Biblia ni nini?

Biblia ni nini?

Biblia ni nini?

Ni neno la Kigiriki, lenye maana ya “mkusanyiko wa vitabu vitakatifu”..kikiwa kitabu kimoja kinaitwa Biblion lakini vikiwa vingi vinaitwa Biblia..

Hivyo Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66 vitakatifu..Vitabu hivyo vimeandikwa na wanadamu, lakini kwa Uongozo wa Roho Mtakatifu, kwasababu Mungu anafanya kazi ndani ya watu..(Warumi 8:28), Wanadamu wachache Mungu aliowachagua waliandika habari za Mambo yahusuyo sheria za Mungu, Maneno ya Mungu, Uweza wa Mungu, Upendo wa Mungu, huruma ya Mungu, Utukufu wa Mungu, na Ukuu wa Mungu..

Bwana Mungu aliwachagua waandishi hao kutoka katika makundi yote, kwa nyakati tofauti tofauti..Iliandikwa na Wafalme, Manabii, Matabibu, Wavuvi wa samaki, Wakusanyaji wa kodi n.k

Biblia imegawanyika katika sehemu mbili:  Agano la Kale na Agano Jipya, au Agano la Kwanza na Agano la Pili..

Agano la kale lina jumla ya vitabu 39, na Agano la Jipya lina jumla ya vitabu 27 kufanya jumla ya vitabu 66 vya Biblia Nzima.

Kiini cha Biblia yote ni mtu mmoja tu anayeitwa YESU KRISTO, Kila kitabu katika Biblia Takatifu kimeandika kwa wazi au kwa kinabii, habari za Yesu Kristo. Maonyo na Mafundisho yaliyomo ndani yake ni maonyo ya Yesu Kristo Mwenyewe.

Biblia ndio kitabu pekee, kilichobeba sauti ya Mungu ndani yake..Hakuna kitabu kingine chochote duniani kilichobeba kusudi la Mungu juu ya mwanadamu zaidi ya Biblia Takatifu. Na hakuna njia nyingine yoyote mwanadamu anaweza kumfikia Mungu tofauti na kitabu hicho


Mada Nyinginezo:

SHETANI NI NANI?

SIKU YA HUKUMU ITAKUWAJE?

DINI NI NINI

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Filbert ladislaus
Filbert ladislaus
3 years ago

Mwenyezi Mungu ndiye kimbilio langu kamwe sitamwacha aende zake bali nitamngangania mpaka siku yanyu yakihama ,jina la Bwana lihimidiwe amen.