kwa watendakazi kama hawa, ambao walikuwa washirika wenza wa Paulo. Kwanza kwa kujitoa kwao kwa hiari kuitumikia injili. Lakini kuzidi kuwa thabiti hata katika mapigo na vifungo bila kuikana imani. Kwamfano tunapoisoma ile safari ya Paulo kama mfungwa kuelekea Rumi jinsi walivyopitia majanga makubwa baharini, mpaka wakakata tamaa ya kuishi, huyu aristarko alikuwa pia katika dhoruba ile.
Kufanikiwa kwa huduma ya mtume Paulo ni kwasababu ya mashujaa kama hawa walioisimama pamoja naye katika nyakati zote.
Bwana awanyanyue wakina Aristarko wengi, kwenye makanisa yetu na huduma zetu. Ili injili ya Bwana ifike na kuenea kiwepesi ulimwenguni kote.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ndugu Yule anayezungumziwa kwenye 2Wakorintho 8:18 ni nani?
Sosthene ni nani katika biblia? (Matendo 18:17)
Mchuuzi ni nani? (Hosea 12:7).
MIMI NA WEWE TU KAZI YA MUNGU.
Rudi Nyumbani
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.
JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..
NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.
Sosthene ni mmoja wa wahudumu wa injili Katika agano jipya. Mshirika mmojawapo wa mtume Paulo, katika kazi ya kuitetea injili.
Katika kitabu cha matendo anatajwa kama mkuu wa sinagogi, kule Korintho
Matendo ya Mitume 18:17
[17]Nao wote wakamshika Sosthene, mkuu wa sinagogi, wakampiga mbele ya
kiti cha hukumu. Wala Galio hakuyaona mambo hayo kuwa ni kitu.
> Alikuwa ni mmoja wa wayahudi(washika-sheria), waliokutana na injili ya Paulo na kuamini.
Paulo alipofika Korintho Mungu alimtokea katika maono na kumwambia asiogope aendelee kuhubiri kwasababu katika Mji huo anao “watu wake wengi”
Hivyo aliendelea kuhubiri kwa ujasiri mwingi kwa muda wa mwaka mmoja na nusu na watu wengi sana miongoni mwa wayahudi waliamini ikiwemo huyu Sosthene na Krispo.
Matendo 18:9-11
[9]Bwana akamwambia Paulo kwa maono usiku, Usiogope, bali nena, wala usinyamaze,
[10]kwa kuwa mimi ni pamoja nawe, wala hapana mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana mimi nina watu wengi katika mji huu.
[11]Akakaa huko muda wa mwaka mmoja na miezi sita akifundisha kati yao neno la Mungu
Baadaye wayahudi wenye wivu waliamka kinyume cha Paulo, na kumpeleka mbele ya Galio liwali ili ashitakiwe kwa kuleta machafuko ndani ya dini yao.
Lakini Galio akawatawanya kwasababu kesi yao haikuwa ya uhalifu au dhuluma bali ya mambo ya kiimani..Ambayo kwa mujibu wa sheria za kirumi hazisikilizwa kwenye mahakama zao.
Hivyo wayahudi kuona Paulo hajahukumiwa, wakamkata huyu Sosthene mkuu wa Sinagogi na kumpiga mbele ya kiti cha hukumu. Na hiyo yote ni kutokana na kwamba aliisapoti huduma ya Paulo, pengine aidha kwa kumruhusu ahubiri injili ndani ya masinagogi yao au kwa kutochukua hatua zozote stahiki dhiki ya injili ya mtume Paulo.
Lakini pia tunakuja kuona baadaye Paulo wakati anaandika waraka kwa Wakoritho anamtaja Sosthene kama mshirika mwenza wa utume wa Kristo.
1 Wakorintho 1:1
[1]Paulo, aliyeitwa kuwa mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
Hiyo ni kuonyesha kuwa alikuja kuwa nguzo hasaa kwa watakatifu wa Korintho. Mpaka Paulo anamtaja kama mshirika mwenza.
Ni Nini cha kujifunza katika habari ya Sosthene?
Ni kuonyesha uweza wa Mungu wa kugeuza watu wa aina zote. Kikawaida kwa taratibu za kiyahudi mpaka mtu ameaminiwa kuwa mkuu wa sinagogi, maana yake ni kuwa mtu huyo amethibitishwa kuijua na kuishiya torati kwelikweli na nidhani zote za kiyahudi na taratibu zao.
Kwahiyo kwa mtu kama Sosthene kubadilika ghafla na kuwa mfuasi wa injili, haikuwa rahisi, ilihitaji neema ya Mungu kubwa, ndio maana kwa wayahudi alionekana kwa mwasi wakampiga sana.
Bwana anataka tusibague wa kuwahubiri injili, kwasababu injili ni uweza wa Mungu(Warumi 1:16), Umwonapo imamu mhubirie, Shehe mhubirie, Buddha mhubirie, baniani mhubirie, padri, askofu, mganga wa kienyeji..wahubirie kwasababu hapo ulipo kuna “watu wa Mungu wengi sana” hujua ni yupi Bwana aliyemkusudia kuwa chombo chake kama Sosthene.We hubiri tu.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MKUU WA GIZA.
Tikiko ni nani kwenye biblia?
Mhunzi ni nani? (Isaya 54:16)
Tikiko ni mmoja wa washirika waliohudumu na mtume Paulo katika kazi injili. Ijapokuwa si mtu anayejulikana sana..lakini ametajwa sehemu kadha wa kadha katika vitabu vya agano jipya.
> Anatajwa kama mmoja wa watu waliomua kufuatana na Paulo katika ziara za injili maeneo mbalimbali (Makedonia na Asia).
Matendo ya Mitume 20:3-4
[3]Alipokwisha kukaa huko miezi mitatu, na Wayahudi kumfanyia vitimvi, alipotaka kwenda Shamu kwa njia ya bahari; basi akaazimu kurejea kwa njia ya Makedonia.
[4]Watu hawa wakafuatana naye, Sopatro Mberoya, mwana wa Piro, na Aristarko na Sekundo, watu wa Thesalonike; na Gayo mtu wa Derbe, na Timotheo; na Tikiko na Trofimo watu wa Asia.
> Paulo anamtaja pia kama Mhudumu mwaminifu katika Bwana. Maana yake aliupima uaminifu wake, akauthbitisha kuwa hauna unafiki, mpaka akamfanya kama mbeba taarifa zake za kihuduma kwa makanisa.
Waefeso 6:21
[21]
Basi ninyi nanyi mpate kuzijua habari zangu, ni hali gani, Tikiko, ndugu mpendwa, mhudumu mwaminifu katika Bwana, atawajulisheni mambo yote;
Wakolosai 4:7-8
[7]Tikiko, ndugu mpendwa, mtumishi mwaminifu, mjoli wangu katika Bwana, atawaarifu mambo yangu yote;
[8]ambaye nimemtuma kwenu kwa sababu iyo hiyo, ili mjue mambo yetu, naye akawafariji mioyo yenu;
> Lakini pia kwa jinsi Paulo alivyomtaja tunaweza kusema alisimama kama mwangalizi-mwenza wa viongozi wa makanisa.
2 Timotheo 4:12
[12]Lakini Tikiko nalimpeleka Efeso.
Tito 3:12
[12]Wakati nitakapomtuma Artema kwako au Tikiko, jitahidi kuja kwangu huku Nikopoli; kwa maana huku nimekusudia kukaa wakati wa baridi.
Hivyo ijapokuwa si mtu aliyemaarifu, lakini alifanyika nguzo si tu katika mafanikio ya huduma ya mtume Paulo lakini pia kwa makanisa ya Mungu.
Je! Makanisa yetu yaweza kuwa akina Tikiko, watu waaminifu kwa viongozi wao, na kwa kanisa la Kristo?
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?
Silwano ni nani,kama tunavyomsoma kwenye biblia?(1Petro 5:12)
Rudi Nyumbani