UKristo Ni Nini?

UKristo Ni Nini?

Ili kuelewa Nini maana ya Ukristo, tutafakari kwanza maana ya Neno UTAIFA…Neno utaifa limetokana na Nomino Taifa…Kwahiyo kitendo chochote kinachofanyika kinachohusisha mapenzi na Taifa, kitendo hicho kinaitwa Utaifa..

Tukirudi katika UKristo, Neno Ukristo nalo pia limetokana na Nomino Kristo…Na maana ya Kristo ni “Mtiwa Mafuta” au “Masihi” na wala sio Yesu,…Mtu aliyetiwa Mafuta na Mungu zamani hizo aliitwa kristo  na hata sasa kibiblia bado wanajulikana hivyo hivyo kama makristo.. Chimbuko la neno hilo Masihi au kristo Ni lugha ya Kigiriki.

Hivyo walikuwepo makristo wengi, sana zamani..Katika Biblia Daudi alijulikana kama ni kristo (yaani masihi wa Bwana) 1Samweli 16:6, kadhalika Mfalme Sauli (1Samweli 24:6) na wengine wengi, walijulikana kama ni makristo/masihi wa Bwana.

Lakini alipokuja mmoja ambaye alikuwa ni mkuu kuliko hao wote, aliyetiwa mafuta na Mungu mwenyewe kuwa juu ya vitu vyote, huyo naye aliitwa masihi au Kristo, isipokuwa ili kumtofautisha na masihi na makristo wengine, huyu jina lake lilianza kwa Herufi kubwa, yaani aliitwa Kristo badala ya kristo. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU. Ndio maana mahali popote katika biblia panapomtaja Kristo Yesu ni lazima hilo neno Kristo lianze kwa herufi kubwa, kuwatofautisha na makristo wengine.

Kwahiyo tukirudi kwenye swali, U-Kristo ni nini? Jibu ni kuwa U-Kristo ni kitendo mtu anachokifanya kinachohusisha mapenzi yake na mtu mmoja anayeitwa Kristo Yesu, zingatia hilo neno Kristo Yesu na sio “kristo yesu”…kwasababu makristo wapo wengi, na ma-yesu wapo wengi  lakini Kristo yupo mmoja na Yesu yupo Mmoja.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

DINI NI NINI?

JE! UKIMWI UNATIBIKA?

SHETANI NI NANI?

JE! UBATIZO SAHIHI NI UPI?

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments